SIRI PART3: MTUNZI PATRICK CK
JASUSI/GAIDI
SEASON 6 : EPISODE 3
“Abu Zalawi habari za leo”
akasema Vahid baada ya
kufika mahala aliko Mathew
Mulumbi
“Ahsante kwa kuja Vahid
na samahani sana kwa
usumbufu” akasema Mathew
“Usijali Abu
Zalawi.Niambie kitu gani
umeniitia hapa? Akauliza
Vahid akionekana kuwa na
haraka
“Vahid kubwa ambalo
nimekuitia hapa ninataka
kuzungumza na Habiba
Jawad” akasema Mathew
“Hilo tu? Akauliza Vahid
“Ndiyo Vahid ni muhimu
sana” akasema Mathew na
Vahid akachukua simu
akazitafuta namba za Habiba
Jawad akapiga halafu akampa
Mathew simu ambaye alimtaka
Vahid atoke nje ili aweze
kuzungumza na Habiba
“Hallow Vahid” akasema
Habiba Jawad baada ya
kupokea simu
“Ni mimi Abu Zalawi”
akasema Mathew
“Mathew habari yako”
“Nzuri mama.Vipi wewe
unaendeleaje?
“Ninaendelea vizuri.Kuna
nini Mathew hadi ukataka
kuonana na Vahid?
“Nilihitaji kuzungumza
nawe ndiyo maana
nikamtumia ujumbe Vahid
nionane naye”
akasemaMathew
“Vahid hajafurahishwa na
amekuja kuonana nawe kwa
sababu yangu.Kuna nini
unataka kuniambia?
“Ninakaribia kuianza kazi
niliyotumwa kuja kuifanya
lakini ili niweze kuikamilsha
kazi hiyo napaswa kujenga
kwanza mtandao na ili nipate
mtandao natakiwa kufanya
kitu kitakachowafanya
waniamini”
“Unataka kufanya nini
Mathew? Akauliza Habiba
“Ninataka kuwaanika
majasusi wa Mossad walioko
hapa Iran.Serikali ya Iran
inafahamu kuwa kuna
majasusi wa Israel hapa Iran
lakini haiwafahamu ni akina
nani na wako
wapi.Nitakapowafumbua
macho majasusi hao ni akina
nani na wako wapi nitakuwa
nimewasaidia kitu kikubwa
sana hivyo nahitaji msaada
wako katika hilo.Tafuta namna
unavyoweza kufanya ili
kuipata orodha ya majasusi wa
Israel walioko hapa
Iran.Nikifanikiwa kuipata
orodha hiyo itanisaidia
kunikutanisha na viongozi wa
hapa na hapo ndipo
nitakapoanza kazi yangu”
akasema Mathew
“Mathew hilo ni wazo zuri
sana tatizo ni namna ya
kuweza kuipata orodha hiyo ya
majasusi wa Israel walioko
Iran” akasema Habiba
“Mama Habiba wewe una
mtandao mkubwa hata ndani
ya mashirika haya ya kijasusi
hivyo fanya kila
linalowezekana niweze kuipata
hiyo orodha ya majasusi wa
Mossad ikiwezekana leo hii
hii” akasema Mathew
“Sawa nitajitahidi niweze
kuipata na nitakapofanikiwa
nitakujulisha” akasema
Habiba
“Nashukuru sana
mama.Naomba uliwekee uzito
jambo hilo.Vipi kuhusu wale
jamaa kule Marekani? Kuna
taarifa zozote umezipata
kutoka kwao? Akauliza
Mathew
“Mpaka sasa bado sijapata
taarifa zozote kutoka
kwao.Usijali kila
nitakachokipata
nitakujulisha”akasema Habiba
Jawad na ukimya mdogo
ukapita halafu Habiba
akasema
“Mathew kuna jambo
lingine ninataka
kukufahamisha” akasema
Habiba na kunyamaza kidogo
“Hivi tuzungumzavyo
Nawal yuko angani anarejea
Riyadh akitokea Tanzania”
“Nawal alikwenda
Tanzania? Akauliza Mathew
“Ndiyo Mathew.Nawal
alikwenda Tanzania kutekeleza
misheni muhimu
niliyomtuma.G20 walikuwa na
mpango wa kusambaza kirusi
hatari nchini Tanzania kwa
lengo la kuwawezesha kuwepo
Afrika Mashariki kwa muda
mrefu zaidi ili waendelee na
uporaji wa rasilimali.Baada ya
kuufahamu mpango huo
nikamtuma Nawal kwenda
kuuharibu .Nawal
akishirikiana na Ruby na timu
yake wamefanikiwa kuzima
jaribio hilo la kusambaza
kirusi hatari nchini Tanzania
na nchi iko salama” akasema
Habiba
“Nawal amekutana na
Ruby? Akauliza Mathew
“Ndiyo.Amekutana na
Ruby na wameshirikiana
katika misheni hiyo” akasema
Habiba
“Ahsante sana mama
Habiba kwa msaada huu
mkubwa.Naamini bila wewe
kuwa na taarifa hizo hivi sasa
nchi ya Tanzania ingekwisha
ingia katika janga lingine
kubwa la watu kupoteza
maisha.Mama ninazidi kuwa
na hasira na hawa watu na
ninaapa lazima nihakikishe
ninarudi tena Marekani
kuwamaliza.Hawawezi
kutufanyia mambo mabaya
kama haya na wakabaki
salama” akasema Mathew
akiwa amejaa hasira
“Mathew kuna jambo
lingine nataka
kukufahamisha.Nawal anakuja
Tehran”
“Anakuja huku?! Mathew
akashangaa
“Ndiyo anakuja Tehran
kukusaidia” akajibu Habiba
“Hapana mama.Nawal
hapaswi kabisa kuja huku.Hii
ni misheni ya hatari mno
mama.Nawal hapaswi kabisa
kufika hapa! Akasema Mathew
“Mathew hili si
ombi.Nawal anakuja Tehran
kukusaidia.Mathew misheni
hii ni hatari sana na wewe uko
peke yako.Lazima uwe na mtu
anayeweza kukusaidia.Usihofu
hatavuruga misheni yako bali
anakuja ili kukupa msaada
pale itakapohitajika” akasema
Habiba
“Mama sidhani kama hilo
ni wazo zuri kwa sasa”
akasema Mathew
“Mathew kama
nilivyokwambia kwamba hili si
suala la kujadili.Nimekwisha
fanya maamuzi Nawal anakuja
Tehran.Mathew hii ni misheni
kubwa na lazima utahitaji
msaada” akasema Habiba na
kuagana na Mathew
“Kila uchao hasira dhidi ya
watu hawa wanaojiita G20
zinaongezeka.Ninatafakari
adhabu mbali mbali
wanazostahili watu hawa bado
sijapata jibu lakini kitu
nitakachowafanyia kitabaki
katika historia ya
Marekani.Sikujua kama
walikuwa na mpango
mwingine wa kwenda
kusambaza virusi nchini
Tanzania kwa lengo la
kuendeleza uporaji wa
rasilimali zetu.Kule Tanzania
tunasema za mwizi
arobaini.Hawa jamaa
wamefikisha siku ya 39
arobaini yao iko kwenye
kona.Laiti kama wangefahamu
wangeanza kujiandaa kutoka
sasa kwani tufani
inayowakaribia ni kubwa”
akawaza Mathew
“Naamini Nawal atakuwa
amekiacha kirusi hicho
Tanzania.Ninatamani kirusi
hicho kingerejeshwa Marekani
ili kikawaangamize wao
wenyewe lakini hatupaswi
kufanya hivyo kwani
hatutakuwa na tofauti na
wao.Wamarekani hawafahamu
kile kinachoendelea nchini
mwao na hawana habari kama
kuna kikundi kinajiita G20
ambacho kinafanya mambo ya
kikatili kabisa sehemu mbali
mbali duniani hasa barani
Afrika kwa lengo la kupora
rasilimali kama vile mafuta na
madini.Bara la Afrika
limekuwa likigubikwa na
migogoro ya mara kwa
mara.Mapigano ya wenyewe
kwa wenyewe yanaibuka kila
mara katika nchi za Afrika na
ukiichunguza mingi ya
migogoro hiyo ina mkono
wake kutoka nchi hizi kubwa
ambazo zinafaidika kwa
kuchochea migogoro
hiyo.Wanapata soko la kuuza
silaha,wanapora mali nk.Kwa
bahati mbaya sana kuna
waafrika wenzetu ambao kwa
tamaa za mali wamejikuta
wakishirikiana na mabeberu
hawa katika kuwasaliti wenzao
na hata kuchochea
mifarakano.Natamani
niitangazie dunia hata sasa kile
kinachoendelea lakini ngoja
nivute subira nimalize misheni
yangu hapa Iran ili niweze
kupata kibali cha kuingia tena
Marekani kukimaliza kikundi
cha G20” akawaza Mathew na
kukumbuka kuwa alikuwa na
simu ya Vahid.Akaufungua
mlango na kumfuata Vahid
sebuleni alikokuwa amekaa
akizungumza na Faqir
“Nashukuru sana mzee
kwa msaada huu mkubwa”
akasema Mathew Vahid
akaipokea simu ile na
kusimama akamtaka Mathew
wasogee pembeni wazungumze
“Kijana naamini tayari
umemaliza shida yako”
“Ndiyo mzee.Nilihitaji
sana kuzungumza na Habiba
jambo la muhimu”
“Hii ni mara yangu ya
mwisho kufika hapa.Kama
ukihitaji kuzungumza tena na
Habiba tafuta namna nyingine
ya kuwasiliana naye lakini si
kunitumia ujumbe nyumbani
kwangu.Sina mashirikiano
yoyote na magaidi mimi !
akasema kwa ukali Vahid na
kuanza kuondoka akimuacha
Mathew amesimama
akimtazama.
“Sipaswi
kukasirika.Napaswa
kuvumilia.Ninamshukuru hata
hivyo kwa msaada alionisaidia
kuzungumza na Habiba mara
mbili.Kwa sasa ngoja
niendelee kusubiri majibu
kutoka kwa Habiba” akawaza
Mathew na kurejea chumbani
kwake.
WASHINGTON DC –
MAREKANI
Imetimu saa nane za
usiku,bado kikao kizito
kiliendelea katika ikulu ya
Marekani kati ya Rais William
Washington na wakuu wa
vyombo vya ulinzi vya
Marekani.Kikao hicho
kilitokana na taarifa ya
kustusha waliyoipata kutoka
Tanzania kwamba kambi
ndogo ya vikosi vya Marekani
vilivyoko nchini Tanzania
ilivamiwa na watu
wasiojulikana ikashambuliwa
na kuteketezwa kabisa huku
wanajeshi wote waliokuwepo
kambini usiku h uo wakiuawa.
Wakati kikao
kikiendelea,walikuwa
wakipokea taarifa mbali mbali
kutoka kwa makamanda
walioko Tanzania vile vile
waliweza kuonyeshwa moja
kwa moja picha za kambi yao
namna ilivyoharibiwa vibaya
sana na wavamizi.Taarifa
nyingine iliyowastua ni
kwamba kuwa nyumba
aliyokuwa akiishi mkuu wa
vikosi vya Marekani vilivyoko
Tanzania Jenerali William
nayo pia ilivamiwa na watu
wasiojulikana,wanajeshi
kadhaa wakauawa na Jenerali
William haikufahamika
mahala alipo.Jumla ya
wanajeshi waliouawa katika
matukio hayo mawili walikuwa
thelathini na moja.
Saa kumi usiku kwa saa za
Marekani ndipo kikoa
kilipomalizika.Baada ya kikao
kumalizika Rais William
hakwenda kulala alikuwa na
kikao kingine muhimu na
makamu wa Rais.Moja kwa
moja wakaenda katika chumba
cha mazungumzo ya
faragha.Bado Mark Piller
alikuwa anazungumza na mtu
simuni.Baada ya muda
akalazimika kumuomba radhi
mtu yule aliyekuwa
akizugumza naye simuni na
kukata simu.
“Mark nimechanganyikiwa
na hiki kilichotokea !
akaanzisha mazungumzo Rais
William Washington
“Mheshimiwa Rais kweli
hili ni jambo la kustusha mno
lakini tunapaswa tuwe
watulivu wakati tunasubiri
kupata taarifa rasmi nini
kimetokea na nani waliofanya
shambulio hilo” akasema Mark
Piller na ukimya ukapita.
“Mark” akaita Rais
William na Mark Piller
akainua kichwa akamtazama
“Tumetazama namna
kambi ilivyoharibiwa vibaya na
wanajeshi wetu walivyouawa
kikatili.Kwa haraka haraka
picha gani inakujia kuhusu
waliofanya tukio lile? Akauliza
Rais William
“Kwa haraka haraka picha
ninayoipata ni kwamba
wavamizi walifanya shambulio
la kustukiza.Inaonekana
wanajeshi wetu hawakuwa
wakifahamu kama
watashambuliwa.Picha
nyingine ninayoipata wavamizi
walikuwa wamejihami kwa
silaha nzito sana na ndiyo
maana wakaweza kuwaua
wanajeshi wetu” akasema
Mark Piller
“Tutajadili kwa kina sana
jambo hili lakini swali ambalo
linatakiwa kutawala vichwa
vyetu muda huu ni nani
waliofanya shambulio lile na
kwa nini?Unadhani ni…ah !
ninazidi kuchanganyikiwa
Mark” akasema Rais William
na kugonga meza kwa hasira
“Halafu mbona hakuna
maiti hata moja ya watu
waliovamia? Je hakuna hata
mmoja aliyeuawa? Akauliza
William
“Mheshimiwa Rais tukio
hili lina utata
mkubwa.Ukizitazama picha za
sehemu ya tukio ninahisi
wanaoweza kufanya shambulio
kama hili ni watu wenye uwezo
mkubwa na mbinu za hali ya
juu za mapigano.Raia wa
kawaida hawana mafunzo ya
hali ya juu namna hii ya
kuweza kusambaratisha kambi
na kuua wanajeshi wetu wote
wenye uwezo mkubwa katika
mapigano”
“Nini unamaanisha Mark?
“Yawezekana ..”Mark
akasita
“Nini Mark? Kama kuna
kitu unakihisi kiweke wazi !
akasema Rais William
“Ninajaribu kujenga picha
mbali mbali kichwani kwangu
lakini ninashindwa
kuziunganisha.Tusubiri tupate
taarifa kutoka kwa wanajeshi
wetu walioko huko Tanzania
ambao wanaendelea na
uchunguzi watatupa picha
nzuri zaidi” akasema Mark
“Mark tuliweke kwanza
pembeni suala hilo nimetaka
tuje hapa tuzungumze
kuhusiana na ule mpango
wenu wa kusambaza kirusi”
akasema Rais William na Mark
akavuta pumzi ndefu
“Mheshimiwa Rais,muda
mwingi wa kikao nilikuwa
nazungumza na simu
nikiwasiliana na wenzagu ili
tufahamu
kinachoendelea.Taarifa si
nzuri hata kidogo” akasema
Mark na sura ya Rais William
ikaonesha mstuko
“Kuna nini kimetokea?
Akauliza
“Kwa taarifa nilizopewa na
wenzangu wanaoendelea
kufuatilia suala hili ni kwamba
mtu tuliyemtuma kwenda
kusambaza kirusi alifika
salama Dar es salaam na
alikabidhiwa kwa Jenerali
William ambaye ndiye
atakayeratibu zoezi zima la
usambazaji akisaidiana na
Assad Ismail kutoka IS.Taarifa
ya kuvamiwa kwa nyumba
anamoishi Jenerali William na
wanajeshi waliokuwa
wakilinda nyumba hiyo
kuuawa na Jenerali William
kutoweka kinaleta wasiwasi
mkubwa sana kuhusu ule
mpango wetu wa kusambaza
kirusi” akasema Mark Piller na
ukimya ukatawala tena
“Huyo mtu wenu wa IS
anapatikana simuni? Akauliza
Rais William
“Hapatikani” akajibu Mark
Piller
“Mark kuna wazo linanijia
japo sijui kama lina msingi
wowote.Hudhani kama watu
wa IS wanaweza kuwa
wamehusika katika shambulio
hili? Akauliza Rais William
“IS? Akauliza Mark Piller
“Ndiyo.Hudhani kama
wanaweza kuwa wamehusika
katika jambo hili?
“IS hawawezi kuhusika
kabisa katika shambulio hili
kwa sababu tunashirikiana nao
na tunawalipa pesa nyingi sana
vile vile tunawawezesha kwa
silaha na mambo mengine
kadhaa” akasema Mark Piller
“Nimejiwa na wazo hilo
kwa sababu yawezekana labda
IS wakawa wanakihitaji hicho
kirusi na wakaamua kufanya
shambulio hilo ili wakichukue
na kukitumia katika mambo
wanayoyajua wenyewe”
akasema Rais William
“Hilo unalosema
mheshimiwa Rais
linawezekana lakini hawa
jamaa tumekuwa
tunashirikiana nao kwa muda
mrefu.Hawawezi kutufanyia
hivi” akasema Mark Piller
“Kama si wao basi nani
aliyefanya shambulio lile?
Akauliza Rais William
“Mheshimiwa Rais kwa
sasa tunahangaika kujua
mahala alipo Jenerali
William.Yeye ndiye
anayefahamu mahala kilipo
kirusi na akipatikana basi
tutafahamu kila kitu” akasema
Mark Piller
“Mark hebu nisaidie
mawazo nini tufanye? Mimi
nimechanganyikiwa hapa”
akasema William
“Rais wa Tanzania
umekwisha zungumza naye?
