Serikali na Hatima ya ATCL

Serikali na Hatima ya ATCL

Hivi Anne Kilango yupo jamani, yule mwanamama mbunge mzalendo.
 
Hivi Anne Kilango yupo jamani, yule mwanamama mbunge mzalendo.

Yupo hili la ATCL hajaliona wala kulisikia yuko Dodoma kapoa akitoka anaenda Jimboni kwake .

Mzalendo JK kakaa kimya itakuwa Kilango ?
 
Yupo hili la ATCL hajaliona wala kulisikia yuko Dodoma kapoa akitoka anaenda Jimboni kwake .

Mzalendo JK kakaa kimya itakuwa Kilango ?


Wanahusika kwa njia moja ama nyingine nini? Maana ndo style ya TZ. Kigogo akihusika na ufisadi au mtu wake wa karibu akihusika na ufisadi uzalendo unawekwa kando...inabaki kigugumizi.

I am wondering about huu ukimya....nakumbuka issue ya Mengi vs Masha...it took less than 24 hrs to get a response from the govt!

Kunani ATCL, mbona serikali yote kimya? mbona wabunge wote kimya? Hakuna wa kumfunga paka kengele?
 
..jamani its time kuacha kumlaumu kila kitu JK,vipi Waziri wa mawasiliano ambaye hajasema chochote mpaka sasa na hata bunge wana uwezo wa kusikiliza na kuchukua hatua yeyote juu ya ufisadi,JK ataunda tume ngapi wakati aliowapa kazi wapo kimya tuu na hawaambiwi chochote au kuwajibishwa...kuna mawaziri na kamati za bunge zina nguvu sana na matatizo kama haya yapo ndani ya uwezo wao!
 
Na huyu ulimwendesha ? Samahani kama naye pia ni rafiki yako.
 
Na huyu ulimwendesha ? Samahani kama naye pia ni rafiki yako.


- Ohh yeah! it works both ways, yaani kuna wakati washikaji wangu wananiendesha na mimi ninawaendesha, juzi nilikuwa ninamuendesha waziri wa jamhuri wa sheria, kwetu haya huwa ni ya kawaida!.

- Inaonekana watu wengi humu JF huwa mnawabeba washikaji zenu migongoni mwenu, huoni kuwa ni hatari sana hiyo? au?

- By the way Mama Kilango, amekua nje ya nchi toka mwezi uliopita na bado hajarudi, leo yupo DC.

Thanxs!
 

- juzi nilikuwa ninamuendesha waziri wa jamhuri wa sheria, kwetu haya huwa ni ya kawaida!.

Mkuu nadhani ulimuuliza kuhusu mabadiliko ya katiba tunayolilia kila siku hapa JF, pia suala la kumpunguzia raisi madaraka bila shaka wakati uansubiri taa zinazoongoza bara bara ziruhusu, ulimuuliza pia JF ingependa kuona serikali haiingilii uhuru wa mahakama....hatupendi kujua mliongelea nini...wewe kama nguzo muhimu JF utakuwa umefikisha kwa namna moja vilio vyetu...

Thanks
 
Inavyoonekana akina DPP na team yake labda hawako makini na kazi zao au hawana utaalamu na mambo ya anga ndo maana wanasua sua katika kuwafikisha bodi ya ATCL mahakamani. Pia yawezekana kabisa hawana ushahidi ingawaje sijua ni ushahidi wa namna gani wautakao ikiwa kama IATA imekwishwa sema kwamba ATCL ina makosa 500. One mistake katika ndege chanzo cha janga la ajali na kupoteza maisha ya abiria wote, makosa 500 ni kama attempted suicide ya maofisa wa ATCL wanayotaka kuifanyia jamii nzima ya wasafiri bila kujali wanatokea wapi. Bahati yao tu hakuna msafiri alilalamika kwamba ATCL wamesababisha fear na hivyo emotional suffering au negligence pia causation itakuwa vigumu kui-prove. Kama hii hakuna, ushahidi miwngine ni circumstancial ambapo unafaa kuifikisha Atcl BODY kwa mzee pilato.
 
..cha ajabu na uzembe wote huo na ufisadi wa hili shirika hakuna hata mbunge mmoja kwa kutumia kamati zao aombe uchunguzi na kuwachukulia hatua wahusika,hii kitu wanachezea maisha ya watu na pesa za walipa kodi!

Hawawezi kuunda kamati kama JF haitatupa makombora kama yale yaliyotupwa kwa EL, NK na fisadiz wengine. Nyie subirieni, haya yakifika tu mtaanza kuwasikia wabunge wakianza kudai uchunguzi. Tuko hapa mtaniambia....
 
Mkuu nadhani ulimuuliza kuhusu mabadiliko ya katiba tunayolilia kila siku hapa JF, pia suala la kumpunguzia raisi madaraka bila shaka wakati uansubiri taa zinazoongoza bara bara ziruhusu, ulimuuliza pia JF ingependa kuona serikali haiingilii uhuru wa mahakama....hatupendi kujua mliongelea nini...wewe kama nguzo muhimu JF utakuwa umefikisha kwa namna moja vilio vyetu...

- Nilimuuliza maswali mengi sana kama ulivyosema na hasa kuhusu mafisadi na kubadili katiba, na ni kweli nilifikisha vilio vyetu hapa na nilipewa majibu mengi ya maswali yetu hapa.

Thanxs!
 
..jamani its time kuacha kumlaumu kila kitu JK,vipi Waziri wa mawasiliano ambaye hajasema chochote mpaka sasa na hata bunge wana uwezo wa kusikiliza na kuchukua hatua yeyote juu ya ufisadi,JK ataunda tume ngapi wakati aliowapa kazi wapo kimya tuu na hawaambiwi chochote au kuwajibishwa...kuna mawaziri na kamati za bunge zina nguvu sana na matatizo kama haya yapo ndani ya uwezo wao!

Kwani huyo JK anachosubiri kumfuta kazi huyo Waziri na hiyo bodi yake ni nini. Ni lazima kuwepo na tume?
 
NOTE: Any off topic response will be muted ASAP. Sorry for those interested to read em comments
 
Bysel

We kweli ni mwendawazi mu kama Mattaka.Unamtetea kwa sababu ya gani. Wewe Mataka kakutuma ili uje kumsafisha humu ndani ya FORUM. ATCL walipewa hizo 13 Bil na serikali na wamezila zoooooote.
JK ameleta USHIKAJI ktk kuendesha nchi matokeo yake ni hayooooooo. We mtu alishafukuzwa kazi na RAISI kwa Manufaa ya UMMA. leo hii unamrudisha na kumpa shirika kama lile. Anachuma Chake Mapema kwani Nafasi kama hizo Haziji Mara mbili.
Inamaa hakuna watanzania wengine wenye uwezo wa kila kitu mpaka amrudishe Mattaka

Nchi haiendeshwi kwa Ushikaji
 
Siwezi nikashangaa hilo. Takriban mwaka na nusu umepita toka nilipotoa ushauri usiolipwa kwa shirika hilo na kuwaambia waangalie upya visheni na misheni yao!

Walinitumia ujumbe feki na tiketi feki ya kuhudhuria mkutano fulani nikaenda kwa ajenti wa usafiri wa ndege na kukuta hakuna kitu kama hicho. Nikawashukuru na ninawashukuru mpaka leo.

Lakini haya ndio matunda ya kukataa ushauri. Na popote pale utakapokuta matatizo ya menejimenti partly hili linasababishwa na kiongozi kichwa ngumu ambaye ama ana pokea na kukubali ushauri mbovu au hakubali ushauri wowote.

Kudonoa nilichowagawia kina Bw. Makatta wakati huo ni kwamba biahsara ya mizigo itawabeba zaidi ATCL kuliko ya abiria kwani walichelewa kulishughulikia hili. Na ninaamini hadi wa leo kuwa shirika hilo likiwa na ndege za mizigo mikubwa bado lina nafasi hasa wakati huu wa bei ya mafuta ya ndege kushuka pia.

Ili kushughulikia abiria nilitamani wanipe nauli nikazungumze na Richard Branson (Virgin Airlines) kwa siku moja tu na ningekuja na dawa ambayo ingeliwafaa. Lakini kwa jinsi tunavyopenda safari sasa naruhusu yoyote tu aende acha mimi nile ugali na mchicha bongo na kutoa ushauri usiothaminiwa wala kulipiwa! Ule unaothaminiwa na kulipiwa kama mnavyojua ndio umeliingiza shirika hapo lilipo. Je, washauri hao wana tofauti na mafisadi wa EPA!
 
SIO haki kuwalaumu kina Makatta tu hapa. Uteuzi wetu wa Bodi za Wakurugenzi Tanzania ni mbovu, mbovu, mbovu kiasi cha kutisha!

ATCL ingelikuwa na Bodi inayofanya kazi kweli kama bodi lakini sio wakala wa kulipwa bila kufanya kazi wa kisiasa haya yasingeikuta jamani.

Wa kulaumu ni serikali na washauri wake wa menejimenti na usimamizi bora wa mashirika. Wakenya na wageni wengine wanakuja nchini kwetu na kuteua bodi za wakurugenzi zenye Watanzania, safi, wachapa kazi na wabunifu lakini sisi wenyewe tunayawekea mashirika yetu 'cluster bombs' halafu yakilipuka na kujerushi kelele kama balaa! Tuamkeni!

Shrika, Kampuni, chama au taasisi yoyote ya binadamu aidha inafanya vizuri au kufanya vibaya kutegemeana na kichwa! Yaani mkuu au wakuu wa mahala hapo. Wakiwa bomu habari ndiyo hiyo---tasisisi inaanguka. Wakiwa safi ---taasisi inapaa. Kwa hiyo tuchague kati ya upenzi na ushabiki wa ksiasa tufe njaa na masikini, au tuchague watu wenye upeo na uwezo wa kuleta mabadiliko tuuupe umasikini 'byebye'!
 
Wajinga ndio waliwao

Tunapoteza TZS Ngapi kwa watalii ambao walikuwa wameshapanga safari zao kuja huku kwetu kupanda Kilimanjaro, Kutembelea mbuga za wanyama, fukwe za Bahari, miji mikogwe kama Z'bar, bagamoyo, Sadan

Serikali yetu imekaaaaaaa kimya haijamchukulia mtu yeyeto hatua za kinidhamu. Kweli ndio tunapima Accountability namna hiii

JK anafanya nini, anakaaa tu au hasomi magazeti au wasauri wake hawampi habari za huku nje ya Ikulu. Mi sipati picha. TV huwa anaaangalia kweli au huwa wanamchagulia Tv station za kuangalia?. Hasomi Internet habari mbali mbali kuhusu nchi yake.

Nisaidie jamani, huyu raisi wety ana washauri kweli madhubuti wanaoangali nchi inateketea na wao wanamficha Uozo Raisi
 
Kamati zitaundwa ngapi.???????????

Yaaani unataka kuwapa watu ulaji tena. Kamati ngapi zimeundwa na hatujaona na report kali zenye kuwachukulia Hatua kali wale waohujumu Uchumi?.

Tumechoka na haya mambo serikali ya JK inayoyafanya. Kweli tumechoka na Kiama Yao ipo njiani yaja. Hakuna Jiwe litaachwa Kuguswa
 
ATC yapigwa nyundo nyingine
*SASA YAZUIWA KUFANYA BIASHARA


Leon Bahati
SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL) limepata pigo jingine baada ya kufungiwa na Umoja wa Mashirika ya Ndege Duniani (IATA), hali ambayo inalifanya shirika hilo kutoweza kufanya shughuli zozote za kibiashara na mashirika mengine ya ndege.

Hatua hiyo imekuwa sawa na masumari wa moto kwenye kidonda cha ATCL, ambayo inasubiri Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga (TCAA) kufanyia kazi nyaraka ilizowasilisha ili irejeshewe cheti cha usalama wa anga.

TCAA ilichukua hatua ya kuinyang'anya ATCL leseni ya kurusha ndege baada ya kubaini kuwa nyaraka zilizojazwa na shirika hilo la serikali la usafiri wa anga zilikuwa na mapungufu kulinganisha na sheria za mamlaka hiyo na hivyo kuitaka ATCL kuzishughulikia upya, jambo ambalo lilifanywa na shirika hilo na hivyo TCAA kuahidi kuzifanyia kazi katika muda wa siku 10 za kazi.

Lakini ATCL ikiwa inasubiri kumalizika kwa siku hizo 10 za kikazi baada ya kufanyia marekebisho nyaraka hizo, imepata pigo jingine baada ya IATA kuifungia kwa muda kwa maelezo kuwa uamuzi huo umetokana na TCAA kulinyang'anya shirika hilo cheti cha usafiri wa anga.

Taarifa zilizolifikia Mwananchi jana zilieleza kuwa IATA imesambaza waraka huo wa kulisimamisha shirika hilo kwa wadau wake, hasa kwa mawakala wa usafiri wa anga na mashirika ya ndege kote duniani.

Waraka huo wa Desemba 15, mwaka huu, umesambazwa na ofisi ya IATA, Kanda ya Afrika Mashariki ambayo iko jijini Nairobi na imesainiwa na meneja wa kanda, Hassim Pandor.

"Tungependa kuwaarifu kuwa IATA imeisimamisha mara moja ATCL (TC-197)," inaeleza barua hiyo. "Shirika hilo limeacha kufanya shughuli zake kutokana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga ya Tanzania kuinyang'anya AOC (cheti cha usafiri wa anga). "Kusimamishwa huko kunaendana na Azimio la 850, kiambatanisho F."

