Rais Samia, unapoingia mkoani Mara fuatilia kuna chembechembe za watu kula kwa urefu wa kamba pale Musoma Airport

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,767
21,241
Nakukumbusha mheshimiwa rais mliidhinisha pesa za upanuzi wa viwanja kadhaa vya ndege hapa nchini na cha Mkoa wa Mara hapo musoma kikiwa ni kimojawapo.

Musoma_Aerial_View.jpg

PICHA: Sehemu ya mji wa musoma unavyoonekana kutokea juu.

Taarifa tulizo nazo pesa ilitolewa ili kufidia wananchi waliopo kwenye eneo la mradi wa upanuzi na katika hali ya kawaida mkandarasi tayari alishakabidhiwa ramani na site kwa ajili ya kuanza kazi, ila sasa...

Kama ilivyo desturi ya mwafrika akiona pesa isiyo yake (as those 7 policeman done) anafikilia kuipiga (kuiba) baadhi ya wananchi wamelipwa na mpaka kufikia eneo palipo na kanisa la Africa Inland Church na kuanzia eneo hilo mpaka kufika eneo maarufu kwa Cabin (soma kibini) wananchi takribani (kama) 17+ wanazungushwa kulipwa ili kupisha upanuzi.

Mgogoro huu unamfanya mkandarasi ashindwe kuanza kazi wakati tayari ameshaweka vifaa eneo husika, kwani katika ramani aliyopewa inaonyesha mpaka au mwisho wa mradi ni nyumba hizo za Cabin.

Taarifa zinaendelea kudadavua kuwa vikao mbalimbali vinafanyika lakini si vya nia nzuri kwa wananchi hao bali wanapanga kuwazungusha haki yao pamoja na kuwaambia nyumba zao hazihusiki na mojawapo ikiwa ni toka walipoambiwa wasifanye maendeleo au ujenzi wowote katika nyumba zao ni muda mrefu so leo/jana wanakuja na vikao visivyo na tija badala ya kuwalipa waondoke.

Mheshimiwa rais yawezekana wananchi wasikupe taarifa sababu mkuu wa mkoa na wilaya wanajua na kufahamu kinachoendelea ila kuna upigaji unataka kufanyika kwa wananchi wa eneo la nyasho kwa Cabin (soma kibini) kwa kuwaambia walishaliowa au nyumba zao hazipo kwenye eneo ka mradi ili pesa husika ziliwe.

Naendelea kufuatilia ila kwa kuwa wewe ndiye umebeba dhima ya nchi hii na ndiye mwenye kutoa neno kisha likawa kitu halisi kwa niaba ya wananchi hao tembelea mradi huo uone wapigaji wanavyotaka kula kwa urefu wa kamba zao.

👉🏾Mwisho nakusalimu kwa jina la jamhuri ya muungano wa Tanzania..."
 
Ndo ashapitisha kula urefu wa kamba.
So walijua Magufuri atafariki so walipiga break malipo ya fidia ili waje wale kwa hiyo kamba isiyo na kishikio?.
Hii nchi ndiyo maana wenye nafasi ya kupoteza wenzao wakiwa na nafasi basi wanawaondoa ili nchi iwe ya namna hii.

Askari ameua raia kwa mali yake halali hampigi kelele, kiongozi flani amefanya uhalifu flani kelele mpaka mbinguni, what`s this?.
 
Halafu extension cost on contract nazo zilipwe kwa mkandarasi, hii nchi basi tu!!!
Mkuu BiM yupo Musoma now na ninadhani analala hapo Penisula au ikulu ndogo jirani na airport so kesho mumpe taarifa kuhusu hizo cost kwa mkandarasi mkikosa hii nafasi baadaye msije andika hapa kuwa watu wamekula kwa urefu wa kamba 🙂!.
 
Back
Top Bottom