Rais Samia kama kweli uko makini na lugha ya Kiswashili basi anzia nyumbani - Tanzania ndio inaongoza kwa kuharibu lugha ya Kiswahili

James Martin

JF-Expert Member
Apr 2, 2016
1,206
1,509
Mimi kama Mtanzania nipendaye lugha yangu ya Kiswahili nasikitika sana kuona lugha hii ikiharibika. Chakusikitisha zaidi ni kwamba hakuna kiongozi yeyote wa juu kuanzia Rais, waziri wa utamaduni n.k. anayefanya jitihada madhubuti ya kukienzi Kiswahili.

Kwenye hotuba yake ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa nimemsikia rais Samia akisema kwamba kuna fedha imetengwa ili kukuza lugha ya Kiswahili. Alitaja fedha hiyo itatumika kama kuchapisha nakala za Kiswashili kwenye jumuiya ta SADC. Lakini kutoa pesa ya kuchapisha nakala za Kiswahili ni kazi bure kama sisi wenyewe hatuongei Kiswashili fasaha.

Mimi binafsi nafikiri Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kuharibu lugha ya Kiswahili. Siku hizi kumeibuka wimbi la maneno ya kijinga kabisa kwenye lugha yetu, kwa mfano,

mdada - dada
mboga mboga - mboga
fasta fasta - haraka

Haya ni baadhi ya maneno ambayo mimi binafsi nayachukia kabisa.

Hatuna haki miliki lakini mimi nasema Kiswahili ni mali yetu! Ni lugha yetu ya taifa na Watanzania tunakitumia Kiswahili kuliko nchi yeyote duniani. Faida za Kiswahili ni kama kuunganisha watu, kuwafanya wanamuziki wetu kuuza nyimbo zao nje ya Tanzania na mwisho Kiswahili kinalinda heshima ya Tanzania kwasababu ni lugha yetu.

Moja ya hatua ninayopendekeza ni kwa vyombo husika kuvipiga faini vituo vya utangazaji na magazeti pale wanaposhindwa kutumia Kiswahili fasaha.

Watu wa nje wanafikiri eti Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kuongea Kiswahili fasaha, lakini hawajui kuwa Tanzania pia ndio nchi inayoongoza kwa kuharibu lugha ya Kiswahili!
 
Kwanini tutumie pesa za walipa kodi kuchapisha machapisho ya lugha ambayo siyo mali yetu? Watanzania hakuna haki miliki ya kiswahili, Kwanini tunakuwa wajinga hivi lakini?
 
Naamini pia Rais Samia atakipa msukumo wa kutosha kama ilivyo kuwa kwa Mtangulizi wake.
 
Huku Pwani wanajifanya wanajua sana kiswahili ila kwa uchunguzi wangu wa miaka kumi na mbili nimegundua wanaharibu Sana kiswahili

Siyo kwenye kuongea tu, yaani lahaja siyo nzuri mpaka kwenye maandishi

Niliwahi kukutana na bango mtaani ambalo limeandikwa na Afisa mtendaji kata (WEO)
Likiwa linawakaribisha/alika wananchi wake kwenye mkutano wa hadhara

Kilichoandikwa sikutarajia kutoka kwake, Tena ni mtu ninayemuamini walau kafuta ujinga

Pia lafudhi ya kibara nayo huchangia kuharibu kiswahili, kwa kiasi kikubwa
Waha, wasukuma, na wote wanaokaa mipakani karibu na nchi jirani.


Lakini Kuna ile "Swangilish" yaani anauudhi mtu ambaye mnazungumza lakini anachanganya kiingereza na kiswahili,

Wakati hapohapo akija mtu ambaye anaongea kiingereza tu Bado hawezi kuongea naye "maajabu haya"

Naunga mkono bandiko kwa asilimia mia moja
 
Huku Pwani wanajifanya wanajua sana kiswahili ila kwa uchunguzi wangu wa miaka kumi na mbili nimegundua wanaharibu Sana kiswahili

Siyo kwenye kuongea tu, yaani lahaja siyo nzuri mpaka kwenye maandishi

Niliwahi kukutana na bango mtaani ambalo limeandikwa na Afisa mtendaji tarafa (WEO)
Likiwa linawakaribisha/alika wananchi wake kwenye mkutano wa hadhara

Kilichoandikwa sikutarajia kutoka kwake, Tena ni mtu ninayemuamini walau kafuta ujinga

Pia lafudhi ya kibara nayo huchangia kuharibu kiswahili, kwa kiasi kikubwa
Waha, wasukuma, na wote wanaokaa mipakani karibu na nchi jirani.


Lakini Kuna ile "Swangilish" yaani anauudhi mtu ambaye mnazungumza lakini anachanganya kiingereza na kiswahili,

Wakati hapohapo akija mtu ambaye anaongea kiingereza tu Bado hawezi kuongea naye "maajabu haya"

Naunga mkono bandiko kwa asilimia mia moja
Afisa mtendaji wa tarafa!!!?? Hakuna cheo cha muuondo huo kuna afisa tawala /katibu tawala tarafa DIVISION ADMNISTRATIVE OFFICER . WEO ni WARD EXECUTIVE OFFICER (Afisa Mtendaji wa Kata)
 
Kwanini tutumie pesa za walipa kodi kuchapisha machapisho ya lugha ambayo siyo mali yetu? Watanzania hakuna haki miliki ya kiswahili, Kwanini tunakuwa wajinga hivi lakini?
Hatuna hati miliki lakini Kiswahili ni lugha yetu
 
Mimi kama Mtanzania nipendaye lugha yangu ya Kiswahili nasikitika sana kuona lugha hii ikiharibika. Chakusikitisha zaidi ni kwamba hakuna kiongozi yeyote wa juu kuanzia Rais, waziri wa utamaduni n.k. anayefanya jitihada madhubuti ya kukienzi Kiswahili.

Kwenye hotuba yake ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa nimemsikia rais Samia akisema kwamba kuna fedha imetengwa ili kukuza lugha ya Kiswahili. Alitaja fedha hiyo itatumika kama kuchapisha nakala za Kiswashili kwenye jumuiya ta SADC. Lakini kutoa pesa ya kuchapisha nakala za Kiswahili ni kazi bure kama sisi wenyewe hatuongei Kiswashili fasaha.

Mimi binafsi nafikiri Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kuharibu lugha ya Kiswahili. Siku hizi kumeibuka wimbi la maneno ya kijinga kabisa kwenye lugha yetu, kwa mfano,

mdada - dada
mboga mboga - mboga
fasta fasta - haraka

Haya ni baadhi ya maneno ambayo mimi binafsi nayachukia kabisa.

Hatuna haki miliki lakini mimi nasema Kiswahili ni mali yetu! Ni lugha yetu ya taifa na Watanzania tunakitumia Kiswahili kuliko nchi yeyote duniani. Faida za Kiswahili ni kama kuunganisha watu, kuwafanya wanamuziki wetu kuuza nyimbo zao nje ya Tanzania na mwisho Kiswahili kinalinda heshima ya Tanzania kwasababu ni lugha yetu.

Moja ya hatua ninayopendekeza ni kwa vyombo husika kuvipiga faini vituo vya utangazaji na magazeti pale wanaposhindwa kutumia Kiswahili fasaha.

Watu wa nje wanafikiri eti Tanzania ndio nchi inayoongoza kwa kuongea Kiswahili fasaha, lakini hawajui kuwa Tanzania pia ndio nchi inayoongoza kwa kuharibu lugha ya Kiswahili!
Wewe huna kitu cha kufanya?
 
Back
Top Bottom