Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,604
Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.
Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini, unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.
Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.
Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.
Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.
Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.
Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.
Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.
Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.
Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.
Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.
Naomba kuwasilisha.
Paskali
Update
Kazi ya ujenzi wa Ngome ya Yesu pale Kimara Temboni, inafanyika kupitia kadi zinaitwa Partnership, hupangiwi kiwango, unajifanyia personal assessment ndipo unajaza!.
Watumishi matapeli kumuona ni lazima utoe 200,000, kuna watu walikuwa na 100,000 walitoa na zikapokelewa, watu wa 200,000 walipoongezeka, wale wa 100,000 walirudishiwa fedha zao, wakaambiwa wakadundulize mpaka zitimie 200,000 ndipo warudi.
Ukimuona Kuhani Mussa anakuombea na kukupatia vifaa vya kiroho bure extra utalipia lakini kuwaona matapeli hawa, unatakiwa kwenda kuleta kwanza sadaka, with the amount, from 6 figures ndipo uombewe!.
P
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.
Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini, unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.
Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.
Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.
Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.
Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.
Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.
Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.
Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.
Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.
Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.
Naomba kuwasilisha.
Paskali
Update
Mkuu Mywangu, usimwingize Mtumishi kweli wa Mungu, Kuhani Mussa, kumuona Kuhani Musa ni bure ila unaweza kuleta sadaka yako yoyote.Kuhani Musa pale Kimara Temboni kaporomosha mjengo wa billion kadhaa! Alianzia kwenye banda la mabati!
Kazi ya ujenzi wa Ngome ya Yesu pale Kimara Temboni, inafanyika kupitia kadi zinaitwa Partnership, hupangiwi kiwango, unajifanyia personal assessment ndipo unajaza!.
Watumishi matapeli kumuona ni lazima utoe 200,000, kuna watu walikuwa na 100,000 walitoa na zikapokelewa, watu wa 200,000 walipoongezeka, wale wa 100,000 walirudishiwa fedha zao, wakaambiwa wakadundulize mpaka zitimie 200,000 ndipo warudi.
Ukimuona Kuhani Mussa anakuombea na kukupatia vifaa vya kiroho bure extra utalipia lakini kuwaona matapeli hawa, unatakiwa kwenda kuleta kwanza sadaka, with the amount, from 6 figures ndipo uombewe!.
P