Serikali yatangaza awamu ya pili ya ajira 5000 za Walimu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,280
Serikali imetangaza awamu ya pili ya ajira ya walimu 5,000 ili kufikia idadi ya walimu 13,000 kutokana na kibali kilichotolewa na Rais John Magufuli.

Septemba 7, mwaka jana Rais John Magufuli alitoa kibali cha ajira mpya za walimu 13,000 wa shule za msingi na sekondari pamoja na mafundi sanifu wa maabara za shule.

Akihutubia mkutano wa pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara jijini hapa jana, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tamisemi, Joseph Nyamhanga alisema awamu ya pili ya ajira ya walimu 5,000 itafanyika mapema mwaka huu.

Nyamhanga alisema awamu hiyo ya pili inafanyika baada ya ajira ya awamu ya kwanza ya walimu 8,000 kutangazwa. Walimu hao wameripoti kazini hasa maeneo ya vijijini tangu Desemba mwaka jana.

Alisema walimu 5,000 watakaoajiriwa awamu ya pili watapelekwa vijijini na kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa kwa shule za msingi na sekondari.

“Kuna shule za msingi na sekondari zaidi ya 2,500 ambazo hazikupangiwa walimu kwenye awamu ya kwanza ya ajira za walimu 8,000,” alisema.
Alisema shule zitapata walimu katika awamu ya pili na umuhimu utawekwa kwa shule zenye uhitaji hasa za vijijini.

Alisema Serikali imeweka utaratibu wa kuingia mkataba na walimu hao kwamba hawatahama kwenye kituo chao cha kazi hadi ipite miaka mitatu.
Nyamhanga alisema Serikali imetoa maelekezo kwa walimu wenye matatizo ya kiafya, lakini alisisitiza kuwa wale wenye visingizio hawataruhusiwa kuhama.

Naye Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Tamisemi, Gerald Mweli aliwataka walimu wakuu waache kuweka barua zenye nembo ya Serikali au halmashauri kwenye makundi ya Whatsapp.

“Matumizi ya mitandao ya kijamii. Tusiweke kila kitu kwenye makundi ya Whatsapp, hatutamvumilia mtu nimeona niseme hili kabla ya kuanza kuchukua maamuzi magumu,” alisema Mweli.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wakuu Tanzania Bara, Rehema Ramote amesema pamoja na juhudi za Serikali za kujenga vyumba vya madarasa, nyumba za Walimu na matundu ya vyoo bado kuna changamoto katika shule nyingi za msingi.
 
Hao walioajiriwa bado wanateseka tu mpaka leo, nina ndg yangu ameaijiriwa Bariadi DC, aliripoti tr 02/12/2020 mpaka leo hajapata pesa ya kujikimu achilia mbali salary, yani ameajiriwa na jamhuri lakini bado inabidi tumtumie hela ya kula.

Bado kama nchi hatujajua kipaombele chetu ni nn, wabunge wakichaguliwa ile wiki ya kuapa tayari wameshachukua hela ya suti na gari, wakiwa wanastaafu ile bunge linavunjwa tayari miamala inafanyika. Watumishi wa umma ni mtihani mkubwa
 
Dodoma,

Serikali imetangaza awamu ya pili ya ajira ya walimu 5,000 ili kufikia idadi ya walimu 13,000 kutokana na kibali kilichotolewa na Rais John Magufuli.

Septemba 7, mwaka jana Rais John Magufuli alitoa kibali cha ajira mpya za walimu 13,000 wa shule za msingi na sekondari pamoja na mafundi sanifu wa maabara za shule.

Akihutubia mkutano wa pili wa Umoja wa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi Tanzania Bara jijini hapa jana, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tamisemi, Joseph Nyamhanga alisema awamu ya pili ya ajira ya walimu 5,000 itafanyika mapema mwaka huu.

Nyamhanga alisema awamu hiyo ya pili inafanyika baada ya ajira ya awamu ya kwanza ya walimu 8,000 kutangazwa. Walimu hao wameripoti kazini hasa maeneo ya vijijini tangu Desemba mwaka jana.

Alisema walimu 5,000 watakaoajiriwa awamu ya pili watapelekwa vijijini na kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa kwa shule za msingi na sekondari.

“Kuna shule za msingi na sekondari zaidi ya 2,500 ambazo hazikupangiwa walimu kwenye awamu ya kwanza ya ajira za walimu 8,000,” alisema.

Alisema shule zitapata walimu katika awamu ya pili na umuhimu utawekwa kwa shule zenye uhitaji hasa za vijijini.

Alisema Serikali imeweka utaratibu wa kuingia mkataba na walimu hao kwamba hawatahama kwenye kituo chao cha kazi hadi ipite miaka mitatu.

Nyamhanga alisema Serikali imetoa maelekezo kwa walimu wenye matatizo ya kiafya, lakini alisisitiza kuwa wale wenye visingizio hawataruhusiwa kuhama.

Naye Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Tamisemi, Gerald Mweli aliwataka walimu wakuu waache kuweka barua zenye nembo ya Serikali au halmashauri kwenye makundi ya Whatsapp.

“Matumizi ya mitandao ya kijamii. Tusiweke kila kitu kwenye makundi ya Whatsapp, hatutamvumilia mtu nimeona niseme hili kabla ya kuanza kuchukua maamuzi magumu,” alisema Mweli.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Walimu Wakuu Tanzania Bara, Rehema Ramote amesema pamoja na juhudi za Serikali za kujenga vyumba vya madarasa, nyumba za Walimu na matundu ya vyoo bado kuna changamoto katika shule nyingi za msingi.

mwananchi.
=======================

maoni:
 
Muwakumbuke walimu wenye Masters na post graduate diploma, uwa mara nyingi hamtoi nafasi kwao kama mlivyofanya mara ya mwisho.
 
Kabisa mkuu hata mimi nakuunga mkono. Dirisha lifunguliwe watu waomba upya ili kutoa nafasi kwa wale ambao walikuwa na nyaraka pungufu kutuma maombi kwa utimilifu
Tumechoka kuomba watumie data hizo hizo mwenye kpata apate na mwenye kukosa akose tu.
 
Hili swala ni kumwachia Mungu tu.
Ogopa sana mtu anae kwambia ukishika namba moja nitakupa zawadi ukaishika lakini zawadi akapewa aliyeshika namba ya mwisho.
 
Hao walioajiriwa bado wanateseka tu mpaka leo, nina ndg yangu ameaijiriwa Bariadi DC, aliripoti tr 02/12/2020 mpaka leo hajapata pesa ya kujikimu achilia mbali salary, yani ameajiriwa na jamhuri lakini bado inabidi tumtumie hela ya kula.

Bado kama nchi hatujajua kipaombele chetu ni nn, wabunge wakichaguliwa ile wiki ya kuapa tayari wameshachukua hela ya suti na gari, wakiwa wanastaafu ile bunge linavunjwa tayari miamala inafanyika. Watumishi wa umma ni mtihani mkubwa
Nafikiri huwa hamfuatilii habari Mimi ninamarafaiki zangu wengi Sana ambao wameapata kazi za ualimu kwa miaka kadhaa iliyopita na wote wameanza kupata salary mwezi wa tatu na wachache Sana mwezi wa pili. Kwa hiyo unapoenda kwenye kazi ya ualimu unatakiwa kufunga mkanda kwanza
 
Back
Top Bottom