Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

Sh. Bilioni 13.9 kukarabati Bombardier nchini Canada

36300a0997c69b5036252e97516eb45c.jpg



MABORESHO yanayofanywa na serikali katika Kampuni ya Ndege nchini (ATCL), yamezidi kuibua mipango ya shirika hilo, yenye lengo la kuongeza tija na ufanisi. Hayo yamefahamika siku chache baada ya kuwasili kwa ndege ya sita aina ya ‘Air Bus A220-300’.

Ujio wa ndege hiyo, unaifanya ATCL kuwa na ndege mbili za aina hiyo, moja ikiitwa ‘Ngorongoro’ na nyingine ‘Dodoma’ kila moja ikiwa urefu wa mita 38.7 na uwezo wa kubeba abiria 141, huku ikitajwa kuwa miongoni mwa ndege zenye matumizi mazuri ya mafuta. Mbali na ndege hizo, ATCL inayo ndege kubwa ya Boeing 787-8 Dreamliner yenye uwezo wa kubeba abiria 262 pamoja na ndege tatu ndogo.

Ndege hizo zilizonunuliwa na serikali ya Tanzania, moja aina ya Bombardier CS300 yenye uwezo wa kuchukua abiria 150 na zingine mbili aina ya Bombadier Q 400-8 zenye uwezo wa kubeba abiria 137, ni hatua ya kuimarisha safari za ndani za kampuni hiyo nchini. Kimsingi, jitihada hizo zinazoendelea kufanywa na Rais Joh Magufuli katika kuifufua ATCL, zimezidi kuifanya kampuni hiyo kuja na muonekana mpya katika utoaji wa huduma za usari nchini wakati huu, ambapo mipango mbalimbali ikiwemo kuanzishwa kwa safari za nje ya nchi zikiwemo za masafa ya mbali zikifanywa.

Katika kuhakikisha inatimiza matakwa yake kibiashara na kuleta ushindani katika soko la ndege, mbali na ununuzi wa ndege hizo, Serikali ya Awamu ya Tano imekuja na mipango mingine mbalimbali. Mikopo ya elimu kwa marubani, wahudumu Chini ya mpango huo, serikali kupitia Chuo cha Taifa cha Usarishaji (NIT) inakusudia kuanza kutoa mikopo ya mafunzo ya uendeshaji wa ndege (urubani), ili kuongeza idadi ya wahitimu watakaosaidia kukabiliana na upungufu uliopo katika kampuni hiyo. Kupitia utaratibu huo, serikali imeanza majadiliano na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) ili kuona uwezekano wa kuwawezesha mikopo wanafunzi wanaohitaji kupata elimu hiyo.

Akitangaza hatua hiyo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe alisema kimsingi mpango huo umelenga kuongeza ufanisi wa kampuni hiyo ili liweze kukia malengo yake ya utoaji wa huduma bora za usari ndani na nje ya nchi, kwa kuwa na wafanyakazi wazawa, hatua itakayoendana na kupunguza gharama zinazotokana na kuajiri marubani kutoka nje ya nchi.

Alisema kupitia mpango huo pia serikali inatarajia kununua ndege mbili kwa ajili ya mafunzo ya marubani, zitakazokabidhiwa NIT ili kuwezesha mafunzo kwa vitendo. Katika kutimiza mipango yake ya kuiboresha kampuni hiyo, mbali na kuzinduliwa kwa mafunzo ya utengenezaji wa ndege na urubani katika Chuo cha NIT mwishoni mwa wiki, chuo hicho pia kimezindua mafunzo ya kwanza ya uhudumu ndani ya ndege.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kozi hiyo, Mkuu wa Chuo cha NIT, Profesa Zacharia Mganilwa, alisema mafunzo hayo yatakayotolewa kwa kipindi cha miezi mitatu, yatasaidia kuongeza idadi ya watumishi hao, ambao kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na mahitaji yao makubwa katika soko hususani ndani ya ATCL.

Kuongezeka kwa safari za ndege Kwa mujibu wa ATCL, ujio wa ndege mbili za ‘Airbus’ utaongeza ufanisi wa shirika hilo kwa kuongeza safari zake za ndani na nje ya nchi, hatua inayotokana na mikakati mbalimbali iliyokuwepo hapo awali. Kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi, ujio wa ndege hizo utaifanya ATCL kuongeza safari za Mbeya, Harare , Zimbabwe, Lusaka na Zambia na safari za kila siku katika mji wa Dodoma. Akizungumzia hatua ya usalama wa ndege, Kamwelwe alisema ujio wa ndege za ‘Airbus’, unatoa nafasi kwa ndege mbili za Bombardier CS300 kwenda nchini Canada kwa ajili ya matengenezo.

