Riwaya: Siri

SIRI
Episode 3
Mtunzi. Patrick CK

Msafara wa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania uliwasili
katika makazi ya bilionea Agrey
Themba.Rais Dr Evans na Agrey ni
marafiki wa muda mrefu na wamekuwa na mazoea ya
kutembeleana kujuliana hali mara
kwa mara.Agrey na mkewe Lucy
Themba wakajulishwa kuhusu
kuwasili kwa rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr Evans
ambaye alifika bila kutoa taarifa,
wakatoka kwenda kumpokea.Rais
alishuka garini na kupokewa na
Agrey na mkewe wakamkaribisha
ndani.Wageni waliokuwa wamefika
kuwapa pole akina Agrey na
mkewe wakalazimika kutoka
kumpisha rais
“Karibu sana Evans” akasema
Agrey
“Agrey tayari tulikwisha
zungumza simuni lakini nimeona itakuwa vyema kama nikija
mwenyewe kuwapeni pole kwa hili
lililotokea.Ni jambo la kustusha
sana” akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
tunashukuru sana kwa kuja
kututembelea na kutupa
pole.Tumefarijika mno kwa ujio
wako” akasema Agrey
“Agrey nimeguswa sana na hili
lililotokea.Dr Olivia ni sawa na
mwanangu hivyo ninakuahidi
kwamba nitafanya kila lililo ndani
ya uwezo wangu kuhakikisha
kwamba anapatikana akiwa
mzima.Nimekwisha toa maelekezo
kwa jeshi la polisi kuhakikisha
wanatumia kila uwezo walionao kumsaka Dr Olivia.Ngoja nimuulize
IGP wamefikia wapi hadi sasa
katika msako” akasema Dr Evans
akachukua simu na kumpigia mkuu
wa jeshi la polisi
“Mheshimiwa rais” akasema
mkuu wa jeshi la polisi baada ya
kupokea simu ya Dr Evans
“IGP naomba unieleze
mmefikia wapi katika msako wa Dr
Olivia? Akauliza rais
“Mheshimiwa rais toka
lilipotokea tukio lile jeshi la polisi
liko kazini na tunafanya juhudi
kubwa kuhakikisha kwamba
tunajua mahala aliko Dr Olivia na
kuwakamata watekaji
wote.Mwelekeo si mbaya mheshimiwa rais na kuna hatua
tayari zimekwisha pigwa mpaka
sasa.Tayari tumeipata helkopta
ambayo ilitumika katika tukio lile
ikiwa imetelekezwa nje kidogo ya
mji.Helkopta hiyo inamilikiwa na
kampuni moja ya kukodisha ndege
ndogo na helkopta.Wamiliki wake
wamekiri kwamba helkopta hiyo ni
yao na kwamba asubuhi ya leo
rubani wake aliondoka nayo katika
mazoezi ya kawaida na hakurejea
hadi pale walipopata taarifa
kwamba helkopta yao imetumika
katika tukio la kumteka Dr
Olivia.Polisi wamemfuatilia rubani
wa helkopta huyo nyumbani kwake
na kumkuta yeye,mkewe na watoto wake wawili wote
wameuawa.Tukio hilo la kuuawa
kwa rubani huyo limeturudisha
nyuma sana hata hivyo bado
tunaendelea na uchunguzi kwani
picha za kamera zilizofungwa pale
nyumbani kwa Dr Olivia
zinaonyesha gari mbili zilizofika na
kumchukua Olivia.Watu
walioshuka katika magari yale
walikuwa wamefunika nyuso zao
wasitambulike.Kingine kinachotupa
ugumu zaidi ni kwamba gari zile
zote mbili zilikuwa na namba
zinazofanana.Watekaji hawa
waliamua kuweka namba bandia
zinazofanana katika magari hayo ili
kutuchanganya.Pamoja na hayo yote mheshimiwa rais napenda
kukuhakikishia kwamba jeshi la
polisi tutatumia kila uwezo tulio
nao kuhakikisha Dr Olivia
anapatikana kabla ya giza kuingia”
akasema mkuu wa jeshi la polisi
“Ninashukuru sana IGP kwa
taarifa hiyo yenye kutia
moyo.Ninakuomba uongeze nguvu
zaidi na hakikisha unafanya kila
uwezalo Dr Olivia apatikane”
“Tutafanya kila tuwezalo
mheshimiwa rais na
ninakuhakikishia Dr Olivia
atapatikana”
“Ahsante sana.Kila la heri”
akasema Dr Evans na kukata
simu.Mazungumzo yake na mkuu wa jeshi la polisi yalisikiwa na
Agrey na mkewe kwani alikuwa
ameweka katika sauti kubwa ili
wote wasikie
“Nadhani mmesikia namna
jeshi la polisi wanavyofanya kila
wawezalo kuhakikisha kwamba Dr
Olivia anapatikana.Ninarejea tena
kuwahakikishia kwamba Dr Olivia
atapatikana” akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
tunakushukuru sana kwa namna
unavyohangaika na suala
hili.Tumefarijika mno kwa juhudi
za jeshi la polisi.Tunaamini
kwamba mwanetu atapatikana
akiwa salama” akasema Agrey “Ninachowaomba kama kuna
chochote mnadhani kinaweza
kusaidia katika uchunguzi
muwasiliane na jeshi la polisi na
kuwaeleza ili wakifanyie kazi hata
kama ni kidogo kiasi
gani.Yawezekana watekaji hawa
lengo lao ni fedha hivyo
watakapowapigia kudai fedha ili
wamuachie mtoto wenu
wasilianeni kwanza na jeshi la
polisi msiogope vitisho
watakavyowapa kwamba
mkiwasiliana na polisi mwanenu
mtamkosa.Tunataka kumuokoa Dr
Olivia vile vile kuwakamata
watekaji” akasema Dr Evans “Tutafanya hivyo mheshimiwa
rais” akajibu Agrey.
Rais Dr Evans hakuchukua
muda mrefu sana pale kwa akina
agrey akawaaga na kuondoka.
********************
Dr Olivia alizinduka kutoka
usingizini na kujikuta akiwa katika
chumba chenye ubaridi mwingi
.Hali ile ya hewa iliyokuwemo mle
chumbani ilikuwa tofauti kidogo na
hali aliyoizoea chumbani
kwake.Akageuza macho kutazama
kila kona na kugundua kwamba
alikuwa katika sehemu tofauti na
ndipo kumbukumbu za kile kilichotokea zilipomrejea.Akainuka
na kwenda katika mlango ambao
ulikuwa unafunguliwa kwa
kutumia kadi maalum akashindwa
kuufungua na kwenda kujikunyata
kitandani akaanza kulia.Aligundua
kwamba tayari amekwisha tekwa
na hakuwa na uwezo wa kutoka
mle ndani.
“It’s time” akasema Devotha
aliyekuwa na timu yake
wakimfuatilia Dr Olivia katika
luninga.Kaiza akarekebisha tai yake
halafu akashuka kuelekea katika
chumba alimo Dr Olivia.
Akiwa bado amejikunyata
kitandani akilia mlango ukafunguka
akayaelekeza macho yake mlangoni na jamaa mmoja mnene akaingia
mle ndani na kuufunga mlango.
“Habari yako Dr Olivia”
akasema Kaiza kwa sauti ya upole
lakini Dr Olivia hakujibu kitu
“Unajisikiaje Dr Olivia?Kuna
sehemu yoyote unahisi
maumivu?Kichwa,miguu..”
“I’m fine.Tell me why I’m
here”akasema Dr Olivia
“Usiogope Dr Olivia.Uko
salama.Can I get you something to
drink? Akasema Kaiza akienda
katika friji kubwa akalifungua na
kuchukua chupa mbili za maji ya
matunda akampatia moja Dr Olivia. “Sihitaji kinywaji chenu nataka
mniambie kwa nini mnaniweka
hapa?akauliza Dr Olivia
“Relax Dr Olivia we’re not bad
people”akajibu Kaiza na kuvuta kiti
akaketi karibu na Dr Olivia
“Mngekuwa watu wazuri
msingethubutu kunivamia mkaua
walinzi wangu na kuniteka.What do
you want from me?You want
money?Semeni ni kiasi gani
mnakihitaji
niwapatie.Hamkupaswa kuua watu
wangu kwa sababu ya fedha”
akasema Dr Olivia na kufuta
machozi
“Dr Olivia hatuhitaji pesa”
akajibu Kaiza “Kama hamuhitaji fedha nini
mnahitaji toka kwangu?Niambieni
basi mnachokitaka niwapatie ili
mniache niende
zangu.Mmewaweka wazazi na
ndugu zangu katika wakati mgumu
sana hawajui mahala
nilipo.Tafadhali niambieni mnataka
kitu gani na mniahidi nikiwapa
mnachokihitaji mtaniacha niende
zangu”akasema Dr Olivia
“Olivia we need to ask you
some questions.There are few
things we want to know from
you.Ukionyesha ushirikiano kwetu
nakuahidi tutakuacha uende zako”
akasema Kaiza “Ni vitu gani mnataka
kuvifahamu kutoka kwangu?Please
tell me.Nitawapa kila
mnachokitaka” akasema Dr
Olivia.Kaiza akakohoa kidogo
kurekebisha koo na kusema
“Dr Olivia hukuwepo nchini
kwa siku kama tano
zilizopita.Ulikwenda wapi?akauliza
Kaiza.Dr Olivia akamtazama kwa
macho makali
“Mmekuwa mnanifuatilia kila
ninachokifanya hadi mkajua
kwamba siko nchini.Who are you
peple?akauliza Dr Olivia
“Please answer the question
Dr Olivia” akasema Kaiza “Kwa nini
mnanifuatilia?akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia naomba ujibu swali
nililokuuliza ili tuokoe muda”
“Fine.Nilikuwa nimekwenda
nchini Congo DRC”
“Ulikwenda kufanya nini
nchini Congo DRC?akauliza Kaiza
“Mimi ni daktari nilikwenda
nchini Congo katika shughuli zangu
za utafiti”akajibu Dr Olivia
“Kitu gani ulikwenda kukitafiti
nchini Congo?
“Ninafanya utafiti wa
magonjwa mbali mbali ya
binadamu na hata
wanyama.Nilikwenda nchini Congo kufanya utafiti kuhusiana na
ugonjwa wa Sonzae”
Kaiza akavuta pumzi ndefu na
kuuliza
“Dr Olivia katika sanduku lako
tumekuta sampuli nne za
damu.Unaweza ukatueleza umetoa
wapi sampuli zile na kwa
madhumuni gani?
“What’s your name?akauliza
Dr Olivia
“Naitwa Kaiza”
“Mr Kaiza nadhani unafahamu
kazi yangu ninayofanya.Mimi ni
mtafiti na sampuli zile nimezitoa
nchini Congo ni damu kutoka kwa
nyani ambao wanasemekana ndio chanzo cha ugonjwa wa Sonzae”
akajibu Dr Olivia
“Dr Olivia sampuli hii ya damu
ina virusi vya Sonzae? Akauliza
Kaiza kwa mshangao
“Kwa nini ukaingiza hapa
nchini damu yenye virusi hatari vya
Sonzae? Hujui kama hili ni kosa
kubwa umelifanya ambalo linaweza
kukugharimu? akauliza Kaiza.Kwa
mara ya kwanza Dr Olivia akatoa
kicheko kidogo.
“Mr Kaiza.Nataka nifanye
makubaliano nanyi”akasema Dr
Olivia
“Makubaliano? Unataka
kufanya makubaliano gani nasi?
akauliza Kaiza “Chukueni sampuli zile za
damu mlizozikuta katika sanduku
langu,mzipeleke maabara
mkazifanyie uchunguzi na muone
kama zina virusi vya ugonjwa wa
Sinzae.Kama damu hiyo itakuwa na
virusi vya Sonzae nichukulieni
hatua na niko tayari kupata adhabu
kwa kuingiza nchini damu yenye
virusi vya Sonzae lakini kama damu
hiyo itakutwa ni salama haina
virusi vya Sonzae basi mtaniacha
niende zangu.Do we have a deal?
Akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia tutafanya uchunguzi
wetu kuhusu sampuli zile za
damu,mimi na wewe nataka
tuzungumze kuhusu suala lingine la muhimu zaidi” akasema
Kaiza,akatoa picha katika bahasha
na kumuonyesha Dr Olivia
“Unamfahamu huyu mtu
pichani?Umewahi kumuona?
“Ndiyo ninamfahamu.Anaitwa
Alzahwir” akajibu Dr Olivia
“Unafahamiana naye vipi?
“He’s my friend”
“Your friend?Mmefahamiana
lini?
“Nimekutana naye nchini
Congo.Mimi na yeye tulifikia katika
hoteli moja tukakutana na kuwa
marafiki”
“Kabla ya kukutana nchini
Congo hamkuwahi kufahamiana
kabla?akauliza Kaiza “Sikumfahamu Zahwir
kabla.Mara ya kwanza nimekutana
naye Kinshasa”
“Dr Olivia ninakuomba
unieleze ukweli bila kuficha
chochote kwani ni ukweli pekee
ndio utakaokusaidia ukawa huru
lakini kama hautakuwa mkweli
ninasikitika kwamba yawezekana
usitoke humu ndani.Nataka
unieleze ukweli kuhusiana na huyu
mtu unayemfahamu kama Zahwir”
“Nikueleze kitu gani
Kaiza?Nimekwisha kueleza
kwamba mtu huyu nimekutana
naye Kinshasa tukawa marafiki na
sikuwahi kumfahamu hapo kabla”
akasema Dr Olivia.Kaiza akaenda katika luninga akaiwasha na video
ikatokea ikimuonyesha Seif
Almuhsin akiwa amekaa pembeni
ya bwawa la kuogelea na akatokea
Dr Olivia akaketi pembeni yake
akiwa na kompyuta yake wakaanza
kuzungumza.Video ile ilionekana
kumstua Dr Olivia
“You were following me?!
Akauliza Dr Olivia kwa ukali.
“Dr Olivia naomba video hii
ukitazama vizuri utagundua
kwamba wewe na Zahwir
mnafahamiana vyema kabla ya
kukutana hapa.Je unamfahamu
vyema huyu mtu ni nani?akauliza
Kaiza “kwa nini mnanifuatilia?
Akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia nataka unijibu swali
nililokuuliza huyu mtu unayedai ni
rafiki yako unamfahamu
vyema?akauliza Kaiza
“Zahwir ni mfanyabiashara”
akajibu Dr Olivia.
“Sikiliza Dr Olivia nimekuuliza
makusudi ili kujua namna
unavyomfahamu huyu mtu na
inaonekana bado humfahamu
vyema.Mtu huyu haitwi Alzahwir
kama alivyokwambia bali anaitwa
Seif Almuhsin.Huyu ni mtu muhimu
sana katika kikundi cha IS na
amekuwa akifanya kazi ya
kukusanya vijana kutoka ukanda huu wa afrika ya mashariki kati na
kusini ambao hujiunga na kikundi
hiki hatari duniani” akasema Kaiza.
“Sifahamu chochote kama Seif
ni mtu hatari,sifahamu kama
anatoka kikundi cha IS” akasema Dr
Olivia
“Are you sure?
“Yes I’m sure.Nimekutana naye
hotelini Congo na sikuwa
nikimfahamu kabla ya hapo”
“Dr Olivia kitendo cha
kuonekana ukiwa karibu na mtu
huyu kinatufanya tuwe na mashaka
nawe sana.Tunataka kufahamu
mipango ya Seif,tunataka kufahamu
nyendo zake ukitusaidiakutueleza
hilo ninakuahidi kwamba tutakuacha huru.Tunaamini wewe
na yeye ni washirika na lazima
unamfahamu vyema” akasema
Kaiza
“Nimekwisha sema kwamba
simfahamu kabisa huyu
mtu,nimekutana naye kwa mara ya
kwanza Congo,kama ningefahamu
jambo lolote kuhusu huyu mtu
ningekueleza” akasema Dr Olivia
“Dr Olivia fikiria kuhusu
hatima ya maisha yako kwani kama
hautatupa ukweli basi hautaweza
kutoka humu ndani.Yawezekana
ukawa ni mwisho wako.Ninakupa
nafasi nyingine ya kutafakari na
nitakaporejea tena humu ndani
nataka nipate maelezo yote kuhusiana na mipango ya Seif
Almuhsin” akasema Kaiza na
kutoka mle ndani akamuacha Dr
Olivia katika mawazo.
“Kaiza sijafurahishwa na kile
ulichokifanya mle ndani!! Akasema
Devotha kwa ukali wakiwa katika
ofisi yao baada ya Kaiza kutoka
kumuhoji Dr Olivia
“Ulitegemea nifanye nini
Devotha? Akauliza Kaiza
“I sent you in there to find
answers.Nilitegemea ungetumia
ujuzi na uzoefu wako katika
kuhakikisha unapata kile
tunachokihitaji.You were too soft.Is
it because she’s so pretty?akauliza
Devotha “Jamani nyote mmefuatilia kile
nilichozungumza na Dr Olivia na
kile alichokisema.This woman is
very smart.Anatakiwa kuhojiwa
taratibu.Tukienda haraka
tutashindwa kupata kile
tunachokihitaji”akasema Kaiza
“C’mon Kaiza we don’t have
much time.Tunatakiwa haraka sana
kutafuta majibu kutoka kwake.Joto
la kupotea kwake linazidi kupanda
huko nje hivyo tujitahidi kwa
haraka tuwezavyo kuhakikisha
tunapata majibu”akasema Devotha
“kwa kumtazama machoni
anaonekana kuna kitu
anakificha.Kuna jambo
analo.alipoiona video ile akiwa na Seif alistuka sana na hakutegemea
kabisa kama alikuwa
anafuatiliwa.Vijana wamefikia wapi
katika kuichunguza kompyuta
yake?Ukitazama katika ile video
Olivia na Seif walikuwa
wanaelekezana kitu katika ile
kompyuta na kwa kuwa Olivia
hakuwa na habai kama anafuatiliwa
naamini hakufuta vitu katika hiyo
kompyuta yake” akasema kaiza na
Devotha akamchukua wakaenda
katika ofisi ambako kompyuta ya
Dr Olivia ilikuwa inafanyiwa
uchunguzi
“Kuna chochote mmekipata
hadi sasa?akauliza Devotha “Tumepata mawasiliano yake
ya barua pepe lakini baada ya
kuyachunguza tumekuta
anawasiliana na mtu ambaye
anaitwa Sayid Omar ambaye
tunaendelea kufuatilia tujue
mahala alipo” akajibu mmoja wa
wale vijana na kumpatia Devotha
karatasi kadhaa.
“Hayo ndiyo mawasiliano yao
lakini wametumia lugha ya
kiarabu”
“Damn! Tutapataje tafsiri ya
mawasiliano yao?Ni Aziz pekee
ambaye alikuwa anafahamu
kiarabu.Kuna ulazima wa kutafuta
mtu anayejua lugha ya kiarabu au
kumpeleka kijana mmoja akajifunze lugha hiyo.Ni muhimu
sana kwa sasa.Yawezekana katika
mawasiliano haya kuna mambo ya
muhimu sana yanayoweza kutupa
mwanga mkubwa lakini hatuwezi
kufahamu chochote kwa kuwa
hatujui kiarabu” akasema Devotha
“Hii pia ni picha ambayo
tumeikuta katika kompyuta yake”
akasema yule kijana na kumpatia
Devotha picha waliyoikuta katika
kompyuta ya Dr Olivia
“Coletha..Huyu ni mtoto wa
rais” akasema Devotha akionekana
kushangaa
“Rais Dr Evans na Agrey baba
yake Olivia ni marafiki wakubwa na
familia zao ni marafiki pia hivyo Olivia kuwa na picha ya Coletha
haileti wasiwasi kwani naamini
wanafahamiana.Kikubwa hapa ni
kuhakikisha tunamfahamu huyu
Sayid Omar ni nani na yuko
wapi.Ingekuwa rahisi sana kwetu
kama tungeweza kujua
kilichoandikwa katika barua pepe
hizi walizokuwa wanatumiana
lakini hatujui kiarabu hivyo kitu
pekee tulichonacho ni kujua mahala
aliko huyo Sayid” akasema Kaiza
“Damn !! akasema mmoja wa
wale vijana mle ndani
“Kuna nini?akauliza Devotha
“Hawa jamaa ni wataalamu
kwani ukijaribu kufuatilia namba
ya kompyuta anayotumia huyo Omar unakuta kuna zaidi ya
kompyuta mia moja ambazo
zinaonekana ziko sehemu mbali
mbali duniani kwa hiyo ni vigumu
kufahamu ni yupi hasa
anayewasiliana na
Olivia.Wamefanya hivi ili
kumchanganya yeyote ambaye
atahitaji kufuatilia kutaka kujua
mahala aliko Sayid”
“Damn !! akasema Devotha
kwa ukali
“Endeleeni kufuatilia kama
kuna chochote tutakipata,Kaiza
tunakwenda tena kwa
Olivia.Lazima atueleze huyu Sayid
Omar ni nani” akasema Devotha.
nitarudi.
 
SIRI
Episode 3
Mtunzi. Patrick CK

Msafara wa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania uliwasili
katika makazi ya bilionea Agrey
Themba.Rais Dr Evans na Agrey ni
marafiki wa muda mrefu na wamekuwa na mazoea ya
kutembeleana kujuliana hali mara
kwa mara.Agrey na mkewe Lucy
Themba wakajulishwa kuhusu
kuwasili kwa rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania Dr Evans
ambaye alifika bila kutoa taarifa,
wakatoka kwenda kumpokea.Rais
alishuka garini na kupokewa na
Agrey na mkewe wakamkaribisha
ndani.Wageni waliokuwa wamefika
kuwapa pole akina Agrey na
mkewe wakalazimika kutoka
kumpisha rais
“Karibu sana Evans” akasema
Agrey
“Agrey tayari tulikwisha
zungumza simuni lakini nimeona itakuwa vyema kama nikija
mwenyewe kuwapeni pole kwa hili
lililotokea.Ni jambo la kustusha
sana” akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
tunashukuru sana kwa kuja
kututembelea na kutupa
pole.Tumefarijika mno kwa ujio
wako” akasema Agrey
“Agrey nimeguswa sana na hili
lililotokea.Dr Olivia ni sawa na
mwanangu hivyo ninakuahidi
kwamba nitafanya kila lililo ndani
ya uwezo wangu kuhakikisha
kwamba anapatikana akiwa
mzima.Nimekwisha toa maelekezo
kwa jeshi la polisi kuhakikisha
wanatumia kila uwezo walionao kumsaka Dr Olivia.Ngoja nimuulize
IGP wamefikia wapi hadi sasa
katika msako” akasema Dr Evans
akachukua simu na kumpigia mkuu
wa jeshi la polisi
“Mheshimiwa rais” akasema
mkuu wa jeshi la polisi baada ya
kupokea simu ya Dr Evans
“IGP naomba unieleze
mmefikia wapi katika msako wa Dr
Olivia? Akauliza rais
“Mheshimiwa rais toka
lilipotokea tukio lile jeshi la polisi
liko kazini na tunafanya juhudi
kubwa kuhakikisha kwamba
tunajua mahala aliko Dr Olivia na
kuwakamata watekaji
wote.Mwelekeo si mbaya mheshimiwa rais na kuna hatua
tayari zimekwisha pigwa mpaka
sasa.Tayari tumeipata helkopta
ambayo ilitumika katika tukio lile
ikiwa imetelekezwa nje kidogo ya
mji.Helkopta hiyo inamilikiwa na
kampuni moja ya kukodisha ndege
ndogo na helkopta.Wamiliki wake
wamekiri kwamba helkopta hiyo ni
yao na kwamba asubuhi ya leo
rubani wake aliondoka nayo katika
mazoezi ya kawaida na hakurejea
hadi pale walipopata taarifa
kwamba helkopta yao imetumika
katika tukio la kumteka Dr
Olivia.Polisi wamemfuatilia rubani
wa helkopta huyo nyumbani kwake
na kumkuta yeye,mkewe na watoto wake wawili wote
wameuawa.Tukio hilo la kuuawa
kwa rubani huyo limeturudisha
nyuma sana hata hivyo bado
tunaendelea na uchunguzi kwani
picha za kamera zilizofungwa pale
nyumbani kwa Dr Olivia
zinaonyesha gari mbili zilizofika na
kumchukua Olivia.Watu
walioshuka katika magari yale
walikuwa wamefunika nyuso zao
wasitambulike.Kingine kinachotupa
ugumu zaidi ni kwamba gari zile
zote mbili zilikuwa na namba
zinazofanana.Watekaji hawa
waliamua kuweka namba bandia
zinazofanana katika magari hayo ili
kutuchanganya.Pamoja na hayo yote mheshimiwa rais napenda
kukuhakikishia kwamba jeshi la
polisi tutatumia kila uwezo tulio
nao kuhakikisha Dr Olivia
anapatikana kabla ya giza kuingia”
akasema mkuu wa jeshi la polisi
“Ninashukuru sana IGP kwa
taarifa hiyo yenye kutia
moyo.Ninakuomba uongeze nguvu
zaidi na hakikisha unafanya kila
uwezalo Dr Olivia apatikane”
“Tutafanya kila tuwezalo
mheshimiwa rais na
ninakuhakikishia Dr Olivia
atapatikana”
“Ahsante sana.Kila la heri”
akasema Dr Evans na kukata
simu.Mazungumzo yake na mkuu wa jeshi la polisi yalisikiwa na
Agrey na mkewe kwani alikuwa
ameweka katika sauti kubwa ili
wote wasikie
“Nadhani mmesikia namna
jeshi la polisi wanavyofanya kila
wawezalo kuhakikisha kwamba Dr
Olivia anapatikana.Ninarejea tena
kuwahakikishia kwamba Dr Olivia
atapatikana” akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais
tunakushukuru sana kwa namna
unavyohangaika na suala
hili.Tumefarijika mno kwa juhudi
za jeshi la polisi.Tunaamini
kwamba mwanetu atapatikana
akiwa salama” akasema Agrey “Ninachowaomba kama kuna
chochote mnadhani kinaweza
kusaidia katika uchunguzi
muwasiliane na jeshi la polisi na
kuwaeleza ili wakifanyie kazi hata
kama ni kidogo kiasi
gani.Yawezekana watekaji hawa
lengo lao ni fedha hivyo
watakapowapigia kudai fedha ili
wamuachie mtoto wenu
wasilianeni kwanza na jeshi la
polisi msiogope vitisho
watakavyowapa kwamba
mkiwasiliana na polisi mwanenu
mtamkosa.Tunataka kumuokoa Dr
Olivia vile vile kuwakamata
watekaji” akasema Dr Evans “Tutafanya hivyo mheshimiwa
rais” akajibu Agrey.
Rais Dr Evans hakuchukua
muda mrefu sana pale kwa akina
agrey akawaaga na kuondoka.
********************
Dr Olivia alizinduka kutoka
usingizini na kujikuta akiwa katika
chumba chenye ubaridi mwingi
.Hali ile ya hewa iliyokuwemo mle
chumbani ilikuwa tofauti kidogo na
hali aliyoizoea chumbani
kwake.Akageuza macho kutazama
kila kona na kugundua kwamba
alikuwa katika sehemu tofauti na
ndipo kumbukumbu za kile kilichotokea zilipomrejea.Akainuka
na kwenda katika mlango ambao
ulikuwa unafunguliwa kwa
kutumia kadi maalum akashindwa
kuufungua na kwenda kujikunyata
kitandani akaanza kulia.Aligundua
kwamba tayari amekwisha tekwa
na hakuwa na uwezo wa kutoka
mle ndani.
“It’s time” akasema Devotha
aliyekuwa na timu yake
wakimfuatilia Dr Olivia katika
luninga.Kaiza akarekebisha tai yake
halafu akashuka kuelekea katika
chumba alimo Dr Olivia.
Akiwa bado amejikunyata
kitandani akilia mlango ukafunguka
akayaelekeza macho yake mlangoni na jamaa mmoja mnene akaingia
mle ndani na kuufunga mlango.
“Habari yako Dr Olivia”
akasema Kaiza kwa sauti ya upole
lakini Dr Olivia hakujibu kitu
“Unajisikiaje Dr Olivia?Kuna
sehemu yoyote unahisi
maumivu?Kichwa,miguu..”
“I’m fine.Tell me why I’m
here”akasema Dr Olivia
“Usiogope Dr Olivia.Uko
salama.Can I get you something to
drink? Akasema Kaiza akienda
katika friji kubwa akalifungua na
kuchukua chupa mbili za maji ya
matunda akampatia moja Dr Olivia. “Sihitaji kinywaji chenu nataka
mniambie kwa nini mnaniweka
hapa?akauliza Dr Olivia
“Relax Dr Olivia we’re not bad
people”akajibu Kaiza na kuvuta kiti
akaketi karibu na Dr Olivia
“Mngekuwa watu wazuri
msingethubutu kunivamia mkaua
walinzi wangu na kuniteka.What do
you want from me?You want
money?Semeni ni kiasi gani
mnakihitaji
niwapatie.Hamkupaswa kuua watu
wangu kwa sababu ya fedha”
akasema Dr Olivia na kufuta
machozi
“Dr Olivia hatuhitaji pesa”
akajibu Kaiza “Kama hamuhitaji fedha nini
mnahitaji toka kwangu?Niambieni
basi mnachokitaka niwapatie ili
mniache niende
zangu.Mmewaweka wazazi na
ndugu zangu katika wakati mgumu
sana hawajui mahala
nilipo.Tafadhali niambieni mnataka
kitu gani na mniahidi nikiwapa
mnachokihitaji mtaniacha niende
zangu”akasema Dr Olivia
“Olivia we need to ask you
some questions.There are few
things we want to know from
you.Ukionyesha ushirikiano kwetu
nakuahidi tutakuacha uende zako”
akasema Kaiza “Ni vitu gani mnataka
kuvifahamu kutoka kwangu?Please
tell me.Nitawapa kila
mnachokitaka” akasema Dr
Olivia.Kaiza akakohoa kidogo
kurekebisha koo na kusema
“Dr Olivia hukuwepo nchini
kwa siku kama tano
zilizopita.Ulikwenda wapi?akauliza
Kaiza.Dr Olivia akamtazama kwa
macho makali
“Mmekuwa mnanifuatilia kila
ninachokifanya hadi mkajua
kwamba siko nchini.Who are you
peple?akauliza Dr Olivia
“Please answer the question
Dr Olivia” akasema Kaiza “Kwa nini
mnanifuatilia?akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia naomba ujibu swali
nililokuuliza ili tuokoe muda”
“Fine.Nilikuwa nimekwenda
nchini Congo DRC”
“Ulikwenda kufanya nini
nchini Congo DRC?akauliza Kaiza
“Mimi ni daktari nilikwenda
nchini Congo katika shughuli zangu
za utafiti”akajibu Dr Olivia
“Kitu gani ulikwenda kukitafiti
nchini Congo?
“Ninafanya utafiti wa
magonjwa mbali mbali ya
binadamu na hata
wanyama.Nilikwenda nchini Congo kufanya utafiti kuhusiana na
ugonjwa wa Sonzae”
Kaiza akavuta pumzi ndefu na
kuuliza
“Dr Olivia katika sanduku lako
tumekuta sampuli nne za
damu.Unaweza ukatueleza umetoa
wapi sampuli zile na kwa
madhumuni gani?
“What’s your name?akauliza
Dr Olivia
“Naitwa Kaiza”
“Mr Kaiza nadhani unafahamu
kazi yangu ninayofanya.Mimi ni
mtafiti na sampuli zile nimezitoa
nchini Congo ni damu kutoka kwa
nyani ambao wanasemekana ndio chanzo cha ugonjwa wa Sonzae”
akajibu Dr Olivia
“Dr Olivia sampuli hii ya damu
ina virusi vya Sonzae? Akauliza
Kaiza kwa mshangao
“Kwa nini ukaingiza hapa
nchini damu yenye virusi hatari vya
Sonzae? Hujui kama hili ni kosa
kubwa umelifanya ambalo linaweza
kukugharimu? akauliza Kaiza.Kwa
mara ya kwanza Dr Olivia akatoa
kicheko kidogo.
“Mr Kaiza.Nataka nifanye
makubaliano nanyi”akasema Dr
Olivia
“Makubaliano? Unataka
kufanya makubaliano gani nasi?
akauliza Kaiza “Chukueni sampuli zile za
damu mlizozikuta katika sanduku
langu,mzipeleke maabara
mkazifanyie uchunguzi na muone
kama zina virusi vya ugonjwa wa
Sinzae.Kama damu hiyo itakuwa na
virusi vya Sonzae nichukulieni
hatua na niko tayari kupata adhabu
kwa kuingiza nchini damu yenye
virusi vya Sonzae lakini kama damu
hiyo itakutwa ni salama haina
virusi vya Sonzae basi mtaniacha
niende zangu.Do we have a deal?
Akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia tutafanya uchunguzi
wetu kuhusu sampuli zile za
damu,mimi na wewe nataka
tuzungumze kuhusu suala lingine la muhimu zaidi” akasema
Kaiza,akatoa picha katika bahasha
na kumuonyesha Dr Olivia
“Unamfahamu huyu mtu
pichani?Umewahi kumuona?
“Ndiyo ninamfahamu.Anaitwa
Alzahwir” akajibu Dr Olivia
“Unafahamiana naye vipi?
“He’s my friend”
“Your friend?Mmefahamiana
lini?
“Nimekutana naye nchini
Congo.Mimi na yeye tulifikia katika
hoteli moja tukakutana na kuwa
marafiki”
“Kabla ya kukutana nchini
Congo hamkuwahi kufahamiana
kabla?akauliza Kaiza “Sikumfahamu Zahwir
kabla.Mara ya kwanza nimekutana
naye Kinshasa”
“Dr Olivia ninakuomba
unieleze ukweli bila kuficha
chochote kwani ni ukweli pekee
ndio utakaokusaidia ukawa huru
lakini kama hautakuwa mkweli
ninasikitika kwamba yawezekana
usitoke humu ndani.Nataka
unieleze ukweli kuhusiana na huyu
mtu unayemfahamu kama Zahwir”
“Nikueleze kitu gani
Kaiza?Nimekwisha kueleza
kwamba mtu huyu nimekutana
naye Kinshasa tukawa marafiki na
sikuwahi kumfahamu hapo kabla”
akasema Dr Olivia.Kaiza akaenda katika luninga akaiwasha na video
ikatokea ikimuonyesha Seif
Almuhsin akiwa amekaa pembeni
ya bwawa la kuogelea na akatokea
Dr Olivia akaketi pembeni yake
akiwa na kompyuta yake wakaanza
kuzungumza.Video ile ilionekana
kumstua Dr Olivia
“You were following me?!
Akauliza Dr Olivia kwa ukali.
“Dr Olivia naomba video hii
ukitazama vizuri utagundua
kwamba wewe na Zahwir
mnafahamiana vyema kabla ya
kukutana hapa.Je unamfahamu
vyema huyu mtu ni nani?akauliza
Kaiza “kwa nini mnanifuatilia?
Akauliza Dr Olivia
“Dr Olivia nataka unijibu swali
nililokuuliza huyu mtu unayedai ni
rafiki yako unamfahamu
vyema?akauliza Kaiza
“Zahwir ni mfanyabiashara”
akajibu Dr Olivia.
“Sikiliza Dr Olivia nimekuuliza
makusudi ili kujua namna
unavyomfahamu huyu mtu na
inaonekana bado humfahamu
vyema.Mtu huyu haitwi Alzahwir
kama alivyokwambia bali anaitwa
Seif Almuhsin.Huyu ni mtu muhimu
sana katika kikundi cha IS na
amekuwa akifanya kazi ya
kukusanya vijana kutoka ukanda huu wa afrika ya mashariki kati na
kusini ambao hujiunga na kikundi
hiki hatari duniani” akasema Kaiza.
“Sifahamu chochote kama Seif
ni mtu hatari,sifahamu kama
anatoka kikundi cha IS” akasema Dr
Olivia
“Are you sure?
“Yes I’m sure.Nimekutana naye
hotelini Congo na sikuwa
nikimfahamu kabla ya hapo”
“Dr Olivia kitendo cha
kuonekana ukiwa karibu na mtu
huyu kinatufanya tuwe na mashaka
nawe sana.Tunataka kufahamu
mipango ya Seif,tunataka kufahamu
nyendo zake ukitusaidiakutueleza
hilo ninakuahidi kwamba tutakuacha huru.Tunaamini wewe
na yeye ni washirika na lazima
unamfahamu vyema” akasema
Kaiza
“Nimekwisha sema kwamba
simfahamu kabisa huyu
mtu,nimekutana naye kwa mara ya
kwanza Congo,kama ningefahamu
jambo lolote kuhusu huyu mtu
ningekueleza” akasema Dr Olivia
“Dr Olivia fikiria kuhusu
hatima ya maisha yako kwani kama
hautatupa ukweli basi hautaweza
kutoka humu ndani.Yawezekana
ukawa ni mwisho wako.Ninakupa
nafasi nyingine ya kutafakari na
nitakaporejea tena humu ndani
nataka nipate maelezo yote kuhusiana na mipango ya Seif
Almuhsin” akasema Kaiza na
kutoka mle ndani akamuacha Dr
Olivia katika mawazo.
“Kaiza sijafurahishwa na kile
ulichokifanya mle ndani!! Akasema
Devotha kwa ukali wakiwa katika
ofisi yao baada ya Kaiza kutoka
kumuhoji Dr Olivia
“Ulitegemea nifanye nini
Devotha? Akauliza Kaiza
“I sent you in there to find
answers.Nilitegemea ungetumia
ujuzi na uzoefu wako katika
kuhakikisha unapata kile
tunachokihitaji.You were too soft.Is
it because she’s so pretty?akauliza
Devotha “Jamani nyote mmefuatilia kile
nilichozungumza na Dr Olivia na
kile alichokisema.This woman is
very smart.Anatakiwa kuhojiwa
taratibu.Tukienda haraka
tutashindwa kupata kile
tunachokihitaji”akasema Kaiza
“C’mon Kaiza we don’t have
much time.Tunatakiwa haraka sana
kutafuta majibu kutoka kwake.Joto
la kupotea kwake linazidi kupanda
huko nje hivyo tujitahidi kwa
haraka tuwezavyo kuhakikisha
tunapata majibu”akasema Devotha
“kwa kumtazama machoni
anaonekana kuna kitu
anakificha.Kuna jambo
analo.alipoiona video ile akiwa na Seif alistuka sana na hakutegemea
kabisa kama alikuwa
anafuatiliwa.Vijana wamefikia wapi
katika kuichunguza kompyuta
yake?Ukitazama katika ile video
Olivia na Seif walikuwa
wanaelekezana kitu katika ile
kompyuta na kwa kuwa Olivia
hakuwa na habai kama anafuatiliwa
naamini hakufuta vitu katika hiyo
kompyuta yake” akasema kaiza na
Devotha akamchukua wakaenda
katika ofisi ambako kompyuta ya
Dr Olivia ilikuwa inafanyiwa
uchunguzi
“Kuna chochote mmekipata
hadi sasa?akauliza Devotha “Tumepata mawasiliano yake
ya barua pepe lakini baada ya
kuyachunguza tumekuta
anawasiliana na mtu ambaye
anaitwa Sayid Omar ambaye
tunaendelea kufuatilia tujue
mahala alipo” akajibu mmoja wa
wale vijana na kumpatia Devotha
karatasi kadhaa.
“Hayo ndiyo mawasiliano yao
lakini wametumia lugha ya
kiarabu”
“Damn! Tutapataje tafsiri ya
mawasiliano yao?Ni Aziz pekee
ambaye alikuwa anafahamu
kiarabu.Kuna ulazima wa kutafuta
mtu anayejua lugha ya kiarabu au
kumpeleka kijana mmoja akajifunze lugha hiyo.Ni muhimu
sana kwa sasa.Yawezekana katika
mawasiliano haya kuna mambo ya
muhimu sana yanayoweza kutupa
mwanga mkubwa lakini hatuwezi
kufahamu chochote kwa kuwa
hatujui kiarabu” akasema Devotha
“Hii pia ni picha ambayo
tumeikuta katika kompyuta yake”
akasema yule kijana na kumpatia
Devotha picha waliyoikuta katika
kompyuta ya Dr Olivia
“Coletha..Huyu ni mtoto wa
rais” akasema Devotha akionekana
kushangaa
“Rais Dr Evans na Agrey baba
yake Olivia ni marafiki wakubwa na
familia zao ni marafiki pia hivyo Olivia kuwa na picha ya Coletha
haileti wasiwasi kwani naamini
wanafahamiana.Kikubwa hapa ni
kuhakikisha tunamfahamu huyu
Sayid Omar ni nani na yuko
wapi.Ingekuwa rahisi sana kwetu
kama tungeweza kujua
kilichoandikwa katika barua pepe
hizi walizokuwa wanatumiana
lakini hatujui kiarabu hivyo kitu
pekee tulichonacho ni kujua mahala
aliko huyo Sayid” akasema Kaiza
“Damn !! akasema mmoja wa
wale vijana mle ndani
“Kuna nini?akauliza Devotha
“Hawa jamaa ni wataalamu
kwani ukijaribu kufuatilia namba
ya kompyuta anayotumia huyo Omar unakuta kuna zaidi ya
kompyuta mia moja ambazo
zinaonekana ziko sehemu mbali
mbali duniani kwa hiyo ni vigumu
kufahamu ni yupi hasa
anayewasiliana na
Olivia.Wamefanya hivi ili
kumchanganya yeyote ambaye
atahitaji kufuatilia kutaka kujua
mahala aliko Sayid”
“Damn !! akasema Devotha
kwa ukali
“Endeleeni kufuatilia kama
kuna chochote tutakipata,Kaiza
tunakwenda tena kwa
Olivia.Lazima atueleze huyu Sayid
Omar ni nani” akasema Devotha.
nitarudi.
Baki huko huko
hahahaha mkuu...NITARUDI.
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni EquatorStory
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
Mzee tunaweza kuongea kwa what's up 0658328596

Nahitaji kuweka stories zangu pia
 
Mtunzi.Patrick CK

Season 1.SIRI

Simu.0764294499

Ndege ya shirika la ndege la Tanzania ilitua katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam ikitokea nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.Ndege ilisimama mlango ukafunguliwa na abiria wakaanza kushuka.

Mtu mmoja ambaye mavazi yake yalionyesha ni mfanyakazi wa kampuni moja ya upakiaji na upakuzi wa mizigo ndegeni alikuwa amejibanza mahala Fulani akiwa ameyaelekeza macho yake katika ndege ile akatoa simu na kupiga “Mlango umefunguliwa na abiria wameanza kushuka Ndege ya shirika la ndege la Tanzania ilitua katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam ikitokea nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Ndege ilisimama mlango ukafunguliwa na abiria wakaanza kushuka. Mtu mmoja ambaye mavazi yake yalionyesha ni mfanyakazi wa kampuni moja ya upakiaji na upakuzi wa mizigo ndegeni alikuwa amejibanza mahala Fulani akiwa ameyaelekeza macho yake katika ndege ile akatoa simu na kupiga “Mlango umefunguliwa na abiria wameanza kushuka”

Ndege ya shirika la ndege la Tanzania ilitua katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam ikitokea nchini jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.Ndege ilisimama mlango ukafunguliwa naabiria wakaanza kushuka.

.Mtu mmoja ambaye mavazi yake yalionyesha ni mfanyakazi wa kampuni moja ya upakiaji na upakuzi wa mizigo ndegeni alikuwa amejibanza mahala Fulani akiwa ameyaelekeza macho yake katika ndege ile akatoa simu na kupiga “Mlango umefunguliwa na abiria wameanza kushuka” “Sijakosea ni mwenyewe” akawaza na kupiga simu “Ameshuka ndegeni.

Amevaa suruali ya jeans ya bluu, fulana nyeupe,miwani myeusi ya jua” akasema yule jamaa “Una hakika ni yeye?akauliza jamaa wa upande wa pili wa simu “Ninamuona kwa mbali lakini nina uhakika ni yeye” “C’mon Denis.Get closer to her and confirm it’s her !!

Akasema kwa ukali jamaa aliyekuwa anazungumza na Denis simuni.Haraka haraka Denis akaanza kusogea kuwafuata abiria waliokuwa wanashuka lengo likiwa ni kumkaribia mrembo yule.

Hakuna aliyemtilia shaka kwani alikuwa ni mfanyakazi wa mle uwanjani.Alijitahidi sana na kumsogelea mrembo yule ambayealikuwa amevaa spika za masikioni na hakuonekana kuwa na wasi wasi wowote. “Confirmed.Ni yeye” Denisakatoa taarifa

“Good job Denis.Malipo yako yatakuja baadae” akasema yule jamaa upande wa pili wa simu na kukata simu. Msichana yule mrembo aliingia ndani ya jengo la uwanja na kukamilisha taratibu zote halafu akatoka akiwa na mkoba mweupe na sanduku dogo la chuma alilokuwa analikokota.Katika sehemu ya kusubiria wageni watu watatu walikuwa
wanamsubiri.

Wote walikuwa wamevaa suti nzuri zilizowapendeza,wakasalimiana kisha mmoja wao akalibeba sanduku la yule mrembo wakaelekea garini. “Anaelekea garini,yuko na walinzi wake” jamaa mmoja aliyekuwa katika sehemu ya kupokelea wageni akawasiliana na wenzake

“Wako walinzi wangapi?akaulizwa “Ana walinzi watatu”akajibu "Good.Kila kitu kiende kama kilivyopangwa” akasema jamaa aliyeonekana ndiye mkubwa wa wale jamaa waliokuwa wakimfuatilia yule mrembo Msichana yule mrembo akaelekea katika gari moja zuri jeusi aina ya Landcruiser V8 akafunguliwa mlango akaingia pamoja na mlinzi mmoja.

Wengine wawili wakaingia katika gari la nyuma yake kisha wakaondoka pale uwanjani. “She’s on move” Jamaa
mwingine aliyekuwa katika gari lililokuwa pale uwanjani akatoa taarifa kisha akawasha gari wakaondoka wakaanza kulifu lile gari alilopanda yule msichana.Jamaa walikuwa wamejipnga kwa kuweka watu katika barabara kadhaa kwa ajili ya kumfuatilia yule msichana lengo kwa kupokezana ili asiweze kugundua kama anafuatiliwa.

Walitumia magari tofauti tofauti ili wasigundulike Gari la yule msichana liliingia barabara ya Msanda ambayo inaelekea pembezoni mwa jiji “Ameingia barabara ya Msanda nadhani anaelekea nyumbani kwake” akasema jamaa aliyekuwa katika gari lililoshika zamu ya kumfuatilia.Wale jamaa walikuwa sahihi kwani msichana yule alikuwa anaeleka nyumbani kwake katika makazi mapya ya Urangi.

Ni eneo tulivu nje kidogo ya jiji ambalo limejengwa majumba ya kifahari sana. Barabara ilikuwa na magari
machache hivyo mwendo wa gari ulikuwa mkali.Gari zile mbili za yule msichana ziliacha barabara kuu na kufuata barabara ya changarawe lakini iliyojengwa vizuri sana, gari zile ambazo zilikuwa zinamfuatilia hazikumfuata tena bali zikaegesha pembeni ya barabara kusubiri maelekezo Mita kama mia tano kabla ya kulifikia jumba lake ikatokea helkopta yenye rangi nyeupe ambayo ilikuwa inapita chini sana.

Helkopta ile ilipofika usawa wa nyumba ya yule mrembo ikageukia barabarani ambako magari mawili ambalo moja wapo amepanda yule msichana yalikuwa yamepunguza mwendo kwani yalikaribia kufika katika jumba kubwa la yule msichana.Kitendo cha helkopta ile kupita chini sana na vile vile kusimama katika jumba lile kiliwashangaza walinzi wa yule mrembo.

“Something is not right.Olivia get down!! Akasema mlinzi aliyekuwa garini na yule msichana kisha akatoa bastora yake.Mlango wa helkopta ukafunguliwa na jamaa mmoja aliyekuwa na bunduki kubwa akajitokeza na kwa kasi ya aina yake akaanza kumimina risasi kuelekea katika yale magari ambayo yalibakiza mita chache sana kufika nyumbani na tayari geti lilikwisha funguliwa.

Dereva wa gari la mbele alilopanda yule msichana mrembo akapigwa risasi ya kichwa na gari lile likapoteza uelekeo na kwenda kugonga ukuta.Mvua ya risasi ikaendelea kunyeshea gari lililokuwa nyuma ambalo lilikwenda kuligonga kwa nyuma gari la mbele alimokuwa amepanda yule msichana mrembo aliyekuwa amelala chini ya kiti.Watu wote waliokuwa katika gari lile la nyuma walikuwa wameuawa na ile mvua ya risasi toka kwa mtu aliyekuwa katika mlango wa helkopta.

Mlinzi mmoja tu aliyebaki alifungua mlango na kutaka kutoka nje ili kukabiliana na watu wale katika helkopta lakini hakufanya chochote kwani alijikuta akichakazwa kwa risasi akaanguka na kufa pale pale. Kwa kasi kubwa zikafika gari mbili ,wakashuka watu sita,waliokuwa na silaha wakiwa wamefunika nyuso zao na kujihami kwa fulana za kujikinga kwa risasi.

Haraka haraka wakaenda katika gari na kumtoa msichana yule mrembo wakamuingiza katika gari lao,likachukuliwa pia sanduku lake pamoja na mkoba mdogo aliokuwa nao kisha magari yale mawili yakaondoka kwa kasi kubwa.Helkopta nayo ambayo bado ilikuwa pale juu ikapaa na kutoweka.

“We have giraffe..I repeat we have giraffe” jamaa mmoja aliyekuwa katika gari moja kati ya zile mbili akawajulisha wenzake “Good job.Kila kitu kiende kama kilivyopangwa” akatoa maelekezo“Sawa mkuu”akajibu yule jamaa. Gari zile zilikwenda kwa mwendo wa kasi na baada ya kufika katika mzunguko wa picha ya kiboko,zikaachana kila moja ikafuata njia yake.

Moja ikafuata barabara ya umoja wa Afrika na nyingine ikafuata barabara ya Kannani.Gari zote mbili zilikuwa na namba zinazofanana ili kuwachanganya wale watakaozifuatilia.Gari ile iliyopita barabara ya Kannani ndiyo ambayo msichana yule mrembo alikuwemo,ilielekea moja kwa moja hadi katika nyuma moja maeneo ya vigenge likafunguliwa geti likaingia ndani.

Haraka haraka msichana yule akashushwa garini akafungwa mikono na miguu akaingizwa katika buti ya gari lingine aina ya mercedece benzi na gari lile likatoka bila kupoteza muda.Lile gari lingine lililokuwa limembeba mwanzo likafunguliwa namba zile za bandia na kufungwa namba zake halisi kisha nalo likatoka.

Gari lile aina ya Mercedece Benz lililokuwa na watu watatu ndani yake,lilikwenda hadi katika jumba moja kubwa likafunguliwa geti na kuingia ndani hadi gereji.Wale jamaa wakashuka garini,buti likafunguliwa yule msichana mrembo akashushwa akaingizwa ndani ya lile jumba akapelekwa katika chumba kimoja akawekwa kitandani.Bado mikono na miguu ilikuwa imefungwa pia usoni alikuwa amefungwa kitambaa hakuweza kuona chochote na mdomoni aliwekewa kitu cha kumzuia kupiga kelele.

Mlango ukafungwa wale jamaa wakatoka. Dakika chache baadae gari mbili zikawasili na kutoka katika gari la nyuma akashuka jamaa mmoja mnene. “Mr Kaiza kazi imemalizika na Dr Olivia yuko ndani tayari”akasema mmoja wa wale jamaa waliofanikisha kumteka Olivia “Kazi nzuri sana Godson” akasema Kaiza

“Huu hapa mkoba wake ndani yake kuna mkufu,simu na vifaa vidogo vidogo” akasema Godson na kumkabidhi Kaiza vile vifaa
******************

Taarifa za tukio la kutekwa kwa Dr Olivia Themba mtoto wa bilionea Agrey Themba zilianza kusambaa kwa kasiya upepo kwani ni mtu ambaye anafahamika sana.Kwanza ni kutokana na shughuli anayoifanya ya udaktari na utafiti wa magonjwa mbali mbali na vile vile kuwa mtoto wa bilionea Agrey Themba. Dr Olivia Themba ni mtoto wa tatu kuzaliwa kati ya watoto watano wa mabilionea Agrey na Lucy Themba.

Baada ya kuhitimu masomo yake ya udaktari alirejea nchini na kufanya kazi katika hospotali kuu ya magonjwa ya moyo kabla ya kuanzisha kituo chake cha utafiti wa magonjwa mbalimbali ya binadamu na wanyama.Kupitia kituo hicho kikubwa cha utafiti katika ukanda wa Afrika mashariki na kati wamefanikiwa kupata tiba ya magonjwa mbali mbali ya wanadamu na wanyama waliyoyafanyia utafiti.

Ni kituo ambacho kimekuwa na mafanikio makubwa na hata seriali wamekuwa wakikitegemea sana
kituo hiki katika tafiti mbali mbali za magonjwa ya binadamu na wanyama. Agrey Themba alipokea taarifa za kutekwa mwanae OIivia akiwa katika kikao muhimu cha kibiashara ikamlazimu kutoka kikaoni haraka sana na kumtaka dereva amuwahishe nyumbani kwa mwanae kujua kilichotokea na kuthibitisha kama taarifa zile ni za kweli.

“Ee Mungu kama kweli mwanangu ametekwa nyara,mlinde dhidi ya mikono ya watu hao waovu ambao hatujui wana lengo gani naye” Agrey akaomba akiwa garini.Alikuwa na wasi wasi mwingi “Nani hawa ambao wamethubutu kumteka mwanangu?Wanataka nini?

Akajiuliza Agrey aliyeonekana kuchanganyikiwa huku simu zake zikiendelea kuita mfululizo lakini alihisi mikono mizito hata kupokea simu “Ninawaza sana lakini mpaka sasa bado sijapata jibu nini hasa ambacho hawa jamaa wanakitaka hadi wamteke mwanangu.Je wamemteka ili wadai malipo ya fedha? Mbona hawajapiga simu kudai chochote mpaka
sasa? Akaendelea kujiuliza Agrey.

Simu aliyoamua kuipokea ni simu ya mke wake Lucy Themba ambaye alitaka kujua kama taarifa zile ni za kweli.Agrey alimueleza kuwa yuko njiani akielekea eneo la tukio kuthibitisha kama ni kweli mwanae ametekwa nyara.Mke wake naye alipanda gari haraka haraka akaanza safari ya kuelekea nyumbani kwa mwanae.

Agrey alifika nyumbani kwa Olivia na kitu cha kwanza kilichomthibitishia kwamba taarifa zile ni za kweli ni uwepo wa magari ya polisi pamoja na askari polisi kadhaa wenye silaha wakilinda eneo lile.Eneo lote la nyumba ya Dr Olivia lilizungushiwa utepe wa njano kulifunga eneo lile na kuzuia watu wasiingie wakati polisi wakiendelea na uchunguzi wao.

Agrey alishuka garini akapokewa na kamanda wa polisi wa wilaya ambaye alikuwa ameambatana na kikosi cha askari waliofika haraka sana eneo la tukio baada tu ya kupewa taarifa za tukio lile.Kamanda Sospeter Mwarabu akamjulisha Agrey kwamba taarifa zile za kutekwa kwa mwanae ni za kweli,akampeleka kumuonyesha gari alimokuwa amepanda Dr Olivia.Miili ya walinzi wa Olivia ilitolewa na kupelekwa hospitali kuhifadhiwa.

Askari polisi walikuwa wamezagaa kila kona ya nyumba ile wengine walikuwa ndani ya nyumba wengine shambani wote wakichunguza tukio lile.Agrey alichanganyikiwa baada ya kuona namna damu ilivyotapakaa ndani ya magari. “Kamanda Mwarabu una uhakika mwanangu ni mzima?akauliza Agrey kwa wasi wasi “Kwa taarifa tulizozipata kutoka kwa mlinzi wa getini ambaye wakati tukio linatokea alikuwa amejificha mwanao alichukuliwa ndani ya gari akiwa mzima na kuingizwa katika gari la watekaji.

Inaonekana hao jamaa lengo lao lilikuwa ni kumpata Olivia ndiyo maana wakawaua walinzi wake wote lakini yeye hawakumgusa.Ni watu wataalamu sana na mpango huu waliupanga kimakini mno” akasema kamanda wa polisi aliyekuwepo eneo la tukio. “My God please help my daughter !! akasema Agrey huku macho yake yakilengwa na machozi.Muda huo huo Lucy Themba mama yake Olivia naye aliwasili eneo la tukio na kushuka garini haraka haraka huku akifuta machozi akamfuata mumewe.

“Agrey tell me it’s not true! Akasema Lucy “Calm down my love.Tum…..” Kabla Agrey hajamaliza mke wake akaangua kilio kikubwa. “Lucy nyamaza kulia.We have to be strong for our daughter” akasema Agrey na kumnyamazisha mke wake. “Agrey please find my daughter!! Fanya kila uwezalo na hakikisha unampata Olivia.Nitakufa kama Olivia hatapatikana!! Akalia Lucy

“Lucy usihofu.Nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kwamba Olivia anapatikana.Polisi wanafanya kila wanaloweza kuhakikisha Olivia anapatikana haraka sana”akasema Agrey “Hao watekaji kama wanataka pesa wapatie kiasi chochote cha pesa wakitakacho ili mradi mwanangu awe salama” akasema Lucy kwa sauti ya chini “Ninaamini hao watekaji shida yao ni pesa hivyo lazima watapiga simu na kudai kiasi kikubwa cha fedha ili waweze kumuachia Olivcia.

Ninakuahidi Lucy kama wakipiga simu na kudai pesa nitawapa kiasi chochote wakitakacho ili wamuache huru binti yetu” akasema Agrey na kamanda wa polisi akawasogelea na kumpa pole Lucy “Kamanda kuna chochote mmekipata hadi sasa kinachoweza kupelekea kuwafahamu hao watekaji ni akina nani?akauliza Agrey

“Mpaka sasa bado ila tunaendelea na uchunguzi na kila pale tutakapopata chochote tutakuwa tunawajulisha.Kwa sasa ninawahitaji tuzungumze kidogo” akasema kamanda Mwarabu wakaelekea ndani sebuleni. “Bwana na bi Themba napenda kuwajulisha kwamba jeshi la polisi tulipokea taarifa kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa Dr Olivia aliyetujulishja kuhusu tukio lililotokea na tukafika hapa ndani ya muda mfupi sana lakini tayari watekaji walikwisha mchukua Dr Olivia na kutoweka.

Tumeambiwa kwamba watekaji walikuwa na helkopta na mtu aliyekuwa na bunduki ambaye alikuwa anarusha risasi kutokea ndani ya helkopta na baadae yakatokea magari mawili na watu wakashuka wakiwa na silaha na kumchukua Dr Olivia.Tayari tunawashikilia watumishi wote wa ndani pamoja na mlinzi aliyekuwepo getini kwa mahojiano,tunafuatilia vile vile picha za kamera za ulinzi kwani jumba hili la Dr OIivia kuna kamera nne.

Ninawahakikishia kwamba tunafanya kila juhudi kuhakikisha kwamba mwanenu anapatikana haraka tena akiwa hai. Ninachoomba ni ushirikiano wenu mkubwa.Bado hatujui lengo la watekaji hawa ni nini, lakini kuna mambo mengi yanayoweza kupelekea wakamteka Dr Olivia.

Yawezekana watekaji wanahitaji fedha,yawezekana ikawa ni visasi,na yawezekana ikawa hata ni wivu wa kimapenzi. Sababu ziko nyingi na tunajaribu kuangalia sababu inayoweza kupelekea Dr Olivia akatekwa.Katika hili tunahitaji sana msaada wenu.Ninyi ni wazazi wake na mwanenu mnamfahamu vyema, nataka kufahamu kutoka kwenu kuhusu maisha yake kwa ujumla”akasema Kamanda Mwarabu Agrey akavuta pumzi ndefu na kusema

“Olivia ni mtu anayependa kuishi maisha ya kawaida sana.Hata baada ya kumaliza masomo yake ya udaktari na kuanza kazi bado tulikuwa tukiishi naye nyumbani kwetu.Ni binti wa pekee kwetu na hatukuwa tayari kumuacha akaishi peke yake lakini alituomba kwamba tayari amekwisha kuwa mtu mzima na anahitaji kuanza maisha yake mwenyewe ndipo tulipomruhusu akaja kuishi hapa katika nyumba hii.

Olivia ni mpole na sina hakika kama ana maadui wowote.Aliamua kusomea udaktari ili awasaidie watu kwani ni kitu alichokipenda toka akiwa mtoto mdogo.Amekuwa anaifanya kazi yake ya udaktari kwa moyo na upendo mkubwa ndiyo maana akawa ni mmoja wa madaktari maarufu hapa nchini”akasema Agrey “Mara ya mwisho kuwasiliana naye ilikuwa lini?akauliza kamanda “Leo asubuhi.Alitupigia simu akiwa Cogo DRC alikoenda kwa shughuli zake za udaktari na akatujulisha kwamba anarejea nchini leo mchana” akajibu Agrey “Dr Olivia yuko kwenye mahusiano? Mnamfahamu mpenzi wake?

“Mpaka sasa Olivia bado hajamuweka wazi mpenzi wake.Kila ninapomuuliza kuhusu suala la mahusiano jibu lake ni kwamba ataweka wazi mambo yote muda ukifika.Amejikita zaidi katika kazi zake ndiyo maana hajaweka wazi mpenzi wake hadi sasa”akajibu Agrey “Bwana na Bi Themba, kama hawa jamaa lengo lao la kumteka Dr Olivia ni kujipatia fedha tuna hakika watawasiliana nanyi na kudai fedha.Kama wakiwapigia simu tafadhali tuwasiliane haraka sana.

Najua wakipiga simu watawatisha msitoe taarifa kwa polisi ama watamuua mtoto wenu lakini nawaomba msiogope,wasilianeni haraka sana na jeshi la polisi na tutafanya kila juhudi za kumkomboa Olivia na kudhibiti matukio kama haya yasiendelee hapa nchini.Endapo pia mtapata taarifa zozote zinazoweza kusaidia kuwafahamu watekaji hawa msisite kutujulisha haraka sana” akasema kamanda wa polisi “Afande tutatoa ushirikiano mkubwa sana kila pale tutakapopata chochote kile kuhusiana na kutekwa kwa binti yetu.

Nakuomba vilevile muwe mnatujulisha kila hatua mnayopiga katika uchunguzi huu” akasema Agrey Themba na kamanda wa polisi akatoka kwenda kuendelea na uchunguzi wao.Agrey akamshika mkono mke wake wakatoka mle ndani hadi katika gari lake wakaondoka eneo la tukio.Bado Lucy alikuwa anaendelea kulia.

KItendo cha binti yake kutekwa nyara kilimuumiza mno.Wakiwa garini Agrey alikuwa na kazi ya kupokea simu zilizokuwa zinaingia mfululizo kutoka kwa watu mbali mbali wakiwapa pole kufuatia kitendo kile cha kutekwa binti yao Dr Olivia.Simu ya Agrey ambayo huitumia kuwasiliana na watu wake wa muhimu ikaita, alikuwa ni rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Evans mwaluba.

Agrey akamuonyesha mke wake “Rais anapiga” akasema Agrey na kupokea ile simu “Dr Evans” akasema Agrey “Agrey nimepata taarifa za tukio la kutekwa Dr Olivia nimestuka sana” akasema Dr Evans Agrey akavuta pumzi ndefu na kusema “Mheshimiwa rais ni kweli tukio hili limetokea na Olivia ametekwa.Lucy na mimi tumetoka eneo la tukio sasa hivi na hali tuliyoikuta pale ni ya kutisha.Walinzi wote wa Olivia wameuawa na yeye kutekwa nyara.

Hatujui ni nani waliomteka nyara na kwa kusudi lipi” akasema Agrey “Poleni sana Agrey.Hizi ni taarifa za kustusha mno.Matokeo kama haya ya utekaji ni mageni sana hapa nchini kwetu.Hatukuzoea mambo ya namna hii”akasema rais “Mheshimiwa rais naomba tafadhali utusaidie binti yetu apatikane na watekaji hawa wajulikane.Kama familia tumeumizwa mno na kitendo hiki” akasema Agrey

“Agrey mimi kama mtu wa karibu na familia yako nimeumizwa pia na jambo hili na ninakuahidi kwamba kwa namna yoyote ile lazima Olivia apatikane akiwa mzima wa afya. Nitatumia kila nguvu niliyonayo kuhakikisha Olivia anapatikana.Tayari nimekwisha toa maelekezo kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini kwamba wahakikishe hadi kufika jioni ya leo Olivia awe amepatikana.Nimeelekeza nguvu kubwa iwekwe katika kuwasaka watekaji ambao tunaamini bado wako hapa hapa Dar es salaam.

Tayari njia zote za kuingia na kutoka Dar es salaam zimefungwa na msako mkali umekwisha anza.Nimeelekeza ikiwezekana ufanyike msako wa nyumba kwa nyumba hadi Olivia apatikane.Ninawatoa hofu Agrey na familia yako kwamba kama serikali tunafanya kila tuwezalo kuhakikisha kwamba Dr Olivia anapatikana.Hatuwezi kuwapa nafasi watekaji hawa ya kufanya kila watakacho katika nchi yetu hii iliyotamalaki amani” akasema Dr Evans naye akionekana kuumizwa sana na tukio lile

“Mheshimiwa rais ninakushukuru sana kwa maneno hayo ambayo yametupa faraja kubwa sana na matumaini ya kumpata mwanetu akiwa salama.Kwa niaba ya familia yangu ninasema ahsante sana” akasema Agrey “Nimeagiza kupewa ripoti kila baada ya saa moja kuhusiana na mwenendo mzima wa kuwasaka hao watekaji na kila nitakapokuwa ninapata taarifa nitakuwa ninawajulisha” akasema rais na kuagana na Agrey.

“Mheshimiwa rais naye ameguswa sana na ameahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha Olivia anapatikana.Amekwisha toa maelekezo kwa jeshi la polisi kufanya kila waliwezalo kuhakikisha Olivia anapatikana” Agrey akamwambia mke wake wakiwa garini wakirejea nyumbani kwao Mara tu rais alipomaliza kuzungumza na Agrey
Themba, akazitafuta namba za Devotha Adolph mkurugenzi wa idara maalum ya siri ya usalama wa ndani wa nchi akapiga na simu ikapokelewa.

“Devotha what’s the situation? akauliza Dr Evans “Kila kitu tayari mheshimiwa rais.We have Olivia in our custody”akajibu Devotha “Good.Hakikisha kila kitu kinakwenda vyema.Sitaki tatizo lolote litokee.Hakikisheni mnatumia kila aina ya mbinu kupata taarifa kutoka kwake.Taarifa alizonazo ni muhimu sana kwetu” “Sawa mheshimiwa rais,tayari tumejipanga vyema kwa ajili ya kuhakikisha anatupa taarifa zote” akasema Devotha

SIKU NNE ZILIZOPITA

Saa kumi na mbili za jioni gari moja jeusi liliwasili katika makazi ya rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania jijini Dar es...
Do
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom