Huyu jamaa vipi jamani?! Nimefuatilia kipindi cha DK45 ITV na leo mgeni ni N/Waziri wa Muungano na Mazingira na mada ilikua ni Mazingira.
Huyu Sam Mahela, kama kawaida yake kuingilia mzungumzaji wakati anatiririka vizuri kwenye mada husika. Anageuka kuwa mzungumzaji Mkuu, anatoa maoni yake Mfano...."Mimi/sisi waandishi wa habari tumefanya tafiti na ni kweli/sio kweli kwamba Kuna uharibifu wa Mazingira".....sasa kama ulikua unajua ukweli/uongo wa jambo ya nini kumwaalika mgeni studioni wakati ulikua na misimamo yako kwenye topic husika?
Mfano alipokua akiagana na N/W huyo, akawa anamsisitiza"fanyakazi, umesikia, fanyakazii, umepewa kazi ufanye, sawa...maana hata mm hapa ITV napiga kazi".....hapa ni kiherehere tu cha huyu maana sio wajibu wake kumweleza hayo.
Nimekuwa nikifuatilia kipindi hiki Lakini watu wengi wanakereka sana na huyu jamaa.....atulie, atoe nafasi ya mgeni husika kusema na baada ya hapo maswali. Mwanzilishi wa kipindi hiki na Buholela walikua wazuri sana sio kama huyu kijana.
Mkuu uko sahihi.
Huyu jamaa anahiyo tabia mbaya ya kukatiza wageni wake wanapookuwa wanashusha points.
Nakumbuka siku alipokuwa na Mch. Msigwa. Sikupfurahia kabisa tabia yake hiyo mbaya. N hasa mtu anapotoa maoniyanayotofautia na serikali au kuikososa serikali.
Ajirekebishe.