Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Nimekubaliana nawe kabisa kabisa...hayo nadhani ni madhara ya mfumo dume tu. Kila tatizo anabebeshwa mwanamke. Na haiishii hapo tu. Binti akiolewa halafu akachelewa kupata mtoto anayelaumiwa ni mwanamke hata kama mwenye tatizo ni mwanaume. Ndivyo jamii yetu ilivyo!
View attachment 2195487
Yaani miaka 20 tu kamkatia tamaa mwenzie 🙆🏻‍♀️🙆🏻‍♀️.. Ana mapepo huyo kaka.. Ila kanda ya ziwa nao wamezidisha mfumo dume khaa!!!
 
Yaani miaka 20 tu kamkatia tamaa mwenzie .. Ana mapepo huyo kaka.. Ila kanda ya ziwa nao wamezidisha mfumo dume khaa!!!
Halafu unakuta pengine mwanaume ndiyo mwenye ishu. Wanaume wengi hudhani kuwa kwa vile wanaweza kupiga bao basi otomatikale wana uwezo wa kutungisha mimba

Na mkoa wa Mara kule ni mchaka mchaka ng'wanawane. Hata wanawake wa huko nao hawataki ujinga...

IMG-20220420-WA0063.jpg
 
Haya mambo hayana fomyula mtumishi. Ni sandakarawe ya kukata na shoka yaani (japo makosa mengi anabebeshwa mwanamke)....Mungu na Awasaidie sana kwa sababu hakuna namna ila ni mtihani wa kutisha mno!

Huyu dadake na Junia hapa yeye kasema hatakaa aolewe ila ikiwezekana atapenda kuwa na katoto kamoja tu. Nami huwa namuunga mkono. Ila najua pengine atabadili msimamo akikutana na tall dark guys huko medical school. Baadhi ya magazeti yako unayoandikaga humu (kama lile la leo) nimeyasevu nitamtafsria awe anayasoma. Asante sana kwa huduma yako yenye upako
Aah dadake Junia atatoboa tu, Mungu ni mwema sana. Huko wenzetu nisiseme kwamba hawajali sana kuhusu familia; ni kwamba majority wanahangaika kuhakikisha mwisho wa maisha yao wanaacha alama ya kudumu kwenye maisha ya watu; they are purpose driven. Kila mtu anataka ahakikishe anatimiza kusudi lake hapa duniani; hata siku akiondoka watu bado wataendelea kufaidika na vitu alivyovifanya akiwa hai. Maisha ya kutokujiwazia wewe na familia yako; na kugusa maisha ya wengine zaidi; ndiyo maisha bora zaidi humu duniani. Sisi huku tukishaolewa, tumepata watoto, kanyumba na kausafiri aaaah maisha ndiyo haya; Yesu rudi tu.


"Vitu unavyovifanya kwa ajili yako, vitakufa siku ukifa; lakini vitu unavyovifanya kwa ajili ya wengine vitaishi hata kama ukifa"

Barikiwa Mtumishi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh mtu miaka inakatika tu haoi.
Si aoe muendelee kutafuta pamoja.


Unadhani upo kwenye mahusiano kumbe upo single,,,anakuja mtu mzuri tu unamuacha.
Aisee akija mzuri tutembee naye mbele .
Ukiwa na conscience; huwezi kumuacha mpenzi wako kwa sababu tu katokea mwingine with a proposal. Kuna watu sio rahisi kuhimili Ile hali kwamba unaona wewe ndiyo sababu ya mtu mwingine kuumia tena bila kosa. Ila ndiyo hivyo tena, unaweza kuja kuachwa solemba teh teh
 
Ukiwa na conscience; huwezi kumuacha mpenzi wako kwa sababu tu katokea mwingine with a proposal. Kuna watu sio rahisi kuhimili Ile hali kwamba unaona wewe ndiyo sababu ya mtu mwingine kuumia tena bila kosa. Ila ndiyo hivyo tena, unaweza kuja kuachwa solemba teh teh
Inabidi kuangalia mwelekeo.
Unaona kabisa hapa hakuna kitu ila unakaza fuvu kuipambania mahusiano ambayo kumbe mwenzio anakuona single 😂
Haya mambo ni magumu .
 
Inabidi kuangalia mwelekeo.
Unaona kabisa hapa hakuna kitu ila unakaza fuvu kuipambania mahusiano ambayo kumbe mwenzio anakuona single 😂
Haya mambo ni magumu .
Shida inakuja pale ambapo "everything seems to be ok". Unaona unapendwa, unajaliwa, unathaminiwa na unaona jinsi mwenzio anavyopambana. Wanaume wengi wasipokuwa na hela eeeeh unasema Jehovah nikurudishie nini. Na hapo ndiyo wengi tunapokwama nao😁😁
 
Back
Top Bottom