mtzmweusi
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 8,697
- 9,051
- Thread starter
- #61
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA TISA
"Nini kimetokea?" Swali la kwanza kulisikia Gunner baada ya simu ile kuipokea. Ilikuwa ni sauti nzito na inafanana na sauti ya redio iliyokwisha betri.
"Ni Masai." Gunner akajibu huku akitetema.
"Masai ndiye nani?" Sauti ile ikauliza kwa ukali na kumfanya Gunner kutojibu chochote. "Acha ujinga we mpumbavu. Nitakuua mimi. Umefanya ujinga ambao hutakiwi kusamehewa kosa lako." Ile sauti ilizidi kufoka.
"Hapana The Shadow. Tunaomba msamaha. Tupe nafasi nyingine tutafanya vema." Gunner alijitetea huku kijasho chembamba kikimtoka.
"Hakuna kitu kama hicho Gunner. Wote mtakufa kwa sababu ya huu ujinga." Mtu aliyeitwa The Shadow, aliongea na kumfanya Gunner kutulia bila kusema chochote. "Natuma watu wangu wawili hatari kuja huko kumuangamiza huyo kinyago wenu. Baada ya hapo, watakuja kuwamaliza nyie. Sitaki muingilie chochote wakati hawa watu wanafanya kazi yao." The Shadow alimaliza na Gunner akajibu sawa. Simu ikakatwa.
GENIVA, USWISI.
Jamaa wawili walikuwa wamesimama nyuma ya kiti kimoja ambacho kilikuwa kimewapa mgongo na sigara kubwa (cigar) ilionekana ikivutwa na moshi wake ukipulizwa juu.
Watu hawa hawakuweza kuona sura ya mtu huyo bali kuisikia sauti yake wakati inaongea na Gunner aliye nchini Tanzania.
"Pinto na Trina." The Shadow aliwaita wale watu bila kugeuka.
"Ndio The Shadow." Waliitika kwa sauti ya pamoja.
"Nawatuma Tanzania kwa kazi moja tu! Ya kuua. Kauweni kundi la mtu anayeitwa Masai." Alipoongea hayo, akarusha bahasha mezani lakini hakugeuka nyuma.
Msichana mmoja anayejulikana kwa jina la Trina, akasogea na kuichukua ile bahasha. Akaifungua na hapo akakuta picha kadhaa za Frank Masai na kundi lake lote.
"Hao wote wanatakiwa kufa. Lakini wa kwanza awe ni Masai. Kichwa chake nikione hapa." The Shadow akapiga pafu nzito kwa kuivuta cigar yake, kisha akapuliza moshi mzito angani.
"Baada ya kumaliza hawa wajinga wa Masai, malizeni na haya majinga mengine." Akatupa bahasha tena mezani na jamaa wa kiume kwa jina la Pinto, aliisogelea na kuifungua bahasha hiyo. Sura za wakina Gunner na Lobo zikaonekana katika picha zilizomo kwenye bahasha ile.
"Yametimia haya Boss." Sauti nzito ya Pinto ilijibu wote wawili, yaani Pinto na Trina, wakatoka kwenye ofisi ile ambayo ilikuwa inawaka mwanga wa bluu.
PINTO NA TRINA.
Pinto au alivyopenda kujiita El Pinto, alizaliwa nchini Mexico. Ana miaka ishirini na nne pekee (24) lakini amekwishaua watu thelathini wakiwemo viongozi wakubwa kumi na mbili. Hajawahi kushindwa kazi ambayo kapewa. Mataifa makubwa yote yamewahi kumtumia huyu kijana na mafanikio yake yalikuwa makubwa kuliko walivyotaraji.
Mwili mdogo kama kawaida ya Wamexico wengi, uliwafanya wale wanaowindwa kudharau kazi ya yule bwana.
Ni mkali wa kutumia silaha za moto. Mwili wake wote hujaza silaha hizo jambo linalofanya asishindwe mpambano wowote. Licha ya kuwa mkali wa silaha hizo za moto (mfano bunduki), pia hakuwa nyuma katika mapambano ya uso kwa uso. Ana mapigo ambayo yanaweza kumfanya adui akimbie bila kupenda.
Historia ya wazazi wake, iliishia pale alipowaua wote kwa sababu ya wao kukubuhu katika kuvuta madawa ya kulevya na kusahau kabisa mahitaji mengine ya familia. Hasira ambazo alikuwanazo Pinto, aliweza kumng'ata baba yake kwenye koo hadi akanyofoa koromeo lake.
Mama yake ambaye alikuwa kalewa madawa, alimchinja kwa kisu kikali kinachotumika jikoni kwa ajili ya kukatia nyama. Baada ya mauaji hayo, Pinto akachukuliwa na kundi la wahuni wa Mexico ambao walimfumdisha njia mbalimbali za kuishi kama muhuni. Katika njia hizo, kamwe hakuwahi kujihusisha na uvutaji wa madawa wala bangi. Kilevi chake kikubwa kilikuwa ni Trina.
Trina yeye katokea nchi ya Italia. Anamiaka ishirini na mbili (22). Kishatekeza roho zipatazo arobaini na tano za watu wakubwa kwa wadogo, matajiri kwa masikini. Yeye yupo kimaslahi zaidi. Ukitaka kazi yako.ifanyike bila kero, mlipe pesa zake zote, majibu utayapata baada ya masaa ishirini na nne.
Yeye kaua watu wengi kuliko Pinto kwa sababu ya uzuri wake ambao uliwafanya mabosi wanaomtuma waamini kuwa unaweza kuwateketeza maadui zao bila shida. Trina alisifika zaidi katika kucheza na silaha zenye ncha kali kama visu, mapanga na silaha za kininja. Pia hakuwa nyuma katika mapigano ya viungo na kutumia sumu. Trina alikuwa vema sana katika kazi yake.
Wazazi wa Trina waliuawa huko Italia na kundi la Mafia baada ya baba yake nna Trina kukutaa kujichinja kwa kosa la kutosambaza madawa ya kulevya katika kituo cha watoto yatima. Hali hiyo ndio ikawapa hasira Mafia na wakaamua kuiteketeza familia nzima ya Trina akiwepo Dada yake aliyekuwa na umri wa miaka sita kipindi hicho. Trina akiwa na miaka mitatu, aliweza kuona mauaji hayo akiwa kwenye kabati alipofichwa na baba yake.
Trina akaishi kwa upweke muda mrefu baada ya familia yake kuuawa. Akawa mtoto wa mitaani huku akiwa na boksi dogo aliloweka baadhi ya picha za wazazi wake na zawadi mbalimbali alizowahi kupewa. Alipotimiza miaka saba, akawa si Trina tena bali Trina wa hatari. Aliweza kuishi katika mtaa wowote kwa amani au kwa vurugu. Japo hakuwa mkali sana katika mapambano ya viungo, lakini aliposhika silaha kali, aliweza kunyamazisha kila ambaye alitaka kuingia anga zake. Aliwahi kumchana mgongo kwa kiwembe mkuu wake anayempa madawa ya kulevya akauze kisa hakukamilisha malipo sahihi ya kazi aliyopewa. Pia aliwahi kukata nyeti za bwana mmoja mtu mzima aliyekuwa akitaka kumuingilia kinguvu mwilini. Na baada ya kukata nyeti hizo kwa kisu kikali, akakinga damu ya baba lile jitu zima na kuinywa.
Sifa hizo na nyingine nyingi, ndizo ziliwafikia Mafia na kuamua kumchukua yule mtoto pasipokujua wamemchukua mtoto wa nyoka waliyemuua.
Baada ya Mafia kumfunza na kumuivisha kwa kila kitu, ndipo Trina akatoa picha fulani ambayo kwa nyuma iliandikwa "Hawa ndiyo adui zako, wauwe ukipata nafasi."
Mwandiko huo wa baba yake, ndiyo ulikuwa muda wa kuufanyia kazi. Akaingia hadi kule anapotaka na kisha akaua maadui zake wote. Baada ya hapo, akapotea kabisa nchini Italia.
Ilikuja kuonekana akiwa na miaka kumi na minane nchini Japan. Alikuwa binti tajiri kuliko binti yeyote pale Japan. Alimiliki miradi mbalimbali iliwemo vituo vya matangazo na viwanda kadhaa vya magari. Mali zote zilikuwa za baba yake na yeye aliziongeza kwa kazi yake ya kuua.
Alipotumwa nchini Hispania kwenda kumuua mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa, ndipo alipokutana na Pinto ambaye yeye alikuwa na jukumu la kuiba siri za usalama wa taifa. Wakiwa hawajuani, wote wakaajiriwa kama wapelelezi katika nchi ile. Kilichokuja kuwaunga, ni pale Trina alipomkamata Pinto anaiba siri nzito za Hispania. Na wakati anamkamata, yeye tayari alikuwa amekwishamuua mkuu wa upelelezi kama alivyoagizwa.
Walichofanya hawa watu ni kutoroka kwa pamoja na baadaye wakaungana na kuwa marafiki wakubwa hadi kufikia kuitwa wapenzi.
Sasa The Shadow kawatuma wapenzi hawa waje Tanzania kummaliza Frank Masai na kundi lake. Masai hajui kama kuna mpango wa yeye kuangamizwa na wakati huo taarifa zinazagaa kuwa kafika Tanzania na anaendesha ugaidi kama kulipua ndege kwenye Bahari ya Hindi na kulipua jengo la usalama wa taifa na kuua wapelelezi kumi na mbili wakuokuwepo katika jengo hilo. Tanzania yote ikabandikwa matangazo na picha za Masai kama " The Most Wanted".
Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vikatapakaa picha nne zikiwatuhumu watu hao kuwa ni magaidi wa kutisha. Picha ziliwaonesha Mubah, Malocha, Lisa na Masai kama ndio tatizo la nchi ya Tanzania.
Rais alishasema mengi kuhusu hawa watu na akaweka vizuizi kadhaa juu ya watu hawa. Lakini tatizo ambalo walikuwa nalo wengi wa wapelelezi, ni kutojua watawapatia wapi watuhumiwa hawa. Ni vigumu kuwapata kwa sababu wanavifaa vingi vya kuzuia mawasiliano yao yasifike sehemu nyingine na zaidi, kabla hujawafikia, tayari wanakuwa wamekwishajua hilo.
"Masai. Ndio kama hivyo kaka, tunasakwa kwa ugaidi. Tuwe makini tu." Mubah aliongea baada ya kuzima runinga iliyokuwa ikionesha taarifa zao.
"Usijali Mubah. Hapa hamna atakayekamatwa. Cha msingi ni kuondoka hii sehemu." Masai alitoa ushauri.
"Twende wapi sasa." Malocha aliuliza.
"Kuna nyumba ya Lisa kule Sinza, nadhani ni sehemu nzuri ya sisi kujificha." Frank akatoa wazo.
"Haa! Yaani twende kule katikati ya jiji tena? Masai unatafuta kukamatwa." Mubah aliongea kama anapinga kauli ile.
"Siku zote penye watu ndipo pa kujificha. Usitegemee simba kutafutwa mjini, anatafutwa porini Mubah. Sisi tunawindwa, lazima watuwindie nje ya mji. Sasa kama hamuamini, subirini siku mbili tu. Mtasikia tumevamiwa, na huyo Rais wa Urusi kaondoka kachukia balaa, lazima alete watu wake watusake."
"Okay. Upo sawa Masai. Ngoja Lisa atoke tuongee naye." Malocha alimaliza maongezi ya asubuhi ile kwa kumsubiri Lisa ambaye bado alikuwa chumbani kalala na mwanaye.
****
"Lobo. Unajua The Shadow kawatuma Pinto na Trina." Gunner alikuwa akimpa taarifa mtu wake wa kazi.
"Kwa hiyo." Lobo akauliza huku akinoa kisu chake chenye meno upande mwingine.
"Wakiwamaliza wakina Masai, ni zamu yetu. Na unawajua wale, hawajawahi kushindwa vita."
"Umewahi kumsikia Masai kashindwa vita? Hata ya makundi ya kigaidi na kipelelezi. Kawahi kushindwa?"
"Sawa, hajawahi kushindwa lakini angalia na uwezo wa wakina Pinto. Angalia watu waliwaondoa, ni tofauti na aliowaua Masai."
"Trina na Pinto, walipata kazi gani katika mauaji yao? Wao ni watu wa kumendea tu! Hata mimi hawaniwezi. Wale ni watu wa kusubiri mtuhumiwa wao atoke sehemu ndio wamvamie. Lakini mimi, nakupa taarifa kuwa ndani ya masaa ishirini na nne au siku kadhaa, uwe umefanya hivi au vile, usipofanya naku kraa." Lobo akaweka ishara ya kuchinja shingoni kwa kutumia kisu chake.
