Riwaya-duka la roho

Riwaya-duka la roho

RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA TISA
"Nini kimetokea?" Swali la kwanza kulisikia Gunner baada ya simu ile kuipokea. Ilikuwa ni sauti nzito na inafanana na sauti ya redio iliyokwisha betri.
"Ni Masai." Gunner akajibu huku akitetema.
"Masai ndiye nani?" Sauti ile ikauliza kwa ukali na kumfanya Gunner kutojibu chochote. "Acha ujinga we mpumbavu. Nitakuua mimi. Umefanya ujinga ambao hutakiwi kusamehewa kosa lako." Ile sauti ilizidi kufoka.
"Hapana The Shadow. Tunaomba msamaha. Tupe nafasi nyingine tutafanya vema." Gunner alijitetea huku kijasho chembamba kikimtoka.
"Hakuna kitu kama hicho Gunner. Wote mtakufa kwa sababu ya huu ujinga." Mtu aliyeitwa The Shadow, aliongea na kumfanya Gunner kutulia bila kusema chochote. "Natuma watu wangu wawili hatari kuja huko kumuangamiza huyo kinyago wenu. Baada ya hapo, watakuja kuwamaliza nyie. Sitaki muingilie chochote wakati hawa watu wanafanya kazi yao." The Shadow alimaliza na Gunner akajibu sawa. Simu ikakatwa.
GENIVA, USWISI.
Jamaa wawili walikuwa wamesimama nyuma ya kiti kimoja ambacho kilikuwa kimewapa mgongo na sigara kubwa (cigar) ilionekana ikivutwa na moshi wake ukipulizwa juu.
Watu hawa hawakuweza kuona sura ya mtu huyo bali kuisikia sauti yake wakati inaongea na Gunner aliye nchini Tanzania.
"Pinto na Trina." The Shadow aliwaita wale watu bila kugeuka.
"Ndio The Shadow." Waliitika kwa sauti ya pamoja.
"Nawatuma Tanzania kwa kazi moja tu! Ya kuua. Kauweni kundi la mtu anayeitwa Masai." Alipoongea hayo, akarusha bahasha mezani lakini hakugeuka nyuma.
Msichana mmoja anayejulikana kwa jina la Trina, akasogea na kuichukua ile bahasha. Akaifungua na hapo akakuta picha kadhaa za Frank Masai na kundi lake lote.
"Hao wote wanatakiwa kufa. Lakini wa kwanza awe ni Masai. Kichwa chake nikione hapa." The Shadow akapiga pafu nzito kwa kuivuta cigar yake, kisha akapuliza moshi mzito angani.
"Baada ya kumaliza hawa wajinga wa Masai, malizeni na haya majinga mengine." Akatupa bahasha tena mezani na jamaa wa kiume kwa jina la Pinto, aliisogelea na kuifungua bahasha hiyo. Sura za wakina Gunner na Lobo zikaonekana katika picha zilizomo kwenye bahasha ile.
"Yametimia haya Boss." Sauti nzito ya Pinto ilijibu wote wawili, yaani Pinto na Trina, wakatoka kwenye ofisi ile ambayo ilikuwa inawaka mwanga wa bluu.
PINTO NA TRINA.
Pinto au alivyopenda kujiita El Pinto, alizaliwa nchini Mexico. Ana miaka ishirini na nne pekee (24) lakini amekwishaua watu thelathini wakiwemo viongozi wakubwa kumi na mbili. Hajawahi kushindwa kazi ambayo kapewa. Mataifa makubwa yote yamewahi kumtumia huyu kijana na mafanikio yake yalikuwa makubwa kuliko walivyotaraji.
Mwili mdogo kama kawaida ya Wamexico wengi, uliwafanya wale wanaowindwa kudharau kazi ya yule bwana.
Ni mkali wa kutumia silaha za moto. Mwili wake wote hujaza silaha hizo jambo linalofanya asishindwe mpambano wowote. Licha ya kuwa mkali wa silaha hizo za moto (mfano bunduki), pia hakuwa nyuma katika mapambano ya uso kwa uso. Ana mapigo ambayo yanaweza kumfanya adui akimbie bila kupenda.
Historia ya wazazi wake, iliishia pale alipowaua wote kwa sababu ya wao kukubuhu katika kuvuta madawa ya kulevya na kusahau kabisa mahitaji mengine ya familia. Hasira ambazo alikuwanazo Pinto, aliweza kumng'ata baba yake kwenye koo hadi akanyofoa koromeo lake.
Mama yake ambaye alikuwa kalewa madawa, alimchinja kwa kisu kikali kinachotumika jikoni kwa ajili ya kukatia nyama. Baada ya mauaji hayo, Pinto akachukuliwa na kundi la wahuni wa Mexico ambao walimfumdisha njia mbalimbali za kuishi kama muhuni. Katika njia hizo, kamwe hakuwahi kujihusisha na uvutaji wa madawa wala bangi. Kilevi chake kikubwa kilikuwa ni Trina.
Trina yeye katokea nchi ya Italia. Anamiaka ishirini na mbili (22). Kishatekeza roho zipatazo arobaini na tano za watu wakubwa kwa wadogo, matajiri kwa masikini. Yeye yupo kimaslahi zaidi. Ukitaka kazi yako.ifanyike bila kero, mlipe pesa zake zote, majibu utayapata baada ya masaa ishirini na nne.
Yeye kaua watu wengi kuliko Pinto kwa sababu ya uzuri wake ambao uliwafanya mabosi wanaomtuma waamini kuwa unaweza kuwateketeza maadui zao bila shida. Trina alisifika zaidi katika kucheza na silaha zenye ncha kali kama visu, mapanga na silaha za kininja. Pia hakuwa nyuma katika mapigano ya viungo na kutumia sumu. Trina alikuwa vema sana katika kazi yake.
Wazazi wa Trina waliuawa huko Italia na kundi la Mafia baada ya baba yake nna Trina kukutaa kujichinja kwa kosa la kutosambaza madawa ya kulevya katika kituo cha watoto yatima. Hali hiyo ndio ikawapa hasira Mafia na wakaamua kuiteketeza familia nzima ya Trina akiwepo Dada yake aliyekuwa na umri wa miaka sita kipindi hicho. Trina akiwa na miaka mitatu, aliweza kuona mauaji hayo akiwa kwenye kabati alipofichwa na baba yake.
Trina akaishi kwa upweke muda mrefu baada ya familia yake kuuawa. Akawa mtoto wa mitaani huku akiwa na boksi dogo aliloweka baadhi ya picha za wazazi wake na zawadi mbalimbali alizowahi kupewa. Alipotimiza miaka saba, akawa si Trina tena bali Trina wa hatari. Aliweza kuishi katika mtaa wowote kwa amani au kwa vurugu. Japo hakuwa mkali sana katika mapambano ya viungo, lakini aliposhika silaha kali, aliweza kunyamazisha kila ambaye alitaka kuingia anga zake. Aliwahi kumchana mgongo kwa kiwembe mkuu wake anayempa madawa ya kulevya akauze kisa hakukamilisha malipo sahihi ya kazi aliyopewa. Pia aliwahi kukata nyeti za bwana mmoja mtu mzima aliyekuwa akitaka kumuingilia kinguvu mwilini. Na baada ya kukata nyeti hizo kwa kisu kikali, akakinga damu ya baba lile jitu zima na kuinywa.
Sifa hizo na nyingine nyingi, ndizo ziliwafikia Mafia na kuamua kumchukua yule mtoto pasipokujua wamemchukua mtoto wa nyoka waliyemuua.
Baada ya Mafia kumfunza na kumuivisha kwa kila kitu, ndipo Trina akatoa picha fulani ambayo kwa nyuma iliandikwa "Hawa ndiyo adui zako, wauwe ukipata nafasi."
Mwandiko huo wa baba yake, ndiyo ulikuwa muda wa kuufanyia kazi. Akaingia hadi kule anapotaka na kisha akaua maadui zake wote. Baada ya hapo, akapotea kabisa nchini Italia.
Ilikuja kuonekana akiwa na miaka kumi na minane nchini Japan. Alikuwa binti tajiri kuliko binti yeyote pale Japan. Alimiliki miradi mbalimbali iliwemo vituo vya matangazo na viwanda kadhaa vya magari. Mali zote zilikuwa za baba yake na yeye aliziongeza kwa kazi yake ya kuua.
Alipotumwa nchini Hispania kwenda kumuua mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa, ndipo alipokutana na Pinto ambaye yeye alikuwa na jukumu la kuiba siri za usalama wa taifa. Wakiwa hawajuani, wote wakaajiriwa kama wapelelezi katika nchi ile. Kilichokuja kuwaunga, ni pale Trina alipomkamata Pinto anaiba siri nzito za Hispania. Na wakati anamkamata, yeye tayari alikuwa amekwishamuua mkuu wa upelelezi kama alivyoagizwa.
Walichofanya hawa watu ni kutoroka kwa pamoja na baadaye wakaungana na kuwa marafiki wakubwa hadi kufikia kuitwa wapenzi.
Sasa The Shadow kawatuma wapenzi hawa waje Tanzania kummaliza Frank Masai na kundi lake. Masai hajui kama kuna mpango wa yeye kuangamizwa na wakati huo taarifa zinazagaa kuwa kafika Tanzania na anaendesha ugaidi kama kulipua ndege kwenye Bahari ya Hindi na kulipua jengo la usalama wa taifa na kuua wapelelezi kumi na mbili wakuokuwepo katika jengo hilo. Tanzania yote ikabandikwa matangazo na picha za Masai kama " The Most Wanted".
Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vikatapakaa picha nne zikiwatuhumu watu hao kuwa ni magaidi wa kutisha. Picha ziliwaonesha Mubah, Malocha, Lisa na Masai kama ndio tatizo la nchi ya Tanzania.
Rais alishasema mengi kuhusu hawa watu na akaweka vizuizi kadhaa juu ya watu hawa. Lakini tatizo ambalo walikuwa nalo wengi wa wapelelezi, ni kutojua watawapatia wapi watuhumiwa hawa. Ni vigumu kuwapata kwa sababu wanavifaa vingi vya kuzuia mawasiliano yao yasifike sehemu nyingine na zaidi, kabla hujawafikia, tayari wanakuwa wamekwishajua hilo.
"Masai. Ndio kama hivyo kaka, tunasakwa kwa ugaidi. Tuwe makini tu." Mubah aliongea baada ya kuzima runinga iliyokuwa ikionesha taarifa zao.
"Usijali Mubah. Hapa hamna atakayekamatwa. Cha msingi ni kuondoka hii sehemu." Masai alitoa ushauri.
"Twende wapi sasa." Malocha aliuliza.
"Kuna nyumba ya Lisa kule Sinza, nadhani ni sehemu nzuri ya sisi kujificha." Frank akatoa wazo.
"Haa! Yaani twende kule katikati ya jiji tena? Masai unatafuta kukamatwa." Mubah aliongea kama anapinga kauli ile.
"Siku zote penye watu ndipo pa kujificha. Usitegemee simba kutafutwa mjini, anatafutwa porini Mubah. Sisi tunawindwa, lazima watuwindie nje ya mji. Sasa kama hamuamini, subirini siku mbili tu. Mtasikia tumevamiwa, na huyo Rais wa Urusi kaondoka kachukia balaa, lazima alete watu wake watusake."
"Okay. Upo sawa Masai. Ngoja Lisa atoke tuongee naye." Malocha alimaliza maongezi ya asubuhi ile kwa kumsubiri Lisa ambaye bado alikuwa chumbani kalala na mwanaye.
****
"Lobo. Unajua The Shadow kawatuma Pinto na Trina." Gunner alikuwa akimpa taarifa mtu wake wa kazi.
"Kwa hiyo." Lobo akauliza huku akinoa kisu chake chenye meno upande mwingine.
"Wakiwamaliza wakina Masai, ni zamu yetu. Na unawajua wale, hawajawahi kushindwa vita."
"Umewahi kumsikia Masai kashindwa vita? Hata ya makundi ya kigaidi na kipelelezi. Kawahi kushindwa?"
"Sawa, hajawahi kushindwa lakini angalia na uwezo wa wakina Pinto. Angalia watu waliwaondoa, ni tofauti na aliowaua Masai."
"Trina na Pinto, walipata kazi gani katika mauaji yao? Wao ni watu wa kumendea tu! Hata mimi hawaniwezi. Wale ni watu wa kusubiri mtuhumiwa wao atoke sehemu ndio wamvamie. Lakini mimi, nakupa taarifa kuwa ndani ya masaa ishirini na nne au siku kadhaa, uwe umefanya hivi au vile, usipofanya naku kraa." Lobo akaweka ishara ya kuchinja shingoni kwa kutumia kisu chake.
"Kwa hiyo wewe hawakutishi hata kidogo?" Gunner akamuuliza Lobo.
"Watanitisha nikikutana nao uso kwa uso. Lakini tukiwindana, watakufa wao mapema tu."
"Unadhani Masai atafanikiwa kuwazima hawa?"
"Uzuri wa Masai anavitu vingi anavyowazidi wale. Wale wanatumia silaha za moto na vitu vyenye ncha kali, Masai ni mkali wa vyote hivyo. Pia Masai anaweza mapigano ya ana kwa ana na anaweza kuwinda pia, vitu ambavyo hao Pinto na Trina wanavyo kwa mmoja mmoja. Lakini tatizo la hao watu wa The Shadow, hawana mbinu za kisheria, Masai akisema nitakuwa hapo dakika moja ijayo, basi jiandae kumpokea. Hawa hawana sumu hizo. Akikutana na Pinto, atacheza naye kwa visu na mapanga. Pinto hawezi hiyo. Akikutana na Trina, atacheza naye kwa bunduki na bastola, unadhani nani atashindwa?" Lobo akampa ufafanuzi yakinifu Gunner.
"Ndio maana The Shadow kawatuma wote wawili. Unadhani Masai atapona?"
"Masai hajui kama hawa watu wanakuja, hilo ni tatizo kubwa sana na atapata shida kuwazuia. Lakini angekuwa anajua kuwa wanakuja, angewamalizia hukohuko kwao."
"Kwa hiyo tumwambie au? Unajua wakifa wale na sisi tutapona."
"Gunner. Acha uoga. Ile si vita yetu, subiri wamalizane na Masai ije zamu yetu. Tutacheza na sheria tu. Watoto wadogo wale, wala hawana tatizo. Na Masai namjua tangu zamani sana, nimesoma naye na kupambana naye. Acha uoga tu!" Lobo aliongea kwa kujiamini.
"Okay. Ila Masai asipouawa na hawa, nitamuua mwenyewe, naapa kwa MUNGU. Bahati yake tumesimamishwa." Lobo akawa mtu wa kutabasamu kwa maneno yale ya Gunner, hadithi zao zikaishia hapo. Gunner akatoka kwenda kuvuta sigara, Lobo akabaki kitini anaendelea kunoa kisu chake.
****
WIKI MOJA MBELE. UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM.
Ndege binafsi lakini kubwa kiasi, ikatua katika uwanja ule kwa mbwembwe zake zote. Pembeni iliandikwa PITRI yaani Pinto na Trina, na kulembwa na rangi za kijani na nyekundu, rangi ambazo zinapatikana kwenye bendera za Italia na Mexico.
Hakuna aliyejua maana ya neno lile la PITRI kwa hapa Tanzania. Hivyo waliiacha ndege ile itulie ndipo wawaangalie wageni wake.
Baada ya dakika tano za ndege ile kutua, wakashuka vijana wa kizungu wawili wakiwa wamevalia suti nyeusi na makoti makubwa juu yake.
Yule wa mbele alitazama huku na huko kabla hajatoka pale mlangoni na kumpisha wa nyuma yake ambaye naye macho yake yakaitazama nchi ya Tanzania vema. Akavaa mawani yake nyeusi na kisha akaanza kushuka katika ngazi za ndege ile ghali.
Wakiwa na mabegi yao kila upande, wakafika sehemu ya ukaguzi na kuyatupia mabegi hayo kwenye vifaa maalum vya kukagulia na wao wakapita kwenye mlango wa ukaguzi bila wasiwasi.
Mabegi yalipita salama, ila wao walivyopita taa nyekundu iliyoambatana na mlio wa hatari, kwa pamoja vilitoa ishara kuwa watu wale wamebeba vitu vya vyuma.
"It's my belt. (Ni mkanda wangu)" Pinto aliongea huku akivua mkanda wenye bakoni kubwa kama wapendavyo kuvaa wamexico wengi. Akauweka juu ya meza ya idara ile na kupita tena lakini bado sauti na taa ile vilitoa ishara tena.
ITAENDELEA
 
uwiii utam utam utam! asante sana mkuuu...nasubiria kwa hamu kubwa
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI.
Wakiwa na mabegi yao kila upande, wakafika sehemu ya ukaguzi na kuyatupia mabegi hayo kwenye vifaa maalum vya kukagulia na wao wakapita kwenye mlango wa ukaguzi bila wasiwasi.
Mabegi yalipita salama, ila wao walivyopita taa nyekundu iliyoambatana na mlio wa hatari, kwa pamoja vilitoa ishara kuwa watu wale wamebeba vitu vya vyuma.
"It's my belt. (Ni mkanda wangu)" Pinto aliongea huku akivua mkanda wenye bakoni kubwa kama wapendavyo kuvaa wamexico wengi. Akauweka juu ya meza ya idara ile na kupita tena lakini bado sauti na taa ile vilitoa ishara tena.
Pinto akamuangalia Trina kwa macho ya kumpa taarifa ya jambo fulani. Wale wana idara ya uhamiaji, wakaweka mikono yao kiunoni kwa kuzikamata bastola zao tayari kwa kuwaweka chini ya Ulinzi.
"Ooooh! PITRI. Welcome in Tanzania." Sauti kutoka kwenye mlango wa kuingilia uwanja wa ndege ilisikika na mara polisi na wanaidara wote walisimama wima kama wapo kwenye gwaride la jeshi.
Alikuwa ni Mheshimiwa Rais wa nchi ya Tanzania akiwa kanyoosha mikono yake na kuwakumbatia Pinto na Trina mmoja baada ya mwingine.
"Hawa ni wageni wangu jamani, hamkuona taarifa zao kuwa nitakuja kuwapokea?" Rais akawauliza wana idara ya uhamiaji na wote wakatulia tuli huku vichwa vikiwa chini.
"Okay Guys, lets pass in VIP doors. (Sawa vijana, twendeni tukapite kwenye milango maalumu)" Rais akawachukua Pinto na Trina na kuanza kwenda nao kwenye mlango wa watu maalumu huku nyuma, mabegi yao yakiwa yamebebwa na wafanyakazi wanne waliokuja na Rais.
"Ilibakia sekunde chache tuangamize watu wako." Pinto alimwambia Rais kwa kiingereza cha shida wakiwa ndani ya gari maalumu walilopanda watu watatu tu. Rais akiwa ndiye dereva.
"Nilichelewa kidogo tu. Samahanini sana." Rais aliomba msamaha na wote wakaupokea. Macho yao, Pinto na Trina, yakawa kwenye vioo vya gari walilopanda wakishangaa jiji la Dar es Salaam.
Baada ya saa moja, Rais alikuwa anawakaribisha Pinto na Trina katika Ikulu na moja kwa moja akawaongoza hadi chumba maalumu kwa ajili ya maongezi.
"Kwa taarifa nilizozipata, Masai anaonekana sana mida ya usiku katika maduka ya Mlimani City. Sasa mkianzia pale, nadhani mtapata nyama yenu bila wasiwasi. Si mnamtaka mzima tu! Nadhani atawasaidia sana kwenye upelelezi wenu." Rais aliongea kwa tabasamu pana akidhani watu wale wapo kwa ajili ya kumkamata Masai, kumbe kumuangamiza.
"Mlimani City ipo wapi." Trina aliuliza huku akitoa mawani yake na kumuangalia Rais kwa macho yake ya kahawia na ya kung'aa kama ya paka.
"Nitawapa dereva awatembeze ili mpajue kote huku." Rais aliongea huku akijichekesha chekesha.
"Fanya sasa hivi." Trina akaongea na kuvaa mawani yake tena kisha akaegemea kochi. Rais akanyanyua simu yake na kuipiga. Akaongea kwa Kiswahili kumpa maelekezo mtu aliyempigia.
Baada ya dakika mbili, akaingia jamaa kalivalia suti ya kupendeza. Akapewa ugeni alioitiwa na kuondoka nao.
Trina na Pinto walilitazama eneo zima la Mlimani City. Wakalichora sehemu zote muhimu na baada ya kumaliza, wakamuomba mwenyeji wao awatafutie hotel yenye hadhi maeneo yale.
Ndipo wakapelekwa kwenye hotel ambayo walipoiona, wakaikubali bila neno. Wakalipia kwa pesa za Marekani na kuchukua chumba cha juu ambacho waliweza kuona mengi ya chini kwa kutumia vifaa vyao.
****
Kundi la Malocha walishahamia kwenye nyumba ya Lisa na baada ya kuhamia, siku mbili mbele, nyumba yao ya Kivule ikivamiwa na wapelelezi walioagizwa kuwasaka. Lakini kwa bahati mbaya wakawakosa.
Bado waliendelea kucheza na mitambo yao na kamwe hawakuwa lelemama katika kusaka kinachoendelea. Kitu ambacho walikikosa, ni ujio wa Pinto na Trina ambao walishajua kuwa Masai anapenda sana kwenda Mlimani City usiku kwa ajili ya kununua mahitaji ya nyumbani lakini pia zawadi kwa Martina ambaye bado alikuwa hamtaki baba yake.
"Lisa." Masai alimuita mpenzi wake mida ya saa mbili usiku. Hiyo ni baada ya siku nne za Trina na Pinto kufika Tanzania.
"Abee switie." Lisa aliitika huku anakimbilia alipo Masai.
"Naenda Mlimani mara moja kuchukua mazaga ya hapa."
"Okay baby. Lakini na hiyo suti yako, harahara wasinipokonye huko." Lisa alitania kwa ile suti ya Masai ambayo alitoka nayo Italia. Hakuivaa tangu kipindi alipoharibu mipango ya Gunner.
"Hahahaaa. Hamna kitu kama hicho."Masai akamuhakikishia mpenzi wake na kumpa busu dogo la shavuni.
"Okay. Bye sweetie." Lisa alimuaga Masai aliyetoka katika chumba kile na kupita sebuleni ambapo pia aliwaaga rafiki zake kama alivomwambia Lisa.
****
Saa tatu, Masai alikuwa ameegesha gari lake nje ya maduka ya Mlimani City na kisha akavaa kofia yake ambayo haikuendana na suti. Alifanya hivyo ili asijulikane na watu hasa ukizingatia Masai anatafutwa kwa udi na uvumba.
Akiwa ameanza kuchagua hiki na kile mle dukani, wazungu wawili ambao walionekana ni wapenzi, waliingia na kuweka mabegi makubwa sehemu ya mapokezi na kisha kuchukua vitoroli maalumu vya kubebea bidhaa na kuanza kwenda kuchagua wavitakavyo.
Wakasogea hadi karibu na Masai, kisha wakawa wanacheka na saa nyingine wananyonyana ndimi zao. Masai hakuwatambua na wala hakuwafatilia, akawa anaendelea kuchagua bidhaa zake.
Wazungu wale wakaanza kuchagua bidhaa upande wa kushoto na Masai upande wa kulia, hivyo wakawa wamepeana migongo. Masai akasogea mbele kidogo na kisha akachagua kioo cha kujiangalia. Akakitazama na kukijaribu kwa kujiangalia. Akajiona ndevu zake alivozifuga ili asijulikane, akatabasamu na kuanza kukirudisha kioo kile.
Lakini kabla hajakishusha, alimuona yule mwanamke wa kizungu nyuma yake akiwa kakamata panga fulani lenye makali pande zote na alikuwa kalinyanyua juu tayari kwa kulishusha katika kichwa cha Masai.
Masai aliruka kwa pembeni na panga lile likamkosa na kukata kabati lililokuwa limebeba bidhaa. Alikuwa ni Trina ambaye kamkosa kwa panga Masai.
Masai akakaa mkao wa kupigana na wakati huo watu walikuwa wameanza kusogea kujionea kinachoendelea. Asivyotegemea Masai labda Trina atasogea yeye kupambana, akatokea mpenzi wake, Pinto ambaye aliruka sarakasi na kutua mbele ya Masai huku kakamata bunduki fupi (short gun) iliyokuwa na matundu mawili lakini imepunguzwa bomba za mbele na kuwa fupi zaidi kiasi kwamba wakaguzi wa duka lile hawakuiona. Pinto alikuwa kaielekeza kifuani kwa Masai na hakusita kuifyatua.
Ikamrusha Masai hatua sita nyuma lakini haikumuua wala kumdhuru kwa sababu ya suti aliyovaa.
Mlio wa short gun ile, ukawafanya wananchi kukimbia hovyo kwenda nje. Masai akanyanyuka haraka na kutaka kikimbia lakini mara viatu vyake vikachomwa na visu na kuvishikilia hapohapo chini. Ikabidi avivue na kubaki peku. Hadi anamaliza kuvivua, tayari Trina alishasogea na kurusha visu vidogo vinne. Masai akavizuia kwa mkono wa kushoto na kudunda juu ya suti yake matata.
Mambo yakawa mazito kwa Masai, alichofanya ni kubonyeza saa yake haraka na suti yake ikajifunga miguuni, kwenye viganja vya mikono na usoni.
Ile anageuka aangalie maadui zake, anakutana tena na midomo ya short gun iliyokuwa imelenga kichwani. Ngoma ikaachiwa tena na kumpaisha Masai mbali na pale aliposimama.
Akili ikamvurugika na maumivu aliyahisi. Akataka kunyanyuka akajikuta anadondokea makabati yenye bidhaa mle Mlimani City. Wakati anahaha na hayo, Trina alikuwa anakuja kwa kasi na kuruka teke lililomkuta kifuani Masai. Masai hoi mbele ya ile miili ya vijana wawili wanaopiga kwa mtindo wa ‘one by one’, yaani wanapigana kwa kuachiana.
Mwanaume akawa anagaa kwa maumivu tele, na sasa ilikuwa zamu ya Pinto kumshambulia. Katika hali ambayo haikutegemewa na kila mtu ambaye alikuwa anashuhudia mpambano ule, Pinto alikimbilia kwenye moja ya mabegi makubwa alilyokuja nayo. Akaingiza mkono wake ndani ya begi lake, na mara akachomoa bunduki nzito inayomwaga risasi karibu mia moja kwa dakika. Wanaiita Min Machine Gun. Ina mkanda wenye risasi zenye idadi kubwa.
Pinto akaikoki vema mbele ya Masai, na bila huruma alianza kumimina risasi zisizo na idadi. Ilitisha na kusikitisha hasa risasi zile zilivyokuwa zinajaribu kutoboa suti maridhawa ya Masai.
Baada ya dakika mbili, Pinto alitulia na kutazama hali ya windo lake. Masai akawa anagaa-gaa chini anashindwa kunyanyuka pale kwa sababu ya kuelemewa na anachofanyiwa.
Akiwa kama mtoto, akawa anatambaa kwa tumbo kuufuata mlango wa kutokea. Masai anajaribu kuokoa nafsi yake, anasikia nyuma yake sauti ya kitu kama injini ya gari dogo la kuchezea watoto. Kugeuka angalie japo kwa shida, anaona viatu vya Trina kwa mbele kuna visu ambavyo vinazunguka kwa kasi miguuni kwake.
Masai akaongeza kasi ya kutambaa kwa tumbo kwenda nje, lakini Trina akamuwahi kukandamiza usoni visu vile na kuvizungushia hapohapo bila huruma. Ni cheche tu ndizo ambazo zilikuwa zinamwagika. Haileweki ni vipi angekuwa huyu Masai kama asingekuwa na ile suti. Amshukuru aliyeitengeneza.
Hali ikazidi kuwa mbaya. Kizunguzungu kikamkumba yule mwanaume na taratibu akaanza kukubali kuwa anashindwa.
"Suti hii pia inaweza kutoa shoti ya umeme mikononi." Maneno ya Alejandro, aliyeitengeneza ile suti yakajirudia kichwani kwa Masai. "Kivipi sasa? Inatoaje hiyo shoti?" Masai akajiuliza bila kupata jibu. "Ngoja nijaribu." Masai akajishauri na kwa kuwa ndio uokozi pekee uliyokuwa umebaki, akajaribu kwa kuukamata mguu wa Trina. Lakini hakuna kilichotokea zaidi ya kazi ya vile visu vya miguuni kuendelea kuchimbua maski iliyoziba uso wake.
Ikabidi Masai aruke pembeni na kumuacha Trina akimfuta kwa kasi. Akaangalia saa yake na kuona kuna kitufe ambacho huwa hakitumii sana, kwa chini kimechorwa alama ya radi. Akakibonyeza na wakati huo Trina alikuwa kafika na viatu vyake.
Mtoto yule wa kike akarusha teke ambalo lilimkuta Masai kifuani. Masai akazidi kuvuruga bidhaa za duka lile kubwa kwa kuzipamia. Trina akaruka sarakasi na kutua juu ya kifua cha Masai, akawa kamkalia kifuani.
Akanyoosha mikono yake juu, na hapo vikachomoza visu virefu kiasi toka kwenye koti la mterezo alilolivaa. Akaanza kuvishusha kwa kasi kuelekea kifuani, hapo ndipo Masai akajaribu bahati yake kwa kunyoosha mikono yake miwili na kugusa kifua cha Trina. Bila kutegemea, Trina akarushwa na umeme mkali toka katika mikono ya Masai. Akarushwa hatua kumi nyuma na kilichomzuia ni ukuta wa uliozunguka mle ndani.
Pinto akashtuka hasa pale alipomuona mpenzi wake anakukuruka kama mtu mwenye degedege au kifafa.
"Shit." Pinto akatukana na kulivua koti lake. Sasa silaha zake baadhi zilizomzunguka mwili mzima, zikaonekana.
Akachomoa bunduki nyingine ya hatari toka mgongoni kwake. M16 naizungumzia. Akaikoki na kuanza kumwaga njugu kwa fujo kumuelekea Masai aliyekuwa bado hajarudisha nguvu ipasavyo. Baadhi ya risasi zilimpata lakini hazikumdhuru sana kwa sababu ya suti yake.
Risasi zikaisha kwenye M16. Pinto akatupa bunduki ile pembeni na kisha katika kifua chake, akanyofoa mabomu mawili yaliyokuwa yananing'inia. Akayarusha sehemu ambayo Masai alikuwa kalala. Pinto akaruka pembeni na Masai alisikia vyuma vikidunda chini ya sakafu ile ya Mlimani City, kutazama anaona mabomu yanakuja kwa haraka.
Mtoto wa kiume akapata nguvu za kunyanyuka na kwa kasi ya ajabu, akajirusha kwenye mlango wa kutokea ambao ni kioo tupu. Kikavunjika na Masai akawa nje wakati huo mabomu yakawa yanalipuka na kuzidi kuleta tatizo katika mtaa ule.
Baada ya mabomu yale kutulia, Pinto alinyanyuka na kuangalia kama kafanikiwa zoezi lake. Akatazama katika mlango wa kutokea, akaona gari likiondoka kwa kasi toka katika uzio wa duka lile. Alijua kuwa ni la Masai kwa sababu katika kumfuatilia, aliliona mara kwa mara Masai analiendesha.
"Bastardo (Mpumbavu)" Pinto akatema tusi dogo kwa lugha ya Kiitaliano. Akakimbilia pale alipo mpenzi wake na kumkuta kazimia. Akampiga makofi kadhaa na Trina akafungua macho yake na kumuangalia Pinto.
"Kakimbia yule mbwa?" Trina akamuuliza Pinto.
"Ndio. Tuondoke hapa haraka." Pinto alijibu na kumnyanyua Trina tayari kwa kuondoka eneo lile ambalo taratibu lilianza kunyemelewa na wanausalama.
****
Masai akiwa hana nguvu za kutosha, akawa anakimbiza gari lake kuelekea maeneo ya Sinza, makao mapya waliyohamia na washirika wake. Kwa bahati nzuri alifika salama na kushuka garini.
Aligonga mlango na Lisa ndiye aliyeufungua. Lisa akakutana na mwili wa Masai ambao hauna nguvu. Ukamdondokea taratibu lakini mtoto wa kike akamdaka na kuanza kuwaita wenzake.
ITAENDELEA
 
  • Thanks
Reactions: ADK
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA ISHIRINI.
Wakiwa na mabegi yao kila upande, wakafika sehemu ya ukaguzi na kuyatupia mabegi hayo kwenye vifaa maalum vya kukagulia na wao wakapita kwenye mlango wa ukaguzi bila wasiwasi.
Mabegi yalipita salama, ila wao walivyopita taa nyekundu iliyoambatana na mlio wa hatari, kwa pamoja vilitoa ishara kuwa watu wale wamebeba vitu vya vyuma.
"It's my belt. (Ni mkanda wangu)" Pinto aliongea huku akivua mkanda wenye bakoni kubwa kama wapendavyo kuvaa wamexico wengi. Akauweka juu ya meza ya idara ile na kupita tena lakini bado sauti na taa ile vilitoa ishara tena.
Pinto akamuangalia Trina kwa macho ya kumpa taarifa ya jambo fulani. Wale wana idara ya uhamiaji, wakaweka mikono yao kiunoni kwa kuzikamata bastola zao tayari kwa kuwaweka chini ya Ulinzi.
"Ooooh! PITRI. Welcome in Tanzania." Sauti kutoka kwenye mlango wa kuingilia uwanja wa ndege ilisikika na mara polisi na wanaidara wote walisimama wima kama wapo kwenye gwaride la jeshi.
Alikuwa ni Mheshimiwa Rais wa nchi ya Tanzania akiwa kanyoosha mikono yake na kuwakumbatia Pinto na Trina mmoja baada ya mwingine.
"Hawa ni wageni wangu jamani, hamkuona taarifa zao kuwa nitakuja kuwapokea?" Rais akawauliza wana idara ya uhamiaji na wote wakatulia tuli huku vichwa vikiwa chini.
"Okay Guys, lets pass in VIP doors. (Sawa vijana, twendeni tukapite kwenye milango maalumu)" Rais akawachukua Pinto na Trina na kuanza kwenda nao kwenye mlango wa watu maalumu huku nyuma, mabegi yao yakiwa yamebebwa na wafanyakazi wanne waliokuja na Rais.
"Ilibakia sekunde chache tuangamize watu wako." Pinto alimwambia Rais kwa kiingereza cha shida wakiwa ndani ya gari maalumu walilopanda watu watatu tu. Rais akiwa ndiye dereva.
"Nilichelewa kidogo tu. Samahanini sana." Rais aliomba msamaha na wote wakaupokea. Macho yao, Pinto na Trina, yakawa kwenye vioo vya gari walilopanda wakishangaa jiji la Dar es Salaam.
Baada ya saa moja, Rais alikuwa anawakaribisha Pinto na Trina katika Ikulu na moja kwa moja akawaongoza hadi chumba maalumu kwa ajili ya maongezi.
"Kwa taarifa nilizozipata, Masai anaonekana sana mida ya usiku katika maduka ya Mlimani City. Sasa mkianzia pale, nadhani mtapata nyama yenu bila wasiwasi. Si mnamtaka mzima tu! Nadhani atawasaidia sana kwenye upelelezi wenu." Rais aliongea kwa tabasamu pana akidhani watu wale wapo kwa ajili ya kumkamata Masai, kumbe kumuangamiza.
"Mlimani City ipo wapi." Trina aliuliza huku akitoa mawani yake na kumuangalia Rais kwa macho yake ya kahawia na ya kung'aa kama ya paka.
"Nitawapa dereva awatembeze ili mpajue kote huku." Rais aliongea huku akijichekesha chekesha.
"Fanya sasa hivi." Trina akaongea na kuvaa mawani yake tena kisha akaegemea kochi. Rais akanyanyua simu yake na kuipiga. Akaongea kwa Kiswahili kumpa maelekezo mtu aliyempigia.
Baada ya dakika mbili, akaingia jamaa kalivalia suti ya kupendeza. Akapewa ugeni alioitiwa na kuondoka nao.
Trina na Pinto walilitazama eneo zima la Mlimani City. Wakalichora sehemu zote muhimu na baada ya kumaliza, wakamuomba mwenyeji wao awatafutie hotel yenye hadhi maeneo yale.
Ndipo wakapelekwa kwenye hotel ambayo walipoiona, wakaikubali bila neno. Wakalipia kwa pesa za Marekani na kuchukua chumba cha juu ambacho waliweza kuona mengi ya chini kwa kutumia vifaa vyao.
****
Kundi la Malocha walishahamia kwenye nyumba ya Lisa na baada ya kuhamia, siku mbili mbele, nyumba yao ya Kivule ikivamiwa na wapelelezi walioagizwa kuwasaka. Lakini kwa bahati mbaya wakawakosa.
Bado waliendelea kucheza na mitambo yao na kamwe hawakuwa lelemama katika kusaka kinachoendelea. Kitu ambacho walikikosa, ni ujio wa Pinto na Trina ambao walishajua kuwa Masai anapenda sana kwenda Mlimani City usiku kwa ajili ya kununua mahitaji ya nyumbani lakini pia zawadi kwa Martina ambaye bado alikuwa hamtaki baba yake.
"Lisa." Masai alimuita mpenzi wake mida ya saa mbili usiku. Hiyo ni baada ya siku nne za Trina na Pinto kufika Tanzania.
"Abee switie." Lisa aliitika huku anakimbilia alipo Masai.
"Naenda Mlimani mara moja kuchukua mazaga ya hapa."
"Okay baby. Lakini na hiyo suti yako, harahara wasinipokonye huko." Lisa alitania kwa ile suti ya Masai ambayo alitoka nayo Italia. Hakuivaa tangu kipindi alipoharibu mipango ya Gunner.
"Hahahaaa. Hamna kitu kama hicho."Masai akamuhakikishia mpenzi wake na kumpa busu dogo la shavuni.
"Okay. Bye sweetie." Lisa alimuaga Masai aliyetoka katika chumba kile na kupita sebuleni ambapo pia aliwaaga rafiki zake kama alivomwambia Lisa.
****
Saa tatu, Masai alikuwa ameegesha gari lake nje ya maduka ya Mlimani City na kisha akavaa kofia yake ambayo haikuendana na suti. Alifanya hivyo ili asijulikane na watu hasa ukizingatia Masai anatafutwa kwa udi na uvumba.
Akiwa ameanza kuchagua hiki na kile mle dukani, wazungu wawili ambao walionekana ni wapenzi, waliingia na kuweka mabegi makubwa sehemu ya mapokezi na kisha kuchukua vitoroli maalumu vya kubebea bidhaa na kuanza kwenda kuchagua wavitakavyo.
Wakasogea hadi karibu na Masai, kisha wakawa wanacheka na saa nyingine wananyonyana ndimi zao. Masai hakuwatambua na wala hakuwafatilia, akawa anaendelea kuchagua bidhaa zake.
Wazungu wale wakaanza kuchagua bidhaa upande wa kushoto na Masai upande wa kulia, hivyo wakawa wamepeana migongo. Masai akasogea mbele kidogo na kisha akachagua kioo cha kujiangalia. Akakitazama na kukijaribu kwa kujiangalia. Akajiona ndevu zake alivozifuga ili asijulikane, akatabasamu na kuanza kukirudisha kioo kile.
Lakini kabla hajakishusha, alimuona yule mwanamke wa kizungu nyuma yake akiwa kakamata panga fulani lenye makali pande zote na alikuwa kalinyanyua juu tayari kwa kulishusha katika kichwa cha Masai.
Masai aliruka kwa pembeni na panga lile likamkosa na kukata kabati lililokuwa limebeba bidhaa. Alikuwa ni Trina ambaye kamkosa kwa panga Masai.
Masai akakaa mkao wa kupigana na wakati huo watu walikuwa wameanza kusogea kujionea kinachoendelea. Asivyotegemea Masai labda Trina atasogea yeye kupambana, akatokea mpenzi wake, Pinto ambaye aliruka sarakasi na kutua mbele ya Masai huku kakamata bunduki fupi (short gun) iliyokuwa na matundu mawili lakini imepunguzwa bomba za mbele na kuwa fupi zaidi kiasi kwamba wakaguzi wa duka lile hawakuiona. Pinto alikuwa kaielekeza kifuani kwa Masai na hakusita kuifyatua.
Ikamrusha Masai hatua sita nyuma lakini haikumuua wala kumdhuru kwa sababu ya suti aliyovaa.
Mlio wa short gun ile, ukawafanya wananchi kukimbia hovyo kwenda nje. Masai akanyanyuka haraka na kutaka kikimbia lakini mara viatu vyake vikachomwa na visu na kuvishikilia hapohapo chini. Ikabidi avivue na kubaki peku. Hadi anamaliza kuvivua, tayari Trina alishasogea na kurusha visu vidogo vinne. Masai akavizuia kwa mkono wa kushoto na kudunda juu ya suti yake matata.
Mambo yakawa mazito kwa Masai, alichofanya ni kubonyeza saa yake haraka na suti yake ikajifunga miguuni, kwenye viganja vya mikono na usoni.
Ile anageuka aangalie maadui zake, anakutana tena na midomo ya short gun iliyokuwa imelenga kichwani. Ngoma ikaachiwa tena na kumpaisha Masai mbali na pale aliposimama.
Akili ikamvurugika na maumivu aliyahisi. Akataka kunyanyuka akajikuta anadondokea makabati yenye bidhaa mle Mlimani City. Wakati anahaha na hayo, Trina alikuwa anakuja kwa kasi na kuruka teke lililomkuta kifuani Masai. Masai hoi mbele ya ile miili ya vijana wawili wanaopiga kwa mtindo wa ‘one by one’, yaani wanapigana kwa kuachiana.
Mwanaume akawa anagaa kwa maumivu tele, na sasa ilikuwa zamu ya Pinto kumshambulia. Katika hali ambayo haikutegemewa na kila mtu ambaye alikuwa anashuhudia mpambano ule, Pinto alikimbilia kwenye moja ya mabegi makubwa alilyokuja nayo. Akaingiza mkono wake ndani ya begi lake, na mara akachomoa bunduki nzito inayomwaga risasi karibu mia moja kwa dakika. Wanaiita Min Machine Gun. Ina mkanda wenye risasi zenye idadi kubwa.
Pinto akaikoki vema mbele ya Masai, na bila huruma alianza kumimina risasi zisizo na idadi. Ilitisha na kusikitisha hasa risasi zile zilivyokuwa zinajaribu kutoboa suti maridhawa ya Masai.
Baada ya dakika mbili, Pinto alitulia na kutazama hali ya windo lake. Masai akawa anagaa-gaa chini anashindwa kunyanyuka pale kwa sababu ya kuelemewa na anachofanyiwa.
Akiwa kama mtoto, akawa anatambaa kwa tumbo kuufuata mlango wa kutokea. Masai anajaribu kuokoa nafsi yake, anasikia nyuma yake sauti ya kitu kama injini ya gari dogo la kuchezea watoto. Kugeuka angalie japo kwa shida, anaona viatu vya Trina kwa mbele kuna visu ambavyo vinazunguka kwa kasi miguuni kwake.
Masai akaongeza kasi ya kutambaa kwa tumbo kwenda nje, lakini Trina akamuwahi kukandamiza usoni visu vile na kuvizungushia hapohapo bila huruma. Ni cheche tu ndizo ambazo zilikuwa zinamwagika. Haileweki ni vipi angekuwa huyu Masai kama asingekuwa na ile suti. Amshukuru aliyeitengeneza.
Hali ikazidi kuwa mbaya. Kizunguzungu kikamkumba yule mwanaume na taratibu akaanza kukubali kuwa anashindwa.
"Suti hii pia inaweza kutoa shoti ya umeme mikononi." Maneno ya Alejandro, aliyeitengeneza ile suti yakajirudia kichwani kwa Masai. "Kivipi sasa? Inatoaje hiyo shoti?" Masai akajiuliza bila kupata jibu. "Ngoja nijaribu." Masai akajishauri na kwa kuwa ndio uokozi pekee uliyokuwa umebaki, akajaribu kwa kuukamata mguu wa Trina. Lakini hakuna kilichotokea zaidi ya kazi ya vile visu vya miguuni kuendelea kuchimbua maski iliyoziba uso wake.
Ikabidi Masai aruke pembeni na kumuacha Trina akimfuta kwa kasi. Akaangalia saa yake na kuona kuna kitufe ambacho huwa hakitumii sana, kwa chini kimechorwa alama ya radi. Akakibonyeza na wakati huo Trina alikuwa kafika na viatu vyake.
Mtoto yule wa kike akarusha teke ambalo lilimkuta Masai kifuani. Masai akazidi kuvuruga bidhaa za duka lile kubwa kwa kuzipamia. Trina akaruka sarakasi na kutua juu ya kifua cha Masai, akawa kamkalia kifuani.
Akanyoosha mikono yake juu, na hapo vikachomoza visu virefu kiasi toka kwenye koti la mterezo alilolivaa. Akaanza kuvishusha kwa kasi kuelekea kifuani, hapo ndipo Masai akajaribu bahati yake kwa kunyoosha mikono yake miwili na kugusa kifua cha Trina. Bila kutegemea, Trina akarushwa na umeme mkali toka katika mikono ya Masai. Akarushwa hatua kumi nyuma na kilichomzuia ni ukuta wa uliozunguka mle ndani.
Pinto akashtuka hasa pale alipomuona mpenzi wake anakukuruka kama mtu mwenye degedege au kifafa.
"Shit." Pinto akatukana na kulivua koti lake. Sasa silaha zake baadhi zilizomzunguka mwili mzima, zikaonekana.
Akachomoa bunduki nyingine ya hatari toka mgongoni kwake. M16 naizungumzia. Akaikoki na kuanza kumwaga njugu kwa fujo kumuelekea Masai aliyekuwa bado hajarudisha nguvu ipasavyo. Baadhi ya risasi zilimpata lakini hazikumdhuru sana kwa sababu ya suti yake.
Risasi zikaisha kwenye M16. Pinto akatupa bunduki ile pembeni na kisha katika kifua chake, akanyofoa mabomu mawili yaliyokuwa yananing'inia. Akayarusha sehemu ambayo Masai alikuwa kalala. Pinto akaruka pembeni na Masai alisikia vyuma vikidunda chini ya sakafu ile ya Mlimani City, kutazama anaona mabomu yanakuja kwa haraka.
Mtoto wa kiume akapata nguvu za kunyanyuka na kwa kasi ya ajabu, akajirusha kwenye mlango wa kutokea ambao ni kioo tupu. Kikavunjika na Masai akawa nje wakati huo mabomu yakawa yanalipuka na kuzidi kuleta tatizo katika mtaa ule.
Baada ya mabomu yale kutulia, Pinto alinyanyuka na kuangalia kama kafanikiwa zoezi lake. Akatazama katika mlango wa kutokea, akaona gari likiondoka kwa kasi toka katika uzio wa duka lile. Alijua kuwa ni la Masai kwa sababu katika kumfuatilia, aliliona mara kwa mara Masai analiendesha.
"Bastardo (Mpumbavu)" Pinto akatema tusi dogo kwa lugha ya Kiitaliano. Akakimbilia pale alipo mpenzi wake na kumkuta kazimia. Akampiga makofi kadhaa na Trina akafungua macho yake na kumuangalia Pinto.
"Kakimbia yule mbwa?" Trina akamuuliza Pinto.
"Ndio. Tuondoke hapa haraka." Pinto alijibu na kumnyanyua Trina tayari kwa kuondoka eneo lile ambalo taratibu lilianza kunyemelewa na wanausalama.
****
Masai akiwa hana nguvu za kutosha, akawa anakimbiza gari lake kuelekea maeneo ya Sinza, makao mapya waliyohamia na washirika wake. Kwa bahati nzuri alifika salama na kushuka garini.
Aligonga mlango na Lisa ndiye aliyeufungua. Lisa akakutana na mwili wa Masai ambao hauna nguvu. Ukamdondokea taratibu lakini mtoto wa kike akamdaka na kuanza kuwaita wenzake.
ITAENDELEA
 
huu mzigo utaletwa mpaka mwisho au manake huwa naumia sana stori zinazoishia njiani. Plz tuhakikishie
 
Wakuu samahanini nilikuwa sina network leo kama kawaida mzigo unashushwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom