mdudu
JF-Expert Member
- Feb 6, 2014
- 6,954
- 9,857
Bado Anafikili tupo awamu ya 5 ya kiki na mipasho,RPC WA Dodoma bado ana mawazo mgando ya kizamani kuwa kila tatizo litatuliwa kwa kutumia nguvu. Ni kama mtu alieshika nyundo ambapo anaona kila tatizo ni msumari hivyo yeye anawaza kupigilia tu.
Katika kuzungunzia maandamano ya CHADEMA ameonekana akiwa na askari wa kike Wawili nyuma yake waliojipamba kwa silaha lengo likiwa ni kuwatisha BAWACHA. Kwanza ule ni ushamba tu. Dunia ya sasa matatizo hayatatuliwi kwa silaha wala vitisho. Kuna wenzake walitumia vitisho na nguvu matokeo yake wakafa wao wakaacha nyumba silaha na askari waliokuwa wakiwatumia kutesa na kuua wenzao. Kamanda acha vitisho vya kizamani badilika huu ni ulimwengu wa diplomasia siyo vita
Muda wake wa kusitaafu umefika,Anafikili anaweza kuongezewa muda,
Ni aibu Sana kutoa vitisho kwa wanawake Tena hawana hata kipande Cha fimbo,nani alimwambia kuandamana ni kosa?