Riwaya-duka la roho

RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI
Nywele ndefu zikavurugika na kupepea hewani baada ya kofia lile kuvuuka.
"Ooh! Ni Zakia. Nadhani mwisho wako unaishia hapa leo. Umekutana na Israel mtoa roho,mbwa jike wee." Malocha hakuwa na maneno mengi mdomoni mwake, akakimbia kwa mwendo wa hatua za karibu~karibu lakini za haraka na Zakia bila kutambua, alikuta mtoto wa kiume yupo naye uso kwa uso.
Ngumi za haraka toka kwa Malocha zilitiririka kwenda usoni kwa Zakia kabla hajamalizia kwa ngumi nyingine nzito ya kidevu iliyomrusha yule mwanamke hadi karibu na bunduki yake. Zakia kwa haraka akaishika bunduki yake tayari kwa kuinyanyua, lakini haraka yake haikuwa kitu mbele ya kasi ya Malocha.
Tayari mwanaume alikuwa kafika na kuikanyaga ile bunduki. Zakia akashangaa kuona kiatu kizuri cha harusi kikiwa kimekanyaga bunduki yake. Akaangalia juu na kumshuhudia dume la mbegu likiwa ndani ya suti mwanana kana kwamba yupo harusini, na kumbe mapambanoni.
Teke lingine la kidevu likatua kwa Zakia na kumsukuma hadi kwenye gari la Malocha ambalo alikuwa kaliharibu kwa risasi zake.
Zakia akasimama tayari kwa mpambano wa ana kwa ana maana mbinu za kuchukua silaha yake zilishindikana. Akawa kakunja ngumi tayari kwa mpambano mkali. Lakini kwa bahati mbaya alikuwa kasimama karibu na mlango wa gari la Malocha ambapo Lisa alikuwa sehemu hiyo.
Na Lisa hakufanya kosa la kipumbavu kama wengi wanavyodhani. Kwa nguvu zake za kike, akausukuma ule mlango na kumkumba Zakia ambaye alipiga yowe la maumivu na kusukumika mbele ambapo Malocha alikuwepo. Hapo naye Malocha aliruka teke zito likamkuta yule mwanamke kwenye shingo na kumgongesha tena kwenye mlango wa gari. Zakia akiwa kakubali yaishe, Malocha ndio kwanza alikuwa kafunguliiwa.
Akamfata palepale na kuanza kumpa ngumi nyingi zilizoanzia kwenye tumbo zikafata kifuani, shingoni na kumalizikia kwenye paji la uso ambapo ngumi ile ilimfanya Zakia ajigonge kisogo kwenye gari la Malocha.
Damu zikaruka kama kuku aliyechinjwa, lakini Malocha hakuona kama inatosha, akamdaka na kumkaba vilivyo Zakia na kilichofuata ni kumvunja shingo mwanamke yule.
"Shit." Malocha aliongea neno hilo huku akitema mate pembeni baada ya kuuacha mwili wa Zakia ukiwa hauna uhai tena.
"R. I. P Zakia." Sauti ya Lisa ilisikika nayo, huku akifungua mlango wa gari yao iliyoshambuliwa.
"Tuondoke hapa haraka Lisa." Malocha aliongea hayo huku akiifuata ile pikipiki ya Zakia na kuiwasha. Lisa ambaye alikuwa karudiwa na nguvu, naye akaenda na kukwea nyuma ya pikipiki hiyo.
Lisa akaangalia maskani yake kwa mara ya mwisho, hapo akamuona Gunner akitoka nje ya nyumba yao na macho yake yakaenda kwenye gari la Malocha. Akakimbia na ghafla alikuwa kama kaishiwa nguvu baada ya kuuona mwili wa Zakia ukiwa hauna uhai.
Gunner akaufuata ule mwili na kisha kwa uchungu akaupakata na kulia kwa sauti ya juu. Wakati huo pikipiki inayoendeshwa na Malocha, ilishatimua vumbi na kuacha tafulani pale mtaani.
Gunner akaangalia pikipiki aliyokuwa anaendesha Malocha ambayo sasa ilikuwa inakata kona kuingia mtaa mwingine mbali na pale. Gunner akauma meno kwa hasira kisha akaanza kupiga ngumi chini. Akaona hiyo haitoshi, akaifata ile bunduki ya Zakia na kuijaza risasi, kisha kwa fujo akaanza kumwaga risasi hizo angani. Ni kama alikuwa kachanganyikiwa kwa sababu ya kifo cha Zakia.
Baada ya risasi kuisha, akausogelea mwili wa Zakia na kuutazama tena huku machozi yakimtoka zaidi ya pale. Lakini kulia siyo suluhisho la tatizo kwa mwanaume yeyote. Na yeye alijua hilo, akatwaa simu ya Zakia aliyokuwanayo mfukoni na kisha akabofya namba kadhaa na kuweka sikioni.
"Haloo Lobo. Wamemuua Zakia." Gunner akaongea na kutulia kusikiliza upande wa pili.
"Ni Malocha na Lisa ndio wamefanya hivi." Gunner akajibu tena na kumsikiliza Lobo.
"Okay. Nataka umuue Lisa. Huyu Malocha nitamuua mimi. Nenda kule nyumba ya shambani, Zakia kampeleka Martina kule. Kichukue hicho kifisadi na kukileta hapo kambini, mimi nipo njiani naanza kuja huko ili tupange." Gunner aliongea kwa hasira huku akianza kuondoka eneo lile akimuacha Zakia palepale alipofia.
Akaenda kwenye gari lake ambalo lilikuwa mbali na nyumbani kwake kwa sababu angeliweka karibu, basi mkewe angelisikia pale wakati anataka kutoroka. Gunner akawasha gari lile na kutitia sehemu nyingine.
****
Majira ya saa mbili usiku, vyombo vya habari hasa vya matangazo ya runinga, vilikuwa vikionesha taarifa ya masamaria mwema kuuawa na magaidi hatari waliokuwa hawajulikani kama magaidi bali wananchi wa kawaida.
Picha ya Zakia kama msamaria huyo, ilioneshwa kwenye runinga na baadaye zikapita picha za Malocha na Lisa kama magaidi hatari yaliyoondoa roho ya Zakia.
"Nasema hivii. Watu hawa hatari, watakamatwa na watahukumiwa hadharani adhabu ya kinyongo. Tunatoa taarifa kwa wananchi wote, kama utawaona watu hawa, toa taarifa kituo cha usalama chochote, nasi tutakuzawadia zawadi nono ya pesa taslimu. Usikose zawadi hii kwa kuyaficha haya ........." Runinga ikazimwa na Malocha baada ya kuitathmini ile taarifa iliyokuwa unasomwa na Kamanda wa Polisi Kanda ya Mashariki.
"Wapumbavu hawa. Wamekwisha wekwa dukani na roho zao. Uoga umekithiri katika nafsi zao. Shenzi kabisa." Malocha aliongea na kuendelea kutakana matusi mbalimbali mbele ya Lisa aliyekuwa kakaa kwenye kitanda na mawazo tele yakimzonga.
Walishafika nyumba ya Kivule na sasa walikuwa wametulia wakitafakari ili na lile hasa kwa kilichotokea muda uliopita.
"Malocha. Martina wangu. Sijui nitampataje mwanangu. Naomba mnisaidie jamani." Lisa aliongea kwa uchungu na chozi la uchungu wa mwana likamtiririka mwanamke huyu.
"Usijali Lisa. Hawawezi kumfanya chochote na tutampata tu. Najua tumekwisha wachokoza, sasa hivi wanapanga cha kufanya ili watuvute twende. Huo ndio utakuwa wakati wa kumwokoa Martina. Hawawezi kumdhulu." Malocha aliongea kwa kumsugua sugua bega binti yule na kwa faraja hiyo, alijikuta akimkumbatia Malocha.
"Usijali Lisa. Everything will be alright." Malocha kwa kunong'ona akambembeleza Lisa ambaye kama mama wengine ambavyo wangekuwa na wasiwasi kuhusu watoto wao, basi na yeye yupo vivyo hivyo.
Baada ya dakika kumi na tano, usingizi wa mchoko na maumivu ambayo yalitokana na kipigo toka kwa Gunner, ukamkamata Lisa na bila hiyana akaruhusu usingizi huo uwe kulala.
Malocha akamfunika vema Lisa na kisha akatoka nje ya chumba kile na kuelekea sebuleni ambapo alimkuta Mubah katika hamasa kubwa ya kutaka kujua nini kilitokea hadi mchumba wake akawa hai na kuwa anashirikiana na wakina Lobo.
"Niambie Malocha. Nini kipo katikati hadi tunaanzisha mahusiano na magaidi halafu hata hamtumbii." Mubah alikuwa anaongea kwa kufoka.
"Ulisahau jana wakati unataka kumuambia Lisa habari za Gunner, nami nilikuambia, jambo usilolijua ni sawa na usiku wa kiza." Malocha kwa makini akamwambia Mubah na kisha akaenda kwenye kochi moja na kukaa kisha akakunja nne kabla hajaanza kuutikisa mguu wake uliojuu ya mwingine kwa chati.
"Kwa hiyo ulikuwa unajua kuwa Zakia ni mbwa wa wakina Lobo." Mubah alimuuliza Malocha kwa kumtolea macho haswa.
"Ndio. Na si wewe tu. Karibu kila mfanyakazi mle FISSA, anamahusiano na gaidi. Lakini magaidi hawa si kama wanashirikiana na wakina Lobo, sema wapo kwa ajili ya dharula tu. Kama hivyo Zakia amekufa, basi anachukuliwa mwingine." Malocha akamjibu Mubah ambaye kwa hasira akaupiga kofi ule mguu wa Malocha uliokuwa unatingishika. Akaona haitoshi, akaushusha kwa nguvu mguu ule chini na kumfanya Malocha atabasamu tu.
"Hakuna GPS iliyotumika kuifata familia yako. Ni Zakia ndiye aliyetoa taarifa kwa Lobo ni wapi walipopelekwa. Na wakati huo mimi nilikuwa sijui kama Zakia pia anamahusiano na Lobo. Nilijua baada ya kufuatilia mawasiliano yote ambayo Lobo alikuwa akiyafanya. Na baadaye nikafuatilia ya Zakia na hadi hapa jana, nilikuwa nayafatilia.
Hakuna mwanamke ambaye alikuwa anapendana na Gunner kama Zakia. Gunner alikuwa anampenda huyu mwanamke mpaka kero na ndio maana nikamuua ili kumpandisha mori yule mbwa." Malocha alizidi kutiririka ukweli wakati huo Mubah alikuwa anamuangalia kwa macho ya hasira.
"Kwa hiyo wajua mengi tu. Mbona hukutuambia wewe mtu. Unakuwa mchoyo wa taarifa za muhimu kama hizi? We ni mtu gani Malocha." Mubah alibwata kama mbwa aliyeona sura asiyoifahamu.
"Mapenzi upofu, Mubah. Ulikuwa kipofu kipindi kile. Ningekwambia kuwa Gunner anatoka na mchumba wako, usingeamini na zaidi ungeniona mchonganishi. Hiyo yote ni kwa sababu ulikuwa umependa. Na isingetokea kwako tu, hata kwa Lisa." Mubah akatafakari na kuyachambua maneno hayo na kuona undani wenye ukweli kuhusu hilo.
Akapunguza jazba na kukaa kwenye kochi huku kajiinamia.
"Lakini Mkuu, ungeniambia tu! Ningekuwa makini japo ni kweli nilikuwa nampenda huyu mshenzi."
"Ukishakuwa ndani ya mapenzi, ni sawa na kuwepo ndani ya pango lenye giza na hujui wapi pa kutokea wala wapi pa kushika. Unaweza kuisikia sauti inaita, lakini hujui pa kuanzia ili uiombe msaada.
Ungesikia nilichokwambia, lakini ungekuwa huna uwezo wa kuamini." Malocha akazidi kuufunua ukweli ambao ulikuwa ni kiza kinene mbele ya macho ya Mubah.
"Nimekuelewa sana Mkuu. Lakini naomba safari hii, aliyeshiriki kuangamiza familia yangu, huyu Lobo, msimuue. Nahitaji kumuua mimi mwenyewe kwa risasi zenye idadi ya familia yangu." Mubah aliongea kwa hamasa na kumfanya Malocha akubaliane na ombi hilo. Swali likabaki, wataweza?
****
Mida ya saa nne usiku, ndani ya kambi kubwa ya Gunner iliyopo katika pori moja huko nje kidogo ya Jiji Dar es Salaam, watu kadhaa walikuwa kwenye chumba cha kompyuta wakijaribu kutafuta mawasiliano ya Malocha. Ilikuwa ngumu sana kwani safari hii Malocha hakuwa tayari kufuatiliwa kama wakati yupo ndani ya FISSA. Lobo alijaribu kumbembeleza Martina ili aseme ni wapi wapo wakina Malocha, lakini mtoto yule alikuwa hana uhakika wa akisemacho. Mara tulienda sokoni, mara barabara inamaji, mara tukapanda na kushuka daraja, haeleweki. Huko ndio kuelekeza alikokuwa anaelekeza Martina.
"Boss." Sauti nzito na yenye ukatili ndani yake ilimuita mkuu wake.
Alikuwa ni kijana mrefu na mwenye misuli na asili ya Kirusi ilikuwa imemtapakaa kila sehemu ya mwili wake.
Gunner akasogea pale alipoitwa na mtaalamu yule aloyekuwa nguli wa kompyuta katika kambi ile.
"Tumekosa mawasiliano ya hawa watu kwa njia hii." Jamaa yule alijibu kwa uhakika na kumfanya Gunner kutulia kwa sekunde kadhaa akitafakari jambo huku akikuna kidevu chake chenye ndevu za kiasi na zimechongwa kwa ufahamu na mtaalamu sijui kutoka wapi.
Macho ya Gunner yalikuwa hayatulii katika anga la jumba lile lililokuwa limetapakaa nyaya za umeme mkali ambao waliutengeneza wenyewe kwa kutumia madini hatari ya sumu ya Yellowstone. Haijulikani madini hayo ya njano yanachimbwa wapi, lakini ni madini yanayoweza kuwa hatari kuliko hata Uranium.
"Fungua SGT." Maneno hayo yakamfanya yule mtaalam wa TEHAMA kubaki akimshangaa mkuu wake kwa maamuzi mazito kama hayo.
"Mkuu. Lakini ni mapema sana kufungua SGT. Tutakamatwa mapema sana kabla ya mpango wetu kukamilika." Yule mtaalam akatoa wazo lake.
"Nimeshasema Boyka. Just Do It." Yule bwana aliyejulikana kwa jina Boyka akaamua kufanya alichoambiwa.
Akafungua mtambo ghali kabisa duniani ambao uliibwa toka mikononi mwa Wachina na watu wasiojulikana na ulikuwa unaogopwa na yeyote ambaye anahusika uhalifu, uliweza kunasa wahalifu karibu sitini baada ya kuindwa.
SGT (Satellite GPS and Traces). Ni mtambo ambao unaweza kuzima Satellites zote duniani na vifaa vyote vinavyoweza kufuatwa kama vina GPS. Hapa nazungumzia simu, kompyuta na vifaa vyote viwezavyo kutumia Internets.
ITAENDELEA
 
hahaaa unamoyo sana mkuu ngoja nikuongeze moja
Tunapenda hadithi zinatuliwaza sana tofauti na kizazi cha sasa wengi hupenda wenyewe wakiita ubuyu ni tofauti kubwa sana ndugu nashukuru kwa kujua nina njaa na story hii mdogomdogo pana watu watajaa hapa muda si mrefu niamini nimesoma story nyingi za nje na za nyumbani hadithi yako ina mpangilio mzuri
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
"Mkuu. Lakini ni mapema sana kufungua SGT. Tutakamatwa mapema sana kabla ya mpango wetu kukamilika." Yule mtaalam akatoa wazo lake.
"Nimeshasema Boyka. Just Do It." Yule bwana aliyejulikana kwa jina Boyka akaamua kufanya alichoambiwa.
Akafungua mtambo ghali kabisa duniani ambao uliibwa toka mikononi mwa Wachina na watu wasiojulikana na ulikuwa unaogopwa na yeyote ambaye anahusika uhalifu, uliweza kunasa wahalifu karibu sitini baada ya kuindwa.
SGT (Satellite GPS and Traces). Ni mtambo ambao unaweza kuzima Satellites zote duniani na vifaa vyote vinavyoweza kufuatwa kama vina GPS. Hapa nazungumzia simu, kompyuta na vifaa vyote viwezavyo kutumia Internets.
Mtambo huu, Gunner akishirikiana na wenzake baadhi kuuiba. Waliuiba kwenye Chuo cha Sayansi kilichopo nchini China baada ya kukamilika kufanyiwa majaribio na kuwa tayari kutumika kwa ajili ya kuiba siri mbalimbali hasa za kipelelezi.
Marekani walipopata sifa za mtambo huo, udenda ukawatoka na kutaka kuumiliki. Wakatengeneza mtambo wao mdogo kutokana na wazo walilopewa na Wanasayansi wao wakuu. Mtambo walioutengeneza waliuita Ant-SGT. Yaani hata wakiwasha STG mtambo huo hauwezi kuzima na unaweza kuungwa kwenye kompyuta zaidi ya trilioni duniani. Lakini kwa kuwa Marekani ni wa binafsi na wanataka SGT uwe wao, wakaamua kuwapa FBI ili wautafute mtambo ulioibwa na Gunner.
Sifa nyingine ya hatari kuhusu SGT, unaweza kuangamiza eneo ambalo wanalishuku linawaharifu. Inamvuto wa hatari ambao umetengezwa kwa madini ya Uranium. Mvuto huo upo kama sumaku au nguvu ya ukinzani, ukichomoka, huwa kama upepo na sifa yake huaribu kwa kulipua eneo zima lililotakiwa kuharibiwa.
Sifa mbaya ya Ant-SGT, mtambo uwezao kuufatilia SGT mahala ulipo, wenyewe huweza kung'amua SGT upo wapi baada ya dakika tatu za mtambo huo kuwaka.
Tatizo hilo, kundi la Gunner ulilitambua na ndio maana hakuwa na shaka sana kuhusu akifanyacho.
Boyka akaanza kubofya vitufe vingi vilivyo kwenye kiparaza (keyboard) cha kompyuta yake anayoitumia.
Mara eneo la nje ya jumba lile kukasikika mtikisiko mkubwa ambao unafanana na tetemeko la ardhi.
Baada ya mtikisiko huo, ardhi ya eneo lile ilifunguka na mwanga mkali ukaangaza eneo lile na kuonekana kama mchana na kumbe ni usiku wa saa tano kasoro.
Baada ya hali hiyo kutulia, ikasikika sauti nyingine kama ya ndege kubwa ya Rais wa Marekani ikipaa au kutua. Sekunde kadhaa ya karaha hiyo ya sauti kubwa, kikachomoka kitu toka katika mlango ule uliofunguka na kwenda angani ambapo kilitawanyika na kutoa vitu kama kambakamba za umeme ambazo zilitengeneza duara na kufunika eneo zima ambalo Gunner alikuwa kaliwekea makazi.
Hiyo yote ilikuwa ni katika kulinda mtambo huo wa SGT na eneo zima ili wanaoutafuta wasiweze kuupata.
"Una dakika mbili za kutafuta nachokitaka." Gunner alimwambia Boyka ambaye naye kwa haraka akaanza kubonyeza kiparaza cha kompyuta yake kwa haraka kuliko kawaida. Hata dakika mbili hazikuisha, tayari alikuwa kamaliza kazi aliyoambiwa lakini alipata mawasiliano ya simu ambayo alikuwa anaitumia Malocha. Aliipata kwa sababu simu ilikuwa wazi na alipoitazama vizuri simu hiyo aligundua kuwa inakifaa ambacho ni kazi kufuatilia mawasiliano yake kikawaida. Hivyo mtambo wa SGT ulikuwa umefaulu vema mtihani wake.
"Safi Boyka. Funga mtambo haraka." Gunner akampongeza mtaalam wake na kubofya vitufe kadhaa na kile kitu kilichoruka angani, kikarudi mahala pake na lango lile la ardhini likajifunga kwa njia ileile ya kelele na tetemeko.
****
NCHINI VATICAN, ITALIA.
Upande wa Dar es Salaam, masaa yalisomeka ni saa nne au saa tano kasoro usiku wakati mtambo wa SGT unafunguliwa lakini kwa upande wa Jiji la Vatican lililopo nchini Italia, ilikuwa ni saa Tatu au saa nne kasoro usiku kwa sababu Tanzania imepishana na Vatican masaa mawili nyuma.