Alisema ndege hizo zinatarajiwa kuondoka wakati wowote Februari mwaka huu, ambapo kila ndege itagharimu Dola za Marekani milioni 3 kwa ajili ya ukarabati huo. Karakana ya matengenezo Katika kuhakikisha shirika hilo linapunguza matumizi yanayotokana na matengenezo, Serikali imeanza mikakati ya kuboresha matengenezo ya karakana (hanger) ya matengenezo ya ndege lililopo katika Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro(KIA).

Kwa mujibu wa Waziri Kamwelwe, kukarabatiwa kwa karakana hiyo kwa kiasi kikubwa kutapunguza gharama za matengenezo ya ndege nje ya nchi, ambazo kimsingi zinaigharimu serikali fedha nyingi za kigeni. Marubani kuishi nyumba za kifahari Katika kuhakikisha inaongeza motisha ya kazi, Waziri Kamwelwe alisema marubani na watoa huduma ndani ya ndege (cabin crew) wanawekewa mikakati mizuri ya kupewa makazi, yatakayowawezesha kufanya kazi kwa ufasaha wakati wote. Alisema kwa kulizingatia hilo, serikali itahakikisha makazi hayo yanakuwa katika maeneo yatakayowapa fursa watumishi hao, kupumzika bila bugudha kwa ajili ya kuzifanya akili zao kujikita zaidi katika kusimamia huduma za usari wa ndege hizo
 
Iwe inafanyiwa baada ya miezi miwili mwaka mmoja haijalishi. Mlisaini mkataba nao matengenezo yoyote Canada wazungu waliona wajinga ndio waliwao. Mkiwavuruga na madini watasubiri ndege iende kwa service halafu wataishikilia END OF THE MOVIE
Acheni kujipa moyo mmelikoroga
Muwe mnasikiliza


Kwa hiyo kwa akili yako ulitaka isifanyiwe service....are you serious? Kama uko serious basi una matatizo fulani kichwani mwako. HAKUNA ndege isiyofanyiwa maintenance hapa duniani labda hiyo yako tu iliyopo sebuleni kwako.
 
Hivi wewe masikini unadhani kila mtu ni mjinga ? unachekwa ujue !


Sasa kama sio wajinga wanashabikia nini maintenance ya ndege zetu wakati ndege zote duniani zinafanyiwa service, huoni ni ujinga huu? Kama wanaelewa wanashabikia nini sasa, umejiuliza hili au hata wewe unashabikia ama kupinga nini ndege zetu kufanyiwa maintenance?
 
Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.
kila kitu inafikia muda kinahitaji ukarabati ni kweli haijalishi kimetumika muda gani.... Kwa maelezo mazuri haya yanatia moyo kiasi.
 
Anaefanya service ni ATCL au serikali coz serikali alimkodishia ATCL sasa inakuaje tena serikali afanye service yeye
 
Habari ni Services ya kawaida lakini Vimada wa Domokrasia wanachepuka nje ya mada kwa raha zao.
 
Hizo ni ndegemajini zimekuja kunyaga pesa za tanzania.

Sent from my SM-G950F using Tapatalk
 
Kwa Analysis ya kilala hoi ..na basics za kayumba...
Q400 moja inabeba abiria 70.
Ili itimize flight hrs 4000 kuqualify service ya billion 6.5 inabidi isafiri kila siku atleast masaa 3 kwa muda wa miaka minne (4)
Assuming wanenda mwanza flight ya SAA 1 na nusu (kwenda na kurudi itatimiza masaa matatu)

Kama bei ya tikiti itakuwa 285,000/-VAT Inc.watakusanya 19,950,000/ per trip. Round it up watakusana million 40 pamoja na mizigo @ trip. Go and return assuming watakuwa wanajaza watakuwa wanatengeneza gross ya milioni 80.

Hii inamaana baadaa ya mwezi watakusanya 2.4bilion. Na ndani ya mwaka hii itageuka kuwa 28.8bilioni.
Na mpaka masaa 4000yanatimia ndani ya miaka minne ndege moja itakuwa imekusanya 115.2bilioni. (Assuming iliruka kilasiku kwenda mwanza na kurudi ikiwa imejaza watu na mizigo)

Sasa tuasume)maana sijui biashara yandege .. Kwamba ukitoa tozo zote, kodi na gharama za uendeshaji..ATCL wapate faida ya 25% tu.. Hii itakuwa 28.8bilioni ambazo huenda ndio zitatoa gawio kwa serikali na kulipia matengenezo .. IDK
 
SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


Hakuna tatizo ndege kama chombo cha Usafiri kukarabatiwa iwe ndani ya nje au nje, Ni muhimu sana kwa Usalama wa Abiria. Habari ipo kwenye Bilioni 13.86 za Ukarabati, Je hizi ni kutoka katika Faida ghafi iliyozalishwa na ndege hizo au ni Fedha ya Mlipa kodi imemegwa tena?. Muhimu Serikali ituambie pia ni kiasi gani cha faida ghafi kilichozalishwa ili tupime na gharama tunayoingia. Je tupo kibiashara au Siasa za kibongo?
 
Ni ile ndege mpya iliyonunuliwa hivi karibuni na kupokelewa kifalmeView attachment 993742

14JAN 2019

Bombardier kukarabatiwa 
Canada kwa bilioni 13.9/-

SERIKALI imesema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada mwezi ujao.
Imesema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).


WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO, ISACK KAMWELWE, PICHA MTANDAO
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa kozi ya wahudumu ndani ya ndege katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja na zimekuwa msaada mkubwa kwa wananchi wanaozitumia kwa safari za ndani ya nchi.


“Bombadier mbili tulizozinunua tunatarajia kuzipeleka nchini Canada kwa ajili ya kufanyiwa 'service', na ndege moja itagharimu Dola za Marekani milioni tatu,” alisema Waziri Kamwelwe.


Waziri huyo alisema kuwa, baada ya kuletewa taarifa hiyo, alilazimika kumfuata Rais John Magufuli na kumshauri serikali ianze kufanya ukarabati kwa hanga lililopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), ili kupunguza gharama kubwa ambazo nchi inaingia katika kuzikarabati ndege.


Alisema katika kulitekeleza hilo, serikali imeshaanza kuchukua hatua kwa kuanza kukarabati hanga hilo kwa kuweka taa na kwamba serikali imeshaingia mikataba mitatu, mmojawapo utakuwa wa kununua vifaa vya matengenezo.
Alisema Rais Magufuli ameshakubali kutoa pesa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vitakavyotumika katika hanga hilo.


“Kwa hiyo, ndugu zangu tutaanza kukarabati ndege sisi wenyewe, nimeamua kusimamia 'industry' inadumu na hakuna kurudi nyuma,” alisema Waziri Kamwelwe.


Kuhusu mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege yaliyoanzishwa na NIT, Waziri Kamwelwe, alisema yatasaidia kupata Watanzania wakaohudumia ndege zilizonunuliwa na serikali.




Aliutaka uongozi wa NIT kuhakikisha mafunzo ya kozi hiyo yanakidhi viwango vya kimataifa.
Mkuu wa NIT, Prof. Zacharia Mganilwa, alisema idadi ya wahandisi wa ndege nchini inaendelea kushuka, akibainisha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na wahandisi 172, mwaka 2016 walikuwa 74, huku asilimia 69 kati yao, wakiwa ni raia wa kigeni.


Prof. Mganiliwa pia alisema zaidi ya asilimia 70 ya matengenezo ya ndege yanafanyika nje ya nchi.
“Tulikuwa na upungufu wa marubani kwa asilimia 60, mwaka 2017, idadi yao ilikuwa 743 kati ya hao 317 walikuwa ni wazawa na 425 ni raia wa kigeni,” alisema Prof. Mganilwa.


Alisema idadi ya wahudumu wa ndege waliosajiliwa nchini imekuwa ikiongezeka tangu serikali ilipoanza kununua ndege.
Alisema mwaka 2013/14, idadi yao ilikuwa 43, mwaka 2014/15 walikuwa 42, mwaka 2015/16 walikuwa 50, mwaka 2016/17 walikuwa 96, mwaka 2017/18 walikuwa 143 na mwaka 2019 waliopo katika mafunzo ni 61.


Alisema kuwa mwaka 2015, NIT ilianzisha shule kuu ya usafiri wa anga ikiwa na idara mbili ya uhandisi wa ndege na wahudumu wa ndege.


Alisema NIT ilipewa ithibati ya kutoa mafunzo ya uhudumu ndani ya ndege Aprili 25, mwaka jana na ithibati ya utengenezaji wa ndege na urubani bado hawajapewa. Alisema kuwa kwa sasa wapo katika hatua ya nne ya kukamilisha matakwa ya kupewa ithibati hiyo.
N siasa tu hzo

