Riwaya-duka la roho

Riwaya-duka la roho

RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
Masai akiwa hana nguvu za kutosha, akawa anakimbiza gari lake kuelekea maeneo ya Sinza, makao mapya waliyohamia na washirika wake. Kwa bahati nzuri alifika salama na kushuka garini.
Aligonga mlango na Lisa ndiye aliyeufungua. Lisa akakutana na mwili wa Masai ambao hauna nguvu. Ukamdondokea taratibu lakini mtoto wa kike akamdaka na kuanza kuwaita wenzake.
Malocha na Mubah wakatoka na kumsaidia Lisa kumuingiza Masai ndani.
"Nini kimetokea Masai?" Malocha aliuliza kwa kitetemeshi.
"Wamenivamia." Masai alijibu kwa shida huku bado maski yake hajaifungua usoni.
"Embu mvue hiyo saa. Malocha alimuamuru Mubah aliyekuwa upande wa mkono uliyovishwa saa. Alipomvua, maski nayo ikajifungua. Uso wa Frank ukaonekana wazi.
Damu zilikuwa zinamtoka puani na masikioni. Kila alipojaribu kuongea, alitokwa na damu sehemu hizo zote hadi mdomoni.
"Kalete vifaa ya huduma ya kwanza." Lisa akatoka haraka na kutekeleza alichoambiwa na Malocha. Vifaa vikaja na Malocha akaanza kuvitumia kumhudumia Masai.
"Mwambie Ndita aende duka lolote la Madawa na kuleta dripu za maji." Malocha akatoa ujumbe huo na mara moja Mubah akatoka kupeleka ujumbe kwa Ndita, mmoja wa wataalam wao.
Ndita akatoka pale nyumbani haraka na kwenda alipoagizwa. Lakini kwa bahati mbaya akakosa dripu. Ikabidi aende hospitali ya Mwananyamala ambako alutumia pesa kiasi na kupata dripu pamoja na damu pakiti mbili. Safari ya kurudi nyumbani anapoishi ikachukua nafasi yake tena.
"Na wewe umechelewa sana. Ila umefanya la maana kuleta na damu." Malocha aliongea huku akipiga piga mkono wa Masai aliyekuwa hajitambui lakini macho yake yakiangaza huku na huko kama mlevi ambaye pombe zimemzidi kichwani. Misuli ilipopatikana, Malocha akatundika pakiti ya dripu ya maji kwanza juu, na kisha kuingiza sindano ndogo iliyoanza kusafirisha maji hayo katika mwili wa Masai.
"Hii damu tutaweka baadae kama itahitajika, ngoja kwanza apate nguvu na haya maji kwanza." Alifuta jasho Malocha baada ya kazi hiyo nzito ya kidaktari.
"Atapona kweli Malocha." Lisa aliuliza kwa mashaka.
"Ondoa shaka Lisa. Hii ni kianzio tu. Nampigia daktari bingwa aje hapa amuangalie zaidi hadi ndani. Usitie shaka." Lisa akapewa moyo. Kwa unyonge akatoka katika chumba kile na kwenda chumbani kwake ambapo alimkuta Martina kakaa juu ya kitanda.
"Mbona hujalala Swetie." Lisa alimuuliza mwanaye huku akichongesha tabasamu.
"Yule atapona." Martina akauliza kwa sauti ya unyonge.
"Atapona. Usijali eeh." Lisa akamjibu na kumkumbatia mwanaye kisha kwa uchungu akaanza kulia kwa ndanindani ili mwanaye asisikie.
Hali ya Masai ilikuwa siyo ile aliyoondoka nayo. Mwili ulikuwa umechoka kwa sababu ya kipigo alichokipata kwa wale wauaji wa Kimataifa. Damu nyingi zilimtoka mwanaume yule, masikioni, puani na mdomoni zilikuwa hazizuiliki wala kukatishwa kirahisi.
Malocha alijaribu kumfunga vitambaa lakini kiukweli hali ilikuwa mbaya kwa Masai ambaye alikuwa anajikaza ili asipoteze fahamu.
Saa nane usiku, Lisa alisikia hodi ikigongwa kwa kengere maalumu na baada ya mlango kufunguliwa, Malocha akasikika akiongea na mtu. Lisa akashuka kitandani na kwenda hadi sebuleni ambapo alikuta Malocha kasimama na mzee mwenye miwani huku kabeba mkoba fulani wenye ukubwa kiasi chake.
"Lisa. Huyu ndiye dokta niliyemuita. Anaitwa Dokta Zabron, ni muaminifu, usitie shaka." Malocha alimtambulisha Daktari kwa Lisa na bila kuchelewa, tabibu yule akapelekwa chumba ambacho Masai kalazwa.
Mzee yule kwa haraka akaanza kazi yake aliyoisomea huku akifungua begi lake na kutoa kamera ndogo na kuanza kuupiga mwili wa Masai hasa ubavuni na sehemu zinazopita mifupa.
"Chukua funguo ya gari langu hii, nenda kafungue kwa nyuma, utakuta begi moja kubwa na mkoba wa kompyuta, vilete haraka." Dokta Zabron aliongea hayo huku akimkabidhi ufunguo wa gari Malocha. Wakati huo Mubah na wengine walikuwa wamezama katika usingizi mzito katika chumba walichoweka mitambo yao.
Baada ya dakika zipatazo tatu, Malocha akawa karudi na vitu alivyoagizwa. Mzee Zabron akatoa kompyuta yake mpakato na kuiwasha. Wakati anasubiria ilete mawasiliano, akaiweka pembeni na kisha akafungua begi kubwa aliloletewa na Malocha, akatoa vyuma fulani virefu ambavyo alivibana katika mbavu za Masai kisha akafanya kama anavijaza. Masai akawa anapanda juu.
"Binti, mshike kichwani na Malocha mshike miguuni ili asipinde." Bila kuchelewa, alolisema Daktari likatekelezwa na yeye akazidi kujaza vile vyuma hadi Masai akafika kiwango fulani pale juu. Wakati huo mwanaume yule alikuwa hajitambui hata chembe. Fahamu alizokuwa akijitahidi zisimuondoke, alishindwa kuzuia zisifanye hivyo. Alikuwa kapoteza fahamu kwa kipigo kikali cha Pinto na Trina.
Haraka Mzee Zabron alichukua kamera yake na kuingiza waya fulani (USB) na kuunga kwenye kompyuta yake. Akafungua programu moja iliyomo katika kompyuta yake na baadaye programu hiyo ikazichuja zile picha na kuonekana kwa mtindo wa picha za x rays.
"Hajavunjika kiungo chochote, sema kidogo kwenye kifua damu imegandia sana ndio maana haikatiki. Hapo nimemnyanyua ili damu iwe inatambaa mwilini kwake kwa kasi na hiyo itasaidia hata huo mgando wa damu kufagiwa taratibu." Mzee Zabron aliongea alichokiona. "Ngoja nimuwekee na hivi ili msipate shida ya kumkamata." Zabron akachukua vyuma vingine na kuviweka kichwani kwa Masai na miguuni. Mwanaume akawa kama anaelea angani.
"Na hii sindano itasaidia kulainisha damu iliyoganda." Mzee yule alizidi kufafanua huku anavuta dawa hiyo na kisha akaidunga kwenye kifua kipana cha Masai. Masai akatoa pumzi ndefu kama mwanariadha aliyetoka kukimbia mbio ndefu. "Kila baada ya masaa manne uwe unamchoma kifuani kwa kiasi kilichoandikwa hapo. Hiyo pia ni busta nzuri ya moyo kama utakuwa unafeli kupeleka damu na hewa." Mzee Zabron alimaliza maongezi yake na kuanza kukusanya vifaa baadhi alivyovitoa kwenyw mkoba wake.
"Asante sana Dokta." Malocha alishukuru wakati daktari yule akifungia vifaa vyake.
"Usijali. Hizo dripu zikiisha, basi. Msimuwekee tena. Kuweni waangalifu sana. Kifuani yaonekana kapigwa sana na vitu kama risasi hivi. Sasa damu imegandia hapo. Ni damu kubwa ambayo mkizembea kumchoma hizo sindano kumi, mtampoteza mtu wenu." Mzee Zabron aliwapa onyo mapema.
"Usijali Mzee wangu. Tumekuelewa." Malocha akaongea.
"Oooh! Halafu nilitaka kusahau." Mzee yule aliongea na kufungua mkoba wake mwingine na kutoa mashine fulani wanayoitumia sana hospitali kwa wagonjwa wasiojitambua. Akamvisha kiduwasha fulani Masai kwenye kidole chake na katika kidubuwasha hicho kuna waya ambao unaenda moja kwa moja katika mashine ile iliyoungwa katika umeme.
"Hii inasoma mapigo yake ya moyo. Sasa hivi yapo sitini na tano, yanatakiwa yapande hadi mia moja hasa hapo mnapomchoma sindano. Akiwa mzima, yacheze kwenye sabini hadi themanini. Sawa?" Mzee Zabron akazidi kutoa maelekezo mbalimbali hadi pale alipoona watu wake wameelewa. Akatoka nje ya nyumba ile saa kumi na yeye akaelekea kwake.
****
"Pumbavu tumemkosa yule." Pinto aliongea kwa lugha zao za huko akiwa na Trina aliyekuwa kaweka barafu kisogoni.
"Itakuwa ngumu sana kumpata sasa hivi na kumuua. Kishajua kuwa tunamuwinda." Trina akaongea.
"Inabidi twende naye hivyohivyo, hakuna kumkawiza tukimpata."
"Ndiyo hivyo. Sema na ile suti sijui kaitoa wapi. Anabahati sana yule mjinga."
"Sijawahi kuona vazi la namna ile duniani. Wote tuliowaua wangejua kuwa kuna vazi lile, tungepata shida sana. Lakini huyu tutamuua tu. Ngoja tufanye mkakati mwingine. Huyo Rais wao tusionekane tena kwake na wala kugusa katika ile hoteli." Pinto alishauri na kunyanyuka kwenda kwenye friji lililokuwepo katika chumba chao kipya. Akafungua na kutoa juisi ambayo alianza kuigida kwa fujo kama mwenye kiu.
****
"Hawa ni Pinto na Trina kumbe?" Sauti ya Malocha ilisikika katika mshangao mkubwa. Ilikuwa ni asubuhi na kituo fulani cha Runinga kilikuwa kinaonesha taarifa ya habari zilizowafikia asubuhi ile.
Ilikuwa ni taarifa ambayo ilieleza tukio zima lililotokea usiku wa jana yake. Kamera zilizopo maduka ya Mlimani City, zilinasa tukio na picha za watuhumiwa wakiwa katika mpambano. Wazungu wawili ambao ni Pinto na Trina, walionekana sura zao lakini mmoja ambaye ni Masai, hakuweza kutambulika haraka kwa sababu ya mavazi aliyokuwa kayavaa.
"Unawajua hawa watu Malocha?" Lisa alimuuliza Malocha ambaye alimuangalia usoni kidogo na kisha kufungua mdomo wake kuongea akijuacho.
"Hawa ni wauaji wa kimataifa. Hutumwa kuua tu! Hawana kazi nyingine zaidi ya hiyo. Na hulipwa mabilioni ya fedha kwa wakifanyacho."
"Kwa hiyo wametumwa kumuua Masai?" Mubah aliuliza.
"Nadhani. Lakini tushukuru MUNGU hawajafanikiwa. Hawa hufanya kazi yao mara moja tu. Masai ndio wa kwanza kutoroka kifo."
"Nani atakuwa kawatuma?" Lisa akatupa swali.
"Itakuwa wanetumwa baada ya yale aliyoyasimamisha. Mtu wa kwanza kumuhisi kafanya haya ni The Shadow. Kama si huyu basi Lobo na Gunner."
"Mmmh! Hii sasa ni hatari hadi wanawatuma Pro Killers? Duh!" Mubah akaonesha mshangao wake waziwazi.
"Hawa ni hatari kuliko simba mwenye njaa. Wamezungukwa na silaha katika miili yao yote." Malocha akaongeza sukari katika chai ya maongezi yale.
"Mmh! Sasa wakijua kuwa tupo hapa kabla Masai hajapona, si watakuja kummaliza?" Lisa wasiwasi wake ukawa juu baada ya maneno ya Malocha.
"Hapana. Hawawezi kujua japo wakijua itakuwa ni tatizo kubwa." Malocha akajibu.
"Itabidi tuwe makini sana. Kaanza Masai, tunaofatia ni sisi. Haya mambo ya kutoka toka hovyo, yatatufanya tuvamiwe hapa. Tujaribu kujificha kwa muda huu hadi Masai apone ndipo tujue jinsi ya kuwakabiri hawa watu." Mubah akatoa pendekezo zuri kabisa.
"Umeeleweka kijana. Ushauri mzuri sana." Malocha alimuunga mkono Mubah.
****
Wiki ilikata huku Masai akiwa kitandani lakini akiwa kashushwa chini alipokuwa kanyanyuliwa na vyuma maalumu kwa ajili hiyo. Alikuwa anapumua vema kabisa lakini bado fahamu zilikuwa hazijarudi.
"Martina. Njoo umuone baba." Lisa alimuita mwanaye ambaye hakuwahi.kuingia chumba alichokuwepo baba yake bali kuishia mlangoni na kuchungulia tu. Aliposikia mama yake anamuita, akabaki kasimama asijue anataka kwenda au kuondoka. "Martina." Lisa akamuita tena mwanaye.
Martina kwa hatua za woga akasogea kwa kusita kama gari linaloendeshwa na mtu anayejifunza. "Njoo." Lisa akamuita zaidi Martina.
Mtoto akajivuta hadi pale alipomama yake lakini hakumsogelea baba yake aliyekuwa kitandani anapumua taratibu bila mashine.
"Kamguse baba pale." Lisa akamuonesha Martina sehemu ya shavu ili Martina akaguse. Mtoto yule akafikiria kwa muda kabla hajafanya maamuzi.
Akakumbuka zawadi za midoli aliyokuwa analetewa na mtu yule. Akakumbuka jinsi anavyofurahi akiwa na mama yake na jinsi anavyojaribu kumvutia ili amkubali. Akaenda mbali zaidi na kumkumbuka Gunner ambaye mara nyingi ni mtu wa kumfundisha mambo ya kigaidi tu. Akafananisha uso wa mama yake awapo na Gunner na awapo na Masai. Akagundua kuwa mama yake kawa na furaha zaidi kuliko kipindi cha nyuma alipokuwa na Gunner.
Hakuishia hapo pekee. Akawaangalia watu aliowazoea mle ndani, wote walikuwa wanaamani wawapo na Masai kasoro yeye tu! Akajiona kama mwenye makosa kukaa mbali na mtu yule.
Taratibu akapiga hatua moja kwenda kitandani alipolala Masai. Baada ya hatua hiyo, akageuka nyuma na kumuaangalia mama yake.
"Nenda." Lisa akamsukuma kwa ishara. Martina akazidi kusogea hadi pale alipo Masai na kisha kwa kutetemeka, akanyoosha mkono wake na kumshika Masai shavuni.
"Mshike kwa mikono miwili." Lisa akampa maelekezo tena mwanaye ambaye naye alifanya hivyo kwa kushika mashavu ya Masai yaloliyokuwa yamejaa ndevu laini.
Mara Masai akapumua pumzi ndefu iliyomfanya Martina arudi nyuma haraka kwa uoga.
"Usikimbie Martina. Ataamka kama ukiwa hapohapo." Lisa akamwambia mwanaye kwa furaha huku naye akinyanyuka na kusomsogeza mwanaye zaidi. "Mshike tena." Lisa akamuongoza mwanaye. Martina akafanya kama alivyofanya mwanzo kwa sekunde kadhaa.
"Mbona haamki?" Martina aliuliza kwa upole wa kitoto.
"Mlalie kifuani na kumkumbatia, utaona anaamka." Martina akamuangalia mama yake kabla hajafanya hivyo lakini kwa kuwa alikusudia kumuamsha baba yake, akaamua kufanya hivyo kwa dakika moja.
Akiwa kamkumbatia na kufumba macho, mara Martina alihisi mkono ukizipapasa nywele zake. Akaamka haraka na kutazama anayefanya hayo, uso kwa uso na sura ya Masai iliyokuwa inatabasamu.
"Asante Martina." Masai akashukuru na wakati huo Lisa alikuwa haamini akionacho. Tabasamu lililoambatana na machozi ya furaha, vyote vilijitokeza.
"Kaamka huyu mama." Martina aliongea huku naye anaonesha furaha yake.
"Ni baba yako Martina." Lisa alijaribu kumuelekeza Martina ambaye alimgeukia Masai na kumuangalia tena.
ITAENDELEA
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI
Akiwa kamkumbatia na kufumba macho, mara Martina alihisi mkono ukizipapasa nywele zake. Akaamka haraka na kutazama anayefanya hayo, uso kwa uso na sura ya Masai iliyokuwa inatabasamu.
"Asante Martina." Masai akashukuru na wakati huo Lisa alikuwa haamini akionacho. Tabasamu lililoambatana na machozi ya furaha, vyote vilijitokeza.
"Kaamka huyu mama." Martina aliongea huku naye anaonesha furaha yake.
"Ni baba yako Martina." Lisa alijaribu kumuelekeza Martina ambaye alimgeukia Masai na kumuangalia tena.
"Siyo baba yangu huyu. Namjua baba aliyenilea." Martina aliongea kwa sauti ya ukali na kumfanya mama yake atake kujibu kwa ukali pia lakini Masai akamuwahi.
"Yupo sahihi Lisa. Martina yupo sahihi sana." Masai aliongea kwa sauti ya chini na kukohoa kidogo.
"Yupo sahihi kumkana baba yake." Lisa akamuuliza huku macho yake ya hasira kamuelekezea Martina.
"Lisa. Nimefanya nini cha maana kwa huyu mtoto hadi astahili kuniita baba? Mi' ni baba kibailojia tu! Ila kiuhalisia Martina hastahili kuniita hata mjomba. Sijui alikuwaje wala sijui ni mangapi aliyapitia. Nachojua ni kwamba nilijificha miaka mitano pasipo wasiliana na wewe wala kutaka kumjua Martina. Hata wewe, ni roho yako njema ndio umenipokea mimi tena, lakini mimi si wa kuwa na wewe Lisa. I don't deserve you, Lisa." Masai aliongea kwa uchungu na kujikuta akitoa machozi.
"Samahani Frank. Labda Martina yupo sawa." Lisa aliongea huku akimkumbatia mpenzi wake pale kitandani.
"Martina. Usijali mama eeh." Lisa alijaribu kumfariji na Martina pia aliyekuwa kakasirika.
"Martina. Mi ni Anko Masai, sawa eeh." Martina akaitikia kwa kichwa kukubali.
"At least naweza kuwa naye karibu. Atabadilika na kunitambua. Usimfanye anichukie Lisa." Masai akatamka hayo baada ya Martina kutoka mle chumbani kwenda kuwaita wakina Malocha waje kumuona Masai.
****
Baada ya siku tano, Masai alikuwa anaweza kutembea na hali yake ilikuwa inarudi taratibu japo bado alikuwa analalamika sana kifua kuwa kinamuuma. Alikuwa anafanya mazoezi ya mwili kwa dakika kadhaa na kukaa kwa sababu ya kifua hicho.
"Bado sijakaa sawa kabisa. Dakika tatu tu! Tayari maumivu yananiganda." Masai alikuwa anampa taarifa Malocha.
"Usijali Kamanda, utakuwa sawa tu." Malocha akamfariji.
"Mmefikia wapi katika kuwasaka hawa wajinga." Masai akauliza kuhusu mkakati wa wakina Malocha katika kuwasaka Pinto na Trina.
"Wajinga bado wapo nchini sema mafichoni sana. Hapa kuna jamaa yupo FISSA mle, ndio anatusaidia sana kutupa taarifa za hawa jamaa." Malocha akajibu.
"Nitawapata tu. Ngoja nitengamae. Na bahati yao hawatumii mawasaliano yanatumia satellite." Masai akaongea huku akichukua taulo na kujifuta jasho.
Baada ya wiki mbili, Masai alikuwa katengamaa na sasa hali yake ilikuwa safi zaidi. Alikuwa tayari kwa lolote japo katika upande wa suti yake, ile maski ya kichwani ilikuwa haifanyi kazi tena na upande wa kushoto wa kifua wa ile suti, kulitengeneza mchakao ambao ungefanya suti ile kuharibika baada ya kupigwa kidogo tu. Lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kumshukuru MUNGU kwa pale alipofikia.
Ukaribu wake na Martina ulianza kuwa mzuri na mtoto yule alikuwa hamuogopi sana Masai kama zamani. Alikuwa akicheza naye hadi usiku ambapo alikuwa analala usingizi mnono kama Masai atamuimbia. Martina akawa mwenye furaha lakini hakumzidi Masai furaha hiyo japo aliitwa Anko na mtoto wake wa damu.
"Hey Masai. Kuna mawasiliano yamenaswa na FISSA kati ya Pinto na mtu ambaye hajulikani yupo huko Hispania." Mtaalamu wa mitambo wa Malocha alimpa taarifa Masai zilizoletwa na mtu anayewasiliana na Malocha ndani ya FISSA. Masai akasogea hadi pale zilipotumwa taarifa zile na kuzisoma vema.
"Okay. Weka hiyo namba kwenye tracer yetu. Tuone inapatikana wapi." Masai akashauri na baada ya muda namba ile ikajieleza imepigwa wapi.
Ilikuwa ni Buza Kanisani na Frank kwa umakini mkubwa, akafunga safari hadi huko kwa kufuata ramani iliyotoka wakati wa kuitafuta namba hiyo.
"Oya." Masai akatoa uso nje ya kioo cha gari na kumuita dereva mmoja wa bajaji aliyekuwepo karibu na pale.
"Sema Bro." Jamaa akasalimia kwa mahashamu.
"Fresh. Najua we' mwenyeji hapa. Naomba kukuulizia kama umewahi kuwaona wazungu wawili, wa kike na wa kiume wakilanda mitaa hii." Masai akauliza na kumfanya yule jamaa asimamishe kichwa angani kama mwenye kufikiria jambo.
"Ahaaa. Wale watasha wawili wanaopiga bendi? Wanakaa pale Buza Tanesco, kama si pale, basi Kipera." Jamaa akajibu kwa furaha huku akitaja mitaa kadhaa ya Buza ambayo Masai anaweza kuwapata wale wazungu.
"Kumbe wasanii?" Masai akajidai kuuliza kwa hamaki.
"Weee. Wale acha kabisa. Wanapiga magitaa kama hawana akili nzuri. Kila Jumamosi wanapiga Toxido hapo." Jamaa yule aliongea na kunyoshea katika kilabu cha pombe za kisasa kiitwacho Toxido.
"Daaah. Nawatafuta sana maana walinipa mawasiliano yao lakini hawapatikani. Waliniambia kuwa wanataka kutafuta wacheza filamu wa kitanzania, sasa hapa kati nikaumwa ndio nikasimama hata kuwasaka." Masai akadanganya ili asishtukiwe.
"Aah! Kumbe wanaigiza. Basi kaka ukitaka kupata waigizaji, mimi tayari nimooo. Yaani napiga mateke kama Damme." Jamaa akajinadi.
"Nittakutafuta jembe langu. Kamata hii, halafu Jumamosi mbili zijazo, njoo hapo Toxido ujionee." Masai akaongea huku akimpa noti ya elfu kumi yule bwana.
"Ohooo. Rangi ya mende hii kaka mkubwa. Asante sana, mmmhmwaaa." Jamaa alishukuru na kuibusu ile elfu kumi. Masai akatabasamu na kuondoka eneo lile akiwa na wazo la kurudi Jumamosi mbili zijazo.
Alinyoosha barabara moja kwa moja kutoka Buza Kanisani na kupita Buza Tanesco. Akatazama mazingira ya pale kidogo, kisha akanyoosha gari lake kuelekea Machimbo Mwisho wa Rami ambapo napo alichora alama za kutosha zitakazo msaidia kufanya mambo yake. Baada ya hapo, akakanyaga mafuta na kutitia mahali pale kwa kurudi nyumbani.
"Nimekwishawapata wale wajinga." Masai aliongea akiwa na Malocha.
"Kazi nzuri Kamanda. Hawa lazima tuwaue." Malocha akajibu huku akivuta glasi yake yenye juisi ya mapera na kunywa.
"Hii kazi nitaitimiza mwenyewe Maloo. Niachie tu! Nyie tulieni."
"Aah! Masai acha zako kaka. Hawa si watu wa kuwapiga peke yako."
"Nimekwishapanga jinsi ya kuwadhibiti. Naomba nijaribu peke yangu. Kama ikitokea nimeshindwa, nitaomba msaada."
"Hapana Masai. Afadhali hata uwe na msaada na mtu mwingine. Hapo sawa."
"Okay. Nimekuelewa. Tutakuwa wote siku hiyo. Lakini naomba Lisa asijue hili. Tutafanya haya chinichini, yeye asikie tu! Tumewaadabisha."
"Hilo si tatizo kaka. Watakaa tu wajinga hao." Malocha alifurahi baada ya kualikwa kwenye vita ile ngumu.
"Jumamosi tutaenda kuwaona wakipiga muziki kule Buza. Halafu Jumamosi itakayofuata tutakuwa tumekwisha wasoma vema na kuelewa njia baadhi za kuwaangamiza bila kujulikana." Masai akaongea huku anamtazama Malocha.
"Hamna tatizo. We' ndiye kiongozi." Baada ya maongezi hayo, wakaanza habari nyingine ambazo zilikuwa zinawatoa mawazo mengine ya ajabu.
****
Siku zikapita na kwenda na hatimaye ikafika Jumamosi ambayo si Malocha au Masai ambao walikuwa hawana hamu ya kuiona. Walihisi kama usiku haufiki na hata pale usiku ulipofika, waliona kama gari lao haliendi haraka kule wanapotaka. Lakini hatimaye walifika katika baa ya Toxido ambayo ilijaa walevi wengi Jumamosi ile kwa sababu ya mwezi kuwa mwisho na hata watumbuizaji waliokuwepo siku hiyo.
"Kwa sasa Manguli Band ndio watapanda na kuanza kutumbuiza kabla ya wale watasha wetu hawajamaliza kazi yao kwa mziki mzito na wa kijanja." Mtangazaji mmoja alitangaza na wakati huo Manguli Band walikuwa wanajaribu vyombo vyao.
Malocha na Masai waliingia katika baa ile wakiwa wamependezea sana kwa suti zao za gharama. Masai kama kawaida hakuiacha suti yake japo ilikuwa haina sumu kama ya zamani. Wakaenda katika nafasi za nyuma na gizani, kisha wakajibweteka na kuagiza vinywaji vinavyowafaa.
"Sehemu nzuri sana hii. Inanikumbusha kipindi kile tupo sekondari." Malocha aliongea huku akifungua bia aina ya Castle na kuipitisha kinywani mwake. Masai naye hakuwa nyuma, dawa alizokuwa anameza, tayari zilikuwa zimekwisha mwilini, bia aina ya Tusker ikawa kama maji katika kinywa chake.
"Hahaaa. Ilikuwa hatari sana. Watu tulienjoy sana." Masai akaungana na Malocha huku akigida Tusker yake.
Manguli Band walishaanza kutumbuiza kwa nyimbo mbalimbali zilizoimbwa na magwiji wa muziki wa Tanzania wa kipindi hicho. Zilibadilishwa nyimbo mbalimbali za kuvutia na kupendeza na kila mtu aliyekuwepo pale alikuwa akitikisa kichwa kuonesha muziki ulikuwa unazama ndani ya medula zao.
"Hao ndio Manguli Band. Wametisha sanaa." Mtangazaji aliongea kwa mbwembwe baada ya Manguli kumaliza kazi yao waliyotumia masaa mawili. Ilikuwa ni raha kwa kila mtu aliyehudhuria hasa pale wale jamaa walipoleta wanawake waliovalia vimini vya kuwavutia wanaume. Baada ya kupanda watoto hao wa kike, walianza kujimenya na kujimenyua na kufanya watu waburudike mara mia zaidi.
Bia zilikuwa zikipita kwenda meza mbalimbali ikiwemo na ya wakina Malocha ambao tayari walishadondosha chupa sita kila mmoja.
"Na sasa ni ule muda ambao tulikuwa tunausubiri kwa muda mrefu. Wale tunaowaita Watasha, sasa wanapanda jukwaani kwa ajili ya kuleta burudani maridadi kutoka kwenye magita yao. Tuwapigie makofi jamani." Mtangazaji alizogoa hayo na kushuka katika kile kisehemu kidogo cha kutolea burudani. Wageni waliokuja kupata burudani hiyo walikuwa wakipiga makofi kwa pamoja lakini mioyo ya Malocha na Masai ilikuwa ikiwadunda huku wakiwa kama hawaamini kile wanachokifikiria.
"Yawezekana si PITRI hawa. Ni vipi waamue kupiga muziki kwenye mabaa? Ni kufulia au?" Malocha alionesha wasiwasi wake kuhusu Pinto na Trina.
"Ni wenyewe Maloo. Wanafanya hivi kuvuta muda tu. Na nahisi kuna kitu hiku Buza wanakifatilia. Tutakijua tu." Masai aliongea kwa makini huku akitazama huku na huko kuona kama watu wao wataingia.
Wakati macho ya wengi yakiwa yanajiandaa na kwa ajili ya sura za Wazungu wale, mara walisikia mlipuko mmoja mdogo wa fataki zilizopaa juu na kulipuka tena huko. Watu wakatazama juu kushuhudia mambo mazuri wanayopewa hasa kwa sababu baa ile ilikuwa haina uzio wa juu ambao utawafanya wasione mazuri hayo. Baada ya fataki, moshi mdogo ukaanza kutokea katika jukwaa ambalo wazungu wale walikuwa wanapanga kuingilia.
Ndani ya moshi ule kwa mbali wakaanza kuonekana watu wawili wakiwa wameshika magitaa makubwa. Sekunde kadhaa, moshi ule ulititia na wazungu wawili wenye miili midogo wakaonekana mbele ya macho ya watazamaji. Shangwe la nguvu likapigwa na watu karibu wote kasoro Malocha na Masai ambao walikuwa wanazitathimini kwa kina sura zile.
"Mbona kama si wale?" Malocha alianza kuuliza.
"Ni wenyewe. Angalia nywele na miili yao. Ni uso tu ndio wamebadili ili wasijulikane na watu au usalama." Masai alijibu huku akiwakazia macho wale wazungu.
"Waone walivyo. Kama watu wema, kumbe ni majoka makubwa yanayobugia na kutafuna kabla hayajameza." Malocha aliongea na kupeleka maongezi yake na mfyonzo mrefu.
Pinto na Trina walianza kupiga magitaa yao kwa utaalam na kufanya wapenzi wa burudani wanyanyuke na kuwatuza pesa mbalimbali kutokana na shughuli yao. Walikuwa wanafanya muziki wa Rock ambao kwa Tanzania hakuna anayediriki hata kuugusa kwa sababu ya sifa zake, hasa uvutaji madawa ya kulevya na kuabudu ushetani.
Baada ya magitaa kupigwa kwa dakika zipatazo kumi na tano, Pinto alishusha gitaa na kwenda kwenye ngoma zilizoandaliwa kwa ajili yao. Kilichofuata hapo ni muziki uliorusha nyoyo za wananchi wengi waliofika pale.
Pinto akipiga ngoma, Trina akilikamua gitaa na kuimba kwa fujo, ni nani ambaye angekaa? Ilikuwa ni mshikemshike.
****
Nusu saa mbele, Trina akabaki mbele ya wahuzuriaji akiburudisha kwa gitaa taratibu na kuimba nyimbo zinazogusa hisia. Pinto akamuacha mchumba wake na kwenda katika chumba kimoja kwa ajili ya kujisaidia.
"Malocha." Masai akaita kwa ulevi.
"Sema Kamanda langu." Malocha akaitika huku kalegea asijue hata ni nini kinaendelea. Pombe zilishamkamata kichwa.
"Naenda msalani Kamanda. Nisubiri." Masai akampa taarifa Malocha ambaye alimruhusu bila shida.
Kwa kupepesuka, Masai akanyoosha hadi kwenye chumba ambacho hutumika kama choo pale baa. Na ndipo huko Pinto alipoelekea.
Masai alipofika katika mlango wa choo kile, aliangalia huku na huko kisha akaufungua kwa kitasa chake na kuingia ndani huku sura yake ikibadilika na kuwa sura yenye uchu na kitu na si tena ya kilevi. Akafunga mlango wa choo kile, kisha akatoa funguo malaya iwezayo kufunga na kufungua vitasa na makufuri karibu yote ya duniani. Akaufunga mlango ule kwa ndani na kisha akaangaza huku na huko kuona kama kuna watu. Hakuona chochote zaidi ya maji yaliyokuwa yanamwagika mlango fulani uliomo mle uwani.
Masai akaupita ule mlango bila sauti yake ya viatu kutoka, akaenda sehemu ambayo wanaume hujisaidia kwa pamoja. Akaanza kufanya yake.
Wakati anajisaidia, alisikia ule mlango wa kile choo cha ndani ukifunguliwa. Akafunga zipu yake na kunawa mikono kisha akaenda ulipo mlango wa kutokea. Hapo alimkuta Pinto akihangaika kuufungua ule mlango na kutokana na kelele zilizokuwa zinaendelea nje, hakusikika purukushani zake za kuufungua.
"Can I help you? (Nikusaidie?)" Masai akimuuliza Pinto akiwa nyuma yake. Pinto akageuka haraka na kumuangalia aliyeongea hayo. Macho yakamtoka kama kakabwa na kiazi kitamu au anapoteza hewa ya Oksijeni
ITAENDELEA
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU
Masai akaupita ule mlango bila sauti yake ya viatu kutoka, akaenda sehemu ambayo wanaume hujisaidia kwa pamoja. Akaanza kufanya yake.
Wakati anajisaidia, alisikia ule mlango wa kile choo cha ndani ukifunguliwa. Akafunga zipu yake na kunawa mikono kisha akaenda ulipo mlango wa kutokea. Hapo alimkuta Pinto akihangaika kuufungua ule mlango na kutokana na kelele zilizokuwa zinaendelea nje, hakusikika purukushani zake za kuufungua.
"Can I help you? (Nikusaidie?)" Masai akimuuliza Pinto akiwa nyuma yake. Pinto akageuka haraka na kumuangalia aliyeongea hayo. Macho yakamtoka kama kakabwa na kiazi kitamu au anapoteza hewa ya Oksijeni.
"Can I help you Pinto." Masai akamuuliza tena huku akimtaja jina lake.
Katika hali ya kushtukiza, kwenye mkono wa koti la Pinto, ikachomoka bastola ndefu sababu ya kufungwa kiwambo cha sauti. Mtoto wa kiume akaifyatua haraka, lakini Masai alikwishasoma kila mchezo. Alijibiringa kiustadi kweye sakafu ile na wakati huo Pinto alikuwa anahaha kumshambulia na bastola yake.
Masai akawa mtu wa kwenda kulia na kushoto na mwisho wake ulikuwa mtama mzito aliomlisha Pinto na kumbwaga. Bastola ya kijana yule ikadondoka na Masai akaimalizia kwa kuipigia mbali na pale. Wote wakiwa chini wakaangaliana kwa macho ya kutamaniana.
Pinto akawa wa kwanza kumvamia Masai kwa kurusha teke la chini kwa chini ambalo Masai alilikwepa na kwa ustadi akarusha lake lililompata Pinto kifuani na kumsogeza hadi kwenye mlango wa kutokea. Pinto akafunua suruali yake kwenye mguu wa kulia, akachomoa bastola nyingine fupi lakini Masai alishawahi kufika na wakati Pinto ananyoosha mkono wake kumlenga mwanaume yule, alikutana na teke lililopiga mkono wake na kuifanya bastola ile nayo kudondokea mbali kabisa ba yeye.
Akiwa haamini kama yale anafanyiwa yeye tena na ngozi nyeusi, akajikuta akipokea teke lingine zito la shavu na kumfanya atokwe na damu mdomoni.
Ulikuwa ni mpambano wa kimyakimya na wakati huo shangwe ziliendelea kuongezeka nje ya maliwato ile ambayo kulikuwa hakuna wateja walishughulika kuingia.
Pinto akamtazama Masai kwa jicho la kithirani hasa kwa anachofanyiwa. Lakini jicho hilo halikumaanisha ndio aogopwe na adui yake bali kuendelea kuvamiwa. Masai akasogea na kurusha teke lingine kama anaye piga mpira, hapo Pinto akadaka teke hilo na kujizungusha chinichini na kuukata mguu wa Masai uliokuwa umesimama.
Frank Masai akadondokea mgongo na kwa wepesi wa hali ya juu, Pinto akaruka kama mwenye kuogolea baharini, kichwa kizito kikatua kwenye kidevu cha Masai. Pinto akazidi kumchanganya adui yake. Akarusha ngumi kwa mkono wa kulia, ikakita kwenye shavu la Masai. Akatupa ngumi nyingine ya kushoto, ikatua pia kwenye shavu. Ngumi ya mwisho akaitupa na kutua kwenye paji la uso wa Masai. Mtoto wa kiume akakubali ngumi hizo zititie mwilini bila shida.
Pinto akajibetua kwenda mbele na kusimama wima wakati Masai akiwa anasikilizia maumivu wa ngumi zilizorushwa na Pinto.
Kwa kasi, Pinto akamfata adui yake na kutupa teke ambalo Masai alilizuia kwa kuweka mikono miwili usoni kwake. Alipohakikisha kuwa kazuia, akajiachia kwa nguvu toka pale chini na kumkumba Pinto maeneo ya tumboni kwa kutumia bega lake.
Mkumbo huo ukamfanya amsukume kijana yule na kuuvunja mlango wa choo kimojawapo kati ya vinne vilivyomo mle. Pinto akalegea kwa pigo lile na Masai akaamua kuukamata mchezo. Akashika nywele laini za boya yule na kusukuma kichwa chake hadi.kwenye ukuta wa marumaru na kukigosha hapo mara tatu.
Alipomgeuza Pinto, alikuwa anavuja damu puani na mdomoni. Masai akakwida koti la Pinto na kuubamiza mgongo wake ukutani na kijana yule alikubali yote bila kubisha.
Baada ya kumgonga mara kadhaa ukutani, Masai akaanza kukandamiza ngumi nzito katika tumbo la Pinto na mwisho akapiga ngumi ya nguvu kwenye koo la kijana yule na kulivunja hapohapo. Pinto akawa anashuka chini huku macho yako kayatoa pima kama mgonjwa wa Pumu. Masai akawa kammaliza muuaji wa kimataifa ambaye hajawahi kushindwa vita na mapambano dhidi ya adui yake.
Akamvuta Pinto hadi choo kingine na kumtupia huko kisha akaufunga mlango ule kwa funguo yake malaya. Akaenda kwenye sinki la maji, akanawa damu zilizokuwepo mikononi kwake na zile zinazomtoka puani. Akatoa kitambaa mfukoni na kujifuta, kisha akauendea mlango wa kutokea.
"Nyie mnajifungia humu mnadhani choo chenu hichi." Jamaa mmoja mlevi alilalama huku anaingia msalani akionesha wazi haja ilimbana. Masai hakutaka maneno naye, akaenda hadi alipo Malocha.
"Oyaa. Utaibwa wewe." Masai aliongea kilevi huku anamtikisa Malocha aliyekuwa kalalia meza na kubebwa na usingizi.
"Aaah! Upo Kamanda. Naona mabwege wanaendelea kuburudisha." Malocha aliongea huku akitazama mbele bila kuangalia uso wa Masai ambao ulikuwa umevimba kiasi.
"Ndiyo maana yake. Naona binti anafanya makubwa pale." Masai akajibu huku naye akimtazama Trina kwa makini. Tayari zilikwisha katika dakika ishirini bila Trina kumuona Pinto, macho yake yakawa yanaangaza huku na huko bila mafanikio ya kumuona mpenzi wake. Masai aliona hali ambayo Trina anayo, akatabasamu baada ya kugundua kuwa atakamilisha lengo lake muda si mrefu.
"Ila naona kimpenzi chake kimechepuka, hakirudi." Malocha aliongea na kumfanya Masai kutabasamu bila kujibu chochote.
"Asanteni sana jamani. Na usiku mwema kwenu." Trina alisikika kwenye kipaza sauti akiongea Kiswahili kwa shida. Akakamata gitaa lake na la mpenzi wake na kuingia chumba walichotokea mwanzo.
"Kaka. Ngoja nikachukue vinywaji tena. Hapa hakuna kulala." Masai alimwambia Malocha na bila kupinga, Malocha akamuacha rafiki yake afanye anachokifanya. Masai kwa kuyumbayumba, akajidai mwenye kukosea njia na moja kwa moja akanyoosha kwenye kile chumba alichoingia Trina.
Akamkuta Trina ambaye kampa mgongo anapanga gitaa lake kwenye begi maalumu la kubebea kifaa kile. Masai hakumshtua bali kumpita na kwenda sehemu moja alipovuta kiti na kwenda nacho hadi mbele ya Trina.
"Hey beautiful. (Halo Mrembo)" Masai akamsalimia Trina ambaye aliinua kichwa chake na kumtazama yule aliyemsalimia. Macho ya Trina yakawa kama yale ya Pinto alipomuona Masai kule msalani.
"Pinto hatunaye duniani. Ukifanikiwa kuniua, utasikia kifo chake redioni na utaona kwenye matv. Usiponiua, basi utakutana naye jehanamu." Masai akaongea huku hamtizami adui yake. Ni kama alikuwa anamdharau kwa jinsi alivyokuwa analeta mbwembwe.
Trina akiwa kapagawa kwa taarifa zile, akafungua gitaa lake lililofunguka kama yale mabegi ya chuma ya wanafunzi wa bweni. Ndani ya gitaa, Trina akachomoka na mapanga mawili ambayo alimfata nayo Masai na kuanza kujaribu kumkata.
Masai akawa mwepesi wa kuruka na kukwepa hatari ile. Mwanamke wa shoka hakuchoka katika kujaribu kumsambaratisha adui yake. Akawa anajaribu kumfyeka Masai kichwa chake lakini anaambulia patupu.
Masai akatulia na kuangalia mwendo wa Trina jinsi anavyotupa mapanga yake, ndipo na yeye akasubiri mtupo fulani wa msichana yule, alipouona unakuja akakwepa tena kidogo na kisha akarusha ngumi iliyopita katikati ya mikono ya Trina na kutua puani. Kwa haraka, akapiga teke panga la kwanza na kudondoka. Trina katika mshangao, akajikuta akipoteza panga lingine lililoporwa kwa ustadi na Masai.
Mwanaume akatupa pembeni panga lile na sasa uso wa Trina ulikuwa katika mapambano ya ana kwa ana.
Mwanamke yule akaruka teke, na wakati yupo angani, kisu fulani kikachomoka kwenye kiatu chake na kwa ghafla, akakirusha na kutua kifuani kwa Masai tena upande ule wa suti uliokwisha. Kisu kile kikachana suti ya Masai lakini hakikumdhuru.
Wakati Masai anashangaa uwezo wa ajabu wa yule dada, akajisahau kuwa alikuwa karukiwa teke. Akakutwa na teke hilo palepale ambapo kisu kimechana. Endapo kama kisu kingezama pale, basi teke lile lingezamisha zaidi. Masai akadondoka chini na sura yake ikakumbwa na hamaniko kubwa kwa pigo lile la kijinga.
Trina akaikuna miguu yake, na viatu vyake vikatengeneza nyayo zenye vyuma vyenye ncha kali. Akamfata Masai ambaye alikuwa chini na hatambui kama viatu vya adui yake vimebadilika. Teke likatoka kwenye mguu wa Trina, Masai akajaribu kulizuia kwa mkono, matokeo yake ilikuwa suti yake kuchanwa katika mkono huo na ngozi yake ya mwili kiasi ikakwanguliwa.
"Hapa umekutana na nyoka, mbwa wee." Trina aliongea kiitaliano na kumfuata adui yake na kutaka kumkanyaga mkono wake, lakini akakosa mkanyago huo baada ya Masai kuutoa haraka pale sakafuni.
Trina akageuza kibao kwa kurusha teke la mguu mwingine ambalo nalo Masai alilikwepa kwa kujivilinga sarakasi ya kinyume huku akiwa bado chini. Haraka Trina, akachomoka na kuruka juu tayari kwa kumkanyaga Masai kwa viatu vyake vyenye vyuma. Kidume akabiringita tena upande wa kushoto na kisha akasimama na kumtazama Trina aliyegeuza shingo yake na kukutana na uso wa mwanaume wa shoka ukitabasamu tabasamu la mauaji.
"You are going down, you Monkey. (Unadondoka/ Nakudondosha nyani wewe)" Trina akamkashifu Masai kwa kumuita nyani kwa sababu ya rangi yake nyeusi.
"Monkey’s fighting with pig. Guess what? ( Nyani anapigana na nguruwe. Otea nini)" Masai naye akajibu kashfa huku akitabasamu tabasamu la upande mmoja wa mdomo wake.
Trina akaacha maongezi na kujitoma kwenye mpambano kwa kasi ya ajabu. Mateke aliyokuwa anayaruka, hayakuwa ya kitoto. Alijizungusha na kumpiga Masai mateke karibu matano bila majibu. Mtoto wa kike akisimama wima na kumuangalia mtu anayepigana naye kama anaweza kunyanyuka kwa kichapo kile.
Masai akapiga ngumi sakafu kuonesha kachukia kile kitendo cha Trina kumgonga vile. Akainuka haraka na kwenda alipo Trina aliyezidi kumuadabisha yule mwanaume kwa kumtuliza kwa teke la kifua na baada ya hapo akamaliza kwa teke lingine lililomsababishia Masai kuchubuka kifuani sababu ya vile viatu vyenye ncha kali chini yake.
Trina akatabasamu baada ya kuona mtoto wa kiume anatiririka damu. Akamfuata Masai pale chini alipokuwa kapiga goti moja, akarusha teke ambalo alilenga kumpiga kidevuni, lakini Masai tayari alikuwa amesoma mwenendo mzima wa pigo lile. Akakwepa kwa kurudisha kichwa chake nyuma na teke lile likapiga hewa.
Katika hali ambayo Trina hakuitegemea, akajikuta tayari imemkumba kwa yeye kudondoka. chini baada ya mtama mzito toka kwa mwanaume wa shoka, Frank Masai. Akiwa katika taharuki ya mtama mzito wa Masai, Trina anapokea teke lingine la mdomo akiwa bado palepale chini.
Masai anajibetua kwenda mbele na kusimama wima na wakati huo muziki wa kawaida toka kwa DJ wa kilabu kile, ulikuwa unazidi kupamba moto huko nje hata wasisikie purupushani kati ya Trina na Masai.
Trina anapitisha kidole kwenye mdomo wake, anachota damu inayomtoka. Anaiangalia kwa macho makali, kisha anamtazama Masai aliyesimama wima huku kakunja ngumi tayari kwa kumngoja yule mwanamke asimame. Trina analamba ile damu, huku anamtazama Masai kwa macho ya shari pekee. Baada ya kuonja utamu wa damu yake, sasa anakuwa kama kapagawa. Anaruka sarakasi ya chinichini hadi karibu na Masai. Anataka kumkata mtama, lakini kidume anakwepa kwa kuruka kidogo juu. Akiwa juu, Trina anajibetua kwa makini na kumtandandika teke la tumbo mwanaume. Masai anasogezwa nyuma kidogo lakini hadhuriki na teke lile japo limesheheni vyuma vya hatari chini yake.
Trina hamuachi Masai, anaruka mtupu na kusogea alipo adui yake na kuanza kurusha ngumi kadha wa kadha zilizokuwa zinamsambaratisha Masai ambaye alishachoka kwa sababu ya mapigano yake na Pinto pamoja na kuchanwa kifuani. Trina anamiliki mpambano na hali ya ushindi inaanza kunukia hasa pale Masai alipokuwa hafanyi lolote kuzuia mapigo ya Trina.
Ngumi kali ya kummaliza Masai, Trina anaivutia toka mbali na kuipeleka kwa kasi kwenda kwenye uso wa Masai. Lakini bahati inakuwa si yake baada ya Masai kukwepa na ngumi ile kugonga ukuta mgumu uliyojengwa kwa theruji bora ya twiga.
Trina anajikuta akiumia mkono wake wa mapambano na Masai halazi damu baada ya kuona hayo. Anamtandika ngumi ya shavu binti yule, kabla hajafikiria kujibu mapigo, kidume anarusha ngumi nyingine kali inayokita puani kwa mtoto mzuri Trina na kumsogeza mbali na pale. Trina anahisi hali kuwa mbaya, anajaribu kutupa ngumi yake ambayo haijaumia, Masai anaidaka vema, kisha anaunyonga mkono ule kwa nguvu zake zote na kuuvunja. Trina analia kama mtoto wa kitanzania kanyimwa titi. Au kama mbwa kapigwa kwa jiwe la mbavu.
Masai anamgeuza Trina na kuzidi kuunyonga mkono ule nyuma ya mgongo wake na kusababisha maumivu kwa Trina.
Kwa kasi, anamsukumia Trina ukutani, mtoto wa kike anajigonga paji la uso na kifua chake. Anaachiwa mkono wake, na Masai anaanza kumpiga ngumi nzito ubavu kwa ubavu. Trina analegea kama denda la tahira akiwa bado anautazama ukuta.
ITAENDELEA
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE
Masai anamgeuza Trina na kuzidi kuunyonga mkono ule nyuma ya mgongo wake na kusababisha maumivu kwa Trina.
Kwa kasi, anamsukumia Trina ukutani, mtoto wa kike anajigonga paji la uso na kifua chake. Anaachiwa mkono wake, na Masai anaanza kumpiga ngumi nzito ubavu kwa ubavu. Trina analegea kama denda la tahira akiwa bado anautazama ukuta.
Baada ya ngumi nyingi, Masai anampiga binti yule nyuma ya magoti, Trina anasaliti amri mwenyewe na kujikuta anapiga magoti huku bado anatazama ukuta na akiwa kalegea kwa kichapo kikali. Masai anamuacha Trina pale alipopiga magoti ya kwenda kwenye gitaa la binti yule alilolikuta wazi. Akapekuwa na kutoa kisu aina ya mundu. Kisu hicho ni sawa na kile kinachotumika kukatia majani ya mifugo sema alichokamata Masai ni kikali na kinatisha hata kwa kukitazama.
"Auae kwa upanga, hufa kwa upanga." Masai aliongea maneno hayo kwa lugha ya Kiitaliano ambayo Trina ilimuingia vema ubongoni. Masai akamgeuza Trina, na wakawa wanatazamana.
"Umeshinda mbwa wewe." Trina aliongea kwa shida huku damu zikimtoka puani na mdomoni.
"Sijawahi kushindwa hata mara moja." Masai akamjibu Trina.
"Utashindwa tu! Siku moja." Trina alitoa maneno ambayo yalimfanya Masai acheke kidogo.
"If I will loose, I will die trying. Just like what I did to you suckers. (Kama nitashindwa, nitajaribu hadi nife. Kama nilivyofanya kwa nyie wajinga)" Masai aliongea huku akipita nyuma ya Trina na kusimama mgongoni kwake.
"One day we will meet again Masai (Siku moja tutakutana tena Masai)" Trina aliongea akiwa tayari kukipokea kifo chake. Masai akamziba Trina mdomo kwa mkono na kuweka ile mundu shingoni kwa binti yule.
"Sehemu yako ni kuzimu baada ya hapa, na mimi ni paradiso. Vipi tutakutana? Msalimie Lusifa. Mwambie kuna zaidi yake huku duniani lakini hayupo upande wake. Nendeni mkazae muongezeke huko kuzimu, wewe na Pinto." Masai akapitisha mundu ile kwenye shingo ya Trina na damu zikaruka na kuchafua ukuta. Trina akaachiwa mwili wake na kudondoka mzima mzima kama kigunia cha mapera.
Mwanaume akawa kamaliza kazi nzito iliyotaka kugharimu maisha yake. Akatoka mle ndani kwa makini, kisha akapitiliza hadi maliwato ambapo alinawa mikono yake vema na kwenda kwenye meza aliyomuacha Malocha.
"Oya kaka. Duuuh! Umezima." Masai aliongea huku akimtikisa rafiki yake. Alichukua dakika kama kumi na nane kupambana na Trina, lakini kwa Malocha aliona kama dakika tatu tu sababu ya pombe ambazo alibwia siku hiyo.
"Aaagh. Umeleta nyingine tayari." Malocha aliongea huku akitikisa chupa za pombe zilizopo mezani.
"Twende nyumbani kaka. Umekunywa sana." Masai alimwambia Malocha huku akijaribu kumnyanyua pale alipokuwa kakaa. Malocha akanyanyuka huku akibeua beua hovyo kama mbuzi aliyeshiba majani na maji. Masai akaweka mkono wa Malocha begani kwake na kuanza kutoka naye kwenye kile kilabu.
"Aaah! Kaka. Umekuja kuwaona wale Watasha." Jamaa wa bodaboda alitokea mbele ya Masai na kwa furaha akamuuliza.
"Nimeonana nao wote. Kesho utapata taarifa njema sana." Masai akajibu huku katabasamu.
"Naisubiri hiyo asubuhi maana si kesho tena, hii tayari ni siku mpya." Jamaa yule aliongea huku akijitahidi kuelewesha majira na mabadiliko yake. Ilikuwa ni saa nane usiku muda huo walipokutana.
"Okay. Asubuhi njoo hapa utakuta taarifa njema." Masai aliongea na kumkokota Malocha hadi lilipo gari lao. Akampandisha rafiki yake na kuondoka eneo lile huku huko ndani ya kilabu kukiendelea kuwashwa moto wa burudani.
****
"Masai, Masai, Masai." Sauti ya Mubah iliita nje ya chumba cha Malocha aliyelala na Masai siku hiyo. Masai na Malocha wote wakaamka na kutazama saa. Ilikuwa ni saa nne asubuhi. Sauti ya Mubah iliendelea kuita pale mlangoni.
"Nini wewe." Malocha aling'aka kwa hasira.
"Pinto na Trina." Mubah akajibu na kufanya kimya kitawale baina yake na Malocha.
"Wamefanyaje?" Malocha ikabidi aulize kile ambacho Mubah alipaswa kukimalizia.
"Wamekutwa wameuawa Toxido Bar." Baada ya maneno hayo ya Mubah, Malocha akamuangalia Masai. Masai akaangalia pembeni na kujifanya anapiga mhayo mrefu.
Malocha akampiga kofi zito la kisogoni rafiki yake. "Wewe ndio umewaua?" Swali la ukali likatoka kwa sauti toka kinywani kwa Malocha.
"Si mimi mkuu. Wametangaza kuwa kuna alama za vidole vya Masai ndivyo walivyovikuta katika kila mwili." Mubah alijibu kana kwamba yeye ndiye aliyeulizwa.
"Sikuulizi wewe pumbavu. Embu toka hapo mlangoni." Malocha akafoka na kumfanya Mubah aondoke.
"Sasa kwa nini hukunishirikisha?" Malocha akamuuliza Masai.
"Ungeweza na pombe zako ulizokuwa umezimimina?" Masai akamjibu kwa swali huku akivua nguo alizokuwa nazo na mara kifuani Malocha akaona kidonda alichojeruhiwa rafiki yake. Akayafikiria maneno yale ya Masai, akaona yana ukweli ndani yake hasa kwa jinsi Masai alivyokuwa. Kavimba na kuchoka japo si kawaida yake hata anywe pombe chupa mia.
"Lakini si ulisema tutafanya Jumamosi ijayo?"
"Zege halilali bro. Sina muda wa kuwaremba maadui." Masai akajibu huku anavaa singlendi fulani yenye rangi nyekundu. "Pia sikutaka kukuingiza matatizoni hadi alama zako zionekane kwenye miili ya wale wajinga." Masai akamaliza.
"Daaah! Sasa uliwezaje kuwaua?" Malocha akauliza na Masai akampa hadithi nzima ilivyokuwa. "Mmmh! Naishi na gaidi bila kujua." Malocha akaongea kwa utani na kunyanyuka pale kitandani. Wakavaa nguo za mazoezi na kutoka chumbani.
"Baby." Lisa alimkimbilia Masai na kumkumbatia.
"Wenye baby wao hao." Malocha akatania huku akiwapita Masai na Lisa waliokumbatiana.
"Jibebe au jikumbatie mwenyewe." Mubah hakuwa nyuma kumshushua bosi wake.
"Umeona eeh Mubah." Lisa akaongea huku akitoka mwilini kwa Masai.
"Halafu mnatakiwa kuwa na wapenzi nyie wajinga. Mmekaa humu kama mazuzu. Hasa we' Malocha." Masai alitania na wote wakacheka.
"Pole sana." Lisa alimpa pole mpenzi wake na kisha kwenda kuchukua vifaa vya huduma ya kwanza na mara moja huduma ikaanza.
****
"Mjinga kawamaliza wale wajinga." Gunner aliongea huku akiwa na kundi lake.
"Walikosea mara ya kwanza walipomkosa. Hawakumjua Masai, walidhani wanapambana na kibabu kizee." Lobo aliongea huku safari hii akiifuta bastola yake nyeusi kwa kitambaa chenye mafuta ya breki.
"Mmh! We Lobo mbona unamsifia sana Masai." Ikabidi Gunner aulize maana alishachoshwa na ile hali ya Lobo kumsifia Masai.
"Kwa sababu anajua anachokifanya. Ni mimi pekee ndiye naweza kupambana naye na si wale wajinga wa kumendea." Lobo alisindikiza maneno hayo kwa kuikoki bastola yake.
"Mmh! Alishakuua yule, leo unajidai mjanja."
"Hakuniua. Alifanya vile sababu sikuwa namjua vema. Sasa hivi namjua vizuri. Nimeshamsoma adui yangu, sasa ajiandae tu." Lobo aliongea kwa kujiamini.
"Tutaona." Gunner akaongea na kukaa sawa kochini kwake.
"Shadow akipiga simu, mwambie tunahitaji ile bidhaa ya Malaysia." Lobo akatoa ombi kwenda kwa Gunner. Akiwa anajiandaa kujibu, simu yake ikaita kwa namba nyingine tofauti kabisa na zile ambazo alizoea kupigiwa nazo. Kifupi hakuwahi kuziona namba zile. Akajua huyo ni The Shadow lakini yupo nchi nyingine tofauti na ile aliyompigia hapo nyuma.
"Haloo." Gunner akapokea na kuita.
"Nadhani mmepata taarifa za Pinto na Trina." Sauti nyembamba ilisikika. Ni tofauti na ile ambayo aliongea nayo mara ya mwisho ambayo ilikuwa nene kama kanda ya redio inayoliwa.
"Ndiyo mkuu." Gunner akajibu kwa heshima zote.
"Sasa nalaumiwa huku na baadhi ya wajinga kwa kitendo cha huyo mbwa mmoja. Nataka ndani ya wiki mbili kuanzia sasa, muue wote hao. Mkianza na Masai." The Shadow akatoa majukumu mengine kwa kundi la Gunner. Gunner akatabasamu na kumuangalia Lobo.
"Usijali mkuu."
"Mnataka nini niwaongezee." The Shadow akauliza.
"Malaysia na wanawake wa Iran watano." Gunner akajibu.
"Imepita. Kesho kawapokee burundi. Huko mtapata magari yatakayowarudisha Tanzania." Maneno hayo yakawa ya mwisho kwa The Shadow. Simu ikakatwa.
"Back in business. (Tunarudi biasharani)" Gunner aliongea kwa tabasamu huku akimuangalia Lobo, na Lobo naye akakita risasi kwenye bastola yake na kuifanya ilie mlio wa kuwa tayari kwa kazi.
****
Kesho yake Gunner na Lobo walichukua ndege ya kukodi ambayo iliwapeleka hadi uwanja fulani wa vumbi uliopo Burundi.
Baada ya kushuka toka kwenye ndege hiyo, gari ya kizamani kabisa ilitokea nyuma ya ndege ile. Ilikuwa Land Rover One Ten toleo la kwanza la Muingereza.
"Naitwa Buyangi Mukundilii. Mimi ndiye nitawafikisha mpatakapo." Dereva wa gari aliongea huku akiwapokea mizigo Lobo na Gunner na kuitupa siti za nyuma ambazo zilikuwa hazina makwisheni. "Mtakaa huku nyie." Buyangi aliongea harakaharaka na kuwafungulia mlango ambao aliung'oa tu na wakina Lobo wakaingia kisha jamaa yule msanii, akaupachika tena mlango wake na safari ndefu ikaanza.
"Hapo ndipo nilipoambiwa niwalete." Buyangi aliwapa taarifa wageni wake huku akiwaonesha kiwanda ambacho hakitumiwi. Kilijengwa kwa mabati kwa asilimia zote.
Buyangi, akatoka nje ya gari lake na kufungua mlango kwa njia ileile ya mwanzo. Lobo na Gunner wakatoka na kupewa mikoba yao.
"Asante Mkuu." Gunner akashukuru na Buyangi akaondoka eneo lile.
Wakapiga hatua zipatazo kumi kwenda kwenye jengo lile lakini walipotaka kusogea mbele zaidi, risasi kadhaa zikapigwa chini, mbele ya miguu yao na kuwafanya wasimame.
"Nyie ni nini na mwataka nani." Sauti ya kike iliuliza lakini hakuoneka ni wapi alipo.
"Gunner, Lobo. Toka kwa The Shadow." Baada ya maneno hayo ya Lobo, kwenye kichaka kimoja akatokea kwanamke mrefu na mwembaba huku begani kabeba SMG akawafuata wageni wale waliposimama.
Akawatazama usoni kwa sekunde, kisha akapiga makofi matatu. Hapo akashuka mwanamke mmoja toka mtini ambaye kavaa kajani na kumfanya aonekane naye kama mti. Mkononi alikuwa kakamata sniper rifle, bunduki maalumu kwa wadunguaji.
Mwanamke mwingine akatokea nyuma ya wakina Gunner naye kabeba SMG. Lakini wote walikuwa Warundi.
"Twendeni huku." Yule wa kwanza kujitokeza akawa mbele yao kuwaongoza wote. Gunner akatazama makalio ya yule mwanamke na kumbonyeza Lobo ambaye alitabasamu bila kusema chochote.
"Mkiendelesa huo upumbafu wenu, natwanga mashine zenu bullet." Mwanamke yule alichimba mkwara ambao ulifanya Gunner atengeneze picha wakati anapigwa risasi nyeti zake. Akajikuta anazikamata.
Ndani ya jengo lile, walikuta wanawake watano wamevalia majuba meusi na kuvaa shungi zilizozunguka nyuso zao vema. Walikuwa ni warembo kwa kuwaangalia, ila walichotumwa kukifanya, urembo wao usingeuona.
Gunner na Lobo wakasimama upande wa meza moja ndefu na hapo mwanamke mmoja wa Kiiran, akasukuma mkoba (briefcase) ikawaendea wale jamaa wawili, yaani Lobo na Gunner.
Wakafungua ule mkoba kwa namba maalumu ambazo walikuwa nazo toka Tanzania. Mkoba ukafunguka na macho yao yakatua kwenye vibanio kumi. Ni sawa na kibanio alichopewa Martina katika siku yake ya kuzaliwa, na ni kilekile kilichotema sumu kwa Mubah.
Gunner akatabasamu na Lobo akakenua kwa kazi ambayo waliitazama mbele yao. Kumuangamiza Masai tu.
"Good Job (kazi nzuri)" Lobo akatamka na wanawake wote wakatabasamu.
Mlango walioingilia, ukafungwa na kufunguka mlango mwingine ambao waliambiwa waende huko pamoja na wasichana wao waliowaomba kwa The Shadow. Huko wakakuta gari sita za kifahari zikiwasubiri. Lobo na Gunner wakapanda gari moja, na wale wanawake wa Iran, wakapanda kila mmoja ya kwake lakini wakaiweka katikati gari walilopanda wakina Gunner. Safari ya kwenda Tanzania, ikachukua nafasi yake.
Ni kama msafara wa matajiri wa mafuta wakikatisha jangwani kwa jinsi vumbi lilivyokuwa linatimka kutokana na gari zile za bei mbaya kwenda mwendo wa kasi kupindukia.
Zilipita katika barabara ya vumbi ambayo haina watu wengi na baadaye gari zile zikaingia kwenye mpaka wa Uganda ambapo ndipo walipopanga kuingilia kwa sababu ya kufupisha safari yao ya kuja Tanzania.
Mpakani hawakukukaa sana kwa sababu wale wa mpakani walikwishapata taarifa za ujio ule. Wakawapa na msaada hadi kwenye mpaka wa kuingilia Tanzania uliopo Kagera. Huko pia hawakupata shida ya kuvuka mpakani, wakachukuliwa tena hadi Bukoba ambapo walipata meli kubwa iliyobeba na magari yao. Meli hiyo ikawasukuma hadi Mwanza kupitia Ziwa Victoria. Ziwa linalosifika kutoa samaki watamu wa Sato.
"Ni Mwanza hii Lobo. Tuanzie kazi hapa au twende tukaanzie Dar es Salaam." Gunner alimuuliza John Lobo ambaye muda mwingi alikuwa akiutumia kutazama maajabu ya jiji lile tajiri kwa mawe.
"Hapahapa ndipo pa kuwapa taarifa wale wajinga. Lazima wajue kuwa Duka La Roho limerudi kuuza na kununua tu!" Lobo alijibu huku uso wake ukionesha chuki isiyo na kifani.
"Watakaa tu." Gunner akampa tano Lobo na wote wakashuka toka katika gari lao na kuwaamuru na wale wanawake washuke kwa sababu walikuwa wamefika katika hoteli moja kubwa na ya kisasa iliyopo Jijini Mwanza.
ITAENDELEA
 
Ukiona kimya jua imeisha story ka hii
Unaposifiwa usijisahau kutekeleza wajibu kwa kulewa sifa kwani ukifanya hivyo kitakachofuata ni kuharibu hata yale mazuri uliyoyafanya
 
Ukiona kimya jua imeisha story ka hii
Unaposifiwa usijisahau kutekeleza wajibu kwa kulewa sifa kwani ukifanya hivyo kitakachofuata ni kuharibu hata yale mazuri uliyoyafanya
mkuu kuwa mpole niliahidi utapata mpaka mwisho na pia kumbuka kila mtu ana majukumu kaka so ukiona sijaweka on time jua nimetingwa na ninajitahd sana kutoa update
 
mkuu kuwa mpole niliahidi utapata mpaka mwisho na pia kumbuka kila mtu ana majukumu kaka so ukiona sijaweka on time jua nimetingwa na ninajitahd sana kutoa update
Anayejidai hataki jambo, yawezekana analipenda ila analikataa kinafiki
Mkuu umetoka mafichoni!! hahaha
 
DUKA LA ROHO
SEHEMU YA PILI

Ndani ya nyambizi ile, kulikuwa kuna pilika za hapa na pale hasa wale mafundi mitambo wanaongoza chombo kile maalumu kwa ajili ya kazi za kijeshi au kiusalama.

Naam, baada ya Lisa na kundi lake wakiwa sambamba na mtuhumiwa wao kuingia kwenye chombo kile, waliongozwa kwenye chumba maalumu na kuoneshwa nafasi zao za kukaa.

Baada ya kukaa, alitokea daktari mmoja akiongozana na kijana aliyebeba sinia dogo lililokuwa na sindano uwezazo kuzikamata kama bastola. Sindano hizo zenye dawa kiasi, kila mmoja alichomwa begani na baada ya dakika chache, macho ya hawa watu yakaanza kuwa mazito.

"Kazi za utumwa hizi. Hamtakiwi kujua hata ni wapi mnafanyia kazi na ndio maana mnapigwa sindano za usingizi ili msione mnapoenda. Stupid peoples." Sauti nzito iliyochanganyanyika na ulevi, ilimtoka yule mtuhumiwa aliyekuwa huru kuongea baada ya kutolewa ile gundi aliyozungushiwa na Mubah.
Hakuna aliyemjibu na badala yake, kila mmoja alibebwa na usingizi mzito.
****

FISSA (Federal Intelligence Secret Service Agencies)
Mlango mmoja mkubwa uliandikwa maandishi hayo ambapo ndipo hasa Lisa na Mubah wanafanya kazi zao. Ule usingizi mrefu ulikuwa umewapaa na sasa walikuwa wanatembea wenyewe huku wakimkwida vema mtuhumiwa wao ili asiwaponyoke.

"Kazi nzuri Agent Lisa. Mmefanya vizuri na kikosi chako." Sauti ya mtu mmoja mrefu kiasi na mweusi, ilisikika ikiwa kwenye jukwaa dogo ambalo mbele yake kulikuwa na watu wanachakalika na kompyuta zao huku skrini moja kubwa ikionesha kazi nzima wafanyazo wale wafanyakazi.

"Asante mkuu." Lisa alishukuru huku akiinama kidogo kuonesha heshima kwa mkuu wake wa kazi.
Mkuu yule akashuka toka kwenye lile jukwaa na moja kwa moja akamfuata yule mtuhumiwa na kumuangalia kwa macho makali kabla hajaanza kuongea.
"John Lobo. Nilishangaa sana nilipoambiwa kuwa u mzima.

Nilikuua kwa mikono yangu, lakini leo ni kama nakutana na mzimu." Sauti ya yule bwana ilipenyeza kwenye masikio ya kila mmoja aliyesikia vema maongezi yale. "Sina kesi na wewe. Nilishakuua kipindi kile, hapa naanza na kesi nyingine." Alimaliza Mkuu wa FISSA na kugeuka nyuma kurudi kwenye lile jukwaa dogo.

"Malocha Malingumu." Sauti ya John Lobo, mtuhumiwa aliyekamatwa na kundi la Lisa, ilimuita yule mkuu wa kitengo cha siri cha huduma za kipelelezi nchini Tanzania. Bwana Malocha akasimama kumsikiliza kimtokacho John Lobo.
"Siyo kosa langu kuua familia yako.

Nilinunua roho zao kwa kuamrishwa na shetani langu. Usilalamike sana. Hahahahahaaa." Lobo alimaliza kwa cheko lake la kukera kushinda hata la katuni au fisi.

"Mpelekeni Hell in Hell." Malocha akaamuru na kila mmoja alishituka baada ya kusikia amri hiyo.
"Hamjanisikia?" Malocha aliuliza baada ya kuona hakuna kinachotendeka baada ya amri.

"Lakini Mkuu huyu tutampoteza kule. Kumbuka CIA na FBi wanamtaka mzima." Lisa akiongea kumuelewesha mkuu wake.
"Kwa hiyo unashauri apelekwe wapi?" Malocha akauliza tena swali.
"Nadhani twende naye 123K." Alitoa wazo Lisa.

"Kwa hiyo akakae tu! Kaja kukaa hapa au kusema ukweli?" Malocha alimtupia swali Lisa.
"Lakini si kumpeleka Hell in Hell. Atasema nini kule?" Lisa alijitetea.
"Hivi mmenileta huku nije kusema kitu au nije kupiga story na 'school mate' wenzangu?" Lobo alifungua kinywa chake na kuwauliza wale wanaoshauriana wapi wampeleke.

"Kama mnataka mnijue au niseme chochote, hilo mmekosea. Hapa hampati kitu wajinga nyie." Lobo akamaliza na hapohapo ngumi nzito ya tumbo ilitua. Alikuwa ni Mubah aliyemuadabisha.

"Utalipa hii dogo." Lobo alimwambia Mubah na Mubah badala ya kutilia maanani yale maneno, alimuongeza konde lingine zito la tumboni.
"Big Mistake(Kosa kubwa) Lakini bado unanafasi ya kulisawazisha." Lobo alimwambia tena Mubah baada ya kuinuka alipokuwa kainama kwa sababu ya kupigwa ngumi ile.

"Mpelekeni 123F6."Malocha aliamuru tena. Na kitendo bila kuchelewa, Lisa na Mubarak walimkamata kushoto na kulia na kuanza kumkokota kwenda chumba walichokiita 123F6.

HELL IN HELL
Hichi ni chumba kipana kilichopo ndani ya FISSA. Ndani ya chumba hiki kuna kiti cha umeme ambacho hutumika kuwasulubu watuhumiwa nguri na saa nyingine kuwaua.

Pia kuna tank kubwa ambalo limejengwa kwa vioo, na tank hilo ndani yake kuna maji. Pia hutumika kusulubisha watuhumiwa kwa kuwazamisha humo au wakiona haongei, hufungulia umeme uliyoungwa ndani ya tank hilo na kuanza kumpiga shoti mtuhumiwa. Hizo ni silaha chache zilizopo katika chumba kiitwacho Hell In Hell. Mbali na hayo, kuna vifaa vya kunyongea na kuchania ngozi.

Ni chumba ambacho kinaogopwa hata na wafanyakazi wenyewe. Kinatisha kwa matendo yanayofanyika huko.
123K

Hiki pia ni chumba kilichopo hukohuko FISSA. Chumba hiki pia ni kipana na kina meza moja kubwa pamoja na kioo ambacho ukiwa ndani huwezi kumuona wa nje lakini wa nje anamuona wa ndani.

Chumba hichi ni kwa ajili ya kumuhoji mtuhumiwa kwa mdomo bila kumsulubisha. Na hata kama watataka.kufanya hivyo, basi hutumia viungo vyao kama ngumi na mateke.

123F6
Hiki ni chumba kipana pia kwa ajili ya mahojiano na watuhumiwa. Ndani ya chumba hiki, mahojiano huwa ni ya kulazimisha uongee ukweli kwa kubanwa na silaha mbalimbali pamoja kuchomwa na vitu vyenye ncha kali lakini lengo likiwa utoke mzima.

Na mara nyingi kama mtuhumiwa ni mgumu, basi hupigwa sindano yenye dawa kali ambayo hufanya ubongo na akili ya mtuhumiwa iwaze kusema ukweli tu.
Humo ndimo ambamo John Lobo kapelekwa. Nyuso mbili ambazo hazina utani zilikuwa zimesimama pembeni ya chumba hicho huku wakijaribu jaribu vifaa vyao.

Mzee mmoja ambaye alikuwa anapuliza gesi yenye moto juu, aligeuka haraka baada ya kusikia mlango wa chumba kile ukifunguliwa.
"Ooh! Lisa. Umefanikiwa kumkamata Lobo. Kazi nzuri sana binti." Mzee yule aliongea kumpongeza Lisa.

"Asante Babu Pujini, hakuleta shida wakati wa kumkamata." Lisa alimjibu Mzee Pujini ambaye alikuwa ana asili fulani ya Kihindi lakini ni Muafrika halisi kutoka Tanzania.
"Good Lisa. Ndio umemleta kwenye shughuli eeh." Mzee Pujini aliongea huku akianza kuchezea tena ile gesi kwenye kibubu maalumu kinachotengeneza moto huo wa gesi.

"Ndio babu. Fanya yako." Lisa alijibu na wakati huo Mubah alikuwa anafungua pingu alizokuwa kamfunga John Lobo.
Licha ya Lisa na Mzee Pujini kuongea mengi yanayomhusu John Lobo, lakini Lobo mwenyewe hakuwepo kwenye dunia yao bali macho yake yalikuwa yakipepesa huku na huko, chini na juu ya chumba kile.

"Huyu hapa Mzee." Sauti ya Mubarak ilisikika huku ikifuatiwa na kumsukuma Lobo kwa mzee yule bingwa wa kutoa adhabu kwa watuhumiwa mbalimbali.
"Beda. Muondoe misuti yake huyu bwana." Mzee Pujini alimsukumia Lobo kwa Beda, jamaa fulani wa makamo na kwenye mwili mkubwa kutokana na kunyanyua vitu vizito.

Naye Beda bila kuchelewa, akaanza kumwondoa nguo John Lobo na wakati huo Lisa na Mubah walishatoka katika chumba kile na Mzee Pujini alishakifunga.
****

"Lobo. Nia yako na washirika wako ni nini?" Sauti ya kiume ilisikika katika chumba kiitwacho 123F6.
Ilikuwa ni sauti ya Malocha ikitoka kwenye spika zilizopo kwenye chumba kile.
Lobo alikuwa akivuja damu nyingi kifuani na maeneo ya usoni. Alikuwa kalegea kwa mateso makali ambayo yalitoka mikononi mwa Beda na Mzee Pujini.
"Kazi yangu ni kuuza au kununua roho tu!

Sina kazi nyingine. Sina nia na wala sijui washirika wangu ni wakina nani." Lobo alijibu swali la Malocha na baada ya jibu hilo, Malocha alitoa ruhusa ya mateso kuendelea.

Mzee Pujini akachukua kile kibubu chenye gesi na kuwasha gesi ile. Baada ya kuweka moto fulani kwenye kibubu kile cha gesi, akamfata Lobo na kuanza kumpitishia machoni bila kumdhuru bali kumsikilizisha joto litokalo mle kwenye kibubu.

"Joto hili linaenda kwenye maungo yako ya uzazi." Mzee Pujini akiwa kavalia kama Daktari, akaongea huku taratibu akianza kushusha moto ule kwenye maeneo ambayo kayataja.

Licha ya hayo yote kutukia, uso wa John Lobo ulikuwa si wenye mashaka wala uoga. Ni kama alishazoea yale mateso, lakini yote ni sababu alikuwa mkomavu katika nyanja kama zile.

Mzee Pujini akafika maeneo ya uzazi ya John Lobo, na bila kusita akapulizia gesi ya moto maeneo yale na kumfanya John Lobo atoe sauti kali iliyochanganyika na maumivu. Hakika mkomavu na kamanda wa mateso, alikuwa anaumia.

"You fu**n, motherfu***r you're hurting me. (We mpumbavu, (tusi). Unaniumiza)." Sauti ya maumivu makali ilisikika kutoka kwenye kinywa cha Lobo ikifuatana na matusi mazito ya wazazi kumuelekea Mzee Pujini.
"Sema ukweli tuache hili zoezi." Mzee Pujini aliacha kuchoka maeneo nyeti ya Lobo na kumuomba aseme ukweli.

"Pale nitakapofanikiwa kusimama kwenye hiki kiti, wewe ndio utakuwa wa kwanza kufa." John Lobo alimwambia Mzee Pujini maneno ambayo yule mzee alitabasamu kwa dharau kisha akaangalia kile kioo ambacho wa ndani hamuoni wa nje ikiwa ni ishara ya kuwaambia waulize swali lingine.

"Lobo. Hatupo hapa kukuumiza. Ni rahisi tu! Unashirikiana na nani na nini nia yako kwa ufanyayo." Swali lilelile lilitoka kwenye kinywa cha Malocha.
"Hahahaaa. Malocha, mbona unajiumiza sana. Nimekwisha kwambia, sina nia zaidi ya kuuza na kununua roho za watu.

Au unataka nikwambie duka la roho lilipo?" Lobo aliuliza huku uso wake ukielekea kwenye kile kioo kana kwamba anawaona wale wanaomtupia maswali kwa kunong'onezana.

"Lobo. Hatupo katika utani. Umemuua Kamanda wa Kikosi cha Upepelezi kanda ya kati. Umewatishia amani mawaziri mbalimbali na kauli yako ya kununua roho zao. Ukawaua baadhi ya viongozi hao. Ukaona haitoshi, ukaanza kuwaondoa mabalozi mbalimbali wa nchi hii kwa kuwaua. Sasa umegusa pabaya zaidi. Marekani.

Umegusa nchi ambayo hatuiwezi kwa kitu chochote....." Sauti ya Malocha ilikuwa ikielezea baadhi ya maovu ya John Lobo lakini kabla hajamaliza maongezi yake, sauti yenye hasira kupindukia, ilimkata kauli.
"Eti hatuiwezi kwa chochote.

Ni ujinga gani ambao umekujaa kichwani we' mpumbavu? Marekani anachotuweza ni nini? Au ndio kasumba zenu za uoga bado zimewatawala kichwani mwenu?

Huyu Frank anapambana na kutafutwa kwa udi na uvumba na watu gani? Si ni hawahawa Wamarekani? Mbona hawampati? Mbona hata wakimpata wanamshindwa? Kaua makomando wangapi Wakimarekani. Usiwe mjinga Malocha. Umiza kichwa fala wewe." Kauli chafu zilitiririka toka kinywani mwa Lobo na hakuna aliyethubutu kumkatiza hadi alipomaliza mwenyewe.

"Sound like it's true. But none of it is real. (Sauti kama ya ukweli. Lakini hakuna kati hivyo chenye uhalisia)." Malocha aliongea kwa kutumia lugha ya ughaibuni.

"Frank, never killed any commander from America. He just killed the terrorists, and bad guys. (Frank hakuua kamanda yeyote wa Kimarekani. Aliua wavamizi na watu wabaya pekee)." Sauti ya Lisa iliunga maelezo ambayo Malocha aliyaacha kati.

"Inaonekana hamjui lolote la kwa nini Frank anatafutwa na kwa nini kajificha. Na mbaya zaidi, hao anaowaua ndio mimi na baadhi yenu nyie wapelelezi mnawasujudia. Mtakufa kama panya kwenye sumu kwa mkono wangu." Lobo aliongea kwa hasira huku akijaribu kuchomoa mikono yake toka kwenye kiti alichokuwa kafungwa barabara na wazee wa kazi wa chumba 123F6.

Hali ya kujikakamua ili atoke pale kwenye kiti, ilifanya mwili wake ututumke na kusambaa misuli kama ananyanyua vitu vizito.
"Mzee Pujini. Fanya yako." Malocha aliongea kumruhusu tena Mzee Pujini aendeleze adhabu zake.

Mzee Pujini naye bila kusita, akajaribu moto wake angani kabla hajaanza kazi ya kuchoma ngozi nyeusi ya John Lobo.
****

"Hahahahahaa. Kuna muda hamna haja ya kulia bali kucheka kwa sababu maumivu uyapatayo, ni sawa na kukutekenya tu." Sauti ya John Lobo iliongea baada ya Mzee Pujini kumaliza kumchoma kwa gesi maeneo ya ndani ya mapaja na kifuani.

"Look like you are so tough. Lets see. (Unaonekana kama mgumu. Ngoja tuone)." Sauti ya Beda, mshirika au msaidizi wa Mzee Pujini ilisikika ikiongea hayo huku ye' mwenyewe akivaa grovu tayari kutimiza majukumu yake.

Beda akachukua visu fulani vidogo vilivyo kwenye mkoba maalumu kwa ajili ya kuvihifahidhia. Na baada ya kukamata visu hivyo viwili, akawa anavinoa kwa kuvisugulisha vyenyewe kwa vyenyewe huku akitembea mbele ya Lobo huku na huko.

Visu vilivyokuwa vinang'aa kama almasi lakini ni vya siliva, vilipita kifuani mwa Lobo haraka na kuacha alama kama ya X kifuani hapo, na kabla hata Lobo hajalia kwa sababu ya maumivu, akamwagiwa mafuta fulani spesheli ambayo yanauma si kawaida pale yawekwapo kwenye vidonda, lakini ni tiba tosha kwa ambaye anavuja damu.

"Fuc*** you FISSA. And fuc** you all and your mama."Lobo alitukana matusi mazito ya Kimarekani kwa sababu ya maumivu makali yaliyokuwa yanampata kwa wakati ule. Hakika alikuwa katika mateso, lakini bado hakuwa tayari kusema ukweli wowote.

"Lobo. Nia yako ni nini na washirika wako ni wakina nani?" Malocha aliuliza kwa sauti kali tena.
"Nia yangu ni kusafisha pasafi kwa kuweka uchafu. Washirika wangu ni uchafu, umenielewa?." Lobo alijibu kwa hasira kali zilizokuwa zimemjaa moyoni sababu ya kuchanjwa na kuteswa na FISSA.

"Mkuu, niachie mimi nikamuhoji mlemle." Mubarak alitoa ombi ambalo halikukataliwa kwa sababu majibu ya John Lobo yalikuwa hayana mashiko hata kidogo vichwani mwao.

"Ooh! Mubah. Umekuja kuchukua ujumbe wako." Lobo alitoa tabasamu pana baada ya kumuona Mubarak kaingia ndani ya chumba kile.
Mubah hakuongea chochote zaidi ya kuchukua chuma chenye ncha kali kwenye ule mkoba wa kuhifadhia vifaa hivyo vya mateso.

"Nauliza swali. Nataka jibu sahihi." Mubah alimwambia Lobo huku akikaa kwenye kiti ambacho alikivutia mbele ya Lobo.
Lobo badala ya kujibu, alitabasamu tena. Tabasamu la kukereketa hata ubongo wa kichaa.


ITAENDELEA
Riwaya. Bora kabisa kuwahi kuandikwa! Imesheheni Taharuki,mikasa na ukatili wa kutisha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom