Ni pigo kwa Chadema...Mungu ailaze roho yake mahali pema..Amina
Nimewasiliana na familia yake kule Kilombero na kupewa uhakika kwamba Regia ametutoka. Nilifahamiana na Regia kwa zaidi ya miaka minane iliyopita, tumekuwa tukiwasiliana mara kwa mara haswa kipindi cha kampeni 2010 jinsi ya kulichukua jimbo la Kilombero. Ninalijua fika jimbo hilo (Kilombero), kero zinazowasumbua wana kilombero, jinsi ya kuongea na wananchi hao, tabia na mila zao. Na sikuona hiyana kumpa Regia undani huo wakati wa kampeni. Tokana na msiba nimempoteza rafiki, mbunge na mtetezi wangu wa karibu sana. Poleni sana wazazi na ndugu wengine wa marehemu, poleni wana JF na wana Chadema kwa msiba huu, poleni sana wana Kilombero wenzangu hasa maeneo ya Lihegama, Mkamba, Mang'ula, Msolwa station na Ifakara ambako Regia aliweza kufungua matawi muhimu na imara ya Chadema.
Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe.
Asanteni,
Kidatu
Nimewasiliana na familia yake kule Kilombero na kupewa uhakika kwamba Regia ametutoka. Nilifahamiana na Regia kwa zaidi ya miaka minane iliyopita, tumekuwa tukiwasiliana mara kwa mara haswa kipindi cha kampeni 2010 jinsi ya kulichukua jimbo la Kilombero. Ninalijua fika jimbo hilo (Kilombero), kero zinazowasumbua wana kilombero, jinsi ya kuongea na wananchi hao, tabia na mila zao. Na sikuona hiyana kumpa Regia undani huo wakati wa kampeni. Tokana na msiba nimempoteza rafiki, mbunge na mtetezi wangu wa karibu sana. Poleni sana wazazi na ndugu wengine wa marehemu, poleni wana JF na wana Chadema kwa msiba huu, poleni sana wana Kilombero wenzangu hasa maeneo ya Lihegama, Mkamba, Mang'ula, Msolwa station na Ifakara ambako Regia aliweza kufungua matawi muhimu na imara ya Chadema.
Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe.
Asanteni,
Kidatu
Wana CHADEMA sasa kazi iliyopo mbele yetu ni kumlilia Mwenyenzi Mungu ili atupatie Mpambanaji atakayesimama badala ya Regia. R.I.P. Regia, Dah! Machozi yananitoka mwanaume mzima.
Habari zilizothibitishwa na JF ni kuwa Regia Mtema (mb) amepata ajali na Kufariki dunia eneo la Ruvu Darajani.
Ndugu wa Karibu wanasema alikuwa kaenda kukagua Kiwanja alichopewa na Wazazi wake na baadae kwenye mkutano wa CHADEMA huko Kibaha.
Habari hizi zimethibitishwa.