Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,115
TAARIFA KWA UMMA
KANUNI ZA MADUKA YA KUBADILISHA FEDHA ZA KIGENI ZA MWAKA 2023
Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuutaarifu umma kwamba, kwa mamlaka iliyopewa chini ya Sheria ya Fedha za Kigeni (Sura namba 271), imetoa Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2023. Kanuni hizo zilichapishwa kwenye Gazeti la Serikali namba 729 la tarehe 6 Oktoba 2023.
Pamoja na mambo mengine, Kanuni hizo zimeweka madaraja matatu ya leseni za biashara ya kubadilisha fedha za kigeni kama ifuatavyo:-
1. Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A
2. (a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A ni duka linalomilikiwa na wageni au wenyeji lililoruhusiwa kufungua matawi sehemu yoyote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(b) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A linalomilikiwa na wageni litatakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania bilioni moja.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A linalomilikiwa na wenyeji lilitakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania milioni mia tano.
(d) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A litaruhusiwa kufanya miamala ya papo kwa papo, kutuma fedha na kufanya biashara kama wakala wa benki, taasisi ya fedha, kampuni ya bima, mtoa huduma wa fedha kwa njia ya simu, au huduma nyingine zozote za fedha kama itakavyoidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania.
Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B
(a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B ni duka la kubadilisha fedha za kigeni linalomilikiwa na wenyeji.
(b) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B halitaruhusiwa kufungua matawi kwa ajili ya kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B litatakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania milioni mia mbili.
(d) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B litaruhusiwa kufanya miamala ya papo kwa papo na kufanya biashara kama wakala wa benki, taasisi ya fedha, kampuni ya bima, mtoa huduma wa fedha kwa njia ya simu, au huduma nyingine zozote za fedha kama itakavyoidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania.
3. Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C
(a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C ni duka la kubadilisha fedha za kigeni lililoanzishwa na hoteli (yenye hadhi ya nyota tatu au zaidi) kwa ajili ya kufanya miamala ya papo kwa papo kwa wateja wa hoteli tu.
(b) Leseni ya Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C itatolewa kwa hoteli au kwa mmiliki wa hoteli.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C halitatakiwa kuwa na mtaji wa kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni.
Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2023, ambazo zimefuta rasmi Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2019, zinapatikana kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania kupitia:
GAVANA BENKI KUU YA TANZANIA
KANUNI ZA MADUKA YA KUBADILISHA FEDHA ZA KIGENI ZA MWAKA 2023
Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuutaarifu umma kwamba, kwa mamlaka iliyopewa chini ya Sheria ya Fedha za Kigeni (Sura namba 271), imetoa Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2023. Kanuni hizo zilichapishwa kwenye Gazeti la Serikali namba 729 la tarehe 6 Oktoba 2023.
Pamoja na mambo mengine, Kanuni hizo zimeweka madaraja matatu ya leseni za biashara ya kubadilisha fedha za kigeni kama ifuatavyo:-
1. Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A
2. (a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A ni duka linalomilikiwa na wageni au wenyeji lililoruhusiwa kufungua matawi sehemu yoyote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(b) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A linalomilikiwa na wageni litatakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania bilioni moja.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A linalomilikiwa na wenyeji lilitakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania milioni mia tano.
(d) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja A litaruhusiwa kufanya miamala ya papo kwa papo, kutuma fedha na kufanya biashara kama wakala wa benki, taasisi ya fedha, kampuni ya bima, mtoa huduma wa fedha kwa njia ya simu, au huduma nyingine zozote za fedha kama itakavyoidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania.
Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B
(a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B ni duka la kubadilisha fedha za kigeni linalomilikiwa na wenyeji.
(b) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B halitaruhusiwa kufungua matawi kwa ajili ya kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B litatakiwa kuwa na mtaji usiopungua Shilingi za Tanzania milioni mia mbili.
(d) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja B litaruhusiwa kufanya miamala ya papo kwa papo na kufanya biashara kama wakala wa benki, taasisi ya fedha, kampuni ya bima, mtoa huduma wa fedha kwa njia ya simu, au huduma nyingine zozote za fedha kama itakavyoidhinishwa na Benki Kuu ya Tanzania.
3. Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C
(a) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C ni duka la kubadilisha fedha za kigeni lililoanzishwa na hoteli (yenye hadhi ya nyota tatu au zaidi) kwa ajili ya kufanya miamala ya papo kwa papo kwa wateja wa hoteli tu.
(b) Leseni ya Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C itatolewa kwa hoteli au kwa mmiliki wa hoteli.
(c) Duka la Kubadilisha Fedha za Kigeni Daraja C halitatakiwa kuwa na mtaji wa kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni.
Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2023, ambazo zimefuta rasmi Kanuni za Maduka ya Kubadilisha Fedha za Kigeni za mwaka 2019, zinapatikana kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania kupitia:
GAVANA BENKI KUU YA TANZANIA