Rais Magufuli, hili la Kangi Lugola hujatenda haki. Sheria ya Uhujumu Uchumi inawahusu wananchi tu?

Tumemsikia wenyewe Rais wetu, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, alipokuwa akitengua uteuzi wa waziri wa mambo ya ndani, Kangi Lugola, akitoa sababu kuwa ni kutokana na waziri huyo kusaini mkataba nje ya nchi, wa kuingiza vifaa vya zimamoto, vyenye thamani ya zaidi ya shilingi trillion moja

Kama madai ya Rais Magufuli ni ya kweli, ni kwanini Jeshi la Polisi nchini halijamkamata Mheshimiwa Lugola na kumfungulia mashitaka ya utakatishaji wa pesa nyingi kiasi hicho?

Tunajua kuwa yupo mwandishi wa habari, Eric Kabendera, anayeendelea kusota rumande, kwa zaidi ya miezi 6 sasa, kwa tuhuma za utakatishaji pesa wa shilingi milioni 170

Tunajua pia yule mfanyakazi wa kituo cha haki za binadamu, Tito Magoti, naye amefunguliwa mashitaka ya utakatishaji pesa wa shilingi milioni 17 pekee!

Inakuwaje kwa hawa akina Lugola, ambapo kwa Maelezo ya Rais wetu Magufuli, amewatuhumu kushiriki kusaini mkataba wa kununua vifaa vya thamani ya zaidi ya shilingi trillion moja, waeendelee kukaa uraiani, ambapo Rais mwenyewe ametuhakikishia kuwa wanahusika na utakatishaji pesa wa zaidi ya shilingi trillion moja?

Hivi ni kipi kikubwa ni trillion moja ya Kangi Lugola au shilingi milioni 17 za Tito Magoti?

Kama Kangi Lugola hajafunguliwa kesi ya utakatishaji pesa basi tutajua kuwa hili suala ni la kisiasa

Tusaidiane katika kulidadavua suala hili kwa maslahi mapana ya Taifa letu

Kuna Maswali mengi sana nyuma ya Pazia.

Naomba kusema wazi ; Mimi ni miongoni mwa Muumini wa Juhudi za Maguful; kiukweli anajitahidi Kwenye baadhi ya mambo.

Lakini namna ya Uongozi wa Magufuli mpaka leo nimeshindwa ku define leadership style ya Gufuli.

1 Anatuelezea sana matatizo badala ya kutupa majibu na solution.
2. Katika tumbua tumbua zake; hakuna hata mmoja aliyewajibika au kuwajibishwa kisheria hata upige Billions of Money
3 .Nyuma ya ishu ya Kangi kuna maswali mengi kuliko majibu.

The whole thing ya Kangi Lugola won’t make any sense until he has brought forth to the law.

Otherwise this is another Customer Retention. Yaani you treat Diabetes you end up in BP; now you will have to deal with Diabetes and BP —Business as Usual
 
Teuzi na Gufuli hazina vetting. Huyu Lugola alikuwa na kesi PCCB. Halafu huko alikuwa kwenye kamati ya LAAC alikuwa mtu wa bahasha kishenzi.

Anayesema Gufuli anachukia wala rushwa hajielewi
 
Nauliza ivi Magufuli anapambana na ufisadi au anawalea mafisadi? Ivi kuna mtu anaweza kuwa fisadi nje ya mfumo wa ccm na serikali yake?

Ile mahakama ilifunguliwa kuwafunga kina nani?

Lugola alishakamatwa na Rushwa tukashangaa kupeaa uwaziri kaenda kusaini mkataba wa matrilioni nashangaa anayejiita mtumbua chunusi hata kusema ashitakiwe kwa kutaka kuliingizia taifa hasara na katibu wake anapewa ubalozi.

Najiuliza lengo la magufuli kumpa ubalozi ili iweje? Kwann wasishitakiwe kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Kabendera kadaiwa kutakatisha milioni 173 yuko jela hawa ma matrilioni wanapewa ubalozi.

Huyu ni mpenzi wa mungu yupi anayesema ukweli?
 
Wasalam, kuna taarifa kwamba imeundwa tume kuchunguza mkataba wa mamilion aliosaini mh lungola kwa niaba ya jeshi LA zimamoto na km itathibitika mkataba ni wakifasadi basi bwana lugola kangi atashitakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi ambayo hayana dhamana hivyo kuna uwezekano akaungana na ndugu Eriki kabendera kule segerea.

Muda ni rafiki mwema tuvute subra tuone km tetesi za taarifa hii zitatokea sio mbali ni karibu sana.
 
Kama uliskiliza vizuri utagundua pale mwenye kosa kuu ni Kamishna wa zimamoto! Katibu na Lugola ni issue ya uwajibikaji, na Katibu alisifiwa kwa sababu alijiuzulu/aliwajibika bila shurti!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nauliza ivi Magufuli anapambana na ufisadi au anawalea mafisadi? Ivi kuna mtu anaweza kuwa fisadi nje ya mfumo wa ccm na serikali yake?

Ile mahakama ilifunguliwa kuwafunga kina nani?

Lugola alishakamatwa na Rushwa tukashangaa kupeaa uwaziri kaenda kusaini mkataba wa matrilioni nashangaa anayejiita mtumbua chunusi hata kusema ashitakiwe kwa kutaka kuliingizia taifa hasara na katibu wake anapewa ubalozi.

Najiuliza lengo la magufuli kumpa ubalozi ili iweje? Kwann wasishitakiwe kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Kabendera kadaiwa kutakatisha milioni 173 yuko jela hawa ma matrilioni wanapewa ubalozi.

Huyu ni mpenzi wa mungu yupi anayesema ukweli?
Ndiyo ujue Mkuu Return Of Undertaker kuwa ile ilikuwa bonge la movie.......

Main character wa picha hiyo alikuwa Jiwe mwenyewe
 
Nauliza ivi Magufuli anapambana na ufisadi au anawalea mafisadi? Ivi kuna mtu anaweza kuwa fisadi nje ya mfumo wa ccm na serikali yake?

Ile mahakama ilifunguliwa kuwafunga kina nani?

Lugola alishakamatwa na Rushwa tukashangaa kupeaa uwaziri kaenda kusaini mkataba wa matrilioni nashangaa anayejiita mtumbua chunusi hata kusema ashitakiwe kwa kutaka kuliingizia taifa hasara na katibu wake anapewa ubalozi.

Najiuliza lengo la magufuli kumpa ubalozi ili iweje? Kwann wasishitakiwe kwa makosa ya uhujumu uchumi.

Kabendera kadaiwa kutakatisha milioni 173 yuko jela hawa ma matrilioni wanapewa ubalozi.

Huyu ni mpenzi wa mungu yupi anayesema ukweli?
Katibu hakuhusika amewajibika kwa sababu tukio limetokea wizarani kwake......uwe unaelewa bwashee!
 
Back
Top Bottom