Akauliza Mark Piller
“Hapana bado
sijazungumza naye”
“Zungumza na Rais wa
Tanzania yawezekana akawa
na taarifa ambazo sisi hatuna
kuhusiana na shambulio
hili.Naamini vyombo vya ulinzi
na usalama vya Tanzania
navyo vinalichunguza jambo
hili na yawezekana tayari
wamepata fununu Fulani
kuhusu nani waliofanya
shambulio hilo” akasema Mark
na simu yake nyingine ambayo
huiweka katika mfuko wa koti
ikaita akaitoa mfukoni
akatazama mpigaji alikuwa ni
Habiba Jawad.Rais William
akamtazama kwa macho ya
udadisi
“Ni Habiba Jawad” Mark
akamwambia Rais kisha
akaipokea ile simu
“Hallow Habiba”
“Mark habari za usiku
huu.Samahani kwa
kukuamsha kama ulikuwa
umelala” akasema Habiba
“Hapana sijalala.Usiku
mzima wa leo umekuwa ni wa
vikao mfululizo.Naamini
umepata taarifa za kile
kilichotokea nchini
Tanzania.Kambi yetu
imeteketezwa na wanajeshi
wengi wameuawa.Ni
shambulio baya kabisa”
akasema Mark Piller
“Tayari nimekwisha zipata
taarifa hizo.Poleni sana kwa
tukio hilo baya.Tayari
mmekwisha fahamu nani
waliofanya shambulio hilo?
Akauliza Habiba
“Mpaka sasa
haijafahamika nani waliofanya
tukio hilo.Habiba tukio hili
limeathiri pia ule mpango
wetu wa kusambaza kirusi”
akasema Mark Piller na
kunyamaza kidogo
“Sattar Sayf Al Din alifika
Tanzania na alipokewa na
mkuu wa vikosi vya Marekani
anaitwa Jenerali William
ambaye ndiye tuliyemkabidhi
jukumu la kumsaidia Sattar
katika mpango wa kusambaza
kirusi hicho.Nyumba anayoishi
Jenerali William nayo pia
imevamiwa na watu
wasiojulikana walinzi wake
wameuawa na yeye mwenyewe
ametoweka hajulikani mahala
alipo.Yeye ndiye mwenye
taarifa zote kuhusiana na
kirusi.Tumekwama na
tunaendelea kusubiri kama
Jenerali William atapatikana
ili tujue kuhusiana na kirusi
kama kiko salama” akasema
Mark Piller
“Vipi kuhusu Assad Ismail
naye pia hapatikani simuni?
Yeye pia alikuwa anategemewa
kumsaidia Sattar katika
usambazaji wa kirusi hicho”
“Assad naye hapatikani
simuni.Hili jambo
linatuchanganya sana Habiba”
“Kama wote hawapatikani
yawezekana wako sehemu
salama wamejificha na
watajitokeza baada ya muda
kupita.Au tayari wako katika
usambazaji wa kirusi” akasema
Habiba
“Hapana Habiba hilo
haliwezekani.Jenerali William
ndiye mkuu wa vikosi vya
Marekani kama angekuwa
amejificha sehemu hadi muda
huu ambao inakaribia saa tano
za asubuhi nchini Tanzania
angekuwa amekwisha jitokeza
lakini hadi sasa hajulikani
alipo.Hii inaongeza wasiwasi
zaidi na kikubwa tunachotaka
kukifahamu ni kama kirusi
kiko salama.Mtu pekee
ambaye anazo taarifa zote za
kuhusiana na kirusi hicho ni
Jenerali William” akasema
Mark Piller
“Mmejiridhisha katika
miili iliyopatikana hakuna
mwili wa Jenerali William au
Sattar au Assad? Akauliza
Habiba
“Hakuna mwili wa Jenerali
William wala hao
wengine.Kukosekana kwa miili
hiyo katika orodha ya
waliouawa inatupa picha
kwamba yawezekana wakawa
hai.Swali ni je wako wapi?
Akauliza Mark Piller
“Kama miili yao
haijapatikana miongoni mwa
wale waliopoteza maisha basi
kuna uwezekano mkubwa
wakawa hai.Ninaamini
watakuwa amejificha sehemu
Fulani na baada ya muda
watajitokeza au yawezekana
tayari usambazaji wa kirusi
umeanza” akasema Habiba
“Tuliweke hilo pembeni
Habiba tunaendelea
kulifuatilia.Nini sababu ya
kunipigia simu? Akauliza Mark
Piller
“Nimekupigia simu
kuhusiana na ile misheni
anayoendelea nayo Abu Zalawi
kule Tehran” akasema Habiba
“Nini kinaendelea huko?
Kuna taarifa yoyote nzuri?
Akauliza Mark
“Nimewasiliana na Abu
Zalawi nikampa taarifa
kuhusiana na ule mpango
wake wa kumuua.Kuna kitu
ameniomba nimsaidie”
“Safi sana Habiba.Ahsante
kwa kumfikishia taarifa hiyo
kwa haraka.Amekuomba
umsaidie nini? Akauliza Mark
Piller
“Abu Zalawi anataka
kuanza kuifanya kazi yake kwa
kujenga mtandao nchini
Iran.Kuna kitu anakihitaji
ambacho kitamsaidia katka
mpango huo” akasema Habiba
“Sema Habiba,Abu Zalawi
anahitaji kitu gani? Akauliza
Mark Piller
“Anahitaji orodha ya
majasusi wa Mossad walioko
nchini Iran” akasema Habiba
“Anahitaji orodha ya
majasusi wa Mossad?! Mark
Piller akashangaa
“Ndiyo Mark.Anaihitaji
orodha hiyo ya majasusi wote
wa Mossad haraka” akasema
Habiba na Mark Piller akavuta
pumzi ndefu
“Hilo ni jambo
lisilowezekana
Habiba.Hatuwezi kuipata
orodha hiyo ya majasusi wa
Mossad.Hata kama tungeweza
kuipata orodha hiyo hatuwezi
kuitoa kwa mtu yeyote kwa
sababu kwa kufanya hivyo
tutakuwa tumehatarisha
usalama wa majasusi hao
kwani watajulikana na
wanaweza kuuawa” akasema
Mark Piller
“Mark kwa namna yoyote
ile lazima orodha hiyo
ipatikane.Abu Zalawi
anaihitaji mno ili kuweza
kujenga mtandao.Hii ni
misheni kubwa na lazima
kufanya kila linalowezekana ili
ifanikiwe.Abu Zalawi anahitaji
kujenga mahusiano na
viongozi wa Iran na orodha
hiyo ndiyo itakayomfanya
aaminiwe na awe na
mahusiano mazuri na
viongozi.Mark ninakuomba
fanya kila uwezalo kuhakikisha
orodha hiyo inapatikana tena
kwa haraka” akasema Habiba
“Habiba narudia tena
kusema kwamba hilo ni jambo
lisilowezekana kabisa.Hakuna
namna ninayoweza kuipata
orodha hiyo ! akasema Mark
Piller
“Mark umewasaliti
wenzako ili misheni ya Abu
Zalawi ikamilike hivyo ni
wajibu wako kuhakikisha
unafanya kila linalowezekana
ili misheni hii
ikamilike.Usiogope kuwaanika
majasusi wa Mossad kwani
kitakachopatikana katika
misheni hii ni kikubwa na kina
umuhimu pia hata kwa Israel
kwani hata wao wamekuwa
wakipokea vitisho vya
mashambulio kutoka kwa
Iran.Mark hii ni nafasi
imepatikana hivyo usiiache
ikapotea bure.Kila
atakachokihitaji Abu Zalawi
anatakiwa akipate ! akasema
Habiba.Mark Piller akafikiri
kidogo na kusema
“Habiba siwezi kukuahidi
chochote kwa sasa.Naomba
unipe muda nilifanyie kazi
jambo hili” akasema Mark
“Mark suala hili ni la leo
hii hii halihitaji kuchukua
muda mrefu”
“Sawa Habiba,nitakupa
majibu baadae kidogo.Naomba
unipe muda nione
ninavyoweza kufanya”
“Sawa Mark
ninakutegemea”
“Habiba tukiliweka hilo
pembeni kuna jambo nataka
tuzungumze na yawezekana
unaweza ukatusaidia kupata
jawabu”
“Nini unahitaji Mark?
“Tumetazama picha za
eneo la tukio limeharibiwa
vibaya mno na waliofanya
shambulio hilo lazima
watakuwa ni watu waliojihami
kwa silaha nzito.Tunahisi
yawezekana kundi la IS
limehusika katika shambulio
hili”
“IS? Habiba akashangaa
“Ndiyo” akajibu Mark
“IS wamekuwa
wakishirikiana nanyi na wao
ndio waliotakiwa kusambaza
kirusi.Iweje wabadilike na
kufanya shambulio?
“Tunahisi labda walikuwa
wanakitaka kirusi” akajibu
Mark Piller
“Hapana Mark.Sina hakika
kama IS wanaweza wakafanya
jambo kama hilo”
“Habiba hatujasema
kwamba IS wamefanya hilo
shambulio ila tunahisi
kwamba yawezekana wakawa
wanahusika.Tunataka
utusaidie kufanya uchuguzi
kujua kama wamehusika na
kama wamehusika kirusi kiko
wapi? Akasema Mark Piller
“Mark nitafanya
uchunguzi huo kujua kama
kweli wamehusika kwa namna
yoyote na shambulio hilo
nikipata chochote
nitakujulisha” akasema
Habiba
“Tunashukuru sana
Habiba.Tunatakiwa kusaidiana
kuhakikisha tunakipata kirusi”
akasema Mark Piller na
kuagana na Habiba Jawad
“Nilikuwa nazungumza na
Habiba Jawad.Nimemuomba
atusaidie kufanya uchunguzi
kufahamu kama IS
wanahusika kwa namna yoyote
na tukio la Dar es salaam”
Mark akamwambia Rais
William
“Amesemaje ulipomtaka
afanye uchunguzi huo?