Heading iko kisias sana

Sent from my itel it1505 using JamiiForums mobile app
 
CAG akague kwa sheria gani bunge lilishapitisha sheria ya kumzuia kukakua ATCL na migodi #2020 Lissu#
Lissu mnamdanganya tu jamani. Hata kura 200000 hawezi pata. Hana issue yaani. In short, hakuna mtu wa kushindana na JPM kwa sasa. Iwe nje au ndani ya chama chake. Propaganda pigeni lakini ukweli mnaujua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi naamania kinachogomba hapa ni kwanza LUGHA na pili ni CHUKI BINAFSI! Nafafanua. LUGHA inagomba hasa hasa kaw uwepo wa neno SERVICE. Kwa wale ambao mmeshawahi kumiliki vyombo vya moto au mashine mbalimbali, mnajua hilo neno SERVICE, yaani kukifanyia chombo chako ukaguzi wa kitaalamu na kiufundi aidha kwa kubadilisha mafuta au oil au some delicate PARTS. Pia hili ni pamoja na kuendana na muda wa saa za kufanya kazi, and in this respect, muda wa kuruka angani. Haya mambo hayana ushabiki, muda wa service ukifika lazima u- complile irrespective na bila kujali Dogo au Mwepesi au Shimo atasema nini. Pili nadhani ushabiki wa kisiasa ndio unasukuma watu kusema na kuandika waandikayo! Na kwa vile ni watu wanao subiri jambo ndiyo waseme kwa sababu wameishiwa HOJA, basi linapotokea jambo kama hili, BASI wanapata kisemeo na wengine wanafuata tu hata kama hawajui suala lenyewe liko vipi!
 
Nimeiosoma habari vizuri tu; kuna mambo ya msingi ya kutizama hapa ilikujua kama biashara inafanyika kwa faida au hasara; ni vizuri kujua kama muda wa hizo ndege kufanyiwa service umefika au laah. Nasema hivyo kwsababu, isije ikawa ni sehemu ya upigaji! Lakini pia, aliyenunnua ndege ni serikali na serikali ikaikodishia ATCL isitumie katika kufanya biashara; sasa kuna maswali ya kujiuliza: gharama za kufanya service iweje zitolewe na serikali tena? Na gharama hizo ni kutoka katika faida iliyopatikana au uwekezaji bado unaendelee tu? Kwa kawaida issue kama hiyo inatakiwa iwe covered kutokana na faida iliyozalishwa katika kipindi chote cha biashara.
Wasiwasi wangu, kuna uwezekano mkubwa sana kuwa ATCL hadi hivi sasa bado inajiendesha bila kupata faida; na huenda ndiyo maana kila kitu inategemea kitolewa na serikali. Ninaendelea kuwa na mashaka na uwekezaji uliofanywa kwenye kuifufua hii kampuni, sidhani kama kuna utafiti ulifanyika wa kujua ilikufaje na je, kuna mahitaji kiasi gani kwa usafiri wa anga hapa nchini mpaka kufikia hatua ya kujiridhisha kuwa biashara hiyo inalipa; lakini pia kuna uwezekano mkubwa huenda hata sababu za kitaalamu hazikuzingatia kuhakikisha biashara inakuwa ni yenye tija.

Mwenye kuelewa zaidi ya haya, naomba anijuze
 
Mimi naamania kinachogomba hapa ni kwanza LUGHA na pili ni CHUKI BINAFSI! Nafafanua. LUGHA inagomba hasa hasa kaw uwepo wa neno SERVICE. Kwa wale ambao mmeshawahi kumiliki vyombo vya moto au mashine mbalimbali, mnajua hilo neno SERVICE, yaani kukifanyia chombo chako ukaguzi wa kitaalamu na kiufundi aidha kwa kubadilisha mafuta au oil au some delicate PARTS. Pia hili ni pamoja na kuendana na muda wa saa za kufanya kazi, and in this respect, muda wa kuruka angani. Haya mambo hayana ushabiki, muda wa service ukifika lazima u- complile irrespective na bila kujali Dogo au Mwepesi au Shimo atasema nini. Pili nadhani ushabiki wa kisiasa ndio unasukuma watu kusema na kuandika waandikayo! Na kwa vile ni watu wanao subiri jambo ndiyo waseme kwa sababu wameishiwa HOJA, basi linapotokea jambo kama hili, BASI wanapata kisemeo na wengine wanafuata tu hata kama hawajui suala lenyewe liko vipi!

Hujui kitu, tumeambiwa ndege zimeingiza bilioni 4.5 kama faida (hii nayo ni uongo kwasababu ATCL inaendeshwa kwa hasara kubwa).

Leo zinaenda kukarabatiwa kwa bilioni 14! Huu ni unyani tu, hakuna kingine.

Tunaoibiwa hapa ni wananchi, waliozinunua bila utaratibu wametajirika sana kwa kupiga cha juu. Na hata haya matengenezo wanaweka cha juu.
Ni suala la muda tu hili shirika litakufa kwa aibu kubwa.
 
Back
Top Bottom