"Kwa hiyo wewe hawakutishi hata kidogo?" Gunner akamuuliza Lobo.
"Watanitisha nikikutana nao uso kwa uso. Lakini tukiwindana, watakufa wao mapema tu."
"Unadhani Masai atafanikiwa kuwazima hawa?"
"Uzuri wa Masai anavitu vingi anavyowazidi wale. Wale wanatumia silaha za moto na vitu vyenye ncha kali, Masai ni mkali wa vyote hivyo. Pia Masai anaweza mapigano ya ana kwa ana na anaweza kuwinda pia, vitu ambavyo hao Pinto na Trina wanavyo kwa mmoja mmoja. Lakini tatizo la hao watu wa The Shadow, hawana mbinu za kisheria, Masai akisema nitakuwa hapo dakika moja ijayo, basi jiandae kumpokea. Hawa hawana sumu hizo. Akikutana na Pinto, atacheza naye kwa visu na mapanga. Pinto hawezi hiyo. Akikutana na Trina, atacheza naye kwa bunduki na bastola, unadhani nani atashindwa?" Lobo akampa ufafanuzi yakinifu Gunner.
"Ndio maana The Shadow kawatuma wote wawili. Unadhani Masai atapona?"
"Masai hajui kama hawa watu wanakuja, hilo ni tatizo kubwa sana na atapata shida kuwazuia. Lakini angekuwa anajua kuwa wanakuja, angewamalizia hukohuko kwao."
"Kwa hiyo tumwambie au? Unajua wakifa wale na sisi tutapona."
"Gunner. Acha uoga. Ile si vita yetu, subiri wamalizane na Masai ije zamu yetu. Tutacheza na sheria tu. Watoto wadogo wale, wala hawana tatizo. Na Masai namjua tangu zamani sana, nimesoma naye na kupambana naye. Acha uoga tu!" Lobo aliongea kwa kujiamini.
"Okay. Ila Masai asipouawa na hawa, nitamuua mwenyewe, naapa kwa MUNGU. Bahati yake tumesimamishwa." Lobo akawa mtu wa kutabasamu kwa maneno yale ya Gunner, hadithi zao zikaishia hapo. Gunner akatoka kwenda kuvuta sigara, Lobo akabaki kitini anaendelea kunoa kisu chake.
****
WIKI MOJA MBELE. UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM.
Ndege binafsi lakini kubwa kiasi, ikatua katika uwanja ule kwa mbwembwe zake zote. Pembeni iliandikwa PITRI yaani Pinto na Trina, na kulembwa na rangi za kijani na nyekundu, rangi ambazo zinapatikana kwenye bendera za Italia na Mexico.
Hakuna aliyejua maana ya neno lile la PITRI kwa hapa Tanzania. Hivyo waliiacha ndege ile itulie ndipo wawaangalie wageni wake.
Baada ya dakika tano za ndege ile kutua, wakashuka vijana wa kizungu wawili wakiwa wamevalia suti nyeusi na makoti makubwa juu yake.
Yule wa mbele alitazama huku na huko kabla hajatoka pale mlangoni na kumpisha wa nyuma yake ambaye naye macho yake yakaitazama nchi ya Tanzania vema. Akavaa mawani yake nyeusi na kisha akaanza kushuka katika ngazi za ndege ile ghali.
Wakiwa na mabegi yao kila upande, wakafika sehemu ya ukaguzi na kuyatupia mabegi hayo kwenye vifaa maalum vya kukagulia na wao wakapita kwenye mlango wa ukaguzi bila wasiwasi.
Mabegi yalipita salama, ila wao walivyopita taa nyekundu iliyoambatana na mlio wa hatari, kwa pamoja vilitoa ishara kuwa watu wale wamebeba vitu vya vyuma.
"It's my belt. (Ni mkanda wangu)" Pinto aliongea huku akivua mkanda wenye bakoni kubwa kama wapendavyo kuvaa wamexico wengi. Akauweka juu ya meza ya idara ile na kupita tena lakini bado sauti na taa ile vilitoa ishara tena.
ITAENDELEA
SEHEMU YA KUMI NA TISA
"Nini kimetokea?" Swali la kwanza kulisikia Gunner baada ya simu ile kuipokea. Ilikuwa ni sauti nzito na inafanana na sauti ya redio iliyokwisha betri.
"Ni Masai." Gunner akajibu huku akitetema.
"Masai ndiye nani?" Sauti ile ikauliza kwa ukali na kumfanya Gunner kutojibu chochote. "Acha ujinga we mpumbavu. Nitakuua mimi. Umefanya ujinga ambao hutakiwi kusamehewa kosa lako." Ile sauti ilizidi kufoka.
"Hapana The Shadow. Tunaomba msamaha. Tupe nafasi nyingine tutafanya vema." Gunner alijitetea huku kijasho chembamba kikimtoka.
"Hakuna kitu kama hicho Gunner. Wote mtakufa kwa sababu ya huu ujinga." Mtu aliyeitwa The Shadow, aliongea na kumfanya Gunner kutulia bila kusema chochote. "Natuma watu wangu wawili hatari kuja huko kumuangamiza huyo kinyago wenu. Baada ya hapo, watakuja kuwamaliza nyie. Sitaki muingilie chochote wakati hawa watu wanafanya kazi yao." The Shadow alimaliza na Gunner akajibu sawa. Simu ikakatwa.
GENIVA, USWISI.
Jamaa wawili walikuwa wamesimama nyuma ya kiti kimoja ambacho kilikuwa kimewapa mgongo na sigara kubwa (cigar) ilionekana ikivutwa na moshi wake ukipulizwa juu.
Watu hawa hawakuweza kuona sura ya mtu huyo bali kuisikia sauti yake wakati inaongea na Gunner aliye nchini Tanzania.
"Pinto na Trina." The Shadow aliwaita wale watu bila kugeuka.
"Ndio The Shadow." Waliitika kwa sauti ya pamoja.
"Nawatuma Tanzania kwa kazi moja tu! Ya kuua. Kauweni kundi la mtu anayeitwa Masai." Alipoongea hayo, akarusha bahasha mezani lakini hakugeuka nyuma.
Msichana mmoja anayejulikana kwa jina la Trina, akasogea na kuichukua ile bahasha. Akaifungua na hapo akakuta picha kadhaa za Frank Masai na kundi lake lote.
"Hao wote wanatakiwa kufa. Lakini wa kwanza awe ni Masai. Kichwa chake nikione hapa." The Shadow akapiga pafu nzito kwa kuivuta cigar yake, kisha akapuliza moshi mzito angani.
"Baada ya kumaliza hawa wajinga wa Masai, malizeni na haya majinga mengine." Akatupa bahasha tena mezani na jamaa wa kiume kwa jina la Pinto, aliisogelea na kuifungua bahasha hiyo. Sura za wakina Gunner na Lobo zikaonekana katika picha zilizomo kwenye bahasha ile.
"Yametimia haya Boss." Sauti nzito ya Pinto ilijibu wote wawili, yaani Pinto na Trina, wakatoka kwenye ofisi ile ambayo ilikuwa inawaka mwanga wa bluu.
PINTO NA TRINA.
Pinto au alivyopenda kujiita El Pinto, alizaliwa nchini Mexico. Ana miaka ishirini na nne pekee (24) lakini amekwishaua watu thelathini wakiwemo viongozi wakubwa kumi na mbili. Hajawahi kushindwa kazi ambayo kapewa. Mataifa makubwa yote yamewahi kumtumia huyu kijana na mafanikio yake yalikuwa makubwa kuliko walivyotaraji.
Mwili mdogo kama kawaida ya Wamexico wengi, uliwafanya wale wanaowindwa kudharau kazi ya yule bwana.
Ni mkali wa kutumia silaha za moto. Mwili wake wote hujaza silaha hizo jambo linalofanya asishindwe mpambano wowote. Licha ya kuwa mkali wa silaha hizo za moto (mfano bunduki), pia hakuwa nyuma katika mapambano ya uso kwa uso. Ana mapigo ambayo yanaweza kumfanya adui akimbie bila kupenda.
Historia ya wazazi wake, iliishia pale alipowaua wote kwa sababu ya wao kukubuhu katika kuvuta madawa ya kulevya na kusahau kabisa mahitaji mengine ya familia. Hasira ambazo alikuwanazo Pinto, aliweza kumng'ata baba yake kwenye koo hadi akanyofoa koromeo lake.
Mama yake ambaye alikuwa kalewa madawa, alimchinja kwa kisu kikali kinachotumika jikoni kwa ajili ya kukatia nyama. Baada ya mauaji hayo, Pinto akachukuliwa na kundi la wahuni wa Mexico ambao walimfumdisha njia mbalimbali za kuishi kama muhuni. Katika njia hizo, kamwe hakuwahi kujihusisha na uvutaji wa madawa wala bangi. Kilevi chake kikubwa kilikuwa ni Trina.
Trina yeye katokea nchi ya Italia. Anamiaka ishirini na mbili (22). Kishatekeza roho zipatazo arobaini na tano za watu wakubwa kwa wadogo, matajiri kwa masikini. Yeye yupo kimaslahi zaidi. Ukitaka kazi yako.ifanyike bila kero, mlipe pesa zake zote, majibu utayapata baada ya masaa ishirini na nne.
Yeye kaua watu wengi kuliko Pinto kwa sababu ya uzuri wake ambao uliwafanya mabosi wanaomtuma waamini kuwa unaweza kuwateketeza maadui zao bila shida. Trina alisifika zaidi katika kucheza na silaha zenye ncha kali kama visu, mapanga na silaha za kininja. Pia hakuwa nyuma katika mapigano ya viungo na kutumia sumu. Trina alikuwa vema sana katika kazi yake.
Wazazi wa Trina waliuawa huko Italia na kundi la Mafia baada ya baba yake nna Trina kukutaa kujichinja kwa kosa la kutosambaza madawa ya kulevya katika kituo cha watoto yatima. Hali hiyo ndio ikawapa hasira Mafia na wakaamua kuiteketeza familia nzima ya Trina akiwepo Dada yake aliyekuwa na umri wa miaka sita kipindi hicho. Trina akiwa na miaka mitatu, aliweza kuona mauaji hayo akiwa kwenye kabati alipofichwa na baba yake.
Trina akaishi kwa upweke muda mrefu baada ya familia yake kuuawa. Akawa mtoto wa mitaani huku akiwa na boksi dogo aliloweka baadhi ya picha za wazazi wake na zawadi mbalimbali alizowahi kupewa. Alipotimiza miaka saba, akawa si Trina tena bali Trina wa hatari. Aliweza kuishi katika mtaa wowote kwa amani au kwa vurugu. Japo hakuwa mkali sana katika mapambano ya viungo, lakini aliposhika silaha kali, aliweza kunyamazisha kila ambaye alitaka kuingia anga zake. Aliwahi kumchana mgongo kwa kiwembe mkuu wake anayempa madawa ya kulevya akauze kisa hakukamilisha malipo sahihi ya kazi aliyopewa. Pia aliwahi kukata nyeti za bwana mmoja mtu mzima aliyekuwa akitaka kumuingilia kinguvu mwilini. Na baada ya kukata nyeti hizo kwa kisu kikali, akakinga damu ya baba lile jitu zima na kuinywa.
Sifa hizo na nyingine nyingi, ndizo ziliwafikia Mafia na kuamua kumchukua yule mtoto pasipokujua wamemchukua mtoto wa nyoka waliyemuua.
Baada ya Mafia kumfunza na kumuivisha kwa kila kitu, ndipo Trina akatoa picha fulani ambayo kwa nyuma iliandikwa "Hawa ndiyo adui zako, wauwe ukipata nafasi."
Mwandiko huo wa baba yake, ndiyo ulikuwa muda wa kuufanyia kazi. Akaingia hadi kule anapotaka na kisha akaua maadui zake wote. Baada ya hapo, akapotea kabisa nchini Italia.
Ilikuja kuonekana akiwa na miaka kumi na minane nchini Japan. Alikuwa binti tajiri kuliko binti yeyote pale Japan. Alimiliki miradi mbalimbali iliwemo vituo vya matangazo na viwanda kadhaa vya magari. Mali zote zilikuwa za baba yake na yeye aliziongeza kwa kazi yake ya kuua.
Alipotumwa nchini Hispania kwenda kumuua mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa, ndipo alipokutana na Pinto ambaye yeye alikuwa na jukumu la kuiba siri za usalama wa taifa. Wakiwa hawajuani, wote wakaajiriwa kama wapelelezi katika nchi ile. Kilichokuja kuwaunga, ni pale Trina alipomkamata Pinto anaiba siri nzito za Hispania. Na wakati anamkamata, yeye tayari alikuwa amekwishamuua mkuu wa upelelezi kama alivyoagizwa.
Walichofanya hawa watu ni kutoroka kwa pamoja na baadaye wakaungana na kuwa marafiki wakubwa hadi kufikia kuitwa wapenzi.
Sasa The Shadow kawatuma wapenzi hawa waje Tanzania kummaliza Frank Masai na kundi lake. Masai hajui kama kuna mpango wa yeye kuangamizwa na wakati huo taarifa zinazagaa kuwa kafika Tanzania na anaendesha ugaidi kama kulipua ndege kwenye Bahari ya Hindi na kulipua jengo la usalama wa taifa na kuua wapelelezi kumi na mbili wakuokuwepo katika jengo hilo. Tanzania yote ikabandikwa matangazo na picha za Masai kama " The Most Wanted".
Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii vikatapakaa picha nne zikiwatuhumu watu hao kuwa ni magaidi wa kutisha. Picha ziliwaonesha Mubah, Malocha, Lisa na Masai kama ndio tatizo la nchi ya Tanzania.
Rais alishasema mengi kuhusu hawa watu na akaweka vizuizi kadhaa juu ya watu hawa. Lakini tatizo ambalo walikuwa nalo wengi wa wapelelezi, ni kutojua watawapatia wapi watuhumiwa hawa. Ni vigumu kuwapata kwa sababu wanavifaa vingi vya kuzuia mawasiliano yao yasifike sehemu nyingine na zaidi, kabla hujawafikia, tayari wanakuwa wamekwishajua hilo.
"Masai. Ndio kama hivyo kaka, tunasakwa kwa ugaidi. Tuwe makini tu." Mubah aliongea baada ya kuzima runinga iliyokuwa ikionesha taarifa zao.
"Usijali Mubah. Hapa hamna atakayekamatwa. Cha msingi ni kuondoka hii sehemu." Masai alitoa ushauri.
"Twende wapi sasa." Malocha aliuliza.
"Kuna nyumba ya Lisa kule Sinza, nadhani ni sehemu nzuri ya sisi kujificha." Frank akatoa wazo.
"Haa! Yaani twende kule katikati ya jiji tena? Masai unatafuta kukamatwa." Mubah aliongea kama anapinga kauli ile.
"Siku zote penye watu ndipo pa kujificha. Usitegemee simba kutafutwa mjini, anatafutwa porini Mubah. Sisi tunawindwa, lazima watuwindie nje ya mji. Sasa kama hamuamini, subirini siku mbili tu. Mtasikia tumevamiwa, na huyo Rais wa Urusi kaondoka kachukia balaa, lazima alete watu wake watusake."
"Okay. Upo sawa Masai. Ngoja Lisa atoke tuongee naye." Malocha alimaliza maongezi ya asubuhi ile kwa kumsubiri Lisa ambaye bado alikuwa chumbani kalala na mwanaye.
****
"Lobo. Unajua The Shadow kawatuma Pinto na Trina." Gunner alikuwa akimpa taarifa mtu wake wa kazi.
"Kwa hiyo." Lobo akauliza huku akinoa kisu chake chenye meno upande mwingine.
"Wakiwamaliza wakina Masai, ni zamu yetu. Na unawajua wale, hawajawahi kushindwa vita."
"Umewahi kumsikia Masai kashindwa vita? Hata ya makundi ya kigaidi na kipelelezi. Kawahi kushindwa?"
"Sawa, hajawahi kushindwa lakini angalia na uwezo wa wakina Pinto. Angalia watu waliwaondoa, ni tofauti na aliowaua Masai."
"Trina na Pinto, walipata kazi gani katika mauaji yao? Wao ni watu wa kumendea tu! Hata mimi hawaniwezi. Wale ni watu wa kusubiri mtuhumiwa wao atoke sehemu ndio wamvamie. Lakini mimi, nakupa taarifa kuwa ndani ya masaa ishirini na nne au siku kadhaa, uwe umefanya hivi au vile, usipofanya naku kraa." Lobo akaweka ishara ya kuchinja shingoni kwa kutumia kisu chake.
"Kwa hiyo wewe hawakutishi hata kidogo?" Gunner akamuuliza Lobo.
"Watanitisha nikikutana nao uso kwa uso. Lakini tukiwindana, watakufa wao mapema tu."
"Unadhani Masai atafanikiwa kuwazima hawa?"
"Uzuri wa Masai anavitu vingi anavyowazidi wale. Wale wanatumia silaha za moto na vitu vyenye ncha kali, Masai ni mkali wa vyote hivyo. Pia Masai anaweza mapigano ya ana kwa ana na anaweza kuwinda pia, vitu ambavyo hao Pinto na Trina wanavyo kwa mmoja mmoja. Lakini tatizo la hao watu wa The Shadow, hawana mbinu za kisheria, Masai akisema nitakuwa hapo dakika moja ijayo, basi jiandae kumpokea. Hawa hawana sumu hizo. Akikutana na Pinto, atacheza naye kwa visu na mapanga. Pinto hawezi hiyo. Akikutana na Trina, atacheza naye kwa bunduki na bastola, unadhani nani atashindwa?" Lobo akampa ufafanuzi yakinifu Gunner.
"Ndio maana The Shadow kawatuma wote wawili. Unadhani Masai atapona?"
"Masai hajui kama hawa watu wanakuja, hilo ni tatizo kubwa sana na atapata shida kuwazuia. Lakini angekuwa anajua kuwa wanakuja, angewamalizia hukohuko kwao."
"Kwa hiyo tumwambie au? Unajua wakifa wale na sisi tutapona."
"Gunner. Acha uoga. Ile si vita yetu, subiri wamalizane na Masai ije zamu yetu. Tutacheza na sheria tu. Watoto wadogo wale, wala hawana tatizo. Na Masai namjua tangu zamani sana, nimesoma naye na kupambana naye. Acha uoga tu!" Lobo aliongea kwa kujiamini.
"Okay. Ila Masai asipouawa na hawa, nitamuua mwenyewe, naapa kwa MUNGU. Bahati yake tumesimamishwa." Lobo akawa mtu wa kutabasamu kwa maneno yale ya Gunner, hadithi zao zikaishia hapo. Gunner akatoka kwenda kuvuta sigara, Lobo akabaki kitini anaendelea kunoa kisu chake.
****
WIKI MOJA MBELE. UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM.
Ndege binafsi lakini kubwa kiasi, ikatua katika uwanja ule kwa mbwembwe zake zote. Pembeni iliandikwa PITRI yaani Pinto na Trina, na kulembwa na rangi za kijani na nyekundu, rangi ambazo zinapatikana kwenye bendera za Italia na Mexico.
Hakuna aliyejua maana ya neno lile la PITRI kwa hapa Tanzania. Hivyo waliiacha ndege ile itulie ndipo wawaangalie wageni wake.
Baada ya dakika tano za ndege ile kutua, wakashuka vijana wa kizungu wawili wakiwa wamevalia suti nyeusi na makoti makubwa juu yake.
Yule wa mbele alitazama huku na huko kabla hajatoka pale mlangoni na kumpisha wa nyuma yake ambaye naye macho yake yakaitazama nchi ya Tanzania vema. Akavaa mawani yake nyeusi na kisha akaanza kushuka katika ngazi za ndege ile ghali.
Wakiwa na mabegi yao kila upande, wakafika sehemu ya ukaguzi na kuyatupia mabegi hayo kwenye vifaa maalum vya kukagulia na wao wakapita kwenye mlango wa ukaguzi bila wasiwasi.
Mabegi yalipita salama, ila wao walivyopita taa nyekundu iliyoambatana na mlio wa hatari, kwa pamoja vilitoa ishara kuwa watu wale wamebeba vitu vya vyuma.
"It's my belt. (Ni mkanda wangu)" Pinto aliongea huku akivua mkanda wenye bakoni kubwa kama wapendavyo kuvaa wamexico wengi. Akauweka juu ya meza ya idara ile na kupita tena lakini bado sauti na taa ile vilitoa ishara tena.
ITAENDELEA