SIRI PART3: MTUNZI PATRICK CK
JASUSI/GAIDI
SEASON 5 : EPISODE 4
“Imekuwa vyema umefika
kwa wakati David kwani
tunakwenda kuonana na
makamu wa Rais amenitaka
nifike ofisini kwake” akasema
Jason Washington mkurugenzi
mkuu wa CIA baada ya David
Walker kufika ofisini kwake.
Bila kupoteza muda
wakaingia katika gari la Jason
na kuondoka kwenda kuonana
na Mark Piller makamu wa
Rais
“Nini kimejiri huko katika
kikao? Akauliza Jason na
David akamweleza kila kitu
walichokubaliana katika kikao
“Vizuri sana.Nilimdokeza
Mark Piller kuhusiana na
mpango wetu wa kumuondoa
Abu Zalawi.Mark amestushwa
sana na jambo hili ndiyo
maana amenitaka nikaonanye
naye kwani tusingeweza
kuzungumza kwa kirefu katika
simu.Haamini kile
nilichomweleza kuhusu Abu
Zalawi” akasema Jason
Washington
“Suala hili la Abu Zalawi
linaumiza vichwa sana.Kila
mtu anashangaa kuhusu
jambo hili limetokeaje?
“Hatuna wa kumlaumu
katika hili David.Tumekosea
sisi wenyewe na lazima
tuchukue hatua za haraka sana
kuhakikisha jambo hili
halitakuwa na madhara
kwetu.Kama tungechukua
tahadhari mapema haya yote
yasingetoke ana misheni
ingeendelea kama kawaida”
akasema Jason
“Kuna kitu nimekuwa
najiuliza vipi kuhusu wale
jamaa wanasayansi tuliokuwa
tunawashikilia kwa muda
mrefu? Tunakubali
tumewapoteza?akauliza David
na Jason akatikisa kichwa
akisikitika
“Watu wale japo
hawajatupa taarifa tulizokuwa
tunazihitaji lakini ni watu wa
muhimu sana kwa Iran.Katika
hili tumewapa Iran ushindi
mwepesi lakini lazima
tuhakikishe nao pia wanauawa
pamoja na Abu Zalawi.”
akasema Jason
Walifika katika ofisi ya
makamu wa Rais ambaye
alikuwa anawasubiri na bila
kupoteza muda wakaingia
katika chumba cha maongezi
ya faragha na kikao kikaanza.
“Jason nimevuruga ratiba
yangu ya siku ya leo ili niweze
kuzungumza nanyi.Nataka
kufahamu kwa kina kuhusiana
na hiki kinachoendelea”
akasema makamu wa Rais
Mark Piller
Jason akamuelezea Mark
Piller kila kitu hadi
walipogundua kuhusu Abu
Zalawi kuwa si gaidi bali ni
jasusi pamoja na maamuzi
waliyoyachukua ya kumuua
“Jason jambo hili
limetokeaje? Kwa nini
haukufanyika uchunguzi wa
kina kuhusiana na huyu mtu
Abu Zalawi hadi tumefika hapa
tulpofika? Akauliza Mark Piller
“Katika hili Mark hatuna
wa kumlaumu mtu bali
tunapaswa kujilaumu sisi
wenyewe.Tulifanya uzembe wa
kutokufanya uchunguzi wa
kina kuhusiana na Abu Zalawi”
akasema Jason
“Lakini yote haya
ameyasababisha Habiba
Jawad ambaye tulimuamini
kwa asilimia mia moja na
hivyo tukamuamini yule mtu
aliyetuletea.Hata mara moja
hajawahi kutuangusha na
katika kila operesheni
tuliyomshirikisha hakujawahi
kutokea matatizo.Hii ni mara
ya kwanza Habiba anatufanyia
kitu cha namna hii” akasema
David Walker
“Mnadhani Habiba
alikuwa na lengo lake binafsi la
kumleta kwetu Abu
Zalawi?akaliza Mark Piller
“Hatuna uhakika bado
ndiyo maana tunataka
kulifanyia uchunguzi suala hilo
lakini wakati uchunguzi huo
ukiendelea tunataka
kumuondoa kwanza Abu
Zalawi pamoja na wale
wanasayansi tuliokuwa
tunawashikilia” akasema
Jason.Baada ya tafakari ya
muda mfupi Mark akauliza
“Kutakuwa na athari gani
kama tukimuacha Abu Zalawi
akaendelea na misheni lakini
tukimfuatilia kwa ukaribu
mkubwa kujua kila
anachokifanya kwa kuwatumia
hao majasusi wa Mossad
ambao mnataka kuwatumia
kumuua?akauliza Mark Piller
na Jason akampa maelezo
aliyopewa na Moshe Levine
mkuu wa Mossad kuhusu Abu
Zalawi na Mark akazidi
kuchoka.
“Mark hatuna namna
lazima tumuondoe Abu Zalawi
haraka sana ili kujihakikishia
usalama wetu.Endapo
tukishindwa kumuondoa Abu
haraka itatugharimu baadae”
akasema Jason.Waliendelea na
majadiliano kwa muda halafu
Mark Piller akasema
“Jason na David
nimekubalianba na
mapendekezo yenu juu ya
suala hili lakini nina
ushauri.Hatuwezi kumuua
Habiba Jawad nchini kwao
Saudi Arabia.Habiba Jawad
ana ukaribu mkubwa na
mfalme wa Saudi Arabia
ambaye ni mshirika mkubwa
wa Marekani hivyo lazima
tujihadhari tusivuruge
mahusiano mazuri kati yetu na
serikali ya Saudi
Arabia.Habiba aitwe Marekani
na akifika huku ndipo
atakapouawa” akashauri Mark
Piller
“Ushauri mzuri
tutauzingatia” akasema Jason
“Angalizo.Habiba asiuawe
kama Mossad hawajamuua
Abu Zalawi.Pale ambapo Abu
Zalawi atakuwa ameuawa
ndipo Habiba auawe kwani
tunaweza kumuua Habiba
halafu Mossad wakashindwa
kumuua Abu Zalawi.Kama
kuna jambo wawili hawa
wanalipanga lazima
tuwaondoe wote wawili
akiondolewa mmoja na
mwingine akabaki hatutakuwa
tumefanya kitu” akasisitiza
Mark Piller.Baada ya
majadiliano Jason na David
wakaondoka .Mark Piller
hakupoteza muda akainua
simu na kumpigia Rais
William Washington
“Mheshimiwa Rais nahitaji
kukuona sasa hivi” akasema
Mark
“Njoo ofisini” akajibu Rais
William na Mark Piller
akatoka ofisini kwake kuelekea
ofisini kwa Rais.
“Mark mpango wenu
unakwenda
vizuri.Nimefurahishwa na
taarifa nilizozipata kwamba
ndege ile iliyopotea
imeonekana ikielekea nchini
Iran” akasema Rais William
baada ya Mark kufika ofisini
kwake
“Mheshimiwa Rais ni
kweli mpango umekwenda
vizuri sana na hivi
tuzungumzavyo tayari mtu
wetu amekwisha kanyaga
ardhi ya Iran” akasema Mark
Piller
“Vipi mna mawasiliano
naye baada ya kuwasili Iran?
Akauliza Rais William
“Mheshimiwa Rais
mpango wetu wa kwanza
ulikuwa ni kumuingiza Abu
Zalawi nchini Iran na mpango
huo umefanikiwa vizuri lakini
kuna tatizo limejitokeza”
akasema Mark Piller na sura
ya Rais William aikabadilika
“Kumetokea tatizo gani
tena” akauliza William
“Baada ya Abu Zalawi
kufika salama Iran tulihitaji
kumpa msaada na kwa vile
hatuna wetu wetu kule Iran
ilitulazimu kuomba msaada
kutoka kwa wenzetu wa
Mossad ambao wana majasusi
wao Iran na hapo ndipo
lilipoibuka jambo ambalo
hatukuwa tukilifahamu”
akasema Mark Piler na
kumueleza Rais William kila
kitu walichokifahamu kutoka
kwa Mossad kuhusiana na Abu
Zalawi.Zilikuwa ni taarifa
zilizomstua sana William
“Mark kwa nini haya yote
yametokea?Kwa nini
hamkuchukua tahadhari
mapema kuhakikisha
mnamfahamu vyema mtu
ambaye mnataka kumtumia
katika misheni kubwa kama
hii? Akauliza William
“Mheshimiwa Rais katika
hilo tunakiri tulikosea na
ndiyo maana tunataka
kuchukua hatua za haraka za
kurekebisha kwa kumuondoa
Abu Zalawi haraka sana kabla
hajaendelea na misheni
aliyotumwa nchini Iran”
“Kumuua Abu Zalawi ni
suluhisho la jambo
hili?akauliza William
akionekana kukasirika
“Mheshimiwa Rais huyu
mtu ni hatari kwetu kama
tukiendelea kumuacha
hai.Tayari anafahamu kila kitu
kuhusu sisi na baya zaidi
anafahamu ni sisi tulio nyuma
ya kile kilichotokea Tanzania
na Afrika mashariki na
anafahamu kwa nini tulifanya
vile….”
“Pamoja na kufahamu !
akasema kwa ukali Rais
William na kumkatisha Mark
Piller
“Pamoja na kufahamu
hayo yote lakini bado Abu
Zalawi au vyovyote vile
anavyofahamika amekubali
kuifanya kazi aliyotumwa na
kwa sasa tayari amefika nchini
Iran.Anafahamu kabisa
kwamba kazi aliyotumwa
kuifanya Iran ni kazi ya hatari
kubwa na kama akijulikana
kuwa ni pandikizi la Marekani
anaweza akauawa muda
wowote ule lakini bado yuko
tayari kufanya.Kumuua Abu
Zalawi ni kosa kubwaMark !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais pamoja
na Abu Zalawi kukubali
kuifanya kazi aliyotumwa
aifanye lakini hakuna anayejua
moyoni mwake nini
anakiwaza,hatujui ana
mipango gani dhidi yetu.Kwa
taarifa tuliyoipata kutoka kwa
Mossad ni kwamba Abu Zalawi
ameyatoa maisha yake katika
kupambana na ugaidi hasa
kundi la IS linaloendelea
kuotesha mizizi katika eneo la
Afrika Mashariki.Abu Zalawi
ni bilionea na ana familia
inaishi Paris Ufaransa lakini
ameacha hivyo vyote
akajielekeza katika kupamba
na na magaidi.Jaribu kupata
picha mtu kama huyu anakuja
kugundua kwamba
tunashirikiana na magaidi wa
IS na kibaya zaidi kuchochea
machafuko katika nchi
anakotoka na kusababisha vifo
vya watu na sisi tukiendelea
kubeba tani na tani za mafuta
unadhani mtu kama huyu
atafanya nini?Lazima atakuwa
na chuki kubwa sana dhidi
yetu na hatujui nini
anakifikiria lakini ni wazi
jambo hili hataweza
kulivumilia” akasema Mark
Piller
“Mark nimekuelewa lakini
maamuzi ya kumuua mtu
kama huyu si sahihi.Mtu kama
huyu bado anaweza akawa
upande wetu.Tunaweza
kuzungumza naye na
kumfanya atuelewe na hata
kama alikuwa na kitu moyoni
mwake tukakiondoa.Sisi ni
taifa kubwa na hatuwezi
kukubali kushindwa kirahisi
namna hii.Hebu fikiria
Mark,nini kingine mtakifanya
kitakachowawezesha
kupandikiza mtu nchini Iran?
Kwa kuwatumia wale mateka
wa Iran imekuwa rahisi kwetu
kuweza kupenyeza mtu ndani
ya Iran na kama mkiharibu
msheni hii itachukua miaka
mingi kuweza kufanikisha
jambo kama hili na pengine
lisiwezekane tena.Kwa kuwa
tayari Abu Zalawi amekwisha
ingia Iran,itafutwe namna ya
kuzungumza naye na
kumuweka sawa aendelee na
jukumu lake badala ya
kufikiria kumuua” akasema
Rais William
“Mheshimiwa Rais…..”