Chumba kimoja cha hoteli iitwayo Aspereado kulikuwa na miili miwili yenye jinsia tofauti ikiendelea kupalangana katika kitanda cha hoteli hiyo. Mwanaume mwenye rangi nyeusi alikuwa anataabisha maungio yake ya kiume katika kiuno chembamba lakini kilichobeba mwili wenye mvuto. Ni miguno ya mapenzi ndio iloyokuwa inaendelea wakati hayo yote yakijiri.
Wakati wakiendelea kupeta katika dunia ya mapenzi kwenye Jiji lenye ulinzi mkali kuliko yote ya dunia hii, mara sauti kali ilianza kulia kutoka kwenye droo ya kitanda wanachokitumia. Yule bwana mweusi kwa haraka akaacha shughuli yake ya uzinzi na kufungua droo hiyo ambayo alitoa saa ikiwa inalia mlio huo. Akaibofya bofya kwa pembeni na ghafla macho yake yakajawa na mshangao mkubwa kwa alichokiona.
"They're opening SGT. (Wamefungua SGT)" Jamaa yule alijisemea huku akitabasamu.
"Quello che hai fatto? (Umesemaje?)" Yule mwanamke akamuuliza yule jamaa kwa lugha ya Kiitaliano.
"Lo sposerò, Veronica. (Nitakuoa, Veronica)" Jamaa yule alijibu huku akimuangalia Veronica, binti wa Kiitalia asiyeelewa Kiingereza. Binti ambaye anasoma Chuo cha Utawa cha pale Vatican, lakini kadondoka kwenye penzi zito la kijana yule mweusi, na sasa hataki tena Utawa bali kuolewa na yule mweusi, japo rangi hiyo inadharirika sana nchini humo.
"Ma stai scherzando, Pirlo? (Unanitania, Pirlo?)" Binti yule alikuwa haamini yale aliyoyasikia na kujikuta akimuuliza swali hilo Bwana Pirlo.
"Sicuro che dico, Veronica. (Ukweli nakwambia Veronica)" Pirlo alimjibu Veronica na kumfanya binti yule amrukie kifuani Pirlo na kisha kwa mbwembwe akaanza kumlamba Pirlo huku na huko na kilichoendelea hapo ni mapenzi tu.
****
"Pirlo, Pirlo svegliati (Pirlo, Pirlo, amka)" Veronica alikuwa akimuamsha kwa sauti ya chini Pirlo ikiwa ni asubuhi matata ya saa moja. "Mio Papà è qui, in cerca di mi. (Baba yangu yupo hapa, ananitafuta mimi)" Pirlo kusikia hivyo, akakurupuka haraka na kuvaa suruali yake. Wakati anaanza kuvaa shati lake mara mlango wa chumba walichopanga ukaanza kugongwa kwa nguvu.
"Aprire la porta bastardo (Fungua mlango we' mpumbavu)" Sauti ilisikika ikifoka kwa hasira mlangoni na wakati huo Pirlo aliinama uvunguni na kuchukua viatu vyake aina ya raba na kuviweka mguuni kabla hajachukua saa yake na kuivaa mkononi.
Pirlo alipomaliza, akamfata Veronica na kisha akaanza kunyonya ulimi wake kwa hamasa.
"Mi mancherai tanto, Veronica (Nitakukumbuka sana, Veronica)" Pirlo alimwambia Veronica.
"Anch'io, Pirlo. (Nami pia, Pirlo)" Wakanyonyana tena ndimi zao na mara mlango ukaanza kufunguliwa kwa kusukumwa kama unataka kuvunjwa.
"Andare veloce, vai Pirlo. ( Ondoka haraka, nenda Pirlo)" Veronica alimwambia Pirlo na Pirlo kwa haraka akakimbilia katika dirisha la chumba kile na kuanza kutoka. Alipofika dirishani, akabusu mkono wake na kupuliza busu lile kwenda kwa Veronica aliyekuwa kavaa gauni laini la kulalia hadi matiti yake machanga yakawa yameinua gauni hiyo na kuleta hamasa kwa kila jicho la mwanaume.
Pirlo akaruka kwa ustadi na kutua dirisha la chini yake kwa sababu walikuwa katika ghorofa ya saba, yeye na Veronica.
Akaruka tena kwenda chini na kutulia kwenye chumba kilichopo katika ghorofa ya tano. Hapo akafungua dirisha la chumba hicho na kuingia ambapo waenyeji waliokuwa katika kustarehesha miili yao walishtuka na kujikunyata pembezoni mwa kitanda chao.
"Scusate.( Samahani)" Pirlo aliongea hayo huku akiwa na tabasamu pana na kuwapita wale vijana kisha kwenda katika mlango wa chumba kile na kutoka. Akaenda kupanda lift ambayo ilimshusha hadi chini na kisha akatoka nje ya hoteli na kuchukua gari yake aina ya Ferrari Gt rangi nyekundu, na kupotea eneo lile.
Kule juu alipomuacha Veronica, mlango ulivunjwa na kuingia Mzee mmoja aliyekuwa kavalia suti ya kijivu na nywele zake za kichwani zikiwa nyeupe huku ndevu zake kaweka brichi ya kijivu upande mmoja, na mwingine kaziacha na weusi wake. Aliingia kakamata bastola yake aina ya revolva pamoja na vijana wawili ambao nao walikuwa na silaha nzito. Walimkuta Veronica akiwa kakaa dirishani akimpungia Pirlo mkono baada ya kufanikiwa kufika chini.
"Dov'è questo bastardo? (Yupo wapi huyu mpumbavu)" Yule mzee aliuliza huku akianza kufunua kitanda cha kile chumba wakati huo Veronica akionekana mwenye kununa kama kakosewa sana.
"Papà, perché stai facendo questo? (Baba, kwa nini unafanya hivi?)" Veronica alimuuliza baba yake na mzee yule akamuangalia na kumuona yupo katika vazi ambalo si sahihi kwa.watu kumuona vile hasa wale alioingia nao.
Akawaangalia wale vibaraka wake, wote wakaonekana wenye kutazama maungio mwanana ya Veronica. Hasira zikamshika yule mzee na kujikuta akiwafukuza wale jamaa wote mle ndani.
"Samahani mwanangu, nilipata taarifa.kuwa upo na mwanaume humu ndio maana nikaja kuhakikisha." Mzee yule alimuomba msamaha mwanaye huku kaangalia pembeni. Veronica akawa anamzomea kwa nyuma kana kwamba yule si baba yake, hakika ilikuwa kituko hasa kwa sababu mtu mwenye hela na msomi kama baba wa Veronica anasumbuliwa na muhuni kama Pirlo.
"Nenda nje. Nashuka baada ya kuvaa." Veronica alimuamuru baba yake ambaye haraka alitoka nje ja kwenda sehemu ya kusubiria wageni.
Veronica akatoka akiwa kavalia mavazi ya Kitawa kama wavaavyo wanachuo wa chuo chao na kisha akachukuliwa na baba yake huku akijiona bora sana kwa kuushinda mpango ule.
*****
DAR ES SALAAM SAA SITA USIKU.
Simu ya Malocha iliita na haraka akaipokea kwa sababu ilikuwa ni namba binafsi imepiga (Private Number). Akamwambia yule opareta wao aiunge ili kila mmoja aliyekuwamo mle ofisini aisikie. Kama alivyotegemea alikuwa ni Gunner na kwa makini akaanza kuongea.
"Hey Malocha." Alisalimia.
"Pole kwa msiba Gunner." Malocha alikejeli.
"Naomba niongee na mke wangu."
Hapohapo Malocha akamtuma Mubah akamuite Lisa.
Lisa alipokuja, Gunner akaanza kuongea kilichompigisha simu.
"Nadhani sasa umekwishajua mimi ni nani. Lakini kosa kubwa ambalo utalijutia, ni kumuua mwanamke nimpendaye kuliko wewe malaya mkubwa. Sasa nitakachokifanya, ni kumuachia Lobo kazi ya kufanya." Gunner akamaliza na kisha akamkabidhi simu John Lobo, mtu ambaye hajui kuhusu huruma, ukisikia hadithi azisimuliazo, utamkimbia. Zote uhusu kuua na mauaji pekee. Sasa simu kakibidhiwa yeye.
"Lisa, kuna machaguo mawili pekee katika haya. Kuuza au Kununua roho ya Martina. Ukitaka kununua roho ya mwanao, njoo mwenyewe tutakapokwambia. Ukitaka kuuza roho ya mwanao, usije tutakapokwambia. Roho yake itakuwa halali yangu.
Una masaa ishirini na nne Lisa kuanzia sasa.
CHAGUO NI LAKO, TICK TOCK." Simu ikakatwa baada ya maneno na sura ya Lisa ilikuwa katika kijasho chembamba.
Ni kumbate dogo kutoka kwa Malocha ndilo lilimtoa katika mateso ya fikra Lisa ambaye kichwa chake chote kilijawa na woga kuhusu kifo cha mwanaye. Alikuwa haelewi ni vipi atamuokoa mtoto wake toka mikononi mwa mikono ya Gunner na alikuwa hajui ni wapi ataanzia kuongea ili sauti yake ipokelewe katika masikio ya mwenye uweza wa yote.
"Ee MUNGU, naomba uniondolee kikombe hiki kizito kilichokuwa mbele yangu. Wajua siwezi bila wewe na siwezi kufanya chochote bila ya uweza wako. Kama malipo ya dhambi ni haya, basi naomba niyalipie mimi lakini si roho ya mwanangu. Nipo tayari kufa lakini naomba roho ya mwanangu uiokoe baba." Lisa aliongea hayo kwa uchungu na kuwafanya wanaume wote mle ndani kukabwa na donge la uchungu kwenye makoo yao.
"Lisa." Malocha aliita huku akiwa kumkumbatia. "Ni kheri nife mimi kuliko wewe au Martina. Nipo tayari kuitoa roho yangu ili ninyi nyote mpone. Hakuna ambaye atakufa baada ya masaa ishirini na nne."
"Nimempoteza Mjomba wangu kipenzi kwa mkono Lobo. Nimuonapo Martina nahisi kama namuona Mjomba wangu. Sitakuwa tayari kumpoteza Martina kama nilivyompoteza Mjomba wangu. Nitakuwa nawe Lisa." Mubah aliongea kwa sauti ya hamasa na kuonekana mwenye utayari kwa lolote lile.
