Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 59,116
- 103,624
Kisheria Kinana hana mamlaka ya kumuagiza RPC
Kinana alitoa Ombi na siyo agizo
Ndio maana alisema "Namsihi IGP apunguze Askari wa usalama........
Sasa hizo nasaha zake Viongozi wa polisi wana uamuzi wa kupima kwanza usalama na kufanya maamuzi sahihi siyo kwa kukurupuka.
Baada ya CCM kupoteza ushawishi kwa umma, wameamua kuja na mbinu ya kufanya siasa za kiki ili kuhadaa umma kuwa wanastahili kuendelea kukaa madarakani. Ndio hapo unaona viongozi wa CCM wakiingilia moja kwa moja watendaji wa serikali. Ni kama wanalazimisha kurudi mfumo wa chama kushika hatamu.
Ni hatari unapokuwa na chama kimoja kukaa madarakani muda mrefu, maana mambo mengi yataanza kutekelezwa kinyume na utaratibu ili kuhalalisha uwepo wa hicho chama madarakani.