Rais Samia Kiwanda cha Chibuku/ Darbrew LTD kilifungwa tangu mwaka 2018. Muwekezaji yupo lakini Watendaji wa Jiji la Ilala wanakwamisha

Hizi taarifa zinatisha sana. Kwa kweli mleta maada kama taarifa zako ni kweli basi umeamua kujilipua kabisa na unafanya kazi iliyotukuka na ya kizalendo hasa. Ni wakati sasa wa vyombo vya serikali kulifanyia uchunguzi hili suala kwa kina na kufikisha kunapohusika ili kama kuna watu wanahujumu wachukuliwe hatua za kisheria haraka. Kila siku najiuliza hivi Tanzania hatuna waandishi wa habari za kiuchunguzi maana ndio eneo la hili lakini utakuta wanahangaika na mambo ambayo hayana tija kwa taifa hili.

Nilikuwa nafika hapo Chibuku kwa shughuki fulani wakati huo meneja anaitwa Kazonda kama sikosei. Baadaye nilibadili upepo nikaingia kwenye shughuli nyingine sasa siku ya siku napita hapo kuulizia naambiwa kiwanda kimefungwa. Nilishangaa kwani Chibuku kilikuwa kiwanda kinafanya kazi vizuri sikutegemea kingekufa kifo cha ghafla kiasi kile. Malighafi zake ni nafaka zinazlimwa hapa hapa Tanzania na pombe yake ni nzuri kwa sababu ni lishe pia. Na wafugaji walikuwa wanajipatia mabaki kwa ajili ya kulishia mifugo yao.
 
SEREKALI INATAFUTA KODI HALAFU WAPUUZI WACHACHE WANAFANYA UKIRITIMBA WA AJABU ALI MRADI SEREKALI IKOSE KODI YAKE STAHILI,HII NI HUJUMA MBAYA SANA TUNAIOMBA SEREKALI ILIONE HILI NA ILIFANYIE KAZI KWA HARAKA,KWANI SEREKALI INASHIDA SANA NA KODI YA HAPO KATIKA KUENDELEZA MIRADI MBALIMBALI YA KIMSINGI.
 
Jf na wengineo,hata maafisa wa Serikali mlishughulikie hili jambo.Hii nchi ni yetu sote,acheni habari za miposho na Kusahau mtakufa na kuziacha hizo posho za Rushwa.Huyu Mzalendo nimempenda.Anapigana KWA ajili ya wengi.Fungulieni kiwanda hicho.Kazi Iendelee
 
Ila nimeamini kuwa duniani kuna watu wenye roho ngumu aisee. Haiwezekani raisi aliyepita pamoja na ukali wake wote na alivyokuwa anahangaika usiku na mchana kufufua viwanda na mawaziri wake wakina Mwijage pamoja na kuimba "slogan" ya Tanzania ya viwanda halafu kuna watu walikuwa wanamhujumu kiasi hiki. Iwapo hizi taarifa ni sahihi kwa sehemu kubwa basi mheshimiwa raisi aliyepo sasa ana kitu kikubwa cha kujifunza kwa watu waliomzunguka na hizi taarifa za kiwanda cha Chibuku zikawe "case study" kwake.
 
Nimeisoma mada lakini Nina mawazo tofauti.

1. Iacheni pombe ya chibuku ice kifo chema wala msilazimishe wananchi waendelee kunywa pombe ya kienyeji.

2. Chibuku ililenga nchi au jamii maskini tu nadhani Tanzania, Botswana, Zambia, Zimbabwe na Malawi ndiyo kuna kampuni kubwa za kutengeneza pombe ya nafaka

3. Mozambique, Uganda na Tanzania wote wameacha kutengeneza. Soko limepungua kwa sababu watu wenye kipato wanakuwa conscious na afya zao hivyo kunywa kwa plastic inakuwa shida

4. Ukiweka kwenye tetra pack lazima upandishe Bei. Ukipansisha unaanza kupoteza wateja dhidi ya pombe za mnazi, kimpumu, mbege na komoni.

5. Hata CEO wa Chibuku na Salesperson wao ikifika jioni wanakunywa Serengeti na Castle Lite. Hii Chibuku ni alama ya umaskini.

Acheni tu Serikali iangalie namna ya kutumia lile eneo pale Ubungo kuliko kugombea kuendelea kupika pombe ya kienyeji kwenye Karne ya 21 wakati nchi iko uchumi wa kati.
 
Asante,tayari kinywaji hiki kilianza kunyweka hadi ushuani kama Masaki na Mbezi beach. Mkoani kilifika pia kama mwambao wa pwani yote ya bahari hadi Mtwara na kilikubalika sana,pia Morogoro.
Kimsingi Chibuku niliifahamu kama pombe ya kilofa toka zama hizo hata kuzungumzwa kwake ilizungumzwa kwa wale kina sokomoko walevi mbwa wa uswahilini
 
Sisi tuliokuwa wafanyakazi wa kiwanda cha DARBREW LTD tunaomba serikali iingilie kati kuwawajibisha watendaji hao waovu wenye kutanguliza maslahi binafsi kwenye jambo lrnye maslahi ya umma,hawa ni wahujumu uchumi maana wameipotezea serikali kodi nyingi kwa muda wote tangu mwaka 2018 hadi leo hii.Pia tunaomba muwekezaji huyu wa Malawi apewe kipaumbele maana ndie aliendesha kiwanda hiki kwa mafanikio na kwa faida ya serikali mwaka 2006-2013.

Tunawasilosha.

Ni sisi tuliokuwa wafanyakazi wa DARBREW LTD-Dar Es Salaam Breweries Limited kiwanda cha kutengeza chibuku.

Mzee mwenzangu umenusurika a kitambi kweli? Zile chakula ni zaidi ya ugali
 
Sio depot ni kiwanda mkuu,tatizo Prof Kitila analijua lakini hatujui kwa nini halifanyii kazi maana sio uwekezaji mpya kwamba unahitaji muda sana, DarBrew Ltd ipo tangu 1967 kinachotakiwa ni muwekezaji mpya tu ila danadana zimezidi ndio maana ni bora mama xajue sasa akina nani wanamkwamisha kupata kodi. Three years of waiting for an investor(and he was there before and they know him) to be accepted!...it's a big joke.
Environment isn't friendly to investors at all !
Sawa ngoja tuone,kibuku ilikuwa inasumbua sana Dar huku uswahili kwetu Buza,Manzese,Tandale,keko Kitintale,Kisiwani,Mchikichini,Chama,Malapa n.k wamekuja hawa wa banana ila bado hawajafikia usumbufu wa kibuku😂😂😂
 
You don't drink it,why bother? Au na we ni muathirika wa huu uzi?😂
Kwa walioguswa mtusamehe,we keep on removing the cockroaches out of the way...nothing can stop us,these hooligans will eat their sheets soon
 
Back
Top Bottom