Simulizi: My Boss, my love

mireille

JF-Expert Member
Mar 4, 2020
523
568
MY BOSS MY LOVE NO:01

MTUNZI....... RITHA STORIES

WHATSAPP.........0763836152

Kwa majina natwa Lilian Adrian jina la tatu mliache nitawatajia siku nyingine

Mimi ni Binti wa miaka 27
Nimezaliwa mkoani Tanga mama yangu ni msambaa alafu baba yangu nasakia ni mpemba

Ninavyosema nasikia iko hivi ngoja nifafanue mimi Simjui baba yangu kwa sura Wala kwasauti

Mama alisema kuwa alimpa mimba kipindi Bado yuko shule akaikataa ile mimba na akatoroka kukwepa kufungwa

Aliamua kupambana mwenyewe alinizaa na kunilea hadi nilipofika miaka 7 akawa amepata mwanaume wa kumuoa akaniacha mm kwa Bibi yangu Tanga na yeye akaenda kuishi mwanza

Namshukuru Mungu mama yangu pamoja na bibi yngu wamekuwa ni watu wathamani sana katika maisha wangu

Kwakua mama yangu aliishia njia katika ndoto zake alikuwa akilia sana na kumuomba Mungu nisiishie njiani

Mungu ni mwema nilisoma hadi nikamaliza elimu ya juu
Mama yangu alifurahi sana

Baada ya kumaliza chuo shida ikabaki kwenye kupata kazi nyie nilizunguka kwenye ma office ya watu mpaka basi miaka 4 yote natafuta kazi bila mafanikio

Mwishoni nikaamua kuachana na habari za kuatafuta kazi nikaniajili mwenyewe

Nilianza kufanya biashara ya vitafunwa mwanzo ilikuwa ni nzuri na yenye faida ila sijui akaingia mdudu gani nikawa siuzi kabisa

Mwanzo nilikuwa nauza chapati maandazi vitumbua na sambusa lakin ilifika mda vyote vikafa nikabaki nauza maandazi tena na yenyewe nilikuwa nauza siku mbili na mda mwingine yanabaki hadi siku ya 3 tunaamua kula siku nzima

"We Lilian kulikoni leo umelala hadi saizi" alikuwa Bibi yangu kipenzi amekuja kuniamsha

" Leo sipiki kitu"

"Hee kwann unaumwa?"

"Hapana Bibi siumwi ila nimechoka kila siku kuamka mapema napik alafu naambulia hasara "

"Sikia mjukuu wangu hasara ni jambo la kawaida kwenye biashara huwezi kupata faida kila siku ndio maana Kuna jua na mwezi kiangazi na masika hivyo hutakiwi kukata tamaa kabisa "

"Hata usihangaike kutafuta misamiati siendi

"Bibi Kila siku unaniambia hivyo hivi mara ya mwisho lini nimepika hayo maandazi yakaisha yaani Kila siku ni hasara tu hadi nachoka "

"Hata usijihangaishe kuongea misamiati siendi nimeshachoka kufanya kazi za hasara "

"Sawa pumzika basi "

Bibi aliondoka chumbani kwangu nikabaki nimelala huku navuta usingizi

Usingizi ukiwa umenoga nilishtuliwa na sm iliyokuwa inaita

"Aaaaa nani tena asubuhi yote hii" nikiangalia aliye kuwa napiga nikakuta ni mama heee nilikurupuka na kukaa nikapokea haraka

"Hallo shikamoo mama"

"Nina habari njema mwanangu"

"Umenishtua nikajua Kuna tatizo"

"We unawazaga matatizo tu"

"Okay niambie habari gani hizo "

"Nimeota umepata kazi tena yenye mshahara mzuri sana "

"Kumbe umeota nikajua unaniambia nimepata niende "

"Hiyo ndio shida yako huna Imani kabisa "

"Imani?mama ni mara ngapi umesema kuwa Mungu kakwambia kuwa napata kazi ?"

"Mwanangu Mungu huwa hadanganyi Wala hawahi au kuchelewa bali anafanya kwa wakati wake na bakuli kua huo Wakati ni sasa"

"Mmmm haya amina "

"Amina mwanangu sasa nakutumia Hela ukanunue nguo za kazin sawa"

"Ila mama na wewe sasa unanitumiaje Hela wakazi yenyewe haijapatikana "

"Imani ni kuwa na hakika na mambo ya tarajiwayo ni baina ya mambo yasiyo onekana"

"Amina tuma mama"

Alikata nikaweka sm pembeni nakuendelea kulala
Nilikuja kuamka saa mbili nikakuta bibi ameshapika chai nikanywa na kwenda kufua nguo

Mchana mama alituma 150000 ili nikanunue nguo

Nyie mama yangu ananipenda basi tu

Mungu anitunzie mama yangu ili aje afaidi matunda ya mwanae

Baada ya kumaliza kazi zote niliamua kukaa zangu chumbani kwangu nikiwa bz napitia picha za mimi na . marafiki zangu kipindi tukiwa chuo

Nilijikuta njisikia vibaya kwani marafiki zangu wote walikuwa wanamisha Yao mazuri tu na kazi nzuri na baadhi yao walikuwa tayari wameshapata wenzi wa maisha yao

Ila mimi sasa sina kazi Sina mchumba Wala msebure miaka ndio hiyo inaenda



MTUNZI......... Ritha stories

WHATSAPP...........0763836152

Nikiwa katika ndimbwi la mawazo nilishitushwa na sm yangu ilikuwa inaita
Haraka niliichukua na kuangalia alikuwa ni rafiki yang Tuli

"Hallo my Tuli".
"Nyooo baada ya kukupigia ndio unajifanya my Tuli"

"Aaaa bwana usiniambie umenuna"
"Nisinune vp wakati hata sim hutaki kunipigia sijui ndo ushapata rafiki mwingine kwaiyo umenisahau"

" Aaa weee naanzaje kukuacha rafiki yang kipenzi "

"Mh hay bhn ,haya tuachane na hayo sikia nimekupigia kukupa habari njema "

"Usiniambie unaolewa"

"We nawe unawazaga kuolewa tu"

"Sasa kimebaki nini kama wewe umesha soma na kazi tayar "..

"Bibi wewe niache kula bata eti nikimbilie kuolewa hivi unadhani ndoa mchezo we zisikie kwa watu tu na uziache hivyo hivyo, hembu ngoja niende kwenye point, ni hivi hapa kazini Kuna nafasi za kazi za watu wa 5 wawili wa kozi yko na hawa wengine wakitengo kingine sasa hapa nimeshakenua meno kwa meneja ili upate nafasi"

"Weeee usiniambie "

"Ndio hivyo mpenzi kwaiyo kesho nakuomba ufike Dar mapema ili kesho kutwa ukafanye interview"

"Ndio maana nakupenda T wangu Mungu akuweke my dear "

"Usijali my utoke sasa maana umeshachoma maandazi hadi ukipita unanukia hiliki tu"

"Hahhahaha hay mpenzi asante sana "

"Poa basi ngoja niende kwa shemeji yako "

"Haya mpe hi"

Tuliagana nikakimbia nje huku nikishangilia na kwenda kumkumbatia bibi akiwa zake bz kufuma mikeka

"Wewe unata kunivunja mabega yangu"

"Bibi na wewe jitahidi kuwa mzungu hata kwa mda basi hapa ulitakiwa usema hey be careful and why you're so happy, sio unataka kunivunja "

"Nimekosa nn hadi niwe mzungu "

"Achana na hayo ni hivi nnimepigiwa sm na T anasema Kuna nafasi ya kazi huko dar kwaiyo natakiwa kuondoka kesho "

"Mama yako ameshaniambia"..

" Mama amekwambia "ilibidi niiulize kwanza kwani mama kajuje T amempigia hapana T hawezi kumpigia mama

"Alisema kuwa Mungu kamwambia "

"Oooo! Basi ndio hivyo "

"Kwaiyo kesho nabaki pekee yangu " bibi aliongea kwa unyonge nilijikuta na jisikia vibaya nikamkumbatia na kumwambia

"Hapana huatakuwa peke yako niko na wewe japo kimwili hatutakuwa wote ila kiroho Niko na wewe"

"Kwaiyo tutoke kwenye huu mwili tuishi kiroho"

",Wewe tena hata sijui babu alikupataje"

"Eee muache Mpenzi wangu"

"Umezidi mwanamke hauko romantic hata kidogo uko kibabe tu"

"Mwezio alinipendea ubabe sasa wewe endelea na uromantic wako"

"Subiri uone kama sijakupindua "

"Si mpaka uweze"

Basi tukipiga story pale ilipofika jioni nilimwaga nguo zote kitandani nikachagua zile nzuri Kisha nikaziweka kwenye begi

Mara sim ikaita kuangalia ni mama

"Hello dada Vanessa"niliongea kimatani, huwa nimezoea kumtania basi akiwa vibaya ananichambaga mpaka basi

"Koma wewe nani dada yako"

"Hahahahahaha wamesha kuvurugwa tayari "

"Mbona hujaniambia kama unaenda kufanya interview kesho kutwa "

"Hee mama we siumeshajua kabla yangu "

"Hata kama ungeniambia "

"Sawa dear mama nisamehe "
"Haya umeshajiandaa"

"Ndio mama "

"Na nguo ulinunua'"

"Hapana nitanunua nilifika huko huko "

"Kwaiyo kwenye hiyo interview utaenda umevaa
nini "

'" nguo za kuvaa zipo nyingi"

"Haya utajua mwenyewe,ila jitahidi kwenda ukiwa smart"

"Hilo tu usijali"

"Haya jioni njema"

"Haya mama byee"

"Alafu uoshe hizo nywele usije kwenda kwenye office za watu na minywele inayonuka "

"Mama bhn ushaanza mambo yako"

"Mambo yangu yamefanya nn we osha hicho kichwa tena ikiwezekana ukasuke kama huna hela sema nikutumie "

"Kusuka tena bora nioshe tu"

"Osha na usuke nakutumia hela ukasuke sasa ole wako bibi yako aniambie hujasuka".

"Sasa mama nasuka sangp wakati safari ni kesho asubuhi "

"Sasaivi unanyonyesha au uko mazishini"

"Eeee haya nitaenda "

"Na uoge vizuri "

"Tena haya mama"

Hakutaka hata kuaga akakata sm

Nyie ngoja niwaambie moja kati ya vitu ambavyo sipendi ni kitu kinaitwa kusuka Nina unywele huo balaa ila nasuka mara moja kwa miezi na zinakuwa kama maboga alafu zimejaa yaani hewa haipiti kwenye ngozi

Huwa natamani kuzinyoa ila mama yangu sasa heee alishaniambia ole wangu ninyoe yan anazipenda kama zake vile

Namvutia waya tu siku atasikia Nina upala

Basi niliosha nywele mda huo muamala ukasoma mama kasha tuma hela huyu mwanamke na nywele ni bala

Baada ya kumaliza kuosha nikaenda kusuka kwa dada mmoja hivi jirani yetu

Kesho yake niliamka asubuhi nikaongozana na bibi hadi stendi tukaagana Kisha nikapanda gari na safari ya kuja dar ikaanza


MY BOSS MY LOVE 03

MTUNZI........... RITHA STORIES

WHATSAPP..... ...0763826152

Baada ya masaa kadhaa nilifika dar nikaona nipite kununua nguo ili nilifika nyumbani nipumzike

*****Nilinunua nguo Kisha nikapanda dala dala hadi kigamboni huko ndiko alikuwa akiishi rafiki yang Tuli

"Heeee mrembo wa kitanga naona umeshaingia "

"Acha maneno mengi we nikaalibishe ndani alafu nipe ugari nile zangu maana hapa naona giza tu"

"Wewe tena nakula hujambo,mh za huko utokako"

"Nitokako nzuri , naomba chakula basi au unataka nife kwa njaa"

"Bwanaee usini pelekeshe we umefika tuliza mshono hapo "

Alienda jikon akaniletea chakula kwajinsi nilivyokuwa na njaa nilikifakamia chap nikamaliza

"Bado tu hujajifunza kula kama mtoto wa kike"

"Unikome yaani ninanjaa alafu nianze kuokota punje moja moja ili iweje au nimekuwa ndege ,

haya unaweza kunisalimia hapa naona mwanga"

"Mh huyo shemeji kazi anayo naona huko aliko aandae mashamba ya kulima maana mke anae"

Basi tulipiga story kama zote mda wa kulala ulipofika tulilala

Nilikuja kuamshwa na sim ya mama akitaka tuombe

Alianza kuimba nyimbo za kusifu akaingia kwenye za kuambudu,Toba kisha akaanza kuomba mimi nilikuwa narudia Yale maneno aliyokuwa anatamka

Aliomba hadi ikafika mda nikachoka nikabaki namsikiliza tu ............ kwanzia saa kumi hadi saa kumi na mbili na robo ndio tukamaliza akaniaga na kunitakia siku njema

"Mh mama yako anakipawa Cha kuomba sio poa yaani mda wote huo haishiwi maneno"

"Nakwambia Kuna watu Mungu kawabariki mimi nikiomba Sana dakika 5 "

"Haya nisikupigishe story ukachelewa bure "

Niliinuka nikaenda kuoga Kisha nikatangulia kutoka yeye siku hiyo alikuwa anachelewa kuingia kazin

Nilifika kwenye hiyo kampuni nilikutana watu wengi yaani kama wamelala pale

Niliangalia watu walivyokuwa wengi na watu wanao hitajika mh moyo ukishuka nikaona hapa sijui labda Mungu aweke mkono wake

lakin nilikumbuka mama alisema kuwa hata kama kutakuwa na watu Zaid ya elfu kumi na wakawa wanahitaji mtu mmoja mimi naamini utapita na ninakili hilo sio mimi tu unatakiwa pia ukili hivyo

Basi nilikaa zamu yangu ilipofika nikaingia nikafanya interview ikaenda vizuri tu Kisha nikaambiwa nitapewa jibu

Baada ya kuambiwa hivyo nilirudi nyumban

Wiki ilipita sijapokea sm wiki ya pili ikapita mh hapo nikaamini kuwa sitopata

Jioni Tuli alikuja akanambia kuwa wamechagua wengine na leo wameanza kazi

Nilijisikia vibaya nikakumbuka mama alivyokuwa anasema kuwa ameoneshwa na maombi yote tuliyokuwa tumeomba jumlisha na sadaka ambazo tumekuwa tukitoka

Nikajikuta nasema kwa sauti yenye maumivu sana

"Mungu kwann lakin"...... Tuli alisikia akanitia moyo pale mwisho nikaona nimpigie mama nimpe taarifa

"Hallo mama"

"Umeshindaje mwanangu mzuri "

"Vibaya ile kazi nimekosa tena"

"Amekwambia nani kuwa umekosa kazi "

"Mama sio kaniambia nani watu wame shachaguliwa na kazi wameanza "

"Subiri wakat wako wa kuchaguliwa unafika Kwan Mungu wangu hawezi kuongea uongo "

Ukweli nilimuona mama kama nini sijui nikaamua kukata sm

Nilipanga nguo zangu tayar kurudi kijijini

"Lakin Lilian kwanini usikae tu hapa tukatafuta kaz nyingine kuliko kwenda kijijini "

"Hapana Tuli bora nikakae na bibi yangu"

Tukiwa bado tunaongea sm yangu iliita niliichuka nakuwangalia ilikuwa ni namba ngeni

Nilibonye kitufe cha kupokea (natumia kiswaswadu)

"Hello"
Ilisikika sauti upande wa pili alikuwa ni mwanamke

"Yes hello"

"Naongea na miss LILIAN ADRIAN"

"ndio ni mm"

Aliongea kitu ambacho kilinishtua nikabaki nimetoa macho

"Wewe vp mbona umekuwa hivyo" Tuli aliuliza baada ya kuona nimetoa macho nilimuangalia na kusema

"Nimepata kazi"weeee aliruka na kushangilia

"Uuuu asante Mungu kukumpatia kazi rafiki yang kipenzi "

"Ila sio kwenye kampuni unayofanya kazi "

"Heee kwa ulifanya interview na kampuni gani"

''moja tu ila Hawa walio nipigia nilifanya interview mwaka mmoja ulio pita ''

"Heee hii inawezekana je"

"Sijui " nilibaki nimekaa tu yaani sikuelewi nini kimetokea nikaona nimpigie mama nimpe taarifa

"Mama nimepata kazi "

"Nilikwambia kuwa Mungu wangu ni Mungu wa kweli akisema anatimiza"

"Amina ila sio kwenye hii niliyoenda kufanya interview bali ni Ike niliyofanya mwaka Jana "

"Mwanangu Mungu hawahi Wala hachelewi Bali anajibu kwa wakati na huu ndio wakat wenyewe "


MY BOSS MY LOVE NO 4

Mtunzi......... Ritha stories

Whatsapp no 0763826152



"sasa hiyo kampuni si Iko dodoma"

"Ndio mama"

"Kwaiyo inakuwaje"

"Inabidi niende na nimeambiwa kuwa natakiwa kuanza kazi kesho kutwa"

"Heee sasa utaweza kupata nyumba kesho "

"sidhani mama mimi naona niende tu nitalala gest alafu nitafuta ndani ya siku mbili hivi nitakuwa nimepata"

"Haya basi ngoja nitakutumia Hela kesho mchana naimani nauli utakuwa nayo"

"Ndio mama "
Alikata sm tukabaki tunayapanga na Tuli wangu

Kesho asubuhi alinisindikiza hadi stend akanipa sma yake kubwa pia akanipa na Hela kiasi

Nilimshukuru Sana Kisha nikapanda gari

Nilifika dodoma muda wa saa kumi nikaenda kwenye gest mbayo nilifikia mwaka Jana

Nilichukua chumba nikalala nilikuja kuamka saa tatu' nikatoka na kwenda kupata chakula

Kesho yake asubuhi niliamka nikajiandaa Kisha nikaenda kupanda dala dala saa kumi na mbili na dakika 45 nikiwa tayar ofisini

Kwakuwa ilikuwa Bado mapema ilibidi nisubiri maana watu walikuwa Bado

Saa moja na nusu ndio watu wakaanza kuingia

"Habari yako dada"

"Nzuri, nikusaidie nn"

Nilijieleza bale akanambia meneja hajafika msubiri

Basi nikakaa kumsubiri

Baada kama nusu saa alifika nikaenda ofisini kwake

"Miss Lilian "
"Yes"
'karibu sana '

'asant '
"Okay shika hili file alafu uende gorofa ya tatu juu chumba no 5 ukifika huko utampa hilo file alafu atakwambia Cha kufanya '"

"Sawa asante sana"

"Karibu"niliinuka na kuondoka nikapanda lift hadi sehemu husika

Nilifika nikagonga mlango Kisha nikaruhusiwa kuingia

"Karibu"alinikaribisha baada ya kuingia ndani

"Asante"

"Bila Shaka wewe ndio miss Lilian Adrian"

"Yeah ndio mimi"

"Okay unatakiwa kusaini huu mkataba "nilipokea nikausoma baada ya kusoma nikalidhika nao nikasain

then akamuita mdada mmoja hivi akasema kuwa huyo ndio atakuwa msaidizi wangu kwakipindi hili ambacho Bado ni mgeni
akamwambia anipeleke kwenye office yangu

Nilimshukuru Sana Mungu kwani nimepata kazi nzuri na ina msharaha mnono

"Waooo office ninzur so poa yaani imekaa kimataifa Zaid nilirudi nyuma na kuangalia mlangoni kulikuwa na jina langu waoo kweli Mungu akikuinua anakuweka viwango vya juu zaidi"

"Samahani we ni ndugu yake Mr Sam ee" aliniuliza yule dada (Recho)

"Mr Sam ndio nani "

" Chef Director"

"Hapana sio ndugu yangu kwann"

" No nimeuliza maana hii kampuni hawaajili mtu asiekuw na uzoefu,na shangaa wewe huna uzoefu na umeajiliwa"

Nilitabasamu na kumwambia
"Ni Mungu tu''"

"Mmh haya bhana basi mimi naondoka ukihitaji kitu utaniita"

"Sawa asante sana "

Aliondoka nikachukua sm na kumpigia mama aliniambia kuwa nikifika kabla sijakaa kwenye kiti changu nimpigie

Alipokea akasema nivyema kumshukuru Mungu na kuomba ulinzi pamoja na kuvunja maroho yote machafu pia kama Kuna kitu kilichomtoa Alie kuwa kabla yangu kisinipate

Basi akaomba mimi kama kawaida yangu namfatiliza kile anacho ongea

Baada ya maombi akaniambia sasa unaweza kukaa Mungu akutangulie katika kazi yako mwanangu

Nikaitika "amen " Kisha nikakata sm na kuanza kazi

Nilifanya kazi hadi mda wa chai nikamfuata Recho tukaenda sehemu ya chakula

Tukifika tukaagiza chai ikaletwa tukanywa mda wakulipa akasema kuwa mimi sitakiwi kulipa kwakua watu walioko ngazi ya juu wana pata chakula bure

Nilishangaa maana sijawahi kuisikia hii

Yaani nimekunywa chai kwa kujibana kumbe ni bure

Tuliinuka na kurudi ofisini ratiba zingine zikaendelea

Mchana ulifika tukaenda kula safari hii nilipiga msosi haswaa chezea vya bure wewe

Wakati tukiwa tunakula nilimuuliza Recho kuhusu nyumba kama anaweza kujua mdalali aniunganishe nao

Akanambia atanifanyia mpango

Kweli jion ilipofika mda wa kuondoka akanipa namba ya dalali nikamtafuta tukapanga kuonana

Kwakuwa ilikuwa bado mapema nikaenda kuonana nae akanipeleka kwenye baadhi ya nyumba nikaangalia

Baada ya kuzunguka sikupata nyumba maana bei ilikuwa juu sana nikiangalia na Hela yangu haitoshi kabisa

Nikamuomba anipeleke ambazo bei yake iko kawaida tu

Tukapata ila shida kukawa ni mbali na kazin

Nikabiga mahesabu ya nauli na hiyo Kodi nikaona nibora nikapange kwenye zile ambazo ziko karibu na kazin ambako sihitaji kupanda gari

Nikaona hapa nina haja ya kukopa Hela nikampigia Tuli nikaongea nae hakuwa na neno kipenzi changu alikubari na baada ya dakika kumi tu akanitumia Kisha akasema

Hain haja ya kunilipa nimekupa kama best friend wangu

Nyie nilishukuru hadi nikatamani kumpigia magoti kwenye sm

Nikalipia miezi yangu sita iliyobaki nikanunua vitu vyichache kama ndoo ya maji na ya kuogea,jiko la mkaa,sufuria 2,sahani mbili, vijiko viwili,
Na vingine vidogo vidogo

Kisha nikarudi kule gest nikalala kumalizia hela yangu

Kesho yake nikaingia job Kama kawaida


MY BOSS MY LOVE 05

Mtunzi........ Ritha stories

WHATSAPP .......0763826152

Nilifanya kazi ipofika jioni nikaenda kule gest nikachukua nguo zangu
Na kumkabidhi chumba Kisha nikaenda kule nilikopanga

Nilifika nikafungua mlango nikaingia

Niliangalia mazingira ya chumba kilikuwa kinachekesha yaani hamna hata godoro ni mkeka na neti ndoo mbili sufuria sahani mbili jiko na beseni ndogo basi

Nilitandika mkeka na kuweka neti kish nikaenda kuoga. (choo na bafu vilikuwa humo humo ndani"

Baada ya kutoka kuoga nilikaa na kupiga story na Tuli hadi saa tano ndio ni kalala

Wiki iliisha huku maisha yakisoga kama kawaida

Siku moja hivi ilikuwa ni weekend
Nikiwa nje nafua liliingia gari mule ndani akashuka mkaka mmoja hivi nilivyomuona tu nilidondoka pale pale na kuzimia

Nilikuja kuamka nikiwa hospital yaani nafungua macho tu namkuta yule kaka kakaa pembeni yangu nikazimia tena

Baada ya mda niliamka tena safari hii hakuwepo

Niliamka na kukaa huku nikiwa na mwazo nilijiuliza hivi nimeona mzimu au nilikuwa naota

Na kama nikuota mbona Niko hapa hapana ni kweli sasa inawezekanaje frank akawa hai jamani au kaanza kunitokea

Sijakaa sawa akaingia nesi

"Heee umeamka?"
(A aha nimelala yaani haya maswali ya kijinga huwa siyapendagi mm yaani mtu anakuja anakuuliza kitu ambacho anajibu nacho kabisa ) niliongea kichwani

"Samahani sana nesi nimefikaje hapa"

" Umeletwa ukiwa umepoteza fahamu "

"Ooo nimeletwa na nani"

"Na jirani yako"
Jirani yupi mbona yule mmama hayupo

Niliwaza maana pale nilipopanga tunakaa wawili tu yaani mimi na mmama mmoja hivi tena na yeye hayupo sasa huyo jirani ni yupi ,ona sasa nilivyoanza kuvurugwa nimeshahau kama pale Kuna mlinzi nahisi atakuwa ndio amenileta hapa

Nikiwa bado nawaza yule kaka akaingia

Nilitoa macho kuhakikisha naota au naona mzimu

Lakin hakuwa mzimu maana alikuwa akiongea na nesi sasa Kam ni mzimu inamaana ningemuona mim
tu

nesi akaondoka yule kaka akasogea karibu yangu na kuniuliza
"Vp hali yako unajisikiaje" sikumjibu zaidi nilikuwa namuangalia kwa huzuni sana nilijikuta namkumbatia huku nikilia