“Amekubali kufanya
uchunguzi huo na atanijulisha
kile atakachokuwa
amekipata.Hata hivyo
dhumuni kuu la kunipigia ni
kunipa taarifa za maendeleo ya
misheni ya Abu Zalawi”
akasema Mark Piller na rais
William aliyekuwa amegeukia
ukutani akageuka haraka
“Anaendeleaje Abu
Zalawi? Akauliza Rais William
“Abu Zalawi tayari yuko
Tehran na taarifa ya mpango
wa kuuawa imekwisha mfikia”
“Vizuri”akasema William
“Abu Zalawi anajiandaa
kuianza kazi yake lakini kuna
kitu anakihitaji ambacho ni
kigumu kidogo”
“Anataka nini? Akauliza
Rais William
“Anataka apatiwe orodha
ya majasusi wa Mossad
walioko nchini Iran” akasema
Mark
“Anataka orodha hiyo
aifanyie nini? Akauliza Rais
Wiliam
“Anataka awaanike kwa
serikali ya Iran”
“Kwa nini anataka kufanya
hivyo? Hajui kwa kufanya
hivyo majasusi hao watakuwa
katika hatari kubwa ya
kuuawa? Iran na Israel hazina
mahusiano mazuri hivyo
wakiwagundua majasusi wa
Israel walioko nchini Iran
watawaua wote.Hilo ni jambo
la hatari kabisa Mark”
“Ni kweli mheshmiwa
Rais, ni jambo la hatari kubwa
kwa majasusi hao lakini Abu
Zalawi anataka kuitumia
orodha hiyo kwa ajili ya
kutengeneza mtandao.Kwa
kuwapa Iran orodha hiyo ya
majasusi wa Israel anaamini
kwamba watamuamini na
kumuweka karibu zaidi”
akasema Mark Piller
“Bila orodha hiyo ya
majasusi wa Israel hataweza
kuendelea na kazi aliyotumwa?
Akauliza Rais William
“Kwa mujibu wa Habiba
Jawad ni kwamba Abu Zalawi
anadai orodha hiyo ni muhimu
sana aipate tena leo hii hii”
akajibu Mark Piller.Rais
William akatafakari kidogo
halafu akauliza
“Wewe una maoni gani
Mark juu ya suala hilo?
“Tumefanya maamuzi
kwamba Abu Zalawi aendelee
na misheni yake hivyo lazima
tuhakikishe tunamsaidia kwa
kila iwezekanavyo ili aweze
kufanikisha misheni hiyo
muhimu.Hatuna namna
mheshimiwa Rais lazima
tuhakikishe tumeipata orodha
hiyo na kumpatia Abu Zalawi”
akasema Mark Piller
“Lakini Mark kwa kufanya
hivyo tutakuwa tumehalalisha
majasusi wa Israel
wauawe.Iran hawatawaacha
salama”
“Mheshimiwa Rais hapa
tumebanwa katika kona
hatuna namna ya kufanya zaidi
ya kumpatia Abu Zalawi hicho
anachokitaka.Tayari damu
nyingi imekwisha mwagika
hadi hapa tulipofika hivyo
hakuna tatizo kama tukiwatoa
sadaka majasusi hao wachache
wa Mossad ili tuweze
kufanikisha lengo letu.Endapo
misheni hii ikifanikiwa
itakuwa na msaada mkubwa
pia hata kwa Israel yenyewe
ambayo imekuwa ikipokea
vitisho vya kushambuliwa na
Iran” akasema Mark Piller
“Mark hili jambo
linanitatiza sana .Kwanza ni
namna ya kuweza kupata
orodha hiyo na pili hata kama
tukifanikiwa kuipata orodha
hiyo tukampa Abu Zalawi na
majasusi wa Israel wakauawa
ni vipi kama Israel ikigundua
kwamba sisi ndio tuliotoa
orodha hiyo kwa Iran? Hili
jambo linaweza kuleta
mtafaruku mkubwa sana kati
ya nchi zetu” akasema Rais
William
“Mheshimiwa Rais
naomba nikutoe hofu kuhusu
jambo hili.Kwanza kuhusu
kuipata orodha hiyo tunaweza
kuipata.Si jambo gumu sana
kuipata orodha hiyo.Nikiamua
kuipata siwezi
kushindwa.Kuhusu wasiwasi
kwamba Israel wanaweza
wakagundua sisi ndio
tuliowaanika majasusi wao
kwa Iran hilo haliwezi kutokea
kwa sababu Iran hawajui kama
tunashirikiana na Abu Zalawi
na Israel hawatajua chochote
kama sisi ndio tuliowaanika
majasusi wao kupitia kwa Abu
Zalawi.Nakuhakikishia
mheshimiwa Rais kwamba
orodha hiyo itapatikana kwa
namna ambayo Mossad
hawataweza kugundua
chochote”
“Una uhakika Mark?
“Naomba uniamini
mheshimiwa Rais.Jambo hili
litafanywa kitaalamu sana na
halitakuwa na madhara yoyote
kwetu” akasema Mark Piller
“Mark kama una uhakika
jambo hilo linawezekana na
halitakuwa na madhara yoyote
kwetu fanya hivyo
tafadhali.Tunahitaji mno
misheni hii ikamilike na kwa
kuwa tumekwisha kubali
kufanya kila linalowezekana ili
misheni hii ifanikiwe hatuna
namna,hakikisha Abu Zalawi
anapata kila anachokihitaji ili
mradi tuwe na umakini
mkubwa sana ili mambo haya
yasije yakatuletea tena
mgogoro mwingine mkubwa
na washirika wetu kama
Israel” akasema Rais William
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais.Ninakuahidi
hakuna kitakachoharibika.Kila
kitu kitakwenda vizuri”
akasema Mark Piller na
ukimya mfupi ukapita
“Mark kuna jambo lingine
nataka tushauriane.Tayari
imekwisha fahamika kwamba
ndege ile ya Marekani ambayo
ilidhaniwa imeangukia
baharini,imeelekea Iran.Waziri
wa mambo ya nje anajiandaa
kutoa tamko mapema asubuhi
kuitaka Iran irejeshe ndege
yetu pamoja na raia wake wote
waliokuwamo ikiwamo
mtuhumiwa wa ugaidi Abu
Zalawi.Unaonaje mpango huo?
Hautaweza kuvuruga misheni
ya Abu Zalawi? Akauliza Rais
William
“Hapana mheshimiwa
Rais hautaweza kuvuruga
misheni ya Abu Zalawi.Hata
Iran wanajua tumekwisha
fahamu ndege yetu imeelekea
nchini kwao.Tukikaa kimya
watakuwa na wasiwasi kwa
nini tumekuwa kimya?
Muache waziri wetu wa
mambo ya nje atoe tamko lake
hapo asubuhi tena liwe ni
tamko kali kabisa” akasema
Mark Piller
“Hudhani baada ya tamko
hilo,Iran wanaweza
wakamfukuza Abu Zalawi au
wakamtaka aondoke kimya
kimya hivyo misheni yetu
ikashindwa kufanikiwa?
Akauliza Rais William
“Iran hawawezi kwa
namna yoyote ile
wakamfukuza au kumuondoa
Abu Zalawi nchini kwao.Ni
mtu muhimu kwao kwanza
amewakombia watu wao
muhimu ambao naamini
walikwisha wasahau na
kuamini wameuawa,pili
atakuwa na umuhimu mkubwa
zaidi kwao pale atakapo
wakabidhi orodha ya majasusi
wa Israel walioko nchini Iran”
akasema Mark Piller
“Ahsante kwa ushauri huo
Mark lakini lazima
nizungumze na Rais wa
Tanzania nijue wamefikia wapi
katika uchunguzi na vile vile
nataka kufahamu kuhusu
Jenerali William” akasema
Rais William na kuchukua
simu yake yenye namba za
simu za marais wote wa dunia
akazitafuta namba za Rais wa
Tanzania akampigia.
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Habari kuu iliyotawala
vinywani mwa watu jijini Dar
es salaam,Tanzania nzima na
dunia kwa ujumla ni
shambulio lililofanywa usiku
na watu wasiojulikana katika
kambi ndogo ya vikosi vya
jeshi la Marekani iliyoko
kandoni mwa bahari jijini Dar
es salaam.Jambo hili lilizusha
hofu kubwa miongoni mwa
wakazi wa jiji la Dar ambalo
kwa siku mbili hakukuwa na
vurugu zozote zilizoripotriwa
na taratibu hali ya maisha
ilianza kurejea na kuwa ya
kawaida.Watu walianza
kuondoka katika makambi
yaliyokuwa yametengwa kwa
ajili ya kuwahifadhi watu
waliokuwa wanakimbia
mapigano na kurejea katika
majumba yao.Baadhi ya
masoko na maduka makubwa
yalianza kufunguliwa japo
yalikuwa chini ya ulinzi mkali.
Rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr
Fabian Kelelo akiwa ofisini
kwake alimaliza mazungumzo
na mkuu wa jeshi la polisi
nchini kuhusiana na hali halisi
ya usalama ilivyo katika jiji la
Dar es salaam na katika miji
mingine hasa Tanga.
