Rais Samia aagiza Barabara Mwanza Mjini ijengwe njia nne

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara ya Ujenzi kufanya usanifu wa kina wa barabara za Mwanza Mjini hadi Round about ya Usagara na barabara ya Mwanza Mjini hadi Igoma ili zipewe kipaumbele katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya kujenga barabara ya njia nne.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema hayo Mkoani Mwanza leo November 12, 2023, wakati wa ziara ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda ambapo ametembelea ujenzi wa daraja la JP Magufuli (Kigongo- Busisi) ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 80.

“Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amenielekeza kufanya haraka sana usanifu wa kina wa barabara mbili, barabara ya Mwanza Mjini Kwenda Usagara Kilometa 22 na Mwanza Mjini kuelekea Igoma ili ziwekwe kwenye vipaumbele vya bajeti ya 2024/25 kujengwa kwa njia nne”

Bashungwa amesema kwa kutambua umuhimu wa daraja la JP Magufuli katika kuunganisha ushoroba wa Ziwa Viktoria unaoanzia Sirari mpakani mwa nchi ya Tanzania na Kenya hadi Mutukula Mpakani mwa Tanzania na Uganda, barabara hiyo itapanuliwa na kuwa na njia nne ili kupunguza msongamano wa magari.

Kwa upande wake Makonda amesema daraja la JP Magufuli ni la kimkakati kwani Mkoa wa Mwanza ni katikati ya Nchi za Afrika Mashariki, hivyo itakuwa ni njia ya mkato wa kufikia Nchi jirani.
#MillardAyoUPDATES
 
Hizi ni siasa tu, kama sio siasa basi Bashungwa muombe Mama akupe barabara moja tu wilayani kwako kutoka Kayanga mpaka wilayani Kyerwa au Mulongo, hauoni watumishi wa halmashauri wanavyoteseka kutoka huko Kyerwa mpaka makao makuu ya mkoa.Lifanyie kazi basi hili ombi na barabara za namna hii ziko nyingi sana na zenye ulazima kuliko hizo mnazosema, Mwanza kuna foleni gani kama sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi.
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara ya Ujenzi kufanya usanifu wa kina wa barabara za Mwanza Mjini hadi Round about ya Usagara na barabara ya Mwanza Mjini hadi Igoma ili zipewe kipaumbele katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya kujenga barabara ya njia nne.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema hayo Mkoani Mwanza leo November 12, 2023, wakati wa ziara ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda ambapo ametembelea ujenzi wa daraja la JP Magufuli (Kigongo- Busisi) ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 80.
Hizi kampeni kumbe zimeshika moto kwelikweli?
Na watu wako tayari kusahau kila kitu kwa hadaa za aina hii kweli?
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara ya Ujenzi kufanya usanifu wa kina wa barabara za Mwanza Mjini hadi Round about ya Usagara na barabara ya Mwanza Mjini hadi Igoma ili zipewe kipaumbele katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 kwa ajili ya kujenga barabara ya njia nne.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema hayo Mkoani Mwanza leo November 12, 2023, wakati wa ziara ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Paul Makonda ambapo ametembelea ujenzi wa daraja la JP Magufuli (Kigongo- Busisi) ambalo ujenzi wake umefikia asilimia 80.

“Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amenielekeza kufanya haraka sana usanifu wa kina wa barabara mbili, barabara ya Mwanza Mjini Kwenda Usagara Kilometa 22 na Mwanza Mjini kuelekea Igoma ili ziwekwe kwenye vipaumbele vya bajeti ya 2024/25 kujengwa kwa njia nne”

Bashungwa amesema kwa kutambua umuhimu wa daraja la JP Magufuli katika kuunganisha ushoroba wa Ziwa Viktoria unaoanzia Sirari mpakani mwa nchi ya Tanzania na Kenya hadi Mutukula Mpakani mwa Tanzania na Uganda, barabara hiyo itapanuliwa na kuwa na njia nne ili kupunguza msongamano wa magari.

Kwa upande wake Makonda amesema daraja la JP Magufuli ni la kimkakati kwani Mkoa wa Mwanza ni katikati ya Nchi za Afrika Mashariki, hivyo itakuwa ni njia ya mkato wa kufikia Nchi jirani.
#MillardAyoUPDATES
Stupid and pathetic! Sasa anafikiri agizo ndio rasilimsli fedha? Na mipsngo? Vitu havijengwi sio kwasababu hakuna maagizo,fund hakuna na mipsngo
 
Hizi ni siasa tu, kama sio siasa basi Bashungwa muombe Mama akupe barabara moja tu wilayani kwako kutoka Kayanga mpaka wilayani Kyerwa au Mulongo, hauoni watumishi wa halmashauri wanavyoteseka kutoka huko Kyerwa mpaka makao makuu ya mkoa.Lifanyie kazi basi hili ombi na barabara za namna hii ziko nyingi sana na zenye ulazima kuliko hizo mnazosema, Mwanza kuna foleni gani kama sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi.
Katika Jimbo lake Bashungwa, Hivi kuna Barabara ambayo ni muhimu sana katika kuunganisha nchi za Africa Mashariki kama kutoka Nyakahanga hadi Benaco kilomita 124 tu. Huyu Bashungwa huwa simuelewi au kwa vile mama yake ni msukuma!
 
shida sana aisee, hela za walipa kodi zinachezewa sana.

Hiyo barabara siku ya kwanza inajengwa hizo lane mbili walipaswa wawe wameshalijua na kulifanya hilo mapema.
Yaani mipango yetu sijui kwanini ipo kwa ajili ya leo na sio kesho.
 
Barabara Njia nne kwenye majiji ni suluhisho ya kuyaweka majiji yawe ya kisasa na kuhimili msongamano wa magari. Wacha tuone kwa Mwanza, Arusha tayari, bado Mbeya na Mwanza. isije ikwa hadaa ya siasa,watu wanaweka kumbukumbu. wanaompiga vita mama watachelewesha ili mradi imuathiri kisiasa. Bashungwa timiza wajibu wako tuone hiyo feasibility study imesemwa muda mrefu.
 
Hizi ni siasa tu, kama sio siasa basi Bashungwa muombe Mama akupe barabara moja tu wilayani kwako kutoka Kayanga mpaka wilayani Kyerwa au Mulongo, hauoni watumishi wa halmashauri wanavyoteseka kutoka huko Kyerwa mpaka makao makuu ya mkoa.Lifanyie kazi basi hili ombi na barabara za namna hii ziko nyingi sana na zenye ulazima kuliko hizo mnazosema, Mwanza kuna foleni gani kama sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi.
Hivi Kayanga-Kyerwa-Murongo bado hakuna lami? Maisha ya kule magumu sana.
 
Hizi ni siasa tu, kama sio siasa basi Bashungwa muombe Mama akupe barabara moja tu wilayani kwako kutoka Kayanga mpaka wilayani Kyerwa au Mulongo, hauoni watumishi wa halmashauri wanavyoteseka kutoka huko Kyerwa mpaka makao makuu ya mkoa.Lifanyie kazi basi hili ombi na barabara za namna hii ziko nyingi sana na zenye ulazima kuliko hizo mnazosema, Mwanza kuna foleni gani kama sio matumizi mabaya ya kodi za wananchi.
Mwanza unaijua au unahadithiwa
 
Mwanza unaijua au unahadithiwa
Bila hata kufika takwimu ziko kiganjani ndugu, Mwanza town/city ina watu 1,200,000 bado idadi ni ndogo sana ambayo haiwezi kusababisha foleni yoyote ile, kwa ufupi inazidiwa na Jimbo la Mbagala, sijaona Mbagala wakihitaji barabara za mitaa ziwe njia 4.Ni busara hiyo fedha kuilekeza kwa barabara za vumbi nazo zikawa na rami.
 
Back
Top Bottom