"Frank kwann uliniacha" niliongea na kilio Cha kwikwi hakunijibu Bali alikuwa akinipapasa mgongoni kama ana nibalembeleza vile

Nilijitoa na kumshika usoni "frank asante asante kwakuja tena kwenye maisha yangu nakupenda sana " yaani nilikuwa Kam chizi gafla tu msikini kaka wawatu alikuwa ananiangalia tu sijui alikuwa anawaza nn au aliniona chizi

Nililia Sana mwisho akaamua kuongea

Mmmm akakohoa kidogo Kisha akasema

"Pole kwa yaliyo kukuta lakin mimi sio Frank ila ni Bosco "

"No wewe ni frank wangu "

"Dada samahani najua hauko sawa ila mimi sio huyo Frank "

Alivyoongea hivyo nilimuachia Kisha nikasogea pembeni huku mchozi yakushuka tu nilimkumba Frank wangu sana nikabaki nalia tu

Alipoona hali yangu akaondoka na kuniacha mwenyewe

Alikaa kama lisaa akarudi tena nilimuangalia vile vyokuwa akiingia yaani hata kutembea anatembea kama frank wangu

"Unajisikiaje kwa sasa"aliuliza baada ya kukaa

"Niko sawa asante" nilijibu kama vile Niko sawa ila sikuwa sawa kabisa kila nilivyomungalia kumbukumbu zote nikiwa na Frank zilikuwa zinajirudia kichwani moyo uliuma sana

Akilini niliwaza inakuwaje watu wakafanana namna hii

Doctor alikuja akasema kuwa niko sawa naweza kwenda nyumbani

Basi tukatoka tuliingia kwenye gari na kurudi nyumbani njia nzima nilikuwa namuangalia tu

Tulifika akashuka na kuja kunifungulia mlango

"Unakaa chumba kipi" aliuliza nikamuonesha akataka kunishika ila nikamwambia niko sawa so naweza kutembea mwenyewe

Basi nikaingia ndani sikutaka hata aingie ndani maana kilivyo hakufai hata mtu kuja

Alielewa akahakikisha nimeingia ndani

Nilifika ndani nikajikuta picha yote ya maisha yangu na Frank ilirudi kwenye kichwa changu

Nilikaa chini kama mzigo kilio kikaanza upya

"Frank kwann lakin"

Nilikumbuka siku ya kwanza kuonana na Frank

Ilikuwa siku ya j 4 kipindi hicho ndio naingia chuo mwaka wakwanza

Siku hiyo nilikuwa nimetoka kumuona mama yangu mdogo gongolamboto nikiwa nimesimama kusubiri gari alikuja mkaka mmoja na kusimama nyuma yangu akanifunika koti kwa nyuma

Nilishtuka sana na kugeuka akaniangalia kama vile hajikatokea kitu akasema

"Umechafuka" aliponiambia hivyo lilinishtuka nikataka kugeuka akasema

"Kuwa na amani nisubiri hapa nakuja"
Nilibaki kimya tu kugeuka nilitamani ila nilifikilia watu walioko nyuma nikaona hiii ni aibu

Baada ya dakika chache akawa amerudi ameshika mfuko hata hakunisemesha
Alinishika mkono tukaongozana yaani nilikuwa kimya nikifikilia kweli siku hiyo ilikuwa siku yangu ya kuingia kwenye siku zangu

Lakin nilisahau na kutoka bila hata bila kuvaa Pedi

Tuliongozana hadi tuka pita lile eneo nililokuwa akaniachia na kunipa ule mfuko

Nilitaka kukataa ila sikuwa na namna maana hata sikuwa na akiba zaidi ya nauli tu

Basi nikapokea na kwenda msalani nikafika huko nikaangalia kwenye ule mfuko kuliwa na gauni chupi na Pedi sabuni na mafuta

Nilibadilisha na kutoka chakushangaza sikumkuta niliangaza macho huku na huko ila hakuwepo

Nikaona nimsubiri ili nimshukuru na pia nimpe koti lake

Nilikaa wee hadi mda ukaenda sana lakin hakutokea
 
MY BOSS MY LOVE . No 6

Mtunzi..........Ritha
stories

Whatsapp.......0763826152

Baada ya kumsubiri kwa mda mrefu nikaamua kuondoka

Nilifika nyumbani nikampa umbea Tuli kama unavyojua marafiki yaani anakucheka kwanza alafu pole baadae

"Kwaiyo ulisahau kama utaingia leo au ndio ukijifyatua"

"Nijifyatue uwezo huo ninao "

"Pole ila hongera maana sijui ungefikaje huku yaani mbona ungekoma"

"Weacha tu Mungu amuweke kaka wawatu"

Nilichukua laptop yangu nikaanza kusoma

Zilipita wiki mbili siku moja tukiwa njian na Tuli nilimuona yule kaka akiwa kwenye gari huku ameshusha kioo Cha mbele

Nilitoa macho Baada ya kuona amevaa nguo za jeshi

Nyie enzi hizo nilikuwa nawaogopa wanajeshi kama ukoma yaani hata nikikutana nae nakuwa kama kifaranga aliezungukwa na mwewe

Nakumbuka kulikuwa na foleni magari yakawa hayaendi tuli simama mda mrefu nikaona anashuka na kwenda kuanza kuelekeza magari

Mda huo nikamtonya Tuli kuwa yule kaka Alie nipa koti yule

Weee alipoona yuko ndani ya gwanda alicheka sana akalinitania kuwa inakuwaje wakat wakumrudishia nguo yake

Kwakweli sijui ilikuwa ni utoto au nini hadi leo sijajua kwann nilikuwa nawaogopa Hawa viumbe

Mgari yanianza kwenda na lakwetu pia likaenda.

Nilifika nyumbani nikalingalia lile koti vizuri nikakumbuka Yale magwanda woi nikaiweka pembeni

Sasa moja kati ya vitu nilivyokuwa napenda actually napenda hadi leo

Ni maji nyie napenda mji Kama samaki sio kunywa no kuogelea yaani weekend zote huwa natamani nizimalizie beach tu

Kingine mziki hapo nahitaji maombi sijui maana mimi na mziki nikama moyo na mishipa au

Hta sijui nikuelezeeje ili unielewe

Basi kutokana na kupenda hivyo vitu nilikuwa ni mtu wa beach pia tulikuwa na kundi letu ambao wote tulipanga kuwa

Kila weekend ya mwisho wa mwezi lazima twende Beach

Na beach tuliyokuwa tunapenda sana kwenda ni south beach Iko sehemu flani hivi huko mji mwema kigamboni

Ile Beach tulikuwa tunapenda kwasababu ya mziki tu pia ilikuwa karibu na nyumbani maana kipindi hicho tulikuwa tumepanga kibada

Basi bhn Kila weekend ya mwisho wa mwezi tulikuwa tunaenda asubuhi kurudi sasa hadi jua lizame

Sasa weekend ya mwisho wa mwezi ikawa imefika Kama kawaida tukajiandaa

Siku hiyo tulikuwa tunaenda wote watu 8 hii ilikuwa ni team ya vichaa yaani tukifika sehemu lazima tu ujue kuwa tupo

Na ilikuwa ni team yenye pisi Kali kama zote

Alafu wenzangu walikuwa wanatoka kwenye familia zenye mapene ya kutosha kwaiyo mara nyingi nilikuwa napata kamseleleko

Baada ya kujiandaa Samira alikuja na gari akatupitia haoo tukachapa laba

Tulifika tukakuta wengine wamekaa wanatusubiri
Basi tukalipia na kwenda kubadilisha nguo Kisha tukaanza utundu wetu

Watu wa pale walitizoea kutokana nakuwa tulikuwa tunaenda mara kwa mara

Ilipofika saa kumi jioni tukiwa tunacheza niligeuka nikashtuka kumuona yule kaka akiwa amekaa huku anakunywa juice tena macho yote yalikuwa kwetu

Nilibaki nikiwa nimeganda tu
Wenzangu walinishangaa
Sasa Tuli siakamuona hee

Acha awambie wenzngu kilichonitokea

Sasa walivyo kuwa wakorofi wakatoka wote Kama walivyo Waka mfuata kaka wawatu

"Habari yako kaka" walimsalimia kwa pamoja

"Nzuri nyie je"

"Tuko poa aaa samahani tumekuja kukushuruku kwa wema uliomdendea rafiki yetu yuleee"
Waliongea na kuniyoshea kidole mimi mda huo nilikuwa natamani kupaa

Kwanza nilikuwa nawaza inaama atanifikilia kuwa mm ni mbea jamani

"Alafu anaogopa wanajeshi sijui mlimfanya nn"

Baada ya kusikia hivyo aliniangalia na kucheka
Nilisikia aibu 🫣balaa

Nikaona bora niende msalani /maliwato

Niliingia na kukaa kwa mda Kisha nikatoka ile natoka mtu huyu apa
Naona na yeye alikuwa ametoka msalani

Nilitamani kukimbia

Ila nikawaza hivi nakimbia nn ili iweje kwani kunakosa nimefanya jibu ni hapana basi

Nikasogea na kumwambia "asante "

"Karibu"

"Siku ile nilitoka nje nikakuta haupo so koti lako"

'"usijali ile nizawadi yako, na usituogope bhn sisi ni watu kama wewe ila ile nikazi kama kazi zingine"

"Sawa asante" nilijibu huku uso umejaa aibu balaa

"Una macho mazuri sana hasa ukiwa na aibu ndio yanakuwa mazuri Zaid " aliongea na kuondoka nikabaki nashangaa tu

Alitoka kabisa eneo lile vivuruge wangu wakaja kuniuliza nilikuwa naongea nn na mkorea mweusi

Yaani Hawa mda huu wameshampa na jina eti mkorea mweusi kisa kanipa koti na kuondoka


MY BOSS MY LOVE NO 07

Mtunzi....... Ritha stories

Whatsapp.........0763826152


Mda wakaondoka ulifika,
tukakusanya vitu vyetu na kuondoka

Njia nzima nilikuwa nakumbuka maneno yake🫣 haikuwa mara yangu ya kwanza kuambia Nina macho mazuri au kusifiwa
Lakin siku ile nilihisi kama ndio mara ya kwanza kusifiwa

Kila nilipokumbuka nilijisikia Raha ya aina yake

Kama unavyojua furaha haifichiki wenzangu waligundua kuwa nilikuwa natabasamu mda wote

Wakauliza kulikoni nikaamua kuwadanganya

Basi tukifika nyumbani wakaniacha wao wakaondoka pale nyumbani nilikuwa na kaa na Tuli

Na siku hiyo alienda kulala kwa Samira

Kwaiyo nikabaki mwenyewe niliuliza kama nilipika hata sikuweza yaani niligeuka chizi fresh

Nilichukua lile koti nikawa naliangalia huku nilifurahi kama nn sijui

Kutoka na kuwaza sana nikajikuta nachelewa Kulala

Kesho yake asubuhi niliamka kwa kuchelewa alafu nilikuwa na kipindi

Nilioga fasta nikajiandaa

Kisha nikatoka mbio

Nilifika kituoni nikakuta Kuna watu wengi sana

Nilinyea maana nilikuwa nachelewa kibindi

Nikaona hapa Bora nichukue bajaji au boda boda

Nikafungua zipu ya mkob wangu kabla hata sijachukua Hela nilishitushwa na gari lililokuwa likipiga honi mbele yangu uwiii niliruka ñikijua kinataka kunigonga ile naangalia kumbe lilikuwa limesimama

Kuangalia ni yule mkaka kanipa ishara kuwa ni niingie

Kwa vile nilivyokuwa nimechelewa nilipanda bila hata kujifikilia mara mbili(kama angekuwa mtu mbaya ingekula kwangu)

"Habari ya asubuhi" alinisalimia baada ya kuingia na kukaa

"Nzuri wewe je,"

"Niko poa unaelekea wapi"

"Udsm"

"Ooo sawa" aliwasha gari na kuondoka

Njia nzima mziki ndio uliongea ila sisi tulikuwa kimyaa

Alinifikisha nikamshukuru na kutaka kushuka Aliniambia nisubiri akatoa kikaratasi akachukua na peni akandika namba na kunipa

"Hii ni namba yangu nitafurahi kama ukinitafuta"
Nilipokea na kumshukuru Kisha anikashuka huyoo akaondoka

Niliingia kwenye kipindi jioni tukarudi nyumbani na Tuli wangu

Wakati wakulala nikachukua ile namba nikiandika kwenye sm na kusevu mkorea mweusi

Kisha nikatuma text "mambo" alafu nikaiweka sma mbali kabisa yaan kama nilitaka kuona akijibu alafu kama sitaki vile kiufupi nilikuwa sijielewi

Ilipita dakika moja Nika sikia zim zim
Chap nikachukua na kufungua alikuwa ni yeye kajibu
"Poa Lilian umeshindaje '"
Heee amejuaje jina langu inamana ananifahamu tena na namba yangu anayo niliwaza na kumjibu "Niko poa umejuaje kuwa naitwa Lilian"

"Hahhahha am nimesikia rafiki zako wakikuita hivyo"

"Okay na mbona umenijibu kwaku niita ulikuwa na namba yangu?"

"No sikuwa nayo ila Nilijua utanitafuta mda huu so nikahisi tu ni wewe na kweli ni wewe"

"Okay vizuri "

"Ufanya nn"

Nilimjibu Kisha akanipa story kama zote tukajikuta tunalala saa nane

Akasema kwakua amenichelewesha kulala basi anadeni la kunipeleka chuo kesho

Mimi ni nani nikatae nikakubari then tukalala

Na huo ndio ukawa mwanzo wa ukaribu wetu

Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa nimepanga na hali mashauri ya kichwa kuwa sitakaa niingie kwenye mahusiano hadi nimalize chuo

Lakin nilipokutana na Frank nilisahau kabisa kama niliwahi kupanga kitu kama hicho tena nikiwa bado mwaka wakwanza

Nikaingia penzini rasmi na Frank ..
Nakili kuwa nilimpenda frank kiasi ambacho siwez kueleza mkanielewa

Yaani kama kuzama basi nilizama hadi unywele au kama ni kufa basi siku Baki hata fuvu

N kipindi chote hicho sikuwahi kumjua mwanaume yeye ndio alikja kuniingiza kwenye Dunia ya mapenzi

Alinioshesha mapenzi ya hali yajuu hadi ikafika mda nikajiuliza kwann sikuwahi kumfahamu toka mwanzo

Nakumbuka siku ya kwanza kukutana nae kimwili ilikuwa ni siku ambayo sitakaa niisahau katika maisha yangu

Nilihisi maumivu lakin nilifurahi sana kuwa nimepa mpenzi zawadi ya thamani Sana. Frank baada ya kumaliza aliniangalia kama dakika tano bila kusema kitu huku machozi ya kimtoka

Nilishtuka nikamuuliza kwann analia hakuongea zaidi ya kunikumbatia na kunikiss huku akishika shika nywele zangu

Baada ya mda akaongea

"Lilian"
"Abee "niliitika kwa woga ñikijua huenda akawa anataka kuniacha nn au kunakitu kakiona ambacho hakijampendeza?

"Nakupenda sana mpenzi wangu nashukuru kwa zawadi hii uliyonipa nakuahidi kukupenda hadi pumzi yangu ya mwisho na nitapambana kuhakikisha nakupa furaha siku zote"

Niliposikia hivyo mchozi yalinitoka nikashindwa kujibu akanikiss Kisha akanibeba na kwenda kuniogesha

Kila nikikumbuka matukio yangu na yeye moyo wangu unagawanyika vipande vipande

Siku zilienda huku penzi lilikuwa Kila siku ilifika mahari nikawa sitaki hata kusikia mwanaume mwingine Akiniambia neno nakupenda yaani nilikuwa nachukia hatari

Nakumbuka kipindi nikiwa mwaka wa watatu Aliniambia tufunge ndoa

Nilikataa na kumwambia anisubiri nimalize kwani nilikuwa nimebakiza miezi tu

Frank wangu hakuwa na shida akakubari ila tukaenda kutambulishana kwa wazazi

Nashukuru Mungu tukilipata kibari kwa familia zote mbili na wakatombea tufikie malengo

Mwezi mmoja baada ya kutambulishana alinivika Pete ya uchumba Kisha tukaa kusubiri nimalize

Kila nikikumbuka nayajutia sana maamuzi yangu nibora ninge kubari huwenda ingekuwa tofauti


MY BOSS MY LOVE 08

Mtunzi...... Ritha stories

Whatsapp.......0763826152


Nakumbuka siku hiyo nilikuwa nyumbani kwake tulikuwa nataangalia tv

Huku tukipanga mambo mengi ambayo tutafanya tukioana kwani ilikuwa imebakia miezi michache ya mimi kumaliza chuo na kama ilivyokuwa makubaliano yetu kuwa
Nikimaliza tu tunafunga ndoa

Baadae akanambia kuwa baada ya wiki mbili anatakiwa kwenda kozi so anaomba nikae nae hata siku mbili tu

Nilimuuliza mbona imekuwa gafla hivyo

Akasema nikitu ambacho alikiomba mda ila alikuwa hajapata ruhusa kutoka kwa mkuu wake.

Basi nikasema poa nilikaa pale kwake wiki zote mbili

Siku moja kabla ya kuondoka alinikabidhi Kila kitu chake na kwanzia card za bank na hadi za viwanja na vingine vingi akanipa na neno Siri ya account zake

Nilijiuliza huyu mtu mbona ananiachia Kila kitu maana haikuwa mara yake yakwanza kusafiri na huwahi kufanya hiki kitu anachofanya leo

Ikabidi nimuulize alinijibu kuwa mimi ni mke wake so niwajibu wangu kutunza hivyo vitu nikiwa kama mke

Nilijisikia furaha kuona jinsi anavyonipenda

Akasema pia kama nitakuwa nahitaji pesa nina ruhusiwa kutoa

Basi nilifurahi na tukaufanya ule usiku kuwa watofauti sana kwa kupeana mahaba mazito

Kutokana na kipogo Cha pweza nilijikuta nachelewa kuamka mida ya saa tatu asubuhi ndio nikifumbua macho nikamkuta Frank
Wangu tayar kashajiandaa yuko ndani ya gwanda

Niliamka tukasalimiana pale nikaangalia mkononi alikuwa ameshika mkufu wa dhahabu

Akanambia "babe naomba nikupe zawadi "

Nikamwambia "sawa mkorea wangu" alicheka sana nilipomwambia hivyo

Lakin nilimuangalia nikahisi Hana furaha kabisa ila sikutaka kuliongelea maana nilihisi itakuwa kwasababu anaondoka

Akanivisha ule mkufu Kisha akanipa kitu French kiss
Yaani wiki hize mbili alikuwa anafanya vitu kwa hisia Kali sana kuliko siku zote

Baada ya kukiss nikifumbua macho nikaona anatokwa na machozi

Nilishtuka nikamuuliza kwann analia akanijibu

"Nalia kwasababu nakuacha mwenyewe "

"No frank huniachi mwenyewe na huto kaa uniache najua tutakuwa mbali na itakuwa ngumu kuwasiliana kwasababu ya mtandao na mazingira lakin naomba utambue ya kuwa niko pamoja na wewe kwa Kila hatua unayopiga mpenzi wangu sawa babe'"

"Niahidi kuwa hautolia au hata kama ukilia usilie sana utaniumiza, kingine naomba usije kunyoa nywele sawa"

Nilitabasamu baada ya kusikia hivyo moja kati ya vitu alivyokuwa navipenda sana katika mwili wangu ni nywele yaani alikuwa anazipenda mpaka

"Okay babe sitonyoa na pia sitolia ila haya yote umeyata wewe mi kila siku nilikuwa nakwambia babe tufuge njiwa unakaa kazi kufuga mbwa ona sasa saiz unaenda mbali ningekuwa na mtuma njiwa anakuletea salamu zangu pamoja na vizawadi vidogo vidogo Ila ubishi sasa umekukosesha Raha"

Niliamua kuongea kubadilisha mada juu kwa juu maana niliona hapa tutaanza kufanya kazi ya kufutana machozi tu japo moyoni kweli nilikuwa naumia .

Nikaamka na kuvaa gauni tukatoka nje wenzake walikuwa kwenye gari wanamsubiri

Akanikumbatia kwanguvu kama sekunde kadhaa hivi akaniachia na kuondoka

Nilibaki na mpungia mkono tu

Alipofika karibu na gari alirudi akikimbia na kufika ananikumbatia tena (nyie acheni Mungu aitwe Mungu yaani kma angeweza kutupa kukuona kesho yetu hata kidogo tu basi tungeepuka mambo mengi lakini ninae anajua siku au saa zaidi yake hakuna anaweza kukupa ishara lakin akili yakutambua ikawa haipo tuishi vizuri jamani )

Alinikumbatia kwa nguvu nikawa naisi kama sipumui vile nikamwambia babe unanikaba bhn

Akaniachia na kunishika uso kwa mikono yake akasema " nakupenda sana naomba uwe na furaha japo kwaajili yangu " kabl sijamjibu alikuwa tayar kasha kutanisha mdomo wake na wangu na kuanza kukiss

Kichwani nikajiuliza kwann huyu leo yuko hivi maana tumekuwa kwenye mahusiano na Frank miaka miwili lakin hakuna siku mbayo alinishika hata kiuno au kunikumbatia mbele ya rafiki zake

Ila leo anathubutu hadi kuninyonya mdomo mmmh sijui

Alini nga'ng'ania hadi dereva akapiga honi ya kumshtua kuwa Wana chelewa

Aliniachia akaniambia tena "nakupenda Lilian"

"Nakupenda pia Frank"

Basi akaondoka
Na mimi nikarudi ndani

Siku hiyo sikuwa na furaha kabisa

Nililala pale kesho yake asubuhi nikafanya usafi na kupanga Kila kitu vizuri then nikarudi kwa Tuli

Zilipita Kama wiki tatu siku hiyo nilikuwa chuo library nikijisomea maana tulikuwa tunatakiwa kufanya mitihani baada ya siku 5

Alikuja Samira pamoja na Linda na martha

Walifika na kuniambia tuondoke nyumbani
Nikawauliza nyumbani kufanya nn wakati tulikubaliana kuwa tutatoka saa kumi

Hawakujibu waliniinua na kunishika

Nilimuangalia Samira alikuwa mwekundu huku macho yakionesha alikuwa akilia

Nilishtuka nikahisi labda kuna kitu kibaya kimemkuta Tuli maana nilimuacha nyumbani anaumwa

"Nyie nini kimempata Tuli"

Niliuliza lakini hakuna alie nijibu walinipeleka hadi kwenye gari tukapanda mda huo bado naongea lakin hawajibu

Tulipoingia kwenye gari nikashangaa kuona wote wanalia

Niliishiwa nguvu nikajua tayar Tuli wangu hayupo tena nikaanza kulia sasa Kila nilipokuwa nikilia nawao wanaongeza gari likawa limetanda vilio tu

Tulifika nyumbani yaani alipopaki gari tu nilichomoka kama risasi nikakimbia ndani ile nafungua nashangaa kumuona Tuli amekaa huku akionesha Amelia sana

Aliponiona aliinuka nakuja kunikumbatia huku akilia kwa nguvu

Sasa nikashangaa Kuna nn maana sote nane tulikuwa pale hakuna alionesha kuzimia au kuumia kokote

Nikauliza kwani Kuna nn mbona sielewi

"Lili frank frank wako " alishindwa kumalizia akakaa chini

"F f f frank amefanya nn"

"Lili be strong ni mapenzi ya Mungu "

"Jamani mbona siwaelewi niambieni basi frank kafanya nn" niliongea kwa ukali

"Frank amefariki"

"What subiri kwanza frank yupi mnae mzungumizia "

"Frank wako amefariki vitani"

"Hahahahahaha acheni ujinga basi frank hawezi kufa kirahisi hivyo alafu frank hayuko vitani so ache hizo drama zenu"


MY BOSS MY LOVE 09

Mtunzi..... Ritha stories

Whatsapp......0763826152


Mda huo huo akaingia Isack huyu alikuwa rafiki mkubwa wa Frank nilipomuona tu nilimkimbilia na kumwambia

"Shem yuko wapi frank" niliuliza maana nilikuwa nauhakika kuwa lazima atajua alipo

Lakin hakunijibu Zaid ya kutokwa na machozi

"Isack sinakuuliza yuko wap Frank '

"Hayupo tena " alijibu kwa sauti iliyojaa uchungu wa hali wa juu

'" hayupo tena kaenda wapi"

"Lili frank amefariki vitani "

"Kwaiyo na wewe unaunga na hawa kufanya drama si ndio "

"Lilian hii nikweli sio drama frank hayuko nasi tena najua ni ngumu kuamini lakin ndio kasha tutoka "

Nilitoa sonyo Kali na kutoka nje nikaenda kwenye gari kuchukua sm yangu maana wakati nashuka niliiacha

Nilichukua na kutafuta jina soulmate hivyo ndivyo nilivyokuwa nimemsave babe wangu

Nikapiga ikanambia haipatikani nikarudia tena haikupatikana

Nikapiga namba zake zote hazi kupatikana

Nikachukua sm y Isack ambae mda huo alikuwa amesimama pembeni yangu

Nikapiga tena haikupatikana nikaona Hawa wananifanya mm mjinga nikamwambia

Samira anipe funguo za gari

"Unataka kwenda wapi "

"Naenda kumtafuta Frank"

"Shemeji tulia basi "

"Isack kaa kimya kwanza sio wewe tu wote msinisemesha Samira na omba funguo haraka"

Samira akakataa kutoa fungua aisee nilimfuata na kumnyanganya Kisha nikatoka fasta

Isack akaniwahi na kuniweka kofi moja takatifu

Kisha kaongea "nimekwambia frank amefariki elewa "

Yaani hilo neno lilipenya hadi kwenye mishipa ya moyo nikaisi kuishiwa nguvu

Nilitikisa kichwa kuashilia hapana huku machozi yakinitoka

"Naomba ulewe frank hatuko nae tena "

"Mnanichanganya frank wangu hawezi kuniacha nyie waongo"

"Najua hawezi kukuacha ila ndio Mungu kashapanga hatuwezi kupinga"

"Hapana hii haiwezi kuwa kweli frank wangu alienda kozi so hawezi kuwa amekufa"

"Alikudanganya kwasababu alijua kaikuambia ukweli hautokubari aende na hakutaka kukuacha ukiwa huna amani "

"No frank wangu hawezi kunidanganya hata siku moja". Samira alichukua sm yake na kunionesha video ambayo ilikuwa ikitoa taarifa ya vifo vya wanajeshi ambao walifariki wakipiga kuisaidia nchi jirani na mmoja wa hao alikuwa ni frank wangu

Niliishiwa nguvu nikaanguka na kupoteza fahamu

Nilikuja kuamka usiku nikawa kama chizi vile sikuamini kama nikweli lakin Kila nikikumbuka maneno aliyokuwa anatamka siku ile nilikuwa naishiwa nguvu kabisa

Mida ya saa tano nilimwambia wanipeke nyumbani kwa kina frank nithibitishe kweli kafa au naota

Wakanipeleka hadi kwao ile nafika nakuta watu wamejaa bala nikaingizwa ndani nikamuona mama yake frank akiwa amekaa anevimba uso yaani ameshalia hadi kachoka

Kulikuwa na mdogo wake Frank ambae tulikuwa timezoeana aliponiona alinikimbilia na kunikumbatia huku akilia na kumtaja frank

Hapo ndipo nikaamini kweli frank wangu hayupo tena

Nilijikuta nakaa chini kama mzigo nilishindwa hata kulia nikabaki kama nimepigwa na shoti

Kumbe mama alipewa taarifa hivyo mda huo na fika na yeye alifika na kunikuta Niko kwenye hali ile alinikumbatia huku akilia mimi mda huo sikuweza hata kufungua mdomo kuongea au kutoa sauti ya kilio

Alikuja mbaba mmoja kasema wahakishe nalia la sivyo naweza kupata shida kubwa sana

Basi kina Samira pamoja na mama wakawa wananitikisa huku wakinisihii nilie ila nilikuwa nawaangalia kama siwaoni vile

Kwa mda ule sauti niliyokuwa nasikia ni ya frank wangu yaani Yale maneno aliyokuwa anaongea wakati ananiaga ndio yalikuwa yakisikika kwenye akili yangu tena kwa sauti ya juu

Kwaiyo walipokuwa wanahangaika kunifanya nilie mm sikuwa pale yaani nikama vile nilihama kwenye huu ulimwengu nikaingia ulimwengu wa kumbukumbu

Sikumbuki hata kama ile siku nililala

Kesho yake walikuwa wanimbembele hata ninywe maji bsi maana nilikuwa sijaweka kitu chochote mdomoni lakin Bado nilikuwa vile vile kwnza hata njaa au kiu sikusikia hata kidogo

Zilipita siku 3 sijala Wala kunywa chochote yaani hata sijui nieleze vip nieleweke

Nilikuwa kama Sanamu siongei sitikishiki Wala kukohoa. (Hali niliyokuwa nayo nahisi naeijua ni Sara maana nayeye alipitia nilipopata mimi Iko siku atakuja kuwaletea kisa chake)

Basi siku ya mazishi ilifika mwili ukaletwa hapo ndipo nikazinduka maan niliamka haraka nikakimbilia jeneza ili nimuone frank wangu

Walinishika na kunirudisha ndani Kisha wakaleta mwili ndani

Nakumbuka Devi (rafiki yake) alikuja na kusema kuwa kabla jeneza halijafungulia kuna ujumbe ambao marehemu alitaka mpenzi wake ausikie kabla hata hajaoneshwa mwili wake

Watu wote waligeukiana huku ming'ono ya chichini ndio ilisikika

Devi alisogea karibu yangu Kisha akanikabidhi kitu


MY BOSS MY LOVE NO 10

Mtunzi ....... Ritha stories

Whatsapp.....0763826152

Ilikuwa ni kidude kama redio hivi akakibonyeza na kunikabidhi

Nilisikia sauti ya frank akiongea

"LILIAN natumai uko mzima japo najua moyo wako umejawa na simanzi kubwa kwakua najua wakati huu unapoisikia sauti hii uko pembeni ya jeneza langu najisikia mwenye hatia sana kwakuwa nimeshindwa kutimiza ahadi yangu kwako

Nilikuahidi kuwa nitakuwa na wewe hadi uzee napia nilikuahidi kukupa furaha siku zote Ila naumia kwasababu nimeshindwa kutimiza hata kimoja nisamehe kukufanya ukaumia nisamehe kuruhusu macho yako yakatokwa na machozi Ila naomba utambue kuwa nakupenda hadi kufa

Namshukuru Mungu kwakunipa nafasi ya kukufahamu na kuwa SEHEMU ya maisha yangu
Ulikuja kwenye maisha yangu nakunifanya kuwa mwanaume mwenye furaha na wakujiamini ulinifanya nikajua nini maana ya mapenzi naweza kusema kuwa ulikuwa zawadi yenye thamani kubwa sana katika maisha kila siku nilikuwa natamani kukuona ukiwa Kando yangu ..

Najisikia maumivu sana natamani kuliona tabasamu lako hata kwa sekunde lakin sina nafasi hiyo tena

LILIAN nilitamani sana kuona tukiishi pamoja hadi uzeeni lakin inaokana haikupangwa kuwa hivyo so naomba Mungu akupe mtu ambae atakupenda na kukupa furaha Zaid yangu

Nakama maisha yajayo MUNGU ataruhusu kuoa na kuolewa basi naomba anipe wewe uwe wakwanza na wa mwisho na kupenda sana Lilian wangu

Kuna zawadi nilikuwa nimeiandaa kwaajili ya kukupa siku ya harusi yetu kwakuwa siwez kufika unaweza kuchukua sasa
Japo Haina umuhimu tena

Lili I love you nakupenda sana naomba usilie sana
Kwani utazidi kuniumiza please be happy just for me
Utafanya hivyo si ndio ee

Naomba nikuombe kitu kingine najua itakuwa ngumu lakin kwaajili yangu naomba ujitahidi kwani hii ndio last wish yangu

Natamani kabla sijafukiwa uniimbie so that niweze kusikia sauti yako for the last time

Nakupenda sana kumbukumbu nilikupenda sana na uwe na furaha byee"

Ile sauti iliishia hapo Mda huo nilikuwa nimekaa chini huku uso umeloa kawa machozi

Nilihisi maumivu ambayo sijawahi kuisikia maisha yangu yote

Baada ya kumaliza kusikia ile voice Aliniambia nifungue kile kibox alichonipa nikafungua kulikuwa na mkufu wa gharama sana ulikuwa umechorwa love alafu kaikati kukawa Kuna helufi ya F& L

Nililia sana jeneza lilifunguliwa nikamuona frank wangu alikuwa kama amelala usingizi

Ilikuwa ngumu kuamini kama ndio kaondoka hivyo

Nilitamani hata kuongea lakina sikuweza nililia mno

Baada ya kumuaga alipelekwa nje akaagwa na Kisha akapelekwa kupumzishwa kwenye ngumba yake ya milele

Kukua alikuwa ameomba kusikia nikiimba ilinilazimu kufanya vile

Nakumbuka niliimbaga mziki mmoja hivi wa west life unaitwa I lay my love on you

Hii ilikuwa ni nyimbo pendwa enzi za uhai wake yaani ilikuwa haipiti siku bila kusikiliza hii nyimbo

Ilikuwa ni ngumu kwangu kutokana na maumivu niliyokuwa nayo kwa wakati ule ila Mungu alinipa nguvu nikaimba hadi mwisho na kurudia hadi jeneza likashuswa na kufukiwa

Sasa ile wanamaliza kufukia tu nilidondoka pale pale na kupeteza fahamu. Nilikuja kushtuka baada ya siku mbili nikiwa hospital huku nimewekewa mpira wa kunisaidia kupumua

Nilifungua macho chakwanza kabisa nilisikia sauti ikiniambia nakupenda sana Lilian

Nikaanza tena kulia kwa sauti mama alishtuka na kuja haraka akaanza kunibembeleza mda huo huo wakaingia kina Samira walifurahi sana kuona nimeamka

Walimuita doctor akaja na kuniangalia kisha akasema nimetoka kwenye hatari ila wanatakiwa kuniangalia kwa ukaribu sana pia akashauri nirafutiwe mwanasaikolojia ili awe ananifanyia saikolojia

Maana kutokana na kilichotokea unaweza kuchukua mda sana kurudi katika hali yangu ya kawaida

Nakumbuka siku hiyo naamka kesho yake ndio ilikuwa tunafanya mitihani ya kumaliza
Sasa kwa ile hali ilikuwa ngumu kwani nilikuwa ni mtu wakulia tu

Mama nakumbuka mama alisema kuwa siwez kuingia
Kwenye chumba cha mtihani
Nikiwa vile so nitarudia tu Haina shida

Ila Tuli alisimama na kumwambia mama kuwa nitafanya mtihani nikiwa hivyo hivyo na sitafeli

Walibishana sana na mama
Mama alisema kuwa yeye ni mzazi wangu anajua vizuri hali niliyonayo kwaiyo hawezi kuruhusu

Nakumbuka usiku mama akiwa ametoka Tuli aliingia chumbani kwangu akanipiga injili takatifu mwishoni akaniambia unakumbuka frank alikuwa abatamni sana kukuona unamaliza sasa leo akikuona umeshindwa tena kwaajili yake unafikili atapumzika kwa amani

Mda wote anaongea mm machozi ndio yanaongea

Si akaanza kuomba bhn

Nyie nivile sikuwa sawa maana ningecheka mpaka maana sikuwahi ht siku kumuona Tuli akiingia kanisani au kusoma biblia ila ile siku hadi alinena kwa ragha. Aliomba kma masaa kadhaa yaani bila hata kukoma

Kesho yake asubuhi walikuja kunichukua na kunipeleka chuo,huku nyumbani mama alibaki akiomba ,tulifika chuo mda huo Niko kimya siongei Wala nn nimachozi tu ndio yanashuka

Tuli aliniangalia akanishika mkono na kusema

"Najua uko kwenye hali ambayo sio nzuri lakin kwauwezo wa Mungu utafanya mtihani na hautafeli kwajina la Yesu

Nilimuangalia tu yaani mda huo sikuwa nasikia kile watu wanaongea zaidi ya sauti ya frank ndio ilikuwa imetawala ufahamu wangu wote

Tuliingia kwenye chumba cha mtihani na kufanya mitihani lakin Cha kushangaza watu walikuwa wananiangalia kama vile niko sawa maan ninavyojua kutokana na hali niliyokuwa nayo nisiruhusiwa kuingia kwenye chumba cha mtihani
Lakini niliingia na watu walikuwa wananiona kama Niko normal tu

Ilikuwa tulimaliza tu mtihani ule mda wa kupumzika wenzangu walinichukua na kunilinywesha uji huku Tuli akiwa ni mtu wakuomba Kila mda (sijui ni roho gani alimuingia kwa wakati ule )

Basi tulifanya mitihani yote na kumaliza ila ungeniuliza nimejibu nini ningekwambia

Sijui maana mwili ulikuwa pale ila akili havikuwepo pale kabisa

chakushangaza matokeo yalitoka nilikuwa mtu wa wakwanza sikuamini kabisa sio mimi tu hata wenzangu hawakuamini

Ila Tuli alicheka na kusema "huyo ndio Mungu anaeweza kufanya kile mwanadamu asichoweza"
 
MY BOSS MY LOVE NO 11


Mtunzi...... Ritha stories

Whatsapp.........0763826152



Siku zilienda huku nikiwa bado mtu wa kulia tu yaani hakuna kitu ambacho niliweza kufanya Zaid ya kujikunyata huku nikikumbatia picha za frank na kulia.
Nilikonda kutoka 75kg hadi 44kg yaani ulikuwa ukiniangalia unaweza kusema nakufa sekunde yoyote

Marafiki zangu wote walipata kazi wakawa bz na maisha yao

Isipokuwa Tuli yeye alikuwa karibu na mimi kama pua na mdomo

Nakumbuka kaka yake alimtafuta na kumwambia kuwa kuna kazi imepatikana Canada na toka tukia secondary alikuwa anasema ndoto yake kubwa anatamani siku moja akaishi Canada

Lakin baada ya kaka yake kumtafuta nakumwambia kuwa amepata kazi tena iliyokuwa na msharaha mnono

Alikataa nakusema hawezi kuondoka nchini na kuniacha nikiwa katika hali ile

Mama alikaa nae chini na kumsihi aende tu kuhusu mimi nitakuwa sawa ila aliendelea kukataa

Siku zilienda huku Kila siku walikuwa wanaKuja wachungaji kunifanyia maombi

Mungu ni mwema nilianza kurudi kwenye hali yangu ya kawaida japo ilichukua mda sana

Ulipita mwaka Tuli akarudi kwao na mm nikaanza kutafuta kazi na hapo ndio kikawa kipilenge
Nilizunguka kwenye office za watu lakin sikupata

Ikafika mda nikatamani hata kupata mwenza wa maisha na mimi niwe na familia yangu lakin hakuna hata mwanaume mmoja aliejitokeza kuonesha Nia

Hadi sasa ni miaka 6 toka frank aondoke

Nilikuwa naendelea vizuri tu lakin nimerudiswa tena kwenye maumivu yaliyokuwa yanaishia

KWANN INAKUWA HIVI LAKINI WHY

baada ya kunirudisha nyumbani niliingia ndani nikafunga mlango na kujilaza

Nikiwa kwenye dimbwi la mawazo sm yangu iliita nikaangalia alikuwa ni Tuli nilipokea na kuanza kulia alishituka na kuuliza Kuna nn mbona nalia

"Tuli frank wangu frank"alishtuka sana baada yakisikia namtaja frank

"Lili umekutwa na nn "
Nilimueleza Kila kitu hakujibu alikata sm

Nikabaki nikilia tu

Mda ulienda ilipofika saa mbili usiku alinipigia na kuniuliza Niko dodoma sehemu gani
Nikamwambia akakata sm

Baada ya dakika 20 nikasikia mlango ukigongwa sikutaka kuamka kwenda kufungua maana nilihisi atakuwa Bosco

"Lilian fungua mlango "ilikuwa ni sauti ya Tuli haraka niliamka na kwenda kufungua mlango

Nilifungua n kumkuta nilikumkumbatia huku nikilia kwa sauti

Bosco alikuja akikimbia naisi alisikia nikilia

Tuli alishtuka sana akikosa lakuongea akabaki akumtolea macho Bosco alinigeukia na kuniuliza

"Wewe naona au naota"kabla sijamjibu Bosco aliongea

"Kuna nn kimetokea mko sawa"

"Jesus Christ hiki ni nini " aliongea Tuli kwa mshangao sikumjibu

"Tuko salama Bosco"nilimjibu kinyonge Kisha nikamshika Tuli tukaingia ndani alikaa kama mzigo
"Lilian mbona huyu kaka amefanana na Frank Kila kitu "
"Sijui nashindwa kuelewa Mungu anampango gani na maisha yangu maana kama kulia nimelia sana umefika mda ambao na mimi nilikuwa nimepata furaha ila anakuja kunirudisha tena kwenye maumivu"
Niliongea huku mchozi yakitoka Tuli alikuja kunimbatia na kunisihi nisilie

"Wait hapa ndio unalala au"aliongea kunitoa kwenye ile mood

"Yeah "
"Uko serious kweli hivi unawezaje kulala sehemu kama hii"

"Nikwa mda tu kwaiyo Haina shida "

"Kwa mda yaan Niko huko najua rafiki yang analala vizuri kumbe unajiegesha tu,kwanza umeshakula"

Nilitikisa kichwa kuashilia hapana
Alinikata jicho hilo Kisha akaamka na kuangalia kama Kuna kitu Cha kupika akaona hakuna alitoka na kuingia kwenye gari akatoa biscuits na soda akanipa nianzie hizo Kisha akatoka hakuniaga

Nilisikia gari likiwashwa tu

Alikaa mda mrefu karibu masaa mawili ndio akarudi

Nilishangaa kuona anarudi akiwa na godoro friji ndogo mtungi mdogo wa gesi na vyombo baadhi

Kisha akaniletea na chakula

"Toka kakae nje na sitaki maswali "Aliniambia huku akinitoa nje na kunipa chakula yeye akawa anasaidizana kupanga vitu na wale vijana alio kuja nao

Nilikaa tu kumsubiri amalize ili tule wote maan hata sikuwa na hamu ya kula

Walipanga Kisha akaja na kukuta sijala
Alinigombeza kama mtoto vile Kisha akachukua kile chakula na kunilisha

Nyie huyu Dada Mungu muwekee amekuwa zaidi ya rafiki kwangu
Sijui hata nimuiteje maana upendo alionao kwangu ni zaidi ya upendo wenyewe

Nilimkumbatia huku nikilia n akumwambia "nakupenda sana Batuli wangu Mungu akubariki"

"Bwanaee niachie nishalia vyakutosha sitaki kulia tena"aliongea na kunitoa
Kisha akaendelea kunilisha hadi chakula kikaisha

Baada ya kupanga vitu tuliingia ndani tukalala kesho yake tulishinda ndani maana alikaja na vitu vyakupika

"Lili".
"Abee"
"Inabidi uhame hapa ukakae sehemu nyingine"
"Kuhama kwnn"
"Kwasababu ya Bosco Sina amani ya wewe kuendelea kukaa hapa"

"Na Kodi niliyotoa ".
" Amani ni bora kama ni Pesa zinatafutwa my dear so nitakopa au hata kuweka gari Bondi ili tu utoke hapa siwez kukaa kwa amani ukiwa hapa"

"Tuli nitakimbia hadi lini na nitaishi katika maumivu hadi lini mi naona Sina haja ya kuhama Bali natakiwa kukubaliana na hali kuwa Frank hayupo tena na hatakuwepo hivyo maisha yanatakiwa kuendelea so sitohama nitakaa hivyo hivyo huenda Mungu nakusudi lake japo sijui ni lipi ila naimani nitakuwa sawa"

"Lakini Lilian "
"No Batuli nitakaa haijalishi nini "
"Okay kwakuwa umeamua hivyo sawa"

Tulikaa hadi mida ya saa mbili Tuli akawa ameondok a kurudi dar

Huyu Binti anau jasiri wakipeke yake haogopi kuendesha usiku ila mimi sasa thubutu

Basi nilibaki menyewe nikalala zangu kesho yake asubuhi nikaamka na kujiandaa

Sm yngu iliita nilichukua nashangaa mama ananipigia video call

Huyu mwanamke amepata wapi smart phone
Mbon nitakoma

"Nilijua tu utakuwa hujafumua hizo nywele yaani sijui ukoje" ilikuwa ni kauli ya kwanza kuongea baada y kupokea

Ohoo nimeisha aliemshauri mama kununua smart phone kaniweza tena sio kidogo.
 
My boss my love no 12

Mtunzi...... Ritha stories

Whatsapp......0763826152


"Nilikuwa bz sana ndio maana sijapata mda wa kufumua" niliongea kwa kujitetea

"Unataka kujitetea kama vile sikujui,hembu fumua hizo nywele haraka"

" Hapana Mama saizi mda umeenda hapa penyewe nimechelewa kazini "

"Kwaiyo unataka kwenda na hizo nywele "

"Na Vaa wigi"

"Hayo mawigi yako ambayo ukivaa unakuwa Kama msukule"

" Heee mama punguza ukali wa maneno"

"Ukali wa maneno kwani yamekukata wapi "

"Embu tuachane na habari ya nywele zangu umenunua sm au umeanzima" niliuliza makusudi ili nimkere

"Niazime kwamba mimi Sina Hela au Sina mume"

"Bado hujajibu swali"

"Hembu peleka pua yako kazini usije kuchelewa".

"Sawa mama ubaki salama'"

Niliongea na kukata kama nimepiga mm vile

Baada ya kukata sm nilijiandaa vizuri na kutoka

Sasa ile natoka nakuta na Bosco nae akiwa anaingia kwenye gari lake

Alivyoniona akatoka na kusimama akinisubiri

"Habari y asubuhi Lilian"
Alinisalimia huku akitabasamu

"Nzuri wewe je "

"Mimi niko poa "

"Haya siku njema " nilijibu n kuanza kuondoka kiukweli sikutaka mazoea nae hata kidogo


"Wait " anataka nini tena aaaa Nilisimama na kumsikiliza..

"Naweza kukupa lifti"
.
"No asante sana ninakoenda ni karibu sana so unaweza kwenda tu"

"Haina shida Kwan hata mm ninaenda karibu "

"Hapana siku nyingine ila kwaleo asante sana "

Baada ya kuona nimekataa aliingia kwenye gari na kuondoka

Na mimi mdogo mdogo nikaanza kutembea

Kutoka pale nyumbani na kazini nilikuwa natumia kama nusu saa kutembea.

Ukweli nilipaona ni karibu hivyo sikuon sababu ya kupanda gari

Nilifika kazini nika sain nakwenda kupanda lift heee nilihshangaa kumuoana Bosco akiwa anakuja huku yuko bz anaongea na sm

Aliponiona akatoa sm sikuoni na kukataa

Kisha akanifuata

"Kumbe unafanya kazi hapa"aliuliza kwa mshangao maana aliona nimevaa kitambulisho Cha mfanyakazi

Mungu wangu huyu anafanya kazi hapa sasa nitamuepukaje

Niliwaza baada ya kuona n yeye amevaa kitambulisho kuonesha kuwa ni mfanyakazi wa pale

Tena alikuwa kwenye kitengo nilichopo mimi

Nilitabasamu kinafiki maana moyoni sikupendezwa kabisa

Tuliingia kwenye lift Kisha tukashuka na Kila Mtu akaingia ofisini kwake

Mda wa kula ulifika akaja kunigongea kuwa twende tikapate chai

"Hello hbar ya mda"

"Nzuri kribu sana Bosco"

"Asante mda wa chai huu vp unampango gani" aaa kabla sijamjibu alikuja boss (Chief Director)

"Niko tayari boss vp tunaweza kwenda"
Niliongea kumwambia Mr Sam ambae alibaki akiwa amshangaa maana hatukuwa tumeonana Wala kupanga kukutana

Ila sijui alihisi nn akakubari safta

" Ooo umemaliza nilikuwa nimekuja kukushtua nikidhani Bado"

"Habari yako mr Bosco "aliongea na kumsalimia Bosco
"Ninzur boss vp wewe"

"Aaa Niko poa samahani nakunyanganya huyu mrembo kwa mda " aliongea na mm nikainuka Bosco nae akaona isiwe kesi akaondoka

Tulitoka na boss hadi sehemu ya chakula nikaa

"Kwann umefanya vile"aliuliza Mr Sam baada ya kukaa

Sasa hapa nimjibu nini

"Alikuwa anaomba kupata chai na mimi " niliamua kumdanganya hivyo

"Naukawa hutaki "aliongea akamaliza kwa kucheka

"Yeah"

", Okay,kwann lakin coz Bosco ni moja kati ya vijana watanashati Sana na anapendwa na mabinti wengi" huu Sasa ni umbea unataka kujua ili iweje niliwaza
Kisha nikamjibu

"Yeah najua kama ni mtanashati ila mimi napenda mtanasweta"

Nilivyoongea hivyo alicheka sana

Basi breakfast ikaletwa tukaanza kupata msosi

Tukiwa bado tunakunywa chai nilimuona Bosco akiwa anatuangalia
 
MY BOSS MY LOVE NO 13
Mtunzi.... Ritha stories

Whatsapp.....0763826152


Tulimaliza kupata kifungua kinywa Kisha tukarudi ofisini

"Thanks for your time miss Lilian" aliongea huku akinipa mkono sikuwa na hiana nikampa tuka

"Karibu" nilijibu na kuondoka akabaki akiwa ananiangalia

Niliingia ofisini kwangu heee nashangaa kumkuta Bosco akiwa amekaa

"Bo bo Bosco umeingia humu sangp" nilimuuliza maana nakumbuka nimemuacha nje

"Nimeingia mda si mrefu huku niona kwasababu ulikuwa bz kuongea na Mr Sam, anyways nimekuletea hii kazi inatakiwa kuwa tayari before lunch time '"

Aliweka mezani na kutoka
Nilibaki na mshangaa maana naona kama amekasirika vile

Bwanaee hanihusu nilivuta kiti na kukaa nikaanza kazi

Nikiwa bz na kazi alikuja mkaka mmoja hivi kaleta file

"Ingia"

"Habari yako msichana mrembo" nilimuangalia kwanza kabla ya kumjibu Kisha nikaongea

"Jina langu ni Lilian Adrian sio msichana mrembo , karibu nikusaidie nn" niliongea hivyo baada ya kumuangalia nikaona huyu sio wa kuwa na mazoea nae maana sura yake imekaa kimbea mbea

"Yeah najua kuwa unaitwa Lilian ila nimeona nikupe Sifa yako maana naona mtoto wakike unanyota sijui unaongea maziwa maana sio kwa kuwateka wanaume hivyo yaani hata wiki mbili hazijaisha ushaanza kuvuruga vichwa vya vigogo ,ila taratibu madam wasije kuuana"

Hahahaha nilicheka kwanza nyie hivi Kuna wanaume wenye vitabia vichafu namna hii

Nilisoma Jina lake kwnye ID yake Kisha nikamuita

"Ooo sawa bwana Paulo nitakugawia maziwa ili tuwachanganye wote" shenzi type niliongea huku nikiweka tabasamu la kinafiki

"Aaa sijakwambia ili kukukera no ila nimekwambia tu alafu Rachel anampenda Bosco kufa sasa angalia dada wawatu asije kufa"

"Hivi hiki ndicho kilichokuleta au unawashwa " ilinibidi niongee hivyo maana niliona ananipotezea mda wangu bure

"Yamenileta yote mawili moja ndio hilo nililo ongea la pili ni hili unatakiwa kuipitia hii kazi alafu uipeleke kwa Mr Sam "

"Okay unaweza kuondoka '"

"Okay bye cute angel " huyu kaka ni mzima kweli au ni mtoto sio ridhiki

Niliendelea na kazi zangu mara paulo akarudi

"Unaingia bila kubisha hodi kama vile unaingia kanisani"

"Samahani vp kwani Kuna mtu nirudi"

"Hapana Kuna maka '"nilitaka kuongea neno nikasita na kumuangalia kwa

"Nyie Mungu anajua kuumba yaani demu wangu angekuwa mzuri kama wewe wallah ningembeba Kila mtu aone, eee mtoto hata ukinuna unapendeza"

"Wewe huo uchizi wako naomba upeleke huko hapa na fanya kazi sitaki usumbufu"

"Jamani hiyo saitu ndio ya kukasirika sijui sauti y kule itakuwaje duh kweli wakubwa wafaidi"

"Paulo toka ofisini kwangu now"

"Come down mrembo nimetumwa na Mr Sam nikuletee maji anataka unywe ili uwe na rangi ya kung'aa au hujawahi kusikia kuwa mtu akinywa maji mengi anakuwa mweupe alafu ngozi inakuwa nyororo akikugusa tu chuma inasimama Dede"

Yaani nikikasirika nilitamani kuponda na kitu kizito ila nikaona ngoja nitulie nisije kumwaga ugali na mboga kwa wakati mmoja

"Byee Lili "aliongea na kuweka maji kwenye meza na kuondoka

Nilibaki na msindikiza na macho tu

Mda huo huo akaingia Rachel

"Kasha kutibua nn maana Paul anakera"

"Kwani huyo kaka ni mzima au dishi limeyumba" niliuliza baada ya Rachel kukaa

"Bora dishi lingeyumba mimi nahisi hana marinda yule maana mwanaume timamu hawezi Ku behave hivyo"

"Mxuuuu anaboa sana"

"Mmh ila Mungu fundi bwana dada umeumbika kweli kweli yaani kwanzia kwenye unywele hadi vidole vya miguu uko alafu unakisaudi flani hivi amazing ndio maana unawachanganya vidume naona hadi Mr Sam kanasa "

Kumbe ndio wale wale chupa na mfuniko aka bwagu na bwaguzi

"Ongea kilichokuleta" niliongea huku nikiweka uso wa serious maana naona wanataka kunipanda kichwani

"Mimi Sina mpya nilitaka tu kukusalimia maana mda wa chai nilikuja nikakuta umeshatoka na Mr Sam"

"Ooh haya unaweza kwenda"

"Alafu nilikuwa naomba nikuulize,hivi unatumia mafuta gani maana unagozi ya kuteleza hadi Raha ,pia ni product gani unatumia kwenye nywele zako "

" kwenye ngozi natumia femo Yale ya kulainishia vyuma na kwenye nywele natumia mavuta ya mende pamoja na utomvu wa ndizi vp nataka kuninunulia au "

"Khaaa we dada kuwa serious basi "

"Ili iweje,alafu Rahel unaweza kwenda nina kazi kibao "

"Heee dda siitwi Rahel tafadhali usiniharibie jina"

"Hivi unajua wanaoitwa Rachel ni watu wa aina gani ,kiufi wewe unatakiwa kuita Rahel na huyo mwenzio anatakiwa kuigwa Paulo "

alitaka kuongea nikamkata hilo jicho akatoka akiwa kafura kama nyoka anaetaka kutema mate

Nilifanya kazi zile zilizotakiwa haraka Kisha nikapeleka kwa Mr Sam

Niligonga akani ruhusu kuingia

"Ooo miss Lilian karibu sana"aliongea na kutoka kwenye kiti chake haraka akaja kunivutia kiti nikae

"Aaam usijisumbue Nita kaa mwenyewe"

"No no sijisumbui bali na fanya wajibu wangu" mhwajibu wako my foot niliwaza huku nilikaa

"Nimeleta hizi kazi zinatakiwa saini yako"

"OOO sawa ,so mda wa lunch unafika tutaenda kula pale pa asubuhi au twende kwingine"

Jeeesu huyu baba vp tena

"No asante sitoshuka chini nitagiza tu kwaiyo unaweza kwenda tu"

"Kwann unajua sio salama kukaa mda mrefu hivyo unatakiwa kunyoosha mgongo"

Kumekucha mbona office inaanza kuwa ya moto

"No Haina shida ofisini kwangu Kuna nafasi ya kutosha nitatembea humo humo"

"Lilian Kuna kitu chochote nilichokukwaza"..

"Ndio aaa sorry hapana ni ni nivile sijisikii kutoka nje"

"Ooo basi nitakuja kukupa company ofisini wako"..

Tena
 
MY BOSS MY LOVE NO 14

Nilitoka ofisini kwa Mr Sam huku nikiwaza kumkwepa

Yani nikishajuta kwann nilienda kupata nae kifungua kinywa bora ningekausha tu

Wakati nikwa na tembea huku mawazo yako mengi kichwani nilijikuta nampamia Bosco sasa kutoka na viatu nilivyovaa nikatekeza na kutaka kudondoka

Aliniwahi na kunishika mkono kiunoni na mwingine mgongoni huku mimi nikiwa nimeweka mikono yote kifuani mwake tukawa zero distance macho yangu yaligongana na yake tukawa tunaangalia nilijikuta picha ya frank akinikiss ikija kichwani mwangu nikapata msisimko wa ajabu sijui kwasababu walifanana au nini

"Are you okay"aliongea lakini sikumjibu nikabaki namuangalia tu

Kumbe wakat tukiwa bado tumeshikana paulo alipita akatuona alivyo mbea akasimama kabisa kuona nini kitatokea demu wa Paulo njoo umchukue bwana wako huku anakutia aibu

"Someone is watching"Aliniambia kwa sauti ya chini kusikia hivyo nilikurupuka na kugeuka ili niondoke akanishika mkono

Huyu nae vp niliwaza na kugeuka

"Naomba kupata lunch na wewe" toba hii office nilikaa mwaka sijui

"No asante nimeshaagiza wataniletea ofisini kwangu"

"Okay fine na mm naagiza basi" aliongea na kuondoka akampita Paulo ambae Bado alikuwa amesimama ila huyu kaka khaaa amenishinda tabia

Sasa bwana watajiju wenyewe

Niliingia ofisini nikachukua sm yngu na kumtafuta Tuli wangu
Nikampa umbea pale tukacheka wee akaomba wakija nitegeshe sm mahari awe anaona live show

Mimi na yeye tena hatuna baya nikamwambia mama hilo ni dogo subiri waje

Baada ya kuchat nae nikaagiza chakula changu pale

Haikuchukua mda nikaona kinaletwa haijapita sekunde Bosco akaja nacha kwake mara Mr Sam nae huyo wahala pro max wakinyongana mimi simo

Basi nilikuwa nimeshategesha kasimu kangu shoga yangu anaangalia show ya buree

Mr Sam alivyoingia na kumuona Bosco alishtuka ila akavunga akavuta kiti na kukaa

Wakawa wanaangaliana kijicho hicho ikabidi niwakaribishe

Wageni wangu au mnasemaje ni wafukuze au

"Karibuni"

"Asante"waliitikiwa kwa pamoja kisha wakaangalia kama vile Kila mmoja na sema we vp

Nikafungua chakula changu na kuanza kula mdogo mdogo huku nikitupia jicho kwa huyu na kwa yule mda huo wako kimya vijiko ndio vinasikika kugongana tu

Tukiwa katika ya msosi nikasikia Bosco anaongea

"Mr Sam vp mkeo na watoto wanaendeleaje alafu yule mwanao watano atakuwa mkubwa sasaiv ee" masikini Mr Sam alipaliwa chakula akakohoa nusu ya kufa

Bosco alivyo na karoho ka pilato alimuweka ngumu ya mgongo hadi nikaisi kavunja mifupa naona alikuwa analipiza kwann umekula kula huku.

Baba wawatu alivyomaliza kukohoa akanywa maji Kisha akaongea

"Yuko poa vp wakwako anaendeleaje na yule mkeo mkurya bado yupo au umebadilisha maana uko vizuri sana"

Watu wanatoboa mabati nikaona kama Bosco kapozi kwanza Kisha akaongea

"Aaa tumesha achana kitambo sasaiv tunalea tu"

"Kumbe na yeye ulizaa nae"

Ohoooo

Kabla hajamjibu sm yake iliita akasema

"Excuse me "akainuka na kuondoka akabaki Mr Sam

"Aaaa usichukulie kweli huyo ni mtani wangu siunajua wachaga na wapare tulivyo" mimi tena haya basi akamaliza kula akaniaga pale na kurudi ofisini kwake

Nikainuka na kuchukua sm yangu mahari nilipoiweka

"Wewe mtoto nyoko kbisa unataka kuniua kwa kicheko saizi"

Tuli aliongea baada ya kushika sm

"Kazi ninayo "

"Tena sio ndogo shoga yangu, ila kuwa makini sawaee"

"Sawa dear ngoja nifanye kazi ili niwahi kuodoka"

"Poa" tuliagana nikakata sm

Kabla sijaweka sm pembeni uliingia ujumbe

"Thanks for your time nine enjoy sana by Bosco"

Sijakaa sawa ukaingia mwingine " asante kwa mda wako nimefurahi sana na nime enjoy chakula kwasababu ya tabasamu lako thanks again natamani iwe hivi Kila siku by Mr Sam "

Duh haya bhn nikajibu

"Glory to God "Kisha nikatuma kwa wote

Jioni mda wa kutoka niliwahi kwakuwa sikutaka kupanda gari la Bosco

Nilifika nyumbani nikaoga na kupika chakula Cha usiku kisha nikaanza kufumua nywele

Nikiwa bz nikasikia mlango ukigongwa nikainuka na kwenda kufungua

Sikuona mtu zaidi ya maua yaliyowekwa chini

Nikainama na kuchukua.

Nikatoa kikaratasi kilichokupo nikafungua na kusoma

"Leo ilikuwa ni siku njema kwangu kwakuwa nimeshinda nikiiona sura yako yenye kupendeza na kuvutia
Asante kwa kuwa my day make i wish kila siku iwe hivyo nakutakia usiku mwema na njozi njema My cute angel bye Bosco "

Aaaa for real Hawa viumbe Wana niona karanga au kishet

Nikafungua mlango na kumfuata kwake

Niligonga baada ya sekunde chache mlango ukafunguliwa

Nilitoa macho huku nilishangaa kile ninachokiona


itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 1, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE NO 15

Nilitoa macho baada ya Bosco kufungua mlango

Alikuwa kifua wazi nilishangaa zaidi nilipoona alama kifuani nakumbuka vizuri na Frank alikuwa nayo

Hivi huyu sio frank wangu jamani mbona anafanana kama yeye

Niliwaza nikiwa bado nimesimama

"LILIAN"aliniita ila sikuitika kwani mawazo yngu yalikuwa mbali sana

Nilishtuka baada ya kunishika mkono wangu huku uso wake ukionesha tabasamu ambalo halikuwa la kawaida

"Karibu ndani"aliongea kwa sauti flan hivi ,
mmmh kengere ya hatari ikagonga kichwani haraka nilitoa mkono wangu aliokuwa ameushika

"Aaaa sorry nimekuja kukuambia asante kwa zawadi" sijui ilikuwaje nikaongea kitu ambacho sikuwa nimepaga kuongea

Lengo la kumfuata kwake ilikuwa ni kumwambia aache kuniletea zawadi zake lakin nimeishia kumshukuru

Shenzi sana mimi

"Karibu kama umeipenda nitakuwa na fanya hivyo Kila siku"

Nilikosa la kujibu nikabaki nacheka cheka tu

Nilirudi chumbani nikakaa picha ya Bosco akiwa kifua wazi ilikuwa inajirudia rudia kichwani

Nilijikuta namkumbuka frank wangu

Nilikumbuka siku ya kwanza kumuona akiwa kifua wazi nilifumba macho kwa aibu

Alikuja akashika mikono yangu na kunitoa taratibu

Nilifungu macho akanipa hot kiss ya hatari ile inayoitwa denda yes hiyo hiyo

Nilipata hisia kali nikajikuta namshika shingo akanunyenyua na kunilaza kitandani na kwa mara yakwanza nikaingia rasmi kwenye ulimwengu wa mapenzi .

Nilivyokumbuka hivyo nilijikuta natokwa na machozi frank wangu kwann uliniacha lakin

Nililia hadi usingizi ukanipitia

Nilikuja kuamka saa tisa njaa ilikuwa inauma vibaya mno

Nilipasha chakula nikala na kurudi kulala

Kesho asubuhi niliamka mapema nikajiandaa na kutoka

Kumbe Bosco alikuwa amenisubiri

"Habari ya asubuhi" nilimsalia baada ya kumfikia

"Nzuri usiku wako ulikuwaje"

"Ulikuwa poa tu"

"Okay tunaweza kwenda"
Aliongea huku akiwa amefungua mlango wa gari ili niingie

Sikuwa na namna nikaingia tukaanza safari sasa kitu nilicho kipenda kwenye gari lake kulikuwa na mziki menene na unajua ninavyopenda mziki

Nilihisi Raha asubuhi yangu ikawa fresh tulifika akasema ngoja nikufungulie mlango nikakataa

Hakuwa mbishi alinisikiliza nikashuka zangu mwenyewe

Sasa kuangalia juu Mr Sam yuko anatuangalia

Mhh hapa mbona naisi kama kitatokea shida

Bosco nae akashuka huku akitabasamu hatari

Tulitembea na Kila mtu akaelekea ofisini kwake sasa nafika ofisini kwangu nakuta Mr Sam amesimama mlangoni huku kashika kikombe

"Good morning miss Lilian"

"Good morning Boss"

"Oh please just call me Mr Sam inatosha"

"Sawa "nilijibu huku nikitaka kuingia ndani

"Am nimekuletea kahawa" ,

"No asante situmii kahawa"

"OOO sorry basi baadae "

"Okay thanks " aliondoka na mimi nikaingia ofisini na kuanza kazi

Mida ya saa tatu hivi akaja Rahel huyu toka ameanza umbea wake simuiti tena Rachel

"Habari yako shemeji wa kampuni"

"Kumekucha unataka nin"

" A a a jamani kwani nikija kukusalimia ni vibaya"

"Hapana ila sitayari umenisalimia basi unaweza kwenda "

"Mmh yaani watu ambao mlibarikiwa uzuri huwa mnajikuta kina nani vile,iko hivi nimekuja unipe umbea nasikia jana ulikuwa uneshikiliwa na Bosco "

"Hpana nilikuwa nimeshikiliwa na makalio yako,hembu naomba uondoke ofisini kwangu Sina mda na huo ujinga wako"

"Sawa bhn watu na nyota zenu mjini"aliongea na kuondoka

Hivi hii kampuni inawatu wa aina gani watu wamekaa kinasiala siala tu

Hazijapita dakika kumi akaja Paulo Yani nilivyomuona tu nilihisi hasira

"Kama huna Cha maana uishie hapo hapo"

"Aaaaa shem wa taifa hutakiwi kununa asubuhi yote hii, umeamkaje "

"Nimeamka upande ,mh nakusikiliza"

"Ok Mr Sam kaniambia nikuletee mziwa na hii chocolate,ila Lili we kiboko unajua Mr Sam hajawahi hta siku moja kuwa karibu na na binti yoyote huku ofisini Zaid ya kazi lakin naona kwako amekuf akaoza ,alafu Jana mlitisha Yani vile alivyokuwa amekushikili kiuno alafu ukawa unamuangalia kwa jicho flani hivi lililo jaa nyege nikajikuta na dindisha , kwakwel nimeipenda couple yenu mna mahaba ya kihindi alafu mkachanganya na yakiingereza mkatia na ya kibongo wallah mtaenda kuwa Best couple in town "

"Umemaliza"

"Bado nameza mate kwanza , sasa ndugu yangu Mr Sam nae unamuweka wapi maana na ye"

"Wewe toka ofisini kwangu now ,nausirudi kuongea utumbo wako"

"Hii ndio shida ya wabongo yaani unamsifia alafu anajiona kama nini sijui"

"Toka bwana kama unaona Dili nenda akakushikilie wewe mchanganye na yakikongo mfyuuu mwanaume unakuwa Kama mwanamke yaani alokuita Paulo alikosea alitakiwa kukuita mwajuma shenzi type "

"Haya bhn maziwa yako haya sijui unakunywa au unachambia maana so kwaku tuvuruga huku "

"Paulo sitaki ugomvi na wewe embu ondoka bhn aaa "

" " Aliondoka na kuniacha nikiwa na hasira niliangalia yale maziwa nikayaweka pembeni

Hivi kwani Hawa wananitakia nn mimi mfyuuu

Nilifanya kazi mda wa bleakest ulifika nikawahi chap sikutaka kukaa na mtu leo

Nilifika nikaona nijichanganye na wadada ili wakija wakute Niko na wenzangu

Cha ajabu wote waliinuka na kuniacha mwenyewe

Heeeeesasa mbona wanaondoka jamani

Sijakaa sawa Bosco na Mr Sam hawa hapa wakavuta viti na kukaa

Nageuka nyuma anakuta watu wanaongea chini chini
 
MY BOSS MY LOVE NO 24

Nilikunywa ile chai Kisha nikaendelea na kazi

Jioni ilipofika nilienda ofisini kwake akanambia naweza kwenda nyumbani mwenyewe

Yeyey atachelewa kwasababu anakazi nyingi

Sikuwa na hiyana mtoto wakike nikarudi zangu nyumban ila moyoni kulikuwa kunafukuta yaani nilikuwa namsubiri kwa hamu

Siku hiyo sikumkuta boss nje kwaiyo niliondoka kwa amani kabisa

Nilifika nyumban nikaoga na kumpigia mama tukapiga story kadhaa Kisha nikaingia mtandaoni ili kupoteza mda huko

Nilika hadi saa nne Bosco akiwa bado hajarudi
Nikaona nimtafute maana mda umeenda

Nikapiga nakuta sm iko bz nikamtumia text Kisha nikaendelea kuperuzi

Saa tano na nusu ndio akarudi niliamka na kutoka nje maana nilikuwa kwangu

Nafika nje nakuta amepiga magoti huku ameshika maua nilibaki mdomo wazi ñikijua jamaa ana proposal

Nilivyokuwa na njaa na hiyo ndoa nikasema yes hata kabla hajaongea

"Yes babe niko tayar kuolewa na wewe kipenzi changu"

Niliongea na kumkimbilia alibaki kimya kwanza Kisha akainuka na kunikiss alafu akasema

"Sikuwa na proposal nilikuwa na kwambia unaweza kuspendi usiku na mimi kwenye ulimwengu wa mahaba"

(Shenzi type yaani ndio upige magoti mimi nikajua unataka kunivika Pete )

Nilinywea sio kidogo nikajitoa kwenye kumbato na kusema

"Kwann umechelewa na nakupigia sm iko bz alafu hujanitafuta"

"Nilitaka unimiss mpenzi wangu. Na siunaona nimefaulu maana sio kwa kunikimbilia huko"

"Haya usiku mwema "

"Hey unalalaje saiz kwamfano"..

"Vp ulitaka niote jua au "

"Come on babe,usiwe na hasira mpenzi wangu mzuri,alafu Nina maongezi na wewe "

Aliposema maongezi nikakumbuka mambo aliyoniambia Paulo nikaona kweli sitakiwi kulala twende tukafanye hayo maongezi

"Poa "..

Alinipa maua na kuchukua vitu vingine kwenye gari kumbe alikuja na pizza pamoja na zawadi zingine

Tukaingia ndani

"Kwakua mda umeenda tuongee kwanza alafu ndio ukaoge".........

"Leo tutaenda kuoga wote"

(Njoo tumalizane kwanza)

Sasa nikataka kuongea akasema Acha aanze yeye alafu nitafuata nikasema sawa

"Babe "

"Mmh"

"Nilichotaka kuongea na wewe ni hiki, kwaanza nashukuru kwa uwepo wako katika maisha yangu, umekuwa wa baraka sana kwani umenifanya kuwa na amani na furaha , umekuwa mwanamke wa ndoto zangu tena umekuwa Zaid ya vile nilivyoomba uwe nashukuru sana mpenzi,pili naomba samahani kwayote ambayo niliyowahi kukosea,hasa Jana ,

Lilian "

"Abee "

"Naomba uwe mke wangu naomba nikuoe uwe wangu kabisa "

Uwiiii yaani kusikia hivyo amatapu tapu yaliyokuwa moyoni yakaondoka yote. Nilimkumbatia na kachozi kaka toka

"Nakupenda sana Bosco niko tayar kuwa mkeo hata sekunde hii"

Niliongea huku nikilia alinitoa kwenye kumbato na kunifuta machozi Kisha akasema

"Nakupenda pia malkia wa moyo wangu "

Kama unavyojua felling za mapenzi bhn hazikaagi mbali tulianza kumwagiana makiss

Tukapelekana hadi kwa kitanda yaani tulikuwa kama tunagombana au tumeambiwa mna dakika tano tu maana sio kwa Fujo zile yaani aliona hadi zipu kazi kufungua alishika kablauzi kangu akachana
Chwaaakakalala yooo

Yani ni upwiru plus upwiru sasa bhn tukiwa bz na kuandaana tukasikia yowe nje

"Mamaaaaaa " kwajinsi tulivyokuwa na hali mbaya hatukutilia manani

Mara tukasikia paaaaaa weeee tuliachiana na Kila mtu akakimbia kivyake

Ilikuwa ni mlio wa risasi
Hatujakaa sawa tukasikia tena paaaaaa paaaaaa

Hapo ndio Nilijua kwenye kifo hakuna mwanaume Wala mwanamke Bosco aliingia kabatini na kuniacha nimejikunja kwenye Kona

Hakuna hata aliye mjali mwenzake ilikuwa pambana na hali yako

Pakawa kimya kwa mda tuka sikia watu wakilia

Bosco Bado yuko kabatini mimi mda huo nimesha Sali sala zote kwaiyo nilikuwa tayar kuisalimisha roho yangu

Mara tukasikia mlango ukigongwa kwa nguvu uwiiiiiiiii sijasema kama wanazika au Wana safirisha

Nikitetemeka sio poa nyie kufa kusikieni tu nilitamani kupaa ila mabawa Sina nikatamani kuwa kama sisimizi ila wapi

Nikasikia "Bosco" oooh kumbe alikuwa baba mmoja jirani ndio alikuwa akiita kwani Bosco alitoa hata kope mwanaume muoga huyu

Yule baba aligonga sana sijui nilipata wapi ujasiri nikainuka na kwenda kufungua hapo nimevaa shati la Bosco alafu nimegeuza nyuma kumekuja mbele alafu mbele kukawa nyuma na Iko nje ndani

"Habari yako jirani"

Alisalimia yule baba

"Nzuri shikamoo"

"Marahaba mwanangu huyu kijana yupo"

Nilitaka kusema yupo ila nikahisi kutakuwa na shida nikasema hayupo

"No hayupo"

"Okay Kuna matatizo ya metokea nyumba ya jirani huyo kijana mwanjeshi kamfumnia mkewe wake amewaua wote na ametoweka sasa tulikuwa tunamtafuta huyu kijana hapa aweze kutoa msaada kuita police"

Weeeee babe Wang msimuingize kwenye huo msala kwanza mtu mwenyewe yuko kwenye kabati htaki hata kutoka

Alafu sisi wanawake bhn hivi unapataje nguvu za kuleta mchepuko nyumbani alafu unajua mumeo ni mjeda hata kama angekuwa sio mjed kumleta nyumbani mchepuko kweli

Ngoja nitulize komwe langu sijafika huko yasije kunikuta

Sasa nikiwa nawaza kabla sijamjibu nikashtuka kumuona boss anaingia huku anakimbia

Alifika hakutaka hata kusalimia au kuuliza nashangaa nakumbatiwa huku akihema hatari tulibaki tukishangaa

"Thank God uko sawa nilikuwa nawasi wasi juu yako"

Aliongea huku akiwa amenikumbatia

Sasa nikabaki namaswali yasiyokuwa na majibu

Mara nikasikia king'ora Cha police, yule baba aliposikia na yeye akaondoka nikabaki kwenye kumbato jamaa hataki kuniachia yaani mapigo yake ya moyo yanaenda speed balaa

Akaniachia na kunishika mkono akanitoa pale

Sasa nikawa najaribu kuongea namwambia ananipeleka wapi anichie ila hasikiii

(Hivi huyu bwege kweli hanisikii au ) niliwaza Bosco atakuwa kafa na mshtuko au maana vile nilikuwa nikulalamika boss anauachie angesikia maana nilikuwa naongea kwa sauti

Lakini hadi natoka nje ya geti simuoni Bosco tulifika akafungua mlango na kuingia akatoa gari

Mda huo na lalamika balaa lakin jamaa yuko serious balaa

Aliendesha hadi kwenye hotel akasimama na kunishika mkono hadi kwenye chumba naona alikuwa ana lala humo

"Utakuwa hapa usiku wote huu"

Aliongea na kuniachia Kisha akatoka sasa nataka kumfuata akafunga mlango nikabaki chumbani mwenyewe

Nilibaki nikigonga mlango wapi hakuja nikawaza Bosco wangu atakuwa kwenye Hali gani

Nilikaa chini hadi nikapitiwa na usingizi nilikuja kuamka saa moja nikakuta niko kitandan tena nimefunikwa na shuka

Nikurupuka naangalia hamna mtu nikaamuka na kufungua mlango nikatoka nakuta Kuna baunsa yuko mlangoni ..

"Habari yako madam"

Nilishangaa nikasema huyu kaniteka au

"Boss amesema ukiamka ujiandae nikupeleke ofisini"

Aliongea baada ya kuona niko kimya

"We kaka huyo boss wako yuko wapi"..

"Kazin"

Alivyonijibu nikataka kutoka akanishika na kunirudisha

"Madam nimeambiwa nisikuache utoke ukiwa umevaa hivyo "

Nilijiangalia Toba hivi kumbe nilikuwa nimevaa shati na chupi tu uwii nilirudi ndani fast
Nikwaza inamaana Jana wakati naongea na yule baba nilikuwa nimevaa hivi

Ndio maana alikuwa ananiangalia sana

Basi ikanibidi nivae nguo nilizoachiwa Kisha nikpanda kwenye gari na kutaka anipeleke nyumbani kwani alinijibu aliendesha Moja kwa hadi ofisini nafika
Tu nje nakutana na Mr CEO ametusubiri

Kanyosha mkono kuwa nimshike nani amshike nikampita na kuingia ndani

Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 25

Niliingia ofisini nashangaa wafanya kazi wananishangaa

Akaja Paulo nakusema
"Wewe wamekuachia ukiwa mzima"

Umeanza Paulo embu naomba uniache leo siko na mood nzuri

"Kwani walikupeleka wapi' maana Bosco kasambaza kuwa umetekwa na watu wasiojulikana"

Niliposikia hivyo nikasimama

"Unasemaje "

Akatoa sm yake na kunionesha Heee yaani Bosco kaenda kupost kwenye mtandao kuwa nimetekwa na watu wasio julikana

"Bosco yuko wapi'"

Nilimuuliza huku nikiwa nimekunja uso

"Hajaja kazin"

"Mshenzi yaani Jana nimelalamika kwasauti kabisa hakutoa hata komwe lake nje alafu leo anatangaza mtandaoni Mungu wangu mama yangu asiwe amepata hizi habari

Nilitoka ofisini kwangu nikikimbia sasa ile na shuka ngazi nikakanyaga vibaya weeeee nilitaka kuanguka huo mwereka bahati nzuri nilivutwa nikazungushwa kama pia vile na kutulizwa kifuani ,kumbe ni Mr CEO ndio kanivuta wallah asante we kaka maana ningeanguka kama sio meno basi ninge ng'oa pua

"Uko sawa" huyu kaka ana sauti nzito balaa alafu imejaa hadi inamwagika

Sasa sijui nilikuwa na waza nin maana nilikuwa namshangaa tu

Alivyoona Simjibu alitabasamu
Waooo kweli wakubwa wanafaidi sio kwa uhandsam huu nilipotea kabisa nikawa kama namuona yeye tu

(Itakuwa mshtuko wa Jana bado uko kichwani mm sio wa kuwaza hivyo nakataa )

Alinichia hapo ndipo akili ilirudi nikataka kuondoka akanishika

Yaani huyu kaka akinishika network huwa inahama kabisa nakuwa kama nimekata moto vile alafu hii hali imeanza lini

Alinishika na kunipeleka ofisini kwake yaani namfata tu kama chizi vile

(Atakuwa aliniwekea dawa jana nilipolala maana siwez hata kusema no Yani naenda tu)

Tulifika ofisini kwake akanikalisha kwenye kiti kulikuwa na chai nzito

"Najua hujala kitu toka Jana mchana , and usiwaze kuhusu mama yako hakuna mtu wako yoyote aliepata taarifa zako so ondoa shaka"

Aliongea na kunikabidhi sm yangu

Niliangalia kweli hakuna hata meseji moj ya kuonesha kuwa nimetekwa zaidi zilikuwa za salamu tu

Nikamjibu Tuli na mama na baadhi yao Kisha akaninyanganya sm akidai nile kwanza

Kwani huyu anajikuta nani hasa mbona kama simuelewi hata kidogo

Basi nikala Kisha nikataka mshukuru

Akasema kafungashe nguo zako leo saa nne tukaondoka

" tunaondoka?"

"Yeah kwanzia leo umehamishwa kazi huku unaenda Dar es salaam"

"What , lakin bo"

" Hii ni amri sio ombi kama hutaki kazi huna "

"Lakin mbona imek"

"Una masaa ma wili tu na saizi imebakia saa moja na dakika 58,ukichelewa hata sekunde kazi huna unaweza kwenda"


Nilitamani nimshike nimtikise tikise alafu nimrushe Nje ila naanzia wapi

Nilitoka mle ofisini nikiwa nimenuna bala nilifika nje nakuta mlinzi wake kafungua mlango niingie sikuwa na jeuri nikaingia akawasha gari hadi nyumbani

Nafika namkuta Bosco amekaa mlangoni kwangu huku ameshika picha yangu aliponiona alinikimbilia na kunikumbatia

"Babe I'm sorry Nilijua umetekwa nisamehe sana mpenzi wangu nakuahidi sitoruhusu mtu amkuguse "

Nilitamani kumsonya ila nikaamua kukausha

"Walikupeleka wapi mpenzi wangu "..
(Nyoo ungekuwa inajali si ungetoa komwe langu nje ila ukakaa tu)

"Sijui ila wameniachia kwasababu wamekosea hawakutakiwa kiniteka mm "

Niliamua kumdanganya maana ningeongea ukweli tungeachana sasaiv na mm na mpenda japo siwez kuwa nae nikasema Nina mtu wa kinipigania kikitokea kitu ila nampenda hivyo hivyo

"Nimeamishwa kikazi natakiwa kwenda dar leo"

"What ,kwann na mbona gafla hivyo"

"Hayo maswali kamuulize boss wako hv mbona anakuwa na mambo ya ajabu hivi yaani unawezaje kumhamisha mtu kwa staili hii"

"Pole babe yule ndivyo alivyo, vp si tunafanya kabla haujaondoka"

"Tunafanya nn"

"Sex"

Mfyuuu yaani nilivyo na hasira nawewe hivi alafu unataka nikupe sahau

"Hamna huo mda hapa penyewe anani hesabia dkika"

"Babe kidogo tu napiga kimoja Cha hamu"

"Hivi Bosco unaona huu ni mda wa kuongea habari za kupiga kimoja Cha hamu"

"Aaa usikasirike mpenzi wangu siunajua jinsi nilivyo na hamu na wewe"

"Leo haiwezekani "

"Kwaiyo itakuwaje"

"Utakuja dar "

"Okay "nilitegemea ataniuliza unaenda kukaa wapi lakin hakuuliza

Niliingia ndani nikafunga nguo zangu vitu vingine nikaviacha kwake nikapanda gari na kurudi ofisini

Nilifika tu nikakuta Mr CEO yuko nje hakutaka hata niingie ndani alipanda Kisha tukaondoka

Tulienda hotelin kachukua vitu vyake Kisha tukapanda ndege binafsi (watu Wana maisha bhn )

Mchana tulikuwa dar nilifika nikabaki nashangaa namna mazingira ya ofisi yalivyokuwa mazuri na ulikuwa ni mjengo wa kisasa

(Sasa kwann wakanipeleka Dodoma wakati huku ofisi Kali"

"Ukimaliza kuangalia nifate ofisini kwangu "

Aliongea baada ya kuona nashangaa

Nilimfuata hdi ofisini kwake waooo palikuwa pazuri utafikili ni ofisi zile nazozioana kwenye series za kichina

Alichukua sm yake na kupiga hakuongea aliweka sikioni na kutoa

Baada ya sekunde chache akaja mdada pisi Kali balaa

"Yes boss "

"Mpeleke ofisini kwake "

"Okay"
Aliitikia tukaongozana hadi kwenye ofisi yangu

Niliangalia mlangoni kulikuwa na jina langu

Tukaingia akanionesha na kuondoka

Kabla sijakaa Mr CEO alikuja na kuniambia

"Mda wa kula "

" Asante bado nimeshiba"
Nilivyosema hivyo akatembea kunifuata wee nikiamka chap maana najua anakuja kunivuta

Tulienda kula ila niliagiza ice cream tu maana sikuwa na hamu na chakula nikashangaa wanalet sahani mbili
Kabla sijamuuliza akaongea

"Hiki chakula kiishe"

"Lakin mimi si"

"Una dakika 29 na sekunde 49"

Sinikataka kujifanya jeuri nikataka kuinuka akanishika mkono
Sijui ananini kwenye mikono maana akinishika tu nakuwa siwez kukataa kitu

Nikala huku kanishik mkono mmoja nilivyomaliza akaniachia niliinuka kwa hasira nikarudi ofisini kwangu

Sasa naingia tu nilishtuka kwa kile nilichokiona

Itendelea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 26

Nilishangaa kumkuta mdada kashika kisu alafu kakunja sura balaa

Niliangalia nyuma kama Kuna mtu anakuja hakukuwa na mtu mh nisije kunywewa
Supu

"Hey mrembo mpya mbona kama unajiogopa come on hii ni ofisi yako mh"

We eti come on na ni acome on na hicho kisu kwanza inaonesha anahasira (sijui chizi)

"Unataka nn ofisini kwangu"

Niliuliza kibabe ila huku moyoni na sikia kimbia fala wewe'

"Ooh njo ukae hpa tuongee vizuri madam Lilian"

Mh anajua hadi jina langu ila lazima ajue maana limeandikwa mlango

Sasa mm sikutaka kusogea ila nikawa nazuga pale maana najua tu lazima Mr CEO Atakuwa anakuja na lazima atapitia kwangu sio kwamba njia ya kuingia ofisini kwake Iko hapa no ila nilihisi tu lazima atakuja

We ukitaka niende nipigwe bisu aaa thubutu we kuweza. Basi bwana yule dada sikaanza kuja nikarudi nyuma huku nikitaka kutimua mbio ile nageka tu nikajikuta nagonga kifua Cha mwamba eee Haina haja ya kumtaja maana harufu ya marashi yake inajieleza

Jamani mimi nahisi huyu kaka anasumaku sio bure yaani mwili wangu na wake ukigusana yaani kunaakuwa na kamvutano flani hivi alafu nakuwa speechless kabisa

Nilijikuta nasahau kama Kuna bisu nilikuwa nilikimbia nikawa navuta harufu ya mrashi tu

Si akauzungusha mikono yke kama ananikumbatia vile

Kiufupi huyu kaka nitaanza kumuita jini maana hii sio akili yangu kbisa nakataa tena nakataa

Niliinua uso na kumuangalia nikkutana na uso wake na yeye akiniangalia

Uwiii anamacho flani hivi very romantic alafu lips zake nzuriii za rangi ya Pink Acha na hizi zetu nyeusi

"Are you okay"

Aliniuliza na sauti yake ya kushimba imejazwa ndi ndi ndio nikajibu "mh" nilikuwa kama zuzu jamani uchawi upo

Akitabasamu n kunitoa Kisha akaweka uso wa kazi

"Rudi kazini"

Heeee mara hii yaani kaongea akiwa kama CEO maana sio kwa sauti hiyo

Sasa nikakumbuka kama kulikuwa na kisu nakikimbia sindio kugeuka heee nakuta kadada kamekaa kwenye kiti kiupole Kama sio kenyewe

Mr CEO akageuka na kutaka kuondoka akasimama na kusema

"Jeni go back to your office"

Haaa kumbe kanaitwa Jeni nyie huyu Dada nikimbau mbau sijawahi kuona yaani kifuani kama Hana nyonyo yaani nyuma kama mbele tu miguu sasa uwii alafu keusii tiii sura yenyewe Pana kama chapati sijasema nywele

Alikuwa amenyoa ila nywele zake zinaanzia huku juu nais atakuwa na kipara Cha ukoo, masikini

Kaka inuka chap na kuondoka alipoondoka tu Mr CEO akanikonyeza na jicho moja huku akiachia bonge la tabasamu akaondoka

Nilikuwa namshangaa huyu zinajaa na kutoka au

Hee nikakumbuka huvi Niko dar inamaana ninaenda kukaa na Tuli wangu nikasema ngoja nimpigie chap nimpe taarifa kuwa nimekuja dar

Nilichukua sm nikapiga haikupokelewa nikapiga tena akapokea hee nasikia sauti ya mwanaume

Nikaangalia namba mara mbili mbili mbona ni yake sasa inakuwaje anapokea mwanaume

"Hallo"

"Yes mambo Lili"

Toba huyu nani tena na Jin langu anakijua

"Sorry naongea na nani"

"Unaongea shemeji yako hapa Tuli yuko bafuni anaoga"

Huyu Binti anagawa mda huu kwani hayuko kazini

"Okay asante "

"Okay bye"

"Poa"

Nilikata kisha nikabaki najiuliza mwishoni nikaamua nifanye kazi zangu ee

Saa kumi jion Tuli akanipiga nikampa maswali yangu pale akasema yuko na shemeji mpya tena hawako dar wameenda kula bata Zanzibar

Mmm "kwaiyo mm nalala wap "

Nilimuuliza kibabe siunajua tunawezana

"Kalale ukweni kwanina frank nyoko wewe ,we unakubari kuhamishwa kazi kiholela hivyo hujui utalala wapi "

"Hivi unamjua boss wangu au unaropoka tu"

"Bwanaee hata kama ,basi akutafutie pa kulala maana huwezi kumuhmisha mtu kazi hivyo"

"Usinitafutie shida nikaenda kulala gest"

"Hayaa au mtafute Samira amerudi bongo "

"Angenitafuta Ningemtafuta ila kwasababu hajanitafuta basi"..

"Haya kula jeuri yako "

Sikutaka kuongea sana maana huyu Boss akinikuta itakuwa kesi

Nilikata sm Kisha nimamalizia kazi

Nikiwa bado na weka vitu sawa alikuja Mr CEO

"Mda wa kazi umeisha twende nyumbani"

Twende nyumbani wapi

"Una dakika tano tu"

Aliongea na kuondoka.......

Nilishindwa kuelewa kwnn anasema twende nyumban
Ina maana naenda kwake au
Nilipanga vitu chap nikatoka

"Tunaenda wapi'

Nilimuuliza baada ya kufika

Hakunijibu Zaid alifungua mlango niingie

Sini kajifanya jeuri nikagoma

Kuingia aliwasha gari na kuondoka nikabaki nimesimama

Heee nguo zangu nilikumbuka kuwa siku shusha mabegi


Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE . 27

Nilichukua sm na kuangalia Kama Nina Hela kwenye account nitoe Nika lale lodge

Nikiwa bado naangalia nilishtuka nabebwa juu juu

" Boss niachie nishushe mimi sitaki nishushe bhn "

Nilalamika lakin hakunishusha akafika nje oo kumbe alipack gari akaja kunichukua

Alifika kwenye gari akanafungua mlango na kunikalisha

Kihele hele changu Sasa ile anazunguka abande nikashuka na kukimbia
.yaani wabongo bhn

Yaani wananiona na ingizwa kwenye gari mkuku mkuku hta kuja kunisaidia hamna

Nilitoka mbio kwani nilipiga hatua hatua nyingi alinishika chap akaniegemesha kwenye gari na kunipiga kiss ya nguvu nilipata hisia ambazo sijazipata kwakipindi cha miaka sita yaani mwili ulisisimka hadi vinyweleo vya kwapa vikasimama.

Na hilo ni busu la kawaida sio denda mwanzo nilikuwa nimetoa macho ila sekunde mbili mbele macho yalikuwa yamefunga Cha ajabu nikafungua mdomo kutaka kunyonya lips zake

Kwakwel kama Kuna mtu kaniroga ali amchukue Bosco wangu alaaniwe hii sio kawaida kwani nilisahau kama niko bara barani

Alijitoa nikabaki nimefumba macho

Alinishika mkono hapo nikafungua macho Toba kumbe Kuna watu nyomi wanatuangalia niliingia kwenye gari kama mshale

Alifunga mlango akaingia sasa akanisogelea nikahisi anataka kunikiss tena nikaangalia pembeni

Kumbe alikuwa hana hta mpango alikuwa ananifunga mkanda sasa si Nika geuza shingo

Mara huyu hapa Kani kiss tena safari hii nikataka kumtoa mkono wangu kwani niliweza uliishia kifuani ukatulia tuli huku dimi ziki salimiana

Haikutosha nikazungushwa mikono yangu kumshika kichwa vizuri

Nilikuwa na hisia kali hata sijui zilitoka wapi au kwasababu nimekaa miaka mingi lakin kwa Bosco mbona sipati hisia hivi

Baada ya kukiss kwa dakika kadhaa akaniachia nikafungua macho nakuta ananiangalia kwa macho yaliyojaa Huba zito

"LILIAN"

Aliniita nilikuwa nimelegea kiasi ambacho siwez kueleza

"Yes"

"I love you"

Nilihisi kama nimeskia vibaya au nikiwa bado nashangaa aliwasha gari na kuondoka

Njia nzima nilikuwa kama mtu kachukua ufahamu wangu kabisa maana sikumuwaza Bosco hata kidogo

Mda wote huo alikuwa anaendesha huku amenishika mkono

Tulifika nyumbani waoooo ni bonge la jumba akashuka na mimi nikashuka sasa nikazinduka kutoka kwenye uchawi maana huu ni uchawi sio bure

"Karibu ndani"

Weee nani aingie ndani

"Hapana Boss naomba nguo zangu niende nyumbani"

Alivyoona nataka kumgomea akanifuata weee nani anataka kukissiwa tena nilikimbia chap ndani
Akabaki akicheka tu

Niliingia ndani akanambia nifwate na mm nikamfuata chap

"Hiki ndio chumba chako"

Aliniambia huku nimekaa maili mia yaani nimeshajua ni mr kiss ukikaa vibaya anakupitia

Aliniangalia nilivyo simama mbali akacheka na kudondoka

Baada ya kuondoka nilijifungia mlango nikakaa kitandani na kuanza kukumbuka yaliyotokea
Cha ajabu nikikumbu tu mwili unabadilika

"Hapana hii sio sawa natkiwa kuondoka hapa haraka iwezekanavyo la sivyo nitamcheat Bosco bure"

Niliongea mwenyewe na kuchukua sm yangu

Niliangalia labda Bosco atakuwa amenitumia text lakin sikukuta hata tafadhali nipigie nikaona ngoja nimtafute

Heee hamna namba yake
Niliangalia sikuliona namba yake naenda kwenye chats hakuna hadi za Whatsapp hakuna

Nyie mimi sijana tu Nilikuwa nimemtumia sms sasa mbona hamna na inakuwaje

Uwiiiii niliishiwa pozi baada ya kuona namba nyingi hazikuwepo

Mara akanipigia Tuli "hee dada kuliko unabdilisha namba kama mwizi au ndio Shem kasema ubadilishe"

"Acha wehu hiyo ndio salama,"

"Toka umeanza kusalimiwa zimekufikisha wapi konyo wewe "


"Umesema kuwa nimebadilisha namba gani"

"Si hii uliyonipigia au"

"Nimekwambia unakuwa chizi mimi nimebadilisha namba sangp"

"Mimi na wewe nani chizi "

Nikakata sm ili niangalie heee nashangaa kweli namba ni mpya tena imesalijilia Kwa jina la DIEGO MATTHEW DAVID

heeeee

Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 28

Hii inawezekana je kwani Kuna mtu kaiba lain yangu

Na ameiiba mimi nikiwa wapi
Wait huyu atakuwa boss maana nakumbuka Jana wakati ananichukua pale nyumbani sikuwa na sm alafu akaja kunipa asubuhi inamaana aliitoa wapi

Nilijiuliza bila kupata jibu nikaona ngoja nimfuate maana anataka kunipanda kichwani hata kama ni boss wangu anatakiwa kuwa na mipaka kwani sm yangu haiingiliani na kazi zake

Nilitoka ndani nikiwa na hasira nikashuka na kwenda seblen nikakuta hayupo nikazunguka hadi nje nikiwa nje nikamuona yuko kwenye chumba kimoja nikaingia ndani na kwenda aliko

Kumbe Alikuwa jikoni anapika Cha ajabu baada ya kumuona hasira zote zikaisha nikabaki nimesimama tu

"Karibu"
Aliongea baada ya kuniona
"Asante , boss lain yangu iko wapi"

Yaani ungekuwepo ungeniona kituko maana sio kwa sauti nilioyongea jamani nikimuita huyu mtu mchawi msinipige mawe kwa vile alivyo handsome

Maana haiwezekani Kila nikiwa Karibu yake nakuwa kama zuzu

Nilivyomuuliza hakujibu akaendelea kupika

Nikiwaza kusogea naogopa atanikiss kwaiyo nikabaki nimesimama mlangoni

Nilivyoona hanijibu nikataka kuondoka kama kawaida yke yaani mwaka huu kama nisipo chomoka mkono basi nitateguka bega

Alinivuta nikaangukia kifua sasa nikahisi anataka kunikiss nikakwepesha mdomo alafu nikasahau kama Kuna Sehemu ambayo ukinigusa tu nimeisha yaani hapo Kuna kisima Cha hisia

Akafanya kama ananing'ata shingoni kiruuu nilihisi nimerushwa sayari ya Saba nilimfinya sio kifinyo no kuna namna flani hivi mtu akikushika Sehemu yenye hisia sana Kuna namna ambavyo unamshika alafu unatoa mhemo flani hivi kama umemwangiwa na maji ya mabaridi

"Kwasababu nataka uwe wangu peke yangu" alininong'oneza sikioni

Yaani ile sauti ilipenya hadi kwenye uvungu wa moyo nikawa hoi gafla

"Kaa hapo ule chakula"

Sikutaka kubisha Nika kaa chap

Akanipa chakula na yeye akakaa nakuanza kula.

Aloooh chakula kitamu bala

"Nimepika vizuri au"

"Ndio nikizuri"

Alitabasamu na kuendelea kula

Nilimaliza kula nikamshukuru kisha nikata kuosha vyombo akanizuia nakusema ataosha Dada wakazi

Kumbe kuna dada wa kazi alafu ukapika mwenyewe

Niliwaza hivyo

"Yeah nimepika mwenyewe coz sikutaka mke wangu ale chakula alichopika Mtu mwingine ikiwa ni siku yake ya kwanza kuja hapa

Mke wako miguu yako
Wait kwanza kajuaje kuwa nimewaza hivyo

Nina wasi wasi na huyu kiumbe usikute sio mtu

Wakati nawaza hivyo si akacheka

Mmmh nilipata wasi wasi juu yake usikute nimekaa hapa kumbe ananileta ninone ili aninywe supu

"Usiwaze Sana nenda kapumzike unatakiwa kuamka saa kumi na moja "

(Saa kumi na moja kwani naenda kupokea lindo)

Niliinuka na kumuaga Kisha nikaingia chumba nilichopewa

Nilifika na kujitupa kitandan nikakumbuka matukio ya siku ya leo Nikaona kuna haja ya kutoka humu ndani laa sivyo nitaliwa bure

Na staki kumsariti babe wangu nampenda sana Bosco wangu

Nilichukua sm nikawaza nitampataje
Nikapata wazo yes la kumtafuta Instagram

Lakin wazo hilo haliku fanikiwa kwani sikumpata

Nikaingia Facebook nako sikumpata

Ila nikakumbuka kuwa sikuwahi kum follow kwenye mtandao wowote na sikuwa najua anatumia jina gani siunajua watu wengine hutumia majina yasiyo yao

Niliishiwa pozi nikaamua nilale tu

Kesho yake asubuhi niliamka mapema nikajiandaa na kutoka

Nikamkuta Boss amekaa akinisubiri

"Good morning my queen (habari ya asubuhi malkia wangu)"..

Who is your queen (nani malkia wako)

"Shikamoo boss "

Niliamua kumzingua

"Usiku wako ulikuwaje"

"Ulikuwa vizuri"

"Okay good tunaweza kwenda"

Sikujibu nikatembea kwenda kwenye gari

Nilifika akanifungulia mlango nikaingia na safari ikaanza


Tulifika ofisini Kila mmoja akaenda ofisini kwake..

Nilifika na kukaa Kisha nikaanza kazi

Nikiwa biz n kazi zangu alikuja mdada na kunipa mziwa na korosho nikapokea maana alisema boss ndio kamuagiza

Mara ikaingia text kwenye sm yangu nikachukua na kangalia ilikuwa imetoka kwa boss

"Naenda kwenye Kikao hivyo sitokuwepo so kumbukumbu kula on time bye "

Sasa yeye kwenda kwenye kikao inanihusu nn mimi

Sikujibu nikakausha tu

Nilifanya kazi asubuhi sikushuka Bali niliagiza mchana nikaona ngoja ninyoshe miguu

Nikaenda mgahawani

Sasa nikamkuta yule cheusi

Alivyoniona tu akanifuata
.
"Nilikuwa na kusubiri kwa hamu mwana haramu wewe mbuzi wa albadili shetani wa mguu mmoja hivi unajiona we mzuri sana ee hadi Kuna kuchukua wanaume wa watu"

( Jamani kwani mm nimechukua mme wa nani Bosco au yupi)

"Samahani unaongea na mm au mwingine"

"No naongea na makalio yako,muone sura ilivyokujaa kama puto nakuonya kaa mbali na boss la sivyo nitakupoteza kinyago wewe"..

Aliongea na kunipiga kikuumbo
Jamani kwani huyo boss mm nimemchukua sangap

"We dada naomba tuheshimiane sawa kama ni huyo boss wako mimi Sina mahusiano nae kwaiyo usinitie nuksi " niliamua kuongea maana naweza kuwekwa kidole Cha m***nd kisa upole

"Nyoo eti Sina mahusiano nae ingekuwa huna mahusiano nae ungehamishwa kutoka huko shamba ukaletwa huku ""

Hiv huyu dada ni nani hasa hadi anijie juu maana kwa muonekano hawezi kuwa ametoka na boss

Nikaona hapa nikibishana na mtu nitaonekana mjinga bure nikageuza ili nirudi zangu ndani

Mara akanivuta nywele wee siunajua ukivutwa nywele zinavyouma nilipiga yowe hilo

Cha ajabu hakuna Alie kuja kunitetea

"Niache bhn unaniumiza". niliongea kwa sauti yenye maumivu

" Mimi naongea na wewe alafu unaondoka hivi unanijua mm ni nani mbwa wewe"

"Niache bhn nimeshakwambia mimi si toki nae"

Alinivuta nikahisi kama anataka kung'oa nywele
Na alionekana anapenda sana Sifa maana alikuwa anaongea kwa sauti

Aaawe hapa nikicheza kidogo tu nitanyofolewa nywele

Nilikuwa nimevaa sikonkido nikamkanyaga kwa nguvu akapiga kelele ya maumivu na kuniachia nikamuweka kofi moja takatifu
Shenzi yaani unataka kunizalilisha mbele za watu

Hakuamini kama nimempiga kofi akachukua glass na kutaka kunipiga nayo aise sijui huyu mwamba alitokea wapi alimsika mkono kwa nyuma huku akionesha kuwa na hasira ya juu

Aliposhikwa akafoka bila kujua nani kamshika "niachie nimnyoshe huyu malaya"

Mimi nimesimama hapo nimesha jisema kazi kwisha habari yake

Nikapange nguo zangu nirudi zangu kijijini tu

Aligeuka na kuona alie mshika uwii aliachia ile glass kwa mshtuko naona hakutegemea kumuona boss pale

Sio yeye tu hata mm sikutegemea maana nilitoka nje ya office na kwenda kwenye mgahawa wa kawaida Sana kwahadhi ya Boss asinge kaa hapo
Ila namuona huyu hapa

Alikuwa amekasirika akamuweka kofi moja Binti kaangukia kule akasogea na kunishika huku akianiuliza..

"Uko sawa mpenzi"

Mpenzi tena huyu hanitakii mema anataka waniue sio bure kwanzia lini nikawa mpenzi wake

Itaendelea


MY BOSS MY LOVE NO 29

"niko sawa"
Nilimjibu Kisha akanishika mkono na kwenda hadi ofisini kwake............

Tulifika akanikumbatia na kuniambia..

"I'm sorry umedhalilika kwaajili yangu"

"Ni sawa niko sawa kwaiyo usijali"

" No hauko sawa naona kabisa kwenye macho yako kuwa hauko sawa please naomba unisamehe nakuahidi haitojirudia tena "

"Bo"

kabla sijamaliza kuongea alinikatisha kwakukiss mwaka huu nitakissiwa mkapa niseme

Kwakwel nashindwa kuelewa kwa nn Kila ninapokuwa karibu na huyu mtu huwa nakuwa mtu wa tofauti nashindwa kuzuia hisia zangu kabisa sijui na nini

Tulikiss kwa mda kidogo Kisha akaniachia yaani hapo kwangu kinachoongea ni hisia tu akili aipo kabisa

Akinishika mkono na kunikalisha kwenye kiti Kisha nikasikia "ingia '

Akaingia yule dada akafika na kupiga magoti

Boss akamwambia aniombe msamaha basi kakanigeukua na kuniomba msamaha

Sikuwa na shida nikamsamehe baada ya hapo akainuka boss akasema

"Kakusanye Kila kilicho chako urudi nyumbani hauna kazi "

Heee nilishtuka sana

Masikini dada wawatu akapiga magoti akilia na kumuomba boss amsamehe

Nikiwa kama mwanadamu nikamuonea huruma nikaona nimuunge mkono

Ile nataka kuongea Boss akasema

"Kaa kimya Lilian ".


Mmmh nifunge mdomo wangu mie🫤 lisije kunikuta jambo

"Jeni ondoka ofisini kwangu now"

Masikini alisimama n kuondoka

Mimi nikamuangali kwa huruma nikitamani hta Kumtetea ila nikiwaza na mimi nisije kutolewa bora nifunge mdomo wangu

Mara sm yake ikaita akapokea

"Yes doctor anakuj sasavi"
Alikta na kuniangalia

Amka twende hospital

Kwni naumwa au

"LILIAN sipendi ubishi amka twende wote hospital"

"Lakini boss mm"

Alinishika mkono tukatok nje

Tuliingia kwenye gari na kuondoka

Baada ya kuingia kwenye gari tulienda nyumbani Badala ya hospital tukakuta doctor yuko nyumbani

Akaniangalia pale Kisha akasema niko sawa

Basi akaondoka boss akamuita mdada akaleta chakula tukala then akarudi kazin

Baada ya kuondoka na mm nikatoka ile nikatafute chumba

Niliingia mtaani nikatafuta madalali wakawa na waniambia hamna nyumba Kila mtu ninaenda anasema hamna nyumba

Nilizunguka Kila mahari lakin sikupata hata chumba cha 15000. Nikaona Bora nikalale lodge hata kama ni wiki ili nitafute taratibu

Nako naambiwa hamna vyumba

Nilizunguka haadi inafika saa mbili usiku sijapata Cha lodge Wala chumba

Ilikuwa ni kitu cha ajabu sana kwangu kweli dar es salaam hii ukose chumba au lodge hii Kali ya mwaka

Baada ya kuzunguka Sana nikaamua nirudi kwa boss uzuri sikubeba mabegi yangu maana ningekoma

Nilifika na kukuta boss anazunguka zunguka kama vile mtu mwenye wasi wasi sana alivyoniona tu alinikimbilia na kunikumbatia

"Ulikuwa wapi mke wangu unajua nilikuwa na wasi wasi kuwa utakuwa umekutwa naa kitu kibaya
"
(Huyu anapataje nguvu za kuniita mke wake )

"Boss niko sawa sorry nilisahau kukuaga ila nilienda kutafuta nyumba "

Nilivyoongea hivyo alijitoa kwenye kumbato na kuniangalia

"Ulikuwa umeenda wapi?'"

Heee mbona anauliza kwa ukali hivi

"Kutafuta Nyumba"

"Kwann hutaki kukaa na mm tena nikosa gani kubwa ambalo nimelifanya la kukufanya wewe kunichukia kiasi ambacho hutaki tena kukaa na mimi"

"No Boss sio kwamba nakuchukia ila siwez kuishi humu ndani"

"Kwann hutaki kuishi humu ndani "

"Boss "

"Please Lilian naomba usiondoke,umekuja kwenye maisha yangu kama nuru ukayamilika maisha yangu yaliyokuwa yametanda kiza why unataka kuniacha gizani tena, please kama Kuna kosa lolote nililofanya naomba unisamehe lakin usiniache please sitoweza kuishi bila wewe "

Aliongea huku akiwa amepiga magoti haraka nikataka kunuinua akasema no haamki hadi nitakapo kubari kubaki

"Boss tafadhali amka"

"Please Lilian naomba usiondoke I love you "

Nilibaki njia panda ukweli sikutaka kukaa humu ndani tena maana Nilijua kinaweza kutokea kitu ambacho hakutakiwa na siko tayar kumsariti Bosco wangu

"Fine sito ondoka but kwa sharti moja"

Aliposikia hivyo akaamka

"Sharti gani hilo "

"Usinikiss"

Niliongea huku nikiangalia chini

"Fine kama inakufanya uwe uncomfortable but naomba ujue kuwa nakupenda na sitoruhusu mtu yoyote kuingilia kati hata wewe mwenyewe na sijali kama una mtu au laa ninachojali ni nakupenda basi so wewe ni wangu utake usitake "

Sasa kaanza kwa kunibembeleza kaja kuishia kwenye amri tena

"Chakula kiko mezani good night "

Aliongea na kuondoka nikabaki namshangaa tu eti niwake nitake nisitake

Kwanzia lini mapenzi yaka lazimishwa

Kwakua nilikuwa na njaa nilienda mezani nikala na kutoa vyombo nikavisuza na kuingia chumbani

Sasa siku iliyokuwa inafuata ilikuwa ni jumamoss kwaiyo hakukuwa na kwenda kazini

Nikaingia chumban na kumtafuta Tuli

Nikamwambia nilikuwa natafuta nyumba na nimekosea

Akaniuliza kwani unataka kutoka hapo nikamwambia yeah siwez kukaa humu

Akaniuliza kwann

Nikamwambia Kila kitu kilichotokea

"Hivi Lilian kwann unakuwa katili juu ya hisia zako mwenyewe,kwann unataka kuishi na mtu usie mpenda wakati unaempenda yupo tena na yeye anakupenda"

"Batuli please Sina mapenzi yoyote na boss hiki kinachotokea sio sawa ndio maana nataka kuondoka"

"Hivi unafikili mapenzi ni kupenda tu, Lilian mapenzi ni hisia sio kupenda tu wewe hujawahi hata siku moja kumpenda Bosco mtu unaempenda ni huyo boss wako ndio maana huwezi kucontro hisia zako ukiwa nae hiyo ni ni sain kuwa unampenda"

"No Sina mapenzi yoyote na boss mimi nampenda sana Bosco na ndio mwanaume ambae moyo wangu umeamua kuwa nitaishi nae maisha yangu yote "

"Eee "

"Ndio ,najua najisikia hivi kwasababu sisi ni jinsia tofauti na kingine huenda kwasababu sijafanya mapenzi kwa miaka mingi"

"Acha ujinga hivi hivyo unavyojisikia ndivyo unavyojisikia ukiwa na Bosco jibu ni hapana usifananishe hisia za mapenzi ya kweli na hisia za kingono hivyo ni vitu viwili tofauti kabisa , shida yako wewe hutaki kukubari kwamba frank hayupo na hiyo ndio sababu inayokufanya uwe na Bosco sio kingine, ni kitu kibaya sana kuingia kwenye mahusiano na kwakumuona mtu mwingine ndani yake , unatakiwa kukubari na kuwa mapenzi yako na Frank yameshakufa toka siku aliyokufa na ndio maana hata yeye aliomba kuwa anatamani upate mtu mwingine atakae kupenda na sio upate yeye ndani ya mtu mwingine

Yaani sijui hata niongee neno gani ili unielewe natamani hata ningekuwa karibu nikakuweka makofi labda ungeamka

Kwanza hata huyo Bosco mwenyewe hakupendi uko kwake kama last option tu kwasababu haiingii akilini mtu kukuita jina la mtu mwingine zaidi ya mara mbili alafu uka kaa kimya hembu jaribu kuliweka hili kwa upande wako unawezaje kuitwa Judith alafu ukukaa kimya bila kuuliza huoni kama ni ajabu

LILIAN angalia sana mdogo wangu usipoangalia utakuja kulia maisha yako yote

Hata siku moja usije kuruhusu mapito yako kuharibu future yako

Past is past usiruhusu kamwe Acha inabaki story na kama unaona Kuna lakujifunza lichukue lakini usiyape nafasi ya kuharibu hatima yako

Embu ngoja niishie hapa maana nitaongea mengi lakin bado nitarudia pale pale humpendi Bosco jipe nasafi nyingine

Achia mapito yako Anza upya
Utakaa gizani hata lini

Natamani ungeingia ndani ya moyo wangu ukaona jinsi ninavyougua kutamani kuona ukiishi maisha yenye furaha

Na sisemi haya yote kwasababu na mchukia Bosco no mimi simchukii mtu ila naongea kile kilichoko sawa

Sasa uamzi ni wako kubari kuachia uanze upya au uendelee kushikilia

Usiku mwema "


Alimaliza kuongea na kukata sm

Nilibakia nikifikilia sana Yale maneno
Moyo uliniambia hivi akili inasema vile mwishoni nikapitiwa na usingizi

Asubuhi niliamka baada ya kugongewa mlango

Niliamka nikapiga mswaki na kwenda seblen nikakuta Bosco ananisubiri

"Za asubuhi Boss"

"Ninzur wewe je"

"Nzuri"

"Okay chai iko tayar ,alafu naitwa DIEGO sio Boss"

Kumbe alisajili lain yangu Kwa jina lake alafu nilikuwa sijui kama anaitwa hivyo

Hii ni ajabu ee yaani unafanya kazi alafu hujui boss wako anaitwa nani

Sikumtuikia nilisogea mezani tukanywa chai Kisha akasema atakuwa na kazi so hatoshinda nyumbani

Nikaona bora maana sikuwa nataka hata kumuona ona

Baada ya chai nikainuka ili kwenda chumbani akanishika mkono

'"naomba jioni tutoke dinner"

Nikajibu "okay"

Alitabasamu na kuniachia mkono nikaondoka

Niliingia chumbani huku nikisubiri aondoke ili nikaogelee.

Siunajua napenda maji Kama samaki basi alivyoondoka mimi huyoo kwenye maji

Siku nzima nilikuwa naogolea yaani nikichoka napimzika alafu narudi tena full rahaa tu

Alirudi jioni nikajiandaa Kisha nikatoka

Jamani jamani duniani kuna mahandsome balaa

Mr CEO boss mwenyewe alikuwa ameshajiandaa yuko zake seblen ametoka kapendeza mwenyewe yuko ile mbaya. Sasa sini kasahau kama nilikuwa nashuka ngazi sangap nisitereze uwii nilikula huo mwereka.

Nashukuru Mungu sokung'oa meno Mr CEO akaja mbio na kuninyenyua

"Are you okay '" kwani nilimjibu basi akili yangu ilikuwa iko bize kuangalia uumbaji wa Mungu naona akahisi nitakuwa nimepata mshtuko akanibeba hadi kwenye sofa sasa ile ananilaza bwana siaka nishika mguu kuangalia kama nimeumia akanivua kiatu mimi hapo nawaza mengine kabisa akawa anauzungusha mguu Kama vile ana unaunyoosha

Nikamshika mkono akanianga naona aliona vile nimelegea jamaa akajiongeza akaona kumbe natoa huduma ambayo sio akainuka na kunisogelea karibu ziadi

Kilichotokea hapo sijui nilikuja tu kushtuka asubuhi nikiwa kitandan huku Sina hata nguo moja hata sijui nilibebwa sangap

Oo kulikuwa na chai pembeni kwenye meza ila yeye hakuwepo sini kaamka heee naona nimevaa Pete kidoleni kitu kina Waka hatari

Nilibaki mdomo wazi hata sijui nini kikanikuta nikajikuta naanza kulia

Nikaangalia pembeni nikaona note

"Hello mrembo wangu mzuri natumai umeamka salama asante kwa penzi zito ulilonipatia usiku ulikuwa ni usiku wa pekee sana kwangu thanks my love, nimetoka mara moja make sure unakunywa chai mara tu utakapo amka I love you "

Niulize niliendalea kulia au nilifanya nn nilicheka. Kama kajinga vile

Nilikunywa chai Kisha nikatandika kitandan na kwenda kuoga

Mida ya mchana alirudi nyumbani mda huo nimejificha chumbani nilikuwa naona aibu kumuangalia

Aligonga akitaka nifungue ila nikauchuna

Mwishoni nikasikia anauliza kama Kuna kitu kimenikuta eee nikaona embu niache ujinga kwani naona aibu ya nn kwani ni mara yangu yakwanza kusex jibu ni no basi nikafungua

Ile nafungua tu mtu huyu hapa kanivamia na kunikumbatia

Itaendelea


MY BOSS MY LOVE 30 FINAL

"nilikuwa na was wasi kuwa utakuwa hauko sawa"

Aliongea huku ameshika uso wangu kama kamdoli

Niseme nini sasa nikawa najiwazia tu si unikiss basi kha hadi niombe

Alafu huyu jamaa atakuwa na nguvu za kusoma mawazo ya mtu sio bure
Maana nilivyowaza hivyo alicheka na kunikiss

Vile nilikuwa na njaa ya miaka mingi nikajikuta namfungua vifungo vya shati aliniangalia na kutabasamu Kisha akafunga mlango tukapata moja mbili tatu pale .

We siunajua tena penzi likiwa jipya mnakuwa mnatamani hata mtafunane tu yaani Kila mda unakuwa na hamu na mwenzio

Basi baada ya mechi kali alifuata chakula jikoni akaleta tukapiga msosi saiyo sikumbuki hata kama Kuna mtu anaitwa Bosco huu siutakuwa umalaya yaani mara hii simkumbuki hata jina kwanza sijui hata kama niliwahi kuonana nae

Bwana bwana siku hiyo ilikuwa ni mechi za kirafiki tu ndo zilikuwa zikichezwa

Kesho yake asubuhi kabla ya kwenda Job nikampa chakula elewa neno chakula
Akala bwana aliposhiba hao tukajiandaa na kwenda kazini sasa tukifika kazin anakuwa boss wangu tukirudi nyumbani anakuwa mpenzi wangu yaani ni

MY BOSS alafu ni MY LOVE

Kituko kinakuja siunajua tunakuwaga na vikao e basi yaani tukikaa kwenye kikao unakuta ameweka sura ya ukauzu balaa sasa mimi nikimuangalia najikuta napata picha tukidinyana au akiwa hajavaa basi naishia kubana kicheko tu wanamuona kauzu mwenyewe kumbe mtu flan hivi

Basi bwana zikapita wiki mbili siku hiyo akanambia anataka kunioa so nimpe taratibu zote afuate ili amiliki kabisa

Nikaona hizi habari nataka niwape watu wangu wanguvu nikiwa nawaona kwa macho ili nione vile watakavyofurahi maana wamelia sana na mimi kipindi ambacho nilikuwa nikilia watu kama Hawa ni muhimu sana kwenye maisha yetu

Ninakuombea na wewe unesoma Mungu akupe watu wa kusimama na wewe katika nyakati zote

Basi nikaomba weekend niende nyumbani akakubari

Nikampigia Tuli wangu nimwambia twende Tanga akakubari

Hao tukasepa zetu

Tulifika nyumbani mama nae alikuwepo tukapika tukala na story za hapa na pale alafu nikawaambia sasa kuwa nataka kuolewa

Weee mama alifurahi jamani alilia kwafuraha akapiga magoti na kumshukuru Mungu

Tuli alinipongeza kwa kuchukua maamuzi mazuri akaniwaoo pale bibi pia akanipongeza

Furaha ikatawala pale mama akasema tuombe basi tukapiga magoti akaomba kama mnavyomjua mama yangu akianza kuomba anaomba masaa aliomba akanena ikabidi tumache aendelee

Weekend ilipoisha nikarudi dar

Sasa nikiwa kazini nikatumiwa picha na Paulo (chaumbea) zilikuwa picha za Bosco zikionesha wanafunga ndoa na mzazi mwenzie yuleee Swaum

Nyie nilimshukuru Sana Mungu nikasema kama asinge mleta My Boss saizi mgekuwa mnanipepea

Basi siku zikaenda akatoa mahari tukafunga ndoa

Kwenye ndoa yetu nilimualika Paulo mda wa zawadi akaja kuninon'oneza sikioni

"Aisee mpe kiuno mganisho bila kusahau kumfinyia kwa ndani ili tupate magorofa "

Alivyosema hivyo nikamfinya mda huo babe yuko bz na wageni wengine alivyoona tuana nong'onezana akanikata hilo jicho chap nikarudi Sehemu yangu

Baada ya ndoa kufungwa tukaanza kuishi rasmi kama wanandoa

Kwakwel namshukuru sana Mungu kwakunipa mume Bora mwenye upendo usio na mshariti

Baada ya miezi minne nilipata ujauzito nikajifungua baby boy anafanana na baba yake huyo balaa yaani utafikili aliingia tumboni mwangu alafu akatoka ,

Maisha yaliendelea tukapata mtoto mwingine nae ni boy

Huku Bado nikiendalea kufanya kazi mtindo ndio ule ule
Akiwa kazini ni
.MY BOSS akiwa nyumbani ni MY LOVE

Rafiki yang kipenzi BATULI alifunga ndoa na mpenzi wake wakajaliwa mtoto wakike kazuri kwnye

Sijamsahau Frank ila sikuhizi uchungu umeisha kabisa yaani imebaki na makumbuka kama mtu aliye kuwa muhimu kwangu

Kila mwaka kwenye birthday yake huwa naenda nafanya usafi kwenye kaburi lake then namuombea Misa kanisani na kumtolea sadaka ili kama Kuna msamaha wawafu basi Mungu amsamehe frank wangu

R I.P FRANK

Na huu ndio mwisho wa simulizi yangu ya my MY BOSS MY LOVE
 
MY BOSS MY LOVE NO 24

Nilikunywa ile chai Kisha nikaendelea na kazi

Jioni ilipofika nilienda ofisini kwake akanambia naweza kwenda nyumbani mwenyewe

Yeyey atachelewa kwasababu anakazi nyingi

Sikuwa na hiyana mtoto wakike nikarudi zangu nyumban ila moyoni kulikuwa kunafukuta yaani nilikuwa namsubiri kwa hamu

Siku hiyo sikumkuta boss nje kwaiyo niliondoka kwa amani kabisa

Nilifika nyumban nikaoga na kumpigia mama tukapiga story kadhaa Kisha nikaingia mtandaoni ili kupoteza mda huko

Nilika hadi saa nne Bosco akiwa bado hajarudi
Nikaona nimtafute maana mda umeenda

Nikapiga nakuta sm iko bz nikamtumia text Kisha nikaendelea kuperuzi

Saa tano na nusu ndio akarudi niliamka na kutoka nje maana nilikuwa kwangu

Nafika nje nakuta amepiga magoti huku ameshika maua nilibaki mdomo wazi ñikijua jamaa ana proposal

Nilivyokuwa na njaa na hiyo ndoa nikasema yes hata kabla hajaongea

"Yes babe niko tayar kuolewa na wewe kipenzi changu"

Niliongea na kumkimbilia alibaki kimya kwanza Kisha akainuka na kunikiss alafu akasema

"Sikuwa na proposal nilikuwa na kwambia unaweza kuspendi usiku na mimi kwenye ulimwengu wa mahaba"

(Shenzi type yaani ndio upige magoti mimi nikajua unataka kunivika Pete )

Nilinywea sio kidogo nikajitoa kwenye kumbato na kusema

"Kwann umechelewa na nakupigia sm iko bz alafu hujanitafuta"

"Nilitaka unimiss mpenzi wangu. Na siunaona nimefaulu maana sio kwa kunikimbilia huko"

"Haya usiku mwema "

"Hey unalalaje saiz kwamfano"..

"Vp ulitaka niote jua au "

"Come on babe,usiwe na hasira mpenzi wangu mzuri,alafu Nina maongezi na wewe "

Aliposema maongezi nikakumbuka mambo aliyoniambia Paulo nikaona kweli sitakiwi kulala twende tukafanye hayo maongezi

"Poa "..

Alinipa maua na kuchukua vitu vingine kwenye gari kumbe alikuja na pizza pamoja na zawadi zingine

Tukaingia ndani

"Kwakua mda umeenda tuongee kwanza alafu ndio ukaoge".........

