Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua MRINDOKO amewataka watumishi wa umma waliopewa dhamana ya kusimamia taasisi za serikali kutunza mali na maeneo yote wanayoyasimamia ili yasivamiwe.
RC Mhe. Mwanamvua MRINDOKO ameyasema hayo katika mkutano wa kusikiliza kero uliofanyika tarehe 05 Machi, 2024 jioni katika Kata ya Shanwe.
"Niwatake wasimizi wa taasisi za serikali kulinda maeneo wanayoyasimamia ili kuepusha migogoro. Haliwezekani mwananchi anavamia eneo la serikali anaanza ujenzi na wewe upo na haujachukua hatua" - Mhe. Mwanamvua MRINDOKO, RC Katavi
Pia, Mwanamvua MRINDOKO amewaasa wananchi waache mara moja tabia ya kuvamia maeneo ya umma, maana yapo kwa ajili yao na hivyo hawana budi kufuata taratibu zilizopo ili kuepusha migogoro.