Serikali ichukue hatua hizi haraka ili kuinusuru nchi na tatizo la upungufu wa fedha za kigeni

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Jan 26, 2020
3,721
11,717
1. Serikali isitishe kwa muda matumizi yasiyo ya lazima (anasa) yanayohitaji fedha za kigeni kama vile kununua magari ya kutembelea viongozi na safari za nje ya nchi (zote mpaka za SSH hazina tija).

2. Kampuni za ndani zitakazolipwa kwa shilingi zipewe kipaumbele kwenye miradi ya ujenzi na uwekezaji mwingine.

3. Serikali isitishe kukopa mikopo ya nje. Kwasasa mapato yetu ya fedha za kigeni mengi yanaishia kuhudumia madeni ya nje yaliyokopwa kwa pupa na serikali hii ya SSH kwa ushauri mbovu wa Mwigulu. Serikali isiongeze mzigo mwingine. Ikope ndani kwa kuuza bondi na njia nyinginezo.

4. Wizara ya fedha na wizara ya mipango ziwekwe chini ya ofisi ya makamu wa rais. Ni wazi kuwa hizo wizara mbili wameshindwa kujisimamia, na mamlaka kuu haina ujuzi wala uwezo wa kuzisimamia. Ni vema kazi hiyo apewe Dr. Mpango kwa wizara hizo kuwekwa chini yake rasmi.

5. Tunakaribia kutumbukia kwenye mgogoro mkubwa wa kiuchumi, majibu ya kisiasa na shortcuts haziwezi kusaidia. Siasa maji taka za kutoa "ufafanuzi" na matamko ya kijingajinga hayatatufikisha popote. Na wala kuvutia uwekezaji wa nje kwa njia za kihuni na rushwa hauwezi kutufikisha popote zaidi ya kutengeneza matatizo mengine.

Hauwezi kuuficha mdororo wa kiuchumi, sote tunaona kinachoendelea kwenye upatikanaji wa mafuta. Serikali ichukue hatua haraka.
 
Kuna nchi moja huko kuna viongozi wa mchongo, hawana uchungu na maisha ya raia pamoja na rasilimali zao.

Kiufupi ni kikundi cha wahuni tu, hawapo kusaidia raia bali kuwaibia tu, wapo kama vibaka.
Wanastaajabisha jinsi wanavyoweka anasa na ubadhirifu mbele mpaka kuitumbukiza nchi kwenye hali iliyonayo sasa.
 
1. Hakuna safari ya kikazi ya Rais ya nje isiyo na tija, kama hufuatilii ni uvivu wako lakini mara kwa mara zinatolewa press conference na DPC Zuhuru kuhusu ziara hizo na faida zake. Dunia ya Sasa inahitaji mazungumzo lakini anapokwenda nje kuzungumza ina tija zaidi kuliko kuwakilishwa bila hivyo tusingesikua Rais wa Marekana anazuru katika nchi za Afrika.

2. Hoja ya pili ni mpaka pale nchi itakapokuwa na wawekezaji wengi na wenye uwezo wa ndani wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa. Kwa mfano uwekezaji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee unagharimi Zaidi ya Dola za kimarekani billion 7 ambazo ni sawa na Trillion 16 za kitanzania. Kwa wawekezaji waliopo ni nani ambaye ana hiko kiwango Cha pesa kutukamilishia ujenzi huo? Hata matajiri 10 wakubwa wakawekeza Kila kitu Chao Bado hawawezi kufanya mradi kama huo. Ingefaa kweli miradi ijengwe na wazawa ili malipo yafanyike Kwa shilingi lakini tuseme kweli tutachelewa Zaidi.

Hoja ya Tatu, Serikali inakopa ili kuharakisha maendeleo na zaidi mikopo hiyo ni Ile yenye riba nafuu sana au isiyo na riba kabisa. Pia, tunakopa ili tuwe na akiba kubwa ya fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi ya nje, bidhaa na Teknolojia. Ingefaa utupe na ufafanuzi, Serikali itumie njia Gani kugharamia Kwa haraka miradi mikubwa kama Tukiachana na mikopo.