Adhabu hiyo inamaanisha kuwa ATCL sasa itashindwa kuwahamishia kwenye ndege za mashirika mengine wasafiri wake waliokuwa wamefanya taratibu za muda mrefu (booking) za safari kwa kutumia ndege za shirika hilo, hali ambayo italifanya lianze kutafuta wateja upya baada ya kupata AOB. Baadhi ya wadau wa safari za ndege nchini waliozungumza na Mwananchi, walieleza kuwa tangazo hilo lina athari kubwa za kibiashara kwa ATCL.

Akizungumza kwa sharti la kutotaja jina gazetini, mmoja wa viongozi katika moja ya kampuni ya huduma za safari za ndege nchini, alisema kuwa hata kama ATCL itaanza huduma zake hivi karibuni, mawakala wengi watakuwa na wasiwasi wa kutumia ndege zake. "Hii ni sawasawa na kutangaziwa sifa mbaya kwa marafiki zako jambo ambalo licha ya kukuchafulia sifa, itatia doa la kutoaminika kwao," alisema.

Mdau mwingine naye alisema kuwa hatua hiyo itazua mzozo mkubwa wa ATCL kukubalika katika shughuli za kibenki kimataifa, maana hiyo ni sawa na sumu ambayo itachukua muda mrefu kufutika. "Taarifa ya kufungiwa inaenda haraka na inachukuliwa kwa umakini mkubwa na mabenki kwa sababu ni jambo linaloweza kuwasababishia hasara. Lakini ikitokea ATCL imeruhusiwa, inawezekana taarifa zake zisiende kwa kasi hiyo," alisema na kuongeza:

"Hali hiyo itasababisha baadhi ya taasisi za kifedha kuifuta ATCL katika milolongo ya kifedha na hata litakaporuhusiwa, hawatairejesha na mawakala wengi watapata wakati mgumu wa kufanya nayo kibiashara. Badala yake watapenda kufanya biashara na mashirika mbadala." Ofisa Mkuu Mtendaji wa ATCL, David Mataka hakupatikana jana kufafanua taarifa hiyo baada ya kuripotiwa kukabiliwa na majukumu ya kikazi.

Ofisa Uhusiano wa TCAA alisema kuwa tayari wamepokea vielelezo vya ATCL vinavyoonyesha masahihisho ya dosari zilizosababisha wawafungie kurusha ndege na kinachofanyika ni uhakiki, hivyo upo uwezekano wa kerejeshewa leseni hiyo wakati wowote.
 
Is Accountability finaly coming to Tanzania? Lets wait and see.

The government has given the Air Tanzania Corporation Limited (ATCL) board seven days to explain why the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) suspended its operations, the Minister for Infrastructure Development, Dr Shukuru Kawambwa, has said.

The minister told a news conference in Dar es Salaam yesterday that the government and the general public were shocked and disappointed by the current state of the ATCL. “I have given the board seven days to present explicit explanations on what has led to such an embarrassing situation … all those involved will be taken to task,” Dr Kawambwa said.

The minister’s remarks come a few days after the TCAA suspended the operations of the airline due to what has been described as ‘documentation’ problems – for which the Authority has also suspended the airline’s Air Operator Certificate for falling short of International Air Transport Association (IATA) requirements.

Workers of the crisis-ridden ATCL who met in Dar es Salaam last week demanded immediate resignation of the company’s management as well as its board of directors. On Wednesday, IATA too suspended the ATCL membership, meaning it cannot deal with its 230-member airlines around the world. However, the minister stated that the government would continue backing the airline in it efforts to regain both its international recognition and business.

“We expect that the ATCL management will soon meet the conditions to enable it go back to business … the government will provide assistance where necessary,” Dr Kawambwa said.
He also said the ATCL needs some $273 million just to remain afloat. But Mr Mohamed Missanga, the chairman of the parliamentary committee for Infrastructure, had earlier said the airline would require at least 633bn/- to keep it flying.

Mr Missanga said the national flag carrier needs about $507m to recapitalize and stabilize it following its ‘divorce’ from the failed South African Airways joint venture. He said the government was the only dependable source of income at the moment – which did not allocate any funds to that effect in its 2008/9 budget despite high expectations, the MP noted.

Meanwhile, the government has asked the Chinese government, through its private companies to run another crisis ridden Tanzania and Zambia Railways Authority (Tazara). Dr Kawambwa told the reporters that the two governments had already held preliminary talks and that they were waiting for response from the Chinese government. He admitted that Tazara was in terrible state and that urgent intervention was needed to rescue it.

Tanzania Standard Newspapers|Home
 
Back
Top Bottom