Rombo wapandisha bendera ya Kenya?

Kwa hiyo Wachagga wa Rombo wameamua kuamia Kenya? Vizuri tunaheshimu maamuzi yao
 
Tarime Na Rorya ndo usiseme watu wameichoka bongo. huko radio RAMOGI FM ndo wanafungulia.
panatawaliwa kijeshi ila wananchi wana hasira sana na huo utawala wa kipolisi.
Polisi,TRA pamoja na Uhamiaji wamejazana daraja la kirumi utadhani ndiyo mpaka.
Viongozi kukosa busara na uchumi mbaya ndo unazidi unazidisha hasira kwa wananchi.
Poleni wana Rombo yote yana mwisho.
 
Tutakuweka wewe! Ama Mramba arudishwe teh teh! Wewe unafikiri hawa Wananchi wenzetu kama wamekataliwa na serekali yenu wafanyeje. Ukimkataa mtoto akiingia mtaani kumsaka baba yake utamlaumu. Rombo kiloa ya sukari shs 4500/= unategemea nini? Tunashindwa kulinda mipaka yetu tunalinda maslahi ya watu wachache. Kama kwa kuzuia magari yalobeba sukari pale Himo basi tuongeapo sukari ingekuwa inapatikana Moshi nzima na mikoa mingine. Eti sasa imekuwa lazima uende kwa mtendaji ukapate kibali cha sukari. Tanzania hii ya Miaka 50! Kweli tunashindwa kujenga miundo madhubuti ya kutoa huduma kwa wananchi wetu.Aibu sana.

Mkuu haya unayoyasema nikweli? Sukari 4500? Nini hasa kimesababisha iwe hivyo? Hakika kama ni kweli, ifike wakati hata mbunge wao apige kelele sasa.
 
Ooh poleni sana wananchi wa rombo, ila kwa ushauri wangu, sioni kama ni busara kuhamia nchi jirani. Nchi ya kenya na yenyewe ina maswaibu yake, tena ni nchi yenye vurugu na vitukoza vya hapa na pale kila kukicha. Kwa hilo naona mmepotea njia.
 
Rombo ipi unayoizungumzia? Maana wakaazi wa Rombo (ya Oloitoktok) ya Kenya huduma zote huzipata Rombo ya Tanzania na Wa-Rombo wa Kenya wanajisikia Watanzania zaidi sasa hii ya Wa-Rombo wa Tanzania kujifanya wa- Kenya inawezekana? Ngoja tujifunze masuala ya hawa wakaazi wa mpakani mwa Tanzania na Kenya:

 
Last edited by a moderator:
Wa Rombo wapuuzi wakubwa.Wakenya wenyewe wanataka kuwa watanzania kukimbia njaa.Kwani lazima munywe chai,si nyinyi huwa munakunywa uji wa ndizi?.
Yaani kukosa sukari tu munakimbia nchi.si watu wa kuaminika hata kidogo.Ndio nyinyi munaobadili dini na vyama kwa kuhongwa vitu vidogo kama pombe na mitumba.Poleni sana warombo.

Naomba uchunge mdomo wako
 
Serikali imekuwa ikiwatenga sana wananchi wa Rombo katika huduma.Mradi wa maji katika vijiji vya katangara na Mrere umeingiliwa kisiasa.Watu wanapata maji kisiasa,watu wa Useri na Tarakea ukanda wa chini ni kama vile hawaoni faida ya kuwapo serikali,halikdhalika watu wa Mkuu na Mengwe hasa maeneo ya Ibukoni

Mradi wa Umeme umekuwa na urasimu mkubwa,mazingiura ya kufanya biashara halali yameingiliwa na kugubikwa na Rushwa.Watendaji wa serikali si waaminifu na mara nyingi hutumia vitisho dhidi ya Raia katika kufanya majukumu yao.

