Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Nilikuwa na jamaa yangu tumetoka nje tumekaa kwenye parking ya bar, si nikaona pisi mbili zimenyooka sana zimeagamia gari, nikasogea, manzi mmoja amenyooka sana, walikuwa wanavuta bangi, mmoja mweusi na mwingine mweupe, yule mweupe alikuwa mkali kinoma ana lafudhi ya Arusha, jamaa yangu kamuelewa mweusi tukasema tugawane.

Yule mweupe nahisi ni chotara sijui wa kizungu/mhindi, anaongea sana, anavuta bangi anapuliza moshi wote kwangu, mwenzangu kaanza kukagusa kale keusi kiuno kakaanza kulegea, huku mimi nakomaa na yule mweupe, huyo mweupe nikagundua ile gari ni yake Subaru Forester XT ina pua itakuwa turbo(nikasema hapa kazi ipo, waendesha subaru akili zao😂), yule manzi mweupe akaanza kumzingua jamaa yangu, kumbe yule mweupe anamsaga yule mweusi,sasa kale keupe kalikuwa kanapambania penzi lake nasikia kanasema "we dem unacheka nini, ingia kwenye gari".

Yule mweupe baada ya kuona jamaa anazidi kumlainisha baby yake ikabidi alianzishe, jamaa yangu akamlamba mtama akatulia mkono 😂 😂 😂 ,nikasogea nikamnyanyua alikuwa amelewa, nikaona leo sipati kitu, akawa analalama amemuumiza mkono.

Baadae waliingia garini nikafika dirishani nikawa namuelewesha aniachie hata namba, nilibaki kukariri plate number tu, hio subaru ilivyotoka hapo niliruka pembeni,nilibaki na nguo inanuka bangi tu, licha ya kufahamu ana tabia hio lakini uzuri wake ulikuwa ni 🔥🔥.

Huyu dada kwa jinsi alikuwa mkali nikaanza kuwaza hivi huyu hawezi badilika kabisa? nilijiuliza sana, alikuwa mzuri balaa.

Nilijishangaa sana mwenyewe.
😅😅😅 Nimecheka sana, akili zetu wanaume huwa za ajabu sana unakumbula kale ka msari kama mfalme ... Wanawake wanabadirika ila unapo amua mabadiriko yake ukubali kutumia mda mwingi sana kuingia ndani yake na kumtoa alie anza kabla yako... nafsi huwa inauma ukikosa gori na hasa ziwe dk za majeruhi ... ingawa mie nilipambana nikabebeshwa mkoba sasa nikawa nikitembea nae ananiambia nifate nafata nikawa kama nimepigwa upofu alafu watu wanatuangalia kweli kweli nikasema nini hii, ila sikuwa kabisa na akili mbele ya yule dadaaa, baadae ananiambia anaenda kulala sasa shughuli pevu ndio ilikuwa hapo anza bebembeleza wee twendee , kakataa alafu yupo serious ananiambia kwani mie nauza huku nimebeba sana mkobaa fataa saka kama bodi gadi nikiwa na matumaini 😅😅😅 tukawa tumesimama mahala hivi akaanza nihoji maswali sijui akili hapo zilikuwa wapi .. kipindi ananiuliza nika test mvuta kwa nyuma nika mkumbatia akachekaa akatulia nikaanza piga siasa huku nimekumbkatia akachomoka akasogea kama main entry fata pale kumbatiana live live sina aibu hapo sijui akili ilienda wapi ila kuondoka wote hataki.. nikakata kabisaa tamaaa nikamuambia poa mie naondoka akasema poa 😅😅 roho ikauma piga hatua mbili nikarudi .. nikaingia na gear ingine mie nasafiri naenda morogoro nikitoka morogoro naenda dodoma akawa hapajui kumbe mgeni, hapo ndio alifanya makosa kusema hapajui huko koteee nikaanza ingiza gear baada ya gear hadi mida ya saa 10 akasema twende alipofikia akachukue mizigo yake twende wote nikahisi utani, hao tukaondoka hadi hotelin kwake ila hatoi mzee, hapo tayari nimetoboa na ni nje ya utaratibu , tukaingia kwenye chuma sijalala hapo nilichofanya piga redbul za kutosha na maji mengi ili mkojo unisimbue ninapo kuwa naendesha nisilale, nilifanikiwa mkoani morogoro na mkoani dodoma na dar es salaam nawasiliana nae tu maana wengine hatujuagi kuachana 😅😅😅
 
Back
Top Bottom