Rais Samia atoa wastani wa madarasa manne na madawati 120 katika kila shule ya Sekondari nchi nzima

Ishu ni Mkopo. Tumeshindwa kufanya hayoyote kwa makusanyao ya kodi, hadi IMF watukopeshe. Hebu niambie ni sekta ipi ambayo serikali kwa 100% inatumia makusanyo yake ya kodi
Bora tushibe,pesa itoke kokote,madhali ajira zitakuwa nyingi.Hapo kuanzia,mafundi,wauza vifaa vya ujenzi,wauza mbao,misumari,vibarua,wachora ramani,mama lishe,wenye virukuu,wamachinga,wauza sokoni,wote watapata pesa.
 
Umesema kweli tupu.
Ndio maana hatutaendelea kamwe kazi kusifia sijui mwalipwa ngapi!
Hizi ni fedha za hao tunaowaita majina yasiyoeleweka.
Kwani bajeti ya hizi wizara inafanya kazi gani? Ndio hapo zinapigwa kimyakimya.
Hamna shida zinunuliwe kwa wingi kwa manufaa.
Vipi na Fire trucks kwani vinaenda sambamba na huduma ya uokoaji?

Tuamke Katiba Katiba ni kipaumbele!


Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
 
😍😍😍😍 Nchi tajiri sana na inajiweza

Kuihudumia bajeti kwa zaidi ya 90% sio mchezo

#KAZIIENDELEE KWA KASI &WELEDI ZAIDI
Hii nchi ni ya ovyo sana yanazungumzwa mengine tofauti na uhalisia...mnasema nchi ni tajiri sana Ila mikopo kila siku mnaichukua....halafu mambo ya kusema "rais atoa" tulishayakataa semeni "serikali yatoa"
 
Hii nchi ni ya ovyo sana yanazungumzwa mengine tofauti na uhalisia...mnasema nchi ni tajiri sana Ila mikopo kila siku mnaichukua....halafu mambo ya kusema "rais atoa" tulishayakataa semeni "serikali yatoa"
Kwani kunatofauti gani kati ya Serikali na Rais,
 
Ndio maana hatutaendelea kamwe kazi kusifia sijui mwalipwa ngapi!
Hizi ni fedha za hao tunaowaita majina yasiyoeleweka.
Kwani bajeti ya hizi wizara inafanya kazi gani? Ndio hapo zinapigwa kimyakimya.
Hamna shida zinunuliwe kwa wingi kwa manufaa.
Vipi na Fire trucks kwani vinaenda sambamba na huduma ya uokoaji?

Tuamke Katiba Katiba ni kipaumbele!


Sent from my SM-A115AZ using JamiiForums mobile app
Kwenye bajeti kuna sehemu ya mikopo pia Chief,
 

Rais Samia atoa wastani wa madarasa manne na madawati 120 katika kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima | Hakika awamu ya Sita Tanzania lazima iwe Tanzania.​

" Hakuna kama Samaia "​


Baada ya janga la Covid-19 kuvuruga Uchumi wa dunia na sisi tukiwemo, Shirika la fedha duniani ( IMF) pamoja na benki ya dunia ( WB) wameanza kuzisaidia nchi mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania mikopo yenye masharti nafuu ili pesa hizo zitumike kama Economic Stimulus & Relief Fund na hapa muelewe vizuri Tanzania tunapokea mikopo na misaada ila "HATUITEGEMEI " ndio maana hata kwenye bajeti yetu hii ya FY2021|22 katia ya Tshs 36.33trl zilizotengwa pesa zetu ni 91.9% huku misaada na mikopo ikiwa ni 8.1% tu,

IMF tayari imeisaidia Tanzania mkopo wenye masharti nafuu kiasi cha Tshs 1.3trl kwaajili ya kusisimua Uchumi wake uliodorora kwasababu ya covod-19 kwani niukweli usiopingika Tanzania tumeumizwa zaidi kwenye Sekta za Utalii,biashara na Usafirishaji,

Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutumia pesa hizo na baada ya kutoa madarasa ya kisasa elfu 15 sawa na wastani wa madarasa manne kwenye kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima huku kipaumbele kikiwa ni shule zenye upungufu wa madarasa lakini furaha iliyoje Rais wetu ametoa tena jumla ya madawati 462,795 ambayo ni sawa na Wastani wa madawati 120 kwenye kila Shule ya Sekondari nchi nzima ambazo jumla ya shule hizo ni 3,863.

Sababu za Rais Samia Suluhu Hassan kutoa madarasa mapya manne ya kisasa na madawati mapya 120 katika kila shule ya Sekondari ya Serikali nchi nzima ni kuhakikisha wazazi wa watoto watakaojiunga na kidato cha kwanza mwakani katika mwaka wa masomo 2021|2025 hawalipi hata Shilingia mia moja kwani Rais wetu mnyenyekevu ameshalipa pia ada za watoto wote 1M wanaotakiwa kuanza shule siku moja nchi nzima yaani trh 06|01|2022,hii haijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu,


VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA

nimeona moyo wa uzalendo na uthubutu wa Mama yetu Samia Suluhu Hassan katika kutuletea maendeleo Wa Tanzania.
Hakika Tanzania inakwenda kupiga hatua kubwa katika Sector ya afya elimu na Maji.
 
Huyu mtu CM1774858 sijui analipwa ngapi? lakini at least ana news positive hata kama anaongeza chumvi kiasi, kuna yule wa youtube anaitwa Musiba wakati wa Magufuli that guy was very negative na kazi yake kutishia watu tuu, nafikiri alikuwa anajiona untouchable
 
nimeona moyo wa uzalendo na uthubutu wa Mama yetu Samia Suluhu Hassan katika kutuletea maendeleo Wa Tanzania.
Hakika Tanzania inakwenda kupiga hatua kubwa katika Sector ya afya elimu na Maji.
Nikweli kabisa mkuu,

Tuendelee kumpigania,
 
Huyu mtu CM1774858 sijui analipwa ngapi? lakini at least ana news positive hata kama anaongeza chumvi kiasi, kuna yule wa youtube anaitwa Musiba wakati wa Magufuli that guy was very negative na kazi yake kutishia watu tuu, nafikiri alikuwa anajiona untouchable
Mkuu naongeza chumvi gani?

Bahati mbaya sana sifahamiana na kiongozi yoyote wa ngazi ya juu,

Mimi ni mwanachama tu mtiifu mwenye Uzalendo kwa nchi yangu,

Nakusihi nawewe uniunge mkono katika hili,

Nimbaya sana kuisemea nchi yako mabaya na kuiombea mabaya


#KAZI IENDELEE KWA KASI & WELEDI ZAIDI
 
Back
Top Bottom