Hoja ya nne, umemtaja Makamu wa Rais Dkt.Mpango kama mtu mwenye uwezo wa kusimamia wizara ya fedha na wizara ya mipango na uwekezaji Kwa uwezo wake wa kitaaluma kwenye masuala ya uchumi na fedha na ndio maana ukataka wizara hizo ziwe chini yake lakini umesahau jambo Moja kubwa ambalo litahitaji majibu baadaye, je asipokuwepo Dkt Mpango katika ofisi ya Makamu wa Rais na akawepo mtaalamu wa Sanaa ofisi ya Makamu wa Rais, je Bado itahitajika wizara hizo chini ya ofisi ya Makamu wa Rais?

Hoja ya Tano, siamini kama unaendesha asasi yoyote ya kufanya tathmini ya uchumi mpaka uje na hoja ya kwamba tunakwenda kutumbukia kwenye mdororo wa kiuchumi. Ni vema hoja yako hii ingejikitika kwenye takwimu halisi Zaidi ya blabla Kwa sababu uchumi ni namba na namba hazidanganyi.
 
1. Hakuna safari ya kikazi ya Rais ya nje isiyo na tija, kama hufuatilii ni uvivu wako lakini mara kwa mara zinatolewa press conference na DPC Zuhuru kuhusu ziara hizo na faida zake. Dunia ya Sasa inahitaji mazungumzo lakini anapokwenda nje kuzungumza ina tija zaidi kuliko kuwakilishwa bila hivyo tusingesikua Rais wa Marekana anazuru katika nchi za Afrika.

2. Hoja ya pili ni mpaka pale nchi itakapokuwa na wawekezaji wengi na wenye uwezo wa ndani wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa. Kwa mfano uwekezaji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee unagharimi Zaidi ya Dola za kimarekani billion 7 ambazo ni sawa na Trillion 16 za kitanzania. Kwa wawekezaji waliopo ni nani ambaye ana hiko kiwango Cha pesa kutukamilishia ujenzi huo? Hata matajiri 10 wakubwa wakawekeza Kila kitu Chao Bado hawawezi kufanya mradi kama huo. Ingefaa kweli miradi ijengwe na wazawa ili malipo yafanyike Kwa shilingi lakini tuseme kweli tutachelewa Zaidi.

Hoja ya Tatu, Serikali inakopa ili kuharakisha maendeleo na zaidi mikopo hiyo ni Ile yenye riba nafuu sana au isiyo na riba kabisa. Pia, tunakopa ili tuwe na akiba kubwa ya fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi ya nje, bidhaa na Teknolojia. Ingefaa utupe na ufafanuzi, Serikali itumie njia Gani kugharamia Kwa haraka miradi mikubwa kama Tukiachana na mikopo.

Hoja ya nne, umemtaja Makamu wa Rais Dkt.Mpango kama mtu mwenye uwezo wa kusimamia wizara ya fedha na wizara ya mipango na uwekezaji Kwa uwezo wake wa kitaaluma kwenye masuala ya uchumi na fedha na ndio maana ukataka wizara hizo ziwe chini yake lakini umesahau jambo Moja kubwa ambalo litahitaji majibu baadaye, je asipokuwepo Dkt Mpango katika ofisi ya Makamu wa Rais na akawepo mtaalamu wa Sanaa ofisi ya Makamu wa Rais, je Bado itahitajika wizara hizo chini ya ofisi ya Makamu wa Rais?

Hoja ya Tano, siamini kama unaendesha asasi yoyote ya kufanya tathmini ya uchumi mpaka uje na hoja ya kwamba tunakwenda kutumbukia kwenye mdororo wa kiuchumi. Ni vema hoja yako hii ingejikitika kwenye takwimu halisi Zaidi ya blabla Kwa sababu uchumi ni namba na namba hazidanganyi.
SAFARI ZA RAHIS HAZINA TIJA HATA KIDOGO
 
1. Hakuna safari ya kikazi ya Rais ya nje isiyo na tija, kama hufuatilii ni uvivu wako lakini mara kwa mara zinatolewa press conference na DPC Zuhuru kuhusu ziara hizo na faida zake. Dunia ya Sasa inahitaji mazungumzo lakini anapokwenda nje kuzungumza ina tija zaidi kuliko kuwakilishwa bila hivyo tusingesikua Rais wa Marekana anazuru katika nchi za Afrika.

2. Hoja ya pili ni mpaka pale nchi itakapokuwa na wawekezaji wengi na wenye uwezo wa ndani wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa. Kwa mfano uwekezaji kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee unagharimi Zaidi ya Dola za kimarekani billion 7 ambazo ni sawa na Trillion 16 za kitanzania. Kwa wawekezaji waliopo ni nani ambaye ana hiko kiwango Cha pesa kutukamilishia ujenzi huo? Hata matajiri 10 wakubwa wakawekeza Kila kitu Chao Bado hawawezi kufanya mradi kama huo. Ingefaa kweli miradi ijengwe na wazawa ili malipo yafanyike Kwa shilingi lakini tuseme kweli tutachelewa Zaidi.

Hoja ya Tatu, Serikali inakopa ili kuharakisha maendeleo na zaidi mikopo hiyo ni Ile yenye riba nafuu sana au isiyo na riba kabisa. Pia, tunakopa ili tuwe na akiba kubwa ya fedha za kigeni kwa ajili ya manunuzi ya nje, bidhaa na Teknolojia. Ingefaa utupe na ufafanuzi, Serikali itumie njia Gani kugharamia Kwa haraka miradi mikubwa kama Tukiachana na mikopo.

Hoja ya nne, umemtaja Makamu wa Rais Dkt.Mpango kama mtu mwenye uwezo wa kusimamia wizara ya fedha na wizara ya mipango na uwekezaji Kwa uwezo wake wa kitaaluma kwenye masuala ya uchumi na fedha na ndio maana ukataka wizara hizo ziwe chini yake lakini umesahau jambo Moja kubwa ambalo litahitaji majibu baadaye, je asipokuwepo Dkt Mpango katika ofisi ya Makamu wa Rais na akawepo mtaalamu wa Sanaa ofisi ya Makamu wa Rais, je Bado itahitajika wizara hizo chini ya ofisi ya Makamu wa Rais?

Hoja ya Tano, siamini kama unaendesha asasi yoyote ya kufanya tathmini ya uchumi mpaka uje na hoja ya kwamba tunakwenda kutumbukia kwenye mdororo wa kiuchumi. Ni vema hoja yako hii ingejikitika kwenye takwimu halisi Zaidi ya blabla Kwa sababu uchumi ni namba na namba hazidanganyi.
1. Kuna tofauti kubwa kati ya safari ya Biden nje ya nchi yake na safari ya rais wetu. USA anamaslahi mengi nje ya nchi, wana makampuni makubwa yanayaiingizia Marekani mabilioni ya fedha yanayofanya operations zake nje ya Marekani.
Safari zetu sisi ni kwenda kuvutia wawekezaji, kwenda kuomba misaada na mikopo. Matunda ya safari za SSH ndio hayo mauzauza ya DPW na madeni makubwa. Hazina tija!

2. Bwawa la umeme na reli havijengwi kwa mwaka mmoja. Hizo gharama ulizozitaja ni makadirio ya mradi wote ambao utachukua karibu miaka 10. Kwakuwa inajengwa na wakandarasi wa nje ni kweli kwamba lazima tutalipa kiasi fulani kwa fedha za kigeni. Lakini tunaweza kuhakikisha materials zote zinazopatika ndani basi zinanunuliwa ndani ( vitu vingi tu kwenye hiyo miradi vinatoka nje wakati tunavyo viwanda vya ndani vyenye uwezo wa kuzalisha), pamoja na subcontractors wote wa ndani wenye uwezo kufanya baadhi ya kazi wanapewa kipaumbele.

Lakini pia, miradi niliyokuwa nimeilenga zaidi ni ya barabara na majengo ya serikali. Hayo tunao wakandarasi wenye uwezo wa kujenga mingi ya miradi hiyo. Wapewe kipaumbele.

Hoja ya kukopa ili kuharakisha maendeleo haina maana kama mikopo hiyo inageuka kuwa mzigo kwenye uchumi wa nchi.

Hoja ya wizara ya fedha kuwekwa chini ya Dr. Mpango ni jambo la kutumia rasilmali ukizonazo kwa wakati huo. Rais angeweza hata kumwondoa Mwigulu na kumweka mtu mwingine pale, lakini itakuwa ni kama kufanya majaribio. Hiki ni kipindi cha mpito, serikali inaye mtaalamu wa uchumi ambaye amethibishwa kwa vitendo uwezo wake mkubwa wa kusimamia uchumi wa nchi, naye ni makamu wa rais. Kushindwa kumtumia kuzisimamia hizo wizara ni kushindwa kutumia rasilmali ulizonazo kutatua matatizo.
 
1. Serikali isitishe kwa muda matumizi yasiyo ya lazima (anasa) yanayohitaji fedha za kigeni kama vile kununua magari ya kutembelea viongozi na safari za nje ya nchi (zote mpaka za SSH hazina tija).

2. Kampuni za ndani zitakazolipwa kwa shilingi zipewe kipaumbele kwenye miradi ya ujenzi na uwekezaji mwingine.

3. Serikali isitishe kukopa mikopo ya nje. Kwasasa mapato yetu ya fedha za kigeni mengi yanaishia kuhudumia madeni ya nje yaliyokopwa kwa pupa na serikali hii ya SSH kwa ushauri mbovu wa Mwigulu. Serikali isiongeze mzigo mwingine. Ikope ndani kwa kuuza bondi na njia nyinginezo.

4. Wizara ya fedha na wizara ya mipango ziwekwe chini ya ofisi ya makamu wa rais. Ni wazi kuwa hizo wizara mbili wameshindwa kujisimamia, na mamlaka kuu haina ujuzi wala uwezo wa kuzisimamia. Ni vema kazi hiyo apewe Dr. Mpango kwa wizara hizo kuwekwa chini yake rasmi.

5. Tunakaribia kutumbukia kwenye mgogoro mkubwa wa kiuchumi, majibu ya kisiasa na shortcuts haziwezi kusaidia. Siasa maji taka za kutoa "ufafanuzi" na matamko ya kijingajinga hayatatufikisha popote. Na wala kuvutia uwekezaji wa nje kwa njia za kihuni na rushwa hauwezi kutufikisha popote zaidi ya kutengeneza matatizo mengine.

Hauwezi kuuficha mdororo wa kiuchumi, sote tunaona kinachoendelea kwenye upatikanaji wa mafuta. Serikali ichukue hatua haraka.
Hoja murua kbs ila sasa hapo Kweny magar ya kifahar na safar za nje labda jua lianze kutoka magharibi kwenda mashariki!!!
 
Nikikumbuka miezi 5 nyuma, bibi alisema Tz inaakiba ya kutosha ya fedha za kigeni kuliko nchi yyte ya EAC 🤣,

Ni wazi kama kikao cha Jana na world bank kisipo zaa Matunda basic, desember salary za polis na teachers hazitoki
Bila shaka ilipigwa kamba na Mwigulu. Ukiwa mvivu kufuatilia mambo utadanganywa sana bongo.
 
Back
Top Bottom