Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

hahahaha nimeacha ndugu yangu huyu MkamaP ni Fisadi na kibaraka!

teh teh teh
Sawa kabisa mtoto mwema

Lakini kinachosikitisha zaidi ni pamoja na elimu yake ya Theolojia Slaa bado ni fisadi . hivi wewe mwongozo wako ni upi hapa?
 
teh teh teh

We mkweli mkuu nisaidie kidogo alihujumiwa na akina nani kweli?

Huyu fisadi Slaa aache uhujumu wake

Mkuu kama hujui maana uliza. Dr Slaa siyo FISADI wala sijaona alipotuhumiwa. Kama alihujumu basi ni tuhuma mpya unaleta, kwahivyo basi MTUHUMU na sio kumhukumu.

Halafu kwa kuwa upo kwenye keyboard huko isiwe sababu za kuandika andika tuu bila kuwa na facts. Unakumbuka Mama Sophia Simba alivyosemaga hovyo hovyo majuzi ??, Mzee Malecela alisema apelekwe wapi vile???

Habari ndio hiyo.
 
Huyu MkamaP ana miaka mingapi?, yaani UMRI wake hapa duniani.

David Solomon naomba uni PM kunipa jibu.
 
teh teh teh
Sawa kabisa mtoto mwema

Lakini kinachosikitisha zaidi ni pamoja na elimu yake ya Theolojia Slaa bado ni fisadi . hivi wewe mwongozo wako ni upi hapa?

Nani Fisadi kati ya hawa hapa chini

a) Rostam Aziz
b) Edward Lowassa
c) Andrew Chenge
d) Basil Mramba
e) Slaa Wilboard
f) Ben Mkapa
 
Mkuu kama hujui maana uliza. Dr Slaa siyo FISADI wala sijaona alipotuhumiwa. Kama alihujumu basi ni tuhuma mpya unaleta, kwahivyo basi MTUHUMU na sio kumhukumu.

Halafu kwa kuwa upo kwenye keyboard huko isiwe sababu za kuandika andika tuu bila kuwa na facts. Unakumbuka Mama Sophia Simba alivyosemaga hovyo hovyo majuzi ??, Mzee Malecela alisema apelekwe wapi vile???

Habari ndio hiyo.

teh teh teh

RA ni fisadi ama si fisadi.mambo mengine yanachekesha sana.
tulia ufikiri kidogo najua ni utoto ukikua utaacha hilo kwa kweli nalitambua.

SLAA ni FISADI
 
Unapoteza muda wako kaka....


utoto ukikutoka utaacha .
tulia kidogo ufikiri kwanini masanilo aliowataja kawaita mafisadi na je? nani kathibitisha?

Kujisaidia ajisaidie kuku tu bata eti kaharisha.

ee kwa heri
 
Duh! Hizi ndizo siasa za waafrika, matatizo kama ndiyo yanawasumbua sana, haipendezi hasa kwa chama kinachoanza kujijenga kwa wananchi kama hiki, Mungu aepushe mbali mambo haya.
 
Nov 12, 2009

ALIYEKUWA Ofisa Habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), David Kafulila amesema licha ya kuvuliwa wadhifa wake, hana mpango wa kuhamia chama kingine.

Kafulila amesema, Chadema ni chama mbadala, hivyo kwa sasa kinahitaji kuwa imara zaidi na yeye kuondoka katika chama ambacho alidai Watanzania wana matumaini nacho, itakuwa si kuwatendea haki.

Amesema, hata alivyokutana na wazee wa Kigoma ambao wanakwenda Hijja Saudi Arabia, walimtia moyo na aliwahakikishia kuwa hawezi kuondoka Chadema, kwani wenye tatizo ndani ya chama hicho ni mtu mmoja mmoja na si chama.

“Sifikirii kuondoka Chadema, kwangu mimi nimeipenda tangu niko shule ya msingi, hilo la kuondoka haliwezekani kamwe,” alisema. Kiongozi mwingine aliyevuliwa wadhifa wake ni Danda Juju, ambaye alikuwa anahusika na mambo ya Bunge.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu madai ya mgogoro ndani ya chama hicho, alisema masuala ya watendaji kuvuliwa nyadhifa, yako chini ya Katibu Mkuu wa Chama.

“Mimi sipendi kuzungumzia suala hilo kwani si la kisiasa, masuala ya kiutendaji tumemwachia Katibu Mkuu ndiye msimamizi wa watendaji wote wa makao mkuu,” alisema Mbowe.

Wakati Mbowe anatoa msimamo huo, Kafulila alisisitiza kuwa licha ya kuwa Katiba inampa mamlaka Katibu Mkuu kuwavua nyadhifa zao watendaji, lakini anaamini Dk Wilbroad Slaa, hakumtendea haki.

Aliongeza kuwa licha ya kuwa haungi mkono kuondolewa kwenye nafasi ya uofisa habari, lakini anaamini kuwa hizo ni changamoto za kisiasa na siku moja Chadema itatengemaa.

Alipotakiwa kueleza undani wa yeye kuvuliwa wadhifa, Kafulila alisema “sitaki kuzungumzia mambo ya ndani ya chama chetu, kufanya hivyo nitakuwa naibomoa Chadema, chama ambacho ni matumaini ya Watanzania.”

Kuhusu kama hatua hiyo inaweza kumdhoofisha kisiasa, alisema haamini kuwa hatua hiyo imemdhoofisha badala yake aliwataka wafuasi wa chama chake Kigoma watulie, kwani hicho ni chama chao wote.

Kafulila pia aligoma kusema alichojadiliana na wazee wa Kigoma; bali akasema tu kwamba walikutana wakajadili mambo mengi yanayohusu siasa.

“Wale wazee si wanasiasa, wale ni viongozi wa dini, siwezi kusema tulichojadiliana nao, ila ninachoweza kusema kwa sasa ni kwamba wazee walinipa ujasiri wa kuendelea mbele katika harakati zangu za siasa,” alisema mwanasiasa huyo chipukizi.

Alisema wazee wale wanafahamu harakati zake za kupigania haki tangu akiwa Kigoma na ndiyo maana waliposikia kuhusu matatizo yake kuwa amevulia wadhifa kwa chuki, waliona vema watete naye kabla ya kwenda Hijja.

Juzi baadhi ya vyombo vya habari vilimkariri Dk Slaa akisema kuwa ametengua ajira za watu hao wawili kwa maslahi ya chama na kuongeza kuwa hatua hiyo ina lengo la kukisafisha chama kwani wakiacha hali hiyo iendelee wanaweza kuingia Ikulu na mambo ya ajabu.

Lakini uamuzi huo ulipingwa na Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe, ambaye alisema unaweza kukidhoofisha chama kwani Kafulila anaandaliwa kugombea ubunge Kigoma Kusini ambako CCM ilifanya vibaya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.


Source: Habari Leo
 
Nielewavyo mimi David Kafulila na Danda Juju walikuwa ni maofisa waajiriwa wa Makao Makuu ya Chadema. Mwajiri ni Katibu Mkuu na endapo ajira yao haina tija kwa Chama kutegemea assessment ya mwajiri, alikuwa na wajibu wa kushitisha ajira ya hao vijana.

Wanasiasa wengi mashuhuri Tanzania walianzia kwa kuajiriwa kama wafanyakazi katika Makao Makuu ya chama cha siasa. Kikwete na Lowasa ni mifano mizuri. Lakini walikuwa ni wachapakazi, na walijifunza kwa makini misimamo ya viongozi wa chama. Waliomba msaada wa viongozi wao walipojihisi wamefikia ukomavu wa kugombea ubunge katika maeneo yao. David Kafulila na Juju jifunzeni. You may have a future if you learn from big shots.

Ninampongeza Dk. Slaa kwa kuwa firm katika kuimarisha Secretariat yake. Niwahimize wote muendelea kwangu sasa na ile Operesheni Sangara, hasa wakati huu chama cha mafisadi kikionyesha dalili za kuparaganyika.
 
11_09_m4qk3a.jpg


Hichi ndio nilichoona cha maana kwenye hio website
 
Bwana "Habarindiyohiyo", Mimi sikuweza kusoma gazeti "lililowavaa" Mnyika na Mrema, lakini hiyo allegation kwamba vijana wote wawili ni Wachagga ni uzushi. John Mnyika mwenyewe kaniambia kwao ni Iringa.

Sioni ajabu kusoma uzushi huu kwa vile kama nilivyosema awali chama cha mafisadi kinachomeka kila aina ya propaganda chafu dhidi ya chama m'badala wakati huu kinapoparaganyika.
 
TUKO PAMOJA KAFULILA KATIKA HILI...kwani sio mtu ukienguliwa kwenye nafasi yako....basi unahama!...Mimi najua hunifahamu, lakini nimekuwa nikifuatilia makala zako mara kwa mara. usirudi nyuma...ni kweli CHADEMA inakabiliwa na changamoto nyingi lakini bado inahitaji vijana kama wenye upeo wa kafulila kwa kujenga na kubomoa hoja. najua umeonewa, lakini usimlaumu slaa...tatizo la chama chako ni mbowe na uchagga tu.....slaa anatumiwa...
 
Back
Top Bottom