Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Ila Kuna kauli sijaipenda
Hiyo ya tecno Aiseee...Mara picha zinatoka vibaya...Sasa si Ni zao na wameridhika nazo ndio maana wakapost.

Kutumia iPhone kusimfanye mtu amdharau mtumiaji wa Samsung infinix au tecno...Ni priority tu jamani...hatuwezi kulingana.

Pia uzuri wa mtu upo machoni pa mtu... mambo ya kuanza kuponda wadada wa watu bila sababu za msingi sio uungwana.
Kama girlfriend wako Ni malaika kwako isiwe sababu ya wewe kuwakandamiza wasichana wengine na kuona hawafai...kuna wanaume wanaowaona wanafaa.
Na nyie wadada muache kuponda girlfriends za watu jamani lol
Mmezidi na nyie....jifunze kupunguza maneno mdomoni.
Ulimi huponza kichwa.

Pia mtu kukaa muda wote humu sio Kama Yuko useless au Hana kazi.
Kazi Ni kazi,haijalishi kubwa au ndogo zote Ni kazi.
Acheni kuona watu hopeless kisa wanashinda humu...kila mtu na priority zake...wengine jf Ni kama rafiki kwao.
It's a matter of choice &priority.
Kuna watu wapo humu nawajua Wana kazi na hela zao za maana...lakini hata siku moja hutawakuta wakikashfu watu

Jifunzeni kuongea na watu vema.
Hii jf Ina Watu wengi,waaminifu ,wema,wazuri...
Kupitia hii unaweza tengeneza undugu ujamaa na urafiki.

Tudumishe upendo,tafuteni Sana kuwa na amani na watu wote.
Heshima Ni kitu Cha bure
Jifunzeni kuongea lugha nzuri.
Ukijibu vizuri ama kukaa kimya hutakatika mkono Wala kichwa.

Samahani kwa nitakaowakwaza.
Ni maoni yangu tu.
Hahahaha mtu anayetumia iphone anaanzaje kumkashifu mtu anayetumia samsung kwa mfano??

Anyway umeongea maneno kuntu sana mama tumekusikia tutajitahidi kutumia lugha nzuri mdogo wangu..
 
Sasa mimi naweza nikamuona mtu nzuri ila rafiki zangu wakasema sio mzuri.
Ndo maana wanasema nasifiaga kila mtu.
Nina rafiki yangu huyo akisifia mtu hadi mimi nashangaaga. Maana anajikubali mbayaaaaa na anajua kuponda kila mtu.
Nahisi katika rafiki zake tuko wawili tu ambao hajawahi kutusema ni wabaya
Sasa tofauti kati ya huyo rafiki yako na mimi ni kwamba huyo rafiki yako anajikubali na anaponda watu ila mimi sijikubali na sipondi watu

Yaani mimi kama mtu ni mzuri namsifia ila kama ni mbaya simpondi huwa nakaa kimya tu maana najua kuna watu wengine wanamuona mzuri
 
Back
Top Bottom