Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Ha ha ha ha ha aaaaaaaaaaaaaaaa. mzazi anapotaka kucontrol maisha ya mkewe. huyo mama hafai kuwa kwenye uongozi. anaishi kwa hisia tu
 
Nina mashaka sana na habari hii, ila kama ni kweli basi nina kila sababu za kumuona Kibanda kuwa aliona mbali zaidi yetu.
 
Zitto needs coaching.

Hawa marafiki zake yaani sijui niwaweke kundi gani, Naombeni elimu za hawa marafiki zake wa karibu kisiasa, yaani kuropoka hovyo hovyo tu magazetini, habari za nyumbani zinavujishwa hovyohovyo. The look like some wahuni wasio na strategies wale vision!

Sorry, lakini baada ya kusoma sana sehemu nyingi na kuulizia around nakubaliana na Absalom Kibanda na pia kwa sasa nipo na Dr Slaa, huyu David Kafulila HAFAI na marafiki wa Zitto kisiasa ni WATOTO.

Mkuu FP nilikuwa naichukia sana signature ya Masatu lakini naona taratiiiibu inaanza kupata nafasi katima Mtima wangu! Si watoto bali wanaamini katika Strategies za TUMPE WAKATI MGUMU ASHINDWE KUONGOZA, NI UPUUZI MTUPU
 
Kama habari hii ina chembe za Ukweli then Kibanda ni Jiwe walilolikataa Waashi
 
Bundi ameanza kunyemelea familia ya Zitto Kabwe. Mama Mzazi wa Zitto Kabwe, Shida Salum ameitisha kikao juzi kujadili mustakabali wa familia. Mtoa habari wetu ambaye ni mmoja wa wanafamilia aliyehudhuria kikao hicho anaeleza kuwa kikao hicho kilihudhuriwa na wanafamilia wa karibu akiwemo kaka wa Zitto anayejulikana kwa jina moja la Salum. Kikao hicho cha kifamilia kilijadili mustakabali wa kisiasa wa Zitto Kabwe na mambo yanayojitikeza ya chama chao cha CHADEMA. Baadhi ya watu wa karibu na familia walioalikwa kwenye kikao hicho ni pamoja na David Kafulila, ambaye Zitto amemtangaza hivi karibuni kuwa kijana mwenye akili anayemuandaa kuwa mbunge wa jimbo la jirani yake la Kigoma Kaskazini.

Kikao hicho cha kifamilia kimeazimia kuwa Zitto ajiuzulu na nafasi ya unaibu Katibu Mkuu CHADEMA ili asipoteze maisha kama Chacha Wangwe. Mama Mzazi wa Zitto Kabwe, ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA amethibitisha familia kuamua Zitto ajiondoe kwa ajili ya kulinda maisha yake. Mama huyo amenukuliwa na Gazeti la RAI akieleza kwamba familia inamtegemea sana Zitto na ameisadia kwa mengi hivyo wamemuandikia barua akiwa ujerumani kumweleza msimamo wao wa kutaka ajitoe.

Kikao hicho kilijadili misaada ya magari ambayo Zitto ametoa kwa baadhi ya vijana wanasiasa ndani ya CHADEMA kwa ajili ya kuwasaidia washinde katika majimbo yao ya uchaguzi. Mmoja kati ya watu hao anatajwa kuwa ni Msafiri Mtemelwa ambaye wakati wa uchaguzi wa ndani ya CHADEMA alikuwa Kampeni Meneja wa Zitto Kabwe kwenye kugombea nafasi ya uenyekiti na hata katika kupanga safu za viongozi wa ngazi zingine ndani ya CHADEMA. Familia ilielezwa kwamba hivi karibuni Msafiri alionekana akiongea na Katibu Mkuu Dr Slaa ofisini. Familia ikaelezwa kuwa alipigiwa simu hivi karibuni na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe. Kutokana na mambo hayo, kikao hicho kilianza kumtilia mashaka kuwa amemgeuka Zitto Kabwe.