“Nashukuru sana kwa hali
ya amani kuimarika kwa kiasi
kikubwa.Hii inachangiwa
kwanza na watanzania
kutokuzoea mambo haya ya
mapigano ya wenyewe kwa
wenyewe na vile vile kitendo
cha SNSA kuwakamata
magaidi waliokuwa
wanachochea vurugu hizi
kimechangia sana kwa vurugu
kukoma.Ruby na wenzake
wamefanya kazi kubwa sana”
Akawaza Dr Fabian ambaye
alitolewa mawazoni baada ya
simu yake kuita.Akaichukua
kutazama mpigaji alikuwa ni
Rais wa Marekani.Dr Fabian
akavuta pumzi ndefu
“Kazi imeanza” akasema
kwa sauti ndogo na kuipokea
simu ile
“Hallo mheshimiwa Rais
William habari za muda huu?
Naamini ni usiku mwingi huko
kwenu”
“Ni kweli mheshimiwa
Rais Dr Fabian,ni usiku
mwingi hapa Marekani lakini
bado tunaendelea na kazi.Vipi
hapo Dar es salaam
mnaendeleaje?
“Sisi tunaendelea vizuri
japo usiku wa kuamkia leo
kumetokea tukio baya ambalo
naamini tayari umekwisha
pata taarifa zake”
“Suala hilo ndilo
limenifanya nikupigie simu Dr
Fabian” akasema William na
kunyamaza kidogo
“Sikuweza kukupigia simu
kwa haraka mara tu baada ya
kupata taarifa za tukio hilo
kwani tumekuwa na mfululizo
wa vikao kujaribu kulitafakari
shambulio hilo na kupata
taarifa kutoka kwa
makamanda wetu walioko
hapo Dar es
salaam.Tumeonyeshwa picha
za tukio tumesikitishwa mno
na jambo hili.Kabla
sijaendelea zaidi naamini
vyombo vyako vya ulinzi na
usalama viliingia kazini
kuanzia muda lilipotokea
shambulio hilo,mmefikia wapi
hadi sasa katika kuwafahamu
waliofanya shambulio hilo?
Akauliza Rais William
“Mheshimiwa Rais kwanza
kabisa ninapenda kutumia
nafasi hii kutoa pole nyingi
sana kwako na kwa wananchi
wa Marekani kwa hiki
kilichotokea na kuwapoteza
wanajeshi wengi.Ni tukio baya
sana na
halivumiliki.Wanajeshi hao
walikuwepo hapa nchini kwa
ajili ya kulinda amani na
hawakustahili haya
yaliyowakuta” akasema Dr
Fabian na kunyamaza kidogo
“Mara tu baada ya kupata
taarifa za shambulio hilo,vikosi
vya jeshi la wananchi wa
Tanzania vilivyokuwa doria
vilifika eneo la tukio kwa
haraka sana lakini tayari
wavamizi hao walikwisha
ondoka.Shughuli za uokozi
kujaribu kutafuta majeruhi
zilianza mara moja lakini
hawakufanikiwa kumpata
yeyote aliye hai.Nilitoa
maelekezo usiku huo huo
kwamba msako uanze haraka
sana kuwatafuta wale
waliofanya shambulio hilo na
mpaka sasa vyombo vyetu vya
uchunguzi vikishirikiana na
wataalamu wa jeshi la
Marekani walioko hapa
wanaendelea na uchunguzi wa
jambo hili na watatupa taarifa
rasmi pale watakapokuwa
wamefanikiwa kugundua
chochote.Ni msiba mkubwa
sana mheshimiwa Rais”
akasema Dr Fabian
“Dr Fabian utanisamehe
kwa hili nitakalolisema lakini
nitalazimika kutuma vyombo
vya uchunguzi kutoka
Marekani kuja kuwatafuta
watu waliofanya shambulio
hilo.Tunahitaji kujua kwa
haraka sana nani
walioshambulia kambi yetu na
kuua wanajeshi wetu” akasema
Rais William
“William hakuna haja ya
kutuma wachunguzi kutoka
Marekani.Tanzania ina
vyombo vya uchunguzi vyenye
ujuzi na weledi mkubwa sana
nina uhakika mkubwa
waliofanya tukio hili
watapatikana hata kama
haitakuwa mapema kama
unavyotaka lakini lazima
watapatikana” akasema Dr
Fabian
“Dr Fabian Marekani tuna
vyombo vyenye uwezo
mkubwa sana na nina imani
ndani ya muda mfupi
watakuwa wamegundua nani
waliofanya tukio hi…..”
“Mheshimiwa Rais
William nina imani na vyombo
vyangu vya ndani hivyo
uchunguzi wa suala hili
utafanywa na vyombo vya
uchunguzi vya Tanzania na
sintaruhusu wachunguzi
wowote wa kutoka nje”
akasema Dr Fabian
“Dr Fabian una historia ya
kutoruhusu wachunguzi
kutoka nje ya nchi yako pale
kunapotokea shambulio baya
katika nchi yako likilenga mali
au watu wa kutoka mataifa ya
kigeni hata kama vyombo vya
uchunguzi vya nchi yako
havina uwezo wa kutosha
kulifanyia uchunguzi jambo
hilo.Tulioshambuliwa ni sisi
na tunataka kushirkiana na
vyombo vyenu katika
kuwatafuta waliotufanyia
hivi.Ugumu uko wapi?
Akauliza Rais William
“Rais William kwanza
nakuomba ufute kauli yako ya
kwamba vyombo vya Tanzania
havina uwezo wa kutosha !
akasema kwa ukali Dr Fabian
“Huo ni ukweli Dr Fabian
kama kweli vyombo vyako
vingekuwa na uwezo mkubwa
mpaka hivi sasa tayari
mngekwisha fahamu nani
walioshambulia kambi yetu !
mkuu wa vikosi vya Marekani
hapo Tanzania Jenerali
William nyumba yake pia
imevamiwa, wanajeshi
waliokuwa wanamlinda
wameuawa na hadi sasa
Jenerali William hajulikani
alipo na vyombo vyako
vimekuwa vikichunguza toka
usiku hadi muda huu na bado
hamna hata fununu za nani
wameshambulia na kuua watu
wetu.Huu ni udhaifu mkubwa
wa vyombo vyako Dr Fabian..”
akasema Rais William
“Rais William sintavumilia
dharau hizo dhidi ya vyombo
vyangu vya uchunguzi.Narudia
tena kukuhakikishia kwamba
tukio hilo limetokea katika
ardhi ya Tanzania na
litachunguzwa na vyombo vya
Tanzania.Hakuna chombo
chochote cha uchunguzi
kutoka nje kitakachoruhusiwa
kuingilia uchunguzi
unaofanywa na vyombo vya
Tanzania ! akasema kwa ukali
Dr Fabian
“Dr Fabian sielewi kwa
nini unapata kigugumizi katika
jambo hili.Au kuna kitu hutaki
kijulikane? Akauliza Rais
William
“Vyovyote utakavyofikiria
William lakini narudia tena
kauli yangu kwamba
uchunguzi wa shambulio
katika kambi ya wanajeshi wa
Marekani utafanywa na
vyombo vya uchunguzi vya
Tanzania pekee.Pale
uchunguzi utakapokuwa
umekamilika basi tutawapeni
taarifa nani waliohusika katika
shambulio hilo.Mheshimiwa
Rais kama hauna jambo
lingine la kuzungumza zaidi ya
hili ninaomba nikuache nina
kikao muhimu kinanisubiri”
akasema DrFabian
“Ni hilo tu kwa sasa Dr
Fabian nitawasiliana nawe
tena baadae saa kumi na mbili
kwa saa za Afrika mashariki
nifahamu kama mmekwisha
wafahamu waliofanya
shambulio hilo na kama
Jenerali William amepatikana
! akasema Rais William na
kukata simu
“Mataifa haya makubwa
yana dharau sana mataifa
kama yetu kwamba hatuwezi
chochote katika masuala ya
ulinzi na usalama.Ninaamini
muda si mrefu sana
tutawaumbua na hawataamini
macho yao ! akawaza Dr
Fabian na kuchukua simu
akampigia Ruby
“Ruby uko wapi?
Niliwataka mje hapa ikulu
baada ya kutoka uwanja wa
ndege” akasema DrFabian
“Tumekaribia mheshimiwa
Rais ndani ya dakika chache
tutakuwa hapo” akajibu Ruby
“Fanyeni haraka nina
vikao vingi siku ya leo.Kuna
masuala ya msingi nataka
kuzungumza nanyi” akasema
Dr Fabian
“SNSA walifanya kazi
nzuri sana kwani mpaka sasa
hakuna hata fununu za nani
waliofanya shambulio lile kwa
mujibu wa mkuu wa jeshi la
polisi.Kinachofuata ni
kuviondoa vikosi vya Marekani
hapa nchini bila wao kujua
kama tayari tumefahamu
kinachoendelea nyuma ya
pazia.Ninajilaumu sana kwa
kukubali haraka haraka
msaada wao lakini sikujua
kama walikuwa na ajenda yao
iliyojificha” akaendelea
kuwaza
Ruby na Gosu Gosu
waliwasili ikulu kuonana na
Rais.Siku zote Dr Fabian
azungumzapo na akina Ruby
hupenda kutumia chumba cha
mazungumzo ya faragha ili
kuzuia mtu mwingine asiweze
kusikia mazungumzo yao.
“Poleni sana naamini
hamjapata muda wa
kupumzika kutokana na kazi
kubwa mliyokuwa
nayo.Msichoke vijana wangu
hadi pale tutakapohakikisha
tumewaondoa mabeberu hawa
nchini kwetu na Afrika
Mashariki kwa ujumla”
akasema Dr Fabian
“Hatujachoka mheshimiwa
Rais na hatuwezi kuchoka hadi
pale tutakapohakikisha beberu
wa mwisho ameondoka katika
nchi yetu hivyo tutaendelea
kukesha macho kupigania nchi
yetu” akajibu Ruby
“Mungu anaipenda sana
nchi yetu na ndiyo maana
ameweza kuwaumbua wabaya
wetu na tumeweza kuifahamu
mipango yao miovu dhidi
yetu.Muda mfupi uliopita
nimezungumza na Rais wa
Marekani .Alitaka kufahamu
kama tayari tumekwisha
wapata waliofanya shambulio
lile nikamjibu vyombo vya
uchunguzi viko kazini
vinaendelea kuwatafuta akadai
atatuma timu ya wachunguzi
kutoka Marekani kuja nchini
kuchunguza tukio hilo lakini
nilimkatalia nikamwambia
kwamba tukio hili
litachunguzwa na vyombo vya
ndani hakuna mtu kutoka nje
ya Tanzania atakayeruhusiwa
kuja kuchunguza kitu chochote
hapa nchini.Mazungumzo yetu
hayakuisha vizuri kwani alitoa
dharau kwa vyombo vyetu
kwamba havina ujuzi mkubwa
lakini pamoja na dharau hizo
nimesimamia msimamo
wangu kwamba hakuna
mchunguzi kutoka nje ya nchi
ataingia hapa nchini”
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais kwa
maamuzi hayo” akasema Ruby
“Nilitamani nimweleze
ukweli kwamba tumekwisha
fahamu kile wanachotufanyia
lakini nikajizuia kutomweleza
chochote kwa sasa hadi pale
mambo yote yatakapokuwa
yamekamilika.Nawapongeza
mlifanya kazi nzuri kwani hadi
sasa hakuna hata dalili za
kuwafahamu nani waliofanya
shambulio katika kambi
yao.Baada ya tukio la jana
nataka kufahamu nini
kinafuata? Akauliza Dr Fabian
“Tunao watu muhimu
tunawashikilia ambao
tutaendelea kuwahoji ili
kuupata mtandao mzima
uliohusika kuchochea vurugu
za kidini zilizopelekea vifo vya
watu wengi hapa
nchini.Tunaye Jenerali
William na vile vile tunaye
Assad Ismail.Kupitia kwao
tutawafahamu watu wote
waliokuwa wanashirikiana
nao”akajibu Ruby
“Nataka kufahamu hatima
ya huyu Jenerali William
kwani tayari amekwisha
julikana ametoweka na
wanamtafuta.Mnadhani
kuendelea kumshikilia
hakutakuwa na madhara
yoyote kwetu?
“Huyu jamaa tutaendelea
kumshikilia na atatusaidia
kutoa ushahidi wa kile
ambacho alitumwa kuja
kukifanya hapa Tanzania na
Afrika Mashariki.Ni mtu
muhimu sana ambaye
hatuwezi kumuachia kwa
sasa.Huyu ni mmoja wa watu
waliochangia katika
machafuko yaliyotokea hapa
nchini.Atakiri kila kitu”
akasema Ruby
“Huyu ni mwanajeshi mna
uhakika anaweza akakubali
kufunguka na kutoa siri za
nchi yake? Akauliza Dr Fabian
“Usihofu mheshimiwa
Rais atafunguka na kueleza
kila kitu.Tutatumia kila mbinu
kuhakikisha anafunguka”
akajibu Gosu Gosu
“Vizuri sana.Hili jambo
linatakiwa lifanyike haraka ili
tuwafahamu watu ambao
wamekuwa wakishirikiana nao
hapa nchini,tuwakamatwe
haraka kabla hawajatoroshwa
ili kuharibu ushahidi” akasema
Dr Fabian
“Tutafanya hivyo
mheshimiwa rais” akasema
Ruby
“Jambo lingine.Jana
tulizungumza kuhusu namna
ya kuviondoa vikosi vya
Marekani hapa nchini na
tulikubaliana kwamba
tuwaondoe kimya kimya kwa
kukata kile ambacho
wamekifuata yaani
mafuta.Damu yote hii
iliyomwagika ya waganda na
watanzania ni kwa sababu ya
mafuta hivyo pale
watakapoyakosa hawatakuwa
na sababu ya kuendelea
kuviweka vkosi vyao hapa
Tanzania na Uganda
wataviondoa mara
moja.Tulikubaliana kulipua
sehemu ya bomba la mafuta”
akasema Dr Fabian na
kufungua droo ya kabati
akatoa karatasi kubwa
akaiweka mezani.Ilikuwa ni
ramani ya bomba la mafuta
kutoka nchini Uganda hadi
Tanga Tanzania.
“Hii ndiyo ramani ya
bomba la mafuta kutokea
Uganda hadi
Tanga.Ninawakabidhi ninyi
jukumu hili.Mtaipitia ramani
hii na kuchagua sehemu
ambapo mtalipua sehemu ya
bomba.Kazi hiyo nataka
ifanyike usiku wa leo.Sitaki
hadi asubuhi ya kesho
Marekani waendelee kuchota
mafuta kwani baada ya kulipua
kipande hicho mafuta
yatafungwa na wamarekani
hawatapata kitu tena hivyo
hawatakuwa na sababu ya
kuendelea kuwepo hapa
nchini.Nadhani mmenielewa
vijana wangu”
“Tumekuelewa
mheshimiwa Rais na
tunakuahidi kazi nzuri”
akasema Ruby
“Nawashukuru sana.Muda
wowote mtakapohitaji msaada
wa aina yoyote nijulisheni
haraka sana” akasema Dr
Fabian kisha wakaagana Ruby
na Gosu Gosu wakaondoka.
WASHINGTON DC –
MAREKANI
Saa mbili za asubuhi kwa
saa za Marekani John Pasero
anayefanya kazi CIA aliwasili
katika makazi ya makamu wa
Rais Mark Piller.Alishuka
garini na kuelekea ndani
ambako makamu wa Rais
alikuwa anajiandaa kuelekea
ofisini kwake.Wakasalimiana
halafu John akatoa bahasha na
kumpatia makamu wa Rais
“Ile kazi yote uliyonituma
iko humu” akasema John
“Ahsante sana
John.Umekwisha ipitia na
kuthibitiosha kwamba ni
halisi?
“Ndiyo nimeipitia na
kujiridhisha ni halisi”akasema
John
“Sitaki kujua namna
ulivyoweza kuipata orodha hii
lakini naamini imechukuliwa
kitaalamu sana kiasi kwamba
haitakuwa na matatizo upande
wetu” akasema Mark Piller
“Usihofu
mheshimiwa,jambo hili
limefanywa kwa umakini
mkubwa sana na hakuwezi
kukawa na tatizo lolote
kwetu.Tunao mawakala wetu
ndani ya Mossad ambao
ameweza kufanikisha orodha
hii ikapatikana” akasema John
“Safi sana John” akasema
Mark Piller na kuelekea ndani
akatoka na bahasha iliyokuwa
na fedha akamkabidhi John
wakaagana akaondoka
zake.Mark Piller akaenda
katika ofisi yake ndogo
akaifungua ile bahasha
aliyopewa na John ndani yake
kulikuwa na diski mweko
akaishika mkononi akaitazama
“Tunafanya kitu cha hatari
sana hiki.Hawa majasusi
wakijulikana watakuwa katika
hatari kubwa ya kuuawa lakini
lazima tufanye hivi kwa
maslahi ya nchi yetu” akawaza
Mark Piller na kuirejesha ile
diski mweko katika bahasha
akaiweka katika mfuko wa
ndani wa koti halafu
akajiandaa kuelekea ofisini.
Mark Piller alipowasili
ofisini kwake, kitu cha kwanza
alichokifanya ni kwenda
kuonana na rais William
Washington
“Mark kuna maendeleo
yoyote toka tulipoachana?
Akauliza Rais William
“Maendeleo ni makubwa
mheshimiwa
Rais.Nimefanikiwa kuipata ile
orodha tuliyoihitaji” akasema
Mark na Rais William
akashusha pumzi
“Safi sana.Lakini imekuwa
mapema sana”
“Nimemtumia mmoja wa
vijana wangu ndani ya CIA
kuipata orodha hiyo.CIA tunao
mawakala wetu ndani ya
Mossad hivyo haikuwa kazi
ngumu kuweza kuipata orodha
hiyo” akasema Mark Piller na
kuitoa ile bahasha
akamuonesha Rais William
“Kila kitu kiko humu”
akasema Mark
“Mark hili ni jambo gumu
sana lakini lazima tulifanye.Ila
bado ninatoa angalizo kwamba
kila juhudi lazima ifanyike ili
kuhakikisha Israel
hawafahamu kama sisi ndio
tuliowaanika majasusi wao”
akasema Rais William
“Narudia tena
kukuhakikishia mheshimiwa
Rais kwamba kila kitu
kimeandaliwa vizuri na
hakutakuwa na tatizo lolote
kwa upande wetu”
“Sawa Mark.Tulipoachana
nilizungumza na Rais wa
Tanzania lakini mazungumzo
yetu hayakwenda
vizuri.Amekataa timu ya
wachunguzi wetu kwenda
kuchuguza shambulio lile
akadai watalichunguza wao
nikajikuta nikipandwa na
hasira na hatukupata muafaka
wowote lakini hadi muda ule
hawakuwa wamepata taarifa
zozote za nani wameshambulia
kambi yetu” akasema Rais
William
“Mheshimiwa
Rais,hukupaswa kutumia
hasira na wala Rais wa
Tanzania hapaswi kuona kama
vile tunalazimisha watu wetu
waende kufanya
uchunguzi.Utakapozungumza
naye wakati mwingine itabidi
ujishushe kidogo umuombe
msamaha kama kuna maneno
ulimtamkia ambayo si mazuri”
“Hapana Mark siwezi katu
kujishusha kwa mtu mweusi !
akasema Rais William kwa
sauti ya ukali
“Mheshimiwa Rais sisi
ndio tunaotafuta kitu,hivyo
lazima tutumie kila aina ya
mbinu.Tumfanye Rais wa
Tanzania awe rafiki yetu na
tujizuie kutumia kauli za
kumshinikiza afanye vile
tunavyotaka sisi.Twende naye
taratibu” akasema Mark Piller
na Rais William hakujibu kitu
na mara ujumbe ukaingia
katika simu ya Mark
akaufungua akausoma
“Mheshimiwa Rais
nitakujulisha baadae kile
kinachoendelea.Kuna mtu
ananisubiri ofisini” akasema
Mark Piller na kutoka
akaelekea ofisini kwake
“David Walker” akasema
Mark Piller baada ya kuingia
ofisini kwake na kumkuta
David Walker akimsubiri.
“Karibu sana David”
akasema Mark Piller
“Ahsante sana Mark”
akajibu David na Mark
akafunga mlango ili aweze
kuzungumza na David
“Mark nimepita hapa mara
moja kukupa mrejesho wa kile
kinachoendelea hadi muda
huu” akasema David na
kunyamaza kidogo
“Mpaka sasa bado hatuna
taarifa zozote za kuhusiana na
kirusi kilipo.Nimekuwa na
mawasiliano ya karibu na
mkuu wa majeshi na bado
taarifa ya mwisho ni ile ile
kwamba mwenye taarifa zote
za kuhusiana na kirusi ni
Jenerali William.Yeye ndiye
aliyekabidhiwa kirusi hicho
baada ya Sattar kuwasili Dar es
salaam.Tumekwamia hapo
kwani watu wetu wote
hawajulikani
walipo.Tumejaribu
kuwasiliana na viongozi wa IS
nao pia hawajui watu wao
akina Assad Ismail wako
wapi.Wote wametoweka.Mark
tunahitaji sana kujua mahala
walipo hawa watu.Tunahitaji
kujua kama ni miongoni mwa
watu waliofariki au
vipi.Nimepita hapa kwako
nikiamini labda ninaweza
kupata taarifa ya tofauti na ile
ya mkuu wa majeshi” akasema
David Walker macho yake
yakiwa mekundu na hii ni
kutokana na kutokulala
usiku.Mark Piller akavuta
pumzi ndefu na kusema
“Ni kweli usiku mzima
nilikuwa na rais na viongozi
wengine wa vyombo vya ulinzi
na usalama tukipokea taarifa
mbali mbali kutoka
Tanzania.Tayari miili yote ya
wanajeshi imekwisha
tambuliwa lakini hakuna mwili
wa Jenerali William,Sattar
wala Assad Ismail” akasema
Mark Piller
“Mungu wangu ! Nini hiki
kimetokea? akasema David
Walker na kukuna kidevu.
“Rais amezungumza na
Rais wa Tanzania kwa simu
akamuuliza kuhusiana na
uchunguzi wa jambo hili lakini
mpaka sasa hakuna taarifa
yoyote waliyoipata ya nani
walioshambulia kambi yetu”
akasema Mark Piller
“Mark hili suala linaumiza
mno vichwa vyetu na hasa
suala la kupotea kwa Jenerali
William na akina Sattar.Sisi
hatutakiwi kupoteza muda
kufuatilia nani kashambulia
kambi au nani kaua sisi
tunachohitaji ni kujua kirusi
kiko wapi? Je kiko
salama?Mtu pekee wa kutupa
majibu ya maswali hayo ni
Jenerali William ambaye
hajulikani alipo hadi hivi
sasa.Nguvu kubwa tuielekeze
hapo kujua mahala alipo
Jenerali William” akasema
David Walker na ukimya
mfupi ukapita
“Mark itumie nafasi yako
kama makamu wa rais
kuhakikisha tunafahamu
mahala alipo Jenerali
William.Bila kumpata huyu
mtu misheni yetu itakuwa
imeharibika.Kama kuna
ulazima wa kutuma hata kikosi
maalum kwenda kumsaka
shughulikia hilo! Mshinikize
Rais aongeze mbinyo kwa
serikali ya Tanzania hata kama
ikibidi kutumianguvu basi
itumike ili kumpata Jenerali
William ! Kama tuliweza
kumpata na kumuua Osama
Bin Laden hatuwezi
kushindwa kumpata mtu wetu
katika nchi kama Tanzania !
akasema David Walker
“David kuna kitu
ninakihisi.Ni vipi kama
Jenerali William amekwenda
na akina Sattar kuanza kazi ya
usambazaji wa kirusi?
Nimekuwa na hisia hizo
kwamba yawezekana hakutaka
kupoteza muda akaamua
kukisambaza kirusi hicho
mara moja kwani ukiangalia
wote wametoweka tena kwa
wakati mmoja” akasema
Mark.David akafikiri kidogo na
kusema
“Hilo linawezekana lakini
nyumba aliyokuwa anaishi
tumeambiwa nayo imevamiwa
na watu wote kuuawa.Je
aliondoka kabla wavamizi
hawajafika? Halafu taarifa
inasema kwamba
anayekosekana si Jenerali
William peke yake bali pia
kuna wafanyakazi wengine
wawili waliokuwa
wakihudumu katika nyumba
hiyo aliyokuwa akiishi nao pia
hawajulikani walipo.Kama
amekwenda kusambaza kirusi
je amekwenda nao? Kama
amekwenda nao ni kwa
madhumuni gani? Walikuwa
na umuhimu wowote? Halafu
jukumu la kusambaza kirusi
halikuwa la Jenerali
William.Yeye jukumu lake
lilikuwa ni kumpokea Sattar na
kumkabidhi kwa Assad na
kuwasaidia waweze
kufanikisha usambazaji.Mark
mpaka hapo bado unaamini
Jenerali William amekwenda
kusambaza kirusi?Akauliza
David Walker na Mark Piller
akazama mawazoni kwa muda
halafu akasema
“Sina hakika David”
akajibu Mark Piller
“Mark kazi kubwa
tuliyonayo ni kuhakikisha
tunajua mahala alipo Jenerali
William.kama nilivyokwambia
kwamba unapaswa kuitumia
vyema nafasi yako kuhakikisha
tunalifahamu hili” akasema
David
“Nitajitahidi.Vipi kuhusu
mpango wa kumteka Habiba
Jawad unaendeleaje? Akauliza
Mark
“Tayari kuna timu
imetumwa Riyadh na…” David
akatazama saa yake ya
mkononi
“Naamini hadi muda huu
watakuwa tayari wamekwisha
fika”
“Vizuri sana.Mpango wa
kumteka umekaaje? Lazima
uwe ni mpango ulioandaliwa
kipekee kabisa ili isijulikane
kama sisi ndio tuliomteka
Habiba.Nilitoa angalizo awali
kwamba Habiba ana
mahusiano ya karibu na
mfalme wa Saudi Arabia
ambaye ni mshirika mkubwa
wa Marekani”
“Tumeuandaa mpango
vizuri Mark usihofu.Habiba
hafahamu chochote hivi
sasa.Nitampigia simu na
kumtaka aende sehemu Fulani
akakutane na mtu mwenye
ujumbe muhimu na akienda
huko atatekwa na kupelekwa
katika ubalozi wetu jijini
Jerusalem.Baada ya
kumpeleka Jerusalem
tutawaita Mossad na
watathibtisha kwamba tunaye
Habiba ili waweze kuharakisha
zoezi la kumuua Abu Zalawi”
“Sawa David.Utanijulisha
kile kitakachokuwa
kinaendelea katika mipango
yote.Mimi nitashughulikia
suala la Jenerali
William.Halafu kuna suala
lingine ambalo nimekuwa
nikilifikiria.Je IS hawawezi
kuwa wanahusika na
shambulio hili? Akauliza Mark
Piller
“Kwa nini umehisi hivyo
Mark? David naye akauliza
“Kwa namna shambulio
lilivyotokea inaonesha wazi
kwamba limefanywa na watu
waliokuwa wamejiandaa
vilivyo tena kwa silaha
nzito.Sina hakika lakini
ninahisi yawezekana IS
wamehusika katika
shambulkio hili na ndiyo
maana Assad na watu wake
wote wametoweka na hatujui
mahala walipo” akasema Mark
Piller.David Walker akafikiri
kwa muda na kusema
“IS wana sababu yoyote ya
kufanya hivyo? Wamekuwa ni
washirika wetu wa muda
mrefu.Tumewawezesha kwa
silaha na tunawapa fedha
nyingi kupitia Habiba Jawad”
akasema David walker
“Ni vipi kama nao
wanakihitaji kirusi kwa ajili ya
mipango yao ya kigaidi au hata
kukiuza kwa mataifa
mahasimu zetu ? Akauliza
Mark Piller na ukimya mfupi
ukapita
“Hilo ni wazo la msingi
Mark.Tusilidharau tulifanyie
uchunguzi kwa sababu haiingii
akilini watu wote hawa
wakatoweka kwa wakati
mmoja na hawajulikani
walipo.Yawezekana IS
wametugeuka wakamteka
Jenerali William wakaua
wanajeshi wetu,wakavamia pia
kambi wakaondoka na kirusi”
“Niachie mimi suala hili
nitalifanyia kazi.Hadi jioni ya
leo tutakuwa na majibu ya
kutosha kuhusu suala hili”
akasema Mark Piller na
kuagana na David Walker .
Baada ya David
kuondoka,Mark akachukua
simu anayoitumia kuwasiliana
na Habiba akampigia
“Hallo Mark Piller”
akasema Habiba
“Habiba habari ya muda
huu”
“Nzuri Mark.Habari za
huko kwenu?
“Huku bado mambo si
mazuri.Mpaka sasa hakuna
taarifa yoyote kuhusiana na
tukio la Tanzania.Kibaya zaidi
hakuna taarifa zozote za
kumuhusu Jenerali William au
akina Sattar” akasema Mark
“Mark tuvute subira
tutafahamu walipo.Kama
hawapo katika orodha ya watu
waliouawa basi wapo sehemu
Fulani.Mimi pia ninaendelea
na ule uchunguzi kama IS
wanahusika katika shambulio
hilo nikipata chochote
nitakujulisha” akasema
Habiba
“Jitahidi Habiba ili
tulifahamu jambo hili kwani
kadiri muda unavyozidi
kwenda ndivyo suala hili
linavyozidi kuwa
gumu.Tuachane na hilo
nimekupigia kwa ajili ya
mambo mawili.Kwanza ni
kukupa taarifa kwamba ile
orodha nimeipata”
“Umeipata? Habiba
akauliza
“Ndiyo
nimeipata.Nitakutumia muda
si mrefu.Jambo la pili ni
kuhusiana na ule mpango wa
kukuteka” akasema Markna
kumuelezea Habiba mpango
wote ulivyoandaliwa
“Mark nakushukuru sana
kwa taarifa hizo.Kuhusu
usalama wangu usiwe na hofu
nimekwisha jiandaa vya
kutosha.Kitu cha msingi
nitumie hiyo orodha nianze
kuifanyia kazi” akasema
Habiba
“Nitakutumia muda si
mrefu Habiba” akasema Mark
Piller na kuagana na Habiba
kwa miadi ya kuwasiliana tena
baadae kupeana taarifa za kile
kinachoendelea.
RIYADH – SAUDI ARABIA
Saa kumi na mbili za jioni
ndege ya Rais wa Tanzania
iliyombeba Nawal iliwasili
jijini Riyadh katika uwanja wa
ndege ambao hutumiwa na
Habiba na familia yake.Nawal
aliwashukuru marubani wa
ndege ile kwa kumfikisha
salama Riyadh na kuwatakia
safari njema ya kurejea
Tanzania.Uwanjani pale
alipokewa na wasaidizi wa
Habiba akaondoa kuelekea
katika makazi ya Habiba
Jawad.
“Karibu tena
Nawal.Nimefurahi mno kuiona
tena sura yako.Wewe na
Mathew ni watoto pekee nilio
baki nao hivyo kukuona tena
ni faraja kubwa mno kwangu”
akasema Habiba Jawad
akimkaribisha Nawal katika
makazi yake baada ya kuwasili
akitokea Tanzania
“Hata mimi nimefurahi
sana kuonana nawe tena
mama Habiba” akasema
Nawal.
“Nawal najua umechoka
na safari ndefu lakini pamoja
na uchovu wa safari nataka
ukajiandae kuna kazi ya
kufanya usiku huu” akasema
Habiba
“Usijali mama mimi nipo
tayari kwa kazi muda
wowote.Niambie ni kazi gani
natakiwa kuifanya” akasema
Nawal
“Nilikueleza kuhusu
mpango wa G20 wa kutaka
kumua Mathew
Mulumbi.Mpango wenyewe
tayari umeanza.Ili Israel itume
majasusi wake wamuue
Mathew wanataka CIA
iwathibitishie kwamba niko
katika mikono yao na baada ya
kumuua Mathew
nitakabidhiwa kwao.Tayari
majasusi wamekwisha tumwa
kuja kuniteka na kunipeleka
Israel katika ubalozi wa
Marekani ambako nitakaa
hapo kabla ya kukabidhiwa
kwa Israel lakini CIA mpango
wao ni kuniua kabla ya
kunikabidhi kwa Mossad”
akasema Habiba
“Nimepigiwa simu na
David Walker jioni hii
amenipa maelekezo ya kwenda
kukutana na hao majasusi wa
CIA waliotumwa kuja
kuniteka.Hawafahamu kama
tayari ninafahamu mipango
yao.Kazi uliyonayo ni
kuhakikisha unawamaliza
majasusi hao wa CIA” akasema
Habiba na kumuelezea Nawal
namna mpango utakavyokuwa
“Usijali mama utakuwa
salama.Hesabu jambo hilo
limekwisha malizika” akasema
Nawal
“Ahsante Nawal.Jambo
lingine ni kwamba Mathew
alihitaji orodha ya majasusi wa
Mossad walioko Iran na tayari
nimeipata orodha hiyo
nitamtumia ili iweze
kumsaidia” akasema Habiba
“Anaendeleaje Mathew?
Nawal akauliza
“Mathew anaendelea
vizuri na baada ya kuipata
orodha hiyo ndipo
atakapoanza rasmi kazi
yake.Mambo mengi
utayafahamu utakapokutana
naye” akasema Habiba na
Nawal akaenda
kujiandaa.Habiba akaelekea
ofisini kwake na kumpigia
simu Vahid Ghorbani.
“Habari yako Vahid”
akasema Habiba baada ya
Vahid kupokea simu
“Habiba naomba nikuweke
wazi mapema kabisa kwamba
kama unahitaji msaada
kuhusu Abu Zalawi utafute
mtu mwingine wa kukusaidia
lakini mimi sitaki tena kuwa
na ukaribu na Yule gaidi”
akasema Vahid
“Vahid ninahitaji msaada
wako na yawezekana hii ikawa
ni mara ya mwisho lakini ni
muhimu mno”
“Unahitaji nini Habiba?
Akauliza Vahid
“Kuna kitu nahitaji
umfikishie Abu Zalawi”
“Habiba utanisamehe
sitaki tena kwenda kule.Sitaki
kuonekana mara kwa mara
ninazungumza na Yule mtu
kwani hata mimi ninaweza
kuanza kuhisiwa vibaya”
“Nalifahamu hilo Vahid
lakini naomba
unisaidie.Nakuhakikishia
kwamba hii itakuwa ni mara
ya mwisho na hutanisikia
nikikuomba tena msaada.Ni
jambo la muhimu mno”
akasema Habiba.Vahid
akafikiri kidogo halafu
akauliza
“Nini unataka nimpelekee
Abu Zalawi?
“Kuna faili nitakutumia
nataka uliweke katika diski
mweko na umfikishie Abu
Zalawi leo hii hii” akasema
Habiba
“Linahusu nini hilo faili?
Akauliza Vahid
“Vahid utanisaidia au vipi?
Akauliza Habiba
“Tuma hilo faili
nitalifikisha kwa Abu Zalawi
ila nakuomba Habiba hii iwe
ni mara ya mwisho kunituma
kwa Abu Zalawi.Mimi ni mtu
mwenye heshima zangu na
sitaki kuanza kuhisiwa vibaya
kuwa ninashirikiana na
magaidi”
“Nakuahidi hii itakuwa
mara ya mwisho” akajibu
Habiba
“Sawa tuma hilo faili”
akasema Vahid na Habiba
akamtumia faili lenye orodha
ya majasusi wote wa Mossad
walioko nchini Iran.
Vahid hakutaka
kusumbuka kulifungua faili lile
akaliweka katika diski mweko
na kumpigia simu Faqir
akamueleza kwamba anahitaji
kuonana na Abu Zalawi.Fakiri
akamuahidi kumfuata pale
nyumbani kwake ili aweze
kuongozana naye kuelekea
katika nyumba aliko Mathew.