Sam Mahela tena... Hivi ITV management hamyaoni haya?

Sam Mahela tena... Hivi ITV management hamyaoni haya?

Kwi kwi kwi...mtu anauliza swali hata hasikilizi jibu...yuko busy anachungulia desa lake for the next question...yani hayupo kabisa kwenye interview....hana hata interest na jibu ...anatimiza wajibu tu....
hiyo ni auto style yake ya kuhoji. unajua wanaokuwa wanajibiwa ni viewers, yeye kazi yake ni kusikiliza na kuingilia kati inapobidi.....na kuendelea na swali lingine. Bado nasisitiza muda ni mchache, mambo ni mengi lazima kupata summary ili viewers wakiguswa na eneo iwe kazi yao kufuatilia.
Huwezi kutafuniwa halafu umezeshwe!!. Bado naona makosa ni kidogo........Mahela kaona maoni bila shaka atayafanyia kazi.
tusimpinge kama hakuna chochote anachofanikisha ikiwa baadhi yetu hatuwezi hata kuthubutu.
 
Huyu jamaa vipi jamani?! Nimefuatilia kipindi cha DK45 ITV na leo mgeni ni N/Waziri wa Muungano na Mazingira na mada ilikua ni Mazingira.

Huyu Sam Mahela, kama kawaida yake kuingilia mzungumzaji wakati anatiririka vizuri kwenye mada husika. Anageuka kuwa mzungumzaji Mkuu, anatoa maoni yake Mfano...."Mimi/sisi waandishi wa habari tumefanya tafiti na ni kweli/sio kweli kwamba Kuna uharibifu wa Mazingira"..... Sasa kama ulikua unajua ukweli/uongo wa jambo ya nini kumwalika mgeni studioni wakati ulikua na misimamo yako kwenye topic husika?

Mfano alipokua akiagana na N/W huyo, akawa anamsisitiza "Fanya kazi, umesikia, fanya kazii, umepewa kazi ufanye, sawa... maana hata mm hapa ITV napiga kazi"..... Hapa ni kiherehere tu cha huyu maana sio wajibu wake kumweleza hayo.

Nimekuwa nikifuatilia kipindi hiki lakini watu wengi wanakereka sana na huyu jamaa..... Atulie, atoe nafasi ya mgeni husika kusema na baada ya hapo maswali.

Mwanzilishi wa kipindi hiki na Buholela walikua wazuri sana sio kama huyu kijana.

Jamaa ana tatizo la kutaka sifa.. ni mropokaji,yaani kwa kifupi ana boa. Kwanza nashindwa kuelewa uongozi wa ITV kumpa mwandishi kama yeye kipindi cha maana kama hicho.. huyu anatakiwa kuwa ripota tu wa matukio ya mitaani.. yaani anaaibisha hicho kituo chao...anahemuka nadhani kwa akili yake anafukuzia ukuu wa wilaya namna hiyo..
 
Zamani nilikuwa namuelewa lakin siku hizi..... Mh, Bahati mbaya watangazaji wengi wazuri wa Itv wameondoa, mgano:
Buhohera
Almas Nyangasa
Masako
Na wengine, naona kabaki Lameck peke yake
 
Siyo kwamba anamgeza au ana baadhi ya sifa za Zeinab Baddawi?, mda mwingine zinafaa kwa baadhi ya interview endapo interviewee anahitajika kujibu maswali bila yeye kujuaswali ni lipi....unammock kabla hajamaliza mazungumzo. Ila kipindi chenyewe sijawahi kukiangalia akiwa anatangaza yeye yawezekana ni kero kama wengi mnavyosema.
 
Km muda mchache afanye km Take One ya Mtetema Clouds... Yaani amuhoji mgeni ata kwa masaa mawil then arushe kwa episod za dakka 45 angalau mara 2 au 3.
maana kwa sasa dakka 20 mgen 25 mahela
 

Attachments

  • 13770292_534695356714538_2272937666833427535_n.jpg
    13770292_534695356714538_2272937666833427535_n.jpg
    111 KB · Views: 83
Kweli yule sijui Simiyu sijue Semuyu alikuwa anajitahidi kidogo na Buhohela wa Ikulu.
Tatizo huyu Sam baada ya kuona mwenzake Buhohela kapewa shavu Ikulu basi anadhani na yeye kwenye Dakika 45 akiitetea Serikali basi ataitwa jumba jeupe.....Bure kabisaaaaaa

Anaingilia ingilia mahojiano,anauliza swali halafu anajijibu mwenyewe yaani ni vurugu tupuuuu....Hawa vijana wa Cameroon tabu tupu aseee.

Yule Simiyu mi alikuwa ananiacha hoi uvaaji wake...Utamkuta ana kiatu kirefu kama chopeo,yaani jamaa ana mguu hatari...juu anavaa tai ya kachumbari ndefuuuuu inafika magotini na suruali ya "selebresheni" kama mcheza show wa Madiluuu,huku shati over size kubwaaaaaa...Au koti la kushona kwa fundi Juma pale Mtaa wa Msisiri Kinondoni....Dressing Code ya Simiyu ilikuwa balaaaa!!Hata sijui yukwapi jamaaa!!
Duh! Hiyo paragraph ya chini umenifurahisha sana.. Eti kama mcheza show wa Madilu
Nimekumbuka ule wimbo wake wa Ya Jean
 
Tangu siku Sam Mahela alipombana Msigwa kwa maswali magumu ambayo msigwa alionekana kuhangaika vijana wa UKAWA hasa chadema mnamchukia sana Sam Mahela.
Hizi chuki zenu hazina msingi wowote acheni jamaa afanye kazi
Hata salim kkk kachukiwa kisa kamuuliza maalim Seif eti kwanini kama alikuwa kashinda kwanini asingeendelea na uchsguzi ili kudhihirisha ulimwengu kuwa aliibiwa kweli!
 
Huyu jamaa vipi jamani?! Nimefuatilia kipindi cha DK45 ITV na leo mgeni ni N/Waziri wa Muungano na Mazingira na mada ilikua ni Mazingira.

Huyu Sam Mahela, kama kawaida yake kuingilia mzungumzaji wakati anatiririka vizuri kwenye mada husika. Anageuka kuwa mzungumzaji Mkuu, anatoa maoni yake Mfano...."Mimi/sisi waandishi wa habari tumefanya tafiti na ni kweli/sio kweli kwamba Kuna uharibifu wa Mazingira"..... Sasa kama ulikua unajua ukweli/uongo wa jambo ya nini kumwalika mgeni studioni wakati ulikua na misimamo yako kwenye topic husika?

Mfano alipokua akiagana na N/W huyo, akawa anamsisitiza "Fanya kazi, umesikia, fanya kazii, umepewa kazi ufanye, sawa... maana hata mm hapa ITV napiga kazi"..... Hapa ni kiherehere tu cha huyu maana sio wajibu wake kumweleza hayo.

Nimekuwa nikifuatilia kipindi hiki lakini watu wengi wanakereka sana na huyu jamaa..... Atulie, atoe nafasi ya mgeni husika kusema na baada ya hapo maswali.

Mwanzilishi wa kipindi hiki na Buholela walikua wazuri sana sio kama huyu kijana.

Anafaa zaidi akabidhiwe kipindi cha Sara Kipingu
 
Tz waandishi wa habari wengi kwenye kuhoji ni Zero plus...
mfano hata wakikutana na wanasiasa wanatumbua mimacho tu kusikiliza wanachosema...hawajiandai kwa maswali magumu na maswali ya papo kwa papo...
Ukilinganisha na wenzetu unaweza kuacha kuangalia vipindi aisee...
Hivi wanajifunza skills za interviews kweli? Hivi wana taaluma yoyote nje ya uandishi? mfano kuna mwandishi wa habari za mazingira?
Sio wote, Kuna huyu Tido Muhando naona yuko vizuri
 
Huyu jamaa vipi jamani?! Nimefuatilia kipindi cha DK45 ITV na leo mgeni ni N/Waziri wa Muungano na Mazingira na mada ilikua ni Mazingira.

Huyu Sam Mahela, kama kawaida yake kuingilia mzungumzaji wakati anatiririka vizuri kwenye mada husika. Anageuka kuwa mzungumzaji Mkuu, anatoa maoni yake Mfano...."Mimi/sisi waandishi wa habari tumefanya tafiti na ni kweli/sio kweli kwamba Kuna uharibifu wa Mazingira"..... Sasa kama ulikua unajua ukweli/uongo wa jambo ya nini kumwalika mgeni studioni wakati ulikua na misimamo yako kwenye topic husika?

Mfano alipokua akiagana na N/W huyo, akawa anamsisitiza "Fanya kazi, umesikia, fanya kazii, umepewa kazi ufanye, sawa... maana hata mm hapa ITV napiga kazi"..... Hapa ni kiherehere tu cha huyu maana sio wajibu wake kumweleza hayo.

Nimekuwa nikifuatilia kipindi hiki lakini watu wengi wanakereka sana na huyu jamaa..... Atulie, atoe nafasi ya mgeni husika kusema na baada ya hapo maswali.

Mwanzilishi wa kipindi hiki na Buholela walikua wazuri sana sio kama huyu kijana.
Hujajua kumbe utaratibu wa mahojiano. Hufuatilii mahojiano mbali mbali huko duniani. Kama unamfuatilia Dr Shaka Ssali vizuri na kila wiki utajua kuwa Sam yupo sahihi. Anayehojiwa anapaswa kuwa chini ya mhojaji. Na mhojaji lazima afahamu vizuri jambo analohoji. Hayupo pale kuhoji kwa niaba yake bali kwa niaba ya watazamaji. Hivyo haupo well informed na namna mahojiano yanavyoendeshwa. Yule aliyeanzisha Seleman Semunyu alikuwa anakosea sana namna ya kumhoji mtu. Alikuwa anaongoza kupata jibu badala ya kumwachia atafute jibu. Hao wawili uliowasifia pia walikuwa wanapwaya. Asante. Tazama na wengine huko duniani wanahoji vipi viongozi. Usitake kuleta mahojiano ya watangazaji wa clouds Fm hapa.
 
Acheni wivu nyie waswahili kama anakuboa tengeneza TV yako.
 
uswazi ya zembwela na musa aliekwenda clouds uje tena hapa dakika 45 za emanuel buhohela na huyu sam utagundua waanzilishi walikuwa vichwa.
Umenikumbusha, Kipindi cha uswazi nilikuwa nakipenda akiwemo Musa lakini sio Zembwela
 
Tatizo la Sam hajui kwamba kuna kitu tunaita closed questions, open ended questions and rhitorical questions
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom