Regia Mtema is No More!

Status
Not open for further replies.
Mtetezi wa wanyonge, mtetezi wa kilombero, mtetezi wa maskini wa Tz hebu ona Kilombero wanavyokulilia, ona watz wanavyokulilia, ona CDM wanavyokulilia, ona JF tunavyokulilia amka basi japo utuage, tukusalimu mara ya mwisho Regia.Dah!! RIP REGIA.
 
Amekufa Siku ya Sabato..

20:8-11 katika orodha ya Amri Kumi:
Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya mlango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.
 
sina cha kusema,ila naamini mungu ametuondolea jiwe atatuwekea jiwe.
innalillah wa innalillah raajun.
 
OMG,

Nafungua JF naona picha kubwa, nikasema wanamfanyia Regia promo gani?

Naona R.I.P, nataka kama nisiamini, labda anasema R.I.P kwa mtu mwingine? Lakini this is too much, ukiweka jina la mtu na R.I.P maana yake amefariki.

Reality kicks in. Amefariki.

Pamoja na differences zetu zote bado alikuwa mbunge wetu, na saa nyingine nikaanza kujisikia kama kawa mbunge wa JF, complete with reporting back here.

May all beings attain enlightenment.
 
sijawai kutokwa na chozi ukubwani.
Sikujua kuna siku itakuja kutokea ivyo.

Ila leo posti hii iliniliza nilipoifungua mchana wa saa 7.

Kweli imeniuma na itaniuma daima.
Tulikupenda na tunakukumbuka milele na daima.
Bwana kakupenda zaidi .
Bwana ametoa bwana ametwaa.
Jina lake lihimidiwe.
 
JF Premium MemberArray


Join Date : 21st November 2009
Posts : 3,061
Rep Power : 956


icon1.png
Niliyoyafanya tangu niwe Mbunge-Shukrani kwa WanaJF


Wakuu habari!

Ni matumani yangu kuwa tumejiandaa kumaliza mwaka vizuri na kuplan vizuri for next year.

Tukiwa tunafunga mwaka nimeona niandike kwa kifupi yale niliyoyafanya kwa kipindi Cha mwaka mmoja tangu kuapishwa kuwa Mbunge wa Vitimaalum Nov 12,2010.

Taarifa hii inaonyesha utekelezaji wa Kazi za Ubunge,Kazi za chama Wilayani Kilombero na Kazi za Chama Kitaifa.

A. KAZI ZA KIBUNGE
Tangu nimeapishwa nimefanikiwa kufanya Kazi mbalimbali za Kibunge Wilayani Kilombero,Jimbo ambalo niligombea na kupata Kura 38,550 sawa na asilimia 45 ya kura zote zilizopigwa. utekelezaji wa awamu hii ulikuwa ni QUICK WINS. Quick zifuatazo zimefanyika;
1. Nimepigania bei ya Sukari ishuke -Kuna maeneo Bei imeshuka lakini maeneo mengine hali bado ni mbaya. Kilombero ni Wilaya inayozalisha Sukari, Kiwanda Cha Illovo hivyo bei ya Sukari unapaswa kuwa chini kuliko maeneo yasiyodhalisha Sukari.
2. Nimepigania kituo Cha Polisi Cha Wilaya kiboreshwe-kimeboreshwa
3. Nimepigania kituo Cha afya Cha Mlimba kipatiwe Maji na Ambulance lirudishwe hivi vyote vimefanyika.Ambulance ilikuwa gereji zaidi ya miezi Sita mwaka 2010.
4. Nimepigania utekelezaji wa huduma bure kwa Wajawazito,Watoto chini ya Miaka Mitano,Wazee na Wenye Ulemavu-Kuna maeneo imefanikiwa maeneo mengi bado.
5. Nimetetea haki za Wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari Na KPL-Baadhi ya Kero zimetekelezwa lakini nyingine bado-Suala la Maslahi bado ni tete,suala la Usalama Kazini bado ni tete.
6. Nimetetea na kusimamia kero ya Wakulima na Wafanyabiashara ya kuongezeka kwa Ushuru bila kushirikishwa katika hatua zote muhimu.
7. Nimepigania haki ya Umeme kwa Wananchi wa Kilombero kwani tunavyanzo viwili ya umeme,Kihansi na Kidatu.REA imeenda kule ila inasua sua sana lakini Wizara imetuhakikishia kuwa inatekeleza azma yake ya kupeleka umeme maeneo yote ya karibu na vyanzo vya umeme.
8. Nimepigania barabara ya Kidatu-Ifakara kwa kiwango Cha lami-imeshindikana kwa mwaka wa fedha 2011-2012.
9. Nimesomesha Wanafunzi 86 Sekondari,13 Vyuo Vikuu hawa wa Vyuo Vikuu walihitaji kutoa advance ili waweze kusajiliwa then wapate Mkopo
10. Nimeezeka madarasa mawili(2) ya shule ya Msingi Mkula
11. Nimegharamia Visima viwili vya maji
12. Nimehudumia Baba aliyekuwa kipofu kwa miaka 8 akaweza kuona tena kupitia hospitali ya CCBRT
13. Nimesaidia wagonjwa wengine zaidi ya 42 wakapata huduma za afya na kupona
14. Nimesaidia Jezi kwa Vijana katika Kata 12 Kati ya 23 za Wilaya ya Kilombero
15. Nimefanikisha ligi Mbili katika Kata Mbili-Ligi za Mpira wa Miguu na Netboli
16. Nimeshiriki kwenye fundraising katika Misikiti 3 na Makanisa 4
17. Nimekuwa sehemu ya kufanikisha Uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishirki Cha Mt Fransisco
18. Nimeshiriki kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko Wilayani Kilombero
19. Nimefanikisha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kushirki Umitashumta ngazi ya Wilaya,Mkoa na Taifa
20. Nimefanikisha Vikundi Viwili vya kina Mama Wajane kuweza Kujiajiri na kuendesha maisha yao wenyewe.
21. Nimefanikisha Vikundi 5 vya kina mama kuweza Kujiajiri.
22. Nimefanikisha Vikundi 3 vya wenye ulemavu Kujiajiri wenyewe.
23. Nimefanya Mikutano ya Hadhara ya Elimu ya Uraia pamoja na Shukrani zaidi ya 20.

Na mengine madogo madogo mengi.

B. KAZI ZA CHAMA WILAYANI KILOMBERO

Katika kukuza chama Wilayani Kilombero nimefanikiwa kufanya yafuatayo;
1. Nimelipia na kufungua Ofisi za CHADEMA katika Kata 5
2. Nimefungua na Kuzindua Matawi 13 yaliyojengewa na yenye Uongozi wa Kudumu
3. Nimeingiza Wanachama zaidi ya 8,000

C. KAZI ZA CHAMA ZA KITAIFA
1. Nimeshiriki Maandamano ya CHADEMA Kanda ya Ziwa katika Mikoa yote ya Kanda hiyo katika kupigania haki za watanzania.
2. Nimeshiriki Maandamano ya CHADEMA Nyanda za Juu Kusini kasoro (Mikoa ya Iringa na Ruvuma) katika kupigania haki za watanzania.
3. Nimeshiriki kwenye Kazi za Siasa Arusha - Sakata la Kuvuliwa Uanachama Madiwani kusaka muafaka.
4. Nimeshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Igunga
5. Nimeshiriki kutoa Mafunzo ya Mapungufu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2011 katika Mkoa wa Ruvuma
6. Nimeshiriki kwenye Siasa za Vyuo Vikuu, Makongamano, Mikutano ya Hadhara na Uzinduzi wa Matawi
7. Nimeshiriki kwenye Siasa za Dodoma, Singida na Morogoro.

Natambua nilipaswa kuyafanya zaidi ya haya lakini kutokana na sababu mbalimbali hayo ndio niliyofanikiwa kuyafanya. Angalau nimefanikiwa kufanya karibu asilimia 70 ya niliyopanga kuyafanya kwa mwaka huu 2011 kama Mbunge wa Vitimaalum Wilayani Kilombero.

Naomba nichukue fursa hii pia kuwashukuru wanaJF wote kwa support yenu kwangu kwa hakika ninawashukuru sana tena sana.JF imekuwa ni nyumbani, JF imekuwa ni darasa, Vile vile JF imekuwa ni Tanuru la Moto maana wakati mwingine huwa ninaingizwa kwenye moto hasa. Na mwisho nichukue fursa hii kuwaomba radhi wale wote niliowakwaza kwa namna moja ama nyingine, tuanze upya mwaka ujao..

With Love
Regia

remember this........​



Pumzika kwa amani na umeonyesha mfano wa kutakana msamaha katika maisha yetu. Ushupavu wako wa kupigania demokrasia na maendeleo ya kweli nchini mwetu ni wa kugwa. Upambanaji wako licha ya ulemavu ulikuwa nayo ni funzo kwetu kuwa ulemavu si sababu ya kutojishughulisha na kuongoza watu. Nasema ulikuwa ni mshumaa uliowaka na kuzimika haraka, lakini simulizi na mguso wako utadumu. Upumzike katika Amani ya Milele! Amina!
 
Upumzike kwa Amani Dada Regia. Tulikupenda ila Mungu kakupenda zaidi.Mungu awajalie nguvu wanafamilia yake wote katika kipindi hiki kigumu sana.
 
Rest in peace kamanda, mwanaharakati, mpambanaji na sauti ya vijana na kina mama wa Tanzania. Mungu ailaze mahali pema paradiso roho ya marehemu.Amina
 
Duuh! Hii dunia kweli ni mapito.So young to go but what else could we do???!!! RIP Regia!
 
Amekufa Siku ya Sabato..

20:8-11 katika orodha ya Amri Kumi:
Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya mlango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya sabato akaitakasa.

Kwahiyo wasabato hawafi siku ya sabato? Acha masihala bwana. Mungu agenda zake hapangi na binadamu wa aina yoyote. Anapanga jinsi inavyompendeza.
 
Kwahiyo wasabato hawafi siku ya sabato? Acha masihala bwana. Mungu agenda zake hapangi na binadamu wa aina yoyote. Anapanga jinsi inavyompendeza.

mkuu, hilo file la sir godi lenye agenda umeshalipiga chabo nini, hebu tumegee kidogo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom