Hizo gharama za kuhamia dodoma heri wangeboresha hospitali na zahanati......Natamani ningefungua uzi huu na kukuta mjadala mzito wa faida na hasara.... Mjadala ambao ungezungumzia athari gani zitalikumba jiji la dar baada ya rwizara na serikali yote kuhamia dodoma,...Je na balozi za nchi zitahamia huko?..Ipi itakuwa athari katika uwanja wa ndege wa Dar?...Pia ni faida gani zitapatikana Dodoma na mikoa jirani, ......Tungejifunza mengi sana....Lakini kama kawa wanaJF kazi kujisifu ugreat thinker tu huku wakiongea pumba na kuhusisha siasa katika kila jambo
Juzi tulikuwa tunajadili hili.Hizo gharama za kuhamia dodoma heri wangeboresha hospitali na zahanati......
Nigeria , Malawi na south afrika baadhi ya ofisi za balozi hazipo miji mikuu wapo kwenye miji ya zamani na huduma zinapatikana kama kawaida , kwanza balozi nyindi Dsm Viza hakuna mpaka watu waombe Nairobi au south afrika , faida ni kubwa kuliko hasara .
Hii ya Dodoma kuwa ni katikati haina mashiko yoyote haina maana yoyote kwa karne hii. Kwanza katikati ukitokea wapi? Katika ya Tanzania reference point ni Dar es Salaaam?Wazo zuri Dodoma ni katikati, atasaidia kusogeza huduma za serikali jirani zaidi na mikoa mingi.
Mkuu, nimejiuliza swali hilo. Kwa karne ya zamani ilikua sawa, kwa sasa haina maana sababu zile. Ila ina maana kwa kupunguza mrundikano wa Ofisi kama walivyofanya Nigeria, issue ya katikati haina mashiko sana.Mbali na kupunguza msongamano Dar hivi bado sababu zile za kipindi cha Nyerere za kuhàmia Dodoma bado zina apply katika zama hizi?
Vizuri kabisaJamaa ipitie tena hiyo map vizuri.inaonesha mpaka wa malawi na Tanzania kwenye ziwa nyassa ambao hatuutambui,na haitatokea iwe hivyo.
Hii ya kuhamia Dodoma makada wa chama hawajaipenda kabisa.
Nashangaa sana vipaumbele vilivyopo....Juzi tulikuwa tunajadili hili.
Na tulikuwa na mawazo hayahaya.
bahati mbaya ramani zote za kimataifa ziko hivyo.Mkuu hii ramani imeitoa Malawi?? Huo mpaka hapo ziwa Nyasa Tanzania hatuutambui
Ndio wasiwasi wangu huo, isijekuwa tu eti kwa sababu Nyerere alisema. Nadhani serikali iwe makini sana kuangalia sababu halisi za kuhamia DodomaMkuu, nimejiuliza swali hilo. Kwa karne ya zamani ilikua sawa, kwa sasa haina maana sababu zile. Ila ina maana kwa kupunguza mrundikano wa Ofisi kama walivyofanya Nigeria, issue ya katikati haina mashiko sana.
Mimi nakubaliana suala la Serikali kuhamia Dodoma ili kuifanya Dar ipumue lakini siyo sababu ya eti ni katikati na hivyo Ulinzi na rahisi, hiyo ilikua ni zamani. Siku hizi Drone inafika popote ulipo!
Exactly....Sijui itapunguzaje umaskini kwakuwa ndio adui yetu namba moja!! Tunataka hospitali za rufaa kila mkoa, vyuo vya ufundi vikubwa kila mkoa,maji,umeme,reli,viwanja vya ndege nk. Tunapaswa kuvitathmini vipaumbele vyetu kwanza kwamba nini tunahitaji kabla ya nini tunapenda!! Kuna vitu vya muhimu na vitu vya muhimu zaidi