"Sijawahi kuingia mapambanoni. Huu ndio muda wangu wa kufanya hivyo. Nitakuwa nyuma yako Lisa." Opareta wa mitambo wa Malocha alisimama na kuungana na wakina Lisa waliokuwa wanafarijiana.
"Mimi pia. Naingia katika mpambano." Jamaa mwingine akakamilisha kundi la watu watano ambao waliweka mikono yao katika umoja na kisha kwa pamoja wakatamka. "Kwa Martina na Lisa." Sauti hizo zikawapa amsha katika mioyo yao na mpango kabambe wa kumuokoa Martina ukaanza papo hapo.
ITAENDELEA
 
Gunner
akamaliza na kisha akamkabidhi
simu John Lobo, mtu ambaye
hajui kuhusu huruma, ukisikia
hadithi azisimuliazo, utamkimbia.
Zote uhusu kuua na mauaji pekee. Sasa simu kakibidhiwa
yeye

ha ha ha ha...!! asante sana mkuu keep going nazidi kuipenda simulizi hii
 
Wapenda hadithi watafika hapa muda si mrefu na wataanza kukusumbua kwa hamu zao endelea kudondosha vitu tunakoelekea utata mwingi .
 
Sorry wakuu itaendelea saa 4 nilikuwa bize kidogo afu kifaa nachotumia chaji iliisha
 
Sorry wakuu itaendelea saa 4 nilikuwa bize kidogo afu kifaa nachotumia chaji iliisha
mkuu jitahidi muda huo uweke maana wengine tuko fasta ktk kuread, halafu tayari weekend sasa natumai utashusha mzigo wakutosha
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Sitakuwa tayari kumpoteza Martina kama nilivyompoteza Mjomba wangu. Nitakuwa nawe Lisa." Mubah aliongea kwa sauti ya hamasa na kuonekana mwenye utayari kwa lolote lile.
"Sijawahi kuingia mapambanoni. Huu ndio muda wangu wa kufanya hivyo. Nitakuwa nyuma yako Lisa." Opareta wa mitambo wa Malocha alisimama na kuungana na wakina Lisa waliokuwa wanafarijiana.
"Mimi pia. Naingia katika mpambano." Jamaa mwingine akakamilisha kundi la watu watano ambao waliweka mikono yao katika umoja na kisha kwa pamoja wakatamka. "Kwa Martina na Lisa." Sauti hizo zikawapa amsha katika mioyo yao na mpango kabambe wa kumuokoa Martina ukaanza papo hapo.
****
TURIN, ITALIA.
Pirlo baada ya kutoroka salama kule Vatican, alichukua ndege binafsi na kwenda moja kwa moja katika Jiji lingine la marah, Jiji la Turin. Si kama alienda huko kwa ajili ya raha, bali alienda kwa ajili ya taarifa maalumu ya alichokipata usiku wa kuamkia siku hiyo.
Akaingia katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro lililopo hapo Turin na kisha akakaa kwenye viti vya kanisa hivyo na kupiga ishara ya msalaba kwa kutazama sanamu ya Bikira la Maria iliyokuwa imembeba mtoto mdogo na shingo yake ikiwa imepindia kushoto kuonesha huruma ya Mama huyo.
Ndani ya kanisa kulikuwepo na watu sita pekee wakionekana wenye kufanya sala za toba baada ya maungamo yao. Pirlo alikuwa katika sala fupi za kujiandaa kabla hajaenda kwenye maungamo.
Ilikuwa ni kawaida yake kufanya maungamo kila Alhamisi, na alikuwa anafanya maungamo hayo katika kanisa moja tu! Ambalo alikuwepo muda huo. Japo pia alikuwa anafanya maungamo hayo katika kanisa hilo, pia alikuwa anafanyia kwenye kijumba kilekile kila akienda. Na muda wa saa saba ndio ulikuwa muda wake wa kufanya maungamo hayo.
Ilipotimu saa saba kamili, akaenda kwenye kijumba hicho maalumu na kupiga magoti tayari kwa maungamo.
"Father. I need to go back in Tanzania. (Baba. Nahitaji kurudi Tanzania)" Pirlo aliongea hayo baada ya kupiga ishara ya msalaba.
"Why? (Kwa nini?)" Yule Padri akamuuliza swali Pirlo. Pirlo akaanza kumuhadithia kila kitu alichokisikia na kukiona.
Wakati yupo kwenye ndege binafsi akielekea Turin, Pirlo alitoa kompyuta yake mpakato na kisha akavua saa yake ambayo ilikuwa inagonga kengere usiku wa jana yake. Kwenye saa hiyo, akachomoa kitu kidogo kama memori kadi lakini hakikuwa memori kadi kwa sababu chenyewe waweza kukiwasha na kukizima.
Akakiwasha na kisha akakichoneka katika kifaa maalumu ambacho hutumika kuchomekea memori kadi. Akaingiza kifaa hicho kwenye kompyuta yake mpakato na kuperuzi kila kitu kilichoonekana mle kwenye kile kifaa alichokitoa kwenye saa. Hapo akaanza kuona tukio zima ambalo limefanyika nchini Tanzania hasa baada ya ule mtambo wa SGT kufunguka. Akaona eneo zima ambapo mtambo ule ulikuwepo na akaona ni nani anamiliki mtambo huo.
Pia akaona kazi uliyoifanya ya kutafuta namba fulani ambayo ni za Malocha na kisha baada ya kuipata, mtambo ule ulifungwa.
Pirlo hakuishia hapo, katika kile kifaa, pia akafanikiwa kudaka maongezi yaliyofanyika katika namba ile iliyochukuliwa na SGT. Pirlo akapumua pumzi ndefu na akawa hana raha baada ya kugundua nia ya wale watu.
Akafunga kompyuta yake mpakato na kutulia. Kisha akili yake akaihamishia China alipowahi kusomea Sayansi.
SHANGHAI, CHINA.
Kulikuwa kuna jopo la wanafunzi wapatao kumi katika chumba kimoja cha kufanya majaribio ya Kisayansi. Katika wanafunzi hao kumi ambao walionekana akili yao wameegemeza kwenye kutengeneza kitu fulani, kulikuwa kuna mweusi mmoja tu!
Mweusi huyo alijiita Hyung Sheing. Wenzake walijuwa historia yake kuwa alikuwa anaasili mbili, ya Kichina na Kimarekani. Hyung aliwaambia kuwa baba yake ni Mchina lakini Mama yake ni Mmarekani mweusi ambaye alifariki pindi anamleta yeye duniani. Pia akawaambia wenzake kuwa baba yake aliondoka duniani wakati yeye anamiaka kumi tu! Aliishi katika uyatima hadi alipopata mfadhili akiwa na miaka kumi na mitano, na ndiye anayemsomesha hadi muda huo akiwa na miaka ishirini na saba.
Historia hiyo ikawafanya wenzake na wanafunzi wote kumuona wa kipekee na kuwa naye bega kwa bega ili atimize ndoto zake za kuwa mwanasayansi mkubwa duniani.
Na ndoto hiyo ndiyo alikuwa anaifanyia kazi siku hiyo ambapo jopo la wanafunzi wenzake lilikuwa likitengeneza mtambo uliyoitwa Satellite GPS Traces (SGT). Baada ya kuumaliza mtambo huo, waliujaribu na kuona unafaa sana kwa ajili ya kufanya kazi za kipelelezi na nyingine nyingi zenye manufaa na zisizo na manufaa.
Lakini japo pia walifanikiwa kuutengeneza mtambo ule, Hyung akatoa wazo kuwa watengeneze kitu ambacho kitaweza kuufatilia mtambo huo kwa chochote utakachofanya. Wengi walikataa wazo hilo kwa sababu kazi waliyopewa na shirika la kipelelezi la China, walikwisha imaliza. Lakini hawakumkatisha tamaa, wakampa formula zote ambazo wameutengenezea mtambo ule, kisha wakamuacha peke yake katika maabara ile.
Hyung akaanza kuunda kitu ambacho kitaufatilia mtambo ule. Tangu saa sita mchana hadi saa nane za usiku, Hyung alikuwa bado anatengeneza kifaa hicho ambacho hakutaka kiwe kikubwa sana. Ndipo mida ya saa kumi usiku, akafanikiwa kumaliza kazi yake na kuijaribu. Kweli kifaa chake kikakubali punde tu, mtambo wa SGT ulipofunguliwa. Akaenda mbali zaidi kwa kuchunguza mambo mbalimbali ya duniani na kwa kile kifaa alichokitengene
za, kikadaka yote hayo. Na ndiyo hiyo saa ambayo sasa anaimiliki Pirlo aliyekuwapo Italia.
Ni kwa nini saa anayo Pirlo? Hili ndilo jibu.
Baada ya kuumaliza ule mtambo na wanafunzi waliofanikisha suala hilo kutunukiwa vyeti maalumu kabisa akiwemo Hyung, mtambo huo ukachukuliwa na kuanza kupelekwa katika shirika la kipelelezi huku Hyung akiwa hajawaambia wenzake wala mtu yeyote kuwa kafanikiwa kutengeneza kifaa kitakachoufatilia mtambo ule.
Kukiwa na ulinzi hafifu wakati mtambo huo mkubwa unapelekwa kwenye idara ya upelelezi China, mbele ya gari lililoubeba mtambo huo, ilitokea gari nyingine kubwa zaidi na kuanza kuishambulia gari yenye mtambo. Haikupita muda, gari hilo likawa kimya na walinzi wote wakiwa maiti.
Kundi la watu wasiojulikana, wakashuka toka garini na kufungua gari lile kubwa lililobeba mtambo. Walipohakiki kuwa kuna mali yao, wakaita helkopta waliyoiandaa na kushusha sumaku kubwa ambayo ilinasa kwenye mtambo ule wenye ukubwa wa duara lile la katikati kwenye uwanja wa mpira lakini kwenda juu mtambo ule ni mrefu zaidi. Helkopta ikauchukua mtambo huo na kutitia nao pasipojulikana.
Baada ya patashika hiyo, ndipo kundi hilohilo, likapewa amri nyingine ya kwenda kuwaangamiza wanafunzi wote walioshiriki kuutengeneza mtambo ule. Wanafunzi karibu wote walipoteza maisha yao kasoro Hyung ambaye alichezwa na chale mapema na kuamua kukimbilia Italia ambapo huko alibadili jina na kujiita Pirlo.
****
"Kwa hiyo unaondoka lini." Padri alimuuliza Pirlo baada ya kusikiliza yote yaliyotokea.
"Leoleo. Natakiwa kufika kule kabla ya saa nne." Pirlo akajibu na yule Padri akamwambia aende chumba fulani kwa ajili ya kukutana naye uso kwa uso na kujadili suala hilo. Pirlo akapiga ishara ya msalaba na kwenda kwenye viti ambapo alitumia dakika kama tano kujifanya anasali. Akatoka hapo na kuelekea nje kwenye chumba alichoelekezwa na yule Padri.
Huko akakutana na Mzee mmoja mwenye mvi nyingi kichwani kwake na walipoonana wakakumbatiana na mzee yule akampeleka kwenye chumba kingine cha siri zaidi.
Chumba kilijaa vifaa vingi vya mapigano hadi kijana Pirlo alikuwa haamini kama huko nje kuna kanisa. Mapanga ya kininja, bunduki na silaha zote aliziona hapo.
"Huku ndipo kwenye nyanja yetu ya upelelezi Pirlo." Mzee yule alimwambia Pirlo huku akicheka na macho ya Pirlo yalikuwa yanalanda huku na huko akishangaa wafanyakazi wenye mavazi ya Kitawa wanavyochalaza kiparaza cha kompyuta. "Ulichagua jina zuri sana kijana. Eti Pirlo, ukajidai yule mchezaji wetu wa Italia. Kwa nini usingejiita Balloteli, Muafrika mwenzako?" Mzee yule alikuwa akiongea kwa utani na kuchechemea kutokana na uzee wake.
Akafika sehemu moja ambayo ndio ilikuwa mwisho wa safari yake. Akagota na kumuita jamaa mmoja aliyekuwa anahusika na sehemu ile.
"Alejandro." Mzee yule aliita kwa sauti kutokana na mtu aliyekuwa anamuita kutokuwepo. Mara akiwa anamtafuta huku na huko, akashangaa kitu kinapita mbele yake kwa kasi halafu kikasimama mbele yake na kuanza kuongea.
"Hellow Mr. Alexander." Kitu hicho kilikuwa kimevaa suti lakini baada ya sauti hiyo, hali fulani ya umeme ikatokea kwenye suti hiyo na sura ya Muitaliano ikaonekana ikiwa inatabasamu.
"Alejandro. Kila wakati we' ni mtu wa kubuni ujinga tu!" Mzee Alexander alilalamika huku akimuangalia yule mtaalamu.
"Hii ni suti ambayo unaweza ukakimbia kwa kasi yoyote bila kuonekana. Na pia haingizi risasi hata kidogo. Mbali na hapo, ukivaa suti hii, na hii saa unaweza kuwa unatoa umeme mwilini mwako." Yule bwana aliyefahamika kwa jina Alejandro alitoa sifa baadhi ya vazi alilovaa na kumfanya Pirlo kuitamani suti ile.
"Achana na mambo yako. Huyu ni yule kijana wetu wa SGT, anasema mtambo umefunguliwa huko na anataka akauteketeze. Nimemleta kwako ili umpe vifaa maalumu." Mzee Alexander alieleza yote kuhusu Pirlo.
"Oooh! Mr. Hyung. Hii suti nakupa wewe Kamanda. Nenda nayo." Alejandro akiongea huku akiivua ile suti na yeye kubaki na boxer. Sekunde kadhaa akachukua rimoti fulani akaibonyeza vitufe fulani na ghafla likasogea begi fulani na kufunguka. Baada ya kufunguka, zikatokea nguo nyingine na mara zikaanza kujivalisha zenyewe mwilini.
"Haya twende." Alejandro alimwambia Pirlo baada mbwembwe nyingi. Pirlo akacheka na kisha akamfuata kijana yule mtukutu sehemu anayotaka waende.
Huko Alejandro akamtengenezea kitambulisho kingine atakachoingilia Tanzania na kisha akampa vifaa maalumu kwa ajili ya mapambano.
Pirlo akalidhika na kazi ya Mzee Alexander na Alejandro.
Akaaga na kuelekea uwanja wa ndege ambapo alikuta ndege maalumu kwa ajili ya kumpeleka Dar es Salaam, Tanzania.
****
Saa mbili usiku, yakiwa yamebaki masaa manne ya Lobo kutimiza adhma yake, Lisa alikuwa kwenye chumba cha mawasiliano akisubiri simu maalumu kutoka kwa Gunner.
Hali ya mawingu ilikuwa imetanda nje na Dar es Salaam nzima. Ilionesha wazi muda wowote mvua itakunya katika Jiji lile.
Saa tatu, simu ya Malocha iliita na hapohapo ikaungwa na mtaalamu wao na maongezi yao yakaanza kusikika bila chenga.
"Haloo FISSA. Lisa kabakiza masaa matatu. Naomba mfuate haya maelezo machache ambayo nitawapa. Mtoto yupo sehemu nyingine ambapo ni huko Gongo La Mboto kwa mbele na Lisa naomba aje huku Kibaha. Najua ndani ya masaa mawili atakuwa amefika. Hamna foleni usiku huu. Kama mnampenda Martina, naomba Lisa aje peke yake. Sitaki mchezo kuhusu hilo. Nawatazama kwa ukaribu, mkijaribu kuleta ukanjanja wowote, Martina mtaletewa mzoga hapo kesho. Zingatieni hilo, nawaoneni. Umebakiza masaa matatu, Lisa. Fanya maamuzi.TICK TOCK." Sauti ya Lobo ilisikika na wala hakuwa na muda wa kusikiliza upande wa pili, akakata simu.
"Mambo yatakuwa magumu hapa. Kama wamefanikiwa kujua mawasiliano yangu, nauhakika wanajua pia kuwa tupo wapi." Malocha aliongea kwa kukata tamaa mbele ya wafanyakazi wake.
"Usijali Malocha, mmefanya kazi kubwa sana hadi hapa. Naomba mwanangu mnilelee vizuri. Mkimpata Frank, muonesheni mwanaye, msimfiche na mwambieni nampenda sana." Lisa alimaliza kuongea maneno machache na kisha akatoka nje tayari kwa safari ya kibaha.
Hakusahau simu ambayo atakuwa anawasiliana na wakina Lobo kama hatowaona. Akawaacha wakina Malocha wakiwa katika masikitiko makubwa mioyoni mwao.
"Hamna jinsi. Tunakupenda Lisa." Malocha alinong'ona maneno ambayo Lisa hakuyasikia. Mtoto wa kike akakwea gari tayari kwa kwenda alipoelekezwa.
****
"Oooh! Lisa. Karibu tena katika mikono yangu." Ni sauti ya Gunner ambayo iliongea baada ya Lisa kusimamishwa kwenye barabara ya rami iliyopo eneo la Kibaha na kutoka nje ya gari lake.
"Muachie mwanangu Gunner." Lisa akafoka kwa hasira.
"Usijali. Tayari nimekwishawaambia mbwa wako mwanao alipo. Wapo njiani wanaelekea huko." Gunner akaongea na wakati huo mvua ya manyunyu ilikuwa imeanza kushika namba eneo hilo. "Zimebaki dakika kumi za Lobo kichukua roho yako. Umefanya maamuzi sahihi sana kwa kununua roho ya Martina." Lobo akazidi kutiririka.
"Fanyeni haraka. Sina muda wa kukaa na hii roho, ni yenu." Lisa akafoka tena.
"Hapana mke wangu, sheria zinasema masaa ishirini na nne. Bado dakika saba tu, utakuwa kuzimu. Lobo yumo mle, anasubiri kazi yake." Gunner alipoonesha sehemu Lobo alipo, taa za gari zikawashwa mara moja na kuzimwa.
ITAENDELEA
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA TATU
"Usijali. Tayari nimekwishawaambia mbwa wako mwanao alipo. Wapo njiani wanaelekea huko." Gunner akaongea na wakati huo mvua ya manyunyu ilikuwa imeanza kushika namba eneo hilo. "Zimebaki dakika kumi za Lobo kichukua roho yako. Umefanya maamuzi sahihi sana kwa kununua roho ya Martina." Lobo akazidi kutiririka.
"Fanyeni haraka. Sina muda wa kukaa na hii roho, ni yenu." Lisa akafoka tena.
"Hapana mke wangu, sheria zinasema masaa ishirini na nne. Bado dakika saba tu, utakuwa kuzimu. Lobo yumo mle, anasubiri kazi yake." Gunner alipoonesha sehemu Lobo alipo, taa za gari zikawashwa mara moja na kuzimwa.
"Mi' si mke wako pia." Lisa aliongea kwa kujiamini mbele ya Gunner ambaye alimpiga kofi zito lililompeleka Lisa chini ya rami. Mara baada ya kofi hilo, akaanza kumpiga mateke mazito binti yule kana kwamba hamjui.
"Mjinga wewe. Nitakuua mimi." Gunner aliongea kwa hasira huku akimtemea maji ya mvua Lisa. Radi nazo zilikuwa zinawaka huku na huko na kuonesha vazi la suti nyeusi aliyovaa Gunner. "Muda wa Lobo umewadia, kwa heri Lisa." Gunner alimuaga mkewe na kwenda kwenye gari alilopo Lobo. Wakati anaingia, John Lobo akawa anatoka upande mwingine.
Koti lake jeusi na refu linalochagizwa na kung'aa kama la majambazi, lilimfanya kumchora Lobo kama katili la hatari sana. Kila radi zilivyocharaza anga, uso wa Lobo ulionekana na mkononi kwake akiwa kakamata bastola iliyofungwa kiwambo cha sauti.
"Muda wa kufa Lisa. Imebaki dakika moja." Alipoongea hayo, radi ikapiga tena na uso wake mweupe kiasi huku kichwani akiwa hana nywele, zikamfanya Lisa aamini kuwa muda wake kweli umeisha.
Akanyanyuka pale alipokuwa kalala baada ya kupigwa na Gunner, akapiga magoti tayari kwa kukipokea kifo chake.
"Kumi, Tisa, Nane, Saba, Sita, Tano ......" Lobo akawa anahesabu sekunde ambazo zilikuwa zimebaki. Lisa akafumba macho yake baada ya sekunde kufikia nne.
Akiwa kajiandaa kufa mtoto wa kike, na wakati huo kifyatulio cha risasi kikiwa tayari kufyatuliwa na Lobo, muujiza wa ajabu ukatokea. Hakika ulikuwa muujiza wa aina yake.
Lobo akiwa anaanza kufyatua kifyatulio cha bastola yake, mara mkono wake wa kushoto ukachomwa na vitu kama nyota zenye ncha kali. Maumivu aliyoyapata dakika hiyo, yalikuwa hayaelezeki. Akiwa katika hali hiyo akajikuta akidondosha bastola yake na kuanza kutazama ni wapi vitu vile vimetokea. Wakati anatazama huku na huko, radi ikapiga na hapo akaona kitu mfano wa mtu aliyevaa nguo nyeusi anakuja kwa kasi ya popo mbele yake. Nasema ni mfano wa mtu kwa sababu kilikuwa kina kasi ambayo mtu wa kawaida hana hata kidogo lakini umbile hilo la mtu lilikuwa limetunukiwa kasi hiyo.
Kuja kutahamaki, kitu hicho kikampiga mateke mawili mazito John Lobo. La kwanza lilimkuta kifuani, kitu hicho kikiwa bado kipo angani, kikammalizia teke la pili la hatari shingoni. Lobo akapaishwa hadi kwenye boneti ya gari walilokuja nalo.
Radi nyingine ikapiga, hapo kile kitu kikaonekana kimesimama wima kwa mtindo wa kupigana. Lobo akagonga boneti la gari ile, na Gunner akawasha taa. Sasa alionekana mtu ambaye kafunikwa sura lakini kavaa suti ya gharama.
Kwa kasi, Lobo akashuka toka kwenye boneti na kumfuata yule mtu asiye na sura na kuanza kupambana naye wakati huo Lisa maswali kibao yaliendelea kutiririka katika kichwa chake asijue kile ni kitu gani au ni mtu gani na kaja sehemu ile kufanya nini.
Lobo akarusha teke, lakini cha kushangaza mtu yule alilidaka teke hilo kwa mguu wake wa kushoto na kulibana nyuma ya goti. Lobo akawa hana ujanja wa kutumia miguu yake. Akaanza kurusha ngumi ambapo yule mtu asiye na sura alikuwa akizitoa nje bila hata kurusha zake.
Ngumi ambayo Lobo aliivuta kwa nguvu zake zote, mtu yule aliidaka na sasa akawa kakamata mkono na mguu wa Lobo. Lobo akawa kakamatika hana la kufanya. Mara yule mtu alirudisha kichwa chake nyuma na kukipeleka mbele kwa kasi, kikatua kwenye pua ya Lobo. Damu zikamchuruzika Lobo lakini hakuenda popote kwa sababu alikuwa kabanwa ipasavyo na mtu yule.
Wakati damu zinaendelea kumtoka, Lobo akajikuta akipokea kichwa kingine palepale alipopigwa mwanzo. Maumivu yaliyompata, hakusita kupiga kelele na nadhani angesimulia hadi kwa wajukuu zake.
Hapo yule mtu alimuachia mkono na kisha akaanza kutandaza ngumi zisizo na idadi kwenye kifua cha Lobo. Ngumi ya mwisho ilitua tena kwenye pua, na hapohapo mtu yule akamuachia Lobo mguu wake na kuruka teke zito la kuzunguka. Lobo akapaa juu na kisha akatua chini kama mzigo akiwa kachafuka kwa damu na hali yake ikiwa wazi ni mbaya.
Yule bwana akawa bado kasimama palepale akiwa kakunja ngumi na sura yake iliyofungwa na sijui nini, ikiwa imeinama kwa kusubiri jambo lingine.
Mvua sasa ilikuwa hainyeshi tena bali kubaki miungurumo ya hapa na pale. Gunner akafungua mlango wa gari yake na kwa madaha akachomoka toka mle ndani na kisha akaenda kwa Lobo na kumuingiza ndani ya gari.
"Safi sana. Yaonekana una uwezo mkubwa wa kupigana. Haijalishi, lakini sasa unapambana na mzimu." Gunner aliongea na muda huohuo akachomoka kwa kasi na alipofika mbele ya yule mtu, alisimama ghafla na kuanza kurusha ngumi nyingi zisizo na idadi. Zilikuwa zinarushwa kuelekea kichwani, kifuani na kila mahali ambapo Gunner aliona patamsaidia kumnyamazisha mpinzani wake aliyekuwa anakazi ya kuzitoa na kuzikwepa.
Kuna ngumi moja ya hatari Gunner aliirusha na jamaa yule aliikwepa kwa kuinama kidogo, lakini kwa bahati mbaya alipoinama, Gunner akaachia ngumi ya mkono mwingine ambayo ilimkuta jamaa yule kidevuni na kumrusha hadi alipo Lisa. Alipotua chini, tayari Gunner alikwishafika, akamkalia kwa juu na kuanza kumtwanga ngumi za usoni.
Ilikuwa ni 'kimuhemuhe' au patashika kwa shimo kuchimbika. Mtu yule ambaye alikuwa kazibwa na mask, ni wazi alikuwa taabani hasa pale mwanaume wa shoka Gunner aliposhika ile mask iliyoungana na suti yake na kutaka kuiondoa.
Alipoishika, ndipo alipogundua inaseli za umeme ambazo ni hadi ubonyeze kitu fulani ndizo nazo zijifungue. Gunner akajaribu kuzamisha vidole vyake kwenye ile mask kwa kutaka kuirarua lakini kwa bahati mbaya alipokea pigo hafifu toka kwa Lisa lililopigwa kwa teke baada ya Lisa kuona mtu anayemsaidia kuzidiwa maarifa. Ni pigo hafifu kwa sababu si lile ambalo ungepigwa nalo na Lisa wakati yu mzima.
Gunner akajikuta akimuachia yule mtu na kumfuata Lisa ambaye alikuwa kasimama pembeni kidogo na pale. Kwa hasira nyingi, Gunner alimpiga kofi zito Lisa na lile kofi yule mtu aliyechini aliliona na likamshtua vilivyo. Mwanamke kupigwa kama mwanaume, yule mtu alistaajabu ya Filauni sasa baada ya kuyashuhudia ya Mussa.
Gunner hakuishia kwenye kofi pekee, Lisa alipoyumba baada ya kofi lile, Gunner akaruka teke la kutanguliza mguu mbele na likakita nyuma ya kiuno cha Lisa. Lisa masikini ya MUNGU akadondoka chini na kugaa gaa kwa maumivu.
Gunner akazidi kuonesha ukatili wake dhidi ya wanawake. Na hakika alikuwa katili. Mateke mazito kwenda tumboni, kifuani na saa nyingine kumkanyaga Lisa kichwani kama mwenye kuua nyoka kwa kumkanyaga na kiatu, usingeweza kusema huyu jamaa ana roho ya utu hata kidogo.
"Heeeey." Sauti kali ilisikika nyuma ya Gunner aliyekuwa anamsulubu Lisa. Akiwa anapumua haraka, Gunner akageuka nyuma kumuangalia anayemuita huku bado mguu wake upo juu ya mwili wa Lisa.
Akamtazama Lisa aliyekuwa anagaragara kwa maumivu, kisha Gunner akampiga teke dogo kama anatoa pasi ya mpira. Akamuacha na taratibu akaanza kwenda alipo yule mtu aliyekuwa kasimama na kuweka mguu mmoja mbele kama wafanyavyo wacheza mapigano ya miguu na mikono (karate).
"Hivyo ndivyo mama yako alivyokufundisha kucheza na mwanamke?" Yule bwana kwa mara ya kwanza aliongea baada ya kufoka.
"Oooh! Mama? Namchukia mama yangu kwa sababu alinitelekeza nilipozaliwa tu. Nampenda sana baba." Gunner alijibu huku akivaa vizuri groves zake nyeusi.
"Kwa hiyo baba yako ndio kakufundisha kuwapiga wanawake? Eti we' tasa." Yule jamaa aliongea maneno ya kukarahisha na Gunner yakamuuma.
"Usiniite hivyo."
"Tayari nimekwisha kuita sasa." Jamaa yule safari hii alikuwa anaongea huku akizunguka kwa hatua ndogondogo akimtazama Gunner kwa makini. "We' ni mgumba tu, hahahaaa." Jamaa akacheka kwa dharau.
"Mmmh! Yaonekana mswahili sana kijana. Lakini mbona hauvui hicho kiuchafu kichwani? Unaogopa nini?" Gunner aliuliza na wakati huo Lobo alikuwa ndani ya gari akifatilia ule mpambano kwa makini japo alikuwa katika maumivu makali ya kuvunjwa mfupa wa pua.
"Ooooh! Nimesahau kuwa ulikuwa unataka kuvua hii sura. Usijali Mgumba, ngoja nitimize." Jamaa yule aliongea na kufunua koti lake la suti sehemu ya mkononi, akaanza kuiobonyeza saa yake na sekunde kadhaa, ile mask ikaanza kutoa sauti za shoti ya umeme na baadaye ikapotea kabisa na kubaki sura ya yule bwana akiwa katika suti mwanana na ya kumpendeza pia.
Ni yuleyule Pirlo wa Italia na Hyung wa China, ndiye sasa alioneokana vema kwenye uso wa Gunner aliyebaki katabasamu tu bila kusema chochote.
"A coward's back. (Muoga karudi)" Gunner aliongea huku bado katabasamu.
"Karudi kuangamiza zao la wagumba na matasa." Pirlo au Hyung akajibu.
"Huwezi kunisimamisha Man'Sai, tayari nina kila kitu." Gunner akaongea akilitaja jina la Man'Sai ambalo ni jina alilojipa Frank Masai. Lisa kusikia jina hilo, akajikuta akipata hata nguvu na kutazama kule Frank Masai alipo.
Tabasamu la shida likamtoka mwanamke yule alipothibitisha sura ya Frank Masai.
"Oooh! Kumbe wanijua eeh. Sasa ndio nimerudi hivyo. Naanza na SGT kisha namalizia na Jet P112. Zote naziharibu." Frank aliongea kwa utulivu na sasa alikuwa kasimama akimuangalia adui yake.
"Hahahaaa. Wameshindwa makundi kama FBI, we bwege utaweza." Gunner akaongea kwa dharau.
"Hizo ni akili za Wagumba wengi wa dunia hii. Wanadhani kufanya kazi katika makundi ndio kufanikiwa. Njia ya kufanikiwa ni kuwa peke yako na kufanya kila kitu peke yako. Sihitaji msaada kutimiza nilichokitaka. Msaada wangu ni MUNGU tu." Masai aliongea kwa utulivu na Gunner akacheka tena.
"Okay Man'Sai. Lisa huyo hapo, nimekulindia sana. Ni mtamu mnooo, hahahaaa." Gunner akajidai anatoa maneno ya kejeli.
"Hahahaa. Usemayo ni ya kweli, ila unapewa utamu unashindwa kuleta matunda ya utamu huo. Mwanaume suruali wewe. Hahahaaa." Masai akakejeli naye jambo lililomfanya Gunner apandwe na hasira na kujikuta akikimbia kwa haraka kwenda kwa Masai ambaye safari hii alimuonesha huyu bwana kwa nini anatafutwa kwa udi na uvumba kwenye hii dunia na hapatikani.
Gunner akiwa katika kasi hiyo, akamfikia Frank Masai na kuanza kurusha ngumi nzito kama kawaida yake, lakini ubaya alimkuta hata Masai akiwa katika hasira za kumuona akimpiga Lisa kama mwanaume mwenzake.
Ngumi nyingi alizorusha Gunner, Masai alizipangua na yeye akawa anarusha zake kwa chati, yaani kwa kumendea. Gunner akajichanganya kidogo kwenye kurusha ngumi hizo, Masai akapangua na kutupa yake ambayo ilimkuta jamaa kwenye pua. Gunner akashika pua yake na kujisahau kuwa yupo mpambanoni. Frank akatupa ngumi nyingine ambayo hiyo ikatua kwenye shavu la kushoto na kumfanya Gunner aegemee upande wa kulia. Kosa kubwa kwa Gunner kwani wakati anaegemea upande huo, tayari Man'Sai alikuwa katupa ngumi nyingine nzito zaidi na kupiga shavu la kulia ambapo alikuwa anaegemea Gunner.
Damu kiasi zikamtoka Gunner lakini haikumaanisha ndio mpambano umeisha. Man'Sai akaruka teke zito lililompeleka Gunner hadi kwenye gari la Lisa.
Frank akiwa katika ubora wake wa kwenye riwaya ya Jina na Ukurasa wa Hamsini, akamuonesha Gunner kuwa yeye si wale aliowategemea katika maisha yake, bali yeye ni yule ambaye hakupaswa hata kumuota ujio wake.
Gunner alisikia sauti ya maji na sauti kama ya karatasi inayopepea ikija nyuma yake. Alipogeuka, kwa msaada wa taa za gari alizoziwasha wakati Lobo anasulubishwa, aliona viatu vya gharama alivyovaa Frank vikichapua katikati ya maji ya mvua iliyokata muda mchache uliopita. Maji hayo kila Frank alipotua mguu wake huku akikimbia, basi yaliruka kwa pembeni kuonesha kuwa zile mbio zilikuwa ni nzito. Sauti kama karatasi inayopepea, ilikuwa ni suti mwanana aliyotinga Man'Sai, ilikuwa inatoa sauti hiyo wakati anakimbia kwa hatua ndogondogo kumfuata Gunner aliyekaribu na gari la Lisa.
ITAENDELEA
 
RIWAYA; DUKA LA ROHO
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Gunner alisikia sauti ya maji na sauti kama ya karatasi inayopepea ikija n yuma yake. Alipogeuka, kwa msaada wa taa za gari alizoziwasha wakati Lobo anasulubishwa, aliona viatu vya gharama alivyovaa Frank vikichapua katikati ya maji ya mvua iliyokata muda mchache uliopita. Maji hayo kila Frank alipotua mguu wake huku akikimbia, basi yaliruka kwa pembeni kuonesha kuwa zile mbio zilikuwa ni nzito. Sauti kama karatasi inayopepea, ilikuwa ni suti mwanana aliyotinga Man'Sai, ilikuwa inatoa sauti hiyo wakati anakimbia kwa hatua ndogondogo kumfuata Gunner aliyekaribu na gari la Lisa.
Gunner kugeuka tu! Anakutana na mzigo mzito wa ngumi ya paji la uso toka kwa Man'Sai, na wala hakupewa muda wa kujitetea au kuuliza kapigwa na nini, maana ngumi nyingine ni kama umegongwa na treni ya umeme. Ngwara au mtama mkali ulipigwa na Masai kwenda kwa Gunner. Jamaa akaruka kimo cha nyani mrukia miti na kutulia mgongo ambapo Frank naye aliruka mtupumtupu na kutuliza mgongo wake juu ya tumbo pa Gunner. Katili yule akawa hoi bin taabani ndani ya dakika mbili tu.
"Siwezi kukuua kwa sasa we' tasa. Nitamkabidhi Lisa roho yako alipe ulichomfanyia baba yake. Na mwambie Lobo, Roho yake nitampa Mubah. Mimi naishia hapa maana naona kama nakuonea tu." Masai aliongea wakati kanyanyuka na kumfuata Lisa pale alipokuwa kalala kwa maumivu ya kipigo cha Gunner.
"Tutakutana tena Masai. Karibu sana. Unamtihani mkubwa wa kununua roho za uwapendao au usiowapenda. Tutakutana tu!" Gunner aliongea hayo huku akienda garini kwake kainama na kushikilia tumbo kama mama mjamzito anayetaka kujifungua.
"Kuuza na kununua roho, ni mchezo wa kufuata sheria pekee. Mmeuziwa roho ya Lisa na Martina, mmeshindwa kuzinunua bali mimi ndiye nimezinunua. Sasa sijui kama mtaweza kununua zenu pale nitakapo wakabidhi roho hizo Lisa na Mubah." Frank naye alijibu huku akimkokota Lisa kumuingiza kwenye gari.
"Ni sheria tu ndizo zitakazofuatwa. Kama leo umefanikiwa, jipange zaidi." Gunner akamaliza na kuingia ndani ya gari lake na kuliwasha kisha akaondoka eneo lile akiwa na Lobo ambaye alikuwa taabani sababu ya kuendelea kuvuja damu.
Masai alipoona watu wale wameondoka, naye akapanda gari la Lisa na kisha akaliingiza barabarani tayari kwa kuelekea katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
"Lisa. Twende hospitali kwanza." Masai alimwambia Lisa wakati anaendesha gari kutoka pale Kibaha.
"Asante Frank. Ila sijajua kama mwanangu yupo salama kweli." Lisa aliongea kwa sauti ya chini.
"Yupo salama kwa Malocha. Usijali."
"Asante sana. Usitie shaka kuhusu hospitali, nitakuwa sawa ukinipeleka kwenye nyumba yangu ya Sinza." Lisa alimwambia Frank wakati huo ilikuwa yapata saa nane za usiku. Frank akabonyeza vitufe kadhaa kwenye kompyuta ya gari lile, kisha akamwambia Lisa ampe namba za nyumba yake. Alipompa, akaziingiza mahala husika na ramani ambayo itampeleka katika nyumba hiyo ikaonekana.
Lisa akawa anapitiwa na usingizi na Frank akawa anaendesha gari kuelekea Sinza. Macho ya Frank yakatua kwenye maungo ya Lisa aliyekuwa kasinzia. Sketi fupi aliyokuwa kaivaa, ikaonesha mapaja ya kuvutia ya Lisa. Blazia ya mtelezo aliyoivaa bila kitu ndani yake, ikiwa imelowana sababu ya mvua, ikaonesha matiti madogo yaliyojaa na kusimama na ambayo hayakunyonywa sana na Martina.
Frank akameza mate ya uchu wa ngono hasa alipokumbuka kwa mara ya kwanza alipomvua Lisa nguo zake. Ilikuwa ni kipindi wanasoma shule ya sekondari. Baada ya kupata chakula kwa pamoja kantini mida ya usiku, wakaamua kwenda darasani usiku huohuo kujisomea. Wakati wanajadili hili na lile kwenye masomo yao, mguu wa Lisa kwa bahati mbaya ukamkanyaga Frank. Lisa alijaribu kumuomba msamaha Frank lakini jamaa alikataa katukatu na kutaka na yeye alipize. Hatimaye Frank akalipiza kwa kumkanyaga Lisa.
Lisa aliumia moyoni lakini Frank yeye alijua kafanya utani tu. Hamu ya kuendelea kusoma, ikamtoka Lisa. Akamuomba Frank watoke darasani na warudi vyumbani mwao. Frank alikubali na kuinuka kitini kwake tayari kwa kuondoka bila kung'amua kuwa mwenzake kachukia.
Lisa akiponyanyuka na kuanza kutembea, akaonekana akiwa anachechemea kidogo. Hali hiyo ikampa mashaka Frank na kumuuliza kwa nini anachechemea wakati walipoingia darasani hakuwa hivyo. Ndipo Lisa akaanza kulia na kumjibu Frank kuwa kamuumiza baada ya kulipizia akivyomkanyaga.
Frank kwa haraka, akamrudisha kwenye kiti Lisa na kwa kuwa darasani mle kulikuwa hamna watu zaidi yao, na darasa lipo mbali na ofisi za walimu, Frank akamvua kiatu cha mguu aliomkanyaga Lisa. Hapo akaona wekundu uliotokana na kulipa kisasi chake. Moyo ukamuuma Frank na kujiona mkosaji. Akamtazama Lisa usoni na macho yao yakagongana lakini ya Lisa yakiwa yanatiririka machozi na ya Frank yakiwa na huruma.
"Samahani Lisa." Maneno yalimtoka Frank. Lisa akafuta machozi na kutulia asijue ajibu nini baada ya ile samahani ya mwanaume ampendaye kuliko chochote. "So sorry Lisa." Akasisitiza kauli yake Frank na kuinuka akipokuwa kachutama wakati anamvua kiatu Lisa. Akamshika mikononi na kumnyanyua mwanadada yule, naye akasimama. Frank akamkumbatia Lisa huku samahani na machozi ya uchungu yakimtiririka mwanaume yule.
"Nimekusamehe Masai. Nakupenda sana." Lisa alimwambia Frank kwa sauti yake laini na yeye akijifunga kwenye kumbate hilo kama Frank alivyofanya.
Sekunde kadhaa za kukumbatiana, wakaanza kuachiana na baada ya hapo, wakajikuta wanaangaliana usoni huku mikono ya Frank ikipita kiunoni kwa Lisa na mikono ya Lisa ikipita mabegani kwa Frank. Macho yao yakiwa yanatazamana, yakawa yanaongea lugha moja pekee, wataalamu tunaiitia lugha ya mapenzi.
Frank ndiye aliyekuwa wa kwanza kusogeza kichwa chake kwenda kwenye kichwa cha Lisa. Lisa akasogeza kidogo lakini kama akasita, na kumfanya Frank pia kusita. Lakini baadaye akasogeza zaidi na midomo yake kugusa midomo ya Lisa.
Lisa ni kama alikuwa akisubiri jambo fulani litokee ndio na yeye aingie. Frank alipoutoa ulimi wake na kujaribu kuuingiza kwenye kinywa cha Lisa kilichokuwa kimefumbwa, Lisa ndipo alipofungua kinywa chake na kuruhusu ulimi ule kupenya na kinywa chake kikaudaka na kuanza kuunyonya ulimi ule kwa chati.
Likawa tendo lenye raha sana hasa ukizingatia ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kupeana busu la namna ile. Frank akamsukumia Lisa katika ukuta mmojawapo wa darasa lile na kuzidi kunyonya ulimi wake.
Mikono yake haikuishia kiunoni pekee, safari hii akapeleka hadi kifuani na kuanza kutomasa matiti ya Lisa. Lisa naye hakuwa nyuma, akapitisha mikono yake kwenye shati la Frank na kuanza kupapasa kifua cha kijana yule na kufanya maruhani ya mapenzi kutapakaa kila sehemu ya miili ya wawili wale.
Frank akaenda mbali zaidi kwa kuitoa blazia wanayoiita kitopu, na Lisa akabaki kifua wazi. Frank akashambulia kifua kile kwa ulimi na kumfanya Lisa awe taabani na mwenye uhitaji wa tendo.
Frank akashusha suruali yake kidogo, kisha akashusha na nguo ya ndani ya Lisa bila kuondoa sketi yake ya shule. Akakamata mguu wa Lisa na kuubana vema kwa mkono wake. Akazidi kumsukumia ukutani ambapo Lisa naye aliruhusu maungo ya Frank kuingia mwilini mwake kwani alimkumbatia ipasavyo mwanaume yule wakati anajaribu kuingia zaidi.
Frank akatabasamu baada ya kukumbuka jambo lile na akili yake kujikuta ikicheka tu. Akawaza endapo angekamatwa siku ile na mwalimu wa nidhamu au mnoko yeyote. Akacheka na kuzidi kuingia Jijini kwa gari la Lisa.
****
Saa kumi kasoro, Frank akawa kasimamisha gari lake kwenye nyumba ambayo Lisa alisema ni yake. Akapitisha gari hilo getini lililokuwa linajifungua lenyewe unapoingiza namba zake kwenye kibonyezeo fulani kilichopo getini hapo. Frank alibonyeza namba hizo kwa sababu tayari Lisa alimwambia.
Alipoingiza gari, akafungua milango ya nyumba ambayo yote inafunguka kwa kadi maalumu inayotumika kama ufunguo. Frank akarudi kwenye gari na kumnyanyua Lisa asiyejitambua kwa sababu ya usingizi na maumivu ya kipigo. Akampeleka ndani na kumlaza kisha akaanza kumpa huduma ya kwanza bila kumuondoa nguo zake. Vifaa vya huduma hiyo vilikuwepo mlemle ndani hivyo hakuhangaika katika hilo. Baada ya kumaliza, naye akachukua barafu na kuweka katika sehemu ambazo aliona kaumia. Kisha akatoka kwenye chumba alicholala Lisa na kwenda sebuleni ambapo yeye alikamatiwa na usingizi hapohapo.
****
Saa nne, Frank alikuja kuamshwa na Lisa ambaye alikuwa anaonekana kama mpya kwa jinsi alivyokuwa mchangamfu.
"Wewe. Hujaacha tu kulala mdomo wazi." Lisa akamtania Frank baada ya kumuamsha.
"Acha zako wewe. We jana ulikuwa unakoroma kwenye gari."
"Kwenda huko. Lione kwanza." Lisa aliongea huku kachanua tabasamu. "Kaoge, maji yapo tayari bafuni." Lisa akamwambia Frank na kumpa mgongo kwa yeye kuelekea chumbani kwake. Huku nyuma Frank alibaki akitabasamu hasa kwa kuona umbo adimu la Lisa pamoja na uchangamfu wake.
Frank akanyanyuka na kuelekea bafuni ambalo lilikuwepo mlemle ndani. Akaoga na kutoka ambapo alielekezwa aende chumba kingine alichokuta vitu kadhaa vya kupaka mwili wake.
Akiwa na taulo pekee chumbani mle, akaingia Lisa huku kashika nguo fulani za kiume. Frank akazipokea na kumuangalia Lisa aliyekuwa naye kavaa taulo kubwa lililo kama gauni.
Frank akaweka nguo zile kitandani na alipogeuka, akamuona Lisa anaelekea mlangoni tayari kwa kutoka.
"Lisa." Frank aliita na Lisa akageuka na kumuangalia Frank ambaye alijongea karibu yake na kumshika mabega.
"I miss you. (Nimekukumbuka)" Frank akaongea maneno hayo na kusogeza.kichwa chake na midomo yake akaikutanisha na midomo ya Lisa. Akaibusu, lakini Lisa akataka zaidi ya pale, akaingiza ulimi wake kwenye kinywa cha Frank na Frank akaupokea kwa furaha. Ndimi zao zikawa zinatimiza kila kitu walichokipanga.
Punde, kila mmoja alikuwa kama alivyozaliwa na mataulo yao yakiwa chini huku kitanda kikilalamika kwa shughuli nzito ya mapenzi. Hakika walikuwa wanafaidi hawa watu.
****
"Bado huu mzuri Lisa. Kamwe hupotezi uzuri wako. You still the same, my wife." Sauti ya Masai ilikuwa inamsifia Lisa aliyekuwa kalala kwenye kifua chake kwa deko.
"Asante. U bado handsome pia Man'Sai. Haubadiliki mambo yako ambayo kamwe hayajawahi kunitoka kichwani." Lisa aliongea kwa sauti ya mahaba huku akizidi kupapasa kifua kilichopasuka katikati sababu ya mazoezi ayafanyayo Frank.
"Asante Lisa. Tuamke sasa twende kwa Malocha maana kuna kazi nyingi za kufanya kule." Frank aliongea lakini Lisa alipandisha mabega juu na kuyashusha kuonesha kuwa hataki. "Acha bwana Lisa. Twende sasa hivi halafu si wajua tunatafutwa kama magaidi. Muda wowote wajinga wanaweza kuwa hapa." Frank alikazia mada yake lakini Lisa hakuelewa na badala yake akapanda juu ya kifua cha Frank na kuchukua ulimi wa Masai kwa kutumia kinywa chake na kuanza kuumumusa kwa raha na burudani.
Baada ya dakika kadhaa za kuchezeana hapa na pale, wakajikuta wapo katika dunia ya mapenzi tena. Kilichoendelea hapo, muamuzi alikuwa ni kitanda na mashuka yaliyokuwa yametandikwa juu yake.
****
Muda wa saa nane mchana, kundi la watu wanne walikuwa wamekaa sebuleni katika nyumba ya Kivule wakijadili hili na lile kuhusu Lisa. Hakuna aliyekuwa na uhakika kama Lisa kapona au hajapona. Simu waliyompa ilikuwa haipatikani na wala yeye mwenyewe hakuwataarifu kama amefika sehemu aliyohitajika.
Hawakuishia hapo pekee. Walikumbuka picha mbaya za usiku wa jana walipoenda kumchukua Martina. Walikuta maiti kadhaa zikiwa hazina uhai kwa kuchomwa na vitu vyenye ncha kali kwenye mishipa yao mikuu iliyopita shingoni. Walipomuuliza
Martina ni nani aliyefanya yale, mtoto yule naye aliwauliza kufanya nini? Martina hakubahatika kuona maiti za wale watu kwa sababu wakati analetwa eneo lile, alikuwa kalala.
"Hatufahamu sasa. Sijui wamemuua au katoka mzima." Malocha aliongea kwa sauti ya chini huku kajiinamia.
"Watakuwa wametimiza adhma yao. Lobo huwa hana utani." Mubah aliongea naye kwa sauti ya kukata tamaa.
"Lakini kama wamemuua, wangetupa taarifa twende kumchukua. Yawezekana wamemteka au kimetokea kilichotokea kwa Martina." Malocha alichangia mada tena na kutulia. Wakakaa kimya kwa dakika tano kila mmoja akiwaza jambo lake. Wakiwa katika mawazo hayo, mara mlango wao uligongwa na jamaa mmoja alienda kuufungua.
"Lisaa!!" Jamaa yule alipiga kelele ya mshangao akiwa haamini kilichokuwa mlangoni kwake kwa wakati ule. Wengine waliobaki pale sebuleni, nao walinyanyuka na kusimama wima, macho yakiwa pima katika mlango ambao wanaingilia wageni wote.
Mara Lisa akaingia huku akiwa na tabasamu la bashasha katika uso wake. Wote waliokuwa pale wakasimama kama askari wa gwaride la jeshi wanamsikiliza mkuu wao. Hawakuamini kama kwa muda ule wanaweza kumuona Lisa aliyemzima wa afya na mwenye kila hali ya furaha.
Lisa akaingia lakini akawa kasimama mahala ambapo anaweza kumuona mtu wa nje kupitia ule mlango wa sebuleni. Kwa kidole cha shahada, akaita kwa kuonesha mkono kule mlangoni. Hapo Frank Masai akaingia akiwa kavaa suti maridadi ya kijivu na viatu vya damu ya mzee huku ndani ya suti hiyo akiwa kavalia shati la matirio ya kung'aa rangi nyekundu.
"You son of the bitch Man'Sai." Malocha alisikika akitukana huku akiwa kachanua tabasamu la haja usoni kwake. Akamfuata Masai na kumkumbatia kwa nguvu huku akicheka kwa furaha.
"Nimerudi sasa. Nimekuja kununua roho." Masai aliongea baada ya kuachiana na Malocha ambaye alikuwa haamini kama mtu aliyedhani hatotokea, atatokea.
"Karibu Jambazi langu. Nilikusubiri kwa muda mrefu sana. Hadi nikaamua kuingia kazini mwenyewe." Malocha alitamka hayo huku akimuangalia Frank usoni.
"Usijali. Subira yavuta heri." Naye akampa msemo wa Kihenga rafiki yake kipenzi Malocha.
ITAENDELEA
 
  • Thanks
Reactions: ADK

Similar Discussions

Back
Top Bottom