GE2025 Rais Samia aweka shada la maua kwenye kaburi la Mwalimu Nyerere

GE2025 Rais Samia aweka shada la maua kwenye kaburi la Mwalimu Nyerere

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu Mpendwa Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge.

Leo Hii amefika na kuweka shada la Maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere. Ikumbukwe ya Kuwa Rais wetu anaendelea na kampeni Kuelekea uchaguzi Mkuu katika kutafuta nafasi ya kuingia Ikulu kuongoza awamu ya pili.

Ikumbukwe ya Kuwa Rais wetu Mpendwa amefanya mambo makubwa sana ambayo ilikuwa ni ndoto ya Baba wa Taifa. Ikumbukwe ilikuwa ni ndoto ya Baba wa Taifa kujenga na kukamilisha Bwawa la Mwalimu Nyerere,kutoa Elimu bure,kutokomeza umaskini,maradhi na ujinga. Mambo na vitu ambavyo Rais wetu amevitekeleza kikamilifu kabisa.
Screenshot_20251010-163804_1.jpg


Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Back
Top Bottom