Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuepuka mashikizo ya kisisa akieleza kuwa kuwa mshikamano kati ya uongozi wa kisiasa na uongozi wa kijeshi ni nguzo muhimu ya usalama wa Taifa, hata hivyo amesisitiza kuwa JWTZ ni jeshi la wananchi na linapaswa kubaki huru na siasa za vyama, likiwa na utii kwa Serikali halali iliyopo madarakani.
Rais Samia ameyasema hayo akizungumza na Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kabla ya kufungua mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga tarehe 15 Desemba 2025.
Rais Samia ameyasema hayo akizungumza na Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kabla ya kufungua mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga tarehe 15 Desemba 2025.