"Leo tutaenda kuoga wote"

(Njoo tumalizane kwanza)

Sasa nikataka kuongea akasema Acha aanze yeye alafu nitafuata nikasema sawa

"Babe "

"Mmh"

"Nilichotaka kuongea na wewe ni hiki, kwaanza nashukuru kwa uwepo wako katika maisha yangu, umekuwa wa baraka sana kwani umenifanya kuwa na amani na furaha , umekuwa mwanamke wa ndoto zangu tena umekuwa Zaid ya vile nilivyoomba uwe nashukuru sana mpenzi,pili naomba samahani kwayote ambayo niliyowahi kukosea,hasa Jana ,

Lilian "

"Abee "

"Naomba uwe mke wangu naomba nikuoe uwe wangu kabisa "

Uwiiii yaani kusikia hivyo amatapu tapu yaliyokuwa moyoni yakaondoka yote. Nilimkumbatia na kachozi kaka toka

"Nakupenda sana Bosco niko tayar kuwa mkeo hata sekunde hii"

Niliongea huku nikilia alinitoa kwenye kumbato na kunifuta machozi Kisha akasema

"Nakupenda pia malkia wa moyo wangu "

Kama unavyojua felling za mapenzi bhn hazikaagi mbali tulianza kumwagiana makiss

Tukapelekana hadi kwa kitanda yaani tulikuwa kama tunagombana au tumeambiwa mna dakika tano tu maana sio kwa Fujo zile yaani aliona hadi zipu kazi kufungua alishika kablauzi kangu akachana
Chwaaakakalala yooo

Yani ni upwiru plus upwiru sasa bhn tukiwa bz na kuandaana tukasikia yowe nje

"Mamaaaaaa " kwajinsi tulivyokuwa na hali mbaya hatukutilia manani

Mara tukasikia paaaaaa weeee tuliachiana na Kila mtu akakimbia kivyake

Ilikuwa ni mlio wa risasi
Hatujakaa sawa tukasikia tena paaaaaa paaaaaa

Hapo ndio Nilijua kwenye kifo hakuna mwanaume Wala mwanamke Bosco aliingia kabatini na kuniacha nimejikunja kwenye Kona

Hakuna hata aliye mjali mwenzake ilikuwa pambana na hali yako

Pakawa kimya kwa mda tuka sikia watu wakilia

Bosco Bado yuko kabatini mimi mda huo nimesha Sali sala zote kwaiyo nilikuwa tayar kuisalimisha roho yangu

Mara tukasikia mlango ukigongwa kwa nguvu uwiiiiiiiii sijasema kama wanazika au Wana safirisha

Nikitetemeka sio poa nyie kufa kusikieni tu nilitamani kupaa ila mabawa Sina nikatamani kuwa kama sisimizi ila wapi

Nikasikia "Bosco" oooh kumbe alikuwa baba mmoja jirani ndio alikuwa akiita kwani Bosco alitoa hata kope mwanaume muoga huyu

Yule baba aligonga sana sijui nilipata wapi ujasiri nikainuka na kwenda kufungua hapo nimevaa shati la Bosco alafu nimegeuza nyuma kumekuja mbele alafu mbele kukawa nyuma na Iko nje ndani

"Habari yako jirani"

Alisalimia yule baba

"Nzuri shikamoo"

"Marahaba mwanangu huyu kijana yupo"

Nilitaka kusema yupo ila nikahisi kutakuwa na shida nikasema hayupo

"No hayupo"

"Okay Kuna matatizo ya metokea nyumba ya jirani huyo kijana mwanjeshi kamfumnia mkewe wake amewaua wote na ametoweka sasa tulikuwa tunamtafuta huyu kijana hapa aweze kutoa msaada kuita police"

Weeeee babe Wang msimuingize kwenye huo msala kwanza mtu mwenyewe yuko kwenye kabati htaki hata kutoka

Alafu sisi wanawake bhn hivi unapataje nguvu za kuleta mchepuko nyumbani alafu unajua mumeo ni mjeda hata kama angekuwa sio mjed kumleta nyumbani mchepuko kweli

Ngoja nitulize komwe langu sijafika huko yasije kunikuta

Sasa nikiwa nawaza kabla sijamjibu nikashtuka kumuona boss anaingia huku anakimbia

Alifika hakutaka hata kusalimia au kuuliza nashangaa nakumbatiwa huku akihema hatari tulibaki tukishangaa

"Thank God uko sawa nilikuwa nawasi wasi juu yako"

Aliongea huku akiwa amenikumbatia

Sasa nikabaki namaswali yasiyokuwa na majibu

Mara nikasikia king'ora Cha police, yule baba aliposikia na yeye akaondoka nikabaki kwenye kumbato jamaa hataki kuniachia yaani mapigo yake ya moyo yanaenda speed balaa

Akaniachia na kunishika mkono akanitoa pale

Sasa nikawa najaribu kuongea namwambia ananipeleka wapi anichie ila hasikiii

(Hivi huyu bwege kweli hanisikii au ) niliwaza Bosco atakuwa kafa na mshtuko au maana vile nilikuwa nikulalamika boss anauachie angesikia maana nilikuwa naongea kwa sauti

Lakini hadi natoka nje ya geti simuoni Bosco tulifika akafungua mlango na kuingia akatoa gari

Mda huo na lalamika balaa lakin jamaa yuko serious balaa

Aliendesha hadi kwenye hotel akasimama na kunishika mkono hadi kwenye chumba naona alikuwa ana lala humo

"Utakuwa hapa usiku wote huu"

Aliongea na kuniachia Kisha akatoka sasa nataka kumfuata akafunga mlango nikabaki chumbani mwenyewe

Nilibaki nikigonga mlango wapi hakuja nikawaza Bosco wangu atakuwa kwenye Hali gani

Nilikaa chini hadi nikapitiwa na usingizi nilikuja kuamka saa moja nikakuta niko kitandan tena nimefunikwa na shuka

Nikurupuka naangalia hamna mtu nikaamuka na kufungua mlango nikatoka nakuta Kuna baunsa yuko mlangoni ..

"Habari yako madam"

Nilishangaa nikasema huyu kaniteka au

"Boss amesema ukiamka ujiandae nikupeleke ofisini"

Aliongea baada ya kuona niko kimya

"We kaka huyo boss wako yuko wapi"..

"Kazin"

Alivyonijibu nikataka kutoka akanishika na kunirudisha

"Madam nimeambiwa nisikuache utoke ukiwa umevaa hivyo "

Nilijiangalia Toba hivi kumbe nilikuwa nimevaa shati na chupi tu uwii nilirudi ndani fast
Nikwaza inamaana Jana wakati naongea na yule baba nilikuwa nimevaa hivi

Ndio maana alikuwa ananiangalia sana

Basi ikanibidi nivae nguo nilizoachiwa Kisha nikpanda kwenye gari na kutaka anipeleke nyumbani kwani alinijibu aliendesha Moja kwa hadi ofisini nafika
Tu nje nakutana na Mr CEO ametusubiri

Kanyosha mkono kuwa nimshike nani amshike nikampita na kuingia ndani

Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 25

Niliingia ofisini nashangaa wafanya kazi wananishangaa

Akaja Paulo nakusema
"Wewe wamekuachia ukiwa mzima"

Umeanza Paulo embu naomba uniache leo siko na mood nzuri

"Kwani walikupeleka wapi' maana Bosco kasambaza kuwa umetekwa na watu wasiojulikana"

Niliposikia hivyo nikasimama

"Unasemaje "

Akatoa sm yake na kunionesha Heee yaani Bosco kaenda kupost kwenye mtandao kuwa nimetekwa na watu wasio julikana

"Bosco yuko wapi'"

Nilimuuliza huku nikiwa nimekunja uso

"Hajaja kazin"

"Mshenzi yaani Jana nimelalamika kwasauti kabisa hakutoa hata komwe lake nje alafu leo anatangaza mtandaoni Mungu wangu mama yangu asiwe amepata hizi habari

Nilitoka ofisini kwangu nikikimbia sasa ile na shuka ngazi nikakanyaga vibaya weeeee nilitaka kuanguka huo mwereka bahati nzuri nilivutwa nikazungushwa kama pia vile na kutulizwa kifuani ,kumbe ni Mr CEO ndio kanivuta wallah asante we kaka maana ningeanguka kama sio meno basi ninge ng'oa pua

"Uko sawa" huyu kaka ana sauti nzito balaa alafu imejaa hadi inamwagika

Sasa sijui nilikuwa na waza nin maana nilikuwa namshangaa tu

Alivyoona Simjibu alitabasamu
Waooo kweli wakubwa wanafaidi sio kwa uhandsam huu nilipotea kabisa nikawa kama namuona yeye tu

(Itakuwa mshtuko wa Jana bado uko kichwani mm sio wa kuwaza hivyo nakataa )

Alinichia hapo ndipo akili ilirudi nikataka kuondoka akanishika

Yaani huyu kaka akinishika network huwa inahama kabisa nakuwa kama nimekata moto vile alafu hii hali imeanza lini

Alinishika na kunipeleka ofisini kwake yaani namfata tu kama chizi vile

(Atakuwa aliniwekea dawa jana nilipolala maana siwez hata kusema no Yani naenda tu)

Tulifika ofisini kwake akanikalisha kwenye kiti kulikuwa na chai nzito

"Najua hujala kitu toka Jana mchana , and usiwaze kuhusu mama yako hakuna mtu wako yoyote aliepata taarifa zako so ondoa shaka"

Aliongea na kunikabidhi sm yangu

Niliangalia kweli hakuna hata meseji moj ya kuonesha kuwa nimetekwa zaidi zilikuwa za salamu tu

Nikamjibu Tuli na mama na baadhi yao Kisha akaninyanganya sm akidai nile kwanza

Kwani huyu anajikuta nani hasa mbona kama simuelewi hata kidogo

Basi nikala Kisha nikataka mshukuru

Akasema kafungashe nguo zako leo saa nne tukaondoka

" tunaondoka?"

"Yeah kwanzia leo umehamishwa kazi huku unaenda Dar es salaam"

"What , lakin bo"

" Hii ni amri sio ombi kama hutaki kazi huna "

"Lakin mbona imek"

"Una masaa ma wili tu na saizi imebakia saa moja na dakika 58,ukichelewa hata sekunde kazi huna unaweza kwenda"


Nilitamani nimshike nimtikise tikise alafu nimrushe Nje ila naanzia wapi

Nilitoka mle ofisini nikiwa nimenuna bala nilifika nje nakuta mlinzi wake kafungua mlango niingie sikuwa na jeuri nikaingia akawasha gari hadi nyumbani

Nafika namkuta Bosco amekaa mlangoni kwangu huku ameshika picha yangu aliponiona alinikimbilia na kunikumbatia

"Babe I'm sorry Nilijua umetekwa nisamehe sana mpenzi wangu nakuahidi sitoruhusu mtu amkuguse "

Nilitamani kumsonya ila nikaamua kukausha

"Walikupeleka wapi mpenzi wangu "..
(Nyoo ungekuwa inajali si ungetoa komwe langu nje ila ukakaa tu)

"Sijui ila wameniachia kwasababu wamekosea hawakutakiwa kiniteka mm "

Niliamua kumdanganya maana ningeongea ukweli tungeachana sasaiv na mm na mpenda japo siwez kuwa nae nikasema Nina mtu wa kinipigania kikitokea kitu ila nampenda hivyo hivyo

"Nimeamishwa kikazi natakiwa kwenda dar leo"

"What ,kwann na mbona gafla hivyo"

"Hayo maswali kamuulize boss wako hv mbona anakuwa na mambo ya ajabu hivi yaani unawezaje kumhamisha mtu kwa staili hii"

"Pole babe yule ndivyo alivyo, vp si tunafanya kabla haujaondoka"

"Tunafanya nn"

"Sex"

Mfyuuu yaani nilivyo na hasira nawewe hivi alafu unataka nikupe sahau

"Hamna huo mda hapa penyewe anani hesabia dkika"

"Babe kidogo tu napiga kimoja Cha hamu"

"Hivi Bosco unaona huu ni mda wa kuongea habari za kupiga kimoja Cha hamu"

"Aaa usikasirike mpenzi wangu siunajua jinsi nilivyo na hamu na wewe"

"Leo haiwezekani "

"Kwaiyo itakuwaje"

"Utakuja dar "

"Okay "nilitegemea ataniuliza unaenda kukaa wapi lakin hakuuliza

Niliingia ndani nikafunga nguo zangu vitu vingine nikaviacha kwake nikapanda gari na kurudi ofisini

Nilifika tu nikakuta Mr CEO yuko nje hakutaka hata niingie ndani alipanda Kisha tukaondoka

Tulienda hotelin kachukua vitu vyake Kisha tukapanda ndege binafsi (watu Wana maisha bhn )

Mchana tulikuwa dar nilifika nikabaki nashangaa namna mazingira ya ofisi yalivyokuwa mazuri na ulikuwa ni mjengo wa kisasa

(Sasa kwann wakanipeleka Dodoma wakati huku ofisi Kali"

"Ukimaliza kuangalia nifate ofisini kwangu "

Aliongea baada ya kuona nashangaa

Nilimfuata hdi ofisini kwake waooo palikuwa pazuri utafikili ni ofisi zile nazozioana kwenye series za kichina

Alichukua sm yake na kupiga hakuongea aliweka sikioni na kutoa

Baada ya sekunde chache akaja mdada pisi Kali balaa

"Yes boss "

"Mpeleke ofisini kwake "

"Okay"
Aliitikia tukaongozana hadi kwenye ofisi yangu

Niliangalia mlangoni kulikuwa na jina langu

Tukaingia akanionesha na kuondoka

Kabla sijakaa Mr CEO alikuja na kuniambia

"Mda wa kula "

" Asante bado nimeshiba"
Nilivyosema hivyo akatembea kunifuata wee nikiamka chap maana najua anakuja kunivuta

Tulienda kula ila niliagiza ice cream tu maana sikuwa na hamu na chakula nikashangaa wanalet sahani mbili
Kabla sijamuuliza akaongea

"Hiki chakula kiishe"

"Lakin mimi si"

"Una dakika 29 na sekunde 49"

Sinikataka kujifanya jeuri nikataka kuinuka akanishika mkono
Sijui ananini kwenye mikono maana akinishika tu nakuwa siwez kukataa kitu

Nikala huku kanishik mkono mmoja nilivyomaliza akaniachia niliinuka kwa hasira nikarudi ofisini kwangu

Sasa naingia tu nilishtuka kwa kile nilichokiona

Itendelea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 26

Nilishangaa kumkuta mdada kashika kisu alafu kakunja sura balaa

Niliangalia nyuma kama Kuna mtu anakuja hakukuwa na mtu mh nisije kunywewa
Supu

"Hey mrembo mpya mbona kama unajiogopa come on hii ni ofisi yako mh"

We eti come on na ni acome on na hicho kisu kwanza inaonesha anahasira (sijui chizi)

"Unataka nn ofisini kwangu"

Niliuliza kibabe ila huku moyoni na sikia kimbia fala wewe'

"Ooh njo ukae hpa tuongee vizuri madam Lilian"

Mh anajua hadi jina langu ila lazima ajue maana limeandikwa mlango

Sasa mm sikutaka kusogea ila nikawa nazuga pale maana najua tu lazima Mr CEO Atakuwa anakuja na lazima atapitia kwangu sio kwamba njia ya kuingia ofisini kwake Iko hapa no ila nilihisi tu lazima atakuja

We ukitaka niende nipigwe bisu aaa thubutu we kuweza. Basi bwana yule dada sikaanza kuja nikarudi nyuma huku nikitaka kutimua mbio ile nageka tu nikajikuta nagonga kifua Cha mwamba eee Haina haja ya kumtaja maana harufu ya marashi yake inajieleza

Jamani mimi nahisi huyu kaka anasumaku sio bure yaani mwili wangu na wake ukigusana yaani kunaakuwa na kamvutano flani hivi alafu nakuwa speechless kabisa

Nilijikuta nasahau kama Kuna bisu nilikuwa nilikimbia nikawa navuta harufu ya mrashi tu

Si akauzungusha mikono yke kama ananikumbatia vile

Kiufupi huyu kaka nitaanza kumuita jini maana hii sio akili yangu kbisa nakataa tena nakataa

Niliinua uso na kumuangalia nikkutana na uso wake na yeye akiniangalia

Uwiii anamacho flani hivi very romantic alafu lips zake nzuriii za rangi ya Pink Acha na hizi zetu nyeusi

"Are you okay"

Aliniuliza na sauti yake ya kushimba imejazwa ndi ndi ndio nikajibu "mh" nilikuwa kama zuzu jamani uchawi upo

Akitabasamu n kunitoa Kisha akaweka uso wa kazi

"Rudi kazini"

Heeee mara hii yaani kaongea akiwa kama CEO maana sio kwa sauti hiyo

Sasa nikakumbuka kama kulikuwa na kisu nakikimbia sindio kugeuka heee nakuta kadada kamekaa kwenye kiti kiupole Kama sio kenyewe

Mr CEO akageuka na kutaka kuondoka akasimama na kusema

"Jeni go back to your office"

Haaa kumbe kanaitwa Jeni nyie huyu Dada nikimbau mbau sijawahi kuona yaani kifuani kama Hana nyonyo yaani nyuma kama mbele tu miguu sasa uwii alafu keusii tiii sura yenyewe Pana kama chapati sijasema nywele

Alikuwa amenyoa ila nywele zake zinaanzia huku juu nais atakuwa na kipara Cha ukoo, masikini

Kaka inuka chap na kuondoka alipoondoka tu Mr CEO akanikonyeza na jicho moja huku akiachia bonge la tabasamu akaondoka

Nilikuwa namshangaa huyu zinajaa na kutoka au

Hee nikakumbuka huvi Niko dar inamaana ninaenda kukaa na Tuli wangu nikasema ngoja nimpigie chap nimpe taarifa kuwa nimekuja dar

Nilichukua sm nikapiga haikupokelewa nikapiga tena akapokea hee nasikia sauti ya mwanaume

Nikaangalia namba mara mbili mbili mbona ni yake sasa inakuwaje anapokea mwanaume

"Hallo"

"Yes mambo Lili"

Toba huyu nani tena na Jin langu anakijua

"Sorry naongea na nani"

"Unaongea shemeji yako hapa Tuli yuko bafuni anaoga"

Huyu Binti anagawa mda huu kwani hayuko kazini

"Okay asante "

"Okay bye"

"Poa"

Nilikata kisha nikabaki najiuliza mwishoni nikaamua nifanye kazi zangu ee

Saa kumi jion Tuli akanipiga nikampa maswali yangu pale akasema yuko na shemeji mpya tena hawako dar wameenda kula bata Zanzibar

Mmm "kwaiyo mm nalala wap "

Nilimuuliza kibabe siunajua tunawezana

"Kalale ukweni kwanina frank nyoko wewe ,we unakubari kuhamishwa kazi kiholela hivyo hujui utalala wapi "

"Hivi unamjua boss wangu au unaropoka tu"

"Bwanaee hata kama ,basi akutafutie pa kulala maana huwezi kumuhmisha mtu kazi hivyo"

"Usinitafutie shida nikaenda kulala gest"

"Hayaa au mtafute Samira amerudi bongo "

"Angenitafuta Ningemtafuta ila kwasababu hajanitafuta basi"..

"Haya kula jeuri yako "

Sikutaka kuongea sana maana huyu Boss akinikuta itakuwa kesi

Nilikata sm Kisha nimamalizia kazi

Nikiwa bado na weka vitu sawa alikuja Mr CEO

"Mda wa kazi umeisha twende nyumbani"

Twende nyumbani wapi

"Una dakika tano tu"

Aliongea na kuondoka.......

Nilishindwa kuelewa kwnn anasema twende nyumban
Ina maana naenda kwake au
Nilipanga vitu chap nikatoka

"Tunaenda wapi'

Nilimuuliza baada ya kufika

Hakunijibu Zaid alifungua mlango niingie

Sini kajifanya jeuri nikagoma

Kuingia aliwasha gari na kuondoka nikabaki nimesimama

Heee nguo zangu nilikumbuka kuwa siku shusha mabegi


Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE . 27

Nilichukua sm na kuangalia Kama Nina Hela kwenye account nitoe Nika lale lodge

Nikiwa bado naangalia nilishtuka nabebwa juu juu

" Boss niachie nishushe mimi sitaki nishushe bhn "

Nilalamika lakin hakunishusha akafika nje oo kumbe alipack gari akaja kunichukua

Alifika kwenye gari akanafungua mlango na kunikalisha

Kihele hele changu Sasa ile anazunguka abande nikashuka na kukimbia
.yaani wabongo bhn

Yaani wananiona na ingizwa kwenye gari mkuku mkuku hta kuja kunisaidia hamna

Nilitoka mbio kwani nilipiga hatua hatua nyingi alinishika chap akaniegemesha kwenye gari na kunipiga kiss ya nguvu nilipata hisia ambazo sijazipata kwakipindi cha miaka sita yaani mwili ulisisimka hadi vinyweleo vya kwapa vikasimama.

Na hilo ni busu la kawaida sio denda mwanzo nilikuwa nimetoa macho ila sekunde mbili mbele macho yalikuwa yamefunga Cha ajabu nikafungua mdomo kutaka kunyonya lips zake

Kwakwel kama Kuna mtu kaniroga ali amchukue Bosco wangu alaaniwe hii sio kawaida kwani nilisahau kama niko bara barani

Alijitoa nikabaki nimefumba macho

Alinishika mkono hapo nikafungua macho Toba kumbe Kuna watu nyomi wanatuangalia niliingia kwenye gari kama mshale

Alifunga mlango akaingia sasa akanisogelea nikahisi anataka kunikiss tena nikaangalia pembeni

Kumbe alikuwa hana hta mpango alikuwa ananifunga mkanda sasa si Nika geuza shingo

Mara huyu hapa Kani kiss tena safari hii nikataka kumtoa mkono wangu kwani niliweza uliishia kifuani ukatulia tuli huku dimi ziki salimiana

Haikutosha nikazungushwa mikono yangu kumshika kichwa vizuri

Nilikuwa na hisia kali hata sijui zilitoka wapi au kwasababu nimekaa miaka mingi lakin kwa Bosco mbona sipati hisia hivi

Baada ya kukiss kwa dakika kadhaa akaniachia nikafungua macho nakuta ananiangalia kwa macho yaliyojaa Huba zito

"LILIAN"

Aliniita nilikuwa nimelegea kiasi ambacho siwez kueleza

"Yes"

"I love you"

Nilihisi kama nimeskia vibaya au nikiwa bado nashangaa aliwasha gari na kuondoka

Njia nzima nilikuwa kama mtu kachukua ufahamu wangu kabisa maana sikumuwaza Bosco hata kidogo

Mda wote huo alikuwa anaendesha huku amenishika mkono

Tulifika nyumbani waoooo ni bonge la jumba akashuka na mimi nikashuka sasa nikazinduka kutoka kwenye uchawi maana huu ni uchawi sio bure

"Karibu ndani"

Weee nani aingie ndani

"Hapana Boss naomba nguo zangu niende nyumbani"

Alivyoona nataka kumgomea akanifuata weee nani anataka kukissiwa tena nilikimbia chap ndani
Akabaki akicheka tu

Niliingia ndani akanambia nifwate na mm nikamfuata chap

"Hiki ndio chumba chako"

Aliniambia huku nimekaa maili mia yaani nimeshajua ni mr kiss ukikaa vibaya anakupitia

Aliniangalia nilivyo simama mbali akacheka na kudondoka

Baada ya kuondoka nilijifungia mlango nikakaa kitandani na kuanza kukumbuka yaliyotokea
Cha ajabu nikikumbu tu mwili unabadilika

"Hapana hii sio sawa natkiwa kuondoka hapa haraka iwezekanavyo la sivyo nitamcheat Bosco bure"

Niliongea mwenyewe na kuchukua sm yangu

Niliangalia labda Bosco atakuwa amenitumia text lakin sikukuta hata tafadhali nipigie nikaona ngoja nimtafute

Heee hamna namba yake
Niliangalia sikuliona namba yake naenda kwenye chats hakuna hadi za Whatsapp hakuna

Nyie mimi sijana tu Nilikuwa nimemtumia sms sasa mbona hamna na inakuwaje

Uwiiiii niliishiwa pozi baada ya kuona namba nyingi hazikuwepo

Mara akanipigia Tuli "hee dada kuliko unabdilisha namba kama mwizi au ndio Shem kasema ubadilishe"

"Acha wehu hiyo ndio salama,"

"Toka umeanza kusalimiwa zimekufikisha wapi konyo wewe "


"Umesema kuwa nimebadilisha namba gani"

"Si hii uliyonipigia au"

"Nimekwambia unakuwa chizi mimi nimebadilisha namba sangp"

"Mimi na wewe nani chizi "

Nikakata sm ili niangalie heee nashangaa kweli namba ni mpya tena imesalijilia Kwa jina la DIEGO MATTHEW DAVID

heeeee

Itaelendea

---
Shared using https://www.writediary.com/getappDate: Nov 3, 2023
Subject: MY BOSS MY LOVE 28

Hii inawezekana je kwani Kuna mtu kaiba lain yangu

Na ameiiba mimi nikiwa wapi
Wait huyu atakuwa boss maana nakumbuka Jana wakati ananichukua pale nyumbani sikuwa na sm alafu akaja kunipa asubuhi inamaana aliitoa wapi

Nilijiuliza bila kupata jibu nikaona ngoja nimfuate maana anataka kunipanda kichwani hata kama ni boss wangu anatakiwa kuwa na mipaka kwani sm yangu haiingiliani na kazi zake

Nilitoka ndani nikiwa na hasira nikashuka na kwenda seblen nikakuta hayupo nikazunguka hadi nje nikiwa nje nikamuona yuko kwenye chumba kimoja nikaingia ndani na kwenda aliko

Kumbe Alikuwa jikoni anapika Cha ajabu baada ya kumuona hasira zote zikaisha nikabaki nimesimama tu

"Karibu"
Aliongea baada ya kuniona
"Asante , boss lain yangu iko wapi"

Yaani ungekuwepo ungeniona kituko maana sio kwa sauti nilioyongea jamani nikimuita huyu mtu mchawi msinipige mawe kwa vile alivyo handsome

Maana haiwezekani Kila nikiwa Karibu yake nakuwa kama zuzu

Nilivyomuuliza hakujibu akaendelea kupika

Nikiwaza kusogea naogopa atanikiss kwaiyo nikabaki nimesimama mlangoni

Nilivyoona hanijibu nikataka kuondoka kama kawaida yke yaani mwaka huu kama nisipo chomoka mkono basi nitateguka bega

Alinivuta nikaangukia kifua sasa nikahisi anataka kunikiss nikakwepesha mdomo alafu nikasahau kama Kuna Sehemu ambayo ukinigusa tu nimeisha yaani hapo Kuna kisima Cha hisia

Akafanya kama ananing'ata shingoni kiruuu nilihisi nimerushwa sayari ya Saba nilimfinya sio kifinyo no kuna namna flani hivi mtu akikushika Sehemu yenye hisia sana Kuna namna ambavyo unamshika alafu unatoa mhemo flani hivi kama umemwangiwa na maji ya mabaridi

"Kwasababu nataka uwe wangu peke yangu" alininong'oneza sikioni

Yaani ile sauti ilipenya hadi kwenye uvungu wa moyo nikawa hoi gafla

"Kaa hapo ule chakula"

Sikutaka kubisha Nika kaa chap

Akanipa chakula na yeye akakaa nakuanza kula.

