Serikali iwalipe walimu wa shule za binafsi mishahara kwa RIBA ndogo kipindi hiki cha Corona

Superbug

JF-Expert Member
Jan 31, 2018
12,417
30,927
Serikali iwakopeshe mishahara walimu wa shule binafsi kipindi hiki Cha Corona kwa RIBA ndogo sana.

Ikumbukwe kwamba Hawa ni WATANZANIA wenzetu japo Kuna wachache sio WATANZANIA.

Serikali ione huruma kwa maelfu ya WATANZANIA watakaoathirika kutokana na janga hili. Binafsi nimetoa machozi kwaajili Yao nimevaa viatu vyao imeniuma Sana.

Madam ni mwajiriwa wa shule X basi hiyo ni dhamana yake alipwe mshahara na serikali halafu shule zitakapofunguliwa ada zikianza kukusanywa basi watarejesha kwa makato kama ya HESLB wanavyofanya ila iwe riba ndogo sana maana sio kosa lao.

Na mkataba useme wazi hatahama shule hiyo mpaka deni liishe.

Naiomba serikali iliangalie hili watu wake wanaanza kuadhirika huku mitaani.

Naamini serikali itasikia kama inavyosikia mengine.
 
Ikumbukwe serikali ndio mfariji mkuu duniani kabla ya Mungu wa mbinguni ambae ndio hatua ya mwisho.
 
Kwanini walimu tu? Ofisi nyingi zimefungwa, viwanda, mabar, hotel etc etc etc.

Kwa muda huu kula mtu atulie tu.
 
Angalau walimu wanadhamana wahudumu wa baa sielewi dhamana kwa mujibu wa mikataba Yao ikoje
Kwanini walimu tu? Ofisi nyingi zimefungwa, viwanda, mabar, hotel etc etc etc.

Kwa muda huu kula mtu atulie tu.
 
Serikali iwakopeshe mishahara walimu wa shule binafsi kipindi hiki Cha Corona kwa RIBA ndogo sana.

Ikumbukwe kwamba Hawa ni WATANZANIA wenzetu japo Kuna wachache sio WATANZANIA.

Serikali ione huruma kwa maelfu ya WATANZANIA watakaoathirika kutokana na janga hili. Binafsi nimetoa machozi kwaajili Yao nimevaa viatu vyao imeniuma Sana.

Madam ni mwajiriwa wa shule X basi hiyo ni dhamana yake alipwe mshahara na serikali halafu shule zitakapofunguliwa ada zikianza kukusanywa basi watarejesha kwa makato kama ya HESLB wanavyofanya ila iwe riba ndogo sana maana sio kosa lao.

Na mkataba useme wazi hatahama shule hiyo mpaka deni liishe.

Naiomba serikali iliangalie hili watu wake wanaanza kuadhirika huku mitaani.

Naamini serikali itasikia kama inavyosikia mengine.
Serikali ipi hiyo unayoisema? Duuuh jiongeze Mdau, hiii hiii Ya jiwe Au unamaaanisha ya mseveni? Au ile ya kenyaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toka nazaliwa sijawai ona ujinga kihasi hiki, Je ulishajiribu kuvaa viatu vya wasio na ajira kabisa ambao munasema wanalialia eti kilasiku kumbe nyie mwezi tu hamuwezi himiri.

Ujinga sana huu.
 
Unapenda sana ku-refer wahudumu wa baa.Umechanjiwa kwa hawa watoa huduma za vilevi?Wewe ni mteja wao mzuri bila shaka.

My take:

Mawazo yako ni mazuri,ila nami nimetafakari beyond!!

Hahahahaha!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaposema napenda kuwazungumzia bar maids ni kwenye post ipi nishawahi kuwataja hao watu au unanifananisha
 
Hapa ndipo ilipo tofauti kati ya nchi tajiri na nchi masikini, hatuwezi kujihudumia kama taifa hata miezi sita. Hili gonjwa likikita mizizi na kuishi na sisi Kwa mwaka mmoja tutashuhudia mageuzi makubwa mno ya maisha ya mwanadamu.

Sikujua kama binadamu ni very delicate kiasi hiki.
 
Back
Top Bottom