Mtoa habari wetu anafafanua kuwa David Kafulila alikieleza kikao kuwa Msafiri Mtemelwa alichangia uteuzi wake kama Afisa utenguliwe kwa kuwa alikuwa mjumbe wa Kikao cha Sekretariati kilichokaa chini ya uenyekiti wa Dr Slaa lakini hakumtetea. Kafulila aliendelea zaidi kukieleza kikao kuwa badala ya kupingana na wajumbe wengine wa sekretariati ili kumnusuru, Msafiri alitoa hoja kwamba atolewe nje ya kikao baada ya kujieleza kwa masaa manne ili maamuzi yaweze kufikiwa. Hivyo, wanafamilia walichukua uamuzi wa kumnyang'anya gari aliyopewa na Zitto Kabwe aina ya Prado. Uamuzi huu umeshatekelezwa kwa Msafiri Mtemelwa kunyang'anywa gari hiyo.


Mtoa habari wetu ameeleza kwamba maamuzi hayo na mambo mengine ya zamani yanaelekea kuigawa familia katika makundi mawili. Kundi moja likiwa ni lile linalolaumu urafiki na Zitto na baadhi ya marafiki wapya ambao wanaelekea kumweka mtoto wao mbali na viongozi wa chama chake na marafiki zake wa zamani na kumzushia migogoro yenye kutishia mustakabali wake wa kisiasa. Kundi lingine ni lile linaloamini kwamba viongozi wote wa kitaifa wa CHADEMA na marafiki wa zamani wanamchukia Zitto hivyo mustakabali wake wa kisiasa utategemea kuwashambulia na kuwamaliza viongozi hao na watu wanaotofautiana na Zitto; kundi hili linamsimamo kwamba kama mpango huu hautawezekana basi ni vizuri Zitto aache siasa kunusuru maisha yake.

Juzi gazeti la Alasiri limeandika ukurasa wa mbele habari ya kwamba Zitto ametangaza tena kuacha kugombea ubunge 2010 na badala yake anataka kuwa Mwalimu wa chuo Kikuu. Habari hiyo imefuatiwa na habari ya jana katika Gazeti la Rai ikimnukuu Mama Zitto akieleza kwamba mwanae ni msomi, afadhali afanye kazi zingine ili aendelee kuisaidia familia badala ya kubaki katika chama na kupoteza maisha yake.

Mwanafamilia huyo anaendelea kudodosa kuwa maadui wa Zitto wanatajwa kuwa ni Freeman Mbowe, Dr Slaa na wakurugenzi wote wa makao makuu ya CHADEMA isipokuwa Msafiri Mtemelwa. Katika orodha hiyo anatajwa pia mfanyabiashara mmoja na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari. Pia wabunge wote wa CHADEMA isipokuwa wawili. Gazeti la jana la Rai limeeleza pia katika kundi la wabunge anayeongoza kwa uadui na Zitto ni Halima Mdee ambaye anatajwa kuwa amewasilisha nyaraka ya tuhumu 22 dhidi ya Zitto Kabwe kwa chama hicho ikiwemo tuhuma zinazohusiana na masuala ya kampuni ya Dowans. Kutajwa kwa jina la Halima Mdee kumethibitisha maelezo ambayo Msaidizi wa Karibu wa Zitto Kabwe, Omar Ilyas aliwahi kuyatoa katika Mtandao wa Jamii Forums, akieleza kwamba yupo mbunge mmoja kijana ambaye alikuwa karibu na Zitto ambaye amemgeuka na kumtuhumu kwa mambo mbalimbali. Omar amekuwa akihusisha mbunge huyo, na jina la Mwafrika katika mtandao huo.

..........ndiyohiyo

Kwa kweli hata mimi niliposoma habari ya gazeti la wiki hii la Rai ambayo limeeleza mambo haya nimebaki mdomo wazi.

serayamajimbo
 
Hivi Tanzania Mpaka lini???
CCM Tumewachoka jamani.
CHADEMA mlishaanza kuonesha mwanga kidogo. nilikua nategemea 2010, Wabunge waupinzani wangeongezeka Bungeni. Nimeanza kupata wasiwasi na mwenendo wa hiki chama tangu Zitto alipotangaza azma yake ya kugombea uenyekiti.
Jamani Tuombe Mungu hawa ''wapiganaji'' ndani ya sisiem waanzishe walau chama chao cha siasa. May be they might take us to another level.
 
Zitto needs coaching.

Hawa marafiki zake yaani sijui niwaweke kundi gani, Naombeni elimu za hawa marafiki zake wa karibu kisiasa, yaani kuropoka hovyo hovyo tu magazetini, habari za nyumbani zinavujishwa hovyohovyo. The look like some wahuni wasio na strategies wale vision!

Sorry, lakini baada ya kusoma sana sehemu nyingi na kuulizia around nakubaliana na Absalom Kibanda na pia kwa sasa nipo na Dr Slaa, huyu David Kafulila HAFAI na marafiki wa Zitto kisiasa ni WATOTO.

Mkuu FP naungana nawe katika hili; at this point of time Mh. Zitto lazima awe makini sana, hii triangle inayomzunguka -- Marafiki, Siasa, Familia -- yaweza mpoteza mwelekeo, narudia tena he has to be extremely carefully coz any of the three components making that triangle yaweza kuwa na agenda ya siri aidha kwa kudhamiria au kwa kutokujua.

Ninaingiwa wasiwasi na uwezo wa kiupeo wa familia ya Zitto (samahani katika hili), hao ndugu wa familia zake wako-well exposed kweli?? wamesoma?? vinginevyo wanahitaji kuwa na busara ya hali ya juu katika kumshauri mtoto wao vinginevyo watampoteza ... na ninaanza kuhisi pia ndio maana mara nyingi Zitto amekuwa haeleweki na pia akiwachanganya wapenzi na wananchama wake kwa misimamo ya ajabu kabisa ... kosa laweza kuwa ni kuchanganywa na hiyo mihimili mitatu isiyo rasmi.

Ushauri mbaya wa Familia plus Marafiki na kudhorota kwa mahusiano na viongozi wenzake wa kamati kuu kwaweza kumuweka huyu kijana katika nafasi ngumu sana kwa ustawi wake kisiasa. Siamini kama Zitto anajua kila kitu katika siasa na fani mbalimbali hapa duniani; na kama ni hivyo, inakuwa mbaya zaidi kama washauri na wapambe wake anaowasikiliza wakiwa hawajasoma na upeo wao ukiwa mdogo sana.

Zitto ndugu yangu, you ought be very smart and careful on your next moves, coz waswahili walishasema "kikulacho kinguoni mwako!!"

Kuwa mvumilivu, na busara itawale mbele yako!
 
vyama vya siasa vya tz bado!! watu wenyewe wachache,wanagombania nini? au vihela na vijisent nini!! sasa tutaendelea na chama chetu kile basi-maana hawachelewi kufuta chama kwa mpango huu!!
Bado nini?
Huu ni uzembe na uoga wako katika siasa.
Siku zote unadhani siasa ni lele mama kwa sababu mlizoea siasa za kibabe za ki sisi m.
 
Akufukuzaye hakwambii toka utajionea mambo yanvyokwenda! Hawa weshajua chama ni cha kina nani na kina malengo gani! Na wameshajua kwamba kitawafaa ama hakitawafaa! Embu tusubiri tuone kile cha wakulima
 
ee kama ni hivo kwa heri
Dr Slaa kaumiza wengi hivyo ana "maadui" wengi pia. Katika ile orodha yake ya MwembeYanga hakuna hata mmoja aliyejinasua na hawa wana ndugu, jamaa, rafiki, wapenzi, mashabiki, nyumbandogo,.....
 
Viongozi wa CHADEMA,
Wawekeni kando WAZAZI, WAKWE zenu. Hawa watakapoanza kuchambuliwa humu na kwenye majukwaa mengine chama chenu na ninyi wenyewe hamtabaki salama na amani itatoweka.
 
Unadhani vijana wetu wa chadema wanagombana au kutofautiana?
HAaaaaa! wanapiga miayo ya uchovu wa viako tu!!

Chadema Imara na ikulu yetu 2010.
 
Mkuu FP naungana nawe katika hili; at this point of time Mh. Zitto lazima awe makini sana, hii triangle inayomzunguka -- Marafiki, Siasa, Familia -- yaweza mpoteza mwelekeo, narudia tena he has to be extremely carefully coz any of the three components making that triangle yaweza kuwa na agenda ya siri aidha kwa kudhamiria au kwa kutokujua.

Ninaingiwa wasiwasi na uwezo wa kiupeo wa familia ya Zitto (samahani katika hili), hao ndugu wa familia zake wako-well exposed kweli?? wamesoma?? vinginevyo wanahitaji kuwa na busara ya hali ya juu katika kumshauri mtoto wao vinginevyo watampoteza ... na ninaanza kuhisi pia ndio maana mara nyingi Zitto amekuwa haeleweki na pia akiwachanganya wapenzi na wananchama wake kwa misimamo ya ajabu kabisa ... kosa laweza kuwa ni kuchanganywa na hiyo mihimili mitatu isiyo rasmi.

Ushauri mbaya wa Familia plus Marafiki na kudhorota kwa mahusiano na viongozi wenzake wa kamati kuu kwaweza kumuweka huyu kijana katika nafasi ngumu sana kwa ustawi wake kisiasa. Siamini kama Zitto anajua kila kitu katika siasa na fani mbalimbali hapa duniani; na kama ni hivyo, inakuwa mbaya zaidi kama washauri na wapambe wake anaowasikiliza wakiwa hawajasoma na upeo wao ukiwa mdogo sana.

Zitto ndugu yangu, you ought be very smart and careful on your next moves, coz waswahili walishasema "kikulacho kinguoni mwako!!"

Kuwa mvumilivu, na busara itawale mbele yako!

Personally nitatafuta email ya Zitto nimshauri mambo kadhaa, sitaki kumshambulia hapa mpaka nimsikilize kwasababu naamini ni mwanasiasa mzuri akijirekebisha. Kuna namna ya kuelezea hisia zako bila ku attack mtu wala viongozi wenzako. Timu yake sio nzuri ...
 
Viongozi wa CHADEMA,
Wawekeni kando WAZAZI, WAKWE zenu. Hawa watakapoanza kuchambuliwa humu na kwenye majukwaa mengine chama chenu na ninyi wenyewe hamtabaki salama na amani itatoweka.

Point zako huaga nazikubali, lakini hapa umeteleza kidogo. Katiba ya Nchi inaeleza kila mtu ana haki ya kugombea, kutoa mawazo n.k. ukiwa tiyari umefikisha 18yrs. Hawa wazazi wako sawa tu kufanya maamuzi yao isipokuwa tu haya maamuzi wanayatolea wapi na kushirikisha nani! Ebu fikiria Mh. Zitto kwenye CHADEMA ni Dhahabu kwa hiyo wanaotafuta kumtumia hawapo mbali!!! na usikute wakapitia kwa wazazi wake!!! kumbuka familia ya Wangwe ulivyotumiwa kwenye Msiba wa Wangwe.

Pia unaweza kutumia uzoefu wako bado, siasa nikama inaambukiza kizazi na kizazi, chukulia familia ya Bush, Clinton, huyu Odinga, Karume, Mwinyi n.k. Mimi sioni cha hajabu kwanini kuishutumu familia ya Zitto kuingia kwenye siasa, isipokuwa tu pale inapoanza kuhujumu Chama.
 
