Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, leo Bungeni ijini Dodoma alisimama kutoa taarifa kuhusu kuidhinishwa kwa sera ya elimu na mafunzo ya Elimu 2014 toleo la 2023, amesema sera ya Elimu na mafunzo imefanyiwa mabadiliko kwenye maeneo kadhaa kulinganisha na sera iliyopita na maeneo hayo ni elimu ya lazima kuwa ya miaka 10 badala ya 7, aidha elimu hiyo lazima inajumuisha elimu ya msingi ya miaka 6 na elimu ya sekondari ya chini itatolewa kwa miaka 4, utekelezwaji wa pendekezo hilo utaanza kufanyika mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa Darasa la 7.

 
Sasa kama mtihani wa elimu ya msingi umefutwa kwa hiyo watafanya mtihani gani na watapimwa vipi?

Halafu nilitegemea wangekuja na pendekezo la kuanza kutumia lugha ya kingereza kufundishia masomo yote isipokuwa kiswahili litabaki somo la lazima kwa elimu zote …
Pia wasinge jiangaisha tungaenza kutumia mfumo wa elimu ya kenya basi kuliko kujidanganya kufuta mitihani…watoto wa elimu ya msingi ni vyema kupimwa!
 
Sasa kama mtihani wa elimu ya msingi umefutwa kwa hiyo watafanya mtihani gani na watapimwa vipi?

Halafu nilitegemea wangekuja na pendekezo la kuanza kutumia lugha ya kingereza kufundishia masomo yote isipokuwa kiswahili litabaki somo la lazima kwa elimu zote …
Pia wasinge jiangaisha tungaenza kutumia mfumo wa elimu ya kenya basi kuliko kujidanganya kufuta mitihani…watoto wa elimu ya msingi ni vyema kupimwa!
Kutakuwa na continuous assessment
 
aidha elimu hiyo lazima inajumuisha elimu ya msingi ya miaka 6 na elimu ya sekondari ya chini itatolewa kwa miaka 4, utekelezwaji wa pendekezo hilo utaanza kufanyika mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa Darasa la 7.
Yule dakitari wa darasa la saba atatambulikaje baada ya hapo
 
02 Novemba, 2023

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI YAFANYA MABORESHO YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO-MAJALIWA

*Asema elimu ya lazima itakuwa miaka 10 badala ya saba kama ilivyo sasa



SERIKALI imefanya maboresho kwenye baadhi ya maeneo katika Sera ya Elimu na Mafunzo ili kutoa elimu ya ujuzi badala ya elimu ya taaluma pekee ambapo elimu ya lazima itakuwa ya miaka 10 badala ya saba kama ilivyo sasa.

Akitoa taarifa kuhusu maboresho hayo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema utekelezaji wa maboresho hayo utaanza mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa darasa la saba na badala yake kuanza kufanyika kwa tathmini darasa la sita kwa ajili ya kujiunga na elimu ya lazima ya sekondari.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 2, 2023) wakati akitoa taarifa kuhusu kuidhinishwa kwa Sera ya Elimu na Mafunzo 2014, Toleo la 2023 na Mitaala ya Elimu Ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu bungeni jijini Dodoma.

Amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya kubainika kwa changamoto mbalimbali zikiwemo, mfumo wa elimu kujikita zaidi kwenye elimu ya jumla na kukosa fursa za elimu na mafunzo kwa kuzingatia mahitaji na njia mbalimbali za ujifunzaji kutokidhi kulingana na mazingira.

Ametaja changamoto nyingine kuwa ni: “Mitaala kutokidhi mahitaji ya mabadiliko ya kiuchumi, kijamii, kisayansi na kiteknolojia, mfumo usio fanisi wa udhibiti na ithibati ya elimu na upungufu wa nguvu kazi. Changamoto hizo zilizaa hitaji la kuboresha sera yetu ya elimu ili kukidhi mahitaji ya sasa na wakati ujao.”

Akifafanua kuhusu maeneo yaliyoboreshwa kwenye sera hiyo ambayo tarehe ya uzinduzi wake itatangazwa baadaye, Mheshimiwa Majaliwa amesema: “Sera ya Elimu na Mafunzo imefanyiwa mabadiliko kwenye maeneo kadhaa ikilinganishwa na sera iliyopita kwa kuongeza fursa za elimu ya amali (elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi) ambayo itaanza kutolewa kuanzia kidato cha kwanza.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema elimu ya ualimu nayo itaanza kuanza kutolewa kwa wahitimu waliomaliza kidato cha sita na kuendelea. “Mafunzo ya ualimu yatajumuisha mwaka mmoja wa mafunzo chini ya uangalizi (internship) baada ya kuhitimu mafunzo tarajali (Pre-service training).”

