MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, amesema wahalifu wanaodaiwa kuwa Panyarodi waliovamia maeneo ya Bunju sio wakazi wa mkoa huo, kwani kazi ya kuwashughulikia wahalifu hao ilishaimaliza.
Wahalifu hao wakiwa kundi la watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya wanane, walifika kwenye mtaa makazi katika eneo la Bunju B Mtaa wa Idara ya Maji saa 8 usiku wa kuamkia jana Februari 10, 2023 na kujeruhi watu kwa mapanga.
Akizungumza leo Jumamosi Februari 11, 2023 alipokutana na uongozi wa Wamachinga na Bodaboda kupokea taarifa ya ziara yao nchini Rwanda, Makalla amesema wahalifu hao sio wakazi wa Dar es Salaam bali ni wa Mapinga mkoani Pwani.
Chanzo:
mwananchi_official
=======
Yaani RC wa Dar es Salaam Amos Makalla anakimbilia kusema hawa Panya Road si wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwakuwa tu huko nyuma aliendesha Oparesheni ya Zimamoto kisha akaja Ikulu Kwako Kukudanganya kuwa ameshawamaliza (Panya Road) wote hivyo leo anasema hawatoki Mkoani hapa Dar es Salaam ili usije Ukakasirika na Kumtumbua.
RC mwenye Akili timamu angesema kuwa kama Mkoa bado tunaendelea Kupambana kukabiliana na Panya Road na si Kukurupuka na kukimbilia kusema hawatoki Mkoani Dar es Salaam na Kusingizia Mikoa mingine ambayo ina Wakuu wa Mikoa very Intelligent and Committed kuliko Yeye.
Rais Samia Binafsi kama MINOCYCLINE ukimuondoa huyu Amos Makalla kama Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nitakushukuru mno kwani hakufai, hana uwezo, muongo muongo na hajui anachokifanya na sijui ni kwanini Mama (Mheshimiwa) na Wewe ulikosea na ukamteua tena kwa Mkoa wenye 'Changanyikeni Brain' kama huu wa Dar es Salaam.
Nyumba uliyozaliwa tu na Kuishi (Kukulia) uliyoachiwa na Marehemu Baba yako iliyoko Kawe Ukwamani (Nyuma ya Hotel ya Victoria) inayotizama na Ghorofa Jipya la Tajiri wa Kiha Muyama One hadi Leo (miaka nenda rudi) umeshindwa Kuiboresha Kiujenzi mpaka inatia Aibu na Kukuaibisha ndiyo utauweza Mkoa wa Dar es Salaam na Kuuendeleza Kimaendeleo?
Hovyo kabisa!
Wahalifu hao wakiwa kundi la watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya wanane, walifika kwenye mtaa makazi katika eneo la Bunju B Mtaa wa Idara ya Maji saa 8 usiku wa kuamkia jana Februari 10, 2023 na kujeruhi watu kwa mapanga.
Akizungumza leo Jumamosi Februari 11, 2023 alipokutana na uongozi wa Wamachinga na Bodaboda kupokea taarifa ya ziara yao nchini Rwanda, Makalla amesema wahalifu hao sio wakazi wa Dar es Salaam bali ni wa Mapinga mkoani Pwani.
Chanzo:
mwananchi_official
=======
Yaani RC wa Dar es Salaam Amos Makalla anakimbilia kusema hawa Panya Road si wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwakuwa tu huko nyuma aliendesha Oparesheni ya Zimamoto kisha akaja Ikulu Kwako Kukudanganya kuwa ameshawamaliza (Panya Road) wote hivyo leo anasema hawatoki Mkoani hapa Dar es Salaam ili usije Ukakasirika na Kumtumbua.
RC mwenye Akili timamu angesema kuwa kama Mkoa bado tunaendelea Kupambana kukabiliana na Panya Road na si Kukurupuka na kukimbilia kusema hawatoki Mkoani Dar es Salaam na Kusingizia Mikoa mingine ambayo ina Wakuu wa Mikoa very Intelligent and Committed kuliko Yeye.
Rais Samia Binafsi kama MINOCYCLINE ukimuondoa huyu Amos Makalla kama Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nitakushukuru mno kwani hakufai, hana uwezo, muongo muongo na hajui anachokifanya na sijui ni kwanini Mama (Mheshimiwa) na Wewe ulikosea na ukamteua tena kwa Mkoa wenye 'Changanyikeni Brain' kama huu wa Dar es Salaam.
Nyumba uliyozaliwa tu na Kuishi (Kukulia) uliyoachiwa na Marehemu Baba yako iliyoko Kawe Ukwamani (Nyuma ya Hotel ya Victoria) inayotizama na Ghorofa Jipya la Tajiri wa Kiha Muyama One hadi Leo (miaka nenda rudi) umeshindwa Kuiboresha Kiujenzi mpaka inatia Aibu na Kukuaibisha ndiyo utauweza Mkoa wa Dar es Salaam na Kuuendeleza Kimaendeleo?
Hovyo kabisa!