Safari milioni 274! Mapumziko ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yanaonyesha kuimarika kwa uchumi wa China

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111434741037.jpg


"Kuweka rekodi", "nguvu kubwa”, "imani”... Haya ni baadhi ya maneno yaliyotumiwa sana na vyombo vya habari vya nchi mbalimbali wakati wa kuripoti mapumziko ya Siku ya Wafanyakazi Duniani hapa China yaliyomalizika hivi karibuni.

Takwimu zinaonyesha kuwa wakati wa mapumziko ya siku tano mfululizo, jumla ya safari za ndani milioni 274 zilifanywa nchini China, na mapato ya utalii wa ndani yalikuwa karibu dola za kimarekani bilioni 21, hayo yote yakizidi kiwango cha kipindi kama hicho mwaka 2019 kabla ya janga la COVID-19 kutokea.

Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC lilimnukuu raia wa China Bi Wu, anayeishi Henan, katikati ya China, akisema: "Mwanangu anataka kwenda Beijing, na binti yangu anataka kwenda Shanghai, lakini walikosa hoteli na tiketi za ndege, hivyo hatimaye nikachagua kutembelea maeneo ya karibu kwa gari... Baada ya kuona hamu ya kufanya matumizi kuwa kubwa, naona biashara yangu itakuwa nzuri mwaka huu. "

Mwaka huu ni mapumziko ya kwanza ya siku ya wafanyakazi duniani nchini China baada ya nchi hiyo kulegeza hatua za kupambana na janga la COVID-19, na hamu kubwa na utalii na matumizi makubwa ya watu wa China vinaonyesha matarajio makubwa ya watu na imani yao katika mustakbali wa uchumi wa China. Tarehe 11, Aprili, Shirika la Fedha la Kimataifa IMF lilitoa matarajio yake mapya kuwa uchumi wa China utakua kwa 5.2% mwaka huu, ikiwa ni asilimi 0.8 zaidi ya matarajio yake iliyotoa mwaka jana. Ikiwa ni nchi ya pili duniani kwa ukubwa wa uchumi, na nchi yenye idadi ya watu inayochangia asilimia 20 ya watu wote duniani, kuimarika kwa uchumi wa China kutakuwa na umuhimu mkubwa kwa ukuaji wa uchumi wa dunia mwaka huu.

Kwanza, uchumi wa China unapoimarika, China itaagiza bidhaa nyingi kutoka nchi nyingine, na watalii wengi zaidi wa China watasafiri nje ya nchi. Takwimu zinaonyesha kwamba wakati kasi ya ukuaji wa uchumi wa China inaongezeka kwa asilimia 1, kasi ya ukuaji wa nchi nyingine itaongezeka kwa karibu asilimia 0.3.

Pili, China ni sehemu muhimu ya mnyororo wa utoaji bidhaa duniani, na uchumi wake imara utasaidia kutuliza utoaji bidhaa duniani, ili kuzuia uhaba wa bidhaa. Mbali na hayo, ukuaji wa uchumi wa China pia inachangia utulivu wa siasa za kijiografia, ambayo ni muhimu hasa wakati ambapo mivutano ya siasa za kijiografia imeongezeka kutokana na mgogoro wa Ukraine.

Ikiwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika na nchi kubwa zaidi ya uwekezaji barani humo, kuimarika kwa uchumi wa China pia kumevutia watu wengi katika nchi za Afrika. Katika miaka ya hivi karibuni, China imeendelea kuongeza uagizaji wake wa bidhaa zisizo za maliasili zikiwemo za kilimo kutoka Afrika, huku ikizipa nchi za Afrika bidhaa za viwandani, miundombinu na teknolojia. Katika miaka hii kumi, China imekuwa mwekezaji mkubwa zaidi barani Afrika, ikichangia 20% ya ukuaji wa uchumi wa Afrika na kutengeneza mamilioni ya nafasi za ajira kwa nchi za Afrika. Katika mwaka wa 2023, nchi duniani kote zinatazamiwa kuingia kihalisi katika "zama za baada ya janga la COVID19", na inatarajiwa kwamba, maendeleo yenye ubora wa juu ya uchumi ya China yataleta fursa zaidi barani Afrika na kuchangia kufufuka kwa uchumi wa Afrika.
 
Back
Top Bottom