Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Jasusi,
Pamoja na yote hayo nyie wanachama (wajumbe) mnayajua yaliyotokea hadi viongozi hawa kunyang'anywa maradaka yao? kama hamjui huoni kuna umuhimu wa nyie kuelezwa ikiwa nyie dio mlowachagua watu hao..

Mkandara,

Maofisa hawachaguliwi, wanateuliwa. Mamlaka iliyowaajiri ndiyo hiyo imewatengua. Ni tofauti na viongozi wa kuchaguliwa ambao wanachama ni muhimu waelezwe wanapoondolewa

Asha
 
Mkandara,

Maofisa hawachaguliwi, wanateuliwa. Mamlaka iliyowaajiri ndiyo hiyo imewatengua. Ni tofauti na viongozi wa kuchaguliwa ambao wanachama ni muhimu waelezwe wanapoondolewa

Asha
Bi.Asha nakusoma sana bibie ila nachojaribu kusema hapa ni UWAZI.. tunahitaji kuweka uwazi pale ambapo panatakiwa hata kama kuna machungu.
Binafsi huyo Kafulila, atakuwa kafulia kweli ikiwa tutafahamishwa madhambi yake ili kesho mtu mwingine asije yarudia lakini pasipo kuyajua inatupa picha tofauti na mawazo mengi yanajengwa kiasi kwamba hata hizi tuhuma hazikutakiwa kuwepo iwapo tu utaratibu huu ungekuwa wazi na huru.

Binafsi nazungumza hivi kwa kuchelea zaidi jinsi Wadanganyika tulivyo, kesho huyo Kafuylila akiamua kuondoa Chadema anaweza kukipata chama hata kisitamanike kwa sababu tu chama kiliamua kuficha ukweli kwa maufaa ya huyo Kafulila au mtu mwingine...
Trust me hoja zangu, hujaribu kufikiria kama mtu aliyeko nje ya chama (out of the box).. na ndipo tunapo tofautiana kimawazo.
 
Bi.Asha nakusoma sana bibie ila nachojaribu kusema hapa ni UWAZI.. tunahitaji kuweka uwazi pale ambapo panatakiwa hata kama kuna machungu.
Binafsi huyo Kafulila, atakuwa kafulia kweli ikiwa tutafahamishwa madhambi yake ili kesho mtu mwingine asije yarudia lakini pasipo kuyajua inatupa picha tofauti na mawazo mengi yanajengwa kiasi kwamba hata hizi tuhuma hazikutakiwa kuwepo iwapo tu utaratibu huu ungekuwa wazi na huru.

Binafsi nazungumza hivi kwa kuchelea zaidi jinsi Wadanganyika tulivyo, kesho huyo Kafuylila akiamua kuondoa Chadema anaweza kukipata chama hata kisitamanike kwa sababu tu chama kiliamua kuficha ukweli kwa maufaa ya huyo Kafulila au mtu mwingine...
Trust me hoja zangu, hujaribu kufikiria kama mtu aliyeko nje ya chama (out of the box).. na ndipo tunapo tofautiana kimawazo.


Babaa, mbona Dr Slaa ameeleza kuwa ametengua uteuzi wao kutokana na wao kukiuka maadili na utendaji kutokana na matamashi waliyoyatoa kwenye vyombo vya habari?

Slaa amesema aliwaita wamejieleza kwa masaa manne na baadaye akaamua kuchukua hatua.

Au haijatosha? Nadhani kwa kuwa Kafulila alisema amepewa barua ni vizuri akatueleza nini kimeandikwa kwenye barua ambayo amepewa.

Lakini kumwambia Slaa aseme ni kulikuza tu hili jambo bila sababu, hawa na maofisa tu mwajiri wao aliyewateua ametengua utuezi wao.

Asha
 
Babaa, mbona Dr Slaa ameeleza kuwa ametengua uteuzi wao kutokana na wao kukiuka maadili na utendaji kutokana na matamashi waliyoyatoa kwenye vyombo vya habari?

Slaa amesema aliwaita wamejieleza kwa masaa manne na baadaye akaamua kuchukua hatua.

Au haijatosha? Nadhani kwa kuwa Kafulila alisema amepewa barua ni vizuri akatueleza nini kimeandikwa kwenye barua ambayo amepewa.

Lakini kumwambia Slaa aseme ni kulikuza tu hili jambo bila sababu, hawa na maofisa tu mwajiri wao aliyewateua ametengua utuezi wao.

Asha
Shukran sana kwa kunifumbua macho sikuliona hilo.. haya huyu Jamaa alichokisema ni kipi haswa! maanake sikumsoma...au nacho ni siri!
 
Babaa, mbona Dr Slaa ameeleza kuwa ametengua uteuzi wao kutokana na wao kukiuka maadili na utendaji kutokana na matamashi waliyoyatoa kwenye vyombo vya habari?
Asha

Asha,
  1. Matamshi gani hayo waliyotoa?
  2. Je ina maana kila anayetoa matamshi tofauti na Mwenyekiti/Katibu inabidi afukuzwe uongozi/uachama?
  3. Walipewa onyo kabla au adhabu yao haina onyo?
Something is definitely wrong here. Zitto tungeomba na wewe utupe maoni yako maana hapo awali ulitupa mtazamo tofauti juu ya hili suala.
 
Shukran sana kwa kunifumbua macho sikuliona hilo.. haya huyu Jamaa alichokisema ni kipi haswa! maanake sikumsoma...au nacho ni siri!


Viongozi wa CHADEMA walikuwa na GHETO Meeting, yaani afisa habari aongee matusi kama haya halafu aachwe?
 
  1. Matamshi gani hayo waliyotoa?
Unajifanya Hujui au

  1. Je ina maana kila anayetoa matamshi tofauti na Mwenyekiti/Katibu inabidi afukuzwe uongozi/uachama?
Mtu yeyote anayetoa matamshi yenye Kukashifu anastahili adhabu stahiki

  1. Walipewa onyo kabla au adhabu yao haina onyo?
Je Una Uhakika hawakupewa Onyo?

Kwa Hiyo akishasema Zitto tu utaamini au
Something is definitely wrong here. Zitto tungeomba na wewe utupe maoni yako maana hapo awali ulitupa mtazamo tofauti juu ya hili suala.
 
Waberoya,
Kwa ajili ya Tanzania njema usijiunge na Chadema kutafuta cheo. Jiunge na Chadema kama njia ya uhakika ya kuleta mabadiliko yanayohitajika Tanzania. Ni ushauri tu.

Kwa mwenye Elimu lazima afikirie mbali..sio kuwa msindikizaji...!!! kama M/Kiti anaogopa mwenye Elimu akataka "yes Man"..au fikira za M/Kiti zidumu basi hapo kazi tunayo...!!...kama ndio urithi tuliochukua kutoka kwa Mwalim basi naona urithi huo haufai...!!!

Bro mabadilikio ya kweli hayawezi kuja kwa kufukuzana tena kwa makosa ambayo very minor...Kweli Kafulia kasema Kikao cha Ghetto...does it enough kumfukuza...? Kule CCM ktk Uchaguzi wa UVCCM kulikuwa na crisis kubwa ya watu kuitana mafisadi...lkn hawakufika kufukazana..na JK akaja na busara zake kusawazisha mambo..."

hivyo mnashindwa kuvumiliana kiasi hicho....? Kikao cha Dodoma cha CCM watu wameambiana maneno Mazito mazito hadi waandishi wanasema hayafai kuandikwa...Nyie Kufanya kikao cha "Ghetto" imekuwa nongwa?..so kuwafukuza kunathibitisha kuwa msimamo wao wa Kumuuunga Mkono Zitto ndio umepelekea wao Kuhukumiwa...???

Kumbuka kipindi hiki ni kipindi cha kutafuta Wanachama sio kufukuzana...!! Ikiwa wanachama wanafanyiwa Hivi, Je washabiki mtawafanyaje...?

OK...Kama mmeamua kweli kuifanya Chadema kuwa NGO...ok endeleeni...otherwise you have to change ur Strategies!!!!
 
Viongozi wa CHADEMA walikuwa na GHETO Meeting, yaani afisa habari aongee matusi kama haya halafu aachwe?
Mkuu maneno haya Ghetto meeting aliyasema wakati kikao kinaendelea Dodoma kuwajadili watu hawa hawa ina maana kulikuwa na makosa kabla ya kikao hicho kuitishwa!...Haya ndio makosa nayotaka kuyasikia maanake kesho kesho kutwa huyu Kafulila anaweza sema vinginevyo.

Matatizo madogo madogo ndani ya chama na hasa vijana ambao wanapenda kusema ovyo ni mambo ya kawaida kabisa. Humu JF kuna watu hutapika maneno tena ya nguvu kuhusiana na vyama lakini uvumilivu ndani ya chama na kukubali fikra huru ambazo zilitangulia. Kafulila anajua fika ana upinzani pia ndani ya chama ktk nafasi ile ya Vijana na wapo watu upande wa pili wanaompinga na husema ovyo vile vile, kwa hiyo haya maneno yake mengi yanatokana na fikra za kwamba anapigwa vita..

Chukulia mfano wa Zitto mwenyewe alipozungumza ovyo kuhusu utawala ndani ya chama, kila mtu alishtuka sana lakini tukashindwa kupima uzito wa maneno yake kuupata ukweli badala yake watu wakarudi na matusi mazito sana ambayo hayakuwa na mpangilio, pasipo heshima wala hekima na waliozungumza hayo yote ni viongozi ndani ya chama ambao walitumia majina bandia.

Sikuona mtu akifukuzwa wadhifa wake hali yaliyosemwa hapa JF yalikuwa mazito sana na wazi kabisa kiasi kwamba mimi binafsi nilikereka..Lakini wakati huo huo nilifahamu mzizi wa fitna hiyo unatokana na kitu gani hivyo matusi yote hayakuwa yakihusiana na chama zaidi ya wahusika wa makundi haya mawili. tatizo la wengi hawakuelewa uchafu wa siasa hasa pale Zitto alipomshambulia Mbowe na mzee Mtei. It's a political game kumweka mpinzani ktk defence wakati wewe unashambulia. Iinakubalika lakini sii kwa jumuiya ya Wadanganyika kwa sababu wataamini kila kilichosemwa au kuandikwa. Hayo ndiyo yalikuwa makosa ya mheshimiwa Zitto lakini tactics za namna ile zinakubalika ndani ya chama kwani wengi wanaelewa ukweli ni upi.

Ni ukweli usiopingika kwamba Chadema imekuwa na makundi mawili ya Uongozi, jambo ambalo linakijenga chama na sii kujenga Uadui baina ya wahusika. Hili ndio tatizo la Wadanganyika kwamba mgombea mpinzani siku zote ni adui yako..Hatukujifunza toka kwa Obama na Clinton, hata kule kulianza na makundi mawili na wajumbe walikuwa huru kushabikia upande..Pia matusi mazito mazito yalirushwa wakati wa Kampeni lakini yote haya yalikwisha baada tu ya uchaguzi. Yakaja matusi baina ya Obama na McCain..Na baada ya Ushindi wa Obama husikii tena maneno yaliyokwisha pita watu wansonga mbele na wanatazama maswal yaliyoko mbele yao na sii nyuma tena. Hii ndio demokrasia inavyojengwa.

Mwisho, nayakubali sana maamuzi ya kamati hiyo maadam yamepata baraka za wazee na mhusika amekubali na kupokea maamuzi hayo pasipo kuanzisha zogo jingine.
 
Bi.Asha nakusoma sana bibie ila nachojaribu kusema hapa ni UWAZI.. tunahitaji kuweka uwazi pale ambapo panatakiwa hata kama kuna machungu.
Binafsi huyo Kafulila, atakuwa kafulia kweli ikiwa tutafahamishwa madhambi yake ili kesho mtu mwingine asije yarudia lakini pasipo kuyajua inatupa picha tofauti na mawazo mengi yanajengwa kiasi kwamba hata hizi tuhuma hazikutakiwa kuwepo iwapo tu utaratibu huu ungekuwa wazi na huru.

Binafsi nazungumza hivi kwa kuchelea zaidi jinsi Wadanganyika tulivyo, kesho huyo Kafuylila akiamua kuondoa Chadema anaweza kukipata chama hata kisitamanike kwa sababu tu chama kiliamua kuficha ukweli kwa maufaa ya huyo Kafulila au mtu mwingine...
Trust me hoja zangu, hujaribu kufikiria kama mtu aliyeko nje ya chama (out of the box).. na ndipo tunapo tofautiana kimawazo.
soma alichozungumza na gazeti la majira, then toa hukumu.
 

Nimeamua kuandika upya habari ya gazeti la majira la tarehe 8 november 2009 siku ya jumapili , toleo namba ISSN 0856-5086 Na.5786.Vol.11/3796.
Lengo ni ili kuweka rekodi sahihi juu ya walichosema wakina Kafulila na kuona nini kilichozungumzwa.

Bifu la Zitto, Mbowe tena.
  • Kikao cha siri chafanyika kuwaengua ‘watu'wa Zitto
  • Mbowe aja juu asema ni ujinga,utovu wa nidhamu

Reuben Kagaruki na Peter Masangwa.

Hali ya kisiasa ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ,inadaiwa kuzidi kuwa tete baada ya kudaiwa kufanyika kikao cha siri mkoani Dodoma kwa lengo la kuwaengua kwenye nyadhifa zao viongozi waandamizi wa chama hicho,hasa wale waliokuwa wakimuunga mkono Bw.Zitto Kabwe wakati wa Uchaguzi Mkuu wa chama hicho,akiwemo mama yake mzazi ,Bi.Shida Salum.

Habari ambazo gazeti hili limezipata Dar Es Salaam jana zilieleza kuwa kikao hicho kilichofanyika mkoani Dodoma November 4,mwaka huu kilihudhuriwa na maofisa ambao wakati wa uchaguzi wa chama hicho walikuwa kwenye kambi ya Bw.Zitto , ambaye wakati alikuwa ametangaza kuwania nafasi ya uenyekiti kwa lengo la kuchuana na Bw.Freeman Mbowe.

Habari hizo zilieleza kuwa waliojadiliwa kwa kina katika mkutano huo ni Ofisa wa Habari wa chama na Katibu wa Sekretarieti ,Bw.David Kafulila ,Ofisa Mwandamizi wa Bunge na Halimashuri ,Bw.Danda Juju na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho,Bi.Shida Salum.

Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Bw.Kafulila alijadiliwa kutokana na kile kilichodaiwa kuendelea kukigawa chama , ukosefu wa nidhamu na tabia anayodaiwa kuwa nayo ya kutaka kukigawa chama.

Ilielezwa kuwa Bi.Shida Salum na Bw.Juju nao wanadaiwa kuwa nyuma ya Bw.Kafulila katika mpango wake unaodaiwa una nia ya kukigawa chama.

"Ndani ya kikao kile mvutano ulikuwa mkubwa ,Mwenyekiti alishikilia msimamo wa kutaka afukuzwe uongozi na uanachama,"zilieleza habari kutoka mmoja wa watoa habari wetu.

Hata hivyo,ilidaiwa kuwa uamuzi wa Bw.Mbowe ulipingwa na wajumbe wa kikao hicho badala yake walishauri aitwe kwenye vikao vya chama hicho ,ili ajieleze. Inadaiwa kuwa wajumbe walisisitiza kuwa isingekuwa busara kumfukuza Bw.Kafulila wadhifa wake wakati hajawahi kupewa hata barua moja ya onyo kuhusu makosa anayotuhumiwa nayo.

Habari zaidi zilidai kuwa msimamo wa Mwenyekiti (Mbowe) uliendelea kubaki pale pale,ambapo inasemekana kesho ndipo atapewa barua za kuenguliwa katika wadhifa wake. Pamoja na msimamo huo wajumbe wawili wa kikao hicho walitahadharisha kuwa endapo hatua hiyo itafikiwa itakigawa chama,kwa kuwa wale waliokuwa kwenye kambi ya Bw.Zitto wakati wa uchaguzi hawatakubali kurudi nyuma .

Gazeti hili lilipomtafuta Bw.Kafulila ili kujua usahihi wa taarifa hizo ,alijibu; "kwanza ndiyo nazipata kutoka kwako. Ninavyojua kwa siku hizi mbili hakuna vikao vya chama vinavyotambulika kikatiba vilivyofanyika," alisema Kafulila na kuongeza kuwa ; "Mimi ndiye katibu wa Sekretarieti ya chama,ndiye mwandishi wa miniti za vikao,kama kuna kikao kilichofanyika kama unavyosema basi hivyo vitakuwa ni vya geto."
Alipoulizwa kama ana taarifa za Bw.Mbowe na maofisa wengine wa cham kukutana Dodoma ,alijibu:
"Habari hizo nimezisoma kwenye vyombo vya habari ,sina taarifa ninachoamini ni kuwa maamuzi ya chama hayafanyiki kwenye geto," alisema Bw.Kafulilana kasha kukata simu kwa hasira.
Kwa upande wake Bi.Shida alikiri kupata taarifa kupitia vyombo vya habari za kikao hicho kufanyika mjini Dodoma,ingawa ajenda na uhalali wa kikao hicho alikuwa hazifahamu. "Sina taarifa kuhusu kujadiliwa kwangu,kwa sasa nafanya upelelezi na kuwauliza waliohudhuria ili kujua kilichojili" alisema.
Alisema kama kikao hicho kilifanyika siyo rasmi na kama kilifanyika atahoji ni kwa nini.

Kwa upande wake Bw.Juju alisema yeye kama kiongozi wa chama hana taarifa za kufanyika kikao hicho na hafahamu ajenda zilikuwa ni zipi. Alibainisha kuwa anachokifahamu ni kuwa kikao kilichofanyika Novemba 1,mwaka huu kilikuwa ni cha Sekretariati kwa ajili ya kufanya tathimini ya uchaguzi wa serikali za Mitaa ,ambapo kiliahirishwa hadi Novemba 3, lakini hakikufanyika kutokana na wajumbe kushindwa kutimia .
"sasa sijajua kama kikao hicho ,ndicho kimekutana Dodoma au hapana ,lakini makubaliano yetu yalikuwa kifanyike Makao Makuu," alisema Bw.Juju.

Bw. Mbowe alipoulizwa kuhusiana na madai hayo,alicheka na kusema "Kamanda ,unajua kuna vitu vingine vya kijinga……sisi siyo wapumbavu kwa kiwango hicho,"alisema.

Alisema watu wenye hofu ndani ya chama hicho ndio wanaosambaza ujinga wa aina hiyo. "Kama mtu ana ujinga ni wake mwenyewe ,huo ndio utovu wa nidhamu tunaozungumzia ,hatuwezi kukubali kufanyia kazi ujingakwani siyo utamaduni wetu". Alibainisha kuwa CHADEMA kina uhuru wa kuendesha vikao vyake sehemu yeyote ndani nchi haizuiwi na mtu.
"Wewe wasiwasi siyo hoja iliyotupeleka," alisisitiza. Alipoulizwa kikao kilichokutana Dodoma kiliwashirikisha akina nani,alijibu kuwa kiliwajumuisha Wakurugenzi wa chama
 
Chadema sasa hali si shwari waendesha vikao vya siri kuwajadili wanachama

Na Fidelis Butahe

HALI ya kisiasa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inaonekana kuyumba baada ya Mwananchi kupata habari kwamba Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe juzi aliongoza kikao cha siri mjini Dodoma kilicholenga kuwajadili baadhi ya wanachama akiwemo mama mzazi wa Zitto Kabwe, Shida Salum.

Habari hizo kutoka ndani ya chama hicho, zilieleza kuwa waliohudhuria kikao hicho ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa, Hemed Sabula, John Mrema, Erasto Tumbo, Benison Kigaila, Halima Mdee, Lucy Owenya na Anna Komu.

Habari hizo zilifafanua kuwa Mbowe aliwasilisha ajenda ya kufukuzwa uanachama kwa afisa habari wa chama hicho, David Kafulila, mama mzazi wa Zitto Kabwe, Shida Salum ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho na Danda Juju ambaye ni afisa Mwandamizi kwa kuwa wanakichafua chama kwa kuchochea mgogoro kutokana na kuvujisha siri za chama kwenye vyombo vya habari.

Habari hizo, zilieleza kwamba baada ya Mbowe kuwasilisha hoja yake, ilipingwa na wajumbe wa kikao hicho kwa maelezo kuwa, Zitto Kabwe hatakubaliana na jambo hilo na kusisitiza kuwa linaweza kukipasua chama, lakini katika majumuisho Mbowe alisisitiza kuwa hataweza kufanya kazi na Kafulila hivyo alisisitiza kuwa Kafulila apewe barua ya kufutwa uanachama.

Kutokana na kusimamia uamuzi huo, ilidaiwa kuwa wajumbe wa mkutano huo walikubali kwa shingo upande umauzi huo.

Baada ya tarifa hizo Mwananchi liliwatafuta wahusika ambao walikiri kuwepo kwa taarifa za kikao hicho na kusisitiza kuwa wanasubiri kuona kama watapatiwa barua za kufutwa uanachama au la.

"Mimi hizo taarifa nimezisikia na nilikuwa najua kuwa kulikuwa na kikao kisicho rasmi kilichokaa Dodoma ila mpaka sasa sijapata barua yeyote, nasikia kuwa wanataka kunitimua uanachama, lakini ngoja tusubiri tuone wakinipatia barua kila kitu kitakuwa wazi," alisema Kafulila ambaye hivi karibuni alitangaza nia ya kuwania Ubunge mwaka 2010 Kigoma Kusini

Kafulila pia aliwahi kuwania nafasi ya Uenyekiti wa Baraza la Vijana la Chama hicho, (Bavicha) katika uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa Agosti mwaka huu, lakini mshindi hakupatikana baada ya mpinzani wake, John Heche kupinga matokeo kwa madai kuwa kura 20 zilikuwa zimeongezeka.

Naye Danda Juju alisema taarifa hizo, amezisikia ingawa hana uhakika nazo na kusisitiza kuwa kwa kiasi fulani anaweza kuziamini kwa kuwa alikuwa na taarifa kuwa Mbowe anafanya kikao kisicho rasmi mkoani Dodoma. Mama mzazi wa Zitto, Shida Salum hakuweza kupatikana kuzungumzia sakata hilo.
kubwa jinga soma na hizo pia, unajua kiongozi wa chama kuwatuhumu wenzake kuwa wanataka kumfukuza uanachama ni jambo kubwa sana , inawezekana huyo Kafulila aliweza ama alishindwa kujitetea pia juu ya hilo. Im trying to think aloud.
 
mtu unapojiunga na chama unakuwa tayari kufuata taratibu zake na masharti yake. Kama hilo linakupa tatizo kaa nje ya chama. Isije kufika mbeleni chama kikaamua kufanya jambo fulani na wewe ukabakia kulalamika "naonewa naonewa". Iwe CCM au Chadema au chama kingine chochote, mwanachama hawezi tu kujiamulia kufanya mambo yake au kuwa na mielekeo yake hasa kama ni kiongozi. Ndio maana hadi leo hii hata hao walio CCM wapiganaji hawashambulii chama chao kama chama kwa sababu kufanya hivyo ni kujaribu kukata tawi walilokalia.
 
As a leader ni lazima ujue kuongea na Media maana watu watashindwa kukutofautisha na Mpiga debe pale Karume. Halafu kila mtu anajaribu kujificha nyuma ya Kivuli cha Mbowe.

Kwa the way Media inavyoripoti hizi habari naamini Mbowe na CHADEMA kwa ujumla vinawanyima usingizi watu
 
Kiranja,
Mkuu nimekusoma na sasa hivi kila kitu wazi kabisaaaa, Ila ktk taarifa hiyo ya gazeti inaonyesha wazi kuna mhuni mmoja alikuwa akituma taarifa zote za mkutano ktk gazeti hilo kiasi kwamba aliondoa Usiri wa mkutano. Huyu ntu (mtu) ndiye chanzo cha mengine yote yaliyofuatia.
 
mkuu unaweza kutuhakikishia ukweli wa habari yako.Kwanza kweli wa kufanyika kwa kikao hicho then Ukweli wa ajenda uliyoitaja kwamba ndio iliyoongelewa
 
Wakuu zangu, Mimi sidhani kama kuna mgogoro kati ya Zitto na Mbowe.. Haukuwepo toka miaka yote ile isipokuwa kuna watu ndio wanachonga ili mradi tu kuharibu ukaribu wa Zitto na Mbowe..
Nijuavyo mimi Zitto na Mbowe wapo karibu zaidi ya mtu mwingine yeyote Chadema nje ya maswala ya chama yaani kuna urafiki na ushikaji. Hilo linaweza pia kuwa sumu kwa baadhi ya watu.
 
Wakuu zangu, Mimi sidhani kama kuna mgogoro kati ya Zitto na Mbowe.. Haukuwepo toka miaka yote ile isipokuwa kuna watu ndio wanachonga ili mradi tu kuharibu ukaribu wa Zitto na Mbowe..
Nijuavyo mimi Zitto na Mbowe wapo karibu zaidi ya mtu mwingine yeyote Chadema nje ya maswala ya chama yaani kuna urafiki na ushikaji. Hilo linaweza pia kuwa sumu kwa baadhi ya watu.

Mimba haifichiki, muda wake utakapofika kichanga kitajitokeza tu, hata kama wahusika wakisingizia ubikira.

Kama Kafulila kaachishwa uongozi kwa sababu za kimazingaombwe za Mbowe, basi tusubiri tu tuone hii mimba inayokataliwa kuwepo itaishia wapi? Yetu macho lakini wachawi wetu tushawaona kutokana na historia ya migogoro ndani ya CHADEMA.

Mbowe na Mzee Mtei ndio wachawi. They have to go if the party is to progress.
 
Mods,
Ingekuwa vema kichwa cha habari cha hii thread kibadilishwe maana kinaondoa hadhi ya JF kwa kujaribu kupamba yanayojadiliwa ndani yake. Tunaongelea mgogoro uliopo na sio jinsi wanavyojaribu kutatua maana wala hatujui kama wanajaribu kutatua.

Kwa sasa kichwa cha habari kimefanana-fanana na vile vya magazeti ya mipasho au uhuru ikiandika kuhusu Lowassa. Hebu kibadilisheni.
 
Kubwajinga Kubwajina bin Kuwajinga

Mimba haifichiki, muda wake utakapofika kichanga kitajitokeza tu, hata kama wahusika wakisingizia ubikira.
Hizo ni Wishfull thinking, hiyo Mimba imesubiriwa sana lakini hamna mtoto, kama mafisadi wameamua kutungisha Mimba then sperm count zao ni chache

Kama Kafulila kaachishwa uongozi kwa sababu za kimazingaombwe za Mbowe, basi tusubiri tu tuone hii mimba inayokataliwa kuwepo itaishia wapi? Yetu macho lakini wachawi wetu tushawaona kutokana na historia ya migogoro ndani ya CHADEMA.

Mazingaombwe gani mkuu?

Mbowe na Mzee Mtei ndio wachawi. They have to go if the party is to progress.
Hamna lolote mnajifanya mnampeeenda Zitto! Roho inawauma kwa sababu lengo lenu halitimii, mnataka mkimalizana na Zitto na Mbowe mje kwa Zitto na Slaa! Ha ha ha Janja ya Nyani kula Indi bichi
 
Back
Top Bottom