Rais Samia amewatuma Mabalozi wakaulize wenzetu wamefanya uchawi gani kukua haraka kiuchumi

Rais Samia Suluhu Hassan anasema :

"Sote tunafahamu kuwa miaka ya 1960/70 nchi yetu na nchi za bara la Asia zilikuwa na uchumi unaolingana, lakini 'baada ya muda' wenzetu wametupita tena sana. Mfano Thailand kwa miaka hiyo ilikuwa na 'GDP Per Capita' ya Dola 166 na Tanzania tulikuwa 165. Leo Thaliland wako Dola 7,495 na sisi tuko 1,227.

Kwa hiyo hao mnaokwenda upande huo (Mabalozi) mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kwenda haraka hivyo na sisi tunakosa nini? 'mentality' au vitu gani? Tuna 'resource' hatuzitumi? Mtuambie wenzetu
wamefanya nini na sisi tufanye nini."

Yaani Rais kushindwa kuelewa suala kama Hilo, why nchi kama Thailand imepaa kiuchumi? Kweli hapa katiba imetukatili..ndio maana nchi zingine Rais akifariki wanaitisha uchaguzi mkuu ili wananchi wampime kama anatosha kukalia hicho kiti na je ana uelewa mpana wa dhana ya maendeleo?
Rais hujui nini cha kufanya ili tuendelee?! Unataka kukopi historia ya nchi nyingine?! Duh!
 
Uchawi waliotumia wenzetu nikukataa kuwa mawakala wa shetani, kila mtu analazishwa kufanya mambo kwa kiasi, kutenda haki na kutoa sadaka siyo kusubiri kupewa, Sasa sisi tupo kinyumenyume, kuwa na familia kubwa sana mpaka tunakosa kutoridhika muda wote unataka mpaka vitu visivyovyako, hatufanyi haki Yale tusiyopenda kufanyiwa sisi tunawafanyia wengine, dhuruma, chuki mpaka mtu anafikia kufanya uchawi ili mwenzie aumie, sisi kila mtu ni ombaomba haridhiki na chake Wala kuishi ndani ya bajeti yake na ikitokea amekopa harudishi.

Sasa viongozi wa dini wanaongoza kufundisha mafanikio ya mali na serikali nayo inapamba na mtu kumiliki mali, na kufundisha dhambi yaani watu waache dhambi wanasahau hakuna haja ya kufundisha mtu yeyote kuacha dhambi Bali wanatakiwa wafundishe kutenda haki maana haki huinua taifa na haki inainua mtu mmojamoja maana yake kila mtu akimtendea mwenzie haki basi Mungu atabariki sehemu hiyo, hata amri kumi za Mungu zipo kwenye mfumo wa kutendea haki ndo maana huoni kule wanasema usilewe, maana unaweza kulewa lakini ukawa unatenda haki, Sasa dhambi ipo kwaajili ya mtu na Mungu na dhambi inampa mtu husika na aibu yake hata maandiko yamesema hivyo, Sasa Africa ni kichaka Cha Mambo ya kishetani kila kitu kinyumenyume na haki haitendeki kwa mtu mmojamoja na hata vyombo vinavyojiita vya kutoa haki kwenye nchi vinafanya dhuruma kwa kunyima watu haki zao, Sasa hebu warudi kufundisha haki kwa wote na kuitendea kila mahali waone nchi itavyoneemeka.
Vile vile mama aambiwe kuwa hizo nchi hazikuingia mikataba mibovu kama huu wa bandari.
 
Rais Samia Suluhu Hassan anasema :

"Sote tunafahamu kuwa miaka ya 1960/70 nchi yetu na nchi za bara la Asia zilikuwa na uchumi unaolingana, lakini 'baada ya muda' wenzetu wametupita tena sana. Mfano Thailand kwa miaka hiyo ilikuwa na 'GDP Per Capita' ya Dola 166 na Tanzania tulikuwa 165. Leo Thaliland wako Dola 7,495 na sisi tuko 1,227.