Kwa kweli kuna ukiukwaji mkubwa haki.Sijui sertikali ya CCM inawachukulia vipi wananchi wa Rombo.Ni miezi michache tu imepita tangu mradi wa shule ya jumuiya ya wazazi ya CCM,shule ya sekondari Shauritanga umeleta mgogoro na wananchi baada ya kulazimisha kuziba barabara na kufanya eneo la barabara kuwa mali ya shule hiyo inayoomilikiwa na chama cha Mapinduzi.Ilizua mtafaruku nusura damu imwagike.Hili suala pamoja na mengine yanahitaji Mbunge asimame kidete na wananchi kuhakikisha haki inatendeka kwa wananchi wa Rombo.They deserve better than this.
 
wengi humu hawaijui Rombo, infact hao watu ni very realistic hata kisiasa. Km utakumbuka zamani sana walishampiga chini mramba then waka mrudisha na the fact kwamba alileta lami bado hakuwa ame-meet objectives alizopewa wakampiga chini. Niambie ni majimbo mangapi yenye upeo huo??
 
siyo kuheshimu maamuzi yao, inatakiwa ujiulize kwanini wamehamia kenya!

Serikali ya sisiemu imewazuilia wasipate bidhaa muhimu kama chakula, sijui inataka wafe?? Sukari inaishia hapo Himo, vipi kuhusu tarakea, mwika, keni...(au hawapendi chai na gah'wa??)
 
Ingawa siungi mkono kitendo cha kupandisha bendera ya nchi nyingine,lakini serikali ya Tanzania ndiyo imewafanya wananchi wakafikia huko.Sukari imezuiliwa Himo bila kujali kuna Eneo lingine la Tanzania mbele ya Himo linaloitwa Rombo.

Rombo inastahili haki zote kama wananchi wa maeneo mengine.Kwa muda mrefu rombo imekuwa ikikandamizwa na kudharauliwa na watawala wetu,sijui ni kwa nini hasa.

Mkuu wa mkoa ameshindwa kuweka mkakati wa kutosha kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma hii wakati huo huo akidhibiti magendo.Ni kwa nini maeneo mengine yaliyopakana na nchi jirani wameweza kudhibiti hali hii bila kubughudhi wananchi ndani ya territory yake halafu mkuu wa mkoa wa kilimanjaro ashindwe.Madiwani wa CCM ndiyo wanaoongoza halmashauri hivi kweli wanashindwa kutengeneza mfumo mzuri wa kuweka ukaguzi katika usambazaji wa sukari kuanzia Himo,Mwika,Mamsera,Mkuu,Mashati,Useri na Tarakea? ni kwanini tusiweke logistics katika level yenye uwajibikaji wa kisiasa kama kata kisha nadharia ya monitoring and evaluation ikatumika?

Wananchi wa Rombo hata katika ugawaji wa Mahindi ya misaada madiwani wa CCM na wenyeviti wa vitongoji walitaka watu waonyeshe vitambulisho kwanza yaani kadi za CCM ndiyo wagawiwe.Nina ushahidi wa majina ya watu wasiojiweza kabisa hawakupewa mahindi,na pia hujuma iliyotumika kudhulumu watu waliostahili kupewa mahindi hawakupewa.Nimeorodhesha malalamiko na ushahidi wote ukajadiliwe kwenye vikao vya baraza la madiwani walifanyie kazi watoe ripoti kwa wananchi wa Rombo

Wananchi wa rombo wanatia huruma kwa jinsi wanavyobambikiwa kesi na watendaji wa serikali,ni ukandamizaji uliopitiliza.Kulikuwa hakuna vituo vya polisi na hata vilivyopatikana vinatumika kama tools za kutisha raia na kujipatia hela.Mojawapo ni kesi iliyomuhusu mwananchi mmoja anaitwa Aristariki Kimaryo aliyewekwa mahabusu na mtoto wake pamoja na mkwe wake kituo cha polisi Mashati kisa hawajatoa hongo ya kumnusuru mtoto wake,hivyo polisi wakaamua kuwasweka mahabusu.Tulipowahoji polisi sababu ni nini wakaishia kutoa vitisho hadi tulipotishia kutumia nguvu ndipo walipowaachia

Tembo wanaotoka nchi jirani wamekuwa wakivamia mashamba ya wananchi,wakiharibu na hata kuuwa watu lakini hakuna fidia ya maana iliyofanyika.Wanachi wa Rombo sasa inabidi kwa ruthless,wanyama wanaoingia kwenye mashamba inabidi wauwa na hakuna kutoa taarifa kwa idara ya maliasili,wauawe na pembe ziuzwe hela iingizwe kwenye akaunti maalumu ya kufidia walioathiriwa na wanyama hao

Leo hii watu wanawalaumu watu wa Rombo kwa kujiskia sehemu ya kenya bila kufikiria saikolojia iliyowaathiri ya muda mrefu.Huduma za kijamii na kiuchumi zimekuwa attached na wakenya.Hata Radio ya Taifa TBC haifiki kule badala yake KBC ndiyo inasikika sijui kama watu walioko Tunduma,Songea na kigoma wanasikiliza redio za Zambia,malawi,msumbiji au DRC kuliko TBC au ni Rombo peke yake?

Sasa serikali itende haki,mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya,madiwani pamoja na Mbunge wa Rombo simamieni maslahi ya wananchi wa Rombo.Serikali iache vitisho,iache kuwatisha wananchi wa Rombo.


mzeee unaunga mkono warombo kupandisha bendera ya kenya?nassari naye alidai jamhuri ya kaskazini
 
Siamini kama kuna Mtanzania Mzalendo anaweza Kufanya ujinga Kama Huu.
Kama ni kweli, basi Hao ni wahaini....serikali ipeleke JWTZ wazunguke na magari yao mitaani
 
Usiwe unaaandika kwa kukurupuka wewe Kibaraka wa CCM!! Unajua taabu ya sukari kule Rombo wewe.

Unajua kilo moja ya sukari sasa hivi kule Ni shilingi Ngapi. Jaribu kufuatilia mambo ndio uandike *****.

Yaani wewe kwasababu ni mwana CCM hutaki kusikia mwananchi akilalamika Matatizo yake.

Jaribu Kutumia Kichwa angalau.

Kwa kupandisha hiyo Bendera serikali yenu sasa itatambua the seriousness of the situation.

Sishabikii kupandishwa Bendera ya Kenya. Ila nafurahia kuwa Hii serikali ya CCM itaona kule kule kuna tatizo.

Tafuta Sehemu nyingine ya kuwatetea magamba. lakini sio katika matatizo yetu.

sawa wewe unayejiita Mzee asiye na hekima?

Kwa hiyo unataka kutuambia hizo ndo mbinu za chadema kudai haki? watu wa aina yako ndo mnaabisha chadema!
 
Siamini kama kuna Mtanzania Mzalendo anaweza Kufanya ujinga Kama Huu.
Kama ni kweli, basi Hao ni wahaini....serikali ipeleke JWTZ wazunguke na magari yao mitaani

Tusitafute njia za mkato.Mbona ilikua rahisi kushulikia madai ya wananchi wa Rombo kuliko kutumia nguvu zote hizo?

Wananchi wa Rombo hawatishwi tena na matumizi ya ngivu kama serikali ilivyokua ikifanya kuwatisha watu kwa kuwapiga na kuwapeleka vijana kwa nguvu maituni kuzima moto katika mlima kilimanjaro

Badala ya serikali kuelimisha wananchi kutunza mazingira na kuwapa wananchi wake haki ili kujenga uzalendo mioyoni mwake wanaona ni afadhali watumie nguvu
 
Baada ya kunyanyaswa na vizuizi vya polisi vilivyomo mji mdogo wa Himo, viliosababsha upungufu mkubwa wa sukari na bidhaa nyingine za chakula, kiasa cha Rombo jimbo linaloongozwa na CDM, na linalopakana na nchi ya Kenya, kujisiakia wageni nchini mwao Tanzania, wamechukizwa na kitendo cha serikali yao ya Tanzania kuwanyanyapaa na wameamua kupandisha bendera ya Kenya! Source ITV

Rombo wana mahusiano mazuri sana na jamii za kenya kuliko za Tanzania.Warombo wamekuwa na unafuu sana kuanza maisha Nairobi kuliko Hata moshi mjini,Mrombo anaweza ona mji wa kwanza kenya kuliko Tanzania,na Bidhaa nyingi watumiazo ni za kutoka Kenya.Warombo wanakodisha mashamba Kenya na kulima huko.

Nadhani ni Kipindi sasa serikali ya majimbo kuanza kufanya kazi, Hizi commands kutoka dar hazina tija kila eneo la Kaskazini.Hazina tija ktk aina ya utalii wetu, rasilimali zetu kama Tanzanite, mila zetu na mengine, Ni vipi ****** atajua haya?Ndio maana anataka Arusha isiwe na mimea.

Watu wa kaskazini kuanzia wameru,waarusha, wachaga huwa hawakai nyumba bila kuwa na miti ya kivuli,amri za dara zinatolewa na watu ambao hawajui jinsi tamaduni za watu wetu nyingi ni tofauti na tajiri sana za ustaarabu.

Im a great fan of greater kilimanjaro , kilimanjaro inajitawala ktk mipango yake ila ibaki kuwa Tanzania, warombo wana wazo zuri ila wamelifanya vibaya.Anyaway kama uamsho wanataka Zenj yao kwanini na wengine wasitake vipande vyao?Ya nini kutawaliwa na watu wasiojua nini mnahitaji na wapi mmefikia?Amri za dar zipo nyuma ya fikra za watu wa sehemu nyingi sana Tanzania,na mwishowe zinarudisha wengine nyuma.Ningependa kama wangebuni bendera yao kwani wangeonyesha kujitawala kuliko kubadili mtawala.
 
Tusitafute njia za mkato.Mbona ilikua rahisi kushulikia madai ya wananchi wa Rombo kuliko kutumia nguvu zote hizo?

Wananchi wa Rombo hawatishwi tena na matumizi ya ngivu kama serikali ilivyokua ikifanya kuwatisha watu kwa kuwapiga na kuwapeleka vijana kwa nguvu maituni kuzima moto katika mlima kilimanjaro

Badala ya serikali kuelimisha wananchi kutunza mazingira na kuwapa wananchi wake haki ili kujenga uzalendo mioyoni mwake wanaona ni afadhali watumie nguvu

Mkuu mimi nakubaliana na wewe....Kwanza tukubaliane kwamba Kama kweli hili tukio limefanyika basi ni Uhaini...
Pili Kuna njia nyingi amabazo ni halali kikatiba amabazo Mtanzania anaweza kuzipitia kufikisha Malalamiko(Maoni).....

Anaweza Kuandamana...anaweza Kufungua Kesi....na mengineyo.....

Lakini Huwezi kufikisha ujumbe kwa Kupandisha bendera ya nchi JIRANI....Huku ni kujidharau na kudharau Wa-Tanzania wengine ....

Nimewahi kuishi na Wakenya ...Ki ukweli Wakenya wana dharau ya Hali ya juu kwa wa-Tanzania,Lakini walikuwa wanakoma Na mimi....

Wa-Tanzania ambao Hawapati huduma za kijamii ni wengi sana.....Kila pande za nchi hii kuna watu wanataabika kuhusu Hospitali,Wajawazito wanakufa Barabarani ,watu hawapati maji ya kunywa ...watu hawana hela ya kununua dawa...shule hakuna...chakula cha Tabu.....

Je hawa wote wapandishe Bendera za Kenya ?
Mimi nimesikia Kuwa Huko kilimanjaro(Rombo) Kuna Maendeleo Kuliko Sehemu nyingi za Tanzania....
Je Wana-Rombo wana Haki zaidi ya Kupandisha Bendera ya Kenya Kuliko Wa-Tanzania wengine ?

Mimi Naunga Mkono harakati zote za Kujiletea Maendeleo...Lakini Siungi Mkono kupandisha Bendera ya nchi Nyengine
Especially Kenya ... angalu wangepandisha ya Rwanda ningeweza Kuvumilia..lakini Kenya...Hapana..Hapana
 
Back
Top Bottom