Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Screenshot_20211122-201807.jpg
 
Kwa anaethubutu kumuuwa mtu kwa sababu zozote zile,I mean zozote zile kama ni kuchukuliana wake au sijui kudhulumiana pesa au kunyang'anyana vyeo iwe yoyote ile inampasa kujua kwamba furaha yake haitoletwa kwa kumtoa yule anayemchukia duniani,tujifunze kuishi katikati ya maadui zetu!

Yeye ameondoka ila duniani wapo watu kuishi kwao walitegemea uwepo wa huyu mtu,watoto walitegemea Baba yao awaletee chakula kama wanao wanavyokutegemea wewe,awalipie school fees kama unavyofanya wewe,Baba/Mama yake pengine ni wazee sana tayari wana maradhi sugu yanayotaka pesa kununua dawa na ilikuwa zitoke kwa huyu marehemu sasa hawazipati ni wengi huwahitaji wapendwa wao pale wanapofariki hii dunia tunategemeana so kila mmoja wao niliowataja atakapokosa huduma atamkumbuka huyu mtu na kila anapomkumbuka nafsi yake huugua na kila atakapoumia machozi yake hulipwa directly kwa muuwaji kwa njia mbalimbali ambazo anaweza azione au asizione hili huwa kama fumbo na hutembea na kizazi cha muuwaji.

Tuheshimu nafsi za watu,inanifaa nini kuuwa mtu kwa kitu ambacho sina guarantee ya kuki-maintain hata miezi miwili ijayo?maana hata kama nitachukua pesa je nikifa kesho then zitanisaidia nini?kazi?je nikifukuzwa?tamaa ya mali nikiondoka mwaka mmoja baada ya kuuwa nitaondoka nazo kiasi gani?

Inasikitisha?Mungu Mwenyezi amrehemu apate pumziko la milele.
Ndugu yangu. Mambo yalibumburuka pale bustani ya Eden na li Abeli kumuua nduguye Kaini baadaye. Tangu hapo ni kizaazaa tu kuanzia vitani huko mpaka kutoana roho kwa mtu mmoja mmoja hata kwa sababu za kijinga ajabu. Na kwa wanasiasa hawa uchwara kukolimbana (kwa waziwazi au kurogana) wala siyo jambo la kushangaza.

Wewe unaongelea katika kiwango cha juu cha urazini kwenye upendo wa kimalimwengu lakini katika uhalisia wake binadamu ni mnyama katili sana. Na ukiangalia kwa umakini na ujumuishi wake, unaweza hata kukosa maana ya maisha yetu hapa duniani. Kwamba eti tumezaliwa tufanye kazi, tule, tunywe, tugegedane na mwisho tufe. Inashangaza sana...

Ila hawa wanaofanya haya mara nyingi mwisho wao huwa siyo mwema. Huwezi kumwaga damu isiyo na hatia halafu ukabakia salama. Karma will always find you....
 
Back
Top Bottom