Kwa hiyo hao mnaokwenda upande huo (Mabalozi) mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kwenda haraka hivyo na sisi tunakosa nini? 'mentality' au vitu gani? Tuna 'resource' hatuzitumi? Mtuambie wenzetu
wamefanya nini na sisi tufanye nini."

Yaani Rais kushindwa kuelewa suala kama Hilo, why nchi kama Thailand imepaa kiuchumi? Kweli hapa katiba imetukatili..ndio maana nchi zingine Rais akifariki wanaitisha uchaguzi mkuu ili wananchi wampime kama anatosha kukalia hicho kiti na je ana uelewa mpana wa dhana ya maendeleo?
Mkuu naona haufikirii kwa usahihi.
- kwamba katiba imetukatili kwa kumuweka madarakani mtu asiyejuwa kwanini nchi kama thailand imetuacha kimaendeleo.
-Sasa hebu uniambie katiba inatuhakikishiaje kuwa mtu anayekwenda ikuru kwa njia ya kura anafahamu chanzo cha udumavu wetu?

- Kama katiba inatuhakikishia kuwa atakeye kaa kwenye kitu cha urais atakuwa anafahamu chanzo cha udumavu wetu(kwani alipigiwa kura tofauti na Samia kwenda ikuru), kwanini tumedumaa? Au takwa la katiba kwa rais ni kujuwa tu chanzo cha tatizo na si kuchukuwa hatuwa dhidi ya tatizo?

-alafu,.........
 
Rais Samia Suluhu Hassan anasema :

"Sote tunafahamu kuwa miaka ya 1960/70 nchi yetu na nchi za bara la Asia zilikuwa na uchumi unaolingana, lakini 'baada ya muda' wenzetu wametupita tena sana. Mfano Thailand kwa miaka hiyo ilikuwa na 'GDP Per Capita' ya Dola 166 na Tanzania tulikuwa 165. Leo Thaliland wako Dola 7,495 na sisi tuko 1,227.

Kwa hiyo hao mnaokwenda upande huo (Mabalozi) mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kwenda haraka hivyo na sisi tunakosa nini? 'mentality' au vitu gani? Tuna 'resource' hatuzitumi? Mtuambie wenzetu
wamefanya nini na sisi tufanye nini."

Yaani Rais kushindwa kuelewa suala kama Hilo, why nchi kama Thailand imepaa kiuchumi? Kweli hapa katiba imetukatili..ndio maana nchi zingine Rais akifariki wanaitisha uchaguzi mkuu ili wananchi wampime kama anatosha kukalia hicho kiti na je ana uelewa mpana wa dhana ya maendeleo?
Siri kubwa ya Asia, Singapore kwa mfano.
- Wanachagua na kuteua bright minds kuwa katika majukumu serikalini na hata mawaziri. hakuna nepotism ya kuteua mtu kwa sababu baba yake alikuwa kiongozi ktk chama.

-Hawacheki kuhusu ufisadi na hawaangalii sura. Ingekuwa nchi za Asia, mikataba ya ajabu ajabu tangu ianze kusainiwa hapa tz, wengi wangeshakula vitanzi. Hata huu wa bandari kuna watu wangeshakuwa buriani.
 
Rais Samia Suluhu Hassan anasema :

"Sote tunafahamu kuwa miaka ya 1960/70 nchi yetu na nchi za bara la Asia zilikuwa na uchumi unaolingana, lakini 'baada ya muda' wenzetu wametupita tena sana. Mfano Thailand kwa miaka hiyo ilikuwa na 'GDP Per Capita' ya Dola 166 na Tanzania tulikuwa 165. Leo Thaliland wako Dola 7,495 na sisi tuko 1,227.

Kwa hiyo hao mnaokwenda upande huo (Mabalozi) mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kwenda haraka hivyo na sisi tunakosa nini? 'mentality' au vitu gani? Tuna 'resource' hatuzitumi? Mtuambie wenzetu
wamefanya nini na sisi tufanye nini."

Yaani Rais kushindwa kuelewa suala kama Hilo, why nchi kama Thailand imepaa kiuchumi? Kweli hapa katiba imetukatili..ndio maana nchi zingine Rais akifariki wanaitisha uchaguzi mkuu ili wananchi wampime kama anatosha kukalia hicho kiti na je ana uelewa mpana wa dhana ya maendeleo?
Tatizo ni wizi wa viongozi kuuza rasilimali za inchi,kupeana vyeo kindugu bila kuzingatia uwezo wa mtu,rushwa, kutokuwa na uzarendo hasa kwa viongozi, na CCM yenyewe imechoka
 
Tanzania haitakaa iendelee kuvuka ngazi ya LDC hadi itakapopata UONGOZI BORA.

Nyerere mwenyewe alitaja kwa usahihi kabisa nguzo kuu tatu za msingi wa maendeleo: watu, siasa safi na uongozi bora. WATU tupo naturally. Mwenyenzi Mungu katuweka kwenye nchi yenye baraka zote.

Kwa bahati mbaya sana JKN mwenyewe akaanza kuongoza nchi kwa misingi ya SIASA DHAIFU na UONGOZI WA MTU MMOJA (one man show). Uongozi wake ulikuwa bora kwa vile yeye binafsi alikuwa na maadili ya kipekee. Hadi anaondoka msingi mbovu wa siasa na uongozi (mfumo CCM) ulibaki na kudumu vile vile hadi leo huku mafisadi wa kila aina wakiingia madarakani.

In short, TUSAHAU KABISA habari ya maendeleo kwa aina ya siasa na mfumo wa uongozi tulio nao. Sina jibu nisije kuunganishwa kwenye kadhia inayoendelea.
 
Muandishi wewe umetafsiri vibaya.

Rais kusema uchawi gani , Amemaanisha mbinu gani hajamaanisha matunguli
...Ina maana hajui Mbinu zilizotumika kuzifanya Nchi zilizotajwa Zirndelee ! Hata MBINU hajui Mpaka Watu anaoteua wakaulize ???
 
Kama anafanya akiwa na dhamira ya haki na Sheria za haki hakuna tatizo.
...Kuzimilikisha Bandari zetu zote Kwa Mkataba usiojulikana Wazi ni WA Muda gani, ndio kuwa na Dhamira ya Haki ???
Pleeaaseee...!
 
Ila kiukweli HATERS NA NYUMBU mnatia huruma wakati mwingine; yaani mnataka kusema mmeshindwa kuelewa mantiki ya alichokisema hapo au mnajitoa ufahamu tu in the name of hatred?!!!!

Hamuwezi kumshinda kwa viroja vyenu vya kijingajinga kama hivi nyie kenge. Mabalozi wanalazimika kuwa na jicho la 'wizi' wa kiuchumi na sio kwenda kula bata tu na kusinzia.......simple tu kuelewa ukiwa katika akili huru.

Mama ataendelea kupiga hatua za kimaendeleo mpende msipende.
 
Rais Samia Suluhu Hassan anasema :

"Sote tunafahamu kuwa miaka ya 1960/70 nchi yetu na nchi za bara la Asia zilikuwa na uchumi unaolingana, lakini 'baada ya muda' wenzetu wametupita tena sana. Mfano Thailand kwa miaka hiyo ilikuwa na 'GDP Per Capita' ya Dola 166 na Tanzania tulikuwa 165. Leo Thaliland wako Dola 7,495 na sisi tuko 1,227.

Kwa hiyo hao mnaokwenda upande huo (Mabalozi) mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kwenda haraka hivyo na sisi tunakosa nini? 'mentality' au vitu gani? Tuna 'resource' hatuzitumi? Mtuambie wenzetu
wamefanya nini na sisi tufanye nini."

Yaani Rais kushindwa kuelewa suala kama Hilo, why nchi kama Thailand imepaa kiuchumi? Kweli hapa katiba imetukatili..ndio maana nchi zingine Rais akifariki wanaitisha uchaguzi mkuu ili wananchi wampime kama anatosha kukalia hicho kiti na je ana uelewa mpana wa dhana ya maendeleo?
ikumbukwe huyo ni form four failure na alikwenda kuolewa baada ya kumaliza form four.

Elimu yake mpaka alipofika ni ya kuunga unga
 
Thailand wameendelea kwa sababu ya uwekezaji wenye tija ambao uko wazi kwa wananchi.Huko hakuna upuuzi wa kuuza Maliasili kama huu upuuzi wa uuzaji maliasili Tanganyika ikiwemo bandari.Kama kweli rais hajui wenzetu wamefanyaje hadi kufika hapo walipo kimaendeleo basi aachie hiyo nafasi.
 
Uchawi mojawapo ni kuingia mikataba inayonyonya rasilimali za waafrika..mkataba wa kinyonyaji kama ule wa Dp world..hapo ndio tatizo linaanzia aache kutaja habari za kichawi..yeye mwenyewe kashalogwa nq waarabu..natabia hizo anazozifanya ndio inafanya bara la Africa lisiendelee
Hili ndiyo tatizo kuu imagine dhahabu iliyochimbwa Geita na Kahama kama 50% tu ya kilichovunwa tangu 98 walipoanza kuzalisha kingetumika kuleta maendeleo kanda ya ziwa ingekuwa na maendeleo makubwa sana lakini leo hii hata jirani na mgodi kuna shule hazina matundu ya vyoo achilia mbali madarasa.
 
Wana jamvi samahani ....naomba kuuliza ili uwe PRESIDENT ni sifa zipi muhimu lazma uwe nazo ....... nahisi kuna mahali tulisha feli kama taifa
 
“Mtuambie wenzetu wamefanya uchawi gani kukua kiuchumi, na sisi tunakosa nini, tuna rasilimali hatuzitumii? au kitu gani, ila niseme ni wazi wenzetu wamepiga hatua kubwa sana licha ya kuwa sisi tumewazidi kwenye rasilimali diplomasia ya uchumi ifanye kazi hapa, tujiulize tuliachwa wapi?” - Rais SuluhuSamia

View attachment 2718932

Haiwezekani tuna kiongozi mkubwa wa nchi bado anaamini masuala ya giza katika kupata maendeleo makubwa ya kiuchumi , it look like hana a,b, c yoyote ili nchi ipate maendeleo ya kiuchumi ifanye nini ?

Hivi hili ni taifa la namna gani mtu yoyote asiwe na uelewa na masuala ya nchi kupiga hatua anapewa nafasi kubwa ya kuwa kiongozi wa nchi katika dira ya maendeleo.

Nikisema kuwa hili taifa linaongozwa na kipofu wa masuala ya maendeleo na uongozi nitakuwa nakosea jamani ?

Kwamba Rais hafahamu kuwa ili China, Russia, Qatar, U.S.A, Germany, Singapore, Malaysia, Korea, Japan n.k walifanya nini ili kupata maendeleo yao ya kiuchumi ?

Kwa kumsaidia nampa hawa watu wawe walimu kwake, ni nini kifanyike ili taifa lipate maendeleo makubwa ya uchumi na aache kuwatupia mzigo mabalozi ambao hata yeye akiaamua kuwa serious anaweza kujifunza nini kutoka kwa hawa viongozi mazuri yao economically na kutuvusha hapa tulipo:-
Francisco Franco
Park Chung Hee
Chiang kai shek
Deng Xiaoping
Urho Kekkonen
Mahathir Mohamad
Muammar Gaddafi
Lee Kuan Yew
Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum
Tanzania na imani za kishirikina
 
Back
Top Bottom