Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Mimi hivyohivyo.
Watu walikuwa waisubiri wale,nikajitoa kimasomaso kupika.

Bora hata ingekuwa ugali
Haikuiva kabisa,ilikuwa inafurumia tu hapo jukoni..blue band inateketa tu pale juu inatoa povu.
Nilichochea usiku kucha,nateketeza tu mkaa lakini wapi.

Ni miaka 6 sasa imepita,ndio nimejaribu tena leo.
😂😂😂keki unaweza ichukulia poa ila ina umbua mbaya siku ile niliaibika sana vitoto vya dada zangu vinakuja jikoni vinachungulia Odo keki bado kumbe kitu ugaliii😂😂😂😂
 
keki unaweza ichukulia poa ila ina umbua mbaya siku ile niliaibika sana vitoto vya dada zangu vinakuja jikoni vinachungulia Odo keki bado kumbe kitu ugaliii
Tena ilikuwa ya graduatuon ya watu.
Vile vipande vya kula tu na chakula.
Imefika asbh hakuna kinachoeleweka,,hapo nilichochea weee,ndio kwanza inafurumianyeupe vilevile.
Mama akawa ananisaidia kuongeza moto akijua itaiva,,
Dada ndio anacheeeka mjinga yule hadi nililia.

Kiherehere changu,hata kupika sijui nikajichanganyia tu,jaza blue band.
 
mie mkaa unanichosha inachelewesha hivi then hapo upo excited unaisubiri ule kwa hamu .

siku moja nikaona YouTube keki inaiva kwa rice cooker nikajaribu aisee kumbe sio rice cooker zote zinaweza kupika cake , nikashangaa pap imezima chini ndo imeiva ,
 
Najua ninatoa kituko
Ila nitapiga moyo konde na kujaribu tena.



Mimi najisikia aibu sana aisee
Sambusa zilivyo tamu vile na sijui kupika,yaani watu wakitaka wale inabidi wanunue...huu ni uzembe.
Jitahidi mpendwa Sambusa kidogo rahisi kujua
 
20211211_101654.jpg
20211211_101652.jpg
 
Back
Top Bottom