Mark Piller akataka kusema
kitu lakini Rais William
akamzuia
“Mark sitaki kuendelea na
mjadala huu.Hatuwezi kuipa
Iran ushindi kirahisi namna
hii lazima kwa namna yoyote
ile misheni hii iendelee.Iran ni
taifa tishio kwa Marekani kwa
sasa na lazima tufahamu
uwezo wake wa silaha hivyo
lazima misheni iendelee.Abu
Zalawi hapaswi kuuawa !
akasema kwa sauti ya msisitizo
kisha wakabaki wanatazamana
“Mheshimiwa Rais sidhani
kama unaiona hatari iliyoko
mbele yetu kama tukiendelea
kumtumia huyu Abu Zalawi !
akasema Mark
“Mark sijali chochote,
ninachohitaji ni Abu Zalawi
aendelee na misheni
aliyotumwa nchini
Iran.Endapo Abu akiuawa na
misheni ikashindwa kuendelea
ninaapa nitakifuta hiki kikundi
chenu kwani hakitakuwa na
maana tena.Sijali kama
nitauawa ama nini kitatokea
lakini lazima nikifute !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais
nilipokuja kukueleza
kuhusiana na kikundi hiki na
mambo yake nilikupa angalizo
kwamba unatakiwa usiri
mkubwa kwani Rais wa nchi
hapaswi kufahamu chochote
kuhusu uwepo wa kikundi
hiki.Utayaweka maisha yetu
sote katika hatari
kubwa.Nakuomba
mheshimiwa Rais usifikirie
kufanya hicho hicho
unachotaka kukifanya”
akasema Mark Piller
“Mark mimi siogopi
chochote na ninakuhakikishia
kwamba nitafanya hivyo na
wamarekani watajua kuwa
nchi yao inashirikiana na
magaidi”
“Mheshimiwa Rais !
akasema Mark
“Mark fanya
ninavyokuelekeza.Ukitaka
kundi lenu liendelee
kuwepo.Nataka Abu zalawi
aendelee na misheni yake
nchini Iran.Sitaki auawe.Fanya
kila linalowezekana
kuhakikisha misheni yake
inafanikiwa.Tunaihitaji sana
misheni hii ama sivyo Iran
itaendelea kutoa vitisho vya
kusishambulia Marekani!
Siwezi kuzivumilia kauli chafu
za vitisho zinazotolewa na Rais
wa Iran dhidi ya Marekani !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais
kufanya hicho unachotaka
nikifanye ni usaliti mkubwa
kwa wenzangu na…..”
“Mark kumbuka kwamba
sisi ndio tunao ongoza nchi hii
na dhamana ya usalama wa
watu wetu tumeibeba sisi na
kwa sasa watu wetu wana hofu
kufuatia vitisho vya Iran kuwa
anao uwezo wa kuishambulia
na kuiharibu Marekani hivyo
basi lazima tufanye kila lililo
ndani ya uwezo wetu
kuhakikisha tunaiweka nchi
yetu salama pamoja na watu
wake ndiyo maana ninasema
kwamba tunaihitaji sana
misheni hii kwa ajili ya
kufahamu wezo wa silaha za
Iran na baada ya hapo
tutaichakaza vibaya
sana.Ikitokea Iran
imeshambulia Marekani
watakaobeba mzigo wa
lawama ni sisi na si hao ambao
unaogopa kuwasaliti.Mark
fanya kila linalowezekana hata
kama ni kwa kuwasaliti
wenzako hakikisha Abu Zalawi
anakuwa salama na
anaendelea na misheni yake
nchini Iran.Vuruga mpango wa
kumuua ! akasema Rais
William na Mark Piller
akainamisha kichwa
akitafakari
“Umenielewa Mark
Piller?akauliza Rais William
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais.Nitafanya
kama ulivyoelekeza lakini
naomba ufahamu kwamba ni
jambo la hatari kubwa”
“Usihofu kuhusu hilo
Mark.Kama kuna hatari yoyote
unaihisi nijulishe na mimi
nitakulinda.Tunayafanya haya
kwa maslahi ya nchi yetu”
akasema Rais William na Mark
Piller akaondoka akarejea
ofisini kwake na kujiegemeza
kitini
“Hili jambo linaendelea
kubadilika kila wakati.Rais
anataka niwasaliti wenzangu
na kuvuruga mipango ya
kumuua Abu Zalawi ! akawaza
Mark
“Lakini ukilitazama jambo
hili kwa kina zaidi,Rais yuko
sahihi.Hatupaswi kumuua Abu
Zalawi badala yake tunapaswa
kufanya kila liwezekanalo
kumuweka upande wetu.Kwa
hiyo kwa mara ya kwanza
nitalazimika kuwasaliti
wenzangu na kuvuruga
mpango wa kumuua Abu
Zalawi.Kuna mtu mmoja tu
ambaye ninatakiwa
kuzungumza naye” akawaza na
kufungua mkoba wake akatoa
simu iliyokuwa na namba
kumi na mbili tu ambazo ni
namba za watu muhimu
akaelekeza kidole chake katika
namba ya sita ambayo ilikuwa
ni namba ya Habiba Jawad
akampigia baada ya sekunde
kadhaa simu ikapokelewa.
“Mark Piller ! akasema
Habiba Jawad akionekana
kushangaa
“Habiba Jawad
unaendeleaje? Akasema Mark
“Ninaendelea vizuri
Mark.Nimeshangaa kidogo leo
umenipigia simu.Sikutegemea
kabisa kupata simu yako”
akasema Habiba Jawad
“Habiba nimelazimika
kukupigia simu kuna mambo
ya muhimu sana ya
kuzungumza mimi nawe na
ninakuomba tafadhali yale
tutakayoyazungumza hapa
yawe ni baina yetu sisi
wawili.Mtu mwingine yeyote
kutoka G20 hatakiwi
kufahamu kama nimekupigia
simu.Umenielewa
Habiba?akauliza Mark Piller
“Nimekuelewa Mark.Nini
unataka kuzungumza
nami?akauliza Habiba
“Kwanza kabisa ninataka
kukupa taarifa kuwa mpango
wetu umekwenda vizuri na hivi
tuzungumzavyo tayari Abu
Zalawi amekwisha ingia nchini
Iran” akasema Mark Piller
“Hizo ni taarifa njema
sana.Nimefurahi kusikia
matokeo mazuri ya mpango
huu.Ninakuhakikishia Mark
kuwa kama tayari Abu
amefanikiwa kuingia nchini
Iran lazima atafanikisha kila
kitu alichotumwa
kukifanya.Kitu cha msingi kwa
sasa ni kujitahidi kutafuta
namna ya kuwasiliana naye na
kujua maendeleo yake”
akasema Habiba
“Tayari tumelifanya hilo
Habiba ila kuna tatizo
limejitokeza”
“Tatizo gani
Mark?akauliza Habiba
“Baada ya kuhakikisha
Abu Zalawi ameingia Iran
ilitulazimu kuomba msaada
kutoka kwa wenzetu wa
Mossad ambao wana watu wao
kule Iran kwa ajili ya kumpa
msaada na hapo ndipo
tulipofahamu kila kitu kuhusu
Abu Zalawi” akasema Mark na
kumueleza Habiba kila kitu
walichokigundua kuhusu Abu
Zalawi.Kupitia spika za simu
Habiba Jawad akasikika
akivuta pumzi ndefu
“Habiba unaweza
ukazungumza chochote
kuhusiana na jambo
hili?akauliza Mark
“Sina cha kuzungumza
Mark lakini kila kitu
mlichoelezwa kuhusu Abu
Zalawi ni cha kweli” akasema
Habiba na Mark Piller akahisi
mwili unamtetemeka
“Kwa nini Habiba kama
ulifahamu kuwa Abu Zalawi ni
jasusi tena anatokea Tanzania
ukamleta kwetu tukampa
misheni kubwa kama hii?
Akauliza Mark Piller
“Kwa sababu Abu Zalawi
ndiye pekee anayeweza
kuifanya kazi hii.Hakuna gaidi
ambaye ana uwezo wa kuingia
Iran na kufanya jambo la
hatari la kuichunguza Iran
zaidi ya Abu Zalawi.Mark hii si
misheni ya kigaidi hii ni
misheni ya kijasusi na mtu
niliyewaletea ndiye anayefaa”
akasema Habiba Jawad
“Habiba sisi tulihitaji gaidi
lakini wewe ukatuletea jasusi
tena anatokea Tanzania nchi
ambayo kwa kushirikiana na
magaidi wa IS tumechochea
machafuko ya kidini na
kusababisha waumini
kushambuliana na damu
nyingi kumwagika na kama
haitoshi bado tunaendelea na
mpango wa kusambaza kirusi
hatari kwa lengo la kuendelea
kuchota utajiri mkubwa ulioko
Afrika Mashariki.Kwa nini
ukatufanyia hivi? Akauliza
Mark
“Mark kama
nilivyokueleza kwamba huyu
ndiye mtu pekee anayefaa kwa
misheni hii” akajibu Habiba
“Habiba japokuwa una
uhakika kuwa mtu huyu ndiye
anayefaa lakini tayari ana
kasoro.Hatujui ni kitu gani
anakiwaza baada ya kugundua
kwamba sisi tuko nyuma ya
kile kinachoendelea Afrika
Mashariki.Hii ni kasoro kubwa
na tayari imetia doa misheni
nzima” akasema Mark
“Mark nataka
nikuhakikishie kwamba Abu
Zalawi hana tatizo lolote na
msiwe na wasiwasi wowote
naye.Anakwenda kutekeleza
kile alichotumwa kukifanya
Iran na uwezo wa kufanya
hivyo anao.Abu Zalawi japo ni
jasusi lakini nimembadilisha
na anafanya kazi
kwangu.Nimembadili kutoka
Jasusi kuwa Gaidi.Ni mimi
pekee anayenisikiliza kila
ninachomuelekeza kukifanya
kwani nimemfanya kuwa
mwanangu,amemuoa
mwanangu Najma hivyo Abu
Zalawi ni sehemu ya familia
yangu” akasema Habiba
“Habiba kama
nilivyokueleza kuwa tayari
misheni imeingia dosari.Baada
ya kugundua kuwa Abu Zalawi
si Yule uliyetuaminisha kuwa
ni gaidi bali ni jasusi tena
anatokea Tanzania,kuna
maamuzi yamefanyika”
akasema Mark Piller na
kunyamaza kidogo
“Mmefanya maamuzi gani
Mark?akauliza Habiba
“Tumekubaliana kumuua
Abu Zalawi na misheni
itakuwa imeishiahapo”
akasema Mark na ukimya
ukapita
“Mark Piller hilo ni kosa
kubwa sana ambalo mtalijutia
kwani hamtapata tena nafasi
nyingine ya kumuingiza mtu
wa kuwafanyia ujasusi nchini
Iran.Hii ni nafasi pekee
mmeipata na mkishindwa
kuitumia vyema ni juu yenu”
akasema Habiba
“Habiba misheni tayari
imevurugika na aliyeivuruga
misheni hii ni wewe kwa
kutuletea mtu ambaye hakuwa
sahihi kwa misheni
hii.Tulikuamini sana Habiba
na ndiyo maana hatukuwa na
wasi wasi wowote na Abu
Zalawi lakini baada ya
kumfahamu vyema Abu Zalawi
umevunja uaminifu na
maamuzi yaliyopitishwa ni
wewe kuuawa pia” akasema
Mark Piller na ukimya
ukawala.
“Mark ! akaita Habiba
Jawad
“Unasemaje Habiba?
“Mnakwenda kufanya kosa
kubwa sana kwa hiyo mipango
yenu mliyoipanga” akasema
Habiba
“Ninafahamu Habiba”
“Kwa nini ukanipigia
kunijulisha kuhusu mipango
yenu?akauliza Habiba
“Nimekupigia kwa sababu
baada ya kutafakari kwa kina
nimegundua kwamba
tutafanya kosa
kubwa.Tunaihitaji mno
misheni hii ifanikiwe hivyo
nimekupigia kuomba msaada
wako” akasema Mark na
ukimya ukatawala tena.Habiba
Jawad akavuta pumzi na
kusema
“Nini unahitaji tena
kutoka kwangu Mark wakati
tayari mmekwisha panga
mipango ya kuniua? Akauliza
Habiba
“Nimeamua kuwasaliti
wenzangu na kukueleza ukweli
kuhusu mipango yetu,kwanza
ili uchukue tahadhari na
kujificha na pili ni kutafuta
namna ya kumfikishia Abu
Zalawi taarifa za kumtaka
achukue tahadhari kwani kuna
watu wanaotaka
kumuua.Nataka Abu aendelee
na misheni hii hadi
atakapoikamilisha” akasema
Mark Piller
“Mark nimekuwa mtumwa
wenu kwa miaka
mingi,nimewafanyia kazi
nyingi kwa manufaa ya nchi
yenu lakini hata baada ya
kuwafanyia hayo yote
ninachoambulia ni kutaka
kuuawa.Mmenisikitisha sana
Mark”
“Habiba ndiyo maana
nimekupa siri hii ili uweze
kuchukua tahadhari na
ikiwezekana uondoke Saudi
Arabia ukajifiche mahala”
akasema Mark
“Siwezi kukimbia
Mark.Siwezi kukimbia.Kama
mnataka kuniua njooni
mtanikuta hapa ninawasubiri
lakini fahamuni ya kwamba
damu yangu haitawaacha
salama ! akasema Habiba
Jawad
“Habiba tafadhali naomba
tusilifanye jambo hili liwe
gumu.Wewe mwenyewe
unafahamu namna misheni hii
ilivyo muhimu.Wengine wote
hawalioni hilo lakini mimi
ninafahamu umuhimu
wake.Habiba tafadhali
nakuhitaji sana.Naomba
tushirikiane kuhakikisha
misheni hii inaendelea na
inafanikiwa.Naomba tafuta
namna ya kumlinda Abu
Zalawi dhidi ya wale wote
watakaotumwa kumuua na
aendelee na kazi aliyotumwa
kuifanya.Habiba nakuahidi
nitakulinda dhidi ya mipango
yoyote mibaya inayopangwa
juu yako” akasema Mark Piller
“Mark….. !