Aloooh chakula kitamu bala

"Nimepika vizuri au"

"Ndio nikizuri"

Alitabasamu na kuendelea kula

Nilimaliza kula nikamshukuru kisha nikata kuosha vyombo akanizuia nakusema ataosha Dada wakazi

Kumbe kuna dada wa kazi alafu ukapika mwenyewe

Niliwaza hivyo

"Yeah nimepika mwenyewe coz sikutaka mke wangu ale chakula alichopika Mtu mwingine ikiwa ni siku yake ya kwanza kuja hapa

Mke wako miguu yako
Wait kwanza kajuaje kuwa nimewaza hivyo

Nina wasi wasi na huyu kiumbe usikute sio mtu

Wakati nawaza hivyo si akacheka

Mmmh nilipata wasi wasi juu yake usikute nimekaa hapa kumbe ananileta ninone ili aninywe supu

"Usiwaze Sana nenda kapumzike unatakiwa kuamka saa kumi na moja "

(Saa kumi na moja kwani naenda kupokea lindo)

Niliinuka na kumuaga Kisha nikaingia chumba nilichopewa

Nilifika na kujitupa kitandan nikakumbuka matukio ya siku ya leo Nikaona kuna haja ya kutoka humu ndani laa sivyo nitaliwa bure

Na staki kumsariti babe wangu nampenda sana Bosco wangu

Nilichukua sm nikawaza nitampataje
Nikapata wazo yes la kumtafuta Instagram

Lakin wazo hilo haliku fanikiwa kwani sikumpata

Nikaingia Facebook nako sikumpata

Ila nikakumbuka kuwa sikuwahi kum follow kwenye mtandao wowote na sikuwa najua anatumia jina gani siunajua watu wengine hutumia majina yasiyo yao

Niliishiwa pozi nikaamua nilale tu

Kesho yake asubuhi niliamka mapema nikajiandaa na kutoka

Nikamkuta Boss amekaa akinisubiri

"Good morning my queen (habari ya asubuhi malkia wangu)"..

Who is your queen (nani malkia wako)

"Shikamoo boss "

Niliamua kumzingua

"Usiku wako ulikuwaje"

"Ulikuwa vizuri"

"Okay good tunaweza kwenda"

Sikujibu nikatembea kwenda kwenye gari

Nilifika akanifungulia mlango nikaingia na safari ikaanza


Tulifika ofisini Kila mmoja akaenda ofisini kwake..

Nilifika na kukaa Kisha nikaanza kazi

Nikiwa biz n kazi zangu alikuja mdada na kunipa mziwa na korosho nikapokea maana alisema boss ndio kamuagiza

Mara ikaingia text kwenye sm yangu nikachukua na kangalia ilikuwa imetoka kwa boss

"Naenda kwenye Kikao hivyo sitokuwepo so kumbukumbu kula on time bye "

Sasa yeye kwenda kwenye kikao inanihusu nn mimi

Sikujibu nikakausha tu

Nilifanya kazi asubuhi sikushuka Bali niliagiza mchana nikaona ngoja ninyoshe miguu

Nikaenda mgahawani

Sasa nikamkuta yule cheusi

Alivyoniona tu akanifuata
.
"Nilikuwa na kusubiri kwa hamu mwana haramu wewe mbuzi wa albadili shetani wa mguu mmoja hivi unajiona we mzuri sana ee hadi Kuna kuchukua wanaume wa watu"

( Jamani kwani mm nimechukua mme wa nani Bosco au yupi)

"Samahani unaongea na mm au mwingine"

"No naongea na makalio yako,muone sura ilivyokujaa kama puto nakuonya kaa mbali na boss la sivyo nitakupoteza kinyago wewe"..

Aliongea na kunipiga kikuumbo
Jamani kwani huyo boss mm nimemchukua sangap

"We dada naomba tuheshimiane sawa kama ni huyo boss wako mimi Sina mahusiano nae kwaiyo usinitie nuksi " niliamua kuongea maana naweza kuwekwa kidole Cha m***nd kisa upole

"Nyoo eti Sina mahusiano nae ingekuwa huna mahusiano nae ungehamishwa kutoka huko shamba ukaletwa huku ""

Hiv huyu dada ni nani hasa hadi anijie juu maana kwa muonekano hawezi kuwa ametoka na boss

Nikaona hapa nikibishana na mtu nitaonekana mjinga bure nikageuza ili nirudi zangu ndani

Mara akanivuta nywele wee siunajua ukivutwa nywele zinavyouma nilipiga yowe hilo

Cha ajabu hakuna Alie kuja kunitetea

"Niache bhn unaniumiza". niliongea kwa sauti yenye maumivu

" Mimi naongea na wewe alafu unaondoka hivi unanijua mm ni nani mbwa wewe"

"Niache bhn nimeshakwambia mimi si toki nae"

Alinivuta nikahisi kama anataka kung'oa nywele
Na alionekana anapenda sana Sifa maana alikuwa anaongea kwa sauti

Aaawe hapa nikicheza kidogo tu nitanyofolewa nywele

Nilikuwa nimevaa sikonkido nikamkanyaga kwa nguvu akapiga kelele ya maumivu na kuniachia nikamuweka kofi moja takatifu
Shenzi yaani unataka kunizalilisha mbele za watu

Hakuamini kama nimempiga kofi akachukua glass na kutaka kunipiga nayo aise sijui huyu mwamba alitokea wapi alimsika mkono kwa nyuma huku akionesha kuwa na hasira ya juu

Aliposhikwa akafoka bila kujua nani kamshika "niachie nimnyoshe huyu malaya"

Mimi nimesimama hapo nimesha jisema kazi kwisha habari yake

Nikapange nguo zangu nirudi zangu kijijini tu

Aligeuka na kuona alie mshika uwii aliachia ile glass kwa mshtuko naona hakutegemea kumuona boss pale

Sio yeye tu hata mm sikutegemea maana nilitoka nje ya office na kwenda kwenye mgahawa wa kawaida Sana kwahadhi ya Boss asinge kaa hapo
Ila namuona huyu hapa

Alikuwa amekasirika akamuweka kofi moja Binti kaangukia kule akasogea na kunishika huku akianiuliza..

"Uko sawa mpenzi"

Mpenzi tena huyu hanitakii mema anataka waniue sio bure kwanzia lini nikawa mpenzi wake

Itaendelea


MY BOSS MY LOVE NO 29

"niko sawa"
Nilimjibu Kisha akanishika mkono na kwenda hadi ofisini kwake............

Tulifika akanikumbatia na kuniambia..

"I'm sorry umedhalilika kwaajili yangu"

"Ni sawa niko sawa kwaiyo usijali"

" No hauko sawa naona kabisa kwenye macho yako kuwa hauko sawa please naomba unisamehe nakuahidi haitojirudia tena "

"Bo"

kabla sijamaliza kuongea alinikatisha kwakukiss mwaka huu nitakissiwa mkapa niseme

Kwakwel nashindwa kuelewa kwa nn Kila ninapokuwa karibu na huyu mtu huwa nakuwa mtu wa tofauti nashindwa kuzuia hisia zangu kabisa sijui na nini

Tulikiss kwa mda kidogo Kisha akaniachia yaani hapo kwangu kinachoongea ni hisia tu akili aipo kabisa

Akinishika mkono na kunikalisha kwenye kiti Kisha nikasikia "ingia '

Akaingia yule dada akafika na kupiga magoti

Boss akamwambia aniombe msamaha basi kakanigeukua na kuniomba msamaha

Sikuwa na shida nikamsamehe baada ya hapo akainuka boss akasema

"Kakusanye Kila kilicho chako urudi nyumbani hauna kazi "

Heee nilishtuka sana

Masikini dada wawatu akapiga magoti akilia na kumuomba boss amsamehe

Nikiwa kama mwanadamu nikamuonea huruma nikaona nimuunge mkono

Ile nataka kuongea Boss akasema

"Kaa kimya Lilian ".


Mmmh nifunge mdomo wangu mie🫤 lisije kunikuta jambo

"Jeni ondoka ofisini kwangu now"

Masikini alisimama n kuondoka

Mimi nikamuangali kwa huruma nikitamani hta Kumtetea ila nikiwaza na mimi nisije kutolewa bora nifunge mdomo wangu

Mara sm yake ikaita akapokea

"Yes doctor anakuj sasavi"
Alikta na kuniangalia

Amka twende hospital

Kwni naumwa au

"LILIAN sipendi ubishi amka twende wote hospital"

"Lakini boss mm"

Alinishika mkono tukatok nje

Tuliingia kwenye gari na kuondoka

Baada ya kuingia kwenye gari tulienda nyumbani Badala ya hospital tukakuta doctor yuko nyumbani

Akaniangalia pale Kisha akasema niko sawa

Basi akaondoka boss akamuita mdada akaleta chakula tukala then akarudi kazin

Baada ya kuondoka na mm nikatoka ile nikatafute chumba

Niliingia mtaani nikatafuta madalali wakawa na waniambia hamna nyumba Kila mtu ninaenda anasema hamna nyumba

Nilizunguka Kila mahari lakin sikupata hata chumba cha 15000. Nikaona Bora nikalale lodge hata kama ni wiki ili nitafute taratibu

Nako naambiwa hamna vyumba

Nilizunguka haadi inafika saa mbili usiku sijapata Cha lodge Wala chumba

Ilikuwa ni kitu cha ajabu sana kwangu kweli dar es salaam hii ukose chumba au lodge hii Kali ya mwaka

Baada ya kuzunguka Sana nikaamua nirudi kwa boss uzuri sikubeba mabegi yangu maana ningekoma

Nilifika na kukuta boss anazunguka zunguka kama vile mtu mwenye wasi wasi sana alivyoniona tu alinikimbilia na kunikumbatia

"Ulikuwa wapi mke wangu unajua nilikuwa na wasi wasi kuwa utakuwa umekutwa naa kitu kibaya
"
(Huyu anapataje nguvu za kuniita mke wake )

"Boss niko sawa sorry nilisahau kukuaga ila nilienda kutafuta nyumba "

Nilivyoongea hivyo alijitoa kwenye kumbato na kuniangalia

"Ulikuwa umeenda wapi?'"

Heee mbona anauliza kwa ukali hivi

"Kutafuta Nyumba"

"Kwann hutaki kukaa na mm tena nikosa gani kubwa ambalo nimelifanya la kukufanya wewe kunichukia kiasi ambacho hutaki tena kukaa na mimi"

"No Boss sio kwamba nakuchukia ila siwez kuishi humu ndani"

"Kwann hutaki kuishi humu ndani "

"Boss "

"Please Lilian naomba usiondoke,umekuja kwenye maisha yangu kama nuru ukayamilika maisha yangu yaliyokuwa yametanda kiza why unataka kuniacha gizani tena, please kama Kuna kosa lolote nililofanya naomba unisamehe lakin usiniache please sitoweza kuishi bila wewe "

Aliongea huku akiwa amepiga magoti haraka nikataka kunuinua akasema no haamki hadi nitakapo kubari kubaki

"Boss tafadhali amka"

"Please Lilian naomba usiondoke I love you "

Nilibaki njia panda ukweli sikutaka kukaa humu ndani tena maana Nilijua kinaweza kutokea kitu ambacho hakutakiwa na siko tayar kumsariti Bosco wangu

"Fine sito ondoka but kwa sharti moja"

Aliposikia hivyo akaamka

"Sharti gani hilo "

"Usinikiss"

Niliongea huku nikiangalia chini

"Fine kama inakufanya uwe uncomfortable but naomba ujue kuwa nakupenda na sitoruhusu mtu yoyote kuingilia kati hata wewe mwenyewe na sijali kama una mtu au laa ninachojali ni nakupenda basi so wewe ni wangu utake usitake "

Sasa kaanza kwa kunibembeleza kaja kuishia kwenye amri tena

"Chakula kiko mezani good night "

Aliongea na kuondoka nikabaki namshangaa tu eti niwake nitake nisitake

Kwanzia lini mapenzi yaka lazimishwa

Kwakua nilikuwa na njaa nilienda mezani nikala na kutoa vyombo nikavisuza na kuingia chumbani

Sasa siku iliyokuwa inafuata ilikuwa ni jumamoss kwaiyo hakukuwa na kwenda kazini

Nikaingia chumban na kumtafuta Tuli

Nikamwambia nilikuwa natafuta nyumba na nimekosea

Akaniuliza kwani unataka kutoka hapo nikamwambia yeah siwez kukaa humu

Akaniuliza kwann

Nikamwambia Kila kitu kilichotokea

"Hivi Lilian kwann unakuwa katili juu ya hisia zako mwenyewe,kwann unataka kuishi na mtu usie mpenda wakati unaempenda yupo tena na yeye anakupenda"

"Batuli please Sina mapenzi yoyote na boss hiki kinachotokea sio sawa ndio maana nataka kuondoka"

"Hivi unafikili mapenzi ni kupenda tu, Lilian mapenzi ni hisia sio kupenda tu wewe hujawahi hata siku moja kumpenda Bosco mtu unaempenda ni huyo boss wako ndio maana huwezi kucontro hisia zako ukiwa nae hiyo ni ni sain kuwa unampenda"

"No Sina mapenzi yoyote na boss mimi nampenda sana Bosco na ndio mwanaume ambae moyo wangu umeamua kuwa nitaishi nae maisha yangu yote "

"Eee "

"Ndio ,najua najisikia hivi kwasababu sisi ni jinsia tofauti na kingine huenda kwasababu sijafanya mapenzi kwa miaka mingi"

"Acha ujinga hivi hivyo unavyojisikia ndivyo unavyojisikia ukiwa na Bosco jibu ni hapana usifananishe hisia za mapenzi ya kweli na hisia za kingono hivyo ni vitu viwili tofauti kabisa , shida yako wewe hutaki kukubari kwamba frank hayupo na hiyo ndio sababu inayokufanya uwe na Bosco sio kingine, ni kitu kibaya sana kuingia kwenye mahusiano na kwakumuona mtu mwingine ndani yake , unatakiwa kukubari na kuwa mapenzi yako na Frank yameshakufa toka siku aliyokufa na ndio maana hata yeye aliomba kuwa anatamani upate mtu mwingine atakae kupenda na sio upate yeye ndani ya mtu mwingine

Yaani sijui hata niongee neno gani ili unielewe natamani hata ningekuwa karibu nikakuweka makofi labda ungeamka

Kwanza hata huyo Bosco mwenyewe hakupendi uko kwake kama last option tu kwasababu haiingii akilini mtu kukuita jina la mtu mwingine zaidi ya mara mbili alafu uka kaa kimya hembu jaribu kuliweka hili kwa upande wako unawezaje kuitwa Judith alafu ukukaa kimya bila kuuliza huoni kama ni ajabu

LILIAN angalia sana mdogo wangu usipoangalia utakuja kulia maisha yako yote

Hata siku moja usije kuruhusu mapito yako kuharibu future yako

Past is past usiruhusu kamwe Acha inabaki story na kama unaona Kuna lakujifunza lichukue lakini usiyape nafasi ya kuharibu hatima yako

Embu ngoja niishie hapa maana nitaongea mengi lakin bado nitarudia pale pale humpendi Bosco jipe nasafi nyingine

Achia mapito yako Anza upya
Utakaa gizani hata lini

Natamani ungeingia ndani ya moyo wangu ukaona jinsi ninavyougua kutamani kuona ukiishi maisha yenye furaha

Na sisemi haya yote kwasababu na mchukia Bosco no mimi simchukii mtu ila naongea kile kilichoko sawa

Sasa uamzi ni wako kubari kuachia uanze upya au uendelee kushikilia

Usiku mwema "


Alimaliza kuongea na kukata sm

Nilibakia nikifikilia sana Yale maneno
Moyo uliniambia hivi akili inasema vile mwishoni nikapitiwa na usingizi

Asubuhi niliamka baada ya kugongewa mlango

Niliamka nikapiga mswaki na kwenda seblen nikakuta Bosco ananisubiri

"Za asubuhi Boss"

"Ninzur wewe je"

"Nzuri"

"Okay chai iko tayar ,alafu naitwa DIEGO sio Boss"

Kumbe alisajili lain yangu Kwa jina lake alafu nilikuwa sijui kama anaitwa hivyo

Hii ni ajabu ee yaani unafanya kazi alafu hujui boss wako anaitwa nani

Sikumtuikia nilisogea mezani tukanywa chai Kisha akasema atakuwa na kazi so hatoshinda nyumbani

Nikaona bora maana sikuwa nataka hata kumuona ona

Baada ya chai nikainuka ili kwenda chumbani akanishika mkono

'"naomba jioni tutoke dinner"

Nikajibu "okay"

Alitabasamu na kuniachia mkono nikaondoka

Niliingia chumbani huku nikisubiri aondoke ili nikaogelee.

Siunajua napenda maji Kama samaki basi alivyoondoka mimi huyoo kwenye maji

Siku nzima nilikuwa naogolea yaani nikichoka napimzika alafu narudi tena full rahaa tu

Alirudi jioni nikajiandaa Kisha nikatoka

Jamani jamani duniani kuna mahandsome balaa

Mr CEO boss mwenyewe alikuwa ameshajiandaa yuko zake seblen ametoka kapendeza mwenyewe yuko ile mbaya. Sasa sini kasahau kama nilikuwa nashuka ngazi sangap nisitereze uwii nilikula huo mwereka.

Nashukuru Mungu sokung'oa meno Mr CEO akaja mbio na kuninyenyua

"Are you okay '" kwani nilimjibu basi akili yangu ilikuwa iko bize kuangalia uumbaji wa Mungu naona akahisi nitakuwa nimepata mshtuko akanibeba hadi kwenye sofa sasa ile ananilaza bwana siaka nishika mguu kuangalia kama nimeumia akanivua kiatu mimi hapo nawaza mengine kabisa akawa anauzungusha mguu Kama vile ana unaunyoosha

Nikamshika mkono akanianga naona aliona vile nimelegea jamaa akajiongeza akaona kumbe natoa huduma ambayo sio akainuka na kunisogelea karibu ziadi

Kilichotokea hapo sijui nilikuja tu kushtuka asubuhi nikiwa kitandan huku Sina hata nguo moja hata sijui nilibebwa sangap

Oo kulikuwa na chai pembeni kwenye meza ila yeye hakuwepo sini kaamka heee naona nimevaa Pete kidoleni kitu kina Waka hatari

Nilibaki mdomo wazi hata sijui nini kikanikuta nikajikuta naanza kulia

Nikaangalia pembeni nikaona note

"Hello mrembo wangu mzuri natumai umeamka salama asante kwa penzi zito ulilonipatia usiku ulikuwa ni usiku wa pekee sana kwangu thanks my love, nimetoka mara moja make sure unakunywa chai mara tu utakapo amka I love you "

Niulize niliendalea kulia au nilifanya nn nilicheka. Kama kajinga vile

Nilikunywa chai Kisha nikatandika kitandan na kwenda kuoga

Mida ya mchana alirudi nyumbani mda huo nimejificha chumbani nilikuwa naona aibu kumuangalia

Aligonga akitaka nifungue ila nikauchuna

Mwishoni nikasikia anauliza kama Kuna kitu kimenikuta eee nikaona embu niache ujinga kwani naona aibu ya nn kwani ni mara yangu yakwanza kusex jibu ni no basi nikafungua

Ile nafungua tu mtu huyu hapa kanivamia na kunikumbatia

Itaendelea


MY BOSS MY LOVE 30 FINAL

"nilikuwa na was wasi kuwa utakuwa hauko sawa"

Aliongea huku ameshika uso wangu kama kamdoli

Niseme nini sasa nikawa najiwazia tu si unikiss basi kha hadi niombe

Alafu huyu jamaa atakuwa na nguvu za kusoma mawazo ya mtu sio bure
Maana nilivyowaza hivyo alicheka na kunikiss

Vile nilikuwa na njaa ya miaka mingi nikajikuta namfungua vifungo vya shati aliniangalia na kutabasamu Kisha akafunga mlango tukapata moja mbili tatu pale .

We siunajua tena penzi likiwa jipya mnakuwa mnatamani hata mtafunane tu yaani Kila mda unakuwa na hamu na mwenzio

Basi baada ya mechi kali alifuata chakula jikoni akaleta tukapiga msosi saiyo sikumbuki hata kama Kuna mtu anaitwa Bosco huu siutakuwa umalaya yaani mara hii simkumbuki hata jina kwanza sijui hata kama niliwahi kuonana nae

Bwana bwana siku hiyo ilikuwa ni mechi za kirafiki tu ndo zilikuwa zikichezwa

Kesho yake asubuhi kabla ya kwenda Job nikampa chakula elewa neno chakula
Akala bwana aliposhiba hao tukajiandaa na kwenda kazini sasa tukifika kazin anakuwa boss wangu tukirudi nyumbani anakuwa mpenzi wangu yaani ni

MY BOSS alafu ni MY LOVE

Kituko kinakuja siunajua tunakuwaga na vikao e basi yaani tukikaa kwenye kikao unakuta ameweka sura ya ukauzu balaa sasa mimi nikimuangalia najikuta napata picha tukidinyana au akiwa hajavaa basi naishia kubana kicheko tu wanamuona kauzu mwenyewe kumbe mtu flan hivi

Basi bwana zikapita wiki mbili siku hiyo akanambia anataka kunioa so nimpe taratibu zote afuate ili amiliki kabisa

Nikaona hizi habari nataka niwape watu wangu wanguvu nikiwa nawaona kwa macho ili nione vile watakavyofurahi maana wamelia sana na mimi kipindi ambacho nilikuwa nikilia watu kama Hawa ni muhimu sana kwenye maisha yetu

Ninakuombea na wewe unesoma Mungu akupe watu wa kusimama na wewe katika nyakati zote

Basi nikaomba weekend niende nyumbani akakubari

Nikampigia Tuli wangu nimwambia twende Tanga akakubari

Hao tukasepa zetu

Tulifika nyumbani mama nae alikuwepo tukapika tukala na story za hapa na pale alafu nikawaambia sasa kuwa nataka kuolewa

Weee mama alifurahi jamani alilia kwafuraha akapiga magoti na kumshukuru Mungu

Tuli alinipongeza kwa kuchukua maamuzi mazuri akaniwaoo pale bibi pia akanipongeza

Furaha ikatawala pale mama akasema tuombe basi tukapiga magoti akaomba kama mnavyomjua mama yangu akianza kuomba anaomba masaa aliomba akanena ikabidi tumache aendelee

Weekend ilipoisha nikarudi dar

Sasa nikiwa kazini nikatumiwa picha na Paulo (chaumbea) zilikuwa picha za Bosco zikionesha wanafunga ndoa na mzazi mwenzie yuleee Swaum

Nyie nilimshukuru Sana Mungu nikasema kama asinge mleta My Boss saizi mgekuwa mnanipepea

Basi siku zikaenda akatoa mahari tukafunga ndoa

Kwenye ndoa yetu nilimualika Paulo mda wa zawadi akaja kuninon'oneza sikioni

"Aisee mpe kiuno mganisho bila kusahau kumfinyia kwa ndani ili tupate magorofa "

Alivyosema hivyo nikamfinya mda huo babe yuko bz na wageni wengine alivyoona tuana nong'onezana akanikata hilo jicho chap nikarudi Sehemu yangu

Baada ya ndoa kufungwa tukaanza kuishi rasmi kama wanandoa

Kwakwel namshukuru sana Mungu kwakunipa mume Bora mwenye upendo usio na mshariti

Baada ya miezi minne nilipata ujauzito nikajifungua baby boy anafanana na baba yake huyo balaa yaani utafikili aliingia tumboni mwangu alafu akatoka ,

Maisha yaliendelea tukapata mtoto mwingine nae ni boy

Huku Bado nikiendalea kufanya kazi mtindo ndio ule ule
Akiwa kazini ni
.MY BOSS akiwa nyumbani ni MY LOVE

Rafiki yang kipenzi BATULI alifunga ndoa na mpenzi wake wakajaliwa mtoto wakike kazuri kwnye

Sijamsahau Frank ila sikuhizi uchungu umeisha kabisa yaani imebaki na makumbuka kama mtu aliye kuwa muhimu kwangu

Kila mwaka kwenye birthday yake huwa naenda nafanya usafi kwenye kaburi lake then namuombea Misa kanisani na kumtolea sadaka ili kama Kuna msamaha wawafu basi Mungu amsamehe frank wangu

R I.P FRANK

Na huu ndio mwisho wa simulizi yangu ya my MY BOSS MY LOVE
Oooh jmn n nzuri balaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom