Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Mi nilichimba mkwara nilipokuwa darasa la 5 kuwa naondoka home kimoja. Hii ilikuwa ni baada ya kupokea kichapo hevi kwa kitu ambacho nilidhani halikuwa kosa langu. Nikaambiwa hata ukiondoka sisi wala hatutahangaika kuja kukutafuta. Dah! Nikaona hawa watakuwa wanatania hawa! Last born kweli nikafanya yangu. Miezi 6 siko home na hakuna aliyekuja kunitafuta mbali tu na kusikia habari kuwa mama yako anakutafuta sana. Mpaka bro mmoja mjeshi akaja likizo ndo akaja kunisaka nilikokuwa + kichapo hevi nikarudishwa shuleni mzobe mzobe. Mwalimu mkuu naye kumbe ana usongo kwa sababu nilikuwa nashika namba wani darasani. Napo kichapo hevi akanipa na cheo cha kuwa time keeper shuleni ili nisiwe mtoro tena. Ndo ikawa pona yangu. Mtihani wa darasa la 7 enzi zile vigumu kweli kwenda sekondari tukachaguliwa watu wawili tu pale kijijini!

Kisa hiki kilinikomaza sana na nimeweza kutembea zaidi ya nchi 16 katika mabara yote ya dunia hii isipokuwa Australia na Antarctica bila woga wala nini. Na mpaka leo naweza kwenda po pote bila woga.

Mwaka 2017 nikakutana na yule mwalimu mkuu nikamkumbusha kisa kile alicheka sana. Ila nilimshukuru mno kwa kunikomalia kusoma....

Kwa hivyo last born wengine siyo wa mchezo mchezo aisee
Hongera sana boss, mwalimu kwangu amebaki kuwa mtu wa pekee kabisa, maana pamoja na majaliwa ya Mungu lakini mwalimu ndio amewezesha kuwa hapa tulipo.
 
Back
Top Bottom