Rais Magufuli, sasa serikali ihamie Dodoma

Rais Magufuli, sasa serikali ihamie Dodoma

Wataalamu tusaidieni faida na hasara za kuhamia dodoma. Ahsanteni
Kwa bajeti ipi labda, kwa bajeti ya mwaka huu haipo, wala kwenye mpango wa miaka mitano haipo pia. Hivi wanaona ni rahisi tu kuhama ofisi kutoka mkoa mmoja hadi mwingine. Kuna mambo mengi wanatakiwa wayajue. Mawaziri wao wanaona sawa tu maana wanafanyiwa kila kitu, je hafanyakazi wamewapangia utaratibu gani? uhamisho,makazi, familia etc.
 
1. Kama serikali haiko Dodoma (sasa hivi) hao watumishi wanakwenda Dodoma kufanya nini?

2. Kama ni suala la bunge, kwa nini shughuli za bunge zisihamishiwe Dar au Kibaha? Hiyo itakuwa cheap kuliko kuanza kujenga 'white house' nyingine Dodoma...pamoja na maofisi yote yaliyopo sasa kuya-duplicate huko Dodoma

3. Suala la jam ni la mipango miji. Kama miundombinu ya barabara ingekuwa bora nina hakika tusingekuwa na jam Dar. Juzi nimetembelea Dar kidogo na sikukumbana na ile jam ya siku zote Morogoro road.

4. Kuhusu hilo la kusambaza maendeleo nitahitaji msaada wa ufafanuzi, maana ninachojua serikali na wadau wa sekta binafsi wana jukumu la kuchochea maendeleo nchi nzima kuanzia Dar, Ukerewe, Mlele, Karema, Nachingwea, Tunduru, Marangu, Kihesa, Dodoma, Nyakanazi, Tarime na kwingineko sawa sawia.
Mbali na yote lazima tujiulize je ni kipaumbele cha mpango wa miaka mitano? kama hapana sioni ulazima wake. Na bajeti hiyoinatoka wapi? ikiwa hata kwenye five years development plan haipo.
 
Hizo gharama za kuhamia dodoma heri wangeboresha hospitali na zahanati......

Ndugu yangu watanzania kazi ni kusifia tu, kuna ulazima gani wa kuhamia Dodoma, je bajeti hiyo inatoka wapi ikiwa hata kwenye bajeti ya mwaka huu wa fdha haipo, hata kwenye mpango wa miaka mitano pia haupo. Kuhamisha makao makuu ya nchi si mchezo, kuantakiwa infrastuxture za kutosha. Vyombo vya ulinzi na usalama, nyumba za wafanyakazi etc. Kwa sasa vyombo vya ulinzi na usalama vingi viko Dar sasa kuanzisha vingine si itakuwa kazi.

Ofisi za balozi, uwanja wa ndege wa kimataifa etc.
 
Labda mawaziri wa nchi ofisi ya Rais mpaka mkubwa akubali wengine Majaliwa kabla hajahama watakuwa wamefika Dodoma kabla ya Sept
 
Ndugu yangu watanzania kazi ni kusifia tu, kuna ulazima gani wa kuhamia Dodoma, je bajeti hiyo inatoka wapi ikiwa hata kwenye bajeti ya mwaka huu wa fdha haipo, hata kwenye mpango wa miaka mitano pia haupo. Kuhamisha makao makuu ya nchi si mchezo, kuantakiwa infrastuxture za kutosha. Vyombo vya ulinzi na usalama, nyumba za wafanyakazi etc. Kwa sasa vyombo vya ulinzi na usalama vingi viko Dar sasa kuanzisha vingine si itakuwa kazi.

Ofisi za balozi, uwanja wa ndege wa kimataifa etc.
Wanaotetea wanadai ofisi zote tayari zilishajengwa. kwa kuwa mimi Dodoma pale napita tu nikiwa ndani ya basi au gari moshi, sina authority dhidi ya hao wenyeji wanaodai CDA ilishamaliza kazi yake.
 
Haya matamko kila rais aka Mwenyekiti wa ccm amekuwa akiitoa ila wanamaliza miaka 10 bado wapo dar....ebu tusubiri tuone na huyu itakuweje...

na mi ndo nasubiri hili litokee, maana wengi huweka malengo ila huwa hayafikii mwisho, itakuwa heri kama watatekeleza, ila cha kuangalia ni hasara na faida, hasara zikiwa nyingi kuliko faida kuhusu kuhama basi isiwe, ila faida kama ni nyingi basi kuhama iwe hata leo.
 
Wanaotetea wanadai ofisi zote tayari zilishajengwa. kwa kuwa mimi Dodoma pale napita tu nikiwa ndani ya basi au gari moshi, sina authority dhidi ya hao wenyeji wanaodai CDA ilishamaliza kazi yake.
kwa hiyo ndo wanaanza matayarisho sa hivi? afu watu wahamie mwez wa tsa? kama wanadhodai baadhi yao?

ONA HABARI HII

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema atahamia rasmi Dodoma mwezi Septemba mwaka huu.

Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Kumbukumbuku ya Siku ya Mashujaa Majaliwa ameagiza mawaziri wote wanahamie Dodoma kutekeleza tamko la Rais John Magafuli la serikali anayoingoza kuhamia Dodoma kabla ya kumaliza kipindi chake cha miaka mitano.

''Natoa maagizo kwa mawaziri wa wizara zote wahame mara moja, wahamie Dododma. Kama ofisi zote za serikali zinahamia hapa, ni wazi wageni nao watakuwa wanakuja Dodoma", alisema Majaliwa.

Mapema Rais Magufuli alisisitiza tamko lake alilotoa wakati wa kukabidhiwa uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) kuhamia Dodoma akisema hakuna sababu ya serikali kukwama kutekeleza mpango huo.

Amesema: 'Watanzania wanachukia rushwa, watanzania nataka kero zao zitatuliwe."

Rais Magufuli alivitaka vyama vyote vya siasa nchini kudumisha amani ili watanzania wakiishi na kutumiza majukumu yao kwa amani

Aidha Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela wamesisitiza wananchi wa Tanzania kumuunga mkono Rais katika mpango wake wa kuhakikisha serikali inahamia Dodoma.

Wamesema kufanikiwa kwa mpango huo si tu kuna manufaa kwa wananchi wa Dodoma bali pia Tanzania nzima.

Chanzo: Habari Leo
 
Sina na sina acces ya kuipata hyo pich kwa sasa ila ukiingia kwa net utaipata tu
 
SASA NINI MAONI YA WANANCHI WA DODOMA, AU WAZAWA , AU WANAOISHI DODOMA, Kuhusu ujio huu wa ugeni wa SERIKALI kwenye ARIDHI YENU................
 
Tuache tunajadili nchi yetu, wewe nenda kwenu ukaongeze nguvu ya kupigana na ndugu zenu wa Korea Kaskazini. Utuache sisi wenyewe tujadili.

kilimbamula mimi ni raia wa Tz kwa makaratasi, leo mh rais kasisitiza tena azma yake ya kuhakikisha serikali ina hamia Dodoma.

Wito wangu, kwa akinaTomaso wenzangu, tumuombea mh rais kwa Mungu apate nguvu na hekima aweze kuitimiza azma yake ya kuhamia. Dodoma.
 
SASA NINI MAONI YA WANANCHI WA DODOMA, AU WAZAWA , AU WANAOISHI DODOMA, Kuhusu ujio huu wa ugeni wa SERIKALI kwenye ARIDHI YENU................
Ni Wa Tanzania wote tunajisikia laha dani ya loho.
 
Ndio wasiwasi wangu huo, isijekuwa tu eti kwa sababu Nyerere alisema. Nadhani serikali iwe makini sana kuangalia sababu halisi za kuhamia Dodoma
Kwani lamani inaonyesha wapi ipo Makao Makuu ili tuamie sasa hibi bila kuchelewa?
 
Kwa bajeti ipi labda, kwa bajeti ya mwaka huu haipo, wala kwenye mpango wa miaka mitano haipo pia. Hivi wanaona ni rahisi tu kuhama ofisi kutoka mkoa mmoja hadi mwingine. Kuna mambo mengi wanatakiwa wayajue. Mawaziri wao wanaona sawa tu maana wanafanyiwa kila kitu, je hafanyakazi wamewapangia utaratibu gani? uhamisho,makazi, familia etc.
Hapo ni kuomba Mungu...isije likatoka tamko kuwa asiyeweza kujihamisha aache kazi...sisi tunabana matumizi
 
safi sana. lazima tuwe tunajiwekea commitment na kuwa results oriented.

stock-vector-tanzania-political-map-political-map-of-tanzania-with-the-capital-dodoma-national-borders-most-151269227.jpg
Hivi ni hii ndo ramani official ya tz?? Mbona sio niliyosoma enzi hizo za nchi yenye maziwa matatu
 
Back
Top Bottom