Mahitaji

Bamia kumi (10)

Mafuta ya maji (African Black castor oil au coconut oil au olive oil)

Juice ya Tangawizi

Asali
Jinsi ya kuandaa

Osha bamia zako vizuri kuondoa uchafu wote

unaweza kukata kata kuwa vipande vidogo vidogo au ukamenya tu (kuexpose undani wake)

Weka kwenye sufuria yako safi

Ongeza maji kiasi (kikombe kimoja au viwili vinatosha) na ufunike

Chemsha kwa dakika 10 hadi 15 mpaka ile gelly au ute wa bamia uwe umetoka wa kutosha

Epua na uache ipoe kwa dakika kadhaa

Baada ya hapo chuja kuondoa vipeke na upate gelly tuu
Kama unatengeneza steaming

chukua ute ulioupata gawanya mara mbili

Nusu ya kwanza changanya na tangawizi na asali na mafuta yoyote ya kimiminika (hasa Castor oil)

Baada ya kuosha nywele kwa shampoo (hakikisha nywele zako ni safi) paka mchanganyiko kwenye nywele zote

Vaa shower cap au steamer na ukae kwa dakika 30+

Osha kwa maji mengi

Chukua ule mchanganyiko uliobaki changanya na mafuta kijiko kimoja hapa utakua umepata leave in conditioner

Nywele zako zikiwa mbichi na safi pakaa vizuri kuanzia kwenye ngozi hadi kwenye ncha.

Chambua vizuri nywele zako kidodgo kidogo kuhakikisha imeingia vizuri kwenywe nywele zote.

Unaweza kusuka mabutu (bantu knots) au twists za njia mbili au tatu au nywele za mistari kawaida nywele lazima ziwe na unyevu kabisa.

Ukiona zinakauka unanyunyiza maji tena.

Ukimaliza acha zikauke vizuri utaendelea kupaka mafuta yako kama kawaida ili kuzifanya zing’ae.

Ukifumua unapata mawimbi mazuri unaweza kubana utakavyo nywele zako.