Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,384
Umegusia jambo la msingi sana. Wenzetu wanapambania legacy. Yaani ni kitu cha muhimu sana kwao. Wakiondoka watakumbukwaje. Unakuta mtu anaishi maisha ya kawaida kumbe ana vimilioni vyake kadhaa ameviweka kwenye trust na ameandika will kabisa kuwa akifa vyote vipelekwe kwenye chuo au shule fulani vikajenge jengo ambalo litapewa jina lake iwe kama kumbukumbu ya kudumu. Ndiyo maana ukienda kwenye vyuo vikuu vyao utakuta majengo karibu yote ni majina ya watu. Utakuta SYB School of Economics. Ukiulizia huyo SYB alikuwa nani utapewa historia yake yote na kiasi cha pesa alichotoa kujenga jengo hilo. Na uzuri majimbo mengi pia wana matching program. Yaani SYB akitoa milioni 10 kujenga jengo serikali ya jimbo nayo ni lazima itoe milioni 10. Hivyo mjengo wa dola milioni 20 unajengwa lakini unaitwa kwa jina la SYB kwa vile ndiye initiator. Legacy!Aah dadake Junia atatoboa tu, Mungu ni mwema sana. Huko wenzetu nisiseme kwamba hawajali sana kuhusu familia; ni kwamba majority wanahangaika kuhakikisha mwisho wa maisha yao wanaacha alama ya kudumu kwenye maisha ya watu; they are purpose driven. Kila mtu anataka ahakikishe anatimiza kusudi lake hapa duniani; hata siku akiondoka watu bado wataendelea kufaidika na vitu alivyovifanya akiwa hai. Maisha ya kutokujiwazia wewe na familia yako; na kugusa maisha ya wengine zaidi; ndiyo maisha bora zaidi humu duniani. Sisi huku tukishaolewa, tumepata watoto, kanyumba na kausafiri aaaah maisha ndiyo haya; Yesu rudi tu.
"Vitu unavyovifanya kwa ajili yako, vitakufa siku ukifa; lakini vitu unavyovifanya kwa ajili ya wengine vitaishi hata kama ukifa"
Barikiwa Mtumishi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Na tabia hii ya kukazania legacy ndiyo imewafanya kwa kiasi kikubwa waondokane na ufisadi huu wa kijinga kama tunaofanyiana huku. Huwezi kula hela za barabara au za visima vya maji kwa sababu kwanza utafungwa na utaharibu legacy yako mazima. Wenzetu hawawazi tu matumbo yao na familia zao. Ndiyo maana hata utajiri wao ni generational. Watoto, wajukuu, vitukuu, vilembwe....kamwe hawatakubali jina la familia life na watapambana kufa na kupona kuhakikisha kuwa biashara inaishi. Akina Ford. Akina Toyota. Akina Benz. Akina Boeing.....




)
)