jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,062
- 28,252
Mnyonge mnyongeni ila sifa yake muachieni.
Sisi waswahilli tunatumia msemo huu kumsemea asiyependa kujikweza.
Kabla ya kuingia katika madaraka ya Urais mhe.Samia Suluhu Hassan amekuwa ni muumini wa kuigwa na kutajwa kama mfano kati ya Viongozi wachache nchini waliotoa kipaumbele kwa vitendo kwa sekta ya Afya.
Ukiongelea kimahsusi Rais Samia amefanya mengi katika sekta ya Afya hususani afya ya uzazi ,wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
Kipekee kama mdau wa afya nitaje machache na muhimu aliyoweza kuyatolea maamuzi na msisitizo.
1-Kampeni ya kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga...Jiongeze tuwavushe salama.
2-Hamasa na ufuatiliaji katika suala la lishe
3-Maamuzi Magumu yatakayorejewa ya kuanzisha tozo iliyojenga vituo vya afya katika kila tarafa na kata zenye jografia ya kimkakati.
4-Maamuzi kuntu ya kupeleka fedha za uviko 19 katika sekta ya afya na maji kwa minajili ya afya kinga na tiba.
5-Sambamba na namba 4 hapo juu ni ujenzi wa miundombinu ya huduma za dharura na mahututi (EMDs na ICUs)katika hospitali za mikoa na wilaya.
6-Ajira ya watumishi wengi wa afya kuliko mtangulizi yoyote kabla yake.
7-Ununuzi wa vifaa tiba muhimu na vya kipekee katika hospitali ngazi ya afya ya msingi na hospitali za rufaa
8-Uboreshaji wa utendaji kazi wa MSD uliombatana na upelekaji wa fedha za dawa /vifaa tiba kwa wakati MSD
9-JARIBIO MAHSUSI LA KUTAKA KUWA NA SERA YA BIMA YA AFYA KWA WOTE(Japo wizara na wabunge hawakulitendea haki).
10-Kutumia diplomasia na weledi wake wa NGOs kuhakikisha uwezeshaji katika sekta ya afya unakuwa mkubwa na rahisi.
Nimetaja machache na ya kipekee ili umma ujionee na kuweka kumbukumbu.
MAONI NA OMBI
-Bado Wizara zinazohusika na Afya hazijajipanga ipasavyo katika kutafsiri dhamira ya mhe. Rais...yaani bado zipo kwenye mvutano usio kuwa na tija kwa jamii.
Hapa kuna uhitaji wa kuwaweka sawa wizara mtambuka zinazogusa afya ili kuona tija ya maamuzi ya Mhe.Rais.
-Asichoke kuwekeza kwenye Afya kwani bado ni adui miongoni mwa maadui watatu wa Taifa.
-Mhe.Rais aitishe wasaidizi wake wote ikiwemo wale waliopo katika ngazi za chini wampe strategies za kuboresha Maswala ya Afya hususani kwa jamii iliyoko chini kabisa kiuchumi ,kielimu,kiutawala na kiujitaji.
MWISHO
Pongezi nyingi kwako Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa hili na Mungu atakulipa.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!
Sisi waswahilli tunatumia msemo huu kumsemea asiyependa kujikweza.
Kabla ya kuingia katika madaraka ya Urais mhe.Samia Suluhu Hassan amekuwa ni muumini wa kuigwa na kutajwa kama mfano kati ya Viongozi wachache nchini waliotoa kipaumbele kwa vitendo kwa sekta ya Afya.
Ukiongelea kimahsusi Rais Samia amefanya mengi katika sekta ya Afya hususani afya ya uzazi ,wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
Kipekee kama mdau wa afya nitaje machache na muhimu aliyoweza kuyatolea maamuzi na msisitizo.
1-Kampeni ya kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga...Jiongeze tuwavushe salama.
2-Hamasa na ufuatiliaji katika suala la lishe
3-Maamuzi Magumu yatakayorejewa ya kuanzisha tozo iliyojenga vituo vya afya katika kila tarafa na kata zenye jografia ya kimkakati.
4-Maamuzi kuntu ya kupeleka fedha za uviko 19 katika sekta ya afya na maji kwa minajili ya afya kinga na tiba.
5-Sambamba na namba 4 hapo juu ni ujenzi wa miundombinu ya huduma za dharura na mahututi (EMDs na ICUs)katika hospitali za mikoa na wilaya.
6-Ajira ya watumishi wengi wa afya kuliko mtangulizi yoyote kabla yake.
7-Ununuzi wa vifaa tiba muhimu na vya kipekee katika hospitali ngazi ya afya ya msingi na hospitali za rufaa
8-Uboreshaji wa utendaji kazi wa MSD uliombatana na upelekaji wa fedha za dawa /vifaa tiba kwa wakati MSD
9-JARIBIO MAHSUSI LA KUTAKA KUWA NA SERA YA BIMA YA AFYA KWA WOTE(Japo wizara na wabunge hawakulitendea haki).
10-Kutumia diplomasia na weledi wake wa NGOs kuhakikisha uwezeshaji katika sekta ya afya unakuwa mkubwa na rahisi.
Nimetaja machache na ya kipekee ili umma ujionee na kuweka kumbukumbu.
MAONI NA OMBI
-Bado Wizara zinazohusika na Afya hazijajipanga ipasavyo katika kutafsiri dhamira ya mhe. Rais...yaani bado zipo kwenye mvutano usio kuwa na tija kwa jamii.
Hapa kuna uhitaji wa kuwaweka sawa wizara mtambuka zinazogusa afya ili kuona tija ya maamuzi ya Mhe.Rais.
-Asichoke kuwekeza kwenye Afya kwani bado ni adui miongoni mwa maadui watatu wa Taifa.
-Mhe.Rais aitishe wasaidizi wake wote ikiwemo wale waliopo katika ngazi za chini wampe strategies za kuboresha Maswala ya Afya hususani kwa jamii iliyoko chini kabisa kiuchumi ,kielimu,kiutawala na kiujitaji.
MWISHO
Pongezi nyingi kwako Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa hili na Mungu atakulipa.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!!