“Habiba tafadhali ! Sisi
nawe tumetoka mbali sana na
umetusaidia mambo mengi
naomba mashirikiano yetu
yaendelee kama kawaida na
ninakuahidi kukulinda hata
kama ni kwenda kinyume na
wenzangu wote niko tayari
kufanya hivyo.Tafadhali
Habiba” akasema Mark
“Mark nimekuelewa lakini
nataka kufahamu jambo
moja.Nataka kufahamu namna
mlivyopanga mipango ya
kutuua mimi na Abu Zalawi”
akasema Habiba na Mark
akamueleza mipango yote
namna ilivyopangwa ya
kuwaua yeye na Mathew
“Mark Piller unadhani nini
kitakutokea pale wenzako
watakapobaini kuwa
umewasaliti?akauliza Habiba
“Ninafahamu nitakuwa
matatizoni lakini niko tayari
kukabiliana na chochote
kitakachonitokea.Misheni hii
ni muhimu mno kwa nchi
yangu na kwa namna yoyote ile
lazima ifanikiwe” akasema
Mark Piller
“Sawa Mark
nimekuelewa.Nitashirikiana
nawe kuhakikisha misheni hii
inafanikiwa.Nitajitahidi
kuhakikisha Abu Zalawi
anapata taarifa mapema kabla
ya watu wa Mossad
hawajamfikia.Ninachotaka
ukifanye ni kuendelea kunipa
taarifa za mipango yenu yote
mnayoipanga ili na mimi
nitafute namna ya kumsaidia
Abu Zalawi” akasema Habiba
“Nitakujulisha kila kitu
Habiba Jawad lakini
nakuomba nawe uchukue
tahadhari kuanzia sasa.Pale
utakapoitwa uje Marekani toa
kisingizio kwamba hautaweza
kwa sasa kuna mambo ya
msingi unayashughulikia na
mimi nitaongeza
nguvu.Ongeza ulinzi na mtu
yeyote asiyefahamika
asikaribishwe katika makazi
yako” akasemaMark Piller
“Nakushukuru Mark.Mimi
nitahakikisha Abu Zalawi
anakuwa salama na
anaendelea na mipango yake
yote kama alivyotumwa nchini
Iran” akasema Habiba
wakaendelea na mazungumzo
kidogo wakapeana mikakati
namna watakavyokuwa
wakiwasiliana kwa siri kisha
wakaagana.
“Nilijua tu lazima
watagundua kuhusu Mathew
lakini sikutegemea iwe
mapema namna
hii.Nilifahamu
watakapogundua kuhusu
Mathew mzigo wote wa
lawama nitaubeba mimi na
nilikwisha jiandaa kwa jambo
hilo.Kwa sasa baada ya
kuifahamu mipango yao
natakiwa kuhakikisha Mathew
anakuwa salama ili aweze
kuikamilisha misheni yake”
akawaza Habiba Jawad na
kuchukua simu nyingine
akazitafuta namba Fulani na
kupiga kisha simu ikapokelewa
“Habiba” akasema mtu
aliyepokea simu upande wa
pili
“Vahid
unaendeleaje?akauliza Habiba
Jawad
“Siwezi kusema naendelea
vizuri Habiba.Bado kifo cha
mwanangu Najma
kinaniumiza mno.Ninajuta
kwa nini nilimruhusu aje
Riyadh.Kama ningeendelea
kukaa naye hapa Tehran
yasingemkuta haya
yaliyomkuta.Kwa ujumla bado
siko sawa na itanichukua
muda mrefu kulizoea jambo
hili” akasema Vahid Ghorbani
baba mzazi wa Najma.Vahid
na Habiba waliwahi kuwa na
mahusiano na wakamzaa
Najma lakini hawakufunga
ndoa na kila mmoja
akaendelea na maisha yake.
“Vahid suala hili
linatuumiza sote.Huwezi kujua
niko katika hali gani kwa sasa
baada ya kuwapoteza wanangu
wawili ndani ya kipindi
kifupi.Ni wakati mgumu sana
huu kwetu sote hivyo
tusaidiane kufarijiana badala
ya kulaumiana” akasema
Habiba
“Sikulaumu Habiba
nafahamu ulivyompenda
Najma.Tuachane na hayo vipi
maendeleo yako?
“Kama nilivyokwambia
Vahdi kwamba siko
sawa.Nimewapoteza watoto
wawili ndani ya kipindi kifupi
ni suala zito kulibeba lakini
ninajitahidi.Hata hivyo
sijakupigia simu kwa suala
hilo.Vahdi kuna jambo nataka
unisaidie”
“Sema chochote
Habiba.Unataka nikusaidie
nini?akauliza Vahid
“Kuna wanasayansi sita wa
Iran waliokuwa wamepotea
lakini leo hii wamerejea
nyumbani”akasema Habiba
“Nimepata taarifa hizo
kwamba wale watu wetu
waliokuwa wamepotea
wamerejea nyumbani leo hii
lakini haijatolewa taarifa rasmi
kwamba walikuwa wapi muda
huu wote” akasema Vahid
“Aliyewakomboa watu hao
na kuwarejesha nyumbani
anaitwa Abu Zalawi”
“Abu Zalawi?! Vahdi
akauliza
“Ndiyo.Anaitwa Abu
Zalawi”
“Ni mtu wa wapi huyo Abu
Zalawi?
“Ni Raia wa Saudi Arabia”
“Hatujafahamishwa jambo
hilo.Nini unataka nikusaidie
Habiba? Akauliza Vahid
“Ninataka ufanye kila lililo
ndani ya uwezo wako uweze
kuonana na huyu Abu Zalawi”
“Nionane na Abu Zalawi?
Vahid akauliza
“Ndiyo.Kuna ujumbe wa
muhimu sana ambao nataka
umfikishie”akasema Habiba
“Habiba sifahamu alipo
huyo Abu Zalawi na wala sijui
ni jinsi gani nitaweza
kumpata” akasema Vahid
“Vahid unatakiwa ufanye
kila linalowezekana
kuhakikisha unampata Abu
Zalawi”
“Habiba sidhani kama
mimi ni mtu sahihi wa
kukusaidia kwenye jambo hilo”
akasema Vahid
“Vahid ni muhimu sana
ukaonana na Abu Zalawi.Huyo
ndiye mume wa Najma”
“Mume wa Najma?! Vahidi
akastuka
“Ndiyo ni mume wa
Najma”
“Najma alikuwa na
mume?Kwa nini hujawahi
kuniambia jambo hili?
“Najma mwenyewe ndiye
aliyetaka iwe siri na
tusikujulishe.Kama
unavyofahamu kuwa Najma
hakuwahi kuwa na mpenzi
lakini alipokutana na Abu
Zalawi akajikuta akimpenda na
kufunga naye ndoa ya kimya
kimya na alitoa maelekezo ya
kutokufahamisha jambo
hili.Alitaka yeye mwenyewe
akujulishe pale atakapokuwa
tayari lakini kwa bahati mbaya
hakuwahi kufanya hivyo mauti
yakamkuta” akasema Habiba
“Habiba ulikosea sana
kukubali kunificha kuhusu
Najma kuolewa wakati mimi
ndiye baba yake
mzazi.Hukunitendea haki
katika hili”akasema Vahid
“Nakubali Vahid kwamba
nilikosea lakini nilifanya hivyo
kuheshimu matakwa ya
mtoto.Alitaka akueleze jambo
hili yeye mwenyewe muda
utakapofika.Tusameheane
katika hilo”
“Nilipokuja msibani kwa
nini huku nijlisha kuwa Najma
alikuwa na mume hadi leo hii?
“Nilikuwa
nimechanganyikiwa Vahid
ndiyo maana sikukueleza
chochote.Tafadhali naomba
sana unisamehe kwa hilo”
akajibu Habiba.Baada ya muda
Vahid akauliza
“Unataka kumfikishia
ujumbe gani huyo Abu
Zalawi?akauliza Vahid
“Nataka uonane naye ana
kwa ana na umpe simu
nizungumze naye”
“Habiba umenipa mtihani
mgumu sana.Kwanza ni nani
huyo Abu Zalawi?Kwa nini
yuko hapa? Akauliza Vahid
“Vahid naomba unisaidie
hilo ninalokuomba ni muhimu
sana”
“Habiba niko tayari
kukusaidia lakini lazima
nifahamu huyu mtu ni nani na
kwa nini yuko hapa Iran?
“Abu Zalawi anataka
kuuawa na Mossad hivyo
nataka niongee naye nimpe
angalizo awe makini” akasema
Habiba
“Anataka kuuawa na
Mossad?akauliza Vahid
“Ndiyo.Kuna majasusi
wanatumwa kuja Tehran kwa
lengo la kumuua.Anatakiwa
aipate haraka sana taarifa
hiyo”akasema Habiba
“Kwani huyu Abu Zalawi
ni nani hadi Mossad watake
kumuua? Akauliza Vahid
“Vahid nitakueleza kila
kitu hapo baadae kuhusiana na
Abu Zalawi lakini kwanza
naomba unisaidie kufanya kila
uwezalo uonane naye na
umpatie simu nizungumze
naye.Unaweza ukanisadia kwa
hilo? Akauliza Habiba
“Sawa Habiba.Nitajitahidi
kumtafuta huyo Abu Zalawi”
“Jitahidi Vahid wewe ni
mfanya biashara mkubwa
nchini Iran unafahamiana na
watu wengi hata viongozi wa
serikali naamini haitakuwa
kazi ngumu kwako kufahamu
mahala alipo Abu Zalawi”
akasema Habiba Jawad na
kuagana na Vahid.
******************
Baada ya kutoka
kuzungumza na makamu wa
Rais,Jason na David walirejea
katika ofisi ya Jason ambaye
bila kupoteza muda akampigia
simu Moshe Levine
mkurugenzi wa Mossad
“Jason Washington”
akasema Moshe baada ya
kupokea simu
“Habari za muda huu
Moshe.Nimekupigia kufuatia
mazungumzo yetu ya awali”
akasema Jason
“Ndiyo Jason.Umefikia
wapi kuhusiana na yale
tuliyoyazungumza?akauliza
Moshe Levine
“Kama nilivyokueleza
asubuhi kwamba tunataka
kumuua Abu Zalawi.Bado
mpango huo unaendelea na
kama nilivyokudokeza
tunataka kuwatumia watu
wako wa Mossad walioko
nchini Iran” akasema Jason
“Jason nina watu wangu
Tehran ambao wanaweza
wakaifanya hiyo kazi muda
wowote watakapopewa
maelekezo lakini nilitoa
masharti asubuhi ya kama
mkitaka tuwasaidie kumuua
Abu Zalawi basi na nyinyi
mtupe taarifa za mahala alipo
Habiba Jawad.Mmefikia wapi
katika suala hilo?akauliza
Moshe Levine
“Tumejadiliana na
tumekubaliana jambo
moja.Habiba Jawad tutamuua
sisi wenyewe pale ambapo
nanyi mtakuwa mmemuua
Abu Zalawi”
“Jason hatukukubaliana
hivyo.Ninataka mtupe taarifa
za mahala alipo Habiba Jawad
na tutamkamata sisi
wenyewe.Hatutaki kumuua
kuna mambo mengi tunahitaji
kuyafahamu kuhusiana na
mtandao wake kabla ya
kumuua hivyo tupeni taarifa za
mahala alipo sisi tutamkamata
hatuhitaji msaada wa kumuua”
akasema Moshe Levine
“Moshe sisi tuko tayari
kutoa aina yoyote ya
ushirikiano kwenu.Kama
hamtaki kumuua Habiba
hatuna tatizo na hilo.Sisi
tutamkamata Habiba na
tutamkabidhi kwenu lakini
lazima kwanza tuhakikishe
Abu Zalawi ameuawa ndipo
tutawakabidhi Habiba
Jawad.Tunakubaliana katika
hilo?akauliza Jason
“Jason tunamtaka Habiba
Jawad kwanza ndipo
tuwafanyie kazi yenu ! Kuna
ugumu gani wa kutupa taarifa
za mahala alipo Habiba ?
akauliza Moshe Levine
“Moshe sisi na ninyi ni
washirika wakubwa tena wa
miaka mingi tunapaswa
kuaminiana.Tuna sababu za
msingi kwa nini hatuwezi
kuwapa taarifa za mahala alipo
Habiba Jawad.Naomba
uniamini Moshe kwamba
tutamkabidhi kwenu Habiba
Jawad pale tutakapokuwa na
uhakika kwamba Abu Zalawi
ameuawa.Hivi tuzungumzavyo
tayari timu inaandaliwa kwa
ajili ya kwenda kumkamata
Habiba Jawad.Tutamuhifadhi
hadi pale ambapo mtakuwa
mmekamilisha zoezi la
kumuua Abu Zalawi”
“Jason kutakuwa na
ugumu katika jambo
hilo.Tupeni Habiba Jawad na
sisi tumuue Abu Zalawi”
“Moshe nakuhakikishia
kwamba hata dakika hii
mkimtaka Habiba Jawad
mtampata lakini hatuwezi
kumkabidhi Habiba kwenu
wakati bado hamjatekeleza
kazi yetu.Muondoeni Abu
Zalawi kwanza ili mumpate
Habiba
“Tufanye
hivi.Tudhihirishieni kwanza
kama kweli mnaye Habiba
Jawad na tutaelekeza apelekwe
katika ubalozi wenu Jerusalem
na baada ya kumuua Abu
Zalawi mtamkabidhi
kwetu.Tunakubaliana katika
hilo”
“Hakuna tatizo katika
hilo.Tutafanya hivyo”
“Vizuri.Nashukuru kama
tumekubaliana hivyo Jason
basi na sisi tunaanza mara
moja mpango wa kumuua Abu
Zalawi.Tutaendelea
kufahamishana kila hatua
tunayopiga” akasema Moshe
Levine wakaagana
“Mambo yanazidi kuwa
magumu David” Jason
akamwambia David na
kumuelezea kila kitu
walichozungmza na Moshe
Levine
“Nini maamuzi yako katika
jambo hili? akauliza David
Walker
“Hatuna ujanja lazima
tumkamate Habiba Jawad na
kumuandaa kwa ajili ya
kuwakabidhi Mossad pale
watakapokuwa wamemuua
Abu Zalawi”
“Jason huo ni mpango wa
hatari sana.Ni vipi kama
wakimchunguza na kugundua
kuwa tumekuwa
tunashirikiana naye?akauliza
David
“Tutamuweka Habiba
Jawad katika ubalozi wetu
jijini Jerusalem na baada ya
wao kumuua Abu Zalawi sisi
pia tutamuua Habiba Jawad
na kuwakabidhi maiti
yake.Hatuwezi kuwakabidhi
Habiba akiwa mzima”
akasema Jason wakaendelea
kujadiliana kuhusiana na
mpango ule halafu Jason
akainua simu na kumjulisha
Mark Piller kuhusu
mazungumzo yake na Moshe
Levine pamoja na mpango
waliouandaa.
Mark Piller baada ya
kumaliza maongezi na Jason
akampigia simu Habiba Jawad
“Mark karibu tena”
akasema Habiba
“Habiba nimerejea tena
kama nilivyokueleza awali
kwamba nitakuwa ninakupa
taarifa mipango yote
inayopangwa dhidi yako”
akasema Mark na kumueleza
Habiba kuhusiana na mpango
ule wa kutuma kikosi kwenda
kumteka na kumpeleka katika
ubalozi wa Marekani jijini
Jerusalem tayari kwa
kukabidhiwa kwa Mossad pale
watakapokuwa wamefanikisha
mpango wa kumuua Abu
Zalawi.
“Ahsante sana Mark Piller
kwa angalizo hilo.Tayari
nimekwisha anza taratibu za
kumtafuta Abu Zalawi na
kujua mahala alipo ili niweze
kumuonya kuhusiana na
mpango wa
kumuua.Nategemea kabla ya
watu hao wa CIA waliotumwa
kuja kunikamata hawajafika
hapa tayari nitakuwa
nimekwisha mpata Abu
Zalawi” akasema Habiba
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Kiza tayari kilikwishatanda
katika jiji la Dar es
salaam,Nawal alitoka
chumbani kwake na kwenda
kukaa sehemu ya kupumzikia
iliyo mbele ya nyumba ile
wanakoishi viongozi wa vikosi
vya jeshi la Marekani vilivyopo
Dar es salaam.Taa zilikuwa
zinawaka katika nyumba hii
kwani walikuwa wanatumia
jenereta .Ulinzi pia ulikuwa
mkali karibu kila pembe ya
nyumba hii kulikuwa na
walinzi.Akiwa amejipumzisha
mbele ya nyumba muhudumu
akamfuata na kumuuliza kama
angependa kutumia kinywaji
chochote na Nawal
akamuagiza amtengenezee
kahawa
“Nilipowasiliana na Ruby
saa kumi na mbili jioni,bado
Jenerali William hakuwa
amerejea ofisini kwake na hadi
giza limeingia hatujui mahala
alipo Sattar.Kwa namna yoyote
ile lazima usiku wa leo tujue
mahala kilipo
kirusi.Nitamvamia Jenerali
William usiku wa leo
chumbani kwake na lazima
ataeleza alipo Sattar na
kirusi.Kitu kikubwa
ninachohitaji kufahamu ni
watu wangapi wanaoishi ndani
ya nyumba hii ili nijue namna
ninavyoweza kukabiliana nao
na kama nikiona sintaweza
basi nitaomba msaada kutoka
SNSA.Nitakaa hapa hapa hadi
jenerali William atakaporejea”
akawaza Nawal na kutolewa
mawazoni baada ya kahawa
yake kuletwa.
“Ahsante sana.Jina lako
nani nimelisahau” akauliza
Nawal
“Naitwa Brenda”
“Ouh Brenda .Naitwa
Chloe” akasema Nawal na
kumtaka Yule muhudumu
kukaa kwa ajili ya
mazungumzo lakini Brenda
akamjulisha kwamba
watazungumza pale
atakapokuwa amekamilisha
majukumu yake
“Huyu Brenda anaweza
akanipa taarifa za kutosha
kuhusu mahala hapa.Ngoja
nimsubiri amalize majukumu
yake” akawaza Nawal
akiendelea kunywa kahawa
yake taratibu
Akiwa ameyaelekeza
macho yake katika geti mara
akawaona wanajeshi
waliokuwa wakilinda geti
wakiwa katika heka heka
akakaza macho zaidi ili kujua
kinachoendelea.Geti
likafunguliwa na gari nne
zikaingia mle ndani.Tatu
zikiwa ni gari za doria za jeshi
la Marekani na moja ikiwa ni
aina ya Prado.Kutoka katika
mojawapo ya gari akashuka
Jenerali William na na
makamanda wengine wawili
na kutoka katika ile Prado
wakashuka watu wanne ambao
hawakuwa wanajeshi.Nawal
alihisi mapigo ya moyo wake
yakibadilika na kwenda haraka
haraka baada ya kuziona sura
za wale jamaa walioshuka
katika Prado
“Sattar ! Assad ! akasema
kwa sauti ndogo ya mshangao
Jenerali William akiwa
ameongozana na wale jamaa
wengine wanne na wanajeshi
wawili wakaanza kupiga hatua
kuelekea ndani ya ile nyumba.
“Chloe ! akasema Jenerali
William baada ya kumkuta
Nawal amekaa nje
“Jenerali William”
akasema Nawal na kusimama
“Habari za toka
mchana?Umeshinda salama?
Akauliza Jenerali William
“Niko salama kabisa
Jenerali William.Nimepata
huduma nzuri”
“Nafurahi kusikia hivyo
Chloe.Hawa ni wenzangu Meja
Greg na Meja Thomas”
akasema Jenerali William na
kufanya utambulisho.
“Huyu ni mmarekani
mwenzetu ambaye alikuwa
hapa Tanzania katika shughuli
zake za upigaji picha lakini
alijikuta amenasa katika
machafuko na jana
amekombolewa na vikosi vya
jeshi la Tanzania akaletwa Dar
es salaam na leo mchana Rais
akanikabidhi.Chloe ataishi na
sisi hapa hadi pale hali ya
amani itakapokuwa nzuri”
akasema Jenerali William na
kumtaka Nawal waingie
ndani.Miguu ya Nawal ilikuwa
inagongana kwa kile
alichokuwa
amekishuhudia.Katika wale
watu walioongozana na
Jenerali William
aliwashuhudia kwa macho
watu wawili waliokuwa
wanawatafuta kwa jasho na
damu.Assad Ismail na Sattar
Sayf Al Din
“Siamini ninachokiona
huu ni kama muujiza
mkubwa.Watu wote hawa
wawili Assad na Satter wote
tunawatafuta kwa kila
namna.Hadi mwili wangu
unatetemeka sikuwa
nimelitegemea kabisa jambo
hili.Lakini mbona hawana yale
masanduku ya
kirusi?Wamekipeleka wapi?
Au tayari wamekwisha anza
kukisambaza?akajiuliza Nawal
“Usiku wa leo lazima kila
kirusi kipatikane.Wamejileta
wenyewe kwenye mdomo wa
Mamba na hawatatoka
salama” akawaza Nawal
Jenerali William
akamuelezea Brenda
kumpeleka Nawal katika
chumba maalum cha
mapumziko wakati yeye
akiendelea na mazungumzo na
wageni wake.Nawal hakwenda
katika chumba cha mapumziko
bali alielekea moja kwa moja
chumbani kwake na kitu cha
kwanza alichokifanya ni
kuishika simu akampigia Ruby
“Hallo Ruby ! akasema
Nawal
“Nawal kuna nini?Mbona
unahema haraka haraka
namna hiyo?Kuna tatizo?
akauliza Ruby
“Ruby wako hapa !
akasema Nawal
“Akina nani
Nawal?akauliza Ruby
“Assad na Sattar wote
wako hapa.Wamekuja na
Jenerali William” akasema
Nawal
“Nawal una uhakika ni
wenyewe?
“Nimewashuhudia mimi
mwenyewe kwa macho
yangu.Wamefika muda si
mrefu wakiwa wameongozana
na Jenerali William”
“Yale masanduku mawili
aliyoshuka nayo Sattar
ndegeni ambayo tunaamini
yana kirusi yameletwa
hapo?akauliza Ruby
“Hapana Ruby kirusi
hakipo hapa.Yawezekana kuna
mahala kimehifadhiwa au
yawezekana tayari kimekwisha
pelekwa kusambazwa”
akasema Nawal
“Hapana bado
hakijasambazwa kwani mtu
pekee aliyeletwa kuja
kusambaza kirusi hicho ni
Sattar Sayf Al Din.Kama
hayuko nacho hapo basi lazima
kirusi hicho kimehifadhiwa
sehemu Fulani wakisubiri
muda ufike
wakisambaze.Nawal usiku huu
wa leo lazima tuhakikishe
tunakipata kirusi hicho.Ni kufa
na kupona leo lazima nyumba
hiyo ivamiwe tuwachuku watu
hao wote waliomo katika hiyo
nyumba na watatuonyesha
mahala kilipo kirusi.Nawal
endelea kufuatilia watu hao
kama wataondoka au watalala
hapo wakati tunaandaa kikosi
kwa ajili ya kuvamia nyumba
hiyo.Kuanzia mchana wa leo
tumekuwa tukiichunguza
nyumba hiyo na kuona namna
walivyojipanga
kiulinzi.Makomando wetu
wako tayari na muda
utakapowadia watavamia
nyumba hiyo.Nawal
tunakutegemea sana uweze
kuwasaidia timu ya
makomando watakapofika
hapo” akasema Ruby
“Tayari nimekwisha
yasoma mazingira ya hapa na
ulinzi ulivyo hivyo hakuna
tatizo nitasaidiana na timu
itakayofika hapa” akasema
Nawal na kumpa Ruby
maelekezo kadhaa
Mara tu alipomaliza
kuzunguma na Nawal Ruby
akampigia Gosu Gosu
akamtaka afike ofisini kwake
mara moja akamueleza
kuhusiana na kile alichoelezwa
na Nawal
“Ruby mpaka hapo
naamini tayari tumekwisha
kipata kirusi.Usiku huu lazima
tuwapate hawa magaidi wote
pamoja na
kirusi.Nitaongozana na
makomando wetu
watakaokwenda kuvamia
nyumba hiyo” akasema Gosu
Gosu
“Hapana Gosu
Gosu.Tuwaache makomando
waende.Wewe utakuwa na kazi
ya kuwahoji akina Assad
kufahamu mahala kilipo kirusi
pale watakapokuwa
wameletwa hapa” akasema
Ruby
“Ruby kwa nini hutaki
nishiriki katika misheni siku
hizi? Kila ninapotaka kushiriki
katika misheni unanizuia.You
don’t trust me?akauliza Gosu
Gosu
“Si hivyo Gosu Gosu.Sitaki
kuyaweka hatarini maisha
yako wakati tayari tunacho
kikosi kinachoweza
kupambana .Kumbuka huko
wanakoenda kunalindwa na
wanajeshi wa Marekani ambao
wana mafunzo ya hali ya juu
hivyo itakuwa ni nusu
vita.Naamini kikosi chetu cha
makomando kina uwezo
mkubwa sana wa kuweza
kufanikisha misheni hii.Kama
nilivyokuahidi kwamba wewe
utafanya kazi ya kuwahoji
akina assad watakapoletwa
hapa” akasema Ruby
“Ruby imekuaje ukabadili
mawazo leo na unataka
niwahoji magaidi?akauliza
Gosu Gosu
“Kwa namna yoyote ile
tunahitaji kukipata kirusi
hivyo basi kila aina ya mbinu
lazima itumike wakati wa
kuwahoji magaidi hao ili
waweze kufunguka kirusi kiko
wapi”
“Sawa Ruby nitaifanya
kazi hiyo” akasema Gosu Gosu
kisha wakatoka kwenda
kuanza maandalizi kwa ajili ya
misheni ile
JASUSI/GAIDI
SEASON 5 : EPISODE 4
“Imekuwa vyema umefika
kwa wakati David kwani
tunakwenda kuonana na
makamu wa Rais amenitaka
nifike ofisini kwake” akasema
Jason Washington mkurugenzi
mkuu wa CIA baada ya David
Walker kufika ofisini kwake.
Bila kupoteza muda
wakaingia katika gari la Jason
na kuondoka kwenda kuonana
na Mark Piller makamu wa
Rais
“Nini kimejiri huko katika
kikao? Akauliza Jason na
David akamweleza kila kitu
walichokubaliana katika kikao
“Vizuri sana.Nilimdokeza
Mark Piller kuhusiana na
mpango wetu wa kumuondoa
Abu Zalawi.Mark amestushwa
sana na jambo hili ndiyo
maana amenitaka nikaonanye
naye kwani tusingeweza
kuzungumza kwa kirefu katika
simu.Haamini kile
nilichomweleza kuhusu Abu
Zalawi” akasema Jason
Washington
“Suala hili la Abu Zalawi
linaumiza vichwa sana.Kila
mtu anashangaa kuhusu
jambo hili limetokeaje?
“Hatuna wa kumlaumu
katika hili David.Tumekosea
sisi wenyewe na lazima
tuchukue hatua za haraka sana
kuhakikisha jambo hili
halitakuwa na madhara
kwetu.Kama tungechukua
tahadhari mapema haya yote
yasingetoke ana misheni
ingeendelea kama kawaida”
akasema Jason
“Kuna kitu nimekuwa
najiuliza vipi kuhusu wale
jamaa wanasayansi tuliokuwa
tunawashikilia kwa muda
mrefu? Tunakubali
tumewapoteza?akauliza David
na Jason akatikisa kichwa
akisikitika
“Watu wale japo
hawajatupa taarifa tulizokuwa
tunazihitaji lakini ni watu wa
muhimu sana kwa Iran.Katika
hili tumewapa Iran ushindi
mwepesi lakini lazima
tuhakikishe nao pia wanauawa
pamoja na Abu Zalawi.”
akasema Jason
Walifika katika ofisi ya
makamu wa Rais ambaye
alikuwa anawasubiri na bila
kupoteza muda wakaingia
katika chumba cha maongezi
ya faragha na kikao kikaanza.
“Jason nimevuruga ratiba
yangu ya siku ya leo ili niweze
kuzungumza nanyi.Nataka
kufahamu kwa kina kuhusiana
na hiki kinachoendelea”
akasema makamu wa Rais
Mark Piller
Jason akamuelezea Mark
Piller kila kitu hadi
walipogundua kuhusu Abu
Zalawi kuwa si gaidi bali ni
jasusi pamoja na maamuzi
waliyoyachukua ya kumuua
“Jason jambo hili
limetokeaje? Kwa nini
haukufanyika uchunguzi wa
kina kuhusiana na huyu mtu
Abu Zalawi hadi tumefika hapa
tulpofika? Akauliza Mark Piller
“Katika hili Mark hatuna
wa kumlaumu mtu bali
tunapaswa kujilaumu sisi
wenyewe.Tulifanya uzembe wa
kutokufanya uchunguzi wa
kina kuhusiana na Abu Zalawi”
akasema Jason
“Lakini yote haya
ameyasababisha Habiba
Jawad ambaye tulimuamini
kwa asilimia mia moja na
hivyo tukamuamini yule mtu
aliyetuletea.Hata mara moja
hajawahi kutuangusha na
katika kila operesheni
tuliyomshirikisha hakujawahi
kutokea matatizo.Hii ni mara
ya kwanza Habiba anatufanyia
kitu cha namna hii” akasema
David Walker
“Mnadhani Habiba
alikuwa na lengo lake binafsi la
kumleta kwetu Abu
Zalawi?akaliza Mark Piller
“Hatuna uhakika bado
ndiyo maana tunataka
kulifanyia uchunguzi suala hilo
lakini wakati uchunguzi huo
ukiendelea tunataka
kumuondoa kwanza Abu
Zalawi pamoja na wale
wanasayansi tuliokuwa
tunawashikilia” akasema
Jason.Baada ya tafakari ya
muda mfupi Mark akauliza
“Kutakuwa na athari gani
kama tukimuacha Abu Zalawi
akaendelea na misheni lakini
tukimfuatilia kwa ukaribu
mkubwa kujua kila
anachokifanya kwa kuwatumia
hao majasusi wa Mossad
ambao mnataka kuwatumia
kumuua?akauliza Mark Piller
na Jason akampa maelezo
aliyopewa na Moshe Levine
mkuu wa Mossad kuhusu Abu
Zalawi na Mark akazidi
kuchoka.
“Mark hatuna namna
lazima tumuondoe Abu Zalawi
haraka sana ili kujihakikishia
usalama wetu.Endapo
tukishindwa kumuondoa Abu
haraka itatugharimu baadae”
akasema Jason.Waliendelea na
majadiliano kwa muda halafu
Mark Piller akasema
“Jason na David
nimekubalianba na
mapendekezo yenu juu ya
suala hili lakini nina
ushauri.Hatuwezi kumuua
Habiba Jawad nchini kwao
Saudi Arabia.Habiba Jawad
ana ukaribu mkubwa na
mfalme wa Saudi Arabia
ambaye ni mshirika mkubwa
wa Marekani hivyo lazima
tujihadhari tusivuruge
mahusiano mazuri kati yetu na
serikali ya Saudi
Arabia.Habiba aitwe Marekani
na akifika huku ndipo
atakapouawa” akashauri Mark
Piller
“Ushauri mzuri
tutauzingatia” akasema Jason
“Angalizo.Habiba asiuawe
kama Mossad hawajamuua
Abu Zalawi.Pale ambapo Abu
Zalawi atakuwa ameuawa
ndipo Habiba auawe kwani
tunaweza kumuua Habiba
halafu Mossad wakashindwa
kumuua Abu Zalawi.Kama
kuna jambo wawili hawa
wanalipanga lazima
tuwaondoe wote wawili
akiondolewa mmoja na
mwingine akabaki hatutakuwa
tumefanya kitu” akasisitiza
Mark Piller.Baada ya
majadiliano Jason na David
wakaondoka .Mark Piller
hakupoteza muda akainua
simu na kumpigia Rais
William Washington
“Mheshimiwa Rais nahitaji
kukuona sasa hivi” akasema
Mark
“Njoo ofisini” akajibu Rais
William na Mark Piller
akatoka ofisini kwake kuelekea
ofisini kwa Rais.
“Mark mpango wenu
unakwenda
vizuri.Nimefurahishwa na
taarifa nilizozipata kwamba
ndege ile iliyopotea
imeonekana ikielekea nchini
Iran” akasema Rais William
baada ya Mark kufika ofisini
kwake
“Mheshimiwa Rais ni
kweli mpango umekwenda
vizuri sana na hivi
tuzungumzavyo tayari mtu
wetu amekwisha kanyaga
ardhi ya Iran” akasema Mark
Piller
“Vipi mna mawasiliano
naye baada ya kuwasili Iran?
Akauliza Rais William
“Mheshimiwa Rais
mpango wetu wa kwanza
ulikuwa ni kumuingiza Abu
Zalawi nchini Iran na mpango
huo umefanikiwa vizuri lakini
kuna tatizo limejitokeza”
akasema Mark Piller na sura
ya Rais William aikabadilika
“Kumetokea tatizo gani
tena” akauliza William
“Baada ya Abu Zalawi
kufika salama Iran tulihitaji
kumpa msaada na kwa vile
hatuna wetu wetu kule Iran
ilitulazimu kuomba msaada
kutoka kwa wenzetu wa
Mossad ambao wana majasusi
wao Iran na hapo ndipo
lilipoibuka jambo ambalo
hatukuwa tukilifahamu”
akasema Mark Piler na
kumueleza Rais William kila
kitu walichokifahamu kutoka
kwa Mossad kuhusiana na Abu
Zalawi.Zilikuwa ni taarifa
zilizomstua sana William
“Mark kwa nini haya yote
yametokea?Kwa nini
hamkuchukua tahadhari
mapema kuhakikisha
mnamfahamu vyema mtu
ambaye mnataka kumtumia
katika misheni kubwa kama
hii? Akauliza William
“Mheshimiwa Rais katika
hilo tunakiri tulikosea na
ndiyo maana tunataka
kuchukua hatua za haraka za
kurekebisha kwa kumuondoa
Abu Zalawi haraka sana kabla
hajaendelea na misheni
aliyotumwa nchini Iran”
“Kumuua Abu Zalawi ni
suluhisho la jambo
hili?akauliza William
akionekana kukasirika
“Mheshimiwa Rais huyu
mtu ni hatari kwetu kama
tukiendelea kumuacha
hai.Tayari anafahamu kila kitu
kuhusu sisi na baya zaidi
anafahamu ni sisi tulio nyuma
ya kile kilichotokea Tanzania
na Afrika mashariki na
anafahamu kwa nini tulifanya
vile….”
“Pamoja na kufahamu !
akasema kwa ukali Rais
William na kumkatisha Mark
Piller
“Pamoja na kufahamu
hayo yote lakini bado Abu
Zalawi au vyovyote vile
anavyofahamika amekubali
kuifanya kazi aliyotumwa na
kwa sasa tayari amefika nchini
Iran.Anafahamu kabisa
kwamba kazi aliyotumwa
kuifanya Iran ni kazi ya hatari
kubwa na kama akijulikana
kuwa ni pandikizi la Marekani
anaweza akauawa muda
wowote ule lakini bado yuko
tayari kufanya.Kumuua Abu
Zalawi ni kosa kubwaMark !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais pamoja
na Abu Zalawi kukubali
kuifanya kazi aliyotumwa
aifanye lakini hakuna anayejua
moyoni mwake nini
anakiwaza,hatujui ana
mipango gani dhidi yetu.Kwa
taarifa tuliyoipata kutoka kwa
Mossad ni kwamba Abu Zalawi
ameyatoa maisha yake katika
kupambana na ugaidi hasa
kundi la IS linaloendelea
kuotesha mizizi katika eneo la
Afrika Mashariki.Abu Zalawi
ni bilionea na ana familia
inaishi Paris Ufaransa lakini
ameacha hivyo vyote
akajielekeza katika kupamba
na na magaidi.Jaribu kupata
picha mtu kama huyu anakuja
kugundua kwamba
tunashirikiana na magaidi wa
IS na kibaya zaidi kuchochea
machafuko katika nchi
anakotoka na kusababisha vifo
vya watu na sisi tukiendelea
kubeba tani na tani za mafuta
unadhani mtu kama huyu
atafanya nini?Lazima atakuwa
na chuki kubwa sana dhidi
yetu na hatujui nini
anakifikiria lakini ni wazi
jambo hili hataweza
kulivumilia” akasema Mark
Piller
“Mark nimekuelewa lakini
maamuzi ya kumuua mtu
kama huyu si sahihi.Mtu kama
huyu bado anaweza akawa
upande wetu.Tunaweza
kuzungumza naye na
kumfanya atuelewe na hata
kama alikuwa na kitu moyoni
mwake tukakiondoa.Sisi ni
taifa kubwa na hatuwezi
kukubali kushindwa kirahisi
namna hii.Hebu fikiria
Mark,nini kingine mtakifanya
kitakachowawezesha
kupandikiza mtu nchini Iran?
Kwa kuwatumia wale mateka
wa Iran imekuwa rahisi kwetu
kuweza kupenyeza mtu ndani
ya Iran na kama mkiharibu
msheni hii itachukua miaka
mingi kuweza kufanikisha
jambo kama hili na pengine
lisiwezekane tena.Kwa kuwa
tayari Abu Zalawi amekwisha
ingia Iran,itafutwe namna ya
kuzungumza naye na
kumuweka sawa aendelee na
jukumu lake badala ya
kufikiria kumuua” akasema
Rais William
“Mheshimiwa Rais…..”
Mark Piller akataka kusema
kitu lakini Rais William
akamzuia
“Mark sitaki kuendelea na
mjadala huu.Hatuwezi kuipa
Iran ushindi kirahisi namna
hii lazima kwa namna yoyote
ile misheni hii iendelee.Iran ni
taifa tishio kwa Marekani kwa
sasa na lazima tufahamu
uwezo wake wa silaha hivyo
lazima misheni iendelee.Abu
Zalawi hapaswi kuuawa !
akasema kwa sauti ya msisitizo
kisha wakabaki wanatazamana
“Mheshimiwa Rais sidhani
kama unaiona hatari iliyoko
mbele yetu kama tukiendelea
kumtumia huyu Abu Zalawi !
akasema Mark
“Mark sijali chochote,
ninachohitaji ni Abu Zalawi
aendelee na misheni
aliyotumwa nchini
Iran.Endapo Abu akiuawa na
misheni ikashindwa kuendelea
ninaapa nitakifuta hiki kikundi
chenu kwani hakitakuwa na
maana tena.Sijali kama
nitauawa ama nini kitatokea
lakini lazima nikifute !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais
nilipokuja kukueleza
kuhusiana na kikundi hiki na
mambo yake nilikupa angalizo
kwamba unatakiwa usiri
mkubwa kwani Rais wa nchi
hapaswi kufahamu chochote
kuhusu uwepo wa kikundi
hiki.Utayaweka maisha yetu
sote katika hatari
kubwa.Nakuomba
mheshimiwa Rais usifikirie
kufanya hicho hicho
unachotaka kukifanya”
akasema Mark Piller
“Mark mimi siogopi
chochote na ninakuhakikishia
kwamba nitafanya hivyo na
wamarekani watajua kuwa
nchi yao inashirikiana na
magaidi”
“Mheshimiwa Rais !
akasema Mark
“Mark fanya
ninavyokuelekeza.Ukitaka
kundi lenu liendelee
kuwepo.Nataka Abu zalawi
aendelee na misheni yake
nchini Iran.Sitaki auawe.Fanya
kila linalowezekana
kuhakikisha misheni yake
inafanikiwa.Tunaihitaji sana
misheni hii ama sivyo Iran
itaendelea kutoa vitisho vya
kusishambulia Marekani!
Siwezi kuzivumilia kauli chafu
za vitisho zinazotolewa na Rais
wa Iran dhidi ya Marekani !
akasema Rais William
“Mheshimiwa Rais
kufanya hicho unachotaka
nikifanye ni usaliti mkubwa
kwa wenzangu na…..”
“Mark kumbuka kwamba
sisi ndio tunao ongoza nchi hii
na dhamana ya usalama wa
watu wetu tumeibeba sisi na
kwa sasa watu wetu wana hofu
kufuatia vitisho vya Iran kuwa
anao uwezo wa kuishambulia
na kuiharibu Marekani hivyo
basi lazima tufanye kila lililo
ndani ya uwezo wetu
kuhakikisha tunaiweka nchi
yetu salama pamoja na watu
wake ndiyo maana ninasema
kwamba tunaihitaji sana
misheni hii kwa ajili ya
kufahamu wezo wa silaha za
Iran na baada ya hapo
tutaichakaza vibaya
sana.Ikitokea Iran
imeshambulia Marekani
watakaobeba mzigo wa
lawama ni sisi na si hao ambao
unaogopa kuwasaliti.Mark
fanya kila linalowezekana hata
kama ni kwa kuwasaliti
wenzako hakikisha Abu Zalawi
anakuwa salama na
anaendelea na misheni yake
nchini Iran.Vuruga mpango wa
kumuua ! akasema Rais
William na Mark Piller
akainamisha kichwa
akitafakari
“Umenielewa Mark
Piller?akauliza Rais William
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais.Nitafanya
kama ulivyoelekeza lakini
naomba ufahamu kwamba ni
jambo la hatari kubwa”
“Usihofu kuhusu hilo
Mark.Kama kuna hatari yoyote
unaihisi nijulishe na mimi
nitakulinda.Tunayafanya haya
kwa maslahi ya nchi yetu”
akasema Rais William na Mark
Piller akaondoka akarejea
ofisini kwake na kujiegemeza
kitini
“Hili jambo linaendelea
kubadilika kila wakati.Rais
anataka niwasaliti wenzangu
na kuvuruga mipango ya
kumuua Abu Zalawi ! akawaza
Mark
“Lakini ukilitazama jambo
hili kwa kina zaidi,Rais yuko
sahihi.Hatupaswi kumuua Abu
Zalawi badala yake tunapaswa
kufanya kila liwezekanalo
kumuweka upande wetu.Kwa
hiyo kwa mara ya kwanza
nitalazimika kuwasaliti
wenzangu na kuvuruga
mpango wa kumuua Abu
Zalawi.Kuna mtu mmoja tu
ambaye ninatakiwa
kuzungumza naye” akawaza na
kufungua mkoba wake akatoa
simu iliyokuwa na namba
kumi na mbili tu ambazo ni
namba za watu muhimu
akaelekeza kidole chake katika
namba ya sita ambayo ilikuwa
ni namba ya Habiba Jawad
akampigia baada ya sekunde
kadhaa simu ikapokelewa.
“Mark Piller ! akasema
Habiba Jawad akionekana
kushangaa
“Habiba Jawad
unaendeleaje? Akasema Mark
“Ninaendelea vizuri
Mark.Nimeshangaa kidogo leo
umenipigia simu.Sikutegemea
kabisa kupata simu yako”
akasema Habiba Jawad
“Habiba nimelazimika
kukupigia simu kuna mambo
ya muhimu sana ya
kuzungumza mimi nawe na
ninakuomba tafadhali yale
tutakayoyazungumza hapa
yawe ni baina yetu sisi
wawili.Mtu mwingine yeyote
kutoka G20 hatakiwi
kufahamu kama nimekupigia
simu.Umenielewa
Habiba?akauliza Mark Piller
“Nimekuelewa Mark.Nini
unataka kuzungumza
nami?akauliza Habiba
“Kwanza kabisa ninataka
kukupa taarifa kuwa mpango
wetu umekwenda vizuri na hivi
tuzungumzavyo tayari Abu
Zalawi amekwisha ingia nchini
Iran” akasema Mark Piller
“Hizo ni taarifa njema
sana.Nimefurahi kusikia
matokeo mazuri ya mpango
huu.Ninakuhakikishia Mark
kuwa kama tayari Abu
amefanikiwa kuingia nchini
Iran lazima atafanikisha kila
kitu alichotumwa
kukifanya.Kitu cha msingi kwa
sasa ni kujitahidi kutafuta
namna ya kuwasiliana naye na
kujua maendeleo yake”
akasema Habiba
“Tayari tumelifanya hilo
Habiba ila kuna tatizo
limejitokeza”
“Tatizo gani
Mark?akauliza Habiba
“Baada ya kuhakikisha
Abu Zalawi ameingia Iran
ilitulazimu kuomba msaada
kutoka kwa wenzetu wa
Mossad ambao wana watu wao
kule Iran kwa ajili ya kumpa
msaada na hapo ndipo
tulipofahamu kila kitu kuhusu
Abu Zalawi” akasema Mark na
kumueleza Habiba kila kitu
walichokigundua kuhusu Abu
Zalawi.Kupitia spika za simu
Habiba Jawad akasikika
akivuta pumzi ndefu
“Habiba unaweza
ukazungumza chochote
kuhusiana na jambo
hili?akauliza Mark
“Sina cha kuzungumza
Mark lakini kila kitu
mlichoelezwa kuhusu Abu
Zalawi ni cha kweli” akasema
Habiba na Mark Piller akahisi
mwili unamtetemeka
“Kwa nini Habiba kama
ulifahamu kuwa Abu Zalawi ni
jasusi tena anatokea Tanzania
ukamleta kwetu tukampa
misheni kubwa kama hii?
Akauliza Mark Piller
“Kwa sababu Abu Zalawi
ndiye pekee anayeweza
kuifanya kazi hii.Hakuna gaidi
ambaye ana uwezo wa kuingia
Iran na kufanya jambo la
hatari la kuichunguza Iran
zaidi ya Abu Zalawi.Mark hii si
misheni ya kigaidi hii ni
misheni ya kijasusi na mtu
niliyewaletea ndiye anayefaa”
akasema Habiba Jawad
“Habiba sisi tulihitaji gaidi
lakini wewe ukatuletea jasusi
tena anatokea Tanzania nchi
ambayo kwa kushirikiana na
magaidi wa IS tumechochea
machafuko ya kidini na
kusababisha waumini
kushambuliana na damu
nyingi kumwagika na kama
haitoshi bado tunaendelea na
mpango wa kusambaza kirusi
hatari kwa lengo la kuendelea
kuchota utajiri mkubwa ulioko
Afrika Mashariki.Kwa nini
ukatufanyia hivi? Akauliza
Mark
“Mark kama
nilivyokueleza kwamba huyu
ndiye mtu pekee anayefaa kwa
misheni hii” akajibu Habiba
“Habiba japokuwa una
uhakika kuwa mtu huyu ndiye
anayefaa lakini tayari ana
kasoro.Hatujui ni kitu gani
anakiwaza baada ya kugundua
kwamba sisi tuko nyuma ya
kile kinachoendelea Afrika
Mashariki.Hii ni kasoro kubwa
na tayari imetia doa misheni
nzima” akasema Mark
“Mark nataka
nikuhakikishie kwamba Abu
Zalawi hana tatizo lolote na
msiwe na wasiwasi wowote
naye.Anakwenda kutekeleza
kile alichotumwa kukifanya
Iran na uwezo wa kufanya
hivyo anao.Abu Zalawi japo ni
jasusi lakini nimembadilisha
na anafanya kazi
kwangu.Nimembadili kutoka
Jasusi kuwa Gaidi.Ni mimi
pekee anayenisikiliza kila
ninachomuelekeza kukifanya
kwani nimemfanya kuwa
mwanangu,amemuoa
mwanangu Najma hivyo Abu
Zalawi ni sehemu ya familia
yangu” akasema Habiba
“Habiba kama
nilivyokueleza kuwa tayari
misheni imeingia dosari.Baada
ya kugundua kuwa Abu Zalawi
si Yule uliyetuaminisha kuwa
ni gaidi bali ni jasusi tena
anatokea Tanzania,kuna
maamuzi yamefanyika”
akasema Mark Piller na
kunyamaza kidogo
“Mmefanya maamuzi gani
Mark?akauliza Habiba
“Tumekubaliana kumuua
Abu Zalawi na misheni
itakuwa imeishiahapo”
akasema Mark na ukimya
ukapita
“Mark Piller hilo ni kosa
kubwa sana ambalo mtalijutia
kwani hamtapata tena nafasi
nyingine ya kumuingiza mtu
wa kuwafanyia ujasusi nchini
Iran.Hii ni nafasi pekee
mmeipata na mkishindwa
kuitumia vyema ni juu yenu”
akasema Habiba
“Habiba misheni tayari
imevurugika na aliyeivuruga
misheni hii ni wewe kwa
kutuletea mtu ambaye hakuwa
sahihi kwa misheni
hii.Tulikuamini sana Habiba
na ndiyo maana hatukuwa na
wasi wasi wowote na Abu
Zalawi lakini baada ya
kumfahamu vyema Abu Zalawi
umevunja uaminifu na
maamuzi yaliyopitishwa ni
wewe kuuawa pia” akasema
Mark Piller na ukimya
ukawala.
“Mark ! akaita Habiba
Jawad
“Unasemaje Habiba?
“Mnakwenda kufanya kosa
kubwa sana kwa hiyo mipango
yenu mliyoipanga” akasema
Habiba
“Ninafahamu Habiba”
“Kwa nini ukanipigia
kunijulisha kuhusu mipango
yenu?akauliza Habiba
“Nimekupigia kwa sababu
baada ya kutafakari kwa kina
nimegundua kwamba
tutafanya kosa
kubwa.Tunaihitaji mno
misheni hii ifanikiwe hivyo
nimekupigia kuomba msaada
wako” akasema Mark na
ukimya ukatawala tena.Habiba
Jawad akavuta pumzi na
kusema
“Nini unahitaji tena
kutoka kwangu Mark wakati
tayari mmekwisha panga
mipango ya kuniua? Akauliza
Habiba
“Nimeamua kuwasaliti
wenzangu na kukueleza ukweli
kuhusu mipango yetu,kwanza
ili uchukue tahadhari na
kujificha na pili ni kutafuta
namna ya kumfikishia Abu
Zalawi taarifa za kumtaka
achukue tahadhari kwani kuna
watu wanaotaka
kumuua.Nataka Abu aendelee
na misheni hii hadi
atakapoikamilisha” akasema
Mark Piller
“Mark nimekuwa mtumwa
wenu kwa miaka
mingi,nimewafanyia kazi
nyingi kwa manufaa ya nchi
yenu lakini hata baada ya
kuwafanyia hayo yote
ninachoambulia ni kutaka
kuuawa.Mmenisikitisha sana
Mark”
“Habiba ndiyo maana
nimekupa siri hii ili uweze
kuchukua tahadhari na
ikiwezekana uondoke Saudi
Arabia ukajifiche mahala”
akasema Mark
“Siwezi kukimbia
Mark.Siwezi kukimbia.Kama
mnataka kuniua njooni
mtanikuta hapa ninawasubiri
lakini fahamuni ya kwamba
damu yangu haitawaacha
salama ! akasema Habiba
Jawad
“Habiba tafadhali naomba
tusilifanye jambo hili liwe
gumu.Wewe mwenyewe
unafahamu namna misheni hii
ilivyo muhimu.Wengine wote
hawalioni hilo lakini mimi
ninafahamu umuhimu
wake.Habiba tafadhali
nakuhitaji sana.Naomba
tushirikiane kuhakikisha
misheni hii inaendelea na
inafanikiwa.Naomba tafuta
namna ya kumlinda Abu
Zalawi dhidi ya wale wote
watakaotumwa kumuua na
aendelee na kazi aliyotumwa
kuifanya.Habiba nakuahidi
nitakulinda dhidi ya mipango
yoyote mibaya inayopangwa
juu yako” akasema Mark Piller
“Mark….. !
“Habiba tafadhali ! Sisi
nawe tumetoka mbali sana na
umetusaidia mambo mengi
naomba mashirikiano yetu
yaendelee kama kawaida na
ninakuahidi kukulinda hata
kama ni kwenda kinyume na
wenzangu wote niko tayari
kufanya hivyo.Tafadhali
Habiba” akasema Mark
“Mark nimekuelewa lakini
nataka kufahamu jambo
moja.Nataka kufahamu namna
mlivyopanga mipango ya
kutuua mimi na Abu Zalawi”
akasema Habiba na Mark
akamueleza mipango yote
namna ilivyopangwa ya
kuwaua yeye na Mathew
“Mark Piller unadhani nini
kitakutokea pale wenzako
watakapobaini kuwa
umewasaliti?akauliza Habiba
“Ninafahamu nitakuwa
matatizoni lakini niko tayari
kukabiliana na chochote
kitakachonitokea.Misheni hii
ni muhimu mno kwa nchi
yangu na kwa namna yoyote ile
lazima ifanikiwe” akasema
Mark Piller
“Sawa Mark
nimekuelewa.Nitashirikiana
nawe kuhakikisha misheni hii
inafanikiwa.Nitajitahidi
kuhakikisha Abu Zalawi
anapata taarifa mapema kabla
ya watu wa Mossad
hawajamfikia.Ninachotaka
ukifanye ni kuendelea kunipa
taarifa za mipango yenu yote
mnayoipanga ili na mimi
nitafute namna ya kumsaidia
Abu Zalawi” akasema Habiba
“Nitakujulisha kila kitu
Habiba Jawad lakini
nakuomba nawe uchukue
tahadhari kuanzia sasa.Pale
utakapoitwa uje Marekani toa
kisingizio kwamba hautaweza
kwa sasa kuna mambo ya
msingi unayashughulikia na
mimi nitaongeza
nguvu.Ongeza ulinzi na mtu
yeyote asiyefahamika
asikaribishwe katika makazi
yako” akasemaMark Piller
“Nakushukuru Mark.Mimi
nitahakikisha Abu Zalawi
anakuwa salama na
anaendelea na mipango yake
yote kama alivyotumwa nchini
Iran” akasema Habiba
wakaendelea na mazungumzo
kidogo wakapeana mikakati
namna watakavyokuwa
wakiwasiliana kwa siri kisha
wakaagana.
“Nilijua tu lazima
watagundua kuhusu Mathew
lakini sikutegemea iwe
mapema namna
hii.Nilifahamu
watakapogundua kuhusu
Mathew mzigo wote wa
lawama nitaubeba mimi na
nilikwisha jiandaa kwa jambo
hilo.Kwa sasa baada ya
kuifahamu mipango yao
natakiwa kuhakikisha Mathew
anakuwa salama ili aweze
kuikamilisha misheni yake”
akawaza Habiba Jawad na
kuchukua simu nyingine
akazitafuta namba Fulani na
kupiga kisha simu ikapokelewa
“Habiba” akasema mtu
aliyepokea simu upande wa
pili
“Vahid
unaendeleaje?akauliza Habiba
Jawad
“Siwezi kusema naendelea
vizuri Habiba.Bado kifo cha
mwanangu Najma
kinaniumiza mno.Ninajuta
kwa nini nilimruhusu aje
Riyadh.Kama ningeendelea
kukaa naye hapa Tehran
yasingemkuta haya
yaliyomkuta.Kwa ujumla bado
siko sawa na itanichukua
muda mrefu kulizoea jambo
hili” akasema Vahid Ghorbani
baba mzazi wa Najma.Vahid
na Habiba waliwahi kuwa na
mahusiano na wakamzaa
Najma lakini hawakufunga
ndoa na kila mmoja
akaendelea na maisha yake.
“Vahid suala hili
linatuumiza sote.Huwezi kujua
niko katika hali gani kwa sasa
baada ya kuwapoteza wanangu
wawili ndani ya kipindi
kifupi.Ni wakati mgumu sana
huu kwetu sote hivyo
tusaidiane kufarijiana badala
ya kulaumiana” akasema
Habiba
“Sikulaumu Habiba
nafahamu ulivyompenda
Najma.Tuachane na hayo vipi
maendeleo yako?
“Kama nilivyokwambia
Vahdi kwamba siko
sawa.Nimewapoteza watoto
wawili ndani ya kipindi kifupi
ni suala zito kulibeba lakini
ninajitahidi.Hata hivyo
sijakupigia simu kwa suala
hilo.Vahdi kuna jambo nataka
unisaidie”
“Sema chochote
Habiba.Unataka nikusaidie
nini?akauliza Vahid
“Kuna wanasayansi sita wa
Iran waliokuwa wamepotea
lakini leo hii wamerejea
nyumbani”akasema Habiba
“Nimepata taarifa hizo
kwamba wale watu wetu
waliokuwa wamepotea
wamerejea nyumbani leo hii
lakini haijatolewa taarifa rasmi
kwamba walikuwa wapi muda
huu wote” akasema Vahid
“Aliyewakomboa watu hao
na kuwarejesha nyumbani
anaitwa Abu Zalawi”
“Abu Zalawi?! Vahdi
akauliza
“Ndiyo.Anaitwa Abu
Zalawi”
“Ni mtu wa wapi huyo Abu
Zalawi?
“Ni Raia wa Saudi Arabia”
“Hatujafahamishwa jambo
hilo.Nini unataka nikusaidie
Habiba? Akauliza Vahid
“Ninataka ufanye kila lililo
ndani ya uwezo wako uweze
kuonana na huyu Abu Zalawi”
“Nionane na Abu Zalawi?
Vahid akauliza
“Ndiyo.Kuna ujumbe wa
muhimu sana ambao nataka
umfikishie”akasema Habiba
“Habiba sifahamu alipo
huyo Abu Zalawi na wala sijui
ni jinsi gani nitaweza
kumpata” akasema Vahid
“Vahid unatakiwa ufanye
kila linalowezekana
kuhakikisha unampata Abu
Zalawi”
“Habiba sidhani kama
mimi ni mtu sahihi wa
kukusaidia kwenye jambo hilo”
akasema Vahid
“Vahid ni muhimu sana
ukaonana na Abu Zalawi.Huyo
ndiye mume wa Najma”
“Mume wa Najma?! Vahidi
akastuka
“Ndiyo ni mume wa
Najma”
“Najma alikuwa na
mume?Kwa nini hujawahi
kuniambia jambo hili?
“Najma mwenyewe ndiye
aliyetaka iwe siri na
tusikujulishe.Kama
unavyofahamu kuwa Najma
hakuwahi kuwa na mpenzi
lakini alipokutana na Abu
Zalawi akajikuta akimpenda na
kufunga naye ndoa ya kimya
kimya na alitoa maelekezo ya
kutokufahamisha jambo
hili.Alitaka yeye mwenyewe
akujulishe pale atakapokuwa
tayari lakini kwa bahati mbaya
hakuwahi kufanya hivyo mauti
yakamkuta” akasema Habiba
“Habiba ulikosea sana
kukubali kunificha kuhusu
Najma kuolewa wakati mimi
ndiye baba yake
mzazi.Hukunitendea haki
katika hili”akasema Vahid
“Nakubali Vahid kwamba
nilikosea lakini nilifanya hivyo
kuheshimu matakwa ya
mtoto.Alitaka akueleze jambo
hili yeye mwenyewe muda
utakapofika.Tusameheane
katika hilo”
“Nilipokuja msibani kwa
nini huku nijlisha kuwa Najma
alikuwa na mume hadi leo hii?
“Nilikuwa
nimechanganyikiwa Vahid
ndiyo maana sikukueleza
chochote.Tafadhali naomba
sana unisamehe kwa hilo”
akajibu Habiba.Baada ya muda
Vahid akauliza
“Unataka kumfikishia
ujumbe gani huyo Abu
Zalawi?akauliza Vahid
“Nataka uonane naye ana
kwa ana na umpe simu
nizungumze naye”
“Habiba umenipa mtihani
mgumu sana.Kwanza ni nani
huyo Abu Zalawi?Kwa nini
yuko hapa? Akauliza Vahid
“Vahid naomba unisaidie
hilo ninalokuomba ni muhimu
sana”
“Habiba niko tayari
kukusaidia lakini lazima
nifahamu huyu mtu ni nani na
kwa nini yuko hapa Iran?
“Abu Zalawi anataka
kuuawa na Mossad hivyo
nataka niongee naye nimpe
angalizo awe makini” akasema
Habiba
“Anataka kuuawa na
Mossad?akauliza Vahid
“Ndiyo.Kuna majasusi
wanatumwa kuja Tehran kwa
lengo la kumuua.Anatakiwa
aipate haraka sana taarifa
hiyo”akasema Habiba
“Kwani huyu Abu Zalawi
ni nani hadi Mossad watake
kumuua? Akauliza Vahid
“Vahid nitakueleza kila
kitu hapo baadae kuhusiana na
Abu Zalawi lakini kwanza
naomba unisaidie kufanya kila
uwezalo uonane naye na
umpatie simu nizungumze
naye.Unaweza ukanisadia kwa
hilo? Akauliza Habiba
“Sawa Habiba.Nitajitahidi
kumtafuta huyo Abu Zalawi”
“Jitahidi Vahid wewe ni
mfanya biashara mkubwa
nchini Iran unafahamiana na
watu wengi hata viongozi wa
serikali naamini haitakuwa
kazi ngumu kwako kufahamu
mahala alipo Abu Zalawi”
akasema Habiba Jawad na
kuagana na Vahid.
******************
Baada ya kutoka
kuzungumza na makamu wa
Rais,Jason na David walirejea
katika ofisi ya Jason ambaye
bila kupoteza muda akampigia
simu Moshe Levine
mkurugenzi wa Mossad
“Jason Washington”
akasema Moshe baada ya
kupokea simu
“Habari za muda huu
Moshe.Nimekupigia kufuatia
mazungumzo yetu ya awali”
akasema Jason
“Ndiyo Jason.Umefikia
wapi kuhusiana na yale
tuliyoyazungumza?akauliza
Moshe Levine
“Kama nilivyokueleza
asubuhi kwamba tunataka
kumuua Abu Zalawi.Bado
mpango huo unaendelea na
kama nilivyokudokeza
tunataka kuwatumia watu
wako wa Mossad walioko
nchini Iran” akasema Jason
“Jason nina watu wangu
Tehran ambao wanaweza
wakaifanya hiyo kazi muda
wowote watakapopewa
maelekezo lakini nilitoa
masharti asubuhi ya kama
mkitaka tuwasaidie kumuua
Abu Zalawi basi na nyinyi
mtupe taarifa za mahala alipo
Habiba Jawad.Mmefikia wapi
katika suala hilo?akauliza
Moshe Levine
“Tumejadiliana na
tumekubaliana jambo
moja.Habiba Jawad tutamuua
sisi wenyewe pale ambapo
nanyi mtakuwa mmemuua
Abu Zalawi”
“Jason hatukukubaliana
hivyo.Ninataka mtupe taarifa
za mahala alipo Habiba Jawad
na tutamkamata sisi
wenyewe.Hatutaki kumuua
kuna mambo mengi tunahitaji
kuyafahamu kuhusiana na
mtandao wake kabla ya
kumuua hivyo tupeni taarifa za
mahala alipo sisi tutamkamata
hatuhitaji msaada wa kumuua”
akasema Moshe Levine
“Moshe sisi tuko tayari
kutoa aina yoyote ya
ushirikiano kwenu.Kama
hamtaki kumuua Habiba
hatuna tatizo na hilo.Sisi
tutamkamata Habiba na
tutamkabidhi kwenu lakini
lazima kwanza tuhakikishe
Abu Zalawi ameuawa ndipo
tutawakabidhi Habiba
Jawad.Tunakubaliana katika
hilo?akauliza Jason
“Jason tunamtaka Habiba
Jawad kwanza ndipo
tuwafanyie kazi yenu ! Kuna
ugumu gani wa kutupa taarifa
za mahala alipo Habiba ?
akauliza Moshe Levine
“Moshe sisi na ninyi ni
washirika wakubwa tena wa
miaka mingi tunapaswa
kuaminiana.Tuna sababu za
msingi kwa nini hatuwezi
kuwapa taarifa za mahala alipo
Habiba Jawad.Naomba
uniamini Moshe kwamba
tutamkabidhi kwenu Habiba
Jawad pale tutakapokuwa na
uhakika kwamba Abu Zalawi
ameuawa.Hivi tuzungumzavyo
tayari timu inaandaliwa kwa
ajili ya kwenda kumkamata
Habiba Jawad.Tutamuhifadhi
hadi pale ambapo mtakuwa
mmekamilisha zoezi la
kumuua Abu Zalawi”
“Jason kutakuwa na
ugumu katika jambo
hilo.Tupeni Habiba Jawad na
sisi tumuue Abu Zalawi”
“Moshe nakuhakikishia
kwamba hata dakika hii
mkimtaka Habiba Jawad
mtampata lakini hatuwezi
kumkabidhi Habiba kwenu
wakati bado hamjatekeleza
kazi yetu.Muondoeni Abu
Zalawi kwanza ili mumpate
Habiba
“Tufanye
hivi.Tudhihirishieni kwanza
kama kweli mnaye Habiba
Jawad na tutaelekeza apelekwe
katika ubalozi wenu Jerusalem
na baada ya kumuua Abu
Zalawi mtamkabidhi
kwetu.Tunakubaliana katika
hilo”
“Hakuna tatizo katika
hilo.Tutafanya hivyo”
“Vizuri.Nashukuru kama
tumekubaliana hivyo Jason
basi na sisi tunaanza mara
moja mpango wa kumuua Abu
Zalawi.Tutaendelea
kufahamishana kila hatua
tunayopiga” akasema Moshe
Levine wakaagana
“Mambo yanazidi kuwa
magumu David” Jason
akamwambia David na
kumuelezea kila kitu
walichozungmza na Moshe
Levine
“Nini maamuzi yako katika
jambo hili? akauliza David
Walker
“Hatuna ujanja lazima
tumkamate Habiba Jawad na
kumuandaa kwa ajili ya
kuwakabidhi Mossad pale
watakapokuwa wamemuua
Abu Zalawi”
“Jason huo ni mpango wa
hatari sana.Ni vipi kama
wakimchunguza na kugundua
kuwa tumekuwa
tunashirikiana naye?akauliza
David
“Tutamuweka Habiba
Jawad katika ubalozi wetu
jijini Jerusalem na baada ya
wao kumuua Abu Zalawi sisi
pia tutamuua Habiba Jawad
na kuwakabidhi maiti
yake.Hatuwezi kuwakabidhi
Habiba akiwa mzima”
akasema Jason wakaendelea
kujadiliana kuhusiana na
mpango ule halafu Jason
akainua simu na kumjulisha
Mark Piller kuhusu
mazungumzo yake na Moshe
Levine pamoja na mpango
waliouandaa.
Mark Piller baada ya
kumaliza maongezi na Jason
akampigia simu Habiba Jawad
“Mark karibu tena”
akasema Habiba
“Habiba nimerejea tena
kama nilivyokueleza awali
kwamba nitakuwa ninakupa
taarifa mipango yote
inayopangwa dhidi yako”
akasema Mark na kumueleza
Habiba kuhusiana na mpango
ule wa kutuma kikosi kwenda
kumteka na kumpeleka katika
ubalozi wa Marekani jijini
Jerusalem tayari kwa
kukabidhiwa kwa Mossad pale
watakapokuwa wamefanikisha
mpango wa kumuua Abu
Zalawi.
“Ahsante sana Mark Piller
kwa angalizo hilo.Tayari
nimekwisha anza taratibu za
kumtafuta Abu Zalawi na
kujua mahala alipo ili niweze
kumuonya kuhusiana na
mpango wa
kumuua.Nategemea kabla ya
watu hao wa CIA waliotumwa
kuja kunikamata hawajafika
hapa tayari nitakuwa
nimekwisha mpata Abu
Zalawi” akasema Habiba
DAR ES SALAAM –
TANZANIA
Kiza tayari kilikwishatanda
katika jiji la Dar es
salaam,Nawal alitoka
chumbani kwake na kwenda
kukaa sehemu ya kupumzikia
iliyo mbele ya nyumba ile
wanakoishi viongozi wa vikosi
vya jeshi la Marekani vilivyopo
Dar es salaam.Taa zilikuwa
zinawaka katika nyumba hii
kwani walikuwa wanatumia
jenereta .Ulinzi pia ulikuwa
mkali karibu kila pembe ya
nyumba hii kulikuwa na
walinzi.Akiwa amejipumzisha
mbele ya nyumba muhudumu
akamfuata na kumuuliza kama
angependa kutumia kinywaji
chochote na Nawal
akamuagiza amtengenezee
kahawa
“Nilipowasiliana na Ruby
saa kumi na mbili jioni,bado
Jenerali William hakuwa
amerejea ofisini kwake na hadi
giza limeingia hatujui mahala
alipo Sattar.Kwa namna yoyote
ile lazima usiku wa leo tujue
mahala kilipo
kirusi.Nitamvamia Jenerali
William usiku wa leo
chumbani kwake na lazima
ataeleza alipo Sattar na
kirusi.Kitu kikubwa
ninachohitaji kufahamu ni
watu wangapi wanaoishi ndani
ya nyumba hii ili nijue namna
ninavyoweza kukabiliana nao
na kama nikiona sintaweza
basi nitaomba msaada kutoka
SNSA.Nitakaa hapa hapa hadi
jenerali William atakaporejea”
akawaza Nawal na kutolewa
mawazoni baada ya kahawa
yake kuletwa.
“Ahsante sana.Jina lako
nani nimelisahau” akauliza
Nawal
“Naitwa Brenda”
“Ouh Brenda .Naitwa
Chloe” akasema Nawal na
kumtaka Yule muhudumu
kukaa kwa ajili ya
mazungumzo lakini Brenda
akamjulisha kwamba
watazungumza pale
atakapokuwa amekamilisha
majukumu yake
“Huyu Brenda anaweza
akanipa taarifa za kutosha
kuhusu mahala hapa.Ngoja
nimsubiri amalize majukumu
yake” akawaza Nawal
akiendelea kunywa kahawa
yake taratibu
Akiwa ameyaelekeza
macho yake katika geti mara
akawaona wanajeshi
waliokuwa wakilinda geti
wakiwa katika heka heka
akakaza macho zaidi ili kujua
kinachoendelea.Geti
likafunguliwa na gari nne
zikaingia mle ndani.Tatu
zikiwa ni gari za doria za jeshi
la Marekani na moja ikiwa ni
aina ya Prado.Kutoka katika
mojawapo ya gari akashuka
Jenerali William na na
makamanda wengine wawili
na kutoka katika ile Prado
wakashuka watu wanne ambao
hawakuwa wanajeshi.Nawal
alihisi mapigo ya moyo wake
yakibadilika na kwenda haraka
haraka baada ya kuziona sura
za wale jamaa walioshuka
katika Prado
“Sattar ! Assad ! akasema
kwa sauti ndogo ya mshangao
Jenerali William akiwa
ameongozana na wale jamaa
wengine wanne na wanajeshi
wawili wakaanza kupiga hatua
kuelekea ndani ya ile nyumba.
“Chloe ! akasema Jenerali
William baada ya kumkuta
Nawal amekaa nje
“Jenerali William”
akasema Nawal na kusimama
“Habari za toka
mchana?Umeshinda salama?
Akauliza Jenerali William
“Niko salama kabisa
Jenerali William.Nimepata
huduma nzuri”
“Nafurahi kusikia hivyo
Chloe.Hawa ni wenzangu Meja
Greg na Meja Thomas”
akasema Jenerali William na
kufanya utambulisho.
“Huyu ni mmarekani
mwenzetu ambaye alikuwa
hapa Tanzania katika shughuli
zake za upigaji picha lakini
alijikuta amenasa katika
machafuko na jana
amekombolewa na vikosi vya
jeshi la Tanzania akaletwa Dar
es salaam na leo mchana Rais
akanikabidhi.Chloe ataishi na
sisi hapa hadi pale hali ya
amani itakapokuwa nzuri”
akasema Jenerali William na
kumtaka Nawal waingie
ndani.Miguu ya Nawal ilikuwa
inagongana kwa kile
alichokuwa
amekishuhudia.Katika wale
watu walioongozana na
Jenerali William
aliwashuhudia kwa macho
watu wawili waliokuwa
wanawatafuta kwa jasho na
damu.Assad Ismail na Sattar
Sayf Al Din
“Siamini ninachokiona
huu ni kama muujiza
mkubwa.Watu wote hawa
wawili Assad na Satter wote
tunawatafuta kwa kila
namna.Hadi mwili wangu
unatetemeka sikuwa
nimelitegemea kabisa jambo
hili.Lakini mbona hawana yale
masanduku ya
kirusi?Wamekipeleka wapi?
Au tayari wamekwisha anza
kukisambaza?akajiuliza Nawal
“Usiku wa leo lazima kila
kirusi kipatikane.Wamejileta
wenyewe kwenye mdomo wa
Mamba na hawatatoka
salama” akawaza Nawal
Jenerali William
akamuelezea Brenda
kumpeleka Nawal katika
chumba maalum cha
mapumziko wakati yeye
akiendelea na mazungumzo na
wageni wake.Nawal hakwenda
katika chumba cha mapumziko
bali alielekea moja kwa moja
chumbani kwake na kitu cha
kwanza alichokifanya ni
kuishika simu akampigia Ruby
“Hallo Ruby ! akasema
Nawal
“Nawal kuna nini?Mbona
unahema haraka haraka
namna hiyo?Kuna tatizo?
akauliza Ruby
“Ruby wako hapa !
akasema Nawal
“Akina nani
Nawal?akauliza Ruby
“Assad na Sattar wote
wako hapa.Wamekuja na
Jenerali William” akasema
Nawal
“Nawal una uhakika ni
wenyewe?
“Nimewashuhudia mimi
mwenyewe kwa macho
yangu.Wamefika muda si
mrefu wakiwa wameongozana
na Jenerali William”
“Yale masanduku mawili
aliyoshuka nayo Sattar
ndegeni ambayo tunaamini
yana kirusi yameletwa
hapo?akauliza Ruby
“Hapana Ruby kirusi
hakipo hapa.Yawezekana kuna
mahala kimehifadhiwa au
yawezekana tayari kimekwisha
pelekwa kusambazwa”
akasema Nawal
“Hapana bado
hakijasambazwa kwani mtu
pekee aliyeletwa kuja
kusambaza kirusi hicho ni
Sattar Sayf Al Din.Kama
hayuko nacho hapo basi lazima
kirusi hicho kimehifadhiwa
sehemu Fulani wakisubiri
muda ufike
wakisambaze.Nawal usiku huu
wa leo lazima tuhakikishe
tunakipata kirusi hicho.Ni kufa
na kupona leo lazima nyumba
hiyo ivamiwe tuwachuku watu
hao wote waliomo katika hiyo
nyumba na watatuonyesha
mahala kilipo kirusi.Nawal
endelea kufuatilia watu hao
kama wataondoka au watalala
hapo wakati tunaandaa kikosi
kwa ajili ya kuvamia nyumba
hiyo.Kuanzia mchana wa leo
tumekuwa tukiichunguza
nyumba hiyo na kuona namna
walivyojipanga
kiulinzi.Makomando wetu
wako tayari na muda
utakapowadia watavamia
nyumba hiyo.Nawal
tunakutegemea sana uweze
kuwasaidia timu ya
makomando watakapofika
hapo” akasema Ruby
“Tayari nimekwisha
yasoma mazingira ya hapa na
ulinzi ulivyo hivyo hakuna
tatizo nitasaidiana na timu
itakayofika hapa” akasema
Nawal na kumpa Ruby
maelekezo kadhaa
Mara tu alipomaliza
kuzunguma na Nawal Ruby
akampigia Gosu Gosu
akamtaka afike ofisini kwake
mara moja akamueleza
kuhusiana na kile alichoelezwa
na Nawal
“Ruby mpaka hapo
naamini tayari tumekwisha
kipata kirusi.Usiku huu lazima
tuwapate hawa magaidi wote
pamoja na
kirusi.Nitaongozana na
makomando wetu
watakaokwenda kuvamia
nyumba hiyo” akasema Gosu
Gosu
“Hapana Gosu
Gosu.Tuwaache makomando
waende.Wewe utakuwa na kazi
ya kuwahoji akina Assad
kufahamu mahala kilipo kirusi
pale watakapokuwa
wameletwa hapa” akasema
Ruby
“Ruby kwa nini hutaki
nishiriki katika misheni siku
hizi? Kila ninapotaka kushiriki
katika misheni unanizuia.You
don’t trust me?akauliza Gosu
Gosu
“Si hivyo Gosu Gosu.Sitaki
kuyaweka hatarini maisha
yako wakati tayari tunacho
kikosi kinachoweza
kupambana .Kumbuka huko
wanakoenda kunalindwa na
wanajeshi wa Marekani ambao
wana mafunzo ya hali ya juu
hivyo itakuwa ni nusu
vita.Naamini kikosi chetu cha
makomando kina uwezo
mkubwa sana wa kuweza
kufanikisha misheni hii.Kama
nilivyokuahidi kwamba wewe
utafanya kazi ya kuwahoji
akina assad watakapoletwa
hapa” akasema Ruby
“Ruby imekuaje ukabadili
mawazo leo na unataka
niwahoji magaidi?akauliza
Gosu Gosu
“Kwa namna yoyote ile
tunahitaji kukipata kirusi
hivyo basi kila aina ya mbinu
lazima itumike wakati wa
kuwahoji magaidi hao ili
waweze kufunguka kirusi kiko
wapi”
“Sawa Ruby nitaifanya
kazi hiyo” akasema Gosu Gosu
kisha wakatoka kwenda
kuanza maandalizi kwa ajili ya
misheni ile