Jamani hayo ni mambo madogo sana kujadili kwa muda mrefu. Wansiasa wote ni wadogo hata zito si mwanasiasa wa kuitwa mkubwa ndio maana visifa vidodovidogo wanavyopewa na vyombo vya habari vina wachanganya wote.
 
Point zako huaga nazikubali, lakini hapa umeteleza kidogo. Katiba ya Nchi inaeleza kila mtu ana haki ya kugombea, kutoa mawazo n.k. ukiwa tiyari umefikisha 18yrs. Hawa wazazi wako sawa tu kufanya maamuzi yao isipokuwa tu haya maamuzi wanayatolea wapi na kushirikisha nani! Ebu fikiria Mh. Zitto kwenye CHADEMA ni Dhahabu kwa hiyo wanaotafuta kumtumia hawapo mbali!!! na usikute wakapitia kwa wazazi wake!!! kumbuka familia ya Wangwe ulivyotumiwa kwenye Msiba wa Wangwe.

Pia unaweza kutumia uzoefu wako bado, siasa nikama inaambukiza kizazi na kizazi, chukulia familia ya Bush, Clinton, huyu Odinga, Karume, Mwinyi n.k. Mimi sioni cha hajabu kwanini kuishutumu familia ya Zitto kuingia kwenye siasa, isipokuwa tu pale inapoanza kuhujumu Chama.
Haya ya Katiba na uhuru wake nayafahamu. Siasa za Nchi hii ni kuchafua na kuchafuana na hasa wanasiasa wetu wanapoishiwa HOJA. Angalia ya Malecela na Mke wake mama Kilango!
 
Haya ya Katiba na uhuru wake nayafahamu. Siasa za Nchi hii ni kuchafua na kuchafuana na hasa wanasiasa wetu wanapoishiwa HOJA. Angalia ya Malecela na Mke wake mama Kilango!

Ukisha amua kuingia kwenye siasa hautakiwi kuogopa, yote hayo watakupaka hiyo ndo siri ya Siasa. Kwa huyo Malecela amezoea kupaka madongo wenzio hivyo, unadhani anashtuka huyo.

Cha kufahamu CHADEMA wanawindwa kila kona wasichanue.
 
...

Kutajwa kwa jina la Halima Mdee kumethibitisha maelezo ambayo Msaidizi wa Karibu wa Zitto Kabwe, Omar Ilyas aliwahi kuyatoa katika Mtandao wa Jamii Forums, akieleza kwamba yupo mbunge mmoja kijana ambaye alikuwa karibu na Zitto ambaye amemgeuka na kumtuhumu kwa mambo mbalimbali. Omar amekuwa akihusisha mbunge huyo, na jina la Mwafrika katika mtandao huo.

..........ndiyohiyo

Na kisha mafisadi waende wamkolimbe Dada Halima buree kwa madai yasiyo na msingi kama haya. Zitto, Omar, Msafiri, Ndanda, Kafulila na wengineo wote kambi ya Zitto.

Mchawi wenu sio Halima Mdee, Mchawi wenu ni matendo yenu wenyewe na maneno yenu mnayoyatoa bila kuyapima. Eleweni kuwa Tanzania (na chadema in this case), ni kubwa zaidi kuliko Zitto Kabwe (bila kujali umaarufu ambao nyie mnadhani kuwa Zitto anao).

Kinachowatokea leo hakikuanza leo, kilianza mara tu Zitto alipokubali kuingia kwenye tume/kamati ya madini ya Kikwete na hivyo kuondoa nafasi ya kuundwa kwa tume huru ya bunge kuchunguza barick na buzwagi.

Msimsingizie Halima kwa kile asichoweza na mkaja kumtia matatani bure. Muulizeni Max atawaambia ni nani anayejiita mwafrika hapa JF (kama akipenda) maana mimi nayeye tunafahamiana vyema. Vinginevyo - mnakoelekea, haitakuwa rahisi kwenu kurudi na kujenga chadema mnayodai kuwa mnaipenda kwa moyo wote.
 
Back
Top Bottom