Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Hahahaa..


Kama nakuona unavyobadilisha laini za simu
...
Nilikuwa na msimamo kama wa joanah ila naona shetani ananizidi nguvu!

Seriously kuna wakati natamani kuonana na watu kwa ajili ya kupeana mawazo ya maendeleo, najua humu hatulingani, humu kuna watu wenye connection mob! Ila wasi wasi wangu ni je, hawa watu tutaendana kitabia?!
 
Sakayo mie kuangalia mwandiko wa nani ni mwema na wa nani sio mwema sijui kwasababu kuna pretenders wengi

Jambo ambalo nazidi kujifunza ni kutrust nobody

Napenda sana kuwa na marafiki,lakini mimi sio risk taker enough kuanza urafiki na mtu wa humu hadi kukutana nae

Nina moyo mwepesi sana wa kuumia,jambo dogo linaweza kuniumiza sana

So ni heri kubaki tusiojulikana ili kustay away from trouble na kuumia
hapana hutakiwi kuwa hivyo marafiki wema, wenye upendo na kujali utu tupo joanah
 
Malizia hii story Karma.

Nipo nimeagiza Pepsi ya baridi kabisa..
Ofcourse kuna mkaka mmoja nilikuwaga namuelewa kuanzia tuko form three hadi tunamaliza form six,, halafu nilikuwaga sina hata story naye nilikuwa namuonea aibuwakati miaka yote hiyo minne hatujawahi kusoma madarasa tofauti yaani tulijikuta tunasoma darasa moja hadi tunamaliza..

Na alikuwa back bencher wakati mie nilikuwa front bencher basi alikuwa akija mbele kuniongelesha nilikuwa nahisi kama kamoyo kameruka mapigo kadhaa,, ilikuwaga ni siri yangu ila kuna siku nilijisahau nikawaambia marafiki zangu bwenini nikaja kushituka taarifa zimesambaanikawa nawaza sijui atakuwa kajua..

Lakini hatukuwahi kuambiana chochote,, zaidi ya kuishia kupiga tu story za kawaida za hapa na pale..

Utoto bwana,, siku hizi namuona tu instagram amekuwa a fine young lad not a boy anymore..
 
Sakayo mie kuangalia mwandiko wa nani ni mwema na wa nani sio mwema sijui kwasababu kuna pretenders wengi

Jambo ambalo nazidi kujifunza ni kutrust nobody

Napenda sana kuwa na marafiki,lakini mimi sio risk taker enough kuanza urafiki na mtu wa humu hadi kukutana nae

Nina moyo mwepesi sana wa kuumia,jambo dogo linaweza kuniumiza sana

So ni heri kubaki tusiojulikana ili kustay away from trouble na kuumia
Nafikiri mpaka uwe rafiki na mtu mshazoeana zaidi ya comments za jukwaani!!

Na mnapokuwa mnawasiliana wawili tuu, lazima kuko na vitabia utaviona kabla hata hamjaonana!!

As for me, inaweza nichukua hata miaka mbili nawasiliana na mtu tuu bila hata kuonana naye akiwa na haraka anaweza kuondoka tuu dear!!

Kiukwelii mimi napenda sana kukutana na watu wapya walonipita umri, kiuchumi, elimu! Napenda kujifunza, kinachonitesa humu ndanii ni kuelewa tabia zao kama kweli zitaendana na zangu!
 
Lunch time...wapi kuko na lunch buffet poa?

Nikaipimie next time nimualike mdada mmoja wa jeiefu ili awe shuhuda kuwa jeiefu iko na wanaume poa pia
IMG_20191109_131925~2.jpeg
 
Cha muhimu ni kujua unaamua kukutana na watu wa aina gani na kwa sababu gani...

Kuna mtu jf nishafanya nae kazi humu ila hadi leo hafahamu kama ni mimi....

But, beyond the ID's we are hiding there are milions of things to share...

Ukipanga kukutana na mtu..Think about the life after meeting


Kwa Kweli mi nimekutana na masela wengi humu JF na Kwa Kweli tumepiga deal za maana na wengine tupo kwenye magroup ya WhatsApp tunajifunza mambo kibao kutoka Kila mmoja wetu. Nimewahi unganishwa kazi kadhaa na hela ndefu tu, JF sio mchezo, Au ni mimi tu ndio lucky
 
Back
Top Bottom