Amesema maeneo yaliyoboreshwa ni katika mfumo wa upimaji na tathmini ambao utazingatia mahiri zinazohitajika kwa kila ngazi kwa lengo la kuwa na upimaji endelevu na matumizi ya mbinu mbalimbali za upimaji na tathmini ya maendeleo ya wanafunzi katika kujifunza.

“Serikali itatoa na kusimamia matumizi ya kitabu kimoja cha kiada kwa kila somo katika elimu ya msingi na Sekondari ili kufanikisha upimaji wa matokeo ya ufundishaji na ujifunzaji unaofanana pia Serikali itaweka utaratibu wa kubaini na kuendeleza wanafunzi wenye vipaji na vipawa mbalimbali.”

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Wizara yenye dhamana na elimu ina wajibu wa kuandaa mikakati na mipango ya sekta ikiwa ni pamoja na kutafuta rasilimali mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji na kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa sera hiyo.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Wizara yenye dhamana na TAMISEMI itakuwa na wajibu wa kuratibu na kusimamia Tawala za Mikoa zenye jukumu la kutekeleza sera kwa kutoa elimu na mafunzo katika ngazi ya awali, msingi na sekondari na Wizara yenye dhamana na Utumishi itahusika na upatikanaji wa rasilimali watu.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa Wizara yenye dhamana na fedha itahusika na utafutaji na upatikanaji wa rasilimali fedha, Tawala za Mikoa zitasimamia utekelezaji wa sera na miongozo ya utoaji elimu na mafunzo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

“Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaendelea na utekelezaji wa sera na hivyo kutoa huduma za elimu ili kuwafikia walengwa wote. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo mashirika ya kidini, mashirika yasiyo ya Serikali na wadau wengine katika kuboresha upatikanaji na utoaji wa elimu na mafunzo.”

Amesema mgawanyo wa majukumu utafuata mifumo ya kitaasisi iliyojengwa kisheria na kwa kadri ya utaratibu wa Serikali. “Wizara yenye dhamana ya elimu pamoja na taasisi zake itaendelea kuwa na wajibu wa kusimamia, kuratibu na kuimarisha upatikanaji na utoaji wa elimu na mafunzo nchini.”

(mwisho)

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

ALHAMISI, NOVEMBA 2, 2023.
 
02 Novemba, 2023

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SERIKALI YAFANYA MABORESHO YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO-MAJALIWA

*Asema elimu ya lazima itakuwa miaka 10 badala ya saba kama ilivyo sasa


View attachment 2801505

SERIKALI imefanya maboresho kwenye baadhi ya maeneo katika Sera ya Elimu na Mafunzo ili kutoa elimu ya ujuzi badala ya elimu ya taaluma pekee ambapo elimu ya lazima itakuwa ya miaka 10 badala ya saba kama ilivyo sasa.



Akitoa taarifa kuhusu maboresho hayo, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema utekelezaji wa maboresho hayo utaanza mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa darasa la saba na badala yake kuanza kufanyika kwa tathmini darasa la sita kwa ajili ya kujiunga na elimu ya lazima ya sekondari.



Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Novemba 2, 2023) wakati akitoa taarifa kuhusu kuidhinishwa kwa Sera ya Elimu na Mafunzo 2014, Toleo la 2023 na Mitaala ya Elimu Ngazi ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu bungeni jijini Dodoma.



Amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya kubainika kwa changamoto mbalimbali zikiwemo, mfumo wa elimu kujikita zaidi kwenye elimu ya jumla na kukosa fursa za elimu na mafunzo kwa kuzingatia mahitaji na njia mbalimbali za ujifunzaji kutokidhi kulingana na mazingira.



Ametaja changamoto nyingine kuwa ni: “Mitaala kutokidhi mahitaji ya mabadiliko ya kiuchumi, kijamii, kisayansi na kiteknolojia, mfumo usio fanisi wa udhibiti na ithibati ya elimu na upungufu wa nguvu kazi. Changamoto hizo zilizaa hitaji la kuboresha sera yetu ya elimu ili kukidhi mahitaji ya sasa na wakati ujao.”



Akifafanua kuhusu maeneo yaliyoboreshwa kwenye sera hiyo ambayo tarehe ya uzinduzi wake itatangazwa baadaye, Mheshimiwa Majaliwa amesema: “Sera ya Elimu na Mafunzo imefanyiwa mabadiliko kwenye maeneo kadhaa ikilinganishwa na sera iliyopita kwa kuongeza fursa za elimu ya amali (elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi) ambayo itaanza kutolewa kuanzia kidato cha kwanza.”



Kadhalika, Waziri Mkuu amesema elimu ya ualimu nayo itaanza kuanza kutolewa kwa wahitimu waliomaliza kidato cha sita na kuendelea. “Mafunzo ya ualimu yatajumuisha mwaka mmoja wa mafunzo chini ya uangalizi (internship) baada ya kuhitimu mafunzo tarajali (Pre-service training).”



Amesema maeneo yaliyoboreshwa ni katika mfumo wa upimaji na tathmini ambao utazingatia mahiri zinazohitajika kwa kila ngazi kwa lengo la kuwa na upimaji endelevu na matumizi ya mbinu mbalimbali za upimaji na tathmini ya maendeleo ya wanafunzi katika kujifunza.



“Serikali itatoa na kusimamia matumizi ya kitabu kimoja cha kiada kwa kila somo katika elimu ya msingi na Sekondari ili kufanikisha upimaji wa matokeo ya ufundishaji na ujifunzaji unaofanana pia Serikali itaweka utaratibu wa kubaini na kuendeleza wanafunzi wenye vipaji na vipawa mbalimbali.”



Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema Wizara yenye dhamana na elimu ina wajibu wa kuandaa mikakati na mipango ya sekta ikiwa ni pamoja na kutafuta rasilimali mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji na kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa sera hiyo.



Aidha, Waziri Mkuu amesema Wizara yenye dhamana na TAMISEMI itakuwa na wajibu wa kuratibu na kusimamia Tawala za Mikoa zenye jukumu la kutekeleza sera kwa kutoa elimu na mafunzo katika ngazi ya awali, msingi na sekondari na Wizara yenye dhamana na Utumishi itahusika na upatikanaji wa rasilimali watu.



Waziri Mkuu ameongeza kuwa Wizara yenye dhamana na fedha itahusika na utafutaji na upatikanaji wa rasilimali fedha, Tawala za Mikoa zitasimamia utekelezaji wa sera na miongozo ya utoaji elimu na mafunzo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.



“Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaendelea na utekelezaji wa sera na hivyo kutoa huduma za elimu ili kuwafikia walengwa wote. Katika kutimiza azma hiyo, Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo mashirika ya kidini, mashirika yasiyo ya Serikali na wadau wengine katika kuboresha upatikanaji na utoaji wa elimu na mafunzo.”



Amesema mgawanyo wa majukumu utafuata mifumo ya kitaasisi iliyojengwa kisheria na kwa kadri ya utaratibu wa Serikali. “Wizara yenye dhamana ya elimu pamoja na taasisi zake itaendelea kuwa na wajibu wa kusimamia, kuratibu na kuimarisha upatikanaji na utoaji wa elimu na mafunzo nchini.”



(mwisho)

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

ALHAMISI, NOVEMBA 2, 2023.
Kuruka na kukanyagana! Nimejikuta nawaza tu.
Lakini wote tuimbe Tanzania nakupenda.
 
Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, leo Bungeni ijini Dodoma alisimama kutoa taarifa kuhusu kuidhinishwa kwa sera ya elimu na mafunzo ya Elimu 2014 toleo la 2023, amesema sera ya Elimu na mafunzo imefanyiwa mabadiliko kwenye maeneo kadhaa kulinganisha na sera iliyopita na maeneo hayo ni elimu ya lazima kuwa ya miaka 10 badala ya 7, aidha elimu hiyo lazima inajumuisha elimu ya msingi ya miaka 6 na elimu ya sekondari ya chini itatolewa kwa miaka 4, utekelezwaji wa pendekezo hilo utaanza kufanyika mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa Darasa la 7.

View attachment 2801381
Nzuri hii
 
Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, leo Bungeni ijini Dodoma alisimama kutoa taarifa kuhusu kuidhinishwa kwa sera ya elimu na mafunzo ya Elimu 2014 toleo la 2023, amesema sera ya Elimu na mafunzo imefanyiwa mabadiliko kwenye maeneo kadhaa kulinganisha na sera iliyopita na maeneo hayo ni elimu ya lazima kuwa ya miaka 10 badala ya 7, aidha elimu hiyo lazima inajumuisha elimu ya msingi ya miaka 6 na elimu ya sekondari ya chini itatolewa kwa miaka 4, utekelezwaji wa pendekezo hilo utaanza kufanyika mwaka 2027 sambamba na kufuta mtihani wa Darasa la 7.

View attachment 2801381
Watakaoanza kabla ya 2027 wao wataendelea na utaratibu wa kawaida si ndio?
 
Kwa miaka 6 ya elimu ya msingi wanafunzi wapimwe kitaifa mara mbili; awamu ya kwanza iwe baada ya miaka minne na awamu ya pili iwe ya kuhitimisha miaka sita. Mitihani ya kuhitimisha mwaka wa sita itumike kuchaguwa wanafunzi wenye sifa za kuendelea na miaka mingine minne.
Wenye sifa wa kuendelea na miaka mingine 4 ni wale watakaonekana wamepata maarifa kamili kwa kufaulu masomo yote kuanzia 50% Hadi 100%

Tukisema elimu ya lazima iwe ni miaka 10 basi Kuna mwingine anaweza kuja na kusema elimu ya lazima iwe ni miaka 12 au 17 na ili iwe lazima basi watakaoenda hatua nyingine ni lazima wawe wamefaulu na wasiofaulu watalazimika kukalili au kuludia hatua husika.
Sekondari ya chini upimaji wa kitaifa ufanyike mara moja kitaifa na mara moja ndani ya mkoa.
Shule zenye wanafunzi kuanzia 400 Hadi 800 walimu wasipungue 4 kwa kila somo kwa shule za sekondari na 5 kwa kila somo kwa shule za msingi.

Karibu 95% ya shule zote nchini Zina upungufu wa walimu.
Malengo ya elimu yazingatie muda. Mada zitakazokusudiwa kufanikisha malengo lazima ziwe sawa na muda utakaopangwa kulingana na muda wa siku za masomo kwa ratiba za nchi Zima..

Ikiwa mpango huu utakaoanza kufanikishwa kuanzia 2027, umeigwa mahali basi ni muhimu kuhakikisha kila njia na nyenzo fanikishi zinaigwa kwanza kabla ya kufanya ubunifu mwingine.
Asante.
 
Kwanza nipongeze Kwa jitihada za serikali kuhusu mabadiliko haya katika Elimu. Swali langu tu ni kwamba haya mabadiliko yamefanyika ila maboresho ya Elimu Naona Bado Kuna shida ,Moja wadau Kwa namna Moja ama nyingine hawajashirikishwa kama ilivyo ktk mchakato wa katiba,Pili, kuhusu walimu hapa Waziri hajataja level watakayoanza kufundisha Hawa kidato Cha sita Kwa maana ya Primary na Secondary. Mimi naamini issue ya ualimu si kidato Cha sita issue ni matengenezo ya huyu mwalimu ,hata kidato Cha nne akiandaliwa vema anaweza tu mbona .

Ahsante.

Fedius Machumu Lugembe
Mdau Elimu ( Vocational training)
 
Kwanza nipongeze Kwa jitihada za serikali kuhusu mabadiliko haya katika Elimu. Swali langu tu ni kwamba haya mabadiliko yamefanyika ila maboresho ya Elimu Naona Bado Kuna shida ,Moja wadau Kwa namna Moja ama nyingine hawajashirikishwa kama ilivyo ktk mchakato wa katiba,Pili, kuhusu walimu hapa Waziri hajataja level watakayoanza kufundisha Hawa kidato Cha sita Kwa maana ya Primary na Secondary. Mimi naamini issue ya ualimu si kidato Cha sita issue ni matengenezo ya huyu mwalimu ,hata kidato Cha nne akiandaliwa vema anaweza tu mbona .

Ahsante.

Fedius Machumu Lugembe
Mdau Elimu ( Vocational training)
Nchi za wenzetu kama huna degree hata moja, huwezi kuwa mwalimu.

Serikali imepanda ngazi kwamba kwa Tz angalau mwl awe amepata elimu ya sekondari ya juu halafu wewe unakuja kutuletea habari za form four.
 
Back
Top Bottom