Remmy Ongala aliwahi kukata rufaa akipinga kushindwa na Masoud sura mbaya katika shindano la wenye sura mbaya

Teko Modise

JF-Expert Member
May 20, 2017
1,914
6,033
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 kuliwahi kuandaliwa shindano la wenye sura mbaya Tanzania kwa upande wa wanaume. Wanawake walikataa hivyo likaandaliwa la wanaume tu.

Washiriki walikuwa wengi lakini waliofanikiwa kufika top 3 walikuwa ni Mzee Jangala, Remmy Ongala na Masoud Sura Mbaya.
06BAF94A-15DE-4115-8C6A-0E9BF7FF3BF9.jpeg


Baada ya mchuano mkali, majaji wakatoa matokeo yao. Mshindi wa kwanza akawa Masoud, wa pili Remmy na wa tatu ni Mzee Jangala.

Basi kama ilivyoada, Masoud akapewa kitita chake kama zawadi, wakati Masoud akikabidhiwa check yake, marehemu Remmy Ongala akaanzisha mzozo wa kutomtambua mshindi huku akijinadi yeye ndio alipaswa kuwa mshindi kwani sura yake ni mbaya na hakuna wa kumkaribia.

Majaji wakamshauri akate rufaa, kweli Remmy akakata rufaa lakini akashindwa na Masoud akapewa mzigo wake wa ushindi.

Ni shindano ambalo halikuwahi kujirudia tena, japo wengi walitamani linhejirudia miaka ya mbeleni. Hiyo ni miaka ya 2000 kabla ya vurugu zenu za Insta, Facebook wala TikTok.

My take:
Hivi hili shindano lingeletwa zama hizi kuna wanaume wangekubali kushiriki kweli? Hawa wanaoedit picha zao photo shoot ili zing’ae huko mitandaoni ili wajizolee “likes” za kutosha!
 
Mwanzoni mwa miaka ya 2000 kuliwahi kuandaliwa shindano la wenye sura mbaya Tanzania kwa upande wa wanaume. Wanawake walikataa hivyo likaandaliwa la wanaume tu.

Washiriki walikuwa wengi lakini waliofanikiwa kufika top 3 walikuwa ni Mzee Jangala, Remmy Ongala na Masoud Sura Mbaya.View attachment 2668120

Baada ya mchuano mkali, majaji wakatoa matokeo yao. Mshindi wa kwanza akawa Masoud, wa pili Remmy na wa tatu ni Mzee Jangala.

Basi kama ilivyoada, Masoud akapewa kitita chake kama zawadi, wakati Masoud akikabidhiwa check yake, marehemu Remmy Ongala akaanzisha mzozo wa kutomtambua mshindi huku akijinadi yeye ndio alipaswa kuwa mshindi kwani sura yake ni mbaya na hakuna wa kumkaribia.

Majaji wakamshauri akate rufaa, kweli Remmy akakata rufaa lakini akashindwa na Masoud akapewa mzigo wake wa ushindi.

Ni shindano ambalo halikuwahi kujirudia tena, japo wengi walitamani linhejirudia miaka ya mbeleni. Hiyo ni miaka ya 2000 kabla ya vurugu zenu za Insta, Facebook wala TikTok.

My take:
Hivi hili shindano lingeletwa zama hizi kuna wanaume wangekubali kushiriki kweli? Hawa wanaoedit picha zao photo shoot ili zing’ae huko mitandaoni ili wajizolee “likes” za kutosha!
Yani nchi yetu kulikuwepo, kukawepo na kunaendelea kuwepo na watu wajinga kama huyu Remmy. upuuz unatamalaki sana kwenye taifa. Unapoteza muda kukata rufaa?

Sasa hivi tuna mwijaku the most handsome man from Kigoma.
 
Afu mbna mzee jangala ni mzuri tu hakustahili kuwepo kwenye top 3
Hata nami nilishangaa kwa Mzee Jangala kuwa mshiriki!
Nakumbuka baada ya rufaa ya Dr Remy kushindwa, alikubali na kumpongeza mshindi, na kudai kuwa kwenye ule mpambano wa kwanza, alikuwa hakumuangalia vizuri! Alikiri, jamaa ni kweli ANA SURA MBAYA kuliko yeye!
Wakati ule, Dar ilikuwa inawaka moto kwa burudani. Na watu walikuwa wanabuni kila aina ya burudani! Miss Tz, miss bantu, miss Kilimanjaro Hotel nk. Vikundi vya sanaa, ma disco, ma dansi kila kona. Kote huko, mwishoni mwa wiki watu wamefurika. Sijui pesa walikuwa wanapata wapi, kwani MICHONGO ya pesa ilikuwa migumu!
